Professional Documents
Culture Documents
Attachment
Attachment
By richard MWAMBE
01
KAMBI YA JESHI KIZUKA
“Mpaka sasa hatujapata ishara yoyote ya kutuonesha mahali
ilipo ndege yetu. Tumejaribu kuitafuta kwa satellite katika anga lote
lakini kazi imekuwa ngumu sana. Taarifa ya mwisho ilituonesha
kwamba mruko wa ndege ile ulikuwa katika anga la katikati ya
India na Pakistan, juu ya jangwa la Kashmir…”
“Ina maana kutoka hapo haijulikani kilichoendelea?” Namba
moja akauliza.
“Haijulikani, kama imedunguliwa au imekuwaje!” mkuu wa
kikosi cha anga Kizuka alikuwa akiwasilisha taarifa ya kupotea kwa
ndege vita ya kisasa kabisa ambayo Serikali ya Tanzania iliinunua
kutoka Urusi ili kuimarisha ulinzi wa anga dhidi ya adui. Ndege
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
02
DAR ES SALAAM
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
03
Siku tatu baadae…
Unguja
Lukundame aliiacha ofisi ya Posta ya Shangani, mjini
Zanzibar na kuingia katika gari lake, tayari kurudi ofisini. Hatua
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
kama mia moja hivi kutoka pale alipoegesha gari lake, kuliegeshwa
gari jingine aina ya Rav 4 ya kijivu. Ndani ya Rav 4 hiyo kulikuwa
na watu wane waliokuwa wakifuatilia nyendo za mwanamke huyo.
Watu wale hawakushuka bali walimfuatilia kutokea ndani ya gari
hilo lililokuwa na vyoo vyeusi kulizunguka. Aliwasha gari na
kuikamata Barabara ya Nyerere kuelekea ofisini kwake maeneo ya
Uwanja wa ndege. Mara tu baada ya kuondoka, na lile Rav 4
likamfuatia nyuma pasi na yeye kujua.
“Kumbukeni hatutakiwi kumdhuru,” mmoja wao aliyekuwa
nyuma ya usukani aliwapa ujumbe wenzake.
“Sawa!”
“Na wala msitumie nguvu kwa kuwa kazi yetu sisi ni kutaka
tu atueleze Mzee Hasheem yuko wapi… shida yetu kubwa ni huyo
mzee,” yule bwana akaendelea kuwaeleza huku akiwa nyuma ya
magari mawili kati yake na lile la Lukundame. Dakika ishirini
zilimtosha mwanamke huyo kuwasili ndani ya majengo ya Uwanja
wa ndege wa Aman Karume. Akaegesha gari lake na kusalimiana
na watu kadhaa aliowakuta hapo nje. Hakuwa na wasiwasi wowote,
wala hakujua kama anafuatiliwa. Luundame, mwajiriwa wa serikali
katika idara ya mambo ya hali ya hewa. Ofisi yake ilikuwa katika
moja ya majengo ya uwanja huo mjini Zanzibar. Alipoingia ofisini
mwake, dakika tatu baadae, mlango wake ukafunguliwa na vijana
wa wili waliovalia kanzu safi nyeupe, waliingia. Mwanamke huyo
aliwakaribisha, nao wakakaribia na kuketi kwenye viti viwili vya
wageni.
“Nawasikioliza kaka zangu,” aliwaambia pasi na woga.
“Masikini…”
“Usiku mmoja hatukulala, mbwa wa mzee alikuwa akibweka
sana kiasi kwamba tkawa na wasiwasi. Kulipokucha tu;ligundua
kuwa kuna watu walikuja usiku pale nyumbani na alama za miguu
yao zinaonekana wazi, ndipo nikaamua kumuondoa mzee
Hasheem nyumbani kwa siri, usiku wa manane pamoja na vifaa
vyake vya kazi,” Lukundame akamwambia.
“Ukampeleka wapi?”
“Siwezi kukwambia… muda bado,”
“Sawa, sasa mimi nikusaidie nini?” Badru akauliza.
“Kutoka kwako, naomba tu unisaidie kuwajua watu hawa,”
akampatia picha alizokuwa ameziprinti kule ofisini. Badru
akazipokea na kuzitazama kwa makini kisha akazikunja na kuzitia
mfukoni.
“Sawa! Kuna lingine?” akamuuliza.
“Ulinzi, ikiwezekana wakamatwe…”
“Kuwakamata ni kazi kubwa sana maana mpaka nijue
nawapata wapi nan i akina nani,”
“Kazi ndogo sana, kesho saa tano asubuhi nimewaahidi
wafike ofisini ili niwapelekea kwa Hasheem,” akaeleza.
“Basi sawa, mi nitapanga vijana na kesho tutakuwa eneo hilo,
tutawakamata na kwenda kuwahoji ili kujua nini hasa nia yao,”
Badru akaeleza.
“Ila mi naogopa hata kurudi nyumbani…” Lukundame
akasema kwa unyonge.
04
Jamila alidondoka vibaya katika bonde la Zalwan. Bonde hilo
lilolimwa mpunga lilikuwa na ardhi yenye tope iliyompokea
mwanajeshi huyo na kumficha kwa ule mwanguko wake. Fahamu
zake ziliondoka, akabaki hapo kalala kama mfu. Usiku huo ambapo
ndege yao iliangushwa, Jamila alitafutwa kila kona. Mansoor
alituma watu wake kila mahali kuzunguka uwanda wote wa
Kashmir, kuanzia milimani mpaka mabondeni wakiwa na kila aina
na njia ya kutafuta mtu aliyetoweka. Saa kumi na tatu zilipita,
hawakuweza kumpata. Si kwamba hawakufika katika bonde hilo,
la. Walifika mpaka Zalwan lakini hawakufanikiwa. Giza lilipoingia
walipunguza nguvu ya msako na kuacha watu wachache wakiwa
huku na kule ili tu waweze kupata fununu zake.
Jamila, alichelewa sekunde kadhaa baada ya wenzake
kufyatuka na kurushwa nje ya ndege ile. Mkanda wa kiti chake,
ulikataa kuachia bako yake. Wakati ndege ile ikitaremka chini kwa
kasi, yeye alikuwa akihangaika kuufyatua mkanda ule. Kepteni
Bakari na Joel tayari walikuwa wamekwishafanikiwa kutoka. Naye
alipofanikiwa, aliiongoza vizuri mwamvuli wake kuelekea chini.
Ukungu uliozingira milima na mabonde ya Kashmir, vilimfanya
asijue hata ni wapi anakoenda kuangukia. Baada ya kufanya juu
chini kuuongoza mwamvuli huo, alilitoka anga lenye ukungu na
hapo ndipo akatumia utaalamu wake wote kupata eneo zuri la
kuangukia. Uwanda wa kijani ulimfanya ajue kuwa kwa vyovyote ni
eneo lenye mpunga. Na eneo kama hilo huwa ni chepechepe
“Yes,” akaitika.
“Tunafanyaje? Kuna njia nyingine ya kupata zile codes maana mtu wa
kwanza nimemhoji amekuwa mgumu kutoa,” sauti ya upande wa pili
ikasema.
“Haujambana sawasawa…”
“Mpaka tunavyoongea hali yake ni mbaya anaweza asifike kesho,”
“Oh Shit, Mansoor, unakosea. Unajua kupata code hizo
kupitia wao ndiyo njia rahisi sana. Njia ya pili ni ngumu kwa
sababu lazima tuingie kwenye server za jeshi la Rusia. Unafikiri ni
kazi ndogo?” Kotvich akamuuliza Mansoor, “mimi nimeshiriki
kutengeneza hiyo mifumo lakini hizo code walitakiwa wao
wenyewe kwa siri watengeneze. Ina maana mtu anayeweza kuzipata
ni yule anayetunza server ya jeshi hilo. Na hapo ilipo hiyo server
huwezi kufika wala kuingia peke yako… lazima ruksa itoke juu…”.
Mansoor akashusha pumzi kutoka upande wa pili. Hakujua la
kufanya. Inabidi nizipate kupitia hawahawa!Akawaza. Akili yake alihisi
ikiuma ghafla. Akaona ugumu wa biashara hiyo aliyoishadidia kwa
kuwa ilikuwa na pesa nyingi sana.
Danval Kotvich, mwanasayansi aliyebobea katika uundaji wa
mifumo ya kusalama kutoka nchi ya Czech alikuwa miongoni mwa
watu wataalam wa jeshi la Urusi walioshiriki kuunda ndege hiyo.
Mtaalam huyu asiye mwaminifu, alipokea simu miezi kadhaa
nyuma ya kumtaka kuingia katika biashara hiyo haramu. Akalghaika
na kujikuta mikononi mwa Mansoor aliyempatia maelfu ya Pound
za Kiingereza.
“Na vipi kama watabadili codes hizo?”
yaliongeza kasi kwa kuwa hakuju nani hasa anayegonga na kwa nia
ipi. Jamila alikuwa mgeni katika mji huo, hivyo hakutegemea kabisa
kupata ugeni. Akaijiweka sawa kwa lolote, akajiinua kutoka pale
kitandani na kuketi kabla hajauendea mlango. Baada ya sekunde
kadhaa akainuka kuufuata ule mlango huku akiwa kajipanga kwa
dhoruba yoyote. Akazungusha funguo na kunyonga kitasa, mlango
ukafunguka.
“Habari!” mwanadada mmoja alikuwa kasimama mlangoni
hapo akiwa na vifaa vyae vya kufanyia usafi. Jamila akamtazama na
kumwambia kuwa kwa muda huo hahitaji usafi katika chumba
chake. Akarudi na kujifungia, kimya. Akili yake ilikuwa akifikiri jinsi
gani ataweza kuwasiliana na baba yake wa kufikia, Mzee Hasheem
ili japo amjuze tu kuwa yupo hai. Hakuwa na simu, Zaidi ni kifaa
kidogo ambacho alikuwa akikitumia kwenye mawasiliano ya ndege
ile. Kifaa kile mfano wa simu ndogo kiliweza kufanya kazi ukiwa
umbali wa kilomita kumi hadi kumi na tano kutoka ndege hiyo
ilipo. Kichwa kilimuuma.
“Lazima nirudi… hata hivyo, nahitaji simu… nitapata wapi
laini?” akajiuliza kama anayemwambia mtu. Ooooooh nimepata wazo!
Akafumbuka. Uamuzi aliouchukua ni kutafuta simu za vibandani ili
aweze kuwasiliana na Mzee Hasheem pamoja na mkuu wake wa
kazi huko Tanzania ili kumjuza nini kimetokea. Jamila akajiandaa,
akachukua kile kifaa chake na kukiweka vizuri. Ni yeye alijua kina
kazi gani. Wote watatu walikuwa na vifaa hivyo vya kuwezesha
mawasiliano kupitia mfumo wa ile ndege. Joel na Bakari walikuwa
wamenyang’anywa, na vifaa hivyo kuhifadhiwa na Bwana Mansoor.
Mpaka siku hiyo, vijana wa Mansoor walifanikiwa kuondoa mfumo
05
Lukundame aliamka mapema sana na kumwandalia kifungua
kinywa baba yake ambaye usiku kucha alishinda kwenye kompyuta
yake akijaribu hiki na hiki ilia pate japo mawasiliano.
“Baba!” akaita kwa sauti ya upole. Mzee Hasheem akageuka
kumtazama binti yake, akapokea kikombe kile cha kahawa na
kupiga funda moja kisha akakitua. “Umefanikiwa?” akamuuliza.
“Hapana! Sasa nagundua kuwa hii ni hujuma kwa sababu
ingekuwa ni ajali ya kawaida, ningeshajua mpaka eneo ambalo
ndege hiyo imeanguka,” akajibu.
“Aisee…!”
“Ina maana hii ndege imeangushwa halafu kuna watu
wameiba Pegan Box,” akamweleza.
“Pegan box, nini?”
“Oh! Pegan box ndiyo huo mfumo ambao tumeuweka
kwenye hiyo ndege vita. Mfumo huu wa kujilinda na mwenye
nguvu katika mawasiliano ya anga ni wa kisasa sana. Nina mashaka
hii ndege imeangushwa, na mtu anayejua vizuri mambo haya,
amezima ule mfumo kisha kauchukua ndiyo maana hapa kwenye
vifaa vyangu kila ninapojaribu kutafuta nakosa. Nimejaribu Zaidi
ya code 1500 lakini imegoma. Oh mwanangu Jamila, heri awe
amekufa…” Hasheem alihuzunika.
kwenye ofisi maalum ya kazi hiyo. Rafu kubwa zenye vyumba vingi
zilisheheni makabrasha kila kona. Alipepesa macho kutazama,
moyoni akakiri kuwa kama kuna watu wanateseka na kazi
wanayoifanya basi hawa wa masijala wanapitia hilo.
“Karibu kaka, nikusaidie nini?” askari wa kike aliyekuwa
kwenye dawati la ofisi hiyo alimkaribisha Amata kwa ukarimu wa
Kiafrika haswa.
“Asante sana, naitwa Amata Ric, kutoka idara ya Usalama wa
Taifa,” akajitambulisha kwa uwazi bila kificho. Hakika hakuna
mkate mgumu mbele ya chai. Yule mwanadada akapigwa na
mshangao.
“Amata? Huyu Amata ninayemsoma habari na harakati zake
kwenye magazeti na vitabu au mwingine?” akajikuta akibwabwaja
na kusahau kama kuna wateja wengine wa kuhudumia.
“Hakuna mwingine!”
“Naitwa Meja Mwaja… karibu Bwana Amata, siamini kama
nimekutana na mtu kama wewe loh!”
Mwaja alikuwa mwanamke wa makamo, kati ya miaka
thelathini na tano na arobaini, mchezi mwenye maneno mengi.
Hata uongeapo naye lazima uwe makini kwa jinsi anavyoongea kwa
haraka. Mweupe kiasi mwenye vibonyo mashavuni kila
akitabasamu. Macho yake yaliokaa kama taa za Hyundai ndiyo
yalioukamilisha haswa uzuri wake.
“Keti kidogo, nisamehe nitakusikioliza baada ya hawa
wachache,” Mwaja akamwambia Amata. Hata kama alikuwa na
haraka, alisahau, akaliendea kochi lililokuwa katika moja ya kona za
ofisi hiyo na kuketi. Mwaja akafanya haraka kuhudumia wachache
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
“Zenji,”
“Kunanukia?”
“Kabisa, ngoja nikamtembelee mjomba…moyo wangu
hautaki kutulia kabisa,” Amata akajibu.
“Sawa mara ufikapo usisite kunijuza hali yake,” simu ile
ikakatika wakati akikaa katika kiti safi cha boti. Akaitazama saa
yake, ilikuwa yapata saa kumi na nusu jioni wakati kile chombo
kilipokuwa kikiliacha gati la Dar es salaam kuelekea visiwa vya
karafuu, Zanzibar. Alifumba macho kwa sekunde kadhaa na
kujiuliza maswai ambayo alihitaji mtu asiyemjua kuyajibu. Baada ya
kuoanisha majibu ya kule alikotembelea kwa Mwaja, kisha ofisi za
Tume ya Uchaguzi na kampuni ile ya simu, Amata aliweka taarifa
pamoja na kujikuta akiitwa katika visiwa hivyo. Kwamba jibu la
kitendawili lipo huko. Akaendelea kubaki kimya akitafakari wapi pa
kuanzia pindi awapo katika kisiwa hicho. Kumekucha
* * * *
06
T.Mi.35, Bomu la kutegwa ardhini lilikuwa limekandamizwa
na mguu wa Jamila. Akiutoa tu basi mlipuko ungetokea na
kumsambaratisha vibaya. Hakulitaka hilo kwani safari ilikuwa bado.
Akiwa bado anatetemeka na jasho likimtoka, alishuhudia lile lori
alilokuja nalo likiendelea na safari. Akatamani alikimbilie lakini
kitendo hicho kingemgharimu uhai wake. Mchakacho wa miguu ya
kiumbe cha miguu miwili ulisikika nyuma yake.
“Tulia hapohapo! Ukijitikisa tu umekwisha kwa kuwa
ulichokikanyaga unakijua ndiyo maana hujakimbia,” sauti ya mtu
huyo ikamwambia. Ni kweli , alichokikanyaga alikijua na ndiyo
maana alitulia palepale. Askari mmoja akifuatiwa na wengine
watatu wenye bunduki nzitonzito mikononi mwao walifika eneo
hilo.
“Ulitaka kwenda wapi?” akauliza akiwa kasimama mbali
kwenye hivyo vichaka.
Kumbe walikuwa wananitafuta! Akawaza Jamila. Hakujibu
chochote.
“Tulia!” sauti nyingine, si ile ya kwanza, ikamwambia.
Mwanajeshi mmoja aliyevalia vazi maalumu akamkaribia Jamila na
kumtaka atulie ili aweze kumsaidia. Mwanamke huyo akatulia bila
kutikisika, ila mwili wote ulitota jasho, maana ilikuwa ni sawa na
kukutana uso kwa uso na Israeli mtoa roho.. Yule askari,
akautazama ule waya ulipoelekea, akaachana nao. Alijua kila kitu.
Akachukua kitu cha bapa, chembamba kama pasi ya mwashi.
Akakipachika taratibu kati ya unyayo wa Jamila na lile bomu.
Akakandamiza kwa nguvu na kumtaka mwanamke huyo kuutoa ule
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
mashine ile. Ikawa hivyo. Joel alihisi kama kuna nyundo ikimgonga
kichwani kwa nguvu sana. Akapiga kelele ili imsaidie kuendelea
kutunza kumbukumbu yake, ikawa ngumu.
“Taja!”
“…X-…”
“Endeleaaaa mpumbavu wewe utakufaaa…” Mansoor alipiga
kelele.
“… 2bPG_”
“Malizia…”
“… **Tz” Joel aliropoka code yote bila kujijua. Akili haikuwa
yake tena. Umeme ukazimwa. Joel akatulia kimya akiwa hana
fahamu. Mwili ulimlegea na kukosa nguvu kabisa. Mansoor
akaiendea meza moja iliyokuwa kando. Juu ya meza huyo kulikuwa
na sanduku jeusi. Akalifungua. Ndani yake palikuwa na kompyuta
kubwa, imara, iliyotengenezwa na kufungwa ndani ya sanduku hilo.
Akaiwasha. Ikawaka. Pale kwenye kioo pakatokea picha ya Joel na
kumdai aweke hiyo code kama nywila. Akaiandika na kubonyeza
batani iliyosomeka ‘ENTER’. Kompyuta ile ikafunguka. Sehemu
ya pili ikamtaka kuweka kiganja cha mkono wa kuume. Mansoor
akaitazama, kisha akageuka kumtazama Joel, yupo kimya.
Akamwamuru kijana wake aibebe ile kompyuta mpaka pale na
kuweka kiganja cha Joel. Ikamkaribisha na kufunguka. Upande wa
kulia wa kioo cha ile kompyuta kukatokea maandishi yaliyosomeka
‘Two more authorised codes needed'. Akairudisha mezani na
kuiweka.
“Bado codes mbili…” akawaambia wageni wake. Nao
wakainuka na kwenda kutazama. Wakaridhika na wanachokiona.
“Sasa bado kidogo tu biashara yetu itafanyika” akawaambia.
“Mimi niko tayari, hata advance nitaacha leo,” Fernandez
akasema. Mabishano makali kati ya Fernandez na Jenerali Kahir
yakataradadi wakati Mansoor akiwaangalia na kutazama tu..
* * * *
mbili kasoro dakika chache. Akatoka nje ya baa ile bila kumuaga
yeyote. Pindi tu alipofika nje na lile taksi likawasili.
“Unaona! Mi mzungu braza!…” yule kijana akamwambia
Amata wakati akiingia katika taksi hilo, “nikupeleke wapi?”
“Hello,” akaipokea.
“Sasa mbona umetufungia mlango? We umekuwa mamluki?”
wakamlalamikia wakijua kuwa mwenzao ndiye aliyewafungia. Wale
vijana hawakuwa wamejiandaa. Amata alitua chini na kumtia
ngwala mmoja aliyedondoka vibaya na kujibamiza kichwa kwenye
meza ya mninga. Yule mwingine, akaona ajaribu bahati yake
kukimbia. Hakufanikiwa, Amata akamkama shati na kumrudisha
ndani. Akampiga kichwa kimoja kizito, akatulia. Kamanda Amata
akawapekua na kuchukua vichache vinavyomfaa. Akiwa katika
harakati hizo akasikia gari jingine likisimama kwa fujo huko nje.
Akafanya haraka,akatoka na kulichukua lile kabrasha. Akakimbilia
mlango wa uwani na kuukwea ukuta ule kwa ustadi wa ajabu.
Akajitupa nje. Hakutaka kabisa watu wengine wajue misheni yake.
Kamanda Amata alijikuta akitua juu ya maji machafu yanayotoka
kwenye nyumba za jirani na kufanya dimbwi kubwa. Kutokana na
lile giza, akajikuta tu keshatumbukia kwenye uchafu huo. Akatoa
tusi la nguoni na kujitahidi kujinasua. Kabrasha lake nalo lilikuwa
halitamaniki lakini hakuliacha.
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
Chini ya nyumba ile ya Hasheem kule Bwejuu kulikuwa na
andaki kubwa lililojengwa vizuri na lenye mahitaji yote muhimu.
Amata hakujua kitu hicho, baada ya kuizunguka ile nyumba kwa
ndani hakugundua siri yoyote ile. Akakata tamaa na kuamua
kuondoka. Nje ya nyumba ile akasimama tena, nafsi yake ikigoma
kukubaliana naye. Akaamua kuikagua kwa nje. Kutoka pale kwenye
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
07
KATIKA BANDARI ya Zanzibar, mchana wa siku hiyo
Kamanda Amata alitulia kusubiri boti ya kumvusha kwenda Dar es
salaam. Miongoni kwa wasafiri wengi waliokuwa katika bandari
hiyo tayari kuabiri kweney boti ya adhuhuri, walikuwapo vijana
wawili wenye mchanganyiko wa asili ya Kihindi na Kiarabu.
Walifanana kwa sura na wajihi wao. Walinyoa nywele katika
mtindo unaofanana, walivaa miwani zinazofanana, saa
zinazofanana. Ni vigumu sana kuamini kama ungeambiwa kuwa
vijana hao hawakuwa ndugu. Kila mtu alivutiwa kuwatazama.
Macho ya wengi hayakuwabanduka. Amata alikuwa kimya
kajiinamia. Kichwa chake kilikuwa kikichakata mambo mengi kwa
wakati mmoja. Hakuwa na habari kabisa na watu hao walioingia
katika bandari hiyo.
Wale vijana wakapachika masikioni mwao vifaa vya mawasiliano.
Kupitia vifaa vile wakapewa maelezo ya nani wanatakiwa
kumuweka chini ya himaya yao.
* * * *
* * * *
* * * *
SHAMBA
MADAM S alitulia tuli katika ofisi yake ndogo iliyojengwa
ndani ya jumba hilo. Juu ya meza yake palikuwapo na kabrasha
moja tu liliandikwa kwa mkono ‘Jamila’. Wino mnene mwekundu
wa marker pen. Lilikuwa kando ya meza limefunikwa huku juu yake
kukiwa na beji nzito ya TSA. Nusu saa tangu akae kwenye kiti kile,
mlango ukafunguliwa, Amata akajitoma ndani.
“Nilitegemea jana ileile ungefika kwangu, nilikuwa nina hamu
sana na wewe…” Madam S akamwambia Amata aliyekuwa anavuta
kiti ili akae.
* * * *
“Utampataje?”
“Yule ni mwanaume na hakuna mwanaume jeuri kwa
mwanamke. Alishawahi kunitongoza, hivyo kumpata ni rahisi
sana,” Mwaja akaeleza. Kwa Fareed ikawa furaha moyoni mwake.
Akajiapia, siku akikutana naye tu hatompa nafasi.
Upande wa Amata, yeye alitulia kimya akiangalia kila
kinachoendelea mahali hapo.
Lazimamuuaji au shoga yake awepo eneo hili! Amata akafikiri huku
macho yake yaliyofichwa nyuma ya miwani myeusi yakimtathmini
kila aliyepo msibani hapo. Kila wakati macho yake yalipotua kwa
Fareed, mwili wake ulisisimka.
Shughuli za mazishi ziliendelea, saa moja na nusu baadae kila
kitu kilikamilika. Watu wakaanza kutawanyika, Amata hakutaka
kumpoteza Fareed kwenye macho yake. Akainua mkono wake wa
kushoto na kuifyatua saa yake. Akaikaribisha Karibu na kinywa
chake na kuongea maneno machache tu kwa mtu wa upande wa
pili. Alipoushusha alishuhudia Fareed na Mwaja wakiingia garini.
Gari lile lilipoondoka likamwacha Chiba eneo lile.
Good boy! Amata akamsifu kijana wake na kuvuta hatua huku
akiwapita watu pasi na kusalimia. Alipomfikia Chiba pale alipo
akaingia garini moja kwa moja, na Chiba vivyo hivyo.
“Vipi Kamanda! Umehisi kitu?” Chiba akauliza.
“Kama kawaida… huyu bwana lazima nimtembelee usiku wa
leo, nina miadi naye…” Amata akajibu na kuondoa gari kuelekea
mjini.
“Sakata linaendaje?”
“Kazi ngumu Chiba, lakini kitaeleweka tu,” Amata akajibu
huku akibadili gia na kuinghia barabara ya Ally Hassan Mwinyi.
Chiba akabofya nobu fulani. Kwenye dashboard ya gari lile
kukachomoza luninga mdogo. Akawasha na kubonyeza vitufe
kadhaa. Ramani ya Dar es salaam ikajitokeza na barabara zake.
Doti nyekundu ikajionesha maeneo ya Upanga.
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
08
Majuma Mawili Yaliyopita…
FAREED aliwasili Tanzania akitokea Pakistan na kuingia
kama mtalii. Alijua maneno kadhaa ya Kiswahili ambayo yaliweza
kuuficha ugeni wake. Mwenyeji wake hakupenda kujitokeza
kumpokea, akamtuma mtu ili amkirimie hilo. Likafanyika bila
tatizo. Fareed alifikishwa kwenye hoteli ya Tiffany ambako huko
angekutana na mwenyeji wake huyo. Fareed alipoingia Tanzania,
naye aliingiza watu wake kwa siri. Aliwaleta kwa kazi moja tu.
Usiku wa saa tatu, siku hiyohiyo ndipo mwenyeji wake
alipokuja kwa mazungumzo na kijana huyo. Mwambope, aliwasili
hapo kwa gari binafsi, akateremka na kuongoza moja kwa moja
mahali walipopanga kukutana, ndani ya hoteli hiyo.
“Bwana mkubwa kaniagiza lile kabrasha tu basi,” Fareed
alimwambia Mwambope.
“Yeye bado anataka kabrasha, siyo rahisi kulipata kama
nilivyomwambia” Mwambope akajibu.
* * * *
Amata aliwasili katika ofisi yake pale kwenye jengo la JM Mall,
ghorofa ya sita. Gina, mara tu alipomkaribisha bosi wake
akamkabidhi bahasha aliyoichukua posta asubuhi ya siku hiyo.
“Imetoka wapi?” akauiliza.
“Ah ntajuaje? Muhuri unasoma Zanzibar,” Gina akamweleza
wakati Amata akiendelea kuichana ile bahasha. Akaifungua karatasi
iliyo ndani, iliandikwa kwa mwandiko mzuri wa kike. Haikuwa
mistari mingi; michache yenye maana.
* * * *
* * * *
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
Mansoor alibaki kimya akimtazama Mwaja aliyekuwa akimpa
habari ya yaliyomkuta jioni hiyo. Mwaja alikuwa akimlalamikia
Mansoor kuhusu gari. Alichojichanganya Mansoor ni kusema tu
kuwa gari lile alimpa rafiki yake. Akaona wazi kuwa sasa muelekeo
wa penzi hilo bandia utapata ukakasi muda si mrefu. Si kwamba
hakujua kama Mwaja ni mwanajeshi, la, alijua vyema. Siri yake yeye
ni kutaka kuchota na kupata habari za kiusalama kutoka upande
huo. Hakujua kuwa swala lile ijapokuwa lilikuwa likifukuta jeshini
lakini uchunguzi wake ulikuwa kwa siri katika mikono ya raia
wema.
Siku zake za kuwapo Tanzania zilikuwa ukingoni, kazi yake
aliyotumwa na matajiri wake Fernandez na Mansoor ilikuwa
ngumu kuliko alivyofikiri. Kupata kabrasha lenye zile code tatu kwa
mara moja. Haikuwa rahisi, akajikuta amemuua Mwambope,
akamteka Lukundame na baada ya hapo mambo yakawa alijojo.
Alipomuona Amata katika kumbukumbu ya kamera za usalama
nyumbani kwa Hasheem akamsaka kwa minajiri ya kuchukua kile
alichochukua. Kabrasha.
Mwambope, marehemu, alimhakikisia Mansoor kulipata kabrasha
lile kupitia Hasheem kwani alimtafsiri mzee hiyo kama ‘Retired but
Extremely Danger’. Siku hii akajikuta akipoteza vijana wake wawili na
kukamatwa kwa boti waliyokuwa wakiitumia. Pigo! Akajikuta ana
hamu ya kumfahamu na kukutana na kiumbe huyo. Hamad! Uso
kwa uso msibani, hakuamini kama anayetambulishwa kwake ndiye.
Akagundua kuwa Mwaja anamfahamu mtu huyo, alipomhoji
kirafiki akathibitishiwa utata wake. Woga ulimwingia jioni hiyo
alipopewa taarifa na Mwaja kuhusu gari lile. Anajua kuwa alimpa
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
“Sawa!”
* * * *
Katika anga la Bagamoyo, jioni ya saa kumi na mbili, ndege
moja ndogo ilikuwa ikirandaranda na kuzunguka bahari kisha kuja
tena pwani. Watu waliokuwa ufukweni mida hiyo walikuwa
wakiishangilia hasa watoto kwa kuwa ilikuwa ikipita chini sana.
Ndani ya ndege hiyo alikuwamo Kamanda Amata akiangalia
kile anachokitaka. Scoba alikuwa katulia akikiongoza kwa weledi
mkubwa chombo hicho cha watu wawili tu.
“Zunguka kuelekea Maghalibi,” Amata akamwambia Scoba.
Naye akafanya hivyo, Amata akatazama kwa umakini kwa kutumia
darubini yake huku akichukua picha kadhaa. Aliporidhika akamtaka
Scoba kurudi.
“Umeridhika au nitue kabisa?” Scoba akamtania.
“Ngoja nishuke kwanza halafu utue peke yako!”
Dakika kumi na tano baadae, tayari walikuwa uwanja wa
ndege terminal 1. Wakaingia kwenye gari na kuondoka zao.
“Kwa hiyo, tutarudi tena?”
“Ndiyo, nipitishe nyumbani, kuna vifaa vichache vya
kuchukua, halafu ongea na Simbeye kuwa tunahitaji boti iendayo
kasi…”
“Kwani kuna nini braza?”
“Kuna mateka pale inabidi aokolewe usiku huu kama ni
kweli…”
“Nimekupata, kazi imeisha” Scoba akamjibu wakati
wakiikamata barabara ya Nyerere kuelekea mjini. Saa tatu usiku
iliwakuta katika kituo cha polisi cha wanamaji eneo la Magogoni
ambapo hapo uhifadhi boti zao. Taarifa ya operesheni hiyo fupi
tayari ilisainiwa na HOT kilichobaki kilikuwa ni utekelezaji tu.
BMW jeusi likaegeshwa nje ya kituo hicho. Daktari Jasmini
* * * *
* * * *
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
HOTELI YA TIFFANY
Kamanda Amata aliwasili Hoteli ya Tiffany katikati ya jiji la
Dar es salaam majira ya saa nane usiku. Akapiga macho kutazama
magari yaliyoegeshwa hapo nje, hakuna alilolitilia shaka.
Akateremka taratibu na kujiweka tayari kuvuka barabara ili aingie
katika hoteli hiyo. Kabla hajavuka, upande wa pili kukatokea taksi
na kumpigia honi kali. Akarudi nyuma. Ile taksi ikasimama katika
kibaraza chenye lango kuu la kuingia hotelini humo. Amata akatulia
kwanza kujua nani anateremka kabla hajaingia kwenye harakati
zake.
Mwaja! Akapigwa na butwaa. Hakuamini anachokiona,
akasubiri mwanamke huyo aingie hotelini mle. Alipohakikisha hilo
limekamilika akavuta hatua kulielekea lango hilo. Amata aliingia
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
SHAMBA
Jasmini na Scoba waliwasili Shamba usiku wa saa saba na
kumwingiza Lukundame aliyekuwa hana fahamu katika chumba
kidogo cha matibabu. Chumba kilichosheheni kila kifaa tiba
unachokijua wewe. Wakamlaza katika kitanda na Jasmini
akamwekea dripu yenye virutubisho ili kumrudishia kidogo uhai
uliopotea. Walipohakikisha wamemuweka vizuri wakatoka na
kuwasha kamera ya siri kumtazama. Wawili hao kila mmoja
akaingia katika chumba chake kujipumzisha.
“Kwa vipi?”
“Niambie…”
“Ndiyo…”
“Aaaaaaa hapana,”
“Sawa”.
* * *
“Ndiyo!” akaitikia.
“Ndiyo naifahamu…”
* * * *
09
KAMA kuna siku ambayo jiji la Dar as salaam lilikuwa na
foleni ya kutisha, ilikuwa hii. Kamanda Amata alikwama kwenye
foleni zaidi ya saa moja na nusu. Alitamani ashuke na kuliacha gari
barabarani lakini haikuwa hivyo. Mvua kubwa iliyoambatana na
radi ilikuwa ikiendelea. Saa tatu asubuhi ilikuwa kama saa kumi na
mbili alfajiri kutokana na giza lililosababishwa na mawingu mazito.
Wimbo wa Lionel Richie, Stuck on you, ulikuwa ukimtumbuiza.
* * * *
Mwaja alikuwa kajilaza kwenye kitanda kile cha kamba kama
mtoto mkiwa. Zilikwishapita saa takribani thelathini tangu
afungiwe mule ndani. Aliposikia mlango ule ukifunguliwa akaketi.
Sura yake ilikuwa imekunjamana kwa usingizi.
“Umeinjoi siyo?” Amata akamuuliza Mwaja.
“Mambo unayonifanyia Amata, sawa tu…” Mwaja
akalalamika.
“Mwaja, nimekuweka hapa kwa usalama wako, usilalamike…”
Amata akamwambia.
“Bila chakula Amata, hapana….” Mwaja akalalamika.
“Nilikupa pipi hukula?”
“Yaani mi wa kushindia pipi?”
“Meza hata moja, kwani mi niliyekupa sina akili!” Amata
akang’aka. Mwaja akabaki kimya.
Chiba akasogea kumtazama huyo mwanamke, “huyu ni nani?”
akauliza.
“Huyu ni Meja Mwaja wa JW kitengo cha Masijala pale
Makao Makuu Upanga,” Amata akajibu.
“Mbona yuko hivi?” Chiba akauliza.
“Huyu nilipomchukua alikuwa hivihivi… naakitoka hapa
anaenda kujibu kesi yake…” Amata akaeleza.
“Pole mrembo!” Chiba akampoza.
“Kula hizo pipi. Saa arobaini na nane tangu nimekuweka
humu zikitimia ndo nitakutoa na kukupeleka panapohusika…”
Amata akamwambia Mwaja na kuufunga ule mlango.Katika
chumba kingine, Chiba na Amata waliketi kwenye kiti hiki na kile.
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
* * * *
SHAMBA
itatuonesa moja kwa moja ni wapi hilo Pegan box lilipo…” Chiba
akaeleza.
“Nahisi tumemaliza kazi!” Amata akamwambia Chiba, "kliki
tuone kinachotokea" akamwambia. Chiba akaweka kila kitu sawa
na kuikliki ile bluu code pale chini ya picha ya Jamila.
* * * *
* * * *
Macho ya Chiba na Amata yaliikodolea ile kompyuta
kutazama nini inataka kuwaambia. Rada ya kidijitali iliyokuwa
katika kompyuta ile ya Mzee Hasheem ikawaonesha uelekeo wa
wapi pegan box ilipo.
Kashmir! Amata akajisemea kichwani mwake.
“Mzigo upo Kashmir!” Chiba akamwambia Amata. TSA 1
akashusha pumzi ndefu. Akavuta hatua na kulifikia jokofu, yeye
hakuchukua Coke, bali pombe Kali. Akajimiminia kitoti kimoja na
kupiga pafu kavukavu. Aliporudi akaenda moja kwa moja kwenye
ramani kubwa iliyobandikwa ukutani na kutazama wapi Kashmir
ilipo. Si kwamba alikuwa haijui bali alitaka kujiridhisha.
“Sawa, sasa naweza kuwarudisha mateka wangu uraiani,
mmoja baada ya mwingine,” Amata akamwambia Chiba. Akaketi
na kuweka taarifa zake vizuri wakati Chiba akijiandaa kuliacha
jumba lile.
“Vipi?” akamuuliza.
“Naenda zangu kuanza likizo” Chiba akajibu huku tayari
mkoba wake ukiwa begani.
“Wasalimie…”
“Unaamini vipi?”
“Jamila alimwandikia email Hasheem masaa kumi na mbili
kabla hajajiua… na inaonekana kuwa hat hakuzisoma barua
hizo…”
Madam S akatikisa kichwa kukubaliana naye, akaendelea kusoma
yale maandishi. “Kashmir…” akatamka. “Naweza kunakili kwenye
laptop yangu?”
“Ndiyo mama!” Amata akajibu.
“Sawa… nitakutana na Rais usiku wa leo… naomba usiwe
mbali sana kwani chochote atachosema kama kinatugusa moja kwa
moja nitakwambia usiku huuhuu,” Madam S akamwambia Amata.
“Halafu, nilikuwa sijakwambia…”
“Kitu gani?”
“Afisa wa jeshi anayetunza kumbukumbu pale Makao Makuu
ametoweka…” akamwabarisha.
“Ninaye mimi!”
“What?”
“Ninaye Mimi…” Amata akarudia jibu lake.
“Kijana una hatari sana wewe! Umemweka wapi na
unamfanya nini huko mpaka anasahau kazi…” Madam akamuuliza
Amata kwa ukali kidogo.
“Sikiliza Madam, yule afisa ni mmoja wa watu ninaowashukia
kwenye sakata hili,”
“Kivipi?”
“Kwanza kabisa, alikuwa hawala yake na Fareed”
“Fareed huyu uliyemuua?”
“Na siku nilipomuua Fareed nilimkuta na huyu mwanamke,
Meja Mwaja, kuna mambo nilikuwa nayataka kutoka kwake ndiyo
maana nikamficha ili niyajue ajuayo…”
“Umepata nini kutoka kwake?” Madam akazidi kuchimba.
* * * *
* * * *
“Naenda na nani?”
“Peke yako! Sitaki mtu yoyote ajue kuwa umeenda huko zaidi
ya Mimi na wewe mwenyewe!” Madam S akaongea pasi na lepe la
tabasamu.
“Nimekupata, naomba niende,” Amata akajibu na kusimama.
“Kesho subiri simu yangu kwa hamu…”
Wakaagana, Amata akaondoka katika kasri like na kuelekea
nyumbani kwake. Kichwa chake kilishaanza kuichakata safari hiyo.
* * * *
Mansoor alihisi kichwa kikitaka kumpasuka. Akawaita watu
wake wa karibu ili kuzungumza machache. Mbele yake kulikuwa na
vijana watatu aliyowaamini sana.
“Kuna mambo matatu ya kujadili… moja, niwafanye nini
hawa mateka! Mbili, ni wapi nifanyie mkutano na wateja wangu!
Tatu, tunaipata vipi code ya tatu,” akawaeleza. “Maana hali
inapoendelea itakuwa mbaya, hili pegan box limeshaanza kuwatoa
mate watu wengi… na tukizubaa tunaweza kosa kila kitu.
Nimepata tetesi kuwa Jeshi la India limepata taarifa ya pegan box na
leo walikuwa na kikao kuhusu hilo!” akawaambia. “Tufanyeje?”
akawauliza.
“Kama tunachokitaka kwa hawa mateka tumekipata hawana
maana kwetu, tukiwaacha huru itakuwa hatari kwetu,” mmoja
akaeleza.
“So!”
“Wauawe!”
* * * *
“Kama nilivyokwambia…” Madam akaanzisha mazungumzo
pindi tu alipokutana na Amata katika uwanja mdogo wa mchezo
wa golf pale Ghymkhana.
“Kwamba…”
“Unapaswa kwenda Kashmir katika uwanja wa vita… Pegan
Box linatakiwa nyumbani kwa udi na uvumba” akamwambia.
Amata na Madam S walikuwa wakitembea kwa hatua za
taratibu wakikizunguka kile kiwanja.
“Sawa!” Amata akajibu. Baada ya mazungumzo marefu
wakafikia mahali penye benchi, wakaketi.
“Kazi hii ni ngumu… na ugumu wake unakuja kutokana na
kwamba hatuna mtangulizi huko uwendako, hivyo akili na
maamuzi ya busara yanatakiwa yatumike katika kujua nini cha
kufanya nani wa kumfuata na kwa nini… Pakistan mpaka Kashimir
si eneo salama hata kidogo kwa usalama, mapigano ya muda wote
yanaendelea, hawa wanamlaumu huyu na huyu anamlaumu yule…”
“Nimekupata mom!”
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
10
AMATA aliwasili Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Islamabad saa tano usiku baada ya kuchelewa Dubai kwa saa
nzima. Mara tu baada ya kutoka kwenye uwanja huo alielekea
katika maegesho ya taksi. Akaitazama saa yake, ilikwishatimu saa
sita kasoro robo usiku. Utata ukamjia; aanze kwenda hotelini au
moja kwa moja aelekee kwenye klabu hiyo aliyoambiwa? Akakosa
jibu. Akaitazama saa yake muda ulizidi kuyoyoma. Hakuwa anajua
umbali wa kutoka hapo kwenda kwenye hicho kilabu wala wa
kwenda hotelini. Mlio wa saa yake kuashiria kuwa saa kamili
imetimia ulimgutusha. Akaitazama, ikamwonesha kuwa saa sita
kamili usiku ilikwishatimu na tayari siku ilikuwa
imebadilika. Akavuta hatua na kuiendea taksi iliyokuwa imeingia
muda huo huo, akaketi katika siti ya nyuma.
“Asalam aleikum!” Amata akamsalimu yule dereva kijana.
“Aleikum asalaam… karibu sana Islamabad…” akamjibu na
kumkaribisha.
“Shukran!”
“Waelekea wapi?”
“Club Islamabad…” Amata akajibu.
“Waoh! Club Islamabad… kilabu cha matajiri hicho kaka….
Karibu sana nitakufikisha..”
“Ila utanisubiri pale kwa kuwa ninaonana tu na tajiri mmoja
halafu nitaenda hotelini…”
“Na hoteli gani utapenda kufikia?”
“Na mara nyingi ni informer wazuri kwa adui zako. Kila mmoja
hupenda kutumia mwanamke kupata habari anazotaka… hapa
Islamabad wanawake wengi ni majasusi kutoka vikundi vya
wanamgambo, so chukua tahadhari braza….” Dhakar alipomaliza
kinywaji kilifika mezani. Kikamiminwa kwenye bilauri kubwa, kila
mmoja na ya kwake. “Cheers” wakagonga bilauri zao na kila mmoja
kupiga mafunda kadhaa kabla hajaitua mezani.
“Nipe mwongozo,” Amata akamwambia Dhakar.
“CIA agent…”
“Copy!” Amata akajibu kisha akainuka tayari kuondoka. “Kwa
lolote nitakutafuta…” akamwambia na kutoka zake nje ya kile
kilabu. Alipoifikia ile taksi, akakuta dereva amechapa usingizi.
Akamtikisa bega na kumwamsha. “Usilale ukiwa kazini…”
akamwambia huku akiingia na kuketi. Yule kijana akajifikicha
macho na kutia injini moto. Akaingia barabara ndogo ya Club na
kuikata barabara kuu ya Srinagar, akaikamata ile ya Constitution na
kukanyaga mafuta mpaka kwenye kona ya barabara ya Agha Khan,
akaifuata hiyo na kuwasili Hoteli ya Mariott salama salimini.
“Hapa ndiyo Mariott Hotel, pazuri na utapafurahia…” yule
kijana akainadi hoteli ile.
“Asante,” Amata akashukuru na kutoa pesa kumlipa dereva
huyo. Yule kijana akampa kadi yake ya mawasiliano, “ukinihitaji,
muda wowote unipigie nitakuhudumia,” akamwambia. Amata
akatikisa kichwa na kuondoka zake.
Ilikuwa hoteli mzuri ya nyota tatu, iliyopendezeshwa kwa taa
mzuri na maua ya kuvutia. Kamanda Amata akawasili katika dawati
la mapokezi na kupata chumba anachokihitaji. Ghorofa ya tatu
chumba namba thelathini na tatu.
Safari hii Nina tatu tatu, namba yangu ya bahati! Akajisemea
moyoni na kuufikia mlango wa chumba hicho. Akatazama kushoto
na kulia, hakuna tatizo. Akaipachika kadi yake kwenye kidubwasha
maalumu kilichokuwa pembeni kwa mlango huo. Akafungua
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
* * * *
Bhara Kahu Night Club ilikuwa kilabu cha siri cha usiku
ambacho watu wengi walikuwa wakikutanika kwa starehe. Kilikuwa
cha siri kwa sababu sheria kali za nchi hiyo hazikuruhusu hadharani
mambo kama hayo. Kijana mmoja wa Izbul aliwasili kwa siri
mpaka katika kilabu hicho. Wenzake wakiwa wamebaki nje kwenye
gari kumsubiri. Yule mmoja aliingia mpaka ndani ya kilabu kile.
Akaangazaangaza macho kutazama, maana alikwishaambiwa kuwa
Dhakar yupo katika yupo humo. Izbul walimpa taarifa mmoja wa
wanadada wa kilabu hicho kuchunguza kama mtu huyo yupo hapo
au la.
Dhakar alikuwa ameketi katika kaunta akiendelea kunywa
kinywaji chake taratibu, pembeni yake akiwa na mwanamke wa
Kizungu. Mguso katika bega lake ukamshtua. Alipogeuka,
akagongana macho na mhudumu wa kilabu hicho. “Kuna mgeni
wako nje!” yule mwanadada akamwambia. Dhakar akaangalia saa
yake, saa tatu na nusu usiku.
* * * *
Akachukua simu ya mmoja wao kisha akatoka nje ya hoteli ile. Vitu
vyake vyote vya muhimu alivichukua kwenye mkoba wake mdogo,
akaufunga kiunoni. Kule chumbani aliacha begi tu alilokuwa
amebebea nguo zake. Alijua, kuna kurudi au la.
* * * *
Jenerali Kahir alikurupuka kutoka kitandani baada ya kupata
taarifa hiyo. Alihisi BP inapanda na kushuka bila mpangilio.
Hakuamini anachosikia. Nini kimetokea? Akajiuliza. Akapiga simu
za vijana wake, zote hazipokelewi. Akapagawa. Simu aliyoipiga kule
kiwandani kwenye kitengo cha dharula ndiyo iliyompa mwanga.
“Tumevamiwa, kuna mtu kaja hapa na gari letu
tukamfungulia… amefanya uharibifu mkubwa sana, malori zaidi ya
matatu hapa yameshika moto, tunahitaji msaada…”. Kahir akahisi
kuchanganyikiwa. Akatoka taarifa haraka katika vikosi vya usalama,
akitumia cheo chake. Yeye mwenyewe, akavaa haraka haraka na
kumwacha mkewe Bi. Zulekha kitandani. Akakimbilia gari lake na
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
* * * *
Jinnah Evenue, barabara safi iliyopo mkabala na hifadhi
ndogo ya Fatima Jinnah katikati ya jiji la Islamabad. Ni upande wa
kushoto mwa barabara hiyo kama unaelekea chuo cha mchezo wa
cricket. Kamanda Amata alikuwa kwenye taksi ileile iliyomchukua
siku ya kwanza. “Niache hapo Punjab Criket…” akamwambia yule
dereva. Alipoteremka akamruhusu kuondoka. Alipohakikisha ile
taksi imepotea. Akajiweka sawa tayari kwa kazi inayoikabili. Amata
akatazama kushoto na kulia, akavuka barabara na kuelekea upande
ulipo mgahawa wa Mac Donald. Akatembea taratibu kuifuata
barabara ndogo ya kuelekea Silver Oaks. Upande huo akaifuata
moja ya ofisi iliyokuwa na kibao kuwa inakodisha magari. Hii ndiyo
hasa ilikuwa ikimleta eneo hili kwanza. Ndani ya ofisi hiyo
alipokelewa na mwanamke aliyeketi nyuma ya dawati kubwa lenye
kompyuta moja na simu ya mezani vikiambatana na makablasha
machache.
“Karibu sana nikusaidie…” yule mwanadada akamkatibisha
Amata.
“Yeah, naweza pata gari la kukodi?”
“Inawezekana, aina gani? Pickup, salon au mini bus? Tuna kila
aina ya gari unalohitaji”
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
SHAMBA
* * * *
* * * *
* * * *
11
KAMANDA Amata na Jamila walifika katika mji wa Ramban
alfajiri ya siku hiyo. Hapo hawakukaa bali safari iliendelea kuelekea
Jammu mpaka Kashmir. Jua lilipoanza kupanda, tayari lile jeep
lililowabeba Amata na Jamila lilikuwa kwenye mlima wa mwisho
kuteremkia kwenye bonde lile. Tayari jangwa walikwishaliacha
nyuma na sasa walikuwa kwenye uwanda wa mipunga na uoto wa
nyasi fupi za asili. Kijani kilichotanda huku na kule kilipendezesha
uwanda wote wa bonde hilo. Amata aliegesha gari pembeni na
kuteremka. Jamila naye akafuata.
Katika ukingo wa mlima ule Kamanda Amata alitazama
bondeni na kuuona mji huo wa Kashmir. Nyumba nyingi kubwa
na ndogo, nzuri kwa mbovu zikiwa zimetapakaa. Hali hiyo iliweza
kuleta maana ya moja kwa moja juu ya maisha halisi ya wakazi wa
eneo hilo.
“Ndege iliangukia wapi?” Amata akauliza.
“Siwezi kukumbuka… ila ni jangwani, hakukuwa na hata
nyasi moja kwa jinsi nilivyoliona eneo hilo toka juu…” Jamila
akaeleza huku mkono wake wa kuume ukiwa juu ya bega la
Amata.
“Tutawezaje kujificha katika jiji hilo tusijulikane?” Amata
akauliza.
“Mtihani… tufike tutajua hukohuko”
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
‘Free Kashmir’,
‘Kashmir is our home’,
‘Bring back our homeland’
* * * *
* * * *
‘Nakualika rafiki,
uje katika himaya yangu japo kunisalimu na
kufurahia pamoja nami chakula cha jioni ya leo…
kuna jambo la kuzungumza nawe…
Wasalaam Mansoor!’
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
Mara baada ya Amata na Jamila kuondoshwa pale sebuleni,
Mansoor na Fernandez wakarudi vitini na kuketi. “Umefanya nini
sasa?” Fernandez akauliza.
“Tumeshapata code ya tatu, tatizo nini? Kinachofuata ni
kumtemesha tu huyo mwanamke aseme…” Mansoor akamjibu.
Fernandez akatulia kwa jozi la sekunde akitafakari halo nzima
ilivyoenda.
“Kwa hiyo nikuandalie pesa?” Fernandez akauliza.
“Yeah! Tutafanya muamala baadae…. Ngoja kwanza nikamtie
adabu huyu mwendawazimu” Mansoor akamwambia mgeni wake
huku akimalizia funda la pombe iliyobaki kwenye bilauri yake.
Mansoor alionekana wazi kuwa na hasira hasa kutokana na kitendo
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
Jamila alifungiwa katika chumba kingine peke yake wakati Joel
na Bakari walitupwa katika chumba kilekile walichokuwamo tangu
awali. Hali ya makepeteni hao ilimtesa sana Jamila. Akaumiza
kichwa afanyeje aweze kuwaokoa, ilikuwa ngumu. Kichwani
mwake alikwishajua kuwa Kamanda Amata huko aliko atakuwa
keshaharibu hali ya hewa. Aliamini kuwa kijana huyo hasingeweza
kukubali kufa kijinga, lazima ajitetee. Alikizunguka kile chumba
huku na huku, akaujaribu mlango wake, akagundua umefungwa
kwa nje. Mlango wa chuma. Akakata tamaa. Akajipapasa kiunoni
mwake, akaichomoa ile pegan flash, akaitazama na kuiweka vizuri.
Jamila alihakikisha kidude hicho hakipotei. Akiwa katika kujiweka
vizuri ule mlango ukafunguliwa. Jamila akarudi nyuma na kuzuiwa
na ukuta. Wakaingia watu wawili waliokuwa wakiongea Kikurdu.
Wale jamaa walikuwa na shotgun kila mmoja. Wakamkamata
Jamila huku na huku na kutoka naye nje ya kile chumba.
Wakamkokota kwa nguvu huku mwenyewe akipinga kuchukuliwa
nao. Pamoja na kukuru-kakara zote hizo hakufanikiwa
kuwachomoka kwani mikono ya wale jamaa ilikuwa na nguvu
mithili ya vaisi.
Jamila akaingizwa katika chumba kingine, mandhali ya mule
ndani haikuwa ngeni kwake, alikikumbuka kwani ni kile
alichokaribishwa akiwa na Amata. Ndani ya chumba kile alimkuta
Mansoor na wanawake wale watatu. Juu ya Meza kulikuwa na like
sanduku la Pegan, mfumo wa kisasa wa usalama wa anga.
Pegan Box! Jamila akapigwa mshangao akawachomoka wale
vijana na kutaka kulivamia lile sanduku. Hakufanikiwa. Wale
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
12
MADAM S alisimama pasi na kusema lolote. Ukuta mdogo
uliojengwa kwenye kibaraza kile ulimkinga asianguke maana
alikuwa juu kabisa ya jengo lenye ghorofa tatu. Ulikuwa mgahawa
mdogo juu ya jengo hilo katika eneo la Bamaga. Bilauri yake
iliyojaa mvinyo ikiwa mkononi, mawazo yalimnyanyua kutoka
kitini mpaka pale na kusimama akitafakari jambo. Upande wa pili
wa jingo lile, ng’ambo ya barabara kuu ya kwenda bagamoyo
kulikuwa na ghorofa refu la kampuni moja ya simu lililozubngukwa
na uwanja mkubwa wa kupendeza.
Dakika kumi hivi zilimpeleka mbali sana kimawazo, mambo
yaliyokuwa yakimtukia katika siku hizo yalimtia hofu. Watu
walikuwa wakiendelea na burudani zao za kula na kunywa katika
jengo hilo huku kaupepo kakiwapa faraja dhidi ya joto kali la Dar
es salaam. Ghafla, kishindo kikubwa cha mtu kuanguka sakafuni
kiliwashtua waliokaa kwenye viti pale mgahawani.
Madam S alikuwa sakafuni, bilauri yake yenye mvinyo
ikitawanyika vipande vipande. Hakuna aliyesogea pale, kila mmoja
alisimama mbali huku akinamama wakipiga kelele za vilio. Hii
iliwavuta watu waliokuwa chini kupanda juu kuona nini
kilichotokea. Yote hayo yakiendelea, mwili wa mwanamke huyo
ulilala kimya, nguo yake aliyovaa ilipambwa kwa doa kubwa
jekundu kifuani pake. Simu yake ilikuwa mkononi ikiita kwa fujo.
Katika kundi lote hilo lililokuwapo, ni mtu mmoja tu
aliyesogea kwenye mwili ule na kuutazama kwa makini.
Akaichukua ile simu inayoita na kusoma ili kujua huyo apigaye.
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
* * * *
Huko Mabwepande, sherehe iliandaliwa, mbuzi wawili
waliangushwa, vinywaji vya kila aina. Wapo waliojua sherehe hiyo
inahusu nini na wapo waliokuwa wakila na kunywa tu bila kujua
lolote.
“Tumemwangusha bibi kizee!” mmoja wa wtu wa heshima
akawaambia wenzake. Wote wakacheka na kugonga cheers wakati
familia zao zikiburudika.
“Hata kama tutakosa hilo box, lakini mshenzi huyu mtibua
mipango ya watu tumemmaliza kuleni na mnywe… hiyo biashara
itafanyika hata kwa siri tu,” mwingine akaongeza kusema.
“Lakini habari za huko zinasemaje?”
“Huko ni maumivu tu, sijui huyo kiumbe aliyetumwa huko
anafananaje! Mpaka sasa hakuna taarifa yoyote tunayoipata, kwa
kifupi ameharibu kila kitu,” mjumbe mwingine akasema.
“Atauawa hapahapa kama bibi yake!”
“Kabisa na huo ndiyo mpango unaotakiwa kusukwa sasa…!”
mjumbe wa kwanza akawaeleza wenzake.
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
Kamanda Amata aliwasili Islamabad katika hoteli ileile ya
Mariott. Akaegesha lile Jeep upande wa pili wa hoteli hiyo ambapo
palikuwa na uwanja mkubwa wa kuegesha magari binafsi. Akavuka
na kuingia katika hoteli ile. Akapokelewa mapokezi kukabidhiwa
kadi ya chumba chake. Akaingia. Amata alijua vyema kucheza na
hisia za watu. Ndani ya chumba kile akachukua vichache
alivyoviacha. Akaiacha kadi katika sehemu yake, akatokea mlango
wa dharula na kuondoka. Nje ya hoteli ile, akachukua simu yake na
kupiga kwa yule dereva taksi aliyempokea. Wakakutana. Hakuwa
na la kuongea, alipakia mizigo yake, pamoja na lile pegani box.
“Nipeleke uwanja wa ndege!” yule kijana akampeleka. Baada
ya kuagana naye. Amata akafanya utaratibu wa kukodi ndege
maalum kwa kubeba wagonjwa. Akatoa taarifa kuwa ana mgonjwa
mmoja, mabaki ya binadamu na mtu mwingine. Ndege ile ilikuwa
maalum kwa kazi kama hizo. Huduma za ndege hii ni pamoja na
muuguzi na daktari.
Katika ofisi ile, Amata alijaza fomu maalumu za safari hiyo.
Maswali kadhaa yakaweka mambo sawa. Amata akajieleza vizuri na
kuchanganya na uongo wa kutosha. Akiwa hapo ofisini, akashtuka
Dar es salaam
13
Saa nane usiku, Scoba na Daktari Jasmini waliwasili uwanja
wa ndege wa kimataifa wa Dar es salaam. Scoba alikuwa
akiendesha gari la wagonjwa la kampuni binafsi ambalo waliliazima
kwa shughuli hiyo. Jasmini alikuwa na Land Rover Defender yenye
vioo vya giza. Katika msafara wao, gari la tatu lilikuwa na Gina
aliyekuwa amekamilika kwa lolote litakalotokea. Bunduki kubwa
aina ya Kalashnikov AK 47 ya kisasa kabisa. Vikinga risasi
viliuzunguka mwili wake, kofia yake ya chuma iliyounganishwa na
chombo cha mawasiliano ilitulia kichwani. Chiba naye alikuwa
katika mavazi hayohayo, waliimarisha ulinzi. Walijua nini kinaweza
kutokea ingawa maandalizi ya safri hiyo yalikuwa siri kubwa
miongoni mwao. Hawakuacha kuchukua tahadhari.
Uwanja walioutumia kuipokelea ndege hiyo haukuwa wa jeshi.
Waliofia siri yao kuvuja. Madam S bado walikwishamhamisha
kutoka Hindu Mandal na kumpeleka Shamba. Yale magari
yakaingia katika eneo la ofisi za kupakulia mizigo za DHL lililopo
katikati ya Uwanja wa Jeshi na ule wa abiria wa kawaida. Saa nane
hiyo, ile ndege ikawasili na kuongozwa kufika katika eneo hilo.
Hakuna mtu yeyote aliyetilia shaka. Ikasogea mpaka jirani kabisa na
jingo hilo ambapo ndege nyingine za mizigo hufanyia upakuaji
wake. Kamanda Amata na Jamila wakawa wa kwanza kabisa
kuteremka. Rubani pamoja na wafanyakazi wake wakasaidiana
kuteremsha mwili wa Bakari uliohifadhiwa vizuri kwenye boxi
maalumu. Kitanda alicholazwa Joel kikateremshwa na
kubadilishwa. Jamila alilichukua Pegan Box mkononi mwake.
* * * *
Kama kuna siku ambayo watu walihadhirika na
kuchanganyikiwa ni hii. Madam S aliwasili Ikulu akiwa na
Kamanda Amata, na kepteni Jamila. Siku hii kulikuwa na kikao
maalum cha maafisa wa jeshi kujadiliana kuhusu swala hilo. Ujio
wa Madam S ulikuwa wa ghafla, hata Mkuu wan chi mwenyewe
hakuutegemea.
Alipokuwa katika mkutano huo akapata taarifa ya ugeni huo
wa dharula na muhimu. Akapigwa na butwaa, hakujua nini
kinatukia.
Madam S! akawaza. Hajafa? Akajiuliza. Hakuwa na jinsi,
akakubali ugeni huo uingie ndani ya ukumbi huo. Mara baada ya
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
* * * *
* * * *
“Jamani, si mlisema mmemuua?” mmoja wa wanajopo
akauliza.
“Niliuiza mara kumikumi, mkanihakikishia amekufa, yule
aliyeleta Pegan Box pale ni nani? Tunazidiwa akili mpaka na
mwanamke… yaani yunapanga jinsi ya kulirudisha hilo box wakati
tayari limeshafika nchini,” huyu aliyekuwa akiongea, alionekana
miguu tu. Sura yake ilifichwa. Yeye aliketi juu na wajumbe
walikuwa chini. “Mbaya Zaidi, amewasilisha ofisibi kwangu,
orodha ya majina yenu wote kuwa mnahusika. Upelelezi
umefanyika saa ngapi, hata mimi sijui…” akaongeza kusema.
Wajumbe wale wakabaki kimya, hakuna aliyeongea. “Tunaliweka
vipi jambo hili?” akauliza.
Sold to Agnes Mbatali O-201126-P035021-K
Written by Richard Mwambe – Call 0672160016/ whatsapp 0734550514
Ф MWISHO Ф