Professional Documents
Culture Documents
7. Serikali ifanye marekebisho katika sheria ya ardhi ya vijiji no. 5 mwaka 1999 ili
kuonyesha ukomo wa eneo la ardhi ya kijiji
8. Serikali itengeneze sera ya namna ya kuandaa mipango ya maendeleo ya wilaya
itakayotoa kipaumbele kwa wakulima wadogo wadogo ili waweze kukabiliana na athari za
mabadiliko ya tabianchi
9. Serikali izuiye matamko yanayotolewa na viongozi wa kisiasa ambayo hudhoofisha
juhudi za wakulima katika kupambana na umasikini na athari za mabadiliko ya tabia nchi
10. Serikali isimamie utekelezaji wa sheria ya kutokulima mita 60 toka chanzo cha maji
11. Serikali itakayoingia madarakani itoe ruzuku kwa mazao yote ya kilimo kwa wakulima
wadogo wadogo katika maeneo husika.
12. Mamlaka zinazosimamia ubora wa mbegu na usambazaji ziimarishwe.
13. Serikali ihusike kuweka bei elekezi ya mazao ya kilimo
14. Serikali itenge fedha za kutosha kwa ajili ya kujenga miundombinu ya umwagiliaji