Professional Documents
Culture Documents
www.wanachuoni.com
Kushikamana Na
Uislamu Kweli Kweli
[Khutbah Ya Ijumaa]
Imetolewa na:
www.wanachuoni.com
2
www.wanachuoni.com
www.wanachuoni.com
Jambo la tatu - nalo ni muhimu sana ambalo wengi wameghafilika nalo [na
kuna watu] wanalikemea - ni mtu kujiweka mbali na washirikina na Dini yao,
na [mtu] aitakidi kuwa (dini zao) ni batili, mtu asiwapende, asiwanusuru,
kuwatetea, hili ni wajibu kwa Waislamu na ndio mila [Dini] ya Nabii Ibraahim
('alayhis Salaam). Ambaye tumeamrishwa kumfuata.
اَّلل َكفَ ْرنَا ِ ِيم َوالَّذِينَ َمعَهُ إِ ْذ قَالُوا ِلقَ ْو ِم ِه ْم إِنَّا ب َُر َءؤُا ِمن ُك ْم َو ِم َّما ت َ ْعبُدُونَ ِمن د
ِ َّ ُون َ سنَةٌ فِي إِب َْراه َ َت لَ ُك ْم أُس َْوة ٌ َح
ْ قَ ْد َكان
َ
ِ َّ ِضاء أبَدًا َحتَّى ت ُؤْ ِمنُوا ب
ُاَّلل َوحْ دَه ْ ْ
َ بِ ُك ْم َوبَدَا بَ ْينَنَا َوبَ ْينَ ُك ُم العَدَ َاوة ُ َوالبَ ْغ
“Hakika nyinyi mna mfano mzuri kwenu kwa Ibraahim na wale walio
kuwa pamoja naye, walipowaambia watu wao: “Hakika sisi tumejitenga
nanyi na hayo mnayoyaabudu badala ya Allaah. Tunakukataeni; na
umekwisha dhihiri uadui na chuki baina yetu na nyinyi mpaka
mtakapo muamini Allaah peke yake”.” (60:4)
Na Ibraahim ('alayhis Salaam) alijiweka mbali na baba yake pindi alipojua kuwa ni
adui wa Allaah.
ألواهٌ َح ِلي ٌم َ َّلل تَبَ َّرأ َ ِم ْنهُ إِ َّن إِب َْراه
َّ ِيم ِ فَلَ َّما تَبَيَّنَ لَهُ أَنَّهُ َعد ٌُّو ِ ه
سولَهُ َولَ ْو َكانُوا آبَاء ُه ْم أ َ ْو أ َ ْبنَاء ُه ْم أ َ ْو ِإ ْخ َوانَ ُه ْم أ َ ْو َّ َّاَّلل َو ْاليَ ْو ِم ْاْل ِخ ِر ي َُوادُّونَ َم ْن َحاد
ُ اَّللَ َو َر ِ َّ ََل ت َِجدُ قَ ْو ًما يُؤْ ِمنُونَ ِب
ار خَا ِلدِينَ فِي َها ُ ت تَجْ ِري ِمن تَحْ تِ َها ْاأل َ ْن َه ٍ اْلي َمانَ َوأَيَّدَهُم بِ ُر
ٍ وح ِ هم ْنهُ َويُد ِْخلُ ُه ْم َجنَّا ِ ْ َب فِي قُلُوبِ ِه ُم َ يرت َ ُه ْم أ ُ ْولَئِكَ َكت
َ َع ِش
ْ
َاَّلل ُه ُم ال ُم ْف ِل ُحون َ
َ اَّلل أ ََل ِإ َّن ِح ْز
ِ َّ ب ِ َّ ب ُ
ُ ضوا َع ْنهُ أ ْولَئِكَ ِح ْز ُ اَّللُ َع ْن ُه ْم َو َر
َّ ي َ ض ِ َر
“Huwakuti watu wanaomuamini Allaah na Siku ya Mwisho kuwa
wanawapenda wanaompinga Allaah Mtume wake, hata wakiwa ni baba
zao, au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao. Hao ameandika katika
nyoyo zao Imani, na amewapa nguvu kwa Roho itokayo kwake. Na
atawaingiza katika Mabustani yapitayo mito kati yake. Humo watakaa
daima Allaah awe radhi nao, na wao wawe radhi naye. Hao ndio
Hizbullahi, Kundi la Allaah. Hakika Kundi la Allaah ndilo
lenye kufanikiwa.” (58:22)
www.wanachuoni.com
“Walipokuwa wamekaa na Mtume (swalla Allaahu 'alayhi wa sallam), alijitokeza mtu haonekani
na uchovu wa safari na hapakuwa hata mmoja aliekuwa akimjua. Akakaa
mbele ya Mtume (swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kwa adabu kabisa, mkao wa mtu mwenye
kutafuta elimu [mwanafunzi], akamwambia ewe Muhammad!: "Nambie nini
maana ya Uislamu? Akasema Uislamu ni kushuhudia kuwa hapana mola
apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume
wa Allaah, kusimamisha Swalah, kutoa Zakaah, kufunga Ramadhaan na
kwenda kuhiji kwa yule mwenye uwezo." Yule mtu (Jibriyl) akasema:
"Umesema kweli". Maswahabah wakashangazwa kuona anamuuliza kisha
anamwambia kasema kweli.
Akasema (Jibriyl): “Niambie kuhusu Qiyaamah. Akajibu Mtume ( صلى هللا عليه
)وسلم: “Muulizwaji si mjuzi kama asivyo vilevile Muulizaji. Nijulishe alama
zake: Akajibu Mtume ()صلى هللا عليه وسلم: “Kijakazi atazaa bibi yake, na utaona
wachunga wenda miguu chini, wenda uchi (wasio na uwezo wa kumiliki hata
mavazi), mafukara (wasiokuwa hata na sehemu ya kuishi kwa umaskini)
wakishindana kujenga majumba ya fakhari. Kisha akaondoka (Jibriyl) na
nilitulia kidogo (nikitafakari). Kisha akasema Mtume ()صلى هللا عليه وسلم: "Ewe
'Umar! Je, unamjua ni nani yule aliyekuwa akiuliza? Nikasema: “Allaah na
Mjumbe wake wanajua zaidi.” Akasema Mtume ()صلى هللا عليه وسلم: “Ni Jibriyl,
alikuja kuwafundisha dini yenu”.”
5
www.wanachuoni.com
Hii ni dalili ya kwamba ni wajibu kwa mtu kujifunza Dini hii na kuiingia kwa
baswiyrah na kikweli kweli mpaka mtu awe Muislamu wa kweli. Si Muislamu
mwenye kufuata tu kichwa mchunga au mwenye madai tu.
َاَّلل َح َّق تُقَاتِ ِه َوَلَ ت َ ُموت ُ َّن إَِلَّ َوأَنتُم ُّم ْس ِل ُمون
َ يَا أَيُّ َها الَّذِينَ آ َمنُواْ اتَّقُواْ ه
“Enyi mlio amini! Mcheni Allaah kama ipasavyo kumcha; wala msife
ila nanyi ni Waislamu.” (03:102)
Shikamana na Dini hii mpaka yatakapokujia mauti, mfe katika Dini hii
mkutane na Allaah ilihali mko nayo.
www.wanachuoni.com
Mcheni Allaah Allaah enyi waja wa Allaah na jueni mambo ya Dini yenu
mpaka muwe imara kwa yale Aliyowateremshia Allaah (Subhaanahu wa
Ta'ala).
Enyi watu! Baada ya kujua neema ya Allaah juu yenu kwa Uislamu huu na
kujua uhakika wa Uislamu, ni juu yenu kumuomba Allaah uthabiti juu yake
(Uislamu). Wengi waliyokuwa wakiujua Uislamu na wakauingia wamepotea
na kuritadi kwa sababu ya fitnah ambayo imewakumba watu leo. Fitnah
ambayo inainga mpaka kwenye manyumba ya watu, wanaisikia na
kuishuhudia wenyewe.
Angalia, Muislamu anakuwa mtu mgeni ilihali kuna wanaodai Uislamu, vipi
kwa Makafiri? Ugeni! Na mgeni ni mtu ambaye yuko kwa watu ambao si
ndugu zake wala wa jinsia yake na hayupo kwenye Mji wake. Huu ndio
ugeni. Na [Uislamu] utarudi kuwa kitu kigeni kwenye Miji ya Waislamu.
7
www.wanachuoni.com
Hakika haokoki mtu (na fitnah hizo) ila yule aliyemuwezesha Allaah na
akamjua Allaah ukweli wa kumjua na akaijua Dini ya Kiislamu uhakika wake
na akasubiria kwa hilo mpaka Akamchukua Allaah ('Azza wa Jalla).