Professional Documents
Culture Documents
Written by
Maximilian Rioba
mrioba@me.com
+255715167419
EXT. MTAANI - MORNING
MALAMSHA
Yaani naingia hapo dakika sifuri
mwanangu msiniache tafadhali
nawaomba.Stendi hii hapa naiona.
MALAMSHA (CONT'D)
Jamani, kwema? Wote kumbe
tumechelewa? Mbona huyu kijana
kanidanganya kwamba ni mimi peke
yangu nimechelewa?
DETECTIVE AYSHA
Do not shoot until you hear from
me. Hakuna risasi hata moja
inayopigwa mpaka tuhakikishe ni wao
kweli. Copy?
KAZOLA
Wauza unga wanne tumewakurupusha
wakiwa maeneo ya chuo cha ICU.
(MORE)
2.
KAZOLA (CONT'D)
Wakakimbia, wawili wameingia mtaa
wa Kizera nyuma ya hoteli ya Kusini
mmoja aliyekuwa ndiye prime
anaelekea mashariki karibu na hapo
ulipo afande. Najaribu kumtega
aingie kumi na nani then unipe amri
nimtoe roho.
DETECTIVE AYSHA
Okay, sikiliza Mazola, nakujua
vizuri sana. Kama unaweza kumkamata
bila kumpiga risasi get his ass
atatusaidia sana upelelezi. Do not
shoot hadi uone imeshindikana. And
besides unajua kabisa bila evidence
kwamba anauza au amebeba dawa za
kulevya hurudhusiwi hata kumfinya,
Umenisoma?
KAZOLA
Kuna haja gani afande kufanya kazi
kwa vikwazo kiasi hicho? Eddy Big
na Kalito wanajulikana.
DETECTIVE AYSHA
So huyo ni Kalito au Eddy Big?
Which one is he?
KAZOLA
Huyu atakuwa ni Kalito.
DETECTIVE AYSHA
Kazola, please don’t make my
morning stressful. Narudia tena, Do
not freaking shoot hadi uwe na
uhakika. Copy?
KAZOLA
Tunakimbizana na wahalifu wanaouza
dawa za kulevya kwa wanafunzi wetu
and then unanipangia namna ya
kumkamata? Kweli afande? Ni sawa
hiyo?
DETECTIVE AYSHA
Have you copied?
MASHA
Nimemuona afande, anakuja upande
huo ameshikilia mfuko ana koti
jeusi na T-shirt nyeupe
iliyochafuka chafuka.
DETECTIVE AYSHA
Do not shoot. Kazola, narudia do
not shoot. Mkamate bila kumjeruhi.
MASHA
Afande hao watu ni wabaya sana.
Akigeuka akamuona Kazola
anamkimbiza atamuua. I suggest a
shoot.
DETECTIVE AYSHA
I said do not shoot.
KAZOLA
Suspect ana mfuko nahisi una gun.
DETECTIVE AYSHA
Kazola, usiipime imani yangu. How
far are you to the suspect?
KAZOLA
Kama mita 25 hivi.
DETECTIVE AYSHA
And you are sure ni yeye?
KAZOLA
Asilimia mia moja afande.
DETECTIVE AYSHA
Mita 25 unaweza kumuamuru asimame
anyooshe mikono juu na aweke chini
kila alicho nacho.
KAZOLA
Anaongeza mbio afande. Please let
me finish him, atatuponyoka huyu.
WACOLOR
Nimempenda huyo mwenye nguo ya
njano hapo. Get her. Also mchukue
huyo mweusi hapo nyuma.
JACKIE
What about this one nanayeingia?
WACOLOR
I don’t like her chest.
WONDER
Oh yes, I see the leadies looking
steaming hot. Kama una u feel mziki
don’t feel shy to show us what your
momma gave you, step to the dance
flow baby, you only live once.
Where my first year ladies at? Let
me hear you say yeeeeah!
WACOLOR
Get that one anayeongea na mwenzake
pale pembeni.
JACKIE
Nimemuongelesha alivyoingia, she’s
kinda shy. Do you think atakufaa?
WACOLOR
Shy girls are the best. Get her.
CUT TO:
NAYDA
Mbona you told me it was just a
birthday party ya Sam? What’s with
all this?
MARIA
Ask him, si huyu hapa? Eti babe
Nayda anasema mbona hii party is
more of a house party than a
birthday party? What’s up?
SAM
Hey, it’s a combo. Let’s just have
fun guys, okay? Drink, eat, merry,
and do whatever you want to lit up
the vibe.
NAYDA
You know sinywi pombe, right?
SAM
Oh, I din’t know, kwa nini?
NAYDA
Beacuse nimeamua, I don’t want to
consume alcohol or smoke. Do you
have a problem with me not drinking
and smoking?
MARIA
Kwani is it a must, babe leave
Nayda alone. There are a million
ways to have fun in this world than
drinking and smoking.
CUT TO:
BOY ONE
Yoh, hivi mnauhakika kweli Vamps
halijui hili so?
BOY TWO
Mwana kwanza mchana mimi nilikuwa
naye chuo. Hajui chochote. Angekuwa
anajua angeshakinukisha
6.
BOY ONE
Ameshafika hapa kwani?
BOY THREE
Nimemuona na pisi yake ile ya first
year and another chic. Wako ndani.
Twenzetu.
CUT TO:
NAYDA
I can have a cup cake and soda. It
that okay Sam?
Sam anajua kuwa cake zina bangi. Anamuangalia kwa jicho flani
akiamini kwamba baada ya kula cake Nayda atapagawa na bangi.
SAM
Sure, you can definitely have cup
cakes, and have them abundantly.
Usijali, nalipia mimi. Excuse me
miss, can you bring my friend some
cup cakes and a cold glass of coke
please?
NAYDA
Diet coke!
USHER
Sure, nimletee cup cakes ngapi?
SAM
Kama mbili hivi. Au unataka ngapi
Nayda?
NAYDA
Nne, please. And the coke should be
very cold, okay?
SAM
Sure, mletee mambo. Coz after that
we are really gonna party for real.
Afu Maria anaongea na nani at this
hour while I’m here, on my
birthday?
7.
NAYDA
Heh, Sam embu acha hizo basi, you
think she’s cheating? Anaongea na
sister ake bana hebu chill kha!
CUT TO:
MARIA
Yaani mpaka summer ndiyo uje?
That’s like forever sis.
MARIA’S SIS
Girl summer is just around the
corner. Ntakuja tu. Vipi birthday
boy hajambo?
MARIA
He’s here thinking that I’m talking
to some guy. Kaniganda like an eel.
Talk to him.
CUT TO:
TRACY
She’s here with her nerdy little
boyfriend.
KITANJEI
Kwa hiyo tunafanyaje sasa?
TRACY
You know nimesikia semester hii una
course mbili unatufundisha, right?
KITANJEI
Absolutely.
8.
TRACY
You want Maria, I want my grades,
it’s a fair trade.
CUT TO:
CUT TO:
MARIA
Baby, is she...
SAM
Relax baby, she’s going to be okay
bana. Just a couple of edibles
nothing much.
MARIA
Sam, what do you mean nothing much?
It’s edibles! Ni bangi!
SAM
Why are you shouting?
MARIA
Hivi do you have any idea
nimewezaje leo ijumaa kutoka and
come to your stupid birthday? Any
freaking clue?
CUT TO:
AYSHA
Where is Maria?
CUT TO:
SAM
Maria why are you making a big deal
out of this?
MARIA
You, mh….. grow up Sam.
SAM
What? Seriously?
MARIA
Mh.. you know what, we are leaving.
Enjoy your birthday.
CUT TO:
TRACY
Hey, Is he acting a fool?
MARIA
No, he’s just being himself
TRACY
Boys always do, you need a man.
MARIA
But I love my boy.
10.
TRACY
Maria, stop wasting your time. Hivi
unajua bado anakuulizia? Nilikupa
namba yake but hujampigia wala kum
text, kwa nini?
MARIA
It’s hard for me to give him what
he wants. I wish anielewe tu. I
have one boyfriend and that’s it. I
can’t mix men like clothes.
TRACY
Who said he wants to be your
boyfriend?
MARIA
Tracy, the answer is no. I can’t be
his sex buddy, side chic, mistress,
one night stand or anything like
that.
TRACY
Sweetie, there’s sex that takes you
nowhere.
TRACY (CONT'D)
I’ll meet you at the VIP darling.
MARIA
Wait, is that Oscar Delarento?
TRACY
MARIA
I have never had sex before. Not
even with my boyfriend. So I’m
definitely going somewhere, if you
ask me.
TRACY
There is always a power dynamic at
play, sweetheart. Even a broken
clock is correct.
11.
MARIA
Twice a day!
TRACY
You know there’s a first time for
everything Maria, right?
MARIA
Right! And when the first time of
anything is done at the right time,
the right way it becomes more
meaningful than kukurupuka bila
mpango.
CUT TO:
NICO
Kitu chochote kile kisije
kukutenganisha na upendo wa kweli
Sam. Hiyo ndiyo hulka ya uanaume wa
kweli.
NICO (CONT'D)
Wakati unajitahidi kuendelea
kulinda na kulithamini penzi lako
kumbuka kwamba adui halai hata
kidogo. Hata usiku kama sasa hivi
yuko macho. Look at her! Una kazi
bro. Na hiki kilichotokea leo, hii
party, drinks, music and all ni
sehemu ndogo sana ya mengi
tuliyokuandalia. Lakini ni lazima
unifanyie favor kidogo. Maelekezo
yote yako humo kwenye zawadi.
Ukikwama nipigie. Happy birthday
boy!
SAM
Hallo!
12.
WACOLOR
Happy birthday Sam.. Rafiki zako
wamekuingiza kwenye matatizo
makubwa sana. Sijui kama unalijuia
hilo.
SAM
We ni nani?
WACOLOR
Mimi ni msamaria mwema na nataka
nikusaidie usiku huu huu yaishe.
SAM
What are you talking about?
WACOLOR
Wiki mbili zilizopita kuna watu
walikuletea assignment uwasaidie.
In the process waka botnet computer
yako.
A moment of silence.
WACOLOR (CONT'D)
Najua unawasaidia wanafunzi wengi
sana wa IT chuoni. Na sio rahisi
kuwakumbuka wote. But hawa watatu
walikuletea assingment inayohusu
hacking ya system, ukawasaidia
ukidhani ni assignment tu kumbe
ilikuwa ni real deal. Wakafanya
Exfiltration, wakaiba fedha za chuo
shilingi milioni kumi na
kusababisha leakage ya mitihani. Do
you remember?
SAM
No, I don’t.
WACOLOR
You know Vamps right?
WACOLOR (CONT'D)
I am Vamps.
WACOLOR (CONT'D)
Then you know what I’m talking
about.
13.
WACOLOR (CONT'D)
You are facing 25 years maximum
jail time and this will escalated
by the judges based on the nature
of the crime.
SAM
They said it was an assignment
WACOLOR
Which turned out to a be punishable
offense.
WACOLOR (CONT'D)
You are a good kid and I know
hukuhusika kwenye huo wizi. Ndo
maana tunataka kukutoa from this
ASAP.
WACOLOR (CONT'D)
You are aware that your birthday
party is mixed with my house party
kwa makusudi kabisa na tumeingia
gharama just to have you enjoy your
day, right?
SAM
Ameniambia Nico, asante sana.
WACOLOR
Ondoka hapo sasa hivi, nenda mbezi
beach mtaa wa Duma nyumba namba 7
utakutana na mtu atajitambulisha
kama Tisha. Atakusaida, kila kitu
kitaisha leo leo.
CUT TO:
NAYDA
Mimi napenda sana keki lakini
sijawahi kula keki tamu kama hizi.
(MORE)
14.
NAYDA (CONT'D)
Naomba niongezee nne tafadhali,
okay darling?
CUT TO:
USHER
But nimesha punch kule dear, nani
atazilipia?
MARIA
But hatujazigusa
NAYDA
Si tuziguse tu jamani? Kwani kuna
tatizo gani kwenye kugusa tu? “Just
a touch of love, a little bit”
Hahahaha. I bet you don’t know
nothing about that, do you?
MARIA
Can I use your phone?
NAYDA
Sure, simu yako imekuwaje kwani?
MARIA
Imezimika.
NAYDA
Washa mama, washa washa, washa moto
wa imani watu waungue, watubu
waache dhambi.
CUT TO:
WACOLOR
Kwa nini huyo mgonjwa bado yuko
hai?
NICO
Hatakuwa hai baada ya masaa mawili
madam. Nimeshapanga kila kitu.
CUT TO:
MARIA
What the hell? Why did you take all
that shit Nayda?
NAYDA
Achana na mimi Maria. Mi sio mtoto
wako. Mimi ni mtu mzima na uzima
wangu. Sihitaji chochote from you.
Niache.
MARIA
I need to help you clean and take
you to your room niende zangu home.
This is messed up for real Nayda.
You jumping on things you’ve never
tried before. Look at yourself now.
NAYDA
Kwenda zako mtoto wa mama wewe.
Kwanza you should stop worrying
about me. Mama ako anakuja
kukuchukua chuo kila Ijumaa kama
kitoto cha daycare basi
unajikuuuuta. Tena inawezekana
anakutafuta right now, Maria
Mariaaaaaaaa!
MARIA
Nayda, stop. Stop it right there.
NAYDA
Kwenda mtoto wa mama wewe. Mimi
mgumu sana Sio maandazi maandazi
kama wewe. Familia yangu ilishindwa
kuja kwenye graduation yangu.
Nilijidai tu niko pa lakini
niliumia sana.
(MORE)
16.
NAYDA (CONT'D)
Watu walikuja na ma V8, coster,
wakajiachia na familia zao kasoro
mimi tu. Lakini niliwatandika na
division one moja baab kubwa. Nalia
lakini naumia, mamamamamae. Usini
dictate kwenye vitu kama hivi
Maria. Let me have some fun. Kama
unasepa, sepa. Achana na mimi.
CUT TO:
AYSHA
Haki ya Mungu tusipompata mwanangu
leo utaondoka nyumbani kwangu.
CUT TO:
MARIA
I’m so sorry Nayda. Your past has
nothing to do with your present or
future. You can shape your future
from now baby.
NAYDA
Naumia sana. Hujui tu.
MARIA
I know baby, I do.
NAYDA
Sometimes natamani tu nife nipotee.
Nina uchungu sana Maria hujui tu.
My life we acha tu, usinione hapa
ukadhani niko poa naumwa moyo,
naumwa, naumia sana Maria, naumia
kuliko unavyojua.
CUT TO:
17.
MALAMSHA
Kama ya kheri halo, kama ya shari
kata, mwenye simu hii hapokei tena
habari mbaya. Keshapigwa na maisha
vya kutosha. Halo nani mwenzangu?
NAYDA
Asalaam Waleikhum Warahmatullah
Wabarakatuh. Mie jina langu Nayda
Bit Said Suleiman Hafidh.
MALAMSHA
Daaah, Waleikhum Salaam moyo wangu.
Nisamehe mama yangu mie, mama mzaa
chema Bit Said mwenyewe, moyo wa
mwanao Malamsha Bin Kombo, enhe,
vipi habari mwanangu, kwema?
NAYDA
Alhamdullilah baba, mie nimekupigia
kukupa habari njema.
MALAMSHA
Enhe, nipe habari bibie.
NAYDA
Mwanao nimemaliza kidato cha sita
na wiki ijayo ndiyo tuna
graduation, baada ya hapo tunakaa
tena wiki moja tunafanya mtihani wa
Taifa, kisha narudi zangu nyumbani
kusubiria matokeo.
MALAMSHA
Daaah, ama kweli siku hazigandi,
tunmshukuru sana Mungu maana baba
yako hapa naona kama ndoto vile.
(MORE)
18.
MALAMSHA (CONT'D)
Ni juzi juzi tu ulikuwa la kwanza
leo umemaliza? Alhamdullilah kwa
kweli. Enhe sasa tunafanyaje mama
yangu?
NAYDA
Najua hali ya nyumbani ilivyo, ila
kama kungekuwepo uwezekano wewe na
mama mkaja kwenye mahafali nadhani
ningekuwa mwnafunzi mwenye furaha
kuliko wanafunzi wote hapa. Lakini
kama itashindikana baba usijali
naelewa kabisa.
NAYDA (CONT'D)
Hello, baba upo?
MALAMSHA
Ninajisikia vibaya sana kwamba
sijawahi kufika shuleni kwako
mwanangu hadi leo unamaliza. Ni
aibu mimi kama baba yako kukosa
fedha hata za nauli tu Nayda.
NAYDA
Sio lazima baba, naelewa hali ya
nyumbani.
MALAMSHA
Nakushukuru mwanangu kwa uelewa.
Hiyo Kradeshin ni wiki ijayo tarehe
ngapi?
NAYDA
Ijumaa tarehe ishirini na saba.
MALAMSHA
Sawa mwanangu, kila la kheri.
CUT TO:
MALAMSHA
Unajua yale mnayoyasema hamyajui
hata kidogo. Kumpa mtoto wa kike
fursa ya elimu ni jambo la pekee
sana.
FARID
Na ndiyo maana tulikwambia umuoze
alipomaliza form four ili kaka
uepukane na hizi adha za kuomba
omba msaada. Akina Zuwena si rika
lake huyo? Mbona wameolewa na
hatushughuliki nao tena?
MALAMSHA
Farid, wewe ni mdogo wangu kabisa
ujue.
FARID
Mama mmoja baba mmoja lakini kaka
wewe mbishi sana, ulitaka
kutuaminisha kwamba Nayda ndiye
mtoto mwenye akili kuliko watoto
wote wa ndugu zako. Beba sasa
msalaba umsaidie.
NUSRAH
Shemeji Farid mbona uonaongea
maneno kama hayo? Ni nani
aliyewahi....
FARID
Tena shemeji wewe ndo usiseme
kabisa. Wewe unaamini kwamba mmezaa
professor mwenye ma PhG yake kama
yote wengine wote mavi.
MALAMSHA
Farid, huko unakoenda unavuka
mipaka. Nimekuomba unikopeshe fedha
niende kumuona mwanao. Kama hutaki
basi sema tu sitaki yaishe mdogo
wangu.
FARID
Sitaki!
20.
MALAMSHA
Nayda atafika mbali sana mke wangu.
Watakuja hawa wanatembelea matako
kuomba awasaidie wallah nakwambia
nikiwa hai mimi Malamsha Bin Hafidh
hapewi mtu thumni. Kweli mtoto ana
akili tusimpe nafasi ya kusoma
tuishie kumuoza kwa mwanaume? Na
hiyo kradesheni nitaenda, na
watashangaa na roho zao kavu kama
korosho za kiangazi.
NUSRAH
Usijali mume wangu, tumetoka mbali
sana na binti yetu. Kama ni mapenzi
ya Mungu utaenda, na kila jambo
litafanyika sawasawa na apangavyo
yeye.
MALAMSHA
Kwani kwa nini sisi? Kwa nini sisi
tumekuwa watu wa shida tu kuomba
omba, kuishi kwa dhiki,
kudhalilishwa hata na ndugu wa
damu? Eh Mola wetu tumekukosea nini
sie ukoo wa Malamsha?
NUSRAH
Ni nani walioandikiwa laana na
Mwenyezi Mungu? Wapo watu hospitali
leo hii tunavyoongea wanakata roho,
wengine wamevunjika vunjika kwenye
ajali, sie tumepewa pumzi ya uhai,
afya, na amani. Hakuna tena utajiri
duniani hapa zaidi ya afya, pumzi
ya uhai na amani mume wangu.
Yatapita tu tusimdhihaki Mwenyezi
Mungu kwa mitihani tunayoipitia.
Tuseme Alhamdullilah kwa kila kitu
mume wangu. Siku moja tutaivuka hii
hatua.
MALAMSHA
Amin Yarab. Asante sana mke wangu.
Mungu hatatutupa.
21.
NUSRAH
Hallo, ni nani mwenzangu?
TWALIB
Mwambie sheikh nimetafakari sana
kuhusu mwanetu. Na mimi namchukulia
Nayda kama mwanangu kabisa wa
kumzaa ingawa Mnyaz Mungu
hakunijaalia watoto.
NUSRAH
Nayda mwanao kabisa shemeji.
Usiseme Mungu hajakujaalia. Amekupa
Nayda.
TWALIB
Alhamdullilah kwa kweli. Na binti
ametuheshimisha kwa kweli
mashallah.
NUSRAH
Kabisa. Nayda sio mpenda makuu
engineer wetu.
TWALIB
Ah kabisa. Na uinjinia ataupata
tukiwa hapa hapa In Sha Allah.
Sasa mwambie huyo bwana
nimefanikiwa kupata kiasi kidogo
kama elfu tisini tu. Nimtumie aende
bwana kwa mtoto. Mwambie namrushia
sasa hivi kwenye simu yake. Yeye
akijaaliwa kuipata atanirudishia
siku yoyote In Sha Allah.
NUSRAH
Wallah shemeji yangu sijui nikupe
zawadi gani. Na anakusikia hapa
anakula michozi inamtoka. Mwenyezi
Mungu mwingi wa Rehema na Barka
akujaalie na kukuongezea pale
ulipotoa.
(MORE)
22.
NUSRAH (CONT'D)
Tisini kwa usawa huu sio kidogo ni
nyingi sana hadi naogopa
tutarudisha lini mwenzangu au hadi
huyo Nadya akipata ajira labda ndo
akulipe mwenyewe.
MALAMSHA
Chochote ntakachopata kitatosha tu.
Hii tisini inatosha nauli ya kwenda
na kubaki thelathini. Wallah
nikipata hamsini tu zingine leo ah
hiyo kradesheni yatanitambua mzee
Malamsha mie.
NUSRAH
Nguo ushajua utavaa ipi? Maana
wenzio watalipuka ile mbaya ujue?
Watu watakuja na ma Vx kama yote
mwenzangu. Uchague nguo nzuri
angalau upendeze kidogo mume wangu.
MALAMSHA
Hahahaha, waje na mav8, ma costa,
ma renji, mimi sijali. Koti langu
lile lile jeusi la kutokea, na ile
suruali yangu pendwa. Wakitaka
kunijua mie wawaweke watoto wao
kwenye mtihani mmoja na mama yangu
waone akavyowagalagaza. Maaaanisha.
Hebu ngoja nikimbie nisije
nikachelewa mke wangu.
NUSRAH
Sasa ukipata siupitie huko huko tu
ukate tiketi moja kwa moja baba?
MALAMSHA
Habari ndo hiyo!
23.
DETECTIVE AYSHA
Hivi kwa nini watu wanapenda
kuandika kwenye noti?
MASHA
Eti wema hauna mwisho. Sasa sijui
anategemea atajibiwa siku moja?
DETECTIVE AYSHA
Hivi unajua ni kosa kisheria
kuchafua noti?
MASHA
I know afande but tatizo ni kumpata
mchafuzi. Hapo ndio kimbembe.
DETECTIVE AYSHA
I know, right?
CUT TO:
MALAMSHA
Eh bwana eh, uko nyumbani?
MKUDE
Nipo swaiba vipi, kwema?
MALAMSHA
Naomba umkimbizie bibie simu yako
niongee naye mara moja ndugu yangu,
tafadhali.
MKUDE
Malamsha ntaanza kuwa nakuchaji
hela ujue. Mnunulie mkeo simu bwana
simu yangu sio ya kijiji.
Hahahahaha.
MALAMSHA
Mwanangu akiwa injinia tutagawa
simu kama peremende mtaani. We
ngoja tu.
MKUDE
Hahahaha, haya bwana tena Bi Nusrah
huyu hapa alikuwa amekuja kupiga
umbea na shoga yake kidawa.
MALAMSHA
Bibie,
NUSRAH
Naam mume wangu.
MALAMSHA
Mungu si Athumani. Yaani huku
nilikokuwa naenda siendi tena.
Nimepata ajali narudi nyumbani.
NUSRAH
Hebu ngoja kidogo. Sasa umepata
ajali unarudi nyumbani maana yake
nini?
25.
MALAMSHA
Mke wangu, yaani kazi ya Mungu siku
zote haina makosa. Nimepata hela,
elfu hamsini.
NUSRAH
Sasa na hiyo ajali unayosema
imekuwaje?
MALAMSHA
Sikiliza sasa, mie nilikuwa nashuka
zangu kwenye daladala, ile kushuka
tu kumbe sijui kuna mwizi huko
polisi wanamkimbiza. Mara mdada
mmoja sijui askari yule akanigonga
wakati nashuka nikaanguka nikiwa
nimeshikilia simu na ile bahasha.
Basi kiswaswadu changu pangala,
kikasambaratika. Mie sasa mawazo
yangu yote wala sio simu
kuharibika, naiwazia ile line yenye
hela maana ikipotea tena hapo
mtihani. Sasa yule dada bwana si
akanionea huruma. Kainama chini
kunisaidia kutafuta akaona
anachelewa. Mara ghafla naona
anaingia mfukoni ananipa elfu
hamsini. Elfu hamsini kahesabu noti
moja hadi tano. Kaniambia niende
kureneu line yangu. Sasa mimi kwa
ubishi si nikaendelea kuitafuta
line? Mara hamad! Hii hapa,
nimeipata. Nikachukua betri lile na
simu nikaiweza fresh ndo nikampigia
Mkude.
NUSRAH
Eh, embu ngoja kwanza. Kwa hiyo
yote haya yametokea saa ngapi?
MALAMSHA
Bwana wewe nakwambia sasa hivi
hapa. Kwa hiyo mie kwa kina Omary
siendi tena, naenda zangu kukata
tiketi kabisa ili niwe tayari,
yasije kutokea ya kutokea.
NUSRAH
Heh, makubwa mwenzangu. Ama kweli
ya Mungu mengi. Haya kuwa makini
basi mume wangu barabarani huko.
Nakuombea ufanikishe. Dooh hii nayo
historia.
26.
MALAMSHA
In Sha Allah mke wangu.
MALAMSHA
Unajua wewe huelewi mke wangu.
Nayda sijamwambia hata kwamba
nitaweza kwenda. Kwa hiyo hategemei
mimi kwenda. Ila takaponiona furaha
yake itakuwa kubwa ajabu.
NUSRAH
Sikatai mume wangu lakini fedha
hazitoshi. Siku ya kurudi
utarudije?
MALAMSHA
Siku ya kurudi anaijua Mungu. Kama
alivyopanga kwenda ndivyo
atakavyopanga kurudi. Ondoa
wasiwasi. Niandalie moka zangu, na
ile suruali yangu na koti langu.
Mengine tumuachie Maulana.
NUSRAH
Malamsha, unakoroma sana bwana hebu
lala vizuri.
MALAMSHA
Muda wa kuamka umeshafika?
27.
NUSRAH
Bado. Lakini sijui kwa nini nawaza
siumtumie tu mtoto hizo hela? Kwani
ni lazima uende?
MALAMSHA
Ah, jamani mke wangu kweli?
Unaendelea na hiyo hoja hadi saa
nane usiku? Sasa nimeshakata
tiketi, tufanyeje? Niiache iende
bure, tupoteze elfu sitini kweli
mama?
NUSRAH
Ukienda hutakukuwa na chochote cha
kumpa mtoto kama zawadi. Ukiwa na
upweke utaendelea tu kuwepo.
MALAMSHA
Mama, hebu tulale, mwenzio kesho
nina safari ndefu sana.
Atakusimulia mwanao akirudi. Sawa
mke wangu?
NUSRAH
Mh. Sawa mume wangu! Haya tulale.
MALAMSHA
Mke wangu, mbona hujaniamsha
mapema?
NUSRAH
Kwani basi linaondoka saa ngapi?
MALAMSHA
Saa kumi na mbili kamili. Sasa hivi
saa kumi na moja na robo bado
sijaondoka.
NUSRAH
Kunywa chai haraka mume wangu
utawahi tu.
28.
MALAMSHA
Hapana mama, ntachelewa acha
nijimwagie maji nikimbie.
NUSRAH
Haya maji nimeshakupashia na
kukuwekea bafuni wahi basi.
CUT TO:
MALAMSHA
Angalia kwenye simu yangu kuna
namba imeandikwa SHULE NAYDA
umpigie Matroni umtumie hela zote
zilizoko kwenye simu yangu elfu
thelethini. Na zingine elfu hamsini
ziko kenye koti. Mtumie ampe
mwanangu anunue keki ale.
(MORE)
29.
MALAMSHA (CONT'D)
Sitaweza kuwahi kwenye mahafali.
Mwambie asiache kusomea uinjinia
amsaidie mama yake. Mpe na mdoli
wake na barua yake kutoka kwa mama
yake.
GODFREY
Good afternoon detective.
DETECTIVE AYSHA
Hey baby, umefikaje hapa?
GODFREY
Nimepigiwa simu ikabidi nitoke
ofisini chap nije. How are you
feeling my love?
DETECTIVE AYSHA
There was a sack alikuwa nayo yule
mzee and some cash like 50k. Wait a
minute, naomba simu yangu baby mara
moja please.
GODFREY
Sweetheart huruhusiwi kushika
chochote right now hadi daktari
apite round jioni atupe maelekezo.
You’re not on duty sasa hivi
unaumwa na ni lazima utibiwe kwanza
upone.
DETECTIVE AYSHA
Baby I need to go, like right now,
Oh my God.
GODFREY
But why baby. Nadhani kila kitu
kilikuwa taken care of. Please
relax. Okay?
30.
DETECTIVE AYSHA
Masha are you sure hakuna
kilichochomolewa? Please nenda sasa
hivi ukaangalie uniambie.
MASHA
Niko hapa storage afande na
nauangalia mfuko wa marehemu. Kila
kitu kimehifadhiwa salama including
mihogo yake ya kuchoma, pesa
taslimu 50k, barua, simu na mdoli
afande.
DETECTIVE AYSHA
Nakuja, right now. Do not let
anybody touch that sack. Umesikia?
MASHA
Copied afande.
Aysha anaingia moja kwa moja kuangalia ule mfuko aliokuwa nao
mzee Malamsha. Anaziangalia zile noti anagundua ni zile fedha
ambazo alimpa walipogongana kituoni. Anaumia zaidi. Anachukua
simu ya mzee Malamsha ambayo imeharibika sana. Anabadilisha
housing na simu nyingine iliyoko hapo storage room ili aweze
kuangalia data zilizomo. Anaikuta namba ya Matron wa shule na
kumpigia.
DETECTIVE AYSHA
Habari, naitwa Aysha. Ni ndugu yake
Nayda Malamsha upande wa baba yake.
MATRON
Oh, karibu sana Aysha, mnakuja
kwenye graduation? Maana Nayda
anatazamiwa kutunukiwa vyeti kama
vyote. Top in Physics, Chemistry,
na Math. Pamoja na Mahudhurio,
Nidhamu, Uadilifu, Usafi. Aisee kwa
kweli Nayda ni mfano wa kuigwa hapa
shuleni. Karibuni sana. Atafurahi
sana kuwaona.
31.
DETECTIVE AYSHA
Matron, kwa bahati mbaya hatutaweza
kufika ila akimaliza tu mitihani
nitakuja mimi binafsi kumfata. Mzee
Malamsha amefariki leo alfajiri
akiwa anajaribu kuwahi basi la kuja
huko.
MATRON
Mungu wangu! Poleni sana. Daaaah
habari ya kusikitisha sana.
Nimeumia kwa kweli. Binafsi
nilikuwa naongea naye mara kwa mara
na kumpa update za mtoto. Ni nini
kimepelekea kufikwa na mauti?
DETECTIVE AYSHA
Tutaongea vizuri. Nakutumia hela
shilingi laki moja unisaidie
kumnunulia keki na zawadi zingine
at least asiwe mpweke sana. Naomba
asijue kuhusu msiba hadi
nitakapomfata shuleni. Hii ni namba
yangu isevu.
MATRON
Nimeishiwa cha kusema. Kwa nini
lakini hii dunia?
DETECTIVE AYSHA
Hey, yameshatokea. Sio wakati wa
kulia. Tufarijiane tumsaidie Nayda
maisha yaendelee. Kuna mambo ni
vigumu sana kuyaelewa sisi kama
binaadamu. Nikutakie siku njema.