Professional Documents
Culture Documents
1. Askofu Zachary Kakobe hana akaunti wala fedha katika taasisi yoyote ya
fedha hapa nchini. Aidha uchunguzi ulibaini kuwa Askofu Kakobe ni mmoja
wa wasimamizi wakuu wa akaunti za kanisa (signatories) zilizopo katika
benki ya NBC zenye jumla ya kiasi cha shilingi 8,132,100,819.00, kiasi hiki
cha fedha kimetokana na sadaka, zaka na changizo ambazo zinatolewa na
waumini wa kanisa tajwa hapo juu, hivyo kwa mujibu wa Sheria hakitozwi
kodi.
WITO:
Mamlaka ya Mapato Tanzaniainatoa wito kwa Taasisi zote za dini ambazo
zinajihusisha na shughuli zozote za kiuchumi kulipa kodi stahiki na kwa
wakati kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kodi.
Charles E. Kichere
KAMISHNA MKUU
MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA