You are on page 1of 6

E D K KIDATO CHA PILI

KAZI
Andikeni kazi ifuatayo ndani ya madaftari yenu ya
Darasani
MADA KUU : FIQHI.
MADA NDOGO : FUNGA YA RAMADHANI NASWAUMU
NYINGINE .
1- MAANA YA SWAUMU
i) Maana ya Swaumu : KILUGHA NI : Kujizuia
kufanya jambo lolote la kawaida ulilolizoea.
ii) KISHERIA NI: Kujizuia na kila chenye kufunguza
kuanzia Alfajiri ya kweli hadi kuzama Jua .

2- AINA ZA SWAUMU
- Kuna aina kuu mbili za Swaumu
i) Funga za Faradhi
ii) Funga za Sunna
- Funga za Faradhi ni mbili
i) Funga ya Ramadhani
ii) Funga za Kafara
3 - UMUHIMU WA FUNGA YA RAMADHANI
a)Funga ya Mwezi wa Ramadhani ni Nguzo ya nne
katika Nguzo za Uislamu.
b)Kufunga Mwezi wa Ramadhani ni utambulisho wa
Uislamu wa Mtu
c) Kufunga Mwezi wa Ramadhani ni kutekeleza Amri
ya Mwenyezi MUNGU (s.w )
d)Kufunga Mwezi wa Ramadhani ni Utambulisho wa
Uislamu wa mtu
e) Kutofunga Mwezi wa Ramadhani makusudi
hupelekea kustahiki kupara Ghadhabu na Adhabu
za Allah (s.w )

3 – KWANINI FUNGA YA RAMADHANI


IMEFARADHISHWA NDANI YA MWEZI WA
RAMADHANI ?
- Kwa sababu ndio Mwezi ambao QUR-AN
imeteremshwa ndani yake .
4 – NGUZO ZA FUNGA
- Swaumu yoyote ina Nguzo kuu mbili , ambazo ni :
i) Nia
- Nia ya funga ya Faradhi hunuiwa kabla ya kuingia
Alfajir . Amma Nia ya Funga ya Sunna hunuiwa
hata baada ya kuchomoza Jua.
ii)Kujizuia na kila chenye kufunguza kuanzia Alfajir
hadi kuzama Jua .

5 – WAISLAMU WANAOLAZIMIKA KUFUNGA .


a)Wenye Akili timamu
b)Waliofikia Balegh
c) Wenye Afya njema
d)Wakazi wa Mji
e) Kwa Wanawake wasiwe katika Hedhi wala
Nifasi
6 - WAISLAMU WENYE RUHUSA
KUTOFUNGARAMADHANI .
a)Wasio na Akili timamu
b)Wasiofikia Balegh
c) Wagonjwa wenye Maradhi yaliyowaondolea
nguvu ya kufunga
d)Wasafiri
e) Wanawake walio katika kipindi cha Hedhi au
Nifasi.
7 - SUNNA ZINAZOAMBATANA NA FUNGA
i)Kuchelewesha kula Daku ( Ndani ya mida ya saa 8,9 na
10 )
ii) Kufuturu mapema ( mara tu baada ya Jua kuzama )
iii)Kuzidisha Ukarimu , Upole na Upendo muda wote wa
Swaumu
iv)Kusoma QUR-AN kwa wingi kipindi chote cha Swaumu
v)Kusimamisha na kudumisha Swala ya Tarawehe Mwezi
mzima wa Ramadhani
vi)Kuutafuta usiku wa LAILATILQADRI kwa kukaa ITIKAAF
katika kumi la mwisho la Mwezi wa Ramadhani.
8 - MIIKO AU MAMBO YANAYOHARIBU AU KUBATILISHA
SWAUMU .
i)Kula au Kunywa chochote makusudi
ii)Kujitapisha Makusudi
iii)Wanawake kupatwa na Hedhi au Nifasi kabla ya
kuzama Jua
iv)Kunuia au kukusudia kuvunja Swaumu kwa hali yoyote
ile
v)Kufanya tendo la Ndoa makusudi
vi)Kujitoa Manii makusudi wakati umefunga.
9 - MAMBO YANAYODHANIWA KUWA YANAHARIBU
SWAUMU , KUMBE HAYAIHARIBU .
a)kula au kunywa bila kukusudia
b)Kuoga wakati umefunga
c)Kutokwa na Manii bila kukusudia
d)Kuamka na Janaba
e)Kwa wana Ndoa kubusiana au kukumbatiana
f)Kupiga MSWAKI,kusukutua,kuosha Masikio au Puani
g)Kupaka Wanja ,Mafuta ,kufukiza Ubani ,Kuweka Dawa
Machoni .
h)Kumeza usichoweza kujizuia nacho
i)Kupiga Sindano
j) Kuumika ( kupiga chuku ) au kuumia na kutokwa na
Damu.
- FUNGA ZA SUNNA
1 – Aina hii ya FUNGA inakusaya Funga nyingi , mfano :
i)Kufunga siku tatu kila Mwezi
ii)Kufuga Jumatatu na Alhamisi
iii)Kufunga siku sita za Mwezi wa Shawwal
iv)Kufunga Arafa
v)Kufunga Ashuuraa
vi)Funga za Mwezi wa Shaaban

TUTAENDELEA SOMO LIJALO NA MLANGO WA


SWAUMU.

You might also like