Professional Documents
Culture Documents
J. C. Ryle (1816-1900)
“Kisha Yesu akawapa wanafunzi wake mfano ili kuwaonyesha kuwa yawapasa
kuomba pasipo kukata tamaa” (Luka 18:1).
Je, ni kwa nini tunapaswa kuomba kutoka katika mioyo yetu? Ni kwa
sababu hali hii inawezesha moyo kumlilia Mungu bila unafiki wowote
na bila uoga wowote: “Hakika nimeyasikia maombolezo ya Efraimu:
Ulinirudi kama ndama mkaidi, nami nimekubali kutii” (Yeremia
31:18). Maombi ambayo yanatoka katika moyo, ni maombi ambayo
hayabadiliki katika hali yoyote. Mtu akiwa peke yake ataomba na hata
akiwa mbele za wengine pia ataomba. Mtu kama huyu haombi kwa
sababu ya kuwafurahisha watu au kwa sababu aonekane yeye ni mtu wa
maombi. Yeye huomba kwa sababu anapenda na anajua kwamba
Mungu wake anamsikia na atajibu. Mungu huwa anatazama ndani ya
moyo, na humo ndimo maombi ya kweli yanafaa kutoka.
119:20). Katika kitabu cha Danieli tunasoma, “Ee BWANA, sikiliza! Ee,
BWANA samehe! Ee, BWANA sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee
Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa
kwa Jina lako” (Danieli 9:19). Yakobo anaita maombi haya kuwa,
maombi yenye nguvu na yanafaa sana. Tunasoma katika Luka kwamba,
“Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii” (Luka
22:44). Yesu Kristo alijua kwamba ni Mungu pekee ambaye angempa
nguvu na uwezo wa kuvumilia msalaba. Wamebarikiwa sana na
wanabarikiwa sana wale wote ambao wanaomba maombi ya aina hii.
Lakini jambo la huzuni ni kwamba kuna wengi leo ambao
wanaomba, lakini maombi yao si yenye nguvu na kwamba pia hayafai.
Wengine wao wengi maombi yao hayatoki katika mioyo yao na
hayazingatii ukuu wa Mungu na huruma zake kwetu wenye dhambi.
Watu kama hawa wanatosheka tu na maneno machache ambayo
wanayarudia mara kwa mara. Ni wakati ambapo tunaomba kutoka kwa
mioyo yetu na kukizingatia ukuu wa Mungu na huruma zake kwetu,
ndipo nafsi zetu zitajengwa na Kristo kutukuzwa. Ni katika maombi
watakatifu wamemaliza muda wao mwingi wakihakikishwa kwamba
wanabarikiwa na Mungu (Zaburi 69:3; 38:10; Mwanzo 32:24,26).
Wengi hawaombi jinsi inanwapasa kwa sababu ya kupuuza na kukosa
tamaa ya utakatifu katika maisha yao. Wengi wao wako na tamaa ya
kufuata dini lakini si tamaa ya kuomba jinsi wanapaswa. Wengi wao pia
hawajui mtu ameokoka ni mtu wa aina gani. Pia hawajui kuwa na
ushirika na Mungu baba kupitia kwa Kristo Yesu na kuwa na nguvu za
utakaso katika moyo wa mtu inamaanisha nini. Hata kama wao
wanaomba, wao bado wanaishi maisha ambayo yamelaaniwa, maisha ya
ulevi, ya zinaa ambayo ni chukizo kwa Mungu. Maisha yao yamejawa
na chuki, wivu, masengenyo na kuwatesa watoto wa Mungu. Wao
hawajui hatari ambayo wako ndani yake. Hukumu ya Mungu inakuja
juu yao. Maombi yao yote ambayo wanaomba hayatawasadia wakati wa
hukumu ya Mungu.
Maombi ni kumsifu Mungu, kumlilia Mungu kwa ajili ya dhambi
zetu na kuleta mahitaji yetu yote mbele zake, kutoka kwa mioyo yetu.
Daudi anasema kwamba, “Ee BWANA, yote ninayoyaonea shauku yako
wazi mbele zako, kutamani kwangu sana hakufichiki mbele zako”
(Zaburi 38:9). Pia Daudi anaomba akisema kwamba, “Nafsi yangu
inamwonea Mungu kiu, Mungu aliye Hai. Ni lini nitaweza kwenda
kukutana na Mungu?..Vitu hivi ninavikumbuka ninapoimimina nafsi
yangu: Jinsi nilivyokuwa nikienda na umati wa watu..” (Zaburi 42:2,4).
Daudi anasema, anaimimina nafsi yake. Hili ni dhihirisho kwamba,
8
yeye amesikia juu ya imani yao katika Kristo na upendo wao juu ya
watu wote amabo wameokoka. Yeye anaambia kanisa kwamba, hakomi
kuendelea kumshukuru Mungu kwa ajili yao na kwamba kila wakati
anawataja katika maombi yake kwa Mungu. Katika Waefeso 1:18-19,
anaandika akisema kwamba, “Ninaomba pia kwamba macho ya mioyo
yenu yatiwe nuru ili mpate kujua tumaini mliloitiwa, utajiri wa urithi
wa utukufu wake kwa watakatifu na uweza wake mkuu usiolinganishwa
kwa ajili yetu sisi tuaminio. Uweza huo unaofanya kazi ndani yetu, ni
sawa na ile nguvu kuu mno.” Tazama jinsi anavyozungumza kuhusu
nguvu hizo na jinsi zilifanya kazi katika kumfufua Kristo na
kumketisha kwa mkono wa kuume wa Mungu Baba. Anaomba, “..na
uweza wake mkuu usiolinganishwa kwa ajili yetu sisi tuaminio. Uweza
huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na ile nguvu kuu mno ambayo
aliitumia alipomfufua Kristo kutoka kwa wafu, akamketisha mkono
wake wa kuume katika mbingu, juu sana kuliko falme zote na mamlaka,
enzi na milki na juu ya kila jina litajwalo, si katika ulimwengu huu tu,
bali na katika ule ujao pia. Naye Mungu ameweka vitu vyote chini ya
miguu yake na amemfanya yeye awe kichwa cha vitu vyote kwa ajili ya
Kanisa, ambalo ndilo mwili Wake, ukamilifu wake yeye aliye yote
katika yote” (Waefeso 1:19-23). Kwa ufupi anawaambia kwamba,
ninaomba kwamba nguvu zile ambazo zilimfufua Kristo kutoka kwa
wafu, zifanye kazi katika maisha yenu na kwamba Kristo ambaye
ameinuliwa juu sana kuliko majina mengine, na ambaye ndiye kichwa
cha kanisa, atawala kanisa lake. Kwa sababu Kristo ameshinda nguvu
za giza ili aletee kanisa lake uzuri, ambalo ni mwili wake. Paulo
anaomba kwamba kila mshirika wa kanisa apate kutawaliwa na nguvu
ambazo zilimfufua Kristo kutoka kwa wafu. Kristo ambaye ndiye
kichwa cha kanisa hawezi kamwe kutenganishwa na mwili wake ambao
ndilo kanisa lake. Muungano huu wa Kristo na kanisa lake
umewezeshwa kwa nguvu za Mungu na ni kwa imani pekee wakristo
wote wanaamini. Kwa sababu ni nguvu za Mungu ambazo zimemfufua
Kristo na kumwinua juu sana kuliko viumbe vyote, pia washirika wa
kanisa wataishi kwa nguvu hizi za Mungu.
16
mingi hawa wako na muda, na mara mingi wanamaliza muda huu kwa
njia ambazo ni za kujifurahisha lakini hawajali mambo ya Mungu
kamwe. Wanasahau kwamba kuna wengi ambao wanahitaji
kufundishwa neno la Mungu, kuna wagonjwa ambao wanahitaji
kutembelewa na maskini ambao wanahitaji kusaidiwa. Watu hawa kwa
nini wanamaliza muda wao katika anasa na wala si katika kazi ya
Mungu. Kwa nini wao hawatumii muda wao katika kuomba? Ukweli ni
kwamba wengi wao wamezembea katika kazi ya Mungu na haswa katika
maombi. Ninatamani kwamba wao wangefanya maombi kuwa jambo la
muhimu sana katika maisha yao na kujitolea katika kumtumikia
Mungu.
d). Maombi pia yanazuiliwa kwa sababu ya kukosa mpangilio katika
maisha ya wengi.
Wengi huwa wanaamka wakiwa wamechelewa na wanaharakisha sana
kuenda kazini kwa sababu wamechelewa. Wengine wanapata kwamba
kwa sababu ya kukosa mpangilio, mambo ambayo hawajayapanga
yanajitokeza mara kwa mara na wanayashughulikia kwa haraka. Wao
hawana nafasi ya kuomba kwa sababu ya shughuli nyingi. Kila mara
mambo yanajitokeza na wanajipata kwamba hawezi kuomba
iwapasavyo. Na kama hata wataomba, utapata kwamba maombi yao
yatakuwa ya haraka-haraka, na maombi kama hayo Mungu hayasikii.
Ni jambo jema kwamba kila mkristo awe na mahali ambapo
ameandika majukumu yake ambayo anayapasa kufanya kila wakati.
Maombi linafaa kuwa jambo la kwanza katika mipangilio yake yote.
Ikiwa utafanya hivi, utapata kuona ni muda gani ambao unamaliza
katika maombi. Utapata kwamba muda wako mwingi uko katika
shughuli zako mwenyewe, unaumaliza na marafiki zako au katika
burudani na wala si na Mungu. Ikiwa utaona hivi, basi huenda
itakusaidia kujichunguza ili ujipatia muda wa kutosha katika maombi .
Hakikisha kwamba muda mwingi uwe ni ushirika na Mungu.
Kristo Yesu. Yeye hatasikia tu, bali atawasamehe wao dhambi zao zote.
Kwa wale ambao hawajaokoka, maombi yao yote ni makelele masikioni
mwa Mungu. Biblia inasema, “Tunajua ya kwamba Mungu hawasikilizi
wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii”
(Yohana 9:31). Mungu atasikia maombi ya watoto wake pekee na wala si
ya wale ambao si wake, yaani hawajaokoka. Pia ni vyema kufahamu
kwamba Mungu husikia maombi ya watoto wake wote, lakini kunao
miongoni mwa watoto wake ambao maombi yao ni dhaifu, yaani
hawatilii manani jambo la maombi. Wao wanaomba, lakini hawaombi
sana, hawamalizi muda wao mwingi katika maombi. Ikiwa mtoto wa
Mungu anapata kwamba maombi yake hayajibiwi, jambo zuri kufanya
ni kujichunguza jinsi anavyoomba na hali ya maisha yao. Ikiwa
tutajichunguza, tutapata jibu sahihi kwa nini maombi yetu hayajibiwi.
3:21). Yeye aliamka mapema sana ili aombe (Marko 1:35). Yeye aliomba
usiku kucha kabla ya kuwachagua wanafunzi wake kumi na wawili
(Luka 6:12). Yeye alikuwa katika maombi wakati sura yake
ilipobadilishwa (Luka 9:29). Maombi ndio ilikuwa njia yake ya
kushinda alipokuwa katika bustani ya Gethsemane (Luka 22:44).
Tutumie muda wetu wa maombi katika mikutano ya maombi
kuombe mambo mbali mbali. Tukumbuke kuombea jamii, kanisa, kazi
ya uinjilisti, makanisa mengine na wachungaji wa makanisa hayo.
Tukumbuke pia kuyaombea mataifa yetu, kazi ya Mungu kote duniani,
Amani katika mataifa ambayo hayana Amani, maskini, na uaminifu
katika uongozi: “Awali ya yote, naishi, kwanza kabisa, naagiza kwamba
dua, sala, maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili watu wote: kwa ajili
ya wafalme na wale wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi kwa Amani
na utulivu, katika uchaji wote wa Mungu na utakatifu. Jambo hili ni
jema tena linapendeza machoni pa Mungu Mwokozi wetu anayetaka
watu wote waokolewa na wafikie kuijua kweli” (1 Timotheo 2:1-4).
Ikiwa siku moja katika juma haitoshi, basi kanisa linafaa kutenga
wakati mwingine wa kuomba pamoja. Muda huu unaweza kuwa hata
mapema siku ya jumapili kabla ibada zianze. Hii ni njia moja sana
nzuri ya kujitayarisha kwa ajili ya ibada za siku hiyo.
Je, katika makanisa ambamo kuna wengi ambao hawahudhurii siku
ya maombi nini inapaswa kufanyika? Ukweli ni kwamba hatuwezi
kamwe kuwalazimisha watu kukua, lakini tunaweza kuwaongoza kwa
njia nzuri kwa upole na ukarimu. Biblia inasema kwamba, “Mwanzi
uliopondeka hatauvunja na utambi ufukao moshi hatauzima” (Isaya
42:3).
Katika makanisa yetu, kuna wale ambao Mungu amewapa karama ya
kuhimiza wengine (Warumi 12:8). Ikiwa wao watatumia karama hii
vyema, watawasaidia wengi kuwa waaminifu katika kuhudhuria
mikutano ya maombi ya kanisa.
Katika mikutano ya maombi ya kanisa, kunahitajika kiongozi
ambaye anapaswa kuongoza na kuhimiza kutoka katika Biblia. Yeye
anastahili kuwahimiza wengine kuomba. Anapaswa kuwaeleza wengine
kwamba hafai kutumia muda mrefu sana kwa sababu hiyo pia inaweza
kuwazuia wengine wasiombe. Kunahitajika maelezo kabla ya kuomba
ili kuwa na mwelekezo mwema. Pia huenda kuwe na haja ya
kuyagawana mambo ambayo yanaombewa. Njia hii itawahimiza
wengine kuomba pia. Yule ambaye anaongoza anapaswa kuacha kuwe
na uhuru wa kuomba kwa wote.
Maombi ya wale ambao wameokoka 29
KUOMBA AU KUTOOMBA
J. C. Ryle (1816-1900)
“Nataka kila mahali wanaume wasali wakiinua mikono mitakatifu pasipo hasira
wala kugombana” (1 Timotheo 2:8).