Professional Documents
Culture Documents
Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo baada ya kupokea ripoti ya timu ya
uchunguzi juu ya uhalisia na ubora wa mafuta ya kula iliyoongozwa na Prof.
Joseph Buchweishaija ambayo imefanya uchunguzi katika matanki 43 yenye tani
105,630 za mafuta ya kula na kubaini kuwa kati ya matanki hayo, 7 yana na
mafuta yaliyoboreshwa (refined oil), 14 yana na mafuta yaliyoboreshwa kiasi
(semi refined oil), 4 yana ni mafuta ya kutengenezea sabuni (Refined Stearin)
na 18 ni mafuta ghafi (crude oil).
Kufuatia matokeo hayo Mhe. Rais Magufuli ameagiza mafuta yote yanayostahili
kutozwa kodi ya asilimia 10 yatozwe hivyo, yanayostahili kutozwa kodi asilimia 25
yatozwe kwa kiwango hicho na wafanyabiashara wote waliofanya udanganyifu
katika nyaraka kwa kuonesha kuwa mafuta yao ni ghafi wakati sio ghafi wapigwe
faini kwa mujibu wa sheria na mafuta yaanze kusambazwa haraka iwezekanavyo.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
15 Mei, 2018