You are on page 1of 21

CHUO KIKUU CHA MOI

BEWA KUU

KITIVO CHA SANAA NA SAYANSI ZA KIJAMII

IDARA. :KISWAHILI NA LUGHA NYINGINE ZA KIAFRIKA.

JINA. :HELLEN.M.NYAMWEYA

NAMBARI YA USAJILI:MS/KIS/5467/21

KOZI. : TRANSLATION TOOLS

MSIMBO WA KOZI: KIS 815

MHADHILI. :PROF. MOSOL KANDAGOR

KAZI. : 1) Dhana na dhima ya vifaa vya tafsiri

2) Vifaa vya tafsiri (Tarakilishi)

3) Programu za kutafsiri, ujuzi na maarifa.

MWAKA. :2020/2021

MUHULA. :KWANZA

TAREHE. : 03/03/2022

VIFAA VYA TAFSIRI


Dhana ya vifaa vya tafsiri

Tuki; Inaeleza kuwa vifaa vya tafsiri ni vyombo ambavyo hutumika kutoa andiko au maelezo
fulani kutoka lugha moja hadi nyingine.

Ni vyombo vya kutafsiri au kuhawilisha mawazo katika maandishi kutoka lugha moja hadi
lugha nyingine

Kwa kutambua umuhimu wa maendeleo ya sayansi na teknolojia katika ukalimani, Manguli


na Wabobezi katika fani hii waliamua kukiweka kipengele hiki Cha matumizi ya teknolojia
kuwa ni moja ya Kanuni namba nane kwa ujumla Kanuni hii pamoja na mambo mengine
inamtaka mkalimani popote alipo kujihusisha na teknolojia katika kuhakikisha anakuwa wa
kileoleo, yaaani anapata maarifa kwa kujiendeleza yeye mwenyewe katika kujifunza njia bora
na za kisasa za ukalimani. Jambo jingine linalotiliwa mkazo katika Kanuni hii ni kwa
mkalimani kufanya juhudi binafsi kuhakikisha anajua kutumia vizuri vifaa hivi vipya vya
kiteknolojia kimsingi utumizi wa teknolojia katika ukalimani si kitu Cha kuhoji ama kujiuliza
mara mbili hasa kwa maendeleo ambayo dunia ya leo imeyafikia.

Mills na Tilden wakinukuliwa na Beck na Cable (1998) Wanadai ya kuwa hakuna namna
mkalimani atakwepa kutumia vifaa vya kiteknolojia , bali yampasa mkalimani kuhakikisha
anatumia vizuri vifaa hivyo na kwa uangalifu mkubwa.

Dhima ya vifaa vya tafsiri

 Husaidia kurahisisha mawasiliano miongoni mwa wanajamii wanaozungumza lugha


tofautitofauti.
 Hutumika Kama njia ya kujipatia kipato.
 Vifaa vya tafsiri hukuza utalii nchini.
 Hutumika kupitisha sera kwa wananchi na hukuza siasa za nchi.
 Hutumika katika mawasiliano na watu wazungumzao lugha tofauti na hivyo kukuza
biashara.
 Huwaunganisha watu wenye lugha na utamaduni tofauti na kuwafanya wawe wamoja.
 Hutumiwa na watu kujifunza lugha na utamaduni watu wengine.

1)TARAKILISHI/TAFSIRI KOMPYUTA

SEHEMU ZA TARAKILISHI

Kiwambo(Skrini)
Bao kuu

C.P.U(Bongo kuu)

RAM( Kumbukumbu ya muda)

Kadi za nyongeza Kama vile kadi mchoro n.k

Ugawi wa umeme

Kiendeshi (CD)

Kiendeshi disk kuu (HOD- Kumbukumbu)

Baobonye

Puku

1)TARAKILISHI

Kompyuta au TARAKILISHI katika tafsiri ya Kiswahili ni kifaa au mashine ambayo


inafafanua na kunyambulisha/ kuchakata habari isiyo rasmi kwenda katika habari rasmi
ambayo mtumiaji au mtu anaweza kuielewa na kuifanyia kazi kutokana na maelekezo
kiliyopewa na mtu.

Hivyo Kompyuta Kama Kompyuta kwa hakiki haifanyi kazi bila kupewa maelekezo.

Bila kupewa maelekezo ifanye Jambo gani Kompyuta ni Kama kopo!.

Hii inabadilisha kabisa kabisa Imani kuwa Kompyuta inafanya kazi kuliko binadamu na
kwamba Ina uwezo wa juu kuliko hata ubongo wa binadamu!

Bila binadamu Kompyuta haiwezi kuwapo.

Kompyuta ni kifaa ambacho hakika kimebadilisha maisha ya binadamu katika karne ya


ishirini na kuweza kufanya kuwa rahisi zaidi kwa maana ya kutenda kazi kwa ufanisi wa hali
ya juu.

Neno Kompyuta kwa kimombo 'computer' linatokana na neno 'computing' likiwa na maana
ya kukokotoa au kuchanganua hesabu kama; kujumlisha, kugawanya, kutoa na kuzidisha.

Kompyuta Ina historia ndefu kutoka katika kipindi Cha kabla ya kuzaliwa kwa Kristi ambako
watu mbalimbali Kama Charles Babbage.
Lakini kifaa Cha kwanza kabisa ambacho kinafanana kiutendaji na Kompyuta ya leo hii
kiligunduliwa mnamo karne ya 20 (kati ya mwaka (1940-1945) ingawa nadharia ya
Kompyuta na mashine mbalimbali zilizo fanana nayo zilikuwapo hapo mwanzoni

Mfululizo wa ugunduzi wa Kompyuta ambazo zilikuwa na nguvu ya kutosha kufanya


hisabati na hata kutunza kiasi kidogo Cha kumbukumbu ulifanyika kati ya miaka ya 1930 na
1940.

Utumiaji wa vifaa vya ki-eletroniki katika Mfumo wa digital ambao uligunduliwa na


kuendelezwa kwa kiasi kikubwa na mtu aliyeitwa Claude Shannon mnamo mwaka 1937
ulifanikisha kwa kiasi kikubwa kuimarisha ubora wa Kompyuta hizo.

Kompyuta inaweza kuelezewa kuwa imepitia hatua kadhaa katika kufikia ubora iliyonayo
sasa.

Kati ya miaka ya 1940 mpaka miaka ya 1950.Kompyuya ilikuwa ikitengenezwa kwa


teknolojia iliyojulikana Kama Vacuum tube. Hii ilikuwa ni teknolojia ambayo ilikuwa
ikitumia tubes ndogo mfano wa vichupa vidogo ambavyo viliondolewa hewa ndani na
kuvitengeneza katika mfumo ambao viliweza kupitisha umeme ambao ndio uliunganishwa
katika chombo kizima kwa ajili ya kufanya kazi kwa kutumia mtiririko wa elektron ambao
umefanywa katika mfumo maalum.

Mfano wa Kompyuta hizi ni Konrad Zuse's electromechanical au" Z machines " au Z3(1941),
Atanasoff- Berry computer (1941), Colossus Computer(1944) ambayo ilitumika kwa ajili ya
shughuli za Siri katika jeshi la Uingereza na ilitumika katika kupata taarifa za Siri za jeshi la
Ujerumani katika kupata taarifa za Siri za jeshi la Ujerumani katika vita vya pili vya dunia,
Harvard.

Mark(1944) na Kompyuta iliyotumika na Jeshi la Wamarekani iliyojulikana Kama ENIAC.

Hata hivyo teknolojia hii ya vacuum tubes ilitumika mpaka mwishoni mwa miaka ya 1950 na
mwanzoni mwa miaka ya 1960 kulizinduliwa teknolojia mpya inayofahamika Kama
"transistor technology".

Kompyuta zilizotumia teknolojia hii ziliweza kufanya kazi kwa urahisi zaidi, hazikuwa ghali
sana, zilitumia umeme mdogo zaidi na ziliweza kufanya kazi kwa uhakika zaidi kuliko zile za
mwanzo
Kumbuka kuwa Kompyuta za mwanzo zilikuwa na ukubwa sawa na chumba kikubwa Cha
nyumba!.

Teknolojia ambayo mpaka sasa inatumika katika utengenezaji wa Kompyuta inaitwa


integrated circuit technology.

Teknolojia hii ilizinduliwa mnamo miaka ya 1970.

Teknolojia hii ndiyo imesababisha kuzaliwa kwa Kompyuta ambazo ni ndogo zaidi kuweza
hata kubebwa katika kiganja Cha mkono!.

Hii ni sababu ya kuundwa kwa kifaa kijulikanacho Kama microprocessor ambacho ndicho
Kama ubongo wa Kompyuta.

Kifaa hiki kina umbo mdogo sana lakini kina jumla ya zaidi ya transistor (sakiti ndogondogo
zinazofanya kazi kwa ushirikiano) milioni moja!.

JINZI AMBAVYO TARAKILISHI HUFANYA KAZI

Electronic kifaa Cha Tafsiri ya lugha hutegemea akili ya bandia kuchakata maneno na
kuyatafsiri katika lugha mpya.

Huweza Kusaidia hadi lugha 170 na vinaweza kulishwa habari kwa njia anuwai.

Mtafsiri wa elektroniki wa mfano hufanya kazi kwa njia zifuatazo;

I)Tafsiri ya sauti- Kifaa kile hutumia spika na kadi ya kumbukumbu kurekodi ujumbe

-Kifaa husikiza maneno yasemwayo Kisha huyasikiza kwa makinina


kuyaelewa k

Kisha kuyachanganua maneno Yale.

ii)Tafsiri ya picha- Mtu huchapisha maneno /picha Kisha kifaa hutumia kamera kuyaona

maneno Yale na kuyachambua.


- Kisha huweza kutafsiri maneno yale yaliyo kwenye maandishi au picha.

UMUHIMU WA TARAKILISHI KAMA KIFAA CHA TAFSIRI

1)Huwezesha watu Kuwasiliana kwa urahisi nje ya nchi- Kutembelea nchi zingine na
kuelewa lugha yao.

2) Kupanua biashara yako- Ni ngumu kuanzisha tawi katika nchi nyingine iwapo hakuna mtu
ofisi yako anayezungumza lugha ya nchi hiyo.

2) PROGRAMU ZA KUTAFSIRI

TAFSIRI YA GOOGLE HUTUMIKA KWA NJIA IPI KWA MFANO;

Naanza kwa kuchagua lugha ambayo nataka kutafsiri kwenye orodha iliyopo

Basi mimi kuchagua lugha ambayo nataka kuwa na Tafsiri kutoka kwa orodha sawa ya lugha
zilizopo.

Kisha mimi kuandika neno ,Mimi kushinikiza kwenda na mimi kupata Tafsiri!.

Na kama sijui jinsi ya kuandika, naweza kubonyeza kipaza sauti na kusema neno na Tafsiri
ya Google itanipa tafsiri yake.

Naweza hata kubofya kamera na programu itafsiri moja kwa moja maneno yaliyoandikwa
kwenye karatasi au Skrini

-Rasilimali zingine za kutafusili pamoja na goole ni Kama; Word reference

Duolingo

Mfano; Programu hii ya kijani ni Duolingo . Kwa hiyo, baada ya kuunda akaunti ,anaweza
kuingia , bonyeza kitufe kwenye kona na Kisha bofya kwenye "plus cours".

Kwa 'default', itakuwa kwa watu wanaozungumza lugha ya kiingereza , lakini ikiwa unapita
chini, utaweza kutafuta na kuchagua lugha yako.

TAFSIRI YA MSAADA WA KOMPYUTA

Mchakato halisi wa kutafsiri hufanyika ndani ya Smartling na zana iliyojengwa katika tafsiri
ya msaada wa Kompyuta (CAT)
Pamoja na CAT ya Smartling, Muktadha wa kuona hutolewa kila wakati kwa watafsiri, na
kuwezesha watafsiri kuelewa ni nini maudhui wanayotafsiri na jinsi maneno yao yanavyofaa
katika muktadha huo.

Mara tu Tafsiri yenyewe imekamilika, watafsiri wanaweza kuhamia haraka kwa shukrani ya
kazi inayofuata kwa uelekezaji otomatiki

Smartling pia inafanya kazi ya kufanya kazi ya waatafsiri wa kibinadamu iwe rahisi
iwezekanavyo pia.

Vifaa Vingine Vya Kutafsiri Lugha Vitumiavyo Programu Za Kutafsiri Ni Kama;

-Kifaa Cha kutafsiri Cha Lincom.

-Kifaa sahihi Cha tafsiri ya lugha

- Tafsiri ya sauti ya sauti ya pesa.

-HI-RES 3.0 INCHI IPS TOUCH SCREEN & SPIKA WAZUNGUMZA.

-WIFI/HOTSPOT/OFFLINE/BLUETOOTH 4 WAY TAFSIRI YA SAUTI YA SAUTI YA


LUGHA.

KAZI AMBAYO PROGRAM ZA KUTAFSIRI HUFANYA

i)Muktadha wa kuona- Watafsiri wanaweza kukagua kazi yao moja kwa moja, kwa muundo
wowote.

ii) Kumbukumbu ya tafsiri ya wakati halisi

iii) Udhibiti wa toleo- Yaliyomo tu, yaliyopakuliwa ni yaliyomo ya zamani yanatafsiriwa


kutoka kwa kumbukumbu ya programu.

iv) Mali ya bidhaa- Rasilimali kwa miongozo ya toni na chapa.

v) Jumuishi ya ukaguzi wa ubora- Ukaguzi wa ubora- wa wakati halisi husaidia kuokoa


usahihishaji wa wakati.

vi) Shortcuts za kinanda- Okoa wakati kwa kila kitendo.

vii) Unganisha kamba- Unganisha sehemu ya kitufe kimoja tu!.

viii) Utunzaji wa tag rahisi- Inatumia ujifunzaji wa mashine kuweka vitambulisho kwa
usahihi.

ix) Utaratibu wa moja kwa moja- Programu inaweka yaliyomo kusonga na inasababisha moja
kwa moja tafsiri iliyokamilishwa kwa hatua inayofuata.
x) Ujanibishaji unaotokana na data- Programu sio tu! Inawapa wateja data ya wakati halisi
juu ya mchakato wao wa kutafsiri, lakini pia ni busara ya kutosha kuwafanyia maamuzi.

xi) Muktadha wa kuona- Watafsiri wanapaswa kuona maneno kwa muktadha ili kutoa kazi ya
hali ya juu. Bila hivyo, uzoefu wa mtumiaji wa mwisho unateseka.

3) UJUZI/MAARIFA

UJUZI- Ni kufahamu, kujua, kuelewa hali, habari na maelezo yanayohusu mazingira


tunapoishi. Tunapata ujuzi kwa maarifa yetu au kwa njia ya kufundishwa tukitazama,
kutambua, kulinganisha na kutafakari Yale tuliyoona na kujifunza.

MAARIFA- Ni njia inayotumiwa kujitoa katika shida ama kuweza kupata kitu kwa kutumia
elimu au ujuzi. Ujuzi huo unaweza ukawa wa kuzaliwa nao au ukatokana na mangamuzi ya
maisha yakiwa pamoja na kusoma, kusikia au kutenda, pia huhusisha ufahamu na uelewa.

Sifa Za Mtafsiri Mwenye Ujuzi na Maarifa.

a)Awe mahiri wa lugha mbili zinazohusika- Kuwa mahiri ni kujua vizuri nyanja mbalimbali
za isimu ya lugha husika Kama vile; fonolojia( matamshi), fonolojia (maumbo),
Sintaksia(muundo).

b)Ajue vizuri utamaduni wa watu mbalimbali.

c) Ajue aghalau lugha mbil.i

d) Awe na maarifa ya TEHAMA (ICT)

e)Awafahamu watu, jamii na utamaduni wao- Mitazamo kuhusu watu, Mitazamo kuhusu
wanyama.

f)Apende kujisomea na kujiendeleza kulingana na mabadiliko ya jamii mfano kusoma vitabu,


majarida, magazeti mbalimbali kusikiliza redio na kuangalia Tv.

g)Awe mwandishi bora.

Maadili Ya Mtafsiri Bora Mwenye Ujuzi/Maarifa

a) Awe mwaminifu kwa matini na kwa Mwenye matini; Yaani asipotoshe habari au kusema
uongo.

b) Awe mchapakazi (kujituma/ Bidii katika kazi).


c) Awe nadhifu- Unadhifu- mwonekano wa moyo, asiwe tapeli/ laghai.

d)Aelewe/ kuelewa taratibu za kazi na kuzifuata. Mfano; bei ya kutafsiri kwa ukurasa au kwa
maneno.

e) Ushirikiano/ kushirikiana na watu mbalimbali wa fani mbalimbali ,makundi mbalimbali,


ikiwa pamoja na wafasiri wenzake.

Taaluma Nyingine Zinazohusiana na Mtafsiri Mwenye Ujuzi na Maarifa

a)Inauhusiano na Isimulinganishi- Isimulinganishi- hujishughulisha na kulinganisha


vipengele mbalimbali vya kiisimu vya lugha mbili au zaidi, pamoja na kuchunguza mbinu za
ulinganishi huu.

Uhusiano wake na tafsiri- humsaidia mtafsiri kuelewa mifumo ya lugha mbalimbali na jinsi
lugha hizo zinavyotumia vipengele vyake vya kiisimu kutolea taarifa mbalimbali.

b) Inahusiana na Isimujamii- Isimujamii inahusika na kuchunguza uhusiano kati ya lugha


fulani na jamii ambayo inatumia lugha hiyo. Rejesta mbalimbali za kijamii pamoja na
maingiliano baina ya lugha . Ujuzi wa isimujamii unamsaidia mfasiri kufahamu athari
zinazotokana na mahusiano baina ya lugha na jamii husika na kuzingatia mambo mbalimbali
katika kutafsiri.

c)Inauhusiano na Semantiki/Pragmantiki- Semantiki ni taaluma inayochunguza maana ya


maneno katika upweke na katika makundi/taaluma inayochunguza maana ya maneno. Kwa
kuwa kinachotafsiriwa ni maawazo au maana ya matini siyo neno( pwekepweke) basi ujuzi
huu wa Semantiki utamwezesha mfasiri kujua au kungamua kuwa maana ya matini hiyo
haitokani na maana ya neno mojamoja badala yake inatokana na maana ya neno mojamoja
badala yake inatokana na maana ya kimatumizi kwa ujumla katika muktadha mahususi.

d)Inauhusiano na Elimumitindo- Hii inahusu uainishaji wa mitindo mbalimbali ya lugha na


miktadha ya Matumizi yake.

e) Elimumitindo( Mitindo mizingi ya kutumia)- Taaluma hii ya Elimumitindo itawezesha


mfasiri kubaini mtindo wa matini chanzi ambao haunabudi kuhamishwa katika matini
lengwa.

f) Inauhusiano na mantiki- Mantiki- inahusu ukweli na uhakika au usahihi wa mambo Kama


inavyosemwa, kuandikwa au kuaminika kwa watu. Mantiki humsaidia mfasiri kubaini kauli
zisizo dhahiri na zinazokanganya katika matini chanzi ili azirekebishe kwanza kabla ya
kuanza kutafsiri.
Umuhimu /Dhima Za Tafsiri

a) Ni njia ya mawasiliano kati ya watu au jamii mbili zinazotumia lugha tofauti mfano;
maelezo mbalimbali ya jinsi ya kutumia bidhaa mbalimbali Kama redio na simu.

b) Ni nyenzo ya kuelezea utamaduni kutoka jamii moja kwenda jamii nyingine mfano;
kupitia dini- Tafsiri ya Biblia au Kuruani.

c) Ni mbinu ya kujifundisha lugha kimsamiati na kisarufi.

d)Ni kazi ya ajira Kama kazi nyingine , hivyo huweza kumpatia mtu kipato.

e) Humliwaza mfasiri ; hii ni baada ya kumaliza kufasiri.

4) CHANGAMOTO/ MATATIZO YA VIFAA VYA TAFSIRI KATIKA ENZI ZA


TAFSIRI

UTANGULIZI

Kuna changamoto mbalimbali zinazowakabili wafasiri zinazotokana na vifaa vya tafsiri


Kama vile tarakilishi na kamusi. Matumizi ya tarakilishi katika tafsiri yamekuja na
changamoto tele kwa sababu ya utandawazi. Maingiliano kati ya watu wamesababisha
mahitaji makubwa ya tafsiri katika nyanja ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Mahitaji hayo
ndiyo yamesababisha uvumbuzi kuhusu matumizi ya tarakilishi katika tafsiri. Mtindo huu
sasa unajulikana Kama tafsiri mashine.

CHANGAMOTO

a) Mashine za tafsiri hutegemea data ya ujozi-lugha ambayo hutokana na utafsiri wa


wataalamu.

b) Mashine za tafsiri huitaji data ili kuwezesha uwezo wa kutafsiri.

c) Data za kutafsiri huitaji huhitaji utafitiwa kina kuhusu lugha mbalimbali ili kutunga
kamusi faafu za kuzipa mashine hizi uwezo.

d) Mashine za tafsiri hazina uwezo wa kufanya tafsiri zinazohusu lugha nyingi za ulimwengu
ambazo hazina data.

e) Lugha nyingi za kiafrika hazina data katika mashine za kutafsiri.

f) Lugha nyingi hazijasanifishwa wala hazitumiki katika ufundishaji au mawasiliano mapana


na hivyo kupata ugumu katika kutafsiri lugha hizo.

g) Lugha nyingine zipo hatarini kupotea na hivyo, harakati za kutunga data katika lugha hizi
zinaweza kukabiliwa na matatizo hasa iwapo juhudi hazitafanywa kuokoa lugha hizi.

h)Changamoto la miundo ya lugha pia nyeti kwa tarakilishi.


i) Tafsiri mashine hukabiliwa na changamoto mingi za kiisimu

j) Changamoto ya semantiki huweza kuathiri matumizi ya tarakilishi katika tafsiri.

k) Mchakato wa tafsiri huhitaji tajriba au ujuzi na uzoefu ambao mashine Kama tarakilishi
hazina

l) Kubadilika kwa lugha pia huathiri tafsiri ya sentensi kwa sababu lugha zote za ulimwengu
hubadilika kulingana na wakati, msamiati uliopo huzeeka na mwingine mpya kuzuka na
kuanza kutumiwa na katika hali hii tafsiri ya tarakilishi hukabiliwa na upungufu iwapo
hakutakuwa na juhudi za kufanya mabadiliko ili kuzifanya mashine hizo ziendane na miundo
ya lugha zinazohusika.

m) pia changamoto ya ubora wa tafsiri wa taarifa zilizofanyiwa tafsiri kwa njia ya mashine
Kama vile changamoto za misamiati huzuka iwapo wataalamu wa tafsiri watachelewa kubuni
misamiati ya kurejelea teknolojia mpya.

HITIMISHO

Imebainika katika makala haya kwamba ingawaje utandawazi umekuja na manufaa mengi
kwa huduma za jamii ikiwamo utoaji wa huduma za tafsiri, Kuna pia changamoto nyingi
ambazo zimeandamana na manufaa hayo. Imebainika kwamba vifaa mbalimbali vya tafsiri
vimekabiliwa na changamoto nyingi ambazo zimewalazimu watafsiri na wasaidizi wao
kupanga mikakati ya kuyasuluhisha . Mikakati hii imekuwa na gharama ambayo watafsiri na
wasaidizi wao wanalazimika kumudu ili kufanikisha kaazi yao. Baadhi ya changamoto
ambazo zimeibuliwa na utandawazi ni zile zinazotokana na tamaduni. Imebainika kwamba
watafsiri na wasaidizi wao sharti wafahamu utamaduni wa matini asilia pamoja na waandishi
wao ili kufanikisha tafsiri zao.

Changamoto ya dini nayo inalazimu wafasiri kufanya utafiti kuhusu dini iliyoathiri matini
asilia ili kuwasaidia kuelewa matini asilia. Changamoto nyingine ni zile zinazotokana na
Kuwepo kwa teknolojia mpya ambayo imekuwa ala muhimu katika mchakato wa tafsiri.

Changamoto hizi zinasababisha hali ambapo watafsiri na wasaidizi wao wanalazimika


kujiandaa kifedha na kuhakikisha kwamba wanajihami na teknolojia mpya ya habari na
mawasiliano.

Vilevile, wafasiri wanatakiwa kupata mafunzo ya kila mara ili kuinua kiwango chao Cha
maarifa na ujuzi unaoendana na mabadiliko katika teknolojia mpya kuhusiana na utoaji wa
huduma za tafsiri.
MAREJELEO

Mwasoko, H.J.M na wenzake. (2003). Kitangulizi Cha Tafsiri. Nadharia na Mbinu. Dar es
Salaam: TUKI.

TUKI.(2003). Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Kenya.Oxford University Press.

Wanjala. S. (2011). Misingi ya Ukalimani na Tafsiri. Tanzania: Serengeti Educational.

Chomsky,N.(2006)."Noam Chomsky chats with washington post Readers" katika The


washing post, imesomwa mtandaoni Machi 24,2020.

Steiner,G.(1975). After Abel: Aspects of Language and Translation. Oxford: Oxford


University Press.

Aspiration(2008). Open Translation Tools: Disruptive Potential to Broaden Access to


Knowledge.

Costales,A.F.(2011)."Translation 2.0: Facing the challenge of the global erra". Linguistics


Antverpiesia. Toleo jipya. Kur. 179-194..
CHUO KIKUU CHA MOI

BEWA KUU

KITIVO CHA SANAA NA SAYANSI ZA KIJAMII

IDARA. :KISWAHILI NA LUGHA NYINGINE ZA KIAFRIKA.

JINA. :HELLEN.M.NYAMWEYA

NAMBARI YA USAJILI:MS/KIS/5467/21

KOZI. : RESEARCH METHODS

MSIMBO WA KOZI: KIS 895

MHADHIRI :PROF. MOSOL KANDAGOR

KAZI. : a) Mbinu za kukusanya data.

Uchunguzi nyanjani

Uchunguzi shirikishi/Usoshirikishi.

MWAKA. :2020/2021

MUHULA. :KWANZA

TAREHE. : 03/03/2022
1)DHANA YA UTAFITI

Utafiti ni uchunguzi unaotumia mbinu za kisayansi katika kutafuta taarifa juu ya Jambo
fulani.

Utafiti hutumika kuanzisha au kuthibitisha ukweli, Kuthibitisha matokeo ya kazi ya awali


kutatua matatizo mapya au yaliyopo kuendeleza nadharia mpya pia upanuzi wa kazi ya
zamani.

Utafiti hujumuisha kazi ya ubunifu ambayo hufanywa kwa misingi ya utaratibu ili kuongeza
maarifa ya elimu mfano; Ujuzi wa wanadamu.

Utamaduni na jamii.

Maatumizi ya ujuzi wa kuunda maombi mapya.

1.1. AINA ZA UTAFITI

a) Utafiti wa msingi

b) Utafiti wa matumizi

UTAFITI WA MSINGI

Ni utafiti unaolenga kupata maarifa au mawazo mapya juu ya tabia ya viasili vinavyoweza
kubadilika kukiwepo hali fulani.

Utafiti wa namna hii huzingatia sana kutumia matokeo yake kwa kutatua tatizo. Mfano;
kufanya Jambo ambalo halijawahi kufanywa ili kupata jibu.

UTAFITI WA MATUMIZI

Ni utafiti unaojihusisha na Kuthibitisha mambo muhimu katika jamii.

1.2. UTARATIBU WA UTAFITI

1.2.1. Ainisha mada ya utafiti- Chagua mada moja utakayo ishughulikia baada ya kusoma
kazi kadhaa za watangulizi katika uwanja unaotaka kushughulikia. Kwa mfano; sababu
ambazo zinaawafanya wanafunzi wengi kuwa watukutu shuleni katika nyakati hizi tunazo
ishi
1.2.2 Fafanua tatizo la utafiti- Changanua tatizo ambalo umelichagua kwa undani ili
kulielewa zaidi kabla ya kuanza kulishughulikia na baada ya kusoma kazi kadha za
kinadharia katika uwanja huo.

1.2.3. Eleza madhumuni na malengo ya utafiti- Tambua Jambo ama sababu la kufanyia utafiti
ili kumfanya mtafiti kuangazia suala moja na lifaalo katika kazi yake.

1.2.4. Eleza nadharia tete zitakazoongoza utafiti wako- Tambua njia au mwelekezo utakao
utumia katika kazi uliyo ichagua kati ya zingine.

1.2.5. Jadili machapisho yaliyoshughulikia suala hilo na onyesha dosari na mapengo yake-
Mtafiti anapaswa kuangalia kazi iliyofanywa mbeleni ili kulitambua Jambo ambalo bado
halijaangaziwa na watafiti waliomtangulia.

1.2.6. Onyesha namna utafiti wako utakavyorekebisha dosari na kuziba mapengo hayo na
matarajio yako- Angalia Kama jawabu lako litaleta suluhisho na kuziba pengo zilizoko .

1.2.7. Eleza mbinu na njia za utafiti zitakazotumika, pamoja na usampulishaji wa watafitiwa


au wa data iwapo utahitajika- Njia inayotumiwa katika utafiti huchangia zaidi katika
kumwezesha mtu kufanya utafiti wa kutegemewa.

1.2.8. Eleza nadharia za kiuchambuzi utakazotumia kuchambua data zako- Njia zitumikazo
katika uchambuzi pia husaidia sana katika kuifanya kazi yako kuwa ya kuaminika.

1.2.9. Onesha ratiba ya utafiti- Panga kazi yako ukianzia na Jambo utakalo lifanya kuanzia la
kwanza hadi la mwisho ili kuwa na mwelekeo wa kazi yako unao onekana.

1.2.10. Onyesha makisio ya bajeti ya utafiti-, bajeti iwiane na ahughuli zitakazo fanyika-
Mtafiti anapaswa kuhakikisha amepiga bajeti ya pesa aatakazo hitaji katika kazi yake ili
kujipanga kuzipata pesa hizo.

1.2.11. Weka orodha ya marejeleo- Mtafiti anapaswa kuorodhesha nakala ambazo aatarejelea
katika kuandika na kufanya utafiti wake

1.2.12. Ambatisha maswali, vidadisi na zanaa nyingine za utafiti atakazozitumia- Vifaa


vitakavyo tumika katika utafiti zinapaswa kuwekwa pamoja ili Mtafiti kuianza kazi yake.

2)DHIMA YA UTAFITI (KIJUMLA)

Umuhimu wa utafiti kaatika taaluma ya Kiswahili katika maeneo mbalimbali ni Kama


ifuatavyo;

a) Utafiti na kujisomea

Utafiti huu utakuwa na umuhimu kutumika Kama rejeleo muhimu katika tafiti za baadaye
kuhusiana na ushairi wa kimapokeo na ule wa kisasa kwa mfano.
Vilevile, utafiti huu hutumika Kama kitabu ama rejeleo kwa wanafunzi wa ngazi za shahada
ya kwanza, uzamilifu katika taaluma za fasihi ya Kiswahili.

b) Kitamaduni

Utafiti huu utaonesha masuala ya kiutamaduni katika jamii za mwambao na jamii za bara.
Kwa kuzibaini tamaduni hizo itakuwa rahisi kwa msomaji na Mtafiti ama mhakiki yeyote
yule kuzielewa kwa undani pale aanapotaka kutumia tamaduni hizo katika maandishi yake.

c)Kinadharia

Katika ngazi ya elimu ya sekondari,utafiti huu utakuwa na umuhimu kwa watunzi sera na
mitaala ya elimu kwamba, wanapotunga mitaala hiyo kuhusu fasihi ya Kiswahili kwa ujumla
na ushairi mahususi wazingatie mambo gani yanayopaswa kuigizwa katika mitaala hiyo.

d)Kihistoria

Utafiti huu utakuwa sehemu mojawapo ya muendelezo wa maendeleo ya historia ya


Kiswahili tangu kupatikana kwa uhuru mpaka kufikia leo.

Baada ya kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika, historia ya ushairi wa kiswahili ilianza kuwa
na mgogoro wa ushairi wa kiswahili na sasa tunaandika kuhusu mambo yatokanayo na
mgogoro huo.

Humwezesha mtafiti kupata suluhisho la kilele la Jambo lililompa msukumo kufanya kazi
yake.

Hutupa habari zote tunazohitaji kuhusu mada ya utafiti wa elimu.

Humsaidia Mtafiti kugundua ujuzi, maarifa au Kanuni mpya zinazosaidia kueleza nadharia
mpya za kielimu.

Humwezesha mtafiti kupima na kukadiria mafanikio.mfano; Tafiti zenye lengo la kuona


ubora wa mihtasali mipya, vitabu vipya, njia mpya za ufundishaji na masomo mbalimbali na
hatimaye kufanya marekebisho ili kufikia kiwango kinachohitajiwa.

Humwezesha mtafiti kuweza kupata mbinu za kutatua matatizo yaliyotokea na uwekaji wa


malengo ya baadae ya kielimu.

DHIMA YA UTAFITI ( KIELIMU)

a) Humwezesha mtafiti kupata taarifa muhimu kuhusu suala linalotafitiwa.

b) Kazi ya utafiti huongeza hazina ya maarifa katika uwanja unaohusika.

c) Kipima-joto Cha hali, fikira, Mitazamo, matarajio ya jamii ya watafitiwa.

d) Kuchangia katika kujenga na kuendeleza fani za fasihi simulizi na fani nyinginezo.


3)UKUSANYAJI WA DATA

Ukusanyaji wa data hutawaliwa na mambo mane;

i) Uwanja wa taaluma unaohusika- Hii ni sehemu ambayo inashughulikiwa na mtafiti katika


kazi yake ya utafiti.

ii)Lengo la utafiti- Ni lile Jambo ambalo mtafiti anataka kupata suluhisho kwalo kutokana na
utafiti anao ufanya.

iii)Uwezo wa nyenzo alizonazo mtafiti - Vifaa ambavyo mtafiti amevichagua kufanya kazi
yake ya utafiti pia huweza kudhihirisha iwapo kazi iliyofanywa ni ya kuaminika au la.

iv)Muda alio nao mtafiti- Iwapo mtafiti ana muda wa kutosha wa kufanya kazi yake, basi
ataifanya kazi yake kikamilifu na kwa makini kuhakikisha kuwa utafiti wake Ni wa
kuaminika.

3.1. NJIA KUU ZA UTAFITI

.Utafiti wa maktabani/ wa nyaraka

.Utafiti wa uwandani

.Utafiti wa maabarani/ studioni.

3.1.a. Utafiti wa Maktabani/Nyaraka

Nyaraka asilia.

Nyaraka rasmi za kiserikali

Nyaraka binafsi (barua, shajara, mjadala, kumbukumbu, vyeti n.k)

3.1.b. Nyaraka Fuatizi

Nyaraka rasmi/ za serikali

Nyaraka binafsi (vitabu, kumbukumbu, ripoti, magazeti n.k)

3.1.c.Utafiti wa Uwandani

Mbinu za Utafiti

Kushuhudia

Kushiriki

Mahojiano

Mijadala ya vikundi lengani.


Kutumia vidadisi na majedwali.

MBINU ZA KUSHUHUDIA

Kushuhudia ni mbinu ya kuangalia tukio linapotendeka na kukusanya taarifa zake.

Namna za Ushuhudiaji

a) Uchunguzi na upimaji -Mtafiti awe na vifaa vinavyohitajika kwa kazi hiyo.

b)Ushuhudiaji fungemno .

c)Ushuhudiaji funge- Unatoa uhuru zaidi.

d)Ushuhudiaji lengani.- Mtafiti huangalia tukio katika mazingira yake asilia bila majedwali.

e) Ushuhudiaji huru/ Usiofunge- Hufanywa kwa siri na mtafiti bila mtafitiwa kufahamu na
bila mpangilio wa wazi.

3.2 MBINU ZA KUKUSANYA DATA

Data inaweza kukusanywa kwa njia mbalimbali Kama vile;

a) Kusikiliza

Mkusanyaji anaweza kusikiliza wasanii katika jamii wakitamba, kusimulia au kuimba tungo
zao.

b)Kushiriki

Mkusanyaji data anaweza kujiunga na jamii kwa Kushiriki katika ngoma, soga, na
masimulizi ya hadithi na tanzu zingine.

UMUHIMU WA KUSHIRIKI

.Mtafiti huja karibu zaidi na jamii na hupata habari za kuaminika moja kwa moja.

.Mkusanyaji hupata hisia halisi ya yanayowasilishwa kwa vile anakabiliana ana kwa ana na
watendaji hivyo kuelewa zaidi mada ya utafiti.

.Hukuza utangamano kati ya mtafiti na wanajamii.

.Ni rahisi kwa mkusanyaji kuuliza maswali kuhusu kipera kinachowasilishwa.

.Kushiriki ni njia bora ya kukusanya habari kutoka kwa watu ambao hawajui kusoma na
kuandika.

UDHAIFU WA KUSHIRIKI

.Huchukua muda mrefu kwani Kushiriki katika utendaji ni kazi.

.Huenda mtafiti akatekwa na yaliyomo na kusahau kurekodi.


.Ugeni wa mtafiti huweza kuleta wasiwasi miongoni mwa washiriki na wakakosa kutenda
Kama kawaida.

.Hii ni njia ghali ya utafiti kwani inamhitaji mtafiti kusafiri mbali ili Kushiriki katika
utendaji.

c)Kurekodi (Filamu, Video)

Mkusanyaji anaweza kusikilizana na watu na kuwarekodi katika vinasa sauti , kanda na


video.

d) Kutazama

Mkusanyaji anaweza kushuhudia kwa macho fasihi fulani ikiendelezwa bila Kushiriki.

UMUHIMU WA UTAZAMAJI

.Ni rahisi kwa mtafiti kurekodi kwa vile hashiriki katika utendaji.

.Mtafiti hupata habari za kutegemewa zaidi hasa pale anapotumia kinasa sauti kurekodi.

.Utendaji wa wahusika hauathiriwi kwani hawafahamu kuwa mtafiti anawaona, hivyo basi
kuaminika.

UDHAIFU WA UTAZAMAJI

.Wanajamii wanaweza kumshukuru mtafiti kuwa anawapeleleza na hivyo kusitisha


uwakilishaji wao.

e) Kutumia Hojaji

Hojaji ni fomu yenye maswali yaliyochapishwa ili kukusanya habari fulani.

Hojaji huandaliwa na mkusanyaji wa data na kutumwa kwa mhojiwa atakaye jaza . Kuna
hojaji wazi na funge.

UMUHIMU WA HOJAJI

.Gharama ya chini.

.Yaweza kutumika katika mahojiano.

.Huokoa muda kwani mtafiti aweza kuituma na kuachia mhojiwa kujaza.

.Hupata habari za kuaminika na kutegemea.

UPUNGUVU WA HOJAJI

.Utata wa maswali husababisha majibu yasiyo sahihi.

.Si nzuri kwa wasiojua kusoma na kuandika.


.Kutopata sifa za uwasilishaji Kama vile kiimbo, toni na ishara.

.waojiwa kukataa kuijaza kutokana na sababu mbalimbali.

f) Kurekodi Katika Kanda za Sauti.

UMUHIMU WA KUREKODI

.Kuweza kudumu na kufikia vizazi Vingine.

.Sifa za uwasilishaji/uhai Kama vile toni na kiimbo kuhifadhiwa.

.Mkusanyaji aweza kurudia uwasilishaji ikiwa hakuelewa.

.Kupata habari za kutegemewa na kuaminika.

.Kuweza kupata hisia halisi za uwasilishaji.

UDHAIFU WA KUREKODI

.Chaweza kukosa nguvu za umeme na utafiti kuathirika.

.Hakiwezi kunasa uigizaji.

.Fanani huenda asiwasilishe vyema akijua anarekodiwa .

.Ghali na kuhitaji kununua kifaa na kumbidi mtafiti kusafiri.

g)Mahojiano

Kuhoji wanao fahamu mengi kuhusu utafiti.

UMUHIMU WA MAHOJIANO

.Kuweza kungamua wakati mhojiwa anatoa habari zisizo za kweli.

.Kuweza kufafanulia mhojiwa maswali ili kuweza kupata habari sahihi zaidi.

.Kuweza kupata sifa za uwasilishaji.

.Ni rahisi kurekodi.

.Kupata habari za kutegemewa na kuaminika.

UDHAIFU WA MAHOJIANO

.Huhitaji muda mrefu.

.Mhojiwa kutotoa habari kwa kutomwamini mtafiti kwa ugeni wake.

.Kikwazo cha mawasiliano- Si njia bora kwa wasiojua kusoma na kuandika.

.Ghali kwa gharama ya usafiri.


MAREJELEO.

Ehtridge, D.E. (2004) "Research Methodology in Applied Economics." John Wiley & Sons
p.24.

Quinn,. P.M. (1990) Qualitative Evaluation and Research Methods.

Nyandemo,S.M (2007) Research Methodology, Methods and Approaches. Richmonds


Designers and Printers.

Mugenda,O and Mugenda A.M (1999) Research Methods. Nairobi:Acts press.

Fox, W. & Bayat, M. S (2007) "A Guide to Managing Research" . Juta publications, p.45.

You might also like