You are on page 1of 2

URAIA

1.Lipi kati ya mashirika yafuatayo ya UN linashughulikia masuala ya chakula? A. UNICEF B. UNESCO C.


FAO D. ILO E.AU.
2. Umoja wa nchi huru za Afrika uliundwa mwaka: A. 1963 B. 1953 C. 1973 D. 1961 E.1954.
3. Tanzania iliingia katika mfumo wa vya vingi mwaka: A. 1990 B. 1992 C. 1985 D. 1995 E.1964.
4. Chombo cha sheria kinachosimamia sheria za nchi zitekelezwe barabara ni: A. Bunge B. Tume ya
Msekwa C. Jeshi la polisi D. Mahakama E.Sungusungu.
5.Kesi ya mauaji hutolewa hukumu na mahakama ipi nchini Tanzania? A. Mahakama alikofanya mauaji
B. Mahakama kuu C. Mahakama yoyote ile D. Mahakama ya rufaa E.Mahakama ya mwanzo.
6. Maana halisi ya Mapinduzi ni ipi? A. Serikali kutawaliwa na wana mapinduzi halisi B. Mabadiliko katika
jamii yanayoleta maendeleo kwa walio wengi C. Kumiliki njia kuu za uchumi D. Mabadiliko ya kijamii
kisiasa E.Mabadiliko ya familia kwa ujumla.
7.Mwaka 2019 Dr. John Pombe Magufuli alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa jumuiya ipi kati ya zifuatazo?
A. Umoja wa Afrika B. Jumuiya ya Afrika Mashariki C. Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa
Afrika D. Jumuiya ya Madola E.Soko la pamoja la nchi za SADC.
8. Mwananchi aliyepatikana na hatia ya kutenda kosa la jinai anaweza kupewa adhabu ya: A. Huonywa
vikali B. Kulipwa fidia C. Kuwekwa kizuizini D. Kulipa fidia E.Kuwekwa rumande.
9. Chombo kipi kati ya hivi vifuatavyo husimamia fedha hapa Tanzania? A. Maduka ya kubadilishia fedha
B. Benki Kuu ya Tanzania C. Wizara ya Fedha D. Benki ya Taifa ya Biashara E.Ikulu.
10. Ni shirika lipi la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia hifadhi ya utamaduni wa jamii? A. HABITAT B.
UNEP C. UNICEF D. UNESCO E.UNCTAD.
11. Jukumu kubwa la Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni: A. Kuteua mawaziri B. Kumteua
Rais C. Kutunga sheria D. Kuhukumu wahalifu E.Kusimamia uchaguzi.
12. Pamoja na kusababisha magonjwa na kuharibu mazingira, serikali bado inahimiza kilimo cha zao la
tumbaku kwa sababu: A. Inawajali sana wavuta sigara B. Mauzo ya tumbaku na sigara huiingizia serikali
pato kubwa C. Inaendeleza kilimo kilichoanzishwa na wakoloni D. Ya msukumo kutoka soko la dunia
E.Tumbaku ni muhimu sana kwa utengenezaji wa dawa.
13. Mojawapo ya athari za biashara ya utalii ni: A. Uharibifu wa mazingira B. Kutoroshwa kwa baadhi ya
vijana C. Kuvurugwa biashara ya ndani D. Watalii kukataa kurudi kwao E.Kuvurugwa utamaduni wetu.
14. Ulinzi na usalama katika familia ni jukumu la: A. Baba B. Baba na mama C. Baba na watoto wa kiume
D. Wanafamilia wote E.Wanamgambo.

HISTORIA

15. Mazao yaliyoletwa Afrika ya Mashariki na Wareno ni pamoja na: A. Mihogo na kahawa B. Kahawa na
karafuu C. Mahindi na mihogo D. Mkonge na mihogo E.Ndizi na korosho.
16. Mataifa ya Ulaya yaliyokuwa yanapigania mto Nile yalikuwa: A. Ufaransa na Ubelgiji B. Uingereza na
Ujerumani C. Ufaransa na Ureno D. Uingereza na Ufaransa E.Ubelgiji na Ureno.
17. Mapambano ya kudai uhuru katika bara la Afrika yalianza baada ya: A. Kuundwa kwa Umoja wa
Mataifa B. Kusambaratika kwa Umoja wa Kisovieti C. Vita kuu ya pili ya dunia D. Kupigwa marufuku
biashara ya watumwa E.Kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi.
18. Michoro ya mapangoni iliko kondoa Irangi inasadikiwa kuchorwa wakati wa zama za ……………………….
A. Mwanzo za mawe B. Kati za mawe C. Mwisho za mawe D. Chuma E.Ugunduzi wa moto.
19. Mkataba wa kufunga soko la watumwa la Zanzibar ulisainiwa mwaka …………………….. A. 1882 B. 1845
C. 1885 D. 1884 E.1873.
20. Ipi kati ya nchi zifuatazo ilipata uhuru kwa njia ya vita? A. Zimbabwe B. Tanganyika C. Ghana D.
Malawi E.Zambia.
21. Utafutaji wa njia ya kwenda India ulifadhiliwa na …………………… A. Vasco Da Gama B. Bartholomeo
Diaz C. King Henry D. Cecil Rhodes E.Henry Stanley.
22. Mkataba wa kwanza uliotiwa saini mwaka 1822 kukomesha biashara ya watumwa Tanganyika na
Zanzibar uliitwa: A. Mkataba wa Moresby B. Mkataba wa Frere C. Mkataba wa Heligoland D. Mkataba
wa Hamerton E.Mkutano wa Berlin.
23. Kundi lipi la mawakala wa ukoloni lilikuwa la kwanza kuja Tanganyika? A. Wamisionari B.
Wafanyabiashara C. Walowezi D. Wapelelezi E.Mabaharia.
24. Tanganyika ilipata uhuru wake kwa njia ya: A. Matumizi ya bunduki B. Vita vya msituni C. Mikataba
ya kilaghai D. Kikatiba E.Matumizi ya veto.
25. Hadi kufikia mwaka 1914, nchi zilizokuwa huru barani Afrika zilikuwa: A. Tanganyika na Zanzibar B.
Ethiopia na Liberia C. Ghana na Misri D. Somalia na Jibuti E.Afrika ya Kusini na Rwanda.
26. Umoja wa hiari wan chi huru zilizowahi kutawaliwa na Uingereza hufahamika kama: A. Jumuiya ya
Madola B. Umoja wa Mataifa C. Nchi zinazoendelea D. Umoja wa Afrika E.Shirikisho la Mataifa.

You might also like