Professional Documents
Culture Documents
kikundi
9/25/2023
2. SEHEMU YA PILI
3.1 DHUMUNI KUU KIKUNDI
a. Kushirikiana kijamii na kiuchumi
Malengo mahususi:
(a) Kushirikiana na kusaidiana wakati wa shida na raha.nk
(b) Kuwezesha wanakikundi kuimarishana kiuchumi na hali ya maisha kwa:-
i. Kupokea na kuweka michango ya fedha za wanakikundi
ii. Kuanzisha na kuendeleza shughuli zozote halali za kiuchumi kwa manufaa ya
wanakikundi kama itakavyokubaliwa katika mkutano halali wa wanakikundi
iii. Kuwezesha kifedha shughuli binafsi za wanakikundi kwa masharti
yaliyokubaliwa na maridhiano ya wanakikundi
iv. Kuhamasisha ushirikiano na wanakikundi wenye changamoto mbalimbali kama
ulemavu, uzee, uyatima, na magonjwa mbalimbali
3. SEHEMU YA TATU
3.1 UANAKIKUNDI
3.1.1 Sifa za kuwa Mwanakikundi
(a) Awe raia wa Tanzania.
(b) Awe ni mtu mwenye akili timamu na wa kuaminika.
(c) Awe anayefanya kazi iliyo rasmi ama isiyo rasmi au shughuli zinazokubalika kisheria
(d) Awe ametimiza umri wa miaka 18.
(e) Awe ni mtu aliye tayari kuiheshimu, kuitetea na kuongozwa kwa katiba ya kikundi na
kanuni zake
(f) Awe ametimiza taratibu zote za kujiunga na kikundi:
i. Kujaza fomu ya maombi na kukubaliwa na uongozi kisha kupitishwa na mkutano
mkuu kuwa mwanachama.
ii. Kulipa kiingilio kama inavyoonyeshwa katika kanuni za kikundi, na taratibu za
kikundi au kama itakavyo amuliwa na Mkutano halali wa kikundi.
iii. Ili kuondoa tofauti ya michango kati ya mwanakikundi ambaye yupo na yule
anayetaka kujiunga, wanakikundi watakubaliana kiasi cha fedha atakachotakiwa
kuchangia mtu anayetaka kijiunga na muda wa kukamilisha mchango huo.
5. SEHEMU YA TANO
6. SEHEMU YA SITA
7. SEHEMU YA SABA
7.1 Kamati za Kikundi
(a) Kikundi kitakuwa na kamati za kudumu zitakazosaidiana na Kamati Kuu kufanikisha
mipango na shughuli za kikundi
(b) Kamati nyingine zozote za Muda zinaweza kuundwa katika mikutano ya kawaida ya
mwezi kulingana na matukio au umuhimu wa kuwepo kamati hizo.
7.1.1 Kamati Tendaji
(a) Itakuwa na viongozi wakuu wawili wa kikundi (kifungu 6.3.1 (a)) pamoja na wenyeviti
wote wa kamati mbalimbali zilizoundwa kwa mujibu wa katiba au kanuni za kikundi.
(b) Kamati tendaji itakuwa na kazi zifuatazo:
i. Kupitia na kujadili mapato na matumizi ya kikundi kabla ya kufikishwa kwenye
Mkutano Mkuu wa Wanakikundi
ii. Kujadili na kupitisha maombi ya wanakikundi wapya watakaoomba kujiunga na
kikundi
iii. Kusimamia utendaji na utekelezaji wa mipango na shughuli za kikundi.
iv. Kusimamia masuala yote ya katiba na kanuni za kuendesha kikundi.
7.1.2 Kamati ya Nidhamu na Maadili
(a) Watachaguliwa na wanakikundi wasipungua theluthi mbili ya wanachama katika uchaguzi
mkuu wa kikundi.
(b) Itakuwa na watu wasiopungua wawili.
(c) Itakuwa na jukumu la kushughulikia masuala ya nidhamu na maadili ya kikundi kwa
viongozi na wanakikundi wa kawaida
7.1.3 Kamati ya Fedha na Mikopo
(a) Watachaguliwa na wanakikundi wote katika uchaguzi mkuu wa kikundi.
(b) Itakuwa na watu wasiopungua wawili wakishirikiana na mwenyekiti na katibu
(c) Itafuatilia masuala yote ya fedha na rasilimali nyingine za kikundi
(d) Itaratibu na kupitisha mikopo ya kikundi na wanakikundi kwa mujibu wa katiba au kanuni
za kikundi
8. SEHEMU YA NANE
9. SEHEMU YA TISA