TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAZISHI YA ALIYEKUWA MBUNGE WA JIMBO
LA BUYUNGU, MAREHEMU MWL. KASUKU SAMSON BILAGO
Kikao cha pamoja baina ya Tume ya Utumishi wa Bunge na Kamati ya
Uongozi ya Bunge kimefanyika leo Jumapili tarehe 27 Mei, 2018 na kukubaliana kuwa, mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Marehemu Mwl. Kasuku Samson Bilago utaletwa Bungeni Jijini Dodoma siku ya Jumanne ya tarehe 29 Mei, 2018 kwa ajili ya Waheshimiwa Wabunge kutoa heshima zao za mwisho.
Uamuzi huo umefikiwa baada ya Uongozi wa Bunge kushauriana na
kukubaliana na Uongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na familia ya marehemu.
Baada ya Waheshimiwa Wabunge kutoa heshima zao za mwisho, siku
hiyo hiyo mwili wa marehemu utasafarishwa kuelekea Kakonko Mkoani Kigoma.
Mheshimiwa Mwl. Bilago aliyefariki siku ya Jumamosi tarehe 26 Mei, 2018
katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili anatarajiwa kuzikwa tarehe 30 Mei, 2018 katika Kijiji cha Kasuga Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma.
Ofisi ya Bunge inaendelea kuratibu taratibu za mazishi kwa kushirikiana na
uongozi wa CHADEMA pamoja na familia ya Marehemu, taarifa zaidi zitaendelea kutolewa. Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi.
Imetolewa na: Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano,