You are on page 1of 16

Na.

6 2016

34567

Ukweli Kuhusu
Maono ya Mbinguni
Kila Toleo Linachapishwa: 58,987,000
34567 Katika LUGHA 282 Na. 6 2016

Vol. 137, No. 16 SWAHILI

GAZETI HILI, Mnara wa Mlinzi, lina-


UNA MAONI GANI?
mheshimu Yehova Mungu, ambaye Ikiwa ungeambiwa ueleze kuhusu hali ya
ndiye Mtawala Mkuu wa ulimwengu.
Linawafariji watu kwa habari njema
mbinguni, ungesemaje?
kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mu- Yesu anaweza kutusaidia kujua hali
ngu ulio mbinguni, utakomesha uovu
wote na kuigeuza dunia kuwa paradi- ya mbinguni kwa sababu alisema hivi:
so. Linawatia moyo watu wamwamini “Mimi ninatoka kwenye makao ya juu.”
Yesu Kristo, ambaye alikufa ili tupate —Yohana 8:23.
uzima wa milele na ambaye sasa
anatawala akiwa Mfalme wa Ufalme Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linaeleza
wa Mungu. Gazeti hili limekuwa liki- mambo ambayo Yesu na Baba yake
chapishwa tangu 1879 na si la kisia- wamefunua kuhusu hali ya mbinguni.
sa. Linashikamana na Biblia ambayo
ndiyo msingi wake.

Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya Ukweli Kuhusu Maono ya Mbinguni


kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwe-
nguni pote inayotegemezwa kwa Ukweli Kuhusu Wale Wanaoishi Mbinguni 3
michango ya hiari.
Maono Kuhusu Wale Wanaoishi Mbinguni 4
Ikiwa ungependa kutoa mchango,
tafadhali tembelea tovuti ya
www.jw.org/sw.
PIA KATIKA TOLEO HILI
Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko
yamenukuliwa kutoka katika Biblia Takatifu Mambo Tunayojifunza Kutokana na
—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.
Ndege wa Mbinguni 8
Je, ungependa kupata habari zai- ´
di au kujifunza Biblia nyumbani `
Lefevre d’Etaples—Alitaka Watu wa Kawaida
kwako bila malipo?
Waelewe Neno la Mungu 10
Tembelea www.jw.org/sw au utu-
me ombi lako ukitumia moja ya Simulizi la Maisha
anwani zilizo hapa chini. Nilipokea Kweli ya Biblia Bila Kuwa na Mikono 13
Biblia Inasema Nini? 16

The Watchtower (ISSN 0043-1087) Issue 16


November 2016 is published monthly with an
additional issue published in January, March, May,
s SOMA HABARI ZAIDI KWENYE INTANETI

July, September, and November by Watchtower


Bible and Tract Society of New York, Inc.;
MAJIBU YA MASWALI MENGINE
L. Weaver, Jr., President; G. F. Simonis, YA BIBLIA
Secretary-Treasurer; 1000 Red Mills Road, Wallkill,
NY 12589-3299, and printed by Watch Tower Bible Je, Mungu Alimuumba Ibilisi
and Tract Society of South Africa NPC, 1 Robert
Broom Drive East, Rangeview, Krugersdorp, 1739. Ili Atujaribu?
5 2016 Watch Tower Bible and Tract Society
(Tafuta kwenye MAFUNDISHO YA BIBLIA ˛

r
of Pennsylvania. Printed in South Africa.
MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA)
HABARI KUU

UKWELI KUHUSU WALE WANAOISHI


MBINGUNI
Je, umewahi kujiuliza ni nani wanaoishi mbinguni? Watu
wengi hujiuliza swali hilo. Kwa miaka mingi watu wamekuwa na
makisio mbalimbali kuhusu hali ya mbinguni. Baadhi ya watu
huamini kwamba mababu waliokufa huishi huko na wanapaswa
kuheshimiwa. Wengine hufikiri kwamba ni mahali ambako malaika
na watu wema waliokufa huishi kwa amani na furaha tele. Ilhali
wengine huamini kwamba mbinguni ni makao ya mamilioni ya
miungu.

Watu wengi huamini kwamba hatuwezi kuelewa nguni. (Zaburi 83:18) Hivyo, Yehova Mungu na
hali ya mbinguni kwa kuwa hakuna mtu aliye- Yesu Kristo ndio wanaoweza kutueleza ukweli.
shuka duniani na kueleza ukweli kuhusu mbi- Waliwafunulia watumishi waaminifu wa zamani
nguni. Hata hivyo, maoni hayo hayafai. Yesu habari nyingi kuhusu hali ya mbinguni kupitia
Kristo aliishi mbinguni kabla ya kuja duniani. maono.
Aliwaambia hivi viongozi wa dini katika karne ya Makala inayofuata itazungumzia baadhi ya
kwanza: “Nimeshuka kutoka mbinguni kufanya, maono yaliyo katika Biblia ambayo wanadamu
si mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenitu- walipokea. Unapochunguza maono hayo, ku-
ma.” Yesu aliwaeleza mitume wake kuhusu hali mbuka kwamba makao ya mbinguni ni tofauti
ya mbinguni aliposema hivi: “Katika nyumba ya na makao ya duniani, hakuna vitu tunavyoweza
Baba yangu mna makao mengi.”—Yohana 6:38; kugusa au kuona. Kwa sababu hiyo, Mungu ali-
14:2. tumia maono rahisi ili kutusaidia kuelewa. Mao-
Kwa kweli, Mungu ambaye jina lake ni Yeho- no hayo yatatusaidia kuwajua wale wanaoishi
va, ndiye baba ya Yesu, na “makao” yake ni mbi- katika “makao” ya mbinguni.

Na. 6 2016 3
MAONO KUHUSU WALE WANAOISHI

MBINGUNI
Biblia inataja maono yenye kustaajabisha ambayo yanatusaidia kuelewa jinsi makao
ya kiroho yalivyo. Tunakutia moyo uchunguze kwa makini maono hayo. Ingawa baadhi
ya mambo katika maono hayo si halisi, yatakusaidia kuwajua wale wanaoishi
mbinguni na jinsi wanavyohusika maishani mwako.

YEHOVA NDIYE MKUU ZAIDI hova ni mkuu na wa kusifiwa sana. Ni mwenye kuo-
“Kiti cha ufalme kilikuwa mahali pake mbi- gopesha kuliko miungu mingine yote. Kwa maana
nguni, na kuna yule aliyeketi juu ya kile kiti cha miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu isiyo
ufalme. Na yule aliyeketi, kuonekana kwake ni na thamani; lakini Yehova, amezifanya mbingu.
kama jiwe la yaspi na jiwe jekundu la thamani, Utukufu na fahari ziko mbele zake; nguvu na uzu-
na upinde wa mvua ambao kuonekana kwake ni ri zipo katika patakatifu pake.”—Zaburi 96:4-6.
kama zumaridi unakizunguka kile kiti cha ufal- Licha ya kwamba Yehova ni Mkuu Zaidi, ana-
me.”—Ufunuo 4:2, 3. tualika tumkaribie kupitia sala na anatuhakikishia
“Naye alikuwa na mwangaza kuzunguka pa- kwamba atatusikiliza. (Zaburi 65:2) Mungu anatu-
nde zote. Kulikuwa na kitu kinachoonekana penda na kutujali sana hivi kwamba mtume Yoha-
kama upinde ambao hutokea katika wingu ku- na aliandika hivi kwa unyofu: “Mungu ni upendo.”
bwa katika siku ya mvua. Hivyo ndivyo ulivyo- —1 Yohana 4:8.
kuwa mwangaza uliozunguka pande zote. Kuli-
kuwa ni kuonekana kwa mfano wa utukufu wa YESU ANAISHI MBINGUNI
Yehova.”—Ezekieli 1:27, 28. “[Mwanafunzi Mkristo Stefano], akiwa ame-
Maono hayo ya mtume Yohana na nabii Ezekieli jaa roho takatifu, akakaza macho mbinguni,
yanaonyesha utukufu wa Mungu Mkuu Zaidi, Ye- akaona utukufu wa Mungu na wa Yesu akiwa
hova, na tunaweza kuyaelewa kwa sababu yanata- amesimama kwenye mkono wa kuume wa Mu-
ja vitu tunavyojua, kama vile, mawe ya thamani ye- ngu, naye akasema: ‘Tazameni! Ninaziona mbi-
nye kung’aa, upinde wa mvua na ukuu wa kiti cha ngu zimefunguka na Mwana wa binadamu aki-
enzi. Maono hayo yanaonyesha kwamba makao ya wa amesimama kwenye mkono wa kuume wa
Yehova yanavutia na ni matulivu sana. Mungu.’ ”—Matendo 7:55, 56.
Ufafanuzi huo kumhusu Mungu unapatana na Kabla ya ono hilo, Yesu alikuwa ameuawa kuto-
maneno haya ya mtunga zaburi: “Kwa maana Ye- kana na uchochezi wa viongozi Wayahudi ambao

4 MNARA WA MLINZI
sasa Stefano alikuwa akizungumza nao. Ono hilo elfu kumi mara elfu kumi walioendelea kusi-
lilithibitisha kwamba Yesu alikuwa amefufuliwa na mama mbele zake.”—Danieli 7:9, 10.
kupewa cheo cha juu. Mtume Paulo alieleza hivi: Katika ono hilo, Danieli aliona maelfu ya malai-
‘[Yehova] alimfufua [Yesu] kutoka kwa wafu na ka wakiwa mbinguni. Bila shaka, hilo lilikuwa ono
kumketisha kwenye mkono wake wa kuume katika lenye kustaajabisha sana! Malaika ni viumbe wa ki-
mahali pa kimbingu, juu zaidi kuliko kila serikali roho wenye utukufu, nguvu, na akili nyingi. Malai-
na mamlaka na nguvu na utawala na kila jina lina- ka hao wanatia ndani maserafi na makerubi. Biblia
lotajwa, si katika mfumo huu wa mambo tu, bali inawataja malaika zaidi ya mara 250.
pia katika ule ujao.’—Waefeso 1:20, 21. Malaika si wanadamu walioishi duniani zamani.
Zaidi ya kueleza kuhusu cheo chake cha juu, Mungu aliwaumba malaika muda mrefu kabla ya
Maandiko yanaonyesha kwamba, kama alivyo Ye- kuwaumba wanadamu. Dunia ilipoumbwa, malai-
hova, Yesu anawajali sana wanadamu. Alipokuwa ka walipaaza sauti na kushangilia.—Ayubu 38:4-7.
duniani, Yesu aliwaponya wagonjwa, walemavu, na Malaika waaminifu wanamtumikia Mungu kwa
kufufua wafu. Pia, alionyesha kwamba anampenda
kushiriki katika kazi muhimu inayofanywa du-
sana Mungu na wanadamu kwa kutoa uhai wake
niani, yaani, kuhubiri habari njema za Ufalme wa
uwe dhabihu. (Waefeso 2:4, 5) Hivi karibuni, Yesu,
Mungu. (Mathayo 24:14) Katika maono, mtume
akiwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu, atatu-
Yohana aliona jinsi malaika wanavyoshiriki katika
mia mamlaka yake kuwaletea wanadamu watiifu
kazi ya kuhubiri, na aliandika hivi: “Nami nika-
hapa duniani baraka nyingi.
mwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbi-
MALAIKA WANAMTUMIKIA MUNGU ngu, naye alikuwa na habari njema ya milele ili
Nabii Danieli alisema hivi: “Nikaendelea ku- aitangaze kuwa habari za furaha kwa wale wanao-
tazama mpaka viti vya ufalme vikawekwa na kaa duniani, na kwa kila taifa na kabila na lugha
Mzee wa Siku [Yehova] akaketi. . . . Kulikuwa na watu.” (Ufunuo 14:6) Ingawa siku hizi malaika
na maelfu elfu walioendelea kumtumikia, na hawazungumzi na wanadamu kama zamani, wao

Na. 6 2016 5
huwaongoza wahubiri wa habari njema kuwahubi- mishi na mifugo ya mwanamume mwaminifu Ayu-
ria watu wanyofu. bu. Kisha, akawaua watoto wote kumi wa Ayu-
bu kwa kuleta “upepo mkubwa” ambao ulivunja
SHETANI HUPOTOSHA MAMILIONI YA WATU
nyumba walimokuwa. Mwishowe, Shetani alimpi-
“Na vita vikatokea ghafula mbinguni: Mikae- ga Ayubu kwa “majipu hatari kuanzia wayo wa
li [Yesu Kristo] na malaika zake wakapigana na mguu wake mpaka kwenye utosi wa kichwa chake.”
yule joka mkubwa, naye joka mkubwa na ma- —Ayubu 1:7-19; 2:7.
laika zake wakapigana lakini hakushinda, wala Hata hivyo, hivi karibuni Shetani ataharibiwa.
mahali hapakupatikana mbinguni kwa ajili yao Tangu alipotupwa duniani, anajua kwamba “ana
tena. Kwa hiyo yule joka mkubwa akatupwa kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:12) Ni ha-
chini, yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa bari njema kujua kwamba Shetani ataangamizwa!
Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima
inayokaliwa; akatupwa chini duniani, na malai- WALE WANAOTOKA DUNIANI
ka zake wakatupwa chini pamoja naye.”—Ufu- ‘Wewe [Yesu] ulimnunulia Mungu watu ku-
nuo 12:7-9. toka katika kila kabila na lugha na watu na tai-
Kuna wakati ambapo mbinguni hakukuwa na fa, nawe ukawafanya kuwa ufalme na makuha-
amani. Mwanzoni kabisa mwa historia ya wanada- ni kwa Mungu wetu, nao watatawala wakiwa
mu, malaika mmoja alitamani kuabudiwa na hivyo wafalme juu ya dunia.’—Ufunuo 5:9, 10.
akamwasi Yehova na kuwa Shetani, jina linalomaa- Kama vile Yesu alivyofufuliwa na kwenda mbi-
nisha “Mpinzani.” Baadaye, malaika wengine wa- nguni, wengine pia wanaenda mbinguni. Yesu
liasi pia nao wakawa roho waovu. Ni waovu sana, aliwaambia hivi mitume wake waaminifu: “Ninae-
nao humpinga Yehova na wamewapotosha watu nda kuwatayarishia ninyi mahali. Pia, . . . nitakuja
wengi wasifuate mwongozo wenye upendo wa Ye- tena nami nitawapokea ninyi nyumbani kwangu
hova. mwenyewe, ili mahali nilipo mimi, ninyi pia muwe
Shetani na roho wake ni waovu na wakatili. Wao hapo.”—Yohana 14:2, 3.
ni adui za wanadamu, nao husababisha mateso Wanadamu wanaoenda mbinguni wanaenda
mengi duniani. Kwa mfano, Shetani aliwaua watu- huko kwa kusudi fulani. Wakiwa pamoja na Yesu,

USIWAOGOPE ROHO WAOVU

Mamilioni ya watu ni kama wa- yeye.” (2 Mambo ya Nyaka- Vivyo hivyo, ili Mungu akulinde
fungwa katika zoea la uwasilia- ti 16:9) Ukimtumaini Mungu unapaswa kuharibu vitu vyote
ni roho nao huwaogopa sana wa kweli, Yehova, atakulinda vinavyohusiana na uwasiliani
roho waovu. Wanatumia hirizi kwa kuwa ana nguvu kuliko roho kama vile hirizi, na vitabu
na uchawi ili kujilinda. Hupaswi Shetani. vya uchawi.
kufanya mambo hayo. Biblia Ili kupata ulinzi wa Yehova, Biblia inasema hivi: “Jitii-
inatufariji kwa kutuhakikishia unahitaji kujifunza mambo ya- sheni kwa Mungu; lakini mpi-
hivi: “Kwa maana, kwa habari nayompendeza na kisha ute- ngeni Ibilisi, naye atawakimbia
ya Yehova, macho yake yanae- nde mambo hayo. Kwa mfano, ninyi.” (Yakobo 4:7) Ukijitiisha
nda huku na huku duniani kote katika karne ya kwanza, Wakri- kwa Mungu na kumtumikia,
ili aonyeshe nguvu zake kwa sto katika jiji la Efeso walivi- unaweza kuwa na uhakika kwa-
ajili ya wale ambao moyo wao choma vitabu vyao vyote vya mba Shetani na roho wake
ni mkamilifu kumwelekea uchawi. (Matendo 19:19, 20) waovu hawatakushinda.

6 MNARA WA MLINZI
watafanyiza Ufalme ambao hatimaye utaitawala
dunia yote na kuwaletea baraka wanadamu. Huo
ndio Ufalme ambao Yesu aliwaambia wanafunzi
wake wasali kuuhusu katika sala ya mfano alipose-
ma hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na li-
takaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na
yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.”—Ma-
thayo 6:9, 10.
Maono hayo ya kinabii yanahusu wakati ambao
MAMBO AMBAYO WALE WALIO Ufalme wa Mungu, utakaofanyizwa na Yesu na
MBINGUNI WATAFANYA wale waliofufuliwa kutoka duniani, utaangamiza
Mtume Yohana alisema hivi: “Ndipo nikasikia utawala wa Shetani na kuifanya dunia iwe paradi-
sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme so. Mambo ambayo yamewasababishia wanadamu
ikisema: ‘Tazama! Hema la Mungu liko pamoja maumivu mengi na huzuni hayatakuwapo tena.
na wanadamu, . . . naye atafuta kila chozi kuto- Hata kifo kitaondolewa.
ka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo Namna gani mabilioni ya watu waliokufa ambao
tena, wala maombolezo wala kilio wala maumi- hawana tumaini la kwenda kuishi mbinguni? Wa-
vu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani ya- kati ujao, watafufuliwa wakiwa na tumaini la kuishi
mepitilia mbali.’ ”—Ufunuo 21:3, 4. milele katika Paradiso duniani.—Luka 23:43. ˇ

Maono hayo yanatuthibitishia kwamba Yehova Mungu, Mwana wake Yesu Kristo, malaika waaminifu, na wale
walionunuliwa kutoka duniani, wanatujali sana na kuhangaikia hali yetu. Ili ujifunze mengi zaidi kuhusu ma-
mbo watakayofanya, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova au tembelea tovuti ya, www.jw.org/sw na
upakue kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

Na. 6 2016 7
Mambo Tunayojifunza
Kutokana
na Ndege
wa Mbinguni
“Tafadhali uliza . . . viumbe vya mbinguni vyenye mabawa, navyo
vitakuambia. Ni nani kati ya hao wote ambaye hajui vema kwamba
ni mkono wa Yehova ambao umefanya haya?”—Ayubu 12:7, 9. Korongo

ZAIDI ya miaka 3,000 iliyopita, mwanamume yako kuu, Ee Yehova wa majeshi, Mfalme wangu
mwaminifu Ayubu alitambua kwamba tunaweza na Mungu wangu!” (Zaburi 84:1-3) Je, sisi pa-
kujifunza mengi kuhusu uumbaji wa Mungu ku- moja na watoto wetu, tuna tamaa hiyohiyo na tu-
pitia ndege. Tabia za ndege hufanya watumiwe nathamini kushirikiana kwa ukawaida na kutani-
katika mifano na vielelezo. Katika Biblia, kuna ko la watu wa Mungu?—Zaburi 26:8, 12.
habari nyingi kuhusu ndege ambazo zinatufundi-
KORONGO ANAJUA MAJIRA YAKE
sha kuhusu maisha na uhusiano wetu pamoja na
Mungu. Acheni tuchunguze mifano michache. Nabii Yeremia aliandika, ‘Korongo wa mbingu-
ni anajua nyakati zake.’ Bila shaka, Yeremia alie-
MAHALI AMBAPO MBAYUWAYU HUJENGA VIOTA lewa vizuri jinsi korongo wanavyohamahama na
Wakazi wa Yerusalemu waliwafahamu vizuri kupita katika Nchi ya Ahadi. Katika majira ya ku-
mbayuwayu, ambao kwa kawaida hujenga viota chipua, korongo weupe zaidi ya 300,000 husafi-
vyao chini ya paa za nyumba. Baadhi yao walije- ri kutoka Afrika kuelekea Ulaya Kaskazini kupitia
nga viota kwenye hekalu la Sulemani. Inaelekea Bonde la Yordani. Uwezo wao wa asili huwaweze-
kwamba, mbayuwayu ambao kila mwaka wali- sha kutambua majira ya kiangazi na hivyo kurudi
jenga viota vyao hekaluni waliona mahali hapo eneo lao la kutagia mayai. Kama ndege wengine
kuwa salama, na wangeweza kulea makinda yao wanaohamahama, korongo “huangalia vema wa-
bila kusumbuliwa. kati wa kila mmoja wao kuingia.”—Yeremia 8:7.
Mwandikaji wa Zaburi ya 84, mmoja wa wana Kitabu Collins Atlas of Bird Migration kinase-
wa Kora, ambaye alitumikia hekaluni kwa juma ma hivi: “Kinachostaajabisha ni kwamba kuha-
moja kila baada ya miezi sita aliona viota hivyo. ma kwa ndege hao ni jambo la kisilika.” Yehova
Alitamani kuwa kama mbayuwayu ambao waliku- Mungu amewapa ndege hekima ya kisilika ku-
wa na makao ya kudumu katika nyumba ya Ye- tambua majira ya kuhama, lakini amewapa wa-
hova. Alisema hivi: “Jinsi ilivyo nzuri maska- nadamu uwezo wa kutambua wakati na majira.
ni yako kuu, Ee Yehova wa majeshi! Nafsi (Luka 12:54-56) Tofauti na hekima ya kisilika ya
yangu imetamani sana na pia imedhoofika kwa korongo, ujuzi kutoka kwa Mungu huwawezesha
kutamani nyua za Yehova. Hata ndege amepata wanadamu kutambua maana ya matukio ya sasa.
nyumba, na mbayuwayu amepata kiota chake, Waisraeli wa siku za Yeremia hawakutambua
ambapo ameweka vifaranga vyake—Madhabahu ishara katika siku zao. Mungu alieleza sababu

8 MNARA WA MLINZI
yenye joto humwezesha tai kuruka kwa urahisi.
Mara tu anapoifikia, tai hutanua mabawa yake na
kuzunguka ndani ya mkondo huo wa hewa, na
hivyo kupaa juu zaidi na zaidi. Kwa hiyo, tai
hategemei nguvu zake kuruka na kupaa. Kama
Tai tai, wale wanaomtumaini Yehova wanaweza ku-
mtegemea kwa kuwa ameahidi kwamba atawapa
“nguvu zinazopita zile za kawaida.”—2 Wakori-
ntho 4:7, 8.
“KAMA VILE KUKU ANAVYOKUSANYA
VIFARANGA VYAKE”
Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu alisima-
Mbayuwayu Kuku na vifaranga ma na kutazama jiji kuu la Wayahudi. Kisha, aka-
sema hivi kwa uchungu: “Yerusalemu, Yerusale-
iliyowafanya watende hivyo aliposema hivi: “Wa- mu, muuaji wa manabii na ambaye huwapiga kwa
melikataa neno la Yehova, nao wana hekima mawe wale waliotumwa kwake, ni mara ngapi ni-
gani?”—Yeremia 8:9. litaka kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku
Leo, kuna mambo mengi yanayothibitisha anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa
kwamba tunaishi katika kipindi ambacho Biblia yake! Lakini hamkutaka.”—Mathayo 23:37.
inakiita “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1-5) Je, Kwa kawaida ndege hujitahidi sana kulinda
utamwiga korongo kwa kutambua ‘majira?’ makinda yao. Ndege wanaojenga viota vyao
ardhini, kama vile kuku, lazima wawe macho dhi-
TAI HUONA MBALI SANA di ya hatari. Kuku anapomwona mwewe angani
Tai wametajwa mara nyingi katika Biblia, nao hutoa sauti ya kuonya, na mara moja vifaranga
walionekana kwa ukawaida katika Nchi ya Ahadi. hukimbilia chini ya mabawa yake, mahali salama.
Akiwa kwenye kiota chake juu ya mwamba, tai Pia, vifaranga wanaweza kujificha humo ili wasia-
“hutafuta chakula; Macho yake huendelea kuta- thiriwe na mvua au jua kali. Vivyo hivyo, Yesu
zama mbali sana.” (Ayubu 39:27-29) Uwezo wa alitaka kuandaa makao na ulinzi wa kiroho kwa
kuona wa tai ni wa pekee sana, hivi kwamba ana- wakazi wa Yerusalemu. Leo, Yesu anatualika tu-
weza kumwona sungura akiwa umbali wa kilome- pate burudisho na ulinzi ili tusilemewe na mizigo
ta moja. na mahangaiko ya maisha.—Mathayo 11:28, 29.
Kama vile tai anavyoweza “kutazama mbali Kwa kweli, kuna mengi tunayoweza kujifunza
sana,” Yehova ana uwezo wa kuona mambo ya kutoka kwa ndege. Unapochunguza tabia zao,
wakati ujao. Yehova alisema hivi: “Yeye anaye- kumbuka mifano ya Kimaandiko kuhusu viumbe
tangaza tangu mwanzo ule mwisho, na kutoka hao. Mbayuwayu hutukumbusha kwamba tuna-
zamani za kale mambo ambayo hayajafanywa.” paswa kuthamini nyumba ya Yehova ya ibada.
(Isaya 46:10) Kwa kutii mashauri ya Yehova, tu- Mtegemee Mungu ili uwe na tumaini litakaloku-
naweza kunufaika na hekima yake nyingi na uwe- wezesha kupaa kama tai. Mfuate Yesu na kupa-
zo wa kuona mambo kimbele.—Isaya 48:17, 18. ta kweli za kiroho zitakazokulinda kama kuku
Pia, Biblia inalinganisha wale wanaomtumai- anavyolinda vifaranga wake. Mfano wa korongo
ni Mungu na tai kwa kusema: “Wale wanaomtu- na ukusaidie kuwa macho na kuelewa maana ya
maini Yehova watapata nguvu mpya. Wataruka matukio ya ulimwengu katika kipindi tunacho-
juu kwa mabawa kama tai.” (Isaya 40:31) Hewa ishi. ˇ

Na. 6 2016 9
´
5 Bibliotheque nationale de France, Paris

`
Lefevre d’Etaples
ALITAKA WATU WA KAWAIDA
`

WAELEWE NENO LA MUNGU

ILIKUWA Jumapili asubuhi mwanzoni mwa `


Lefevre akaacha kujifunza falsafa na kuelekeza
miaka ya 1520, wakazi wa Meaux, mji mdogo nguvu zake zote katika kutafsiri Biblia.
ulio karibu na Paris, hawakuamini mambo wali- `
Mwaka wa 1509, Lefevre alitoa chapisho lililo-
yosikia kanisani. Walisikia vitabu vya Injili viki- linganisha tafsiri tano za Zaburi za Kilatini,1 ku-
somwa kwa lugha yao ya asili, yaani, Kifaransa tia ndani marekebisho yake ya Vulgate. Tofauti
na wanatheolojia wa wakati huo, Lefevre` alijita-
badala ya Kilatini!
Mtafsiri wa Biblia aliyeongoza kazi hiyo, Jac- hidi kutafuta “maana halisi” ya Maandiko. Mbi-
` ´
ques Lefevre d’Etaples (Kilatini, Jacobus Faber nu yake ya kutafsiri Maandiko iliwachochea wa-
Stapulensis), baadaye alimwaandikia hivi rafi- somi wengine wa Biblia.—Ona Sanduku “Jinsi
Martin Luther Alivyochochewa na Lefevre.”`
ki yake wa karibu: “Inashangaza sana kuona ji-
`
Lefevre alikuwa Mkatoliki, na aliamini kwa-
nsi Mungu anavyowasaidia watu wengi kuelewa
Neno lake.” mba ingewezekana kulifanya upya kanisa iki-
Wakati huo, Kanisa Katoliki na wanatheolojia wa watu wa kawaida watafundishwa Maandiko
wa Paris walipinga kutumia Biblia zilizotafsiriwa ifaavyo. Lakini watu wa kawaida wangenufaika-
kwa lugha zilizozungumza na watu wengi. Kwa je na Maandiko, kwa kuwa maandishi hayo ma-
hiyo, ni nini kilichomchochea Lefevre ` atafsiri takatifu yaliandikwa kwa Kilatini?
Biblia katika Kifaransa? Alifaulu jinsi gani kuwa- TAFSIRI YA BIBLIA ILIYOPATIKANA KWA WOTE
saidia watu wengi waelewe Neno la Mungu? `
Kwa kuwa Lefevre alilipenda sana Neno la
ALITAFUTA MAANA SAHIHI YA MAANDIKO Mungu, aliazimia kuwasaidia watu wengi iweze-
`
Kabla ya kuwa mtafsiri wa Biblia, Lefevre ali- kanavyo wapate Biblia. Hivyo, Juni 1523, ali-
jitahidi kurudisha maana ya awali ya maandishi chapisha tafsiri ya Kifaransa ya vitabu vya Injili
ya kale ya falsafa na theolojia. Alitambua kwa- katika mabuku mawili madogo. Biblia hiyo ili-
mba kwa karne nyingi maandishi ya kale yaliku- gharimu nusu ya bei ya tafsiri ya kawaida, na hi-
wa yamepotoshwa. Alipokuwa akitafuta maana vyo kuwawezesha watu wengi kupata Biblia.
sahihi ya maandishi ya kale, alianza kujifunza Watu wa kawaida walifurahia sana. Wanaume
kwa makini Biblia iliyokuwa ikitumiwa na Kani- kwa wanawake walitamani sana kusoma masi-
sa Katoliki, yaani, Vulgate ya Kilatini. mulizi ya Yesu katika lugha yao, na nakala 1,200
Kuchunguza kwa bidii Maandiko kulimfanya 1 Kitabu Fivefold Psalter kilikuwa na tafsiri tano za Zaburi kwenye safu
afikie mkataa kwamba “kujifunza kweli za Neno tofauti na sanduku lenye majina ya cheo ya Mungu, kutia ndani Te-
tragramatoni, yaani, herufi nne za Kiebrania zinazowakilisha jina la
la Mungu huleta . . . furaha kubwa.” Kwa hiyo, Mungu.

10 MNARA WA MLINZI
zilizochapishwa mara ya kwanza zilikwisha baa- `
Lefevre pia alijitahidi kufunua maoni yenye
da ya miezi michache tu. makosa ya wale waliopinga kutafsiri Biblia ka-
tika Kifaransa. Alifichua unafiki wao, kwa ku-
MSIMAMO DHABITI KUELEKEA BIBLIA
` sema hivi: “Watawafundishaje [watu] kushika
Katika utangulizi wa Injili, Lefevre alieleza mambo yote ambayo Yesu aliamuru, ikiwa wa-
kwamba alitafsiri Injili hiyo kwa Kifaransa ili napinga watu wa kawaida kuona na kusoma Inji-
“washiriki wa kawaida” wa kanisa “waelewe ma- li ya Mungu kwa lugha yao wenyewe?”—Waro-
fundisho ya Injili kama wale waliosoma kwa lu- ma 10:14.
`
gha ya Kilatini.” Lakini kwa nini Lefevre alita- Haishangazi kwamba muda mfupi baadaye,
mani sana kuwasaidia watu wa kawaida waelewe wanatheolojia wa Chuo Kikuu cha Sorbonne,
mambo ambayo Biblia inafundisha?
`
Lefevre alijua vizuri kwamba mafundisho na
falsafa za wanadamu ziliathiri Kanisa Katoliki.
(Marko 7:7; Wakolosai 2:8) Aliamini kwamba
muda ulikuwa umefika wa Injili “kutangazwa uli-
mwenguni kote, ili watu wasidanganywe tena na
mafundisho ya uwongo ya wanadamu.”
5 Bibliotheque nationale de France, Paris
`

, Sanduku lenye majina ya cheo ya Mungu katika


Zaburi, kama yanavyopatikana katika kitabu
Fivefold Psalter, Toleo la mwaka 1513

Utangulizi wa vitabu vya Injili ulifunua wazi


`
tamaa ya Lefevre ya kutaka watu wote wawe
na Biblia katika lugha yao )
`
5 Bibliotheque nationale de France, Paris

Na. 6 2016 11
`
Paris, walijaribu kumnyamazisha Lefevre. Mna- kuwa njia bora ya kuwajibu wale ambao hawaku-
mo Agosti 1523, walipinga tafsiri na habari za thamini “lulu” zenye thamani za kweli ya Biblia.
Biblia zilizokuwa katika lugha za asili, wakidai —Mathayo 7:6.
kuwa tafsiri hizo ni “hatari kwa kanisa.” Bila Mwaka mmoja hivi baada ya Lefevre` kukimbi-
msaada wa Mfalme wa Ufaransa, Francis wa I, lia Strasbourg, Mfalme Francis wa I alimchagua
`
Lefevre angehukumiwa kuwa mwasi. awe mwalimu wa mtoto wake mwenye miaka mi-
MTAFSIRI AKAMILISHA KAZI YAKE nne aliyeitwa Charles. Kazi hiyo ilimruhusu ku-
` malizia tafsiri yake ya Biblia. Mwaka wa 1530,
Lefevre hakuruhusu upinzani mkali umvunje `
Biblia nzima ya Lefevre ilichapishwa jijini Ant-
moyo katika kazi yake ya kutafsiri Biblia. Mwa-
werp, Ubelgiji, kwa kibali cha maliki Charles wa
ka wa 1524, baada ya kukamilisha kutafsiri Maa-
Tano.1
ndiko ya Kigiriki (ambayo kwa kawaida huitwa
Agano Jipya), alitoa tafsiri ya Kifaransa ya Za- MATARAJIO AMBAYO HAYAKUTIMIA
buri, ili watu waweze kusali “kwa kujitoa zaidi `
Katika maisha yake yote, Lefevre alitumaini
na kwa hisia nyingi.” kwamba kanisa lingeacha mapokeo ya wanada-
Mara moja, wanatheolojia wa Sorbonne walia- mu na kurudia ujuzi sahihi wa Maandiko. Alia-
`
nza kuchunguza kwa makini tafsiri ya Lefevre. mini kabisa kwamba “kila Mkristo ana haki na
Kisha, wakaagiza tafsiri yake ya maandiko ya Ki- wajibu wa kusoma na kujifunza Biblia kibinafsi.”
giriki ichomwe moto hadharani, na wakapiga Hiyo ndiyo sababu alijitahidi sana kuhakikisha
marufuku maandishi mengine wakidai kwamba kwamba kila mtu anaweza kupata Biblia. Ingawa
“yanaunga mkono uasi wa Luther.” Wanatheo- tamaa yake ya kuona kanisa likibadilika haikuti-
`
lojia walipomwita ili atetee maoni yake, Lefevre mia, matokeo ya kazi yake yanaonekana. Aliwa-
aliamua kukaa kimya na kisha akakimbilia Stra- saidia watu wa kawaida kujua Neno la Mungu. ˇ
sbourg. Akiwa huko, aliendelea kutafsiri Biblia.
1 Miaka mitano baadaye, mwaka 1535, mtafsiri Mfaransa Olivetan ´
Ingawa wengine waliona jambo alilofanya kuwa alitoa tafsiri ya Biblia iliyotegemea lugha za awali. Alitumia sana taf-
ni kukosa ujasiri, yeye aliamini kwamba hiyo ili- `
siri ya Lefevre kutafsiri Maandiko ya Kigiriki.

`
Jinsi Martin Luther Alivyochochewa na Lefevre

Martin Luther alikuwa mtawa tano mkubwa kwa Luther, kwa


asiyejulikana alipoanza kuchu- mtafsiri wa Biblia William Tyndale,
`
nguza kazi za Lefevre. Luther ali- na Mwanaharakati John Calvin.
` `
tambua kwamba Lefevre alifafa- Ingawa Lefevre alikuwa Mkatoliki
nua mistari ya Biblia kwa njia hadi alipokufa, kazi yake ina
rahisi na yenye kueleweka tofauti mchango mkubwa katika kutafsiri
na wasomi wa siku zake waliotu- Biblia na iliongoza kwenye Mare-
mia lugha ya mafumbo. Mbinu ya kebisho ya Kidini.
`
utafsiri ya Lefevre ilikuwa na uvu-

12 MNARA WA MLINZI
SIMULIZI LA MAISHA

Nilipokea Kweli ya
Biblia Bila Kuwa
na Mikono
LIMESIMULIWA NA BERNHARD MERTEN

Kwa kawaida watu hushikilia kitu fulani


wanapokuwa na woga. Siwezi kufanya hivyo
kwa kuwa sina mikono. Nilikuwa na umri wa
miaka saba nilipokatwa mikono ili nisife.

Mama yangu alikuwa na umri wa miaka 17 nilipo- ngua vibaya sana hivi kwamba ilihitaji kukatwa ili
zaliwa mwaka wa 1960. Baba alimwacha mama kuzuia sumu isiingie kwenye damu. Unaweza ku-
kabla ya mimi kuzaliwa. Mimi na mama tuliishi pa- wazia jinsi tukio hilo lilivyokuwa pigo kubwa kwa
moja na babu na bibi (nyanya) katika mji mdogo mama, babu, na bibi yangu. Kwa kuwa nilikuwa
wa Burg, nchini Ujerumani Mashariki ambayo za- mtoto, sikuelewa vizuri jinsi ambavyo kutokuwa
mani ilikuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Ujeru- na mikono kungeathiri maisha yangu.
mani. Watu wengi katika mji huo hawakuamini Baada ya kulazwa hospitali kwa muda, nilianza
Mungu, hata familia yetu ilikuwa na maoni hayo. tena kwenda shuleni. Watoto walinitania, walini-
Hatukuona umuhimu wa kumwamini Mungu. sukuma, na kunirushia vitu kwa kuwa sikuweza
Nilipoendelea kukua, nilifurahia kutunzwa vi- kujilinda. Maneno yao ya ukatili na kutojali yalini-
zuri na Babu. Babu alinituma kufanya kazi mbali- fanya niumie sana. Hatimaye, nilihamishiwa Shule
mbali, kama vile kukata matawi kwenye miti. Niki- ya Watu Wenye Ulemavu ya Birkenwerder, ni shu-
wa mtoto, nilipenda sana mambo hayo. Maisha le ya bweni kwa watoto wenye ulemavu. Kwa kuwa
yangu yalikuwa yenye shangwe na furaha. shule ilikuwa mbali sana na nyumbani, mama,
babu, na bibi yangu hawakuweza kunitembelea.
AKSIDENTI YABADILI MAISHA YANGU
Nilionana nao wakati wa likizo pekee. Kwa miaka
Tukio fulani la kutisha lilitokea nilipokuwa na kumi iliyofuata, nilikua bila malezi yao.
umri wa miaka saba. Ilikuwa mwanzoni mwa mwa-
ka wangu wa pili tangu nianze shule. Nilipokuwa KUISHI BILA MIKONO
njiani nikirudi nyumbani, nilipanda katika nguzo Nilijifunza kutumia miguu yangu kufanya kazi
ya umeme. Nikiwa urefu wa futi 25 (mita 8) kuto- mbalimbali. Wazia ukila chakula kwa uma au kiji-
ka chini, nilipigwa na shoti kubwa ya umeme na ko, ukitumia vidole vya miguu! Kwa kiasi fula-
kupoteza fahamu. Nilipoamka nikiwa hospitalini, ni nilifaulu kujifunza ustadi huo. Pia, nilijifunza
sikuhisi uwepo wa mikono yangu. Mikono iliu- kupiga mswaki na kuchana nywele kwa kutumia

Na. 6 2016 13
Kuwahubiria
wengine habari
njema hunipa
furaha

miguu. Hata nilitoa ishara kwa miguu nilipozu- hakuna Mungu. Kuanzia siku hiyo, nilianza ku-
ngumza na watu. Naam, miguu ikawa kama miko- mwepuka mtu huyo.
no yangu. Baada ya muda fulani, mfanyakazi mwenzangu
Nilipokuwa tineja, nilipenda kusoma machapi- alinialika kuitembelea familia yao. Tulipokuwa tu-
sho ya sayansi. Nyakati fulani nilijiwazia nikiwa kinywa kahawa, wazazi wake walianza kuongea
na mikono bandia ambayo ingeniwezesha kufanya kuhusu Mungu, yaani, Yehova. Kwa mara ya kwa-
kila kitu. Nilipokuwa na umri wa miaka 14 nilianza nza nilisikia kwamba Mungu ana jina. (Zaburi
kuvuta sigara. Nilihisi kwamba kuvuta sigara kuli- 83:18) Hata hivyo, niliwaza hivi: ‘Ingawa wameta-
ja jina la Mungu, bado naamini hakuna Mungu.
fanya nijiamini na kuwa sawa na watu wengine. Ni
Nitawathibitishia kwamba huo ni uwongo.’ Nikiwa
kama nilisema: ‘Bila shaka, mimi pia ninaweza ku-
na uhakika na maoni yangu, nilikubali tuwe na
fanya hivyo. Sigara huvutwa na watu wazima iwe
mazungumzo ya Biblia. Kwa kushangaza, nilishi-
wana mikono au hawana.’ ndwa kuthibitisha kwamba hakuna Mungu.
Nilikuwa mwenye shughuli nyingi na nilijihusi- Kadiri tulivyochunguza unabii wa Biblia, maoni
sha na utendaji wa kijamii. Nilijiunga na Free Ge- yangu kwamba hakuna Mungu yalianza kubadili-
rman Youth, chama cha Kisoshalisti kilichofadhili- ka. Unabii mwingi umetimia, ingawa uliandikwa
wa na serikali, nikawa karani, cheo cha juu katika mamia au hata maelfu ya miaka mapema. Wa-
chama. Pia, nilijiunga na kikundi cha uimbaji, ni- kati fulani, tulilinganisha hali ya ulimwengu na
litunga mashairi, na kushiriki michezo ya watu we- unabii wa Mathayo sura ya 24, Luka sura ya 21,
nye ulemavu. Baada ya kuhitimu masomo ya ufu- na 2 Timotheo sura ya 3. Kama vile dalili fula-
ndi, nilianza kazi katika kampuni fulani kwenye ni zinavyoweza kumsaidia daktari kutambua ugo-
mji wetu. Nilipoendelea kukua, mara kwa mara ni- njwa, mambo yaliyo katika unabii huo yalinisaidia
livaa viungo vya bandia ili nionekane mtu kamili. kutambua kwamba tunaishi katika kipindi amba-
cho Biblia hukiita “siku za mwisho.”1 Nilishangaa
KUPOKEA KWELI YA BIBLIA sana. Ninajionea unabii huo ukitimia.
Siku moja nilipokuwa ninasubiri treni ili kwe- Niliamini kwamba yale niliyojifunza ni kweli.
nda kazini, mwanaume fulani alikuja na kuzu- Nilianza kusali kwa Yehova Mungu na nikaacha
ngumza nami. Aliniambia niwazie wakati ambao kuvuta sigara, ingawa nilikuwa mvutaji wa sigara
Mungu atanirudishia tena mikono yangu miwi- kwa zaidi ya miaka kumi. Niliendelea kujifunza
li. Nilishangaa! Kwa kweli, nilitamani kuwa na 1 Kwa habari zaidi kuhusu siku za mwisho, soma sura ya 9, “Je, Tu-
mikono, lakini wazo hilo lilikuwa kama hadithi naishi Katika ‘Siku za Mwisho’?” ya kitabu Biblia Inafundisha Nini
Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, na kinachopatika-
na jambo lisilowezekana! Mimi niliamini kwamba na kwenye tovuti ya www.jw.org/sw.

14 MNARA WA MLINZI
Biblia kwa karibu mwaka mmoja. Aprili 27, 1986, ntho 11:29) Kwa kuwa bado nina akili na sauti, ni-
nilibatizwa kwa siri katika kidimbwi cha bafu, kwa najitahidi kuwasaidia wengine licha ya ulemavu
kuwa wakati huo Mashahidi walikuwa chini ya ma- wangu. Kwa sababu sina mikono, ninaelewa vizuri
rufuku Ujerumani Mashariki. hali ya watu wengine wenye udhaifu. Ninajua jinsi
ambavyo wao huhisi wanaposhindwa kufanya ja-
KUWAHUBIRIA WENGINE
mbo fulani wanalotaka kufanya. Ninajitahidi ku-
Kwa sababu ya marufuku, tulifanya ibada katika watia moyo. Kuwasaidia wengine kwa njia hiyo hu-
vikundi vidogo kwenye nyumba za watu, na nili- nifurahisha.
wajua waamini wachache tu. Bila kutarajia, niliku-
baliwa na serikali kusafiri kwenda Ujerumani Ma- YEHOVA HUNISAIDIA KILA SIKU
gharibi, ambako Mashahidi hawakuwa wamepigwa Kusema kweli, nyakati nyingine mimi hushuka
marufuku. Kwa mara ya kwanza, nilihudhuria ku- moyo. Ninatamani kuwa mtu kamili. Ingawa ni-
sanyiko na kukutana na maelfu ya ndugu na dada. naweza kufanya kazi nyingi za kila siku, ninatu-
Hilo lilikuwa tukio la pekee sana. mia muda, jitihada, na nguvu nyingi kuliko ili-
Baada ya Ukuta wa Berlin kubomolewa, Ma- vyo kawaida. Ninakumbuka wazo hili kila siku:
shahidi wa Yehova waliondolewa marufuku. Hati- “Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yeye ana-
maye, tulimwabudu Yehova Mungu kwa uhuru. yenipa nguvu.” (Wafilipi 4:13) Kila siku Yehova
Nilitamani kufanya mengi zaidi katika kazi ya ku- hunipa nguvu ili kufanya kazi za “kawaida.” Ni-
hubiri. Hata hivyo, niliogopa sana kuzungumza mejifunza kwamba Yehova ataendelea kunisaidia.
na watu nisiowafahamu. Nilijiona dhaifu kwa sa- Hiyo ndiyo sababu sitaacha kumtumikia.
babu ya ulemavu na kwa kuwa niliishi kwa miaka Yehova amenibariki kwa kunipatia familia, ja-
mingi katika shule ya watu wenye ulemavu. Lakini mbo ambalo sikufurahia nilipokuwa mtoto na ki-
mwaka wa 1992, nilijaribu kuhubiri saa 60 kwa jana. Nina mke mzuri sana, Elke, ambaye ana upe-
mwezi. Nilifaulu kufanya hivyo na nilipata sha- ndo na huruma. Kwa kuongezea, nipo kwenye
ngwe kubwa. Kwa hiyo, niliamua kufanya hivyo familia ya ulimwenguni pote ya mamilioni ya Ma-
kila mwezi na niliendelea kwa karibu miaka mi- shahidi wa Yehova ambao ni ndugu na dada zangu
tatu. wa kiroho.
Mimi hukumbuka maneno haya ya Biblia: “Ni Pia, ninafarijiwa sana na ahadi ya Mungu ya Pa-
nani aliye dhaifu, nami si dhaifu?” (2 Wakori- radiso, atakapofanya “vitu vyote kuwa vipya,” ku-
tia ndani mikono yangu. (Ufunuo 21:5) Ninaele-
Nikiwa na mke wangu mpendwa, Elke
wa ahadi hiyo vizuri sana ninapotafakari mambo
ambayo Yesu alifanya alipokuwa duniani. Kwa
muda mfupi tu, alimponya kilema na kurudisha si-
kio la mtu lililokuwa limekatwa. (Mathayo 12:13;
Luka 22:50, 51) Ahadi za Yehova na miujiza ya
Yesu hunipa uhakika kwamba hivi karibuni nita-
kuwa tena mtu kamili.
Hata hivyo, baraka kubwa zaidi ni kumjua Yeho-
va Mungu. Yeye amekuwa baba na rafiki yangu,
nguvu na mfariji wangu. Ninahisi kama Mfalme
Daudi aliyeandika hivi: “Yehova ni nguvu zangu
. . . Nami nimesaidiwa, hivi kwamba moyo wangu
unashangilia.” (Zaburi 28:7) Hii ndio kweli amba-
yo ninataka kuishikilia maishani mwangu. Nimei-
pokea bila kuwa na mikono. ˇ

Na. 6 2016 15
BIBLIA INASEMA NINI?

Je, Mungu husikiliza sala zote? Je, unapaswa kusali ukiwa katika
JE, ANAJIBU SALA ZA . . . mkao fulani hususa?
˙ Kila mtu BAADHI YA WATU WANAAMINI kwamba wanapaswa
˙ Baadhi ya watu kupiga magoti, kuinamisha kichwa, au kuweka
˙ Hamjibu yeyote mikono pamoja wanaposali. Wewe una maoni
gani?
BIBLIA INASEMA HIVI
“Yehova yuko karibu na wote . . . wanaomwitia BIBLIA INASEMA HIVI
yeye katika ukweli.”—Zaburi 145:18. Mungu alisikiliza watu waliosali wakiwa ‘wame-
keti,’ ‘wamesimama,’ ‘wamelala kifudifudi,’ au
MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA ‘kupiga magoti.’ (1 Mambo ya Nyakati 17:16;
˙ Mungu hasikilizi sala za watu wasiomtii. 2 Mambo ya Nyakati 30:27; Ezra 10:1; Mate-
(Isaya 1:15) Hata hivyo, wanaweza ‘kunyoosha ndo 9:40) Mungu hahitaji tuwe katika mkao
mambo’ kati yao na Yehova kwa kubadili njia zao. fulani hususa tunaposali.
—Isaya 1:18.
˙ Ili Mungu ajibu, ni lazima sala ipatane na NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?
matakwa yake yanayotajwa katika Biblia. ˙ Mungu huwasikiliza watu wanyenyekevu.
—1 Yohana 5:14. —Zaburi 138:6.
˙ Unaweza kusali kwa lugha yoyote au hata
kimyakimya.—2 Mambo ya Nyakati 6:32, 33;
Nehemia 2:1-6.

Tafadhali nitumieni kitabu LUGHA


Biblia Inafundisha Nini Hasa? JINA
Kwa habari zaidi, soma sura ya 17 ANWANI
ya kitabu hiki, kilichochapishwa na
Mashahidi wa Yehova
BIBLIA
INAFUNDISHA Pia, kinapatikana
NINI Hasa? kwenye www.jw.org/sw
Ili upate anwani zetu, tazama ukurasa wa 2

s
n Pakua
matoleo yaliyotangulia p kwenye intaneti katika
gazeti hili na Biblia inapatikana Tembelea
www.jw.org/sw,
o bila malipo
wp16.6-SW

lugha zaidi ya 130 au tumia alama hii


160914

kufungua Tovuti yetu

You might also like