You are on page 1of 6

AGANO LA DAMU 18.09.

2022

ANDIKO KUU: MWANZO 15:3-18

Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu


ndiye mrithi wangu. 4 Nalo neno la Bwana likamjia likinena, Huyu hatakurithi,
bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. 5 Akamleta nje,
akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu.
Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako. 6 Akamwamini Bwana, naye
akamhesabia jambo hili kuwa haki. 7 Kisha akamwambia, Mimi ni Bwana,
niliyekuleta kutoka Uru wa Wakaldayo nikupe nchi hii ili uirithi. 8 Akasema, Ee
Bwana MUNGU, nipateje kujua ya kwamba nitairithi? 9 Akamwambia, Unipatie
ndama wa miaka mitatu, na mbuzi mke wa miaka mitatu, na kondoo mume wa
miaka mitatu, na hua, na mwana njiwa. 10 Akampatia hao wote, akawapasua
vipande viwili, akaweka kila kipande kuelekea mwenzake, ila ndege hakuwapasua.
11 Hata tai walipotua juu ya mizoga Abramu akawafukuza. 12 Na jua lilipokuwa
likichwa usingizi mzito ulimshika Abramu, hofu ya giza kuu ikamwangukia.
13 Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa
mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa
miaka mia nne. 14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye
watatoka na mali mengi. 15 Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani,
utazikwa katika uzee mwema. 16 Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana
haujatimia uovu wa Waamori bado. 17 Ikawa, jua lilipokuchwa likawa giza,
tazama, tanuru ya moshi na mwenge unaowaka ulipita kati ya vile vipande vya
nyama. 18 Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako
nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,

Waebrania 9:16-22, “Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake
aliyelifanya. 17 Kwa maana agano la urithi lina nguvu palipotukia kufa kwa mtu;
kwa kuwa halina nguvu kabisa, akiwa yu hai yeye aliyelifanya. 18 Kwa hiyo hata
lile la kwanza halikuanzwa pasipo damu. 19 Maana kila amri ilipokwisha kunenwa
na Musa kwa hao watu wote, kama ilivyoamuru sheria, aliitwaa damu ya ndama na
ya mbuzi, pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo, akakinyunyizia kitabu
chenyewe, na watu wote, 20 akisema, Hii ni damu ya agano mliloamriwa na
Mungu.
21 Na ile hema nayo na vyombo vyote vya ibada alivinyunyizia damu vivyo hivyo.
22 Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga
damu hakuna ondoleo.

“Zimesamehewa, zimesahauliwa, milele, dhambi zangu hazitakumbukwa tena”.

1. Maana ya Agano

Agano ni mapatano au makubaliano kati ya pande mbili; Mungu au miungu na


mtu, familia, ukoo au taifa.

Kila agano lina mambo makuu matatu; kwanza AHADI; yaani manufaa ya hilo
agano au kusudi la hilo agano, pili kila agano lina MASHARTI, yaani mambo
yanayofanya agano liweze kudumu, tatu kila agano lina SADAKA, yaani kitu
ambacho kinatolewa ili mtu apate AHADI.

Katika agano na Mungu; Mungu ndiye anayeahidi, na kuapa


kutimiza ahadi zake kwa binadamu, pasipo kutegemea mchango wa binadamu
katika utekelezaji wa ahadi za Mungu. Mungu amejiweka katika nafasi ya
kuwa mwaminifu wa kutimiza ahadi kwa binadamu pasipo binadamu
kuchangia kitu chochote kwenye agano la damu.

2. Maana ya Damu

Biblia inasema damu ni UHAI. Walawi 17:11 “Kwa kuwa uhai wa mwili u
katika hiyo damu, nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili
kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo
upatanisho kwa sababu ya nafsi”.

"Msipo ula mwili wake mwana wa Adamu, na kuinywa damu yake, hamna
uzima ndani yenu" (Yohana 6:53).

Dhambi huleta mauti (Warumi 6:23), “ili dhambi iwe dhambi hasa, huleta
mauti” yaani, dhambi humwaga damu (Warumi 7:13). Kwa sababu hii wana
wa Israel walitazamiwa kumwaga damu ya mnyama kila wakati walipotenda
dhambi, ili kuwakumbusha kuwa dhambi inaleta mauti, maana pasipo
kumwaga damu hakuna ondoleo la dhambi (Waebrania 9:22).
 Kwa sababu hii, Adamu na Hawa walipojifunika wenyewe na majani ya mtini
hayakukubalika; badala yake, Mungu alimchinja mwanakondoo na kuwagawia
ngozi za kujifunika dhambi zao (Mwanzo 3:7, 21 Mstari wa 21 unasema,
“BWANA Mungu akawafanyia Adamu na mkewe mavazi ya ngozi,
akawavika”). Vivyo hivyo, dhabihu za wanyama wa Habili ilikubalika zaidi
kuliko matoleo ya nafaka na mboga ya Kaini, kwa kuwa alielewa jambo hili ya
kwamba pasipo kumwaga damu ingekuwa vigumu kusamehewa na kukubalika
kumkaribia Mungu (Mwanzo 4:3-5).

3. Mifano ya Agano la Damu

 Nuhu. Tendo la kwanza la Nuhu baada ya kutoka kwenye safina ni kufanya


agano la damu na Mungu. Mwanzo 8:20, “Nuhu akamjengea Bwana
madhabahu, akatwaa katika kila mnyama aliye safi, na katika kila ndege aliye
safi, akavitoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu”.

 Ibrahimu. Mwanzo 17:10, “hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi
na wewe, na uzao wako baada yako, kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa”
Yeye hapo mwanzo aliitwa Abramu maana yake “Baba” maandiko yanasema
Mwanzo 17:5 Mungu akamwambia hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako
litakuwa Ibrahimu kwani nimekuweka kuwa Baba wa mataifa mengi”.

 Biblia inasema katika Kutoka 2:23-24, “hata baada ya siku zile mfalme wa
Misri akafa, wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia,
kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa, Mungu
akasikia kuugua kwao, Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya na
Ibrahimu na Isaka na Yakobo”.

Yesu amenituma ili uweke agano jipya na Yesu Kristo leo naye hatakuacha
milele. Israeli waligua, najua nawe unaugua, nafsi yako inaugua, natangaza
Mungu atakukumbuka leo.

 Musa. Baada ya Mungu kutoa amri kumi, maandiko yanasema wana wa Israeli
walifanya agano na Mungu. Kutoka 24:8, “Ndipo Musa akachukua ile damu,
akainyunyiza juu ya watu akasema, hii ni damu ya agano ambalo Bwana
amefanya nanyi kufuatana na maneno haya yote”
 Isaya 28:15 inasema “kwa sababu mmesema, tumefanya agano na mauti,
tumepatana na kuzimu, pigo lifurikalo litakapopita, halitatufikia sisi, kwa
maana tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu, tumejificha chini ya
maneno yasiyo kweli”. Imeandikwa Isaya 28:18, “Na agano lenu mliloagana
na mauti litabatilika” Kwa damu ya mwana-kondoo kila agano lililowekwa na
mababu, agano na kuzimu, na waganga, na wasoma nyota, na wapiga ramli,
ili kuharibu maisha yangu, ninalifuta, sitalitumikia agano hilo kwa jina la
Yesu”.

 Katika Yeremia 7:18, “Watoto huokota kuni, na baba zao huwasha moto, na
wanawake hukanda unga, ili kumfanyizia mikate malkia wa mbinguni na
kuwamiminia miungu mingine sadaka za kinywaji, wapate kunikasirisha
mimi”. Sadaka za kinywaji; kinywaji hiki ni damu inayotolewa kwa malkia wa
mbinguni na miungu mingine, na majini na mapepo.

4. Tabia ya Damu

Damu ina sauti, inaweza kulia na inaweza kuleta laana. Mungu amekataza kula
au kunywa damu kwa sababu hizi tatu. Mwanzo 4:10, “akasema umefanya
nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi”.
Kumbukumbu 12:23, “ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu
ndiyo uhai, na uhai usile pamoja na nyama”.
Damu inanena; Damu iliyomwagika chini inaweza kunena mema au yaweza
kunena mabaya, damu inenayo mema ni ya Yesu peke yake, Waebrania 12:24
inasema, “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo
mema kuliko ile ya Habili.” Kumbe kuna damu inayonena mema (damu ya
Yesu Kristo) na pia kuna damu inayonena mabaya (damu ya ndege, wanyama,
hata watu). Damu yaweza kuongea mabaya juu ya mtu; damu ikimwagwa
hunena na ndio maana hata nchi yaweza kuingia kwenye matatizo kwa sababu
ya damu inenayo iliyomwagika.

5. Kwa nini mashetani na Wachawi hutumia damu.

Katika Mwanzo 4:10 Neno la Mungu linasema Mungu alimuuliza Kaini,


umefanya nini, Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi”.
Kumbe damu ina sauti, kumbe damu inalia! Kumbe damu inaongea!
Mungu alikuwa na maana gani aliposema, “sauti ya damu ya ndugu yako
inanililia kutoka katika ardhi?”. Ina maana kwamba damu ya Habili ilikuwa
inalilia au inadai kulipiwa kisasi. Damu ya Habili ililia ili haki itendeke. Ooh
damu ya Habili ililia kutaka kisasi, lakini damu ya Yesu inataka msamaha na
urejesho!

Sasa kwa kujua kuwa kila damu iliyomwagwa inauwezo wa kusema, wachawi
hutumia tabia hiyo ya damu kufunga maisha ya watu. Kwa hiyo wanachofanya
wachawi au waganga ni kuchukua mnyama na kumchinja yule mnyama na
kuinuizia inene tatizo lako. Kimsingi; hii damu iliyomwagwa ndiyo inayoitwa
madhabahu ya tatizo lako. Na ndio maana waganga wa kienyeji huagiza kuku,
mbuzi au ng’ombe kwa ajili ya kumwaga damu ili inene mabaya juu ya mtu.

Damu inapomwagwa inatoa sauti; yaani katika ulimwengu wa roho ni sauti


kubwa ili mtu akae katika tatizo; kinachotokea pale damu inaponena mashetani
husikia rohoni na kwa njia hiyo mashetani yanapata mlango wa kuingia
kwenye maisha ya mtu. Hivyo mashetani huja ili kutekeleza sauti ya ile damu
inayonena. Kwa njia hiyo shetani amefunga maisha ya watu na kifungo
kinakuwa kikubwa kulingana na wingi na aina ya damu iliyomwagwa.

6. Damu ya Yesu Kristo

 Yesu Kristo alipomwaga damu yake Kalvari alitupatia sisi uhai wake kabisa.

 Damu ya Yesu ni ulinzi. Kutoka 12:12-13, Neno la Mungu linasema, “maana


nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza
wote katika nchi ya Misri wa mwanadamu na wanyama, nami nitafanya
hukumu juu ya miungu yote ya Misri, na ile damu itakuwa ishara kwenu katika
zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu,
lisiwapate pigo lolote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri”. Neno la
Mungu linasema, mwanakondoo wetu, pasaka wetu ni Yesu Kristo.

1 Wakorinto 5:7, “Basi jisafisheni mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa
donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu, kwa maana pasaka wetu
amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani Kristo”.
 Damu ya Yesu inatupa wokovu na ushindi dhidi ya nguvu za giza na
mashetani. Katika Ufunuo 12:10-11, “Nikasikia sauti kuu mbinguni ikisema,
sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya
Kristo wake, kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye
awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa
damu ya mwanakondoo, na kwa neno la ushuhuda wao, ambao hawakupenda
maisha yao hata kufa”.

 Kuna ukombozi ndani ya damu ya Yesu. 1 Petro 1:18-19 Biblia inasema,


“Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa
fedha au dhahabu, mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea
kwa baba zenu, bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na
ila, asiye na waa, yaani, Kristo”.

Katika Wakolosai 1:13-14 Neno la Mungu linasema, naye alituokoa katika


nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa pendo
lake, ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani msamaha wa dhambi”.
Ninaamuru ukombozi wako sasa haijalishi umefanya dhambi kiasi gani,
pokea msamaha wa dhambi kwa damu ya Yesu, msamaha unaachilia
ukombozi wa afya yako, kazi yako, biashara yako, ndoa yako kwa jina la
Yesu Kristo.

 Kuna utakaso katika damu ya Yesu. Waebrania 13:12, “Kwa ajili hii Yesu naye,
ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe aliteswa nje ya lango”. Ni damu yake
ndiyo inatufanya watakatifu na kutuosha maovu yote. Tunaikimbilia kupata utakatifu
na kutufanya safi bila mawaa yoyote wala dosari.

 Damu ya Yesu huondoa laana. Weka agano na Yesu leo. Mathayo 27:29,
“Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika
mkono wake wa kuume, wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki,
wakisema, salaam, mfalme wa Wayahudi”. Hebu sema maneno haya;
“imeendikwa ardhi ililaaniwa itazaa michongoma na miiba, kwa damu ya Yesu
ilitoka katika taji la miiba, ninaifuta laana ya ardhi, sasa ardhi itazaa uzima,
furaha, na upendo.

You might also like