You are on page 1of 1

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI


IDARA YA UHAMIAJI
Anuani ya Simu:
NUKUSHI:

UHAMIAJI

OFISI YA UHAMIAJI (M)


S.L.P 369
SIMU:MUSOMA
+255 282622426

OFISI YA UHAMIAJI WILAYA


S.L.P 417

BUNDA
Tuesday, 24 May 2016

KUMB .BND/IMM/INV/VOL.II/21/18

MENEJA MAPATO WILAYA


S.L.P
BUNDA
YAH: PIKIPIKI NAMBA T.213 CDF
Tafadhali rejea kichwa cha habari hapo juu, pikipiki yenye namba hapo juu ina
tuhuma ya kumpakia raia wa Ethiopia siku ya tarehe 06/11/2013.
Tukiwa eneo la darajani rubana kwenye doria zetu dereva wa pikipiki hiyo alipita
akiwa amempakia raia huyo wa Ethiopia na aliposimamishwa hakusimama. Ndipo
tukaomba msaada wa gari binafsi na kumfuatilia na kwa ujanja wake akapita njia za
panya. Lakini kwa kushirikiana na askari wa kizuizi wa upande wa Lamadi
mtuhumiwa alipita kwa mbali na kukimbizwa na pikipiki nyingine hadi akamshusha
raia huyo wa Ethiopia na kukimbia zake. Na bahati nzuri namba za pikipiki
zilijulikana.
Hivyo tunaomba ushirikiano na ofisi yako namna ya kumpata mmiliki wa chombo
hicho ili kukomesha biashara hiyo kwa sheria kuchukuliwa dhidi ya mhusika.
Nswima
O.S
Kny; Afisa Uhamiaji Wilaya
BUNDA
NAKALA;
AFISA UHAMIAJI (M)
S.L.P 369
MUSOMA
OC CID WILAYA
S.L.P 50
BUNDA

You might also like