You are on page 1of 2

Na.

46 Uendelee Kuwa Muaminifu Mupaka Mwisho


MAAGIZO KWA MUSEMAJI: Mu hii hotuba, zungumuzia mustari kwa mustari wa sura ya 3 na
ya 4 ya kitabu ya Waebrania. Kama unapenda, unaweza kutumikisha picha zenye kuwa mu
hii plan kwa wakati wenye kufaa

TUNAPASWA KUTIA NGUVU TUMAINI YETU (Dak. 4)


Inaombaka kujikaza juu tuendelee kumutumainia Yehova na ahadi zake
Leo, tunaishi mu dunia yenye ni kawaida kuwa na mashaka (Yoh 18:38)
Wakati fulani tunaweza kuchoka ao kuvunjika moyo (Ebr 12:3)
Mutume Paulo aliandikia Wakristo Waebrania barua yenye kuongozwa na roho yenye
ingewasaidia waendelee kuwa na imani yenye nguvu
Bila shaka barua ya Paulo iliwatiaka moyo, na siye inaweza kututia moyo (w98-SW 15/7
uku. 9-10 fu. 3-7)

WAZA SANA JUU YA MUFANO WA YESU NA NAMNA YAKE YA KUONGOZA (Dak. 6)


Tunaweza kupata nguvu kwa kufikiria mufano wa Yesu [Soma Waebrania 3:1, 2]
Yehova alimubariki Yesu juu ya imani yake, na siye atatubariki
“Washiriki wa mwito wa mbinguni” watatawala pamoya na Yesu; wengine watapata
uzima wa milele hapa ku dunia
Tunapaswa kumutumainia Yesu, mutawala wetu mwenye haonekanake (Ebr 3:3-6;
w98-SW 15/7 uku. 11 fu. 10-11)
Wakristo Waebrania walipaswa kukumbuka kama Yesu alikuwa mukubwa zaidi kupita
Musa [Picha 1]
Kumbuka kama Yesu eko na nguvu zaidi kupita wanadamu wenye kutawala na pia
matengenezo

TUJIFUNZE KUTOKANA NA MUFANO WENYE KUONYA (Dak. 10)


Tunaweza kujifunza kutokana na mufano mubaya ya Waisraeli wenye walipotezaka tumaini
yao kwa Yehova [Soma Waebrania 3:7-9]
Hata kama walionaka matendo ya nguvu ya Yehova, waliendelea kuwa na mashaka na
kunungunika (Kut 17:1-5; 32:1-6)
Juu walikosa imani, walipoteza zawadi yenye Mungu aliwaahidi (Hes 13:25–14:4; 14:22, 23;
Ebr 3:10, 11) [Picha 2]
Kama mutu anaanza kuangaikia sana vitu vya kimwili na mambo ya kujifurahisha, Imani
yake itakuwa zaifu [Soma Waebrania 3:12]
Imani zaifu inaweza kumufanya ashindwe na “nguvu za udanganyifu za zambi” [Soma
Waebrania 3:13]
Mutu wa vile haonake uzito wa matokeo ya zambi na anatafutaka sababu za kuchambua
mafundisho ya Biblia ao wamini wenzake juu ya kutetea mwenendo wake mubaya
Kupitia maneno yetu na matendo yetu, tunaweza kutiana moyo mumoya na mwingine juu
tushinde nguvu za udanganifu za zambi
Juu Waisraeli hawakukuwa na imani, ile ilifanyaka wakose kumutii Mungu, na walishindwaka
hata kuingia mu inchi ya Ahadi (Ebr 3:14-19)
Kama tunaendelea kuwa na imani ya nguvu, tunaweza kufurahia “pumuziko’’ ya pekee leo
[Soma Waebrania 4:1, 2]
Juu tuingie mu pumuziko ya Mungu, ni lazima tuelewe kusudi yake na kuishi kulingana nayo
(Ebr 4:3-10)
Ile inatia ndani kutii na kufuata mashauri ya Biblia mu maisha yetu (Ebr 4:11;
w11-SW 15/7 uku. 28 fu. 16-17)
Na. 46 Uendelee Kuwa Muaminifu Mupaka Mwisho Ukurasa wa 2
ACHA “NENO LA MUNGU” LIKUCHOCHEE (Dak. 5)
Tunaweza kutumainia Neno ya Mungu yenye kuwa na ahadi [Soma Waebrania 4:12]
Yehova anaendelea kutumika juu ya kutimiza ahadi zote zenye alitoaka (w11-SW 15/7 uku. 32
fu. 20)
Tunaweza kutia nguvu imani yetu kwa kuwaza sana juu ya mambo yenye Yehova alishafanya
na yenye iko nafanya
Tunapaswa kusoma Neno ya Mungu, Biblia, kila siku na kutenda kulingana na mambo yenye
tuko najifunza
Ujumbe wa Biblia unaweza kutusaidia tujione vile Yehova anatuona (w11-SW 15/7 uku. 29
fu. 6)
Kama tunafuata muongozo wa Mungu, hatuna sababu ya kuogopa atuchunguze
(Ebr 4:13)
KUBALI MUSAADA KUTOKA KWA YEHOVA NA YESU (Dak. 5)
Yehova aliweka Mwana wake akuwe Kuhani wetu Mukubwa mbinguni (Ebr 4:14)
Tunaweza kutia nguvu imani yetu kwa “kumutangaza [Yesu Kristo] mbele ya watu wote”
Kama Imani yetu inakuwa zaifu ao tunafanya zambi, Yehova na Yesu wako tayari kutusaidia
[Soma Waebrania 4:15, 16]
Juu ya zabihu ya ukombozi, hatuna sababu ya kuwaza kama hatupendwe ao hatustahili
musaada
Kupitia Yesu, tunaweza kumukaribia Yehova waziwazi mu sala (w16.07 uku. 25 fu. 12-13)
Tunaweza kutafuta musaada kwa wazee Wakristo wenye wanaiga mufano wa Yesu wa
upendo (1Pe 5:2, 3)
Kama tunakubali musaada wenye Yehova na Yesu wanatutolea, tutaendelea kuwa na imani
ya nguvu, na tutafurahia baraka yenye Mungu ametuahidi wakati wenye kuya
[Fuata kabisa habari yenye kuwa ku plan, na uheshimie wakati wa kila sehemu. Haiko lazima
kusoma ao kuzungumuzia maandiko yote yenye kutajwa. Ona kitabu Shule ya Huduma,
ukurasa wa 52-55, 166-169]
ITOLEWE KWA DAKIKA 30
˘ 2023 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
S-34-ZS Na. 46 9/20

You might also like