Professional Documents
Culture Documents
WAFILIPI 3:20-21
“Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni, kutoka huko tena tunamtazamia
mwokozi, Bwana Yesu Kristo; atakaye ubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na
mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote
Kuna aina mbili za uraia ambazo Binadamu anaweza kuwa nazo. Uraia wa duniani
Mtu anapozaliwa kupitia wazazi wa dunia hii (baba ba mama), anaandikishwa katika
kitabu cha serikali cha vizazi na vifo, ambacho kinapatikana wilayani, mahali pale
alipozaliwa mtu huyo. Kinaandaliwa cheti cha kuzaliwa mahali pale alipozaliwa. Hivyo moja
kwa moja anatambulika kuwa na uraia wa mahali pale, au nchi ile alipozaliwa.
Na hata baada ya kufa, mtu huyo atawekwa katika kumbukumbu la watu waliokufa,
katika kitabu cha vizazi na vifo pale wilayani, hivyo kumbukumbu lake linatoweka katika
dunia hii lakini bado anaandikishwa katika kitabu hicho pale alipokuwa raia wa nchi hiyo.
Uraia huu wa kidunia sio wa kudumu, kwa sababu ni wa muda mfupi tu, si wa milele.
Na wakati mtu anapokuwa na utambulisho wa uraia katika taifa hilo kama vile Tanzania,
serikali inakuwa na jukumu la kuhakikisha usalama wa raia huyu awe mahali pale
alipozaliwa katika nchi yake au awe sehemu nyingine kama vile nje ya nchi, Kuhakikishiwa
usalama wake ni kwa mujibu wa katiba ya nchi; kwa Tanzania ni haki ya kikatiba
Pia kulingana na haki ya kuishi kila mtu anakuwa na haki ya kuishi na kupata kutoka
katika jamii hifadhi ya maisha yake, kwa mujibu wa sheria. [haki ya kuwa hai sheria ya
1
Hiyo ndiyo maana kunapotokea tukio lolote lenye kuhatarisha usalama wa raia
(ambaye ana uhalali wote wa kuishi au kufanya kazi mahali pale pasipo kuvunja sheria au
kufanya uhaini katika namna au njia yoyote), hapo serikali inachukua hatua za haraka za
kutetea usalama wake pia kumlinda na kutengeneza mazingira salama ya mtu huyo ili
Hii ndiyo maana imeshatokea baadhi ya mataifa mawili kuingia mgogoro na baadae
kutibua uhusiano wa kidiplomasia baina ya hizo nchi mbili pale inapokuja kutambulika kuwa
raia wake amehatarishiwa usalama wake au hata kupoteza uhai wake katika mazingira
tatanishi akiwa katika nchi hiyo nyingine. Hii ni moja ya mambo ya msingi na nyeti kabisa
Kwa hiyo uraia huu wa kidunia ni uraia wa kimwili ambao ni muhimu sana
Kwa wakristo, wanasema atakapo lala. (kwa sababu upo wakati ataamka-siku ya mwisho
katika ufufuo).
Na hivyo tukiwa katika mwili huu na uraia huu wa duniani maandiko matakatifu
yanatuhimiza kuandaa mazingira ya kuishi kwa haki na kweli ili kujiandaa kwa ajili ya uraia
mwingine ambao ni wa milele na usio na kikomo hasa tukijua kwamba ipo hesabu ya kuja
kuitoa kulingana na kile tulichokifanya hapa duniani katika uraia huu wa muda mfupi.
kiroho, baada ya kumwamini Bwana Yesu Kristo, kumpokea na kubatizwa katika maji. Mtu
anakuwa amezaliwa katika ufalme wa Bwana Yesu Kristo. Anapokea uraia wa mbinguni.
Angalia hapa Yesu anaongea na mwalimu mkubwa sana wa kiyahudi jina lake Nikodemo.
2
YOH 3:1-6.
ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu. Nikodemo akamwambia awezaje mtu kuzaliwa
akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
Yesu akajibu akasema, amini Amini nakuambaia mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho
Bwana Yesu anasema mtu hawezi kuuona [kuuelewa] ufalme wa Mungu. Maana kuna
kuuona na pia kuna kuuingi. Wapo waliouona (kuuelewa) lakini wasiingie kama Yuda
Eskarioti. Kwa sababu naye aliuelewa na kuuona na aliahidiwa kuuingia (LUKA 10:20)
Lakini kuingia katika ufalme wa Mungu tunaingia kwanza katika Roho, tunakuwa
pamoja na Kristo katika ulimwengu wa kiroho, EFESO 2:6 lakini tutaingia katika mwili
Hivyo mtu huyo aliyezaliwa mara ya pili, ni raia wa mbinguni, amezaliwa katika
ufalme wa mbinguni, ameikana dunia na mambo yake yote. Naye kwa mujibu wa maandiko
matakatifu, basi hapa duniani anakuwa ni Balozi wa Bwana Yesu Kristo (2KOR5:20), kwa
sababu ipo siku atarudi katika nchi yake ya milele, ambako kuna maisha ya milele ya raha na
faraja. Na akirudi huko atatakiwa kwenda kutoa hesabu ya kazi zote alizofanya hapa duniani
akiwa katika nchi ya hii ya ugeni-duniani akiwa katika uraia wa kidunia ambao ni wa muda
mfupi tu.
Pia tunapokuwa katika uraia huu wa muda mfupi, tunajitahidi kutafuta tiba ya haraka
tunapopatwa na matatizo ya kiafya, hata tunaweka bima ya afya ili kujihakikishia afya njema
wakati wote wa maisha. Hii ndio maana yapo mataifa mengi yaliyojiwekea sheria ya utoaji
wa huduma za afya kwa kutumia utaratibu wa bima. Kwa mfano serikali ya Tanzania ipo
3
katika hatua ya kutaka kupitisha sheria itakayowafanya watu wote kuwa katika mfumo wa
bima ya afya. Hii ni kwa sababu kila mtu ana haki ya kuishi kwa kuhakikishiwa huduma ya
kazini, shuleni,n:k ili kupata tiba ya awali endapo itatokea dharura ya kiafya katika mazingira
ambayo ni vigumu kumuona daktari muda huo huo. Wakati mwingine tunapata masomo
kutoka kwa matabibu na wataalamu wa afya kuhusu afya zetu kupitia vyombo vya habari
kama TV.
Hii yote inaonyesha kwamba tunapenda kuishi tena bila kuzeeka. Maana upo ukweli
kwamba kila mtu hapendi kuzeeka haraka. Hasa kama maisha yamekuwa na mafanikio na
matatizo ni machache yenye misukosuko ya nadra. Na hata kama leo hii ingetokea mtu
anauza kwa gharama kubwa sana dawa ya kurefusha maisha, basi watu wengi wangejitahidi
kuuza kila alichonacho ili kununua dawa hiyo ili apate kuendelea kufanya maendeleo yake na
Unaona jinsi ambavyo watu wanataka kuishi milele katika raha? Na huo ni uraia wa
dunia hii tiu, ni uraia wa muda mfupi tu, lakini unang’ang’aniwa kweli kweli.
Sasa basi ikiwa maisha ya dunia hii ni muhimu sana, je si zaidi maisha ya milele?
Ikiwa uraia wa dunia hii ni muhimu sana, je si zaidi uraia wa mbinguni? Uraia wa mbinguni
ulipotezwa pale Bustani ya Edeni, maisha ya milele yalipotea pale Edeni baada ya anguko la
Adamu na Hawa. Mahusiano kati ya Mungu na binadamu yalitibuliwa pale na hivyo kuingia
laana ya kifo kwa binadamu. Laana ambayo haikutakiwa kuwepo hapo kabla ya dhambi
Lakini Mungu wa upendo alimleta Bwana Yesu ili tupate uzima wa milele, naye ndiye mti
wa uzima, ili tuingie katika ahadi ya kuishi milele baada ya msamaha wa dhambi. Kwa njia
ya kuamini kifo na kumwagika kwa damu yake pale msalabani kalvari. Tunajihakikishia
4
Maisha ya milele, uraia wa mbinguni haununuliwi kwa fedha ili kuupata, wokovu
haupatikani kwa kutoa hongo ili kuupata ila ni kwa imani tunaokolewa, kwa neema tumeitwa
Na hakuna njia nyingine ya kuingia katika ufalme wa Mungu ili kupata uraia wa
mbinguni ila ni kwa kumwamini Bwana Yesu. Kuamini ile kazi iliyofanyika pale msalabani
kalvari. Wapo watu wanaopinga wokovu kwa kusema kuwa njia ya kuingia katika ufalme wa
Mungu ni kutenda mema tu. Sasa huo ni upotovu kwa sababu kifo cha Yesu msalabani
kitakuwa hakina maana. Lakini yesu alisema kuwa yeye ndio njia, kweli na uzima
(YOHANA 14 :6). Kwa kumwamini Yeye tumepona (ISAYA 53 :5, 1PETRO2 :24).
Sasa mtu akisema kwamba anaingia katika ufalme wa Mungu kwa kuzijua amri za
Mungu na kuzishika na kuzitii na kukataa sadaka iliyotolewa pale msalabani kalvari ni sawa
na mtu anayetaka kwenda mbinguni kwa mguu. Yesu alisema pasipo yeye sisi hatuwezi kitu.
(YOHANA 15 :5) Hivyo ni lazima kuifuata kanuni aliyoiweka Mungu kwamba tunamuhitaji
Yesu ili tuweze kuwa mfano na sura ya Mungu kama ilivyokuwa pale bustani ya edeni, kwa
sababu tokea pale ndipo tulipoteza utukufu wa Mungu na Adamu wa pili (Yesu) ndiye
kumkataa Bwana Yesu. (LUKA 18:19-25) Tunaokolewa kwa neema, sio kwamba Mungu
anawatafuta wale wanaojua kutenda mema ndio awape wokovu, hapana. (WAEFESO 2 :8).
Mungu anawatafuta waliopotea ili waokolewe, waijue neema na wakae katika neema hiyo
(LUKA 19 :10). Hii ndio maana ni vigumu sana kuokolewa mtu anayeamini na kujijua kuwa
MUNGU ATUBARIKI
0763-53-25-56