Professional Documents
Culture Documents
UTANGULIZI
Kwa Uelewa wa Wengi,Wanahesabu matukio yafuatato kama majaribio ya kuiangusha
serikali ya Mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE
Nimeorodhesha Visa Vinne Na nitaanza kwa kusimulia kisa kimoja baada ya kingine katika
series hii ya masimulizi ninayoipa jina la FAILED ATTEMPTED COUPS
MUTINY-MAASI YA KIJESHI
Mutiny ni kitendo cha kikundi cha Wanajeshi kuasi na kupinga amri au uongozi wa juu wa
kijeshi. Pia hali hii hutokea kwenye Maswala ya Ubaharia ambapo officers wa chini huasi
maelekezo ya Uongozi wa melini.
Kuna siku ambazo historia rasmi ya Tanzania haipendi kuzikumbuka, lakini haitaweza kukaa
bila kuzikumbuka
Januari 20, 1964, siku kulipotokea maasi ya kijeshi katika Tanganyika, ni miongoni mwa siku
hizo. Hiyo ilikuwa ni wiki moja tu baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12.
Hata Mwalimu Nyerere alijua kuwa ni vigumu kusahau, ingawa inawezekana kwa kuificha
historia. Kwa huzuni Nyerere alikaririwa na jarida TIME (Jan. 31, 1964), chini ya makala
yake, The Rise of the Rifles, akisema: “Itachukua miezi, na hata miaka, kufuta katika bongo
za walimwengu kile walichosikia kuhusu matukio ya juma hili.” Hata hivyo imeshaanza
kufutika katika bongo za walimwengu.
Kwa maneno mengine tunaweza kusema haya yalikuwa ni Mapinduzi ya Tanganyika. Tofauti
kati ya Mapinduzi ya Zanzibar yale ya Tanganyika ni kwamba: Mapinduzi ya Zanzibar
yaliruhusiwa yafaulu, lakini Mapinduzi ya Tanganyika hayakuruhusiwa kufaulu.
January 20, 1964 kulitokea zahama mjini Dar es Salaam katika Kambi ya jeshi ya Colito (sasa
inajulikana kama Lugalo), ambalo lilisambaa hadi kambi nyingine nchini.
Baada ya tukio hilo, maswali mengi yaliulizwa. Ingawa tayari mengi yamejibiwa, majibu hayo
ni ya ‘kuzunguka mbuyu’. Je, yalikuwa ni mapinduzi ya serikali (kama yale ya Zanzibar)?
Yalikuwa ni maasi tu ya kijeshi? Ulikuwa ni mgomo tu wa wanajeshi waliotaka kuongezwa
mishahara?
Tafsiri zao zilikuwa hivi: kama ingekuwa ni mapinduzi, ilikuwa ni lazima kwanza wanajeshi
walioasi wangeteka maeneo yote muhimu ya kama Bunge na Ikulu. Ilikuwa ni lazima
wawakamate mawaziri, jambo ambalo hawakufanya. Hawakuwa wamemtangaza kiongozi
wa nchi.
Ilidaiwa kuwa aliyekuwa afaidike na maasi hayo ni Waziri wa zamani wa Ulinzi na Mambo ya
Nje wa Tanganyika, Oscar Kambona ambaye alikuwa na uhusiano wa karibu sana na Kaasim
Hanga wa Zanzibar.
Tanganyika ilirithi jeshi kutoka kwa wakoloni wa kiingereza baada ya Uhuru Dec 9 1961
likijulikana kama KING’S AFRICAN RIFLES(KAR) na baadae kuitwa TANGANYIKA RIFLES(TR)
Baada ya Uhuru,ili kukidhi matarajio ya watanganyika,zilitakiwa nafasi zote za juu za utawala
nchini,zikabidhiwe kwa wazarendo.Ulikuwa ni utamaduni uliojengeka kwa nchi zote
zilizopata uhuru kufanya hivyo.
Mwalimu Nyerere akiwa ni waziri mkuu wa serikali mpya,hakuchukua hatua hizo kwa
haraka.Hata aliyekuwa waziri wake wa mambo ya ndani GEORGE KAHAMA hakuchukua
hatua zozote kubadilisha uongozi wa Waingereza ndani ya Jeshi la polisi.
Yakaanza malumbano ndani ya kamati Kuu ya TANU kuwa mwalimu Nyerere alikuwa
anaikumbatia serikali ya kikoloni.
Ili kuhepuka malumbano hayo ambayo yangevunja mshikamano baina ya
wanachama,Mwalimu akaachia madaraka na kurudi kijijini kwake kukiimarisha chama kama
mwenyekiti wa TANU. RASHIDI KAWAWA akampokea kijiti katika nafasi ya Waziri mkuu na
OSCAR KAMBONA aliyekuwa waziri wa elimu,akachukua madaraka ya waziri wa mambo ya
ndani nafasi ambayo ilikuwa mwanzoni inashikiliwa na GEORGE KAHAMA.
Uongozi huu mpya ukabebeshwa mzigo wa kuleta hayo mabadiriko ya kuwatoa wazungu na
kuwaweka watanganyika katika madaraka serikalini.
Haraka sana,KAMBONA akamtimua kamishna wa polisi Mwingereza na kumteua ELANGWA
SHAIDI kuchukua nafasi hiyo. Kasi hii ilianza kuishtua jumuiya ya kimataifa.
Jambo hili liliwaudhi wengi hasa Wanajeshi wa TANGANYIKA RIFLES wazarendo na vyama
vya wafanyakazi.
Hali iliendelea namna hiyo hadi mwaka uliofuata ambapo January 12 1964 kulitokea
mapinduzi ya Zanzibar na Abeid Karume akakimbilia bara.
Kuanzia January 13 1964 Nyerere akawa busy na mgogoro wa Zanzibar ambapo alimshauri
Karume arudi Zanzibar kwani kukimbia kwake kutamfanya aonekane ni mwoga.
John Okelo aliyeongoza mapinduzi yale akamtangaza Karume kuwa rais asiye mtendaji huku
akimtaka ajitokeze popote alipo mafichoni aende akachukue madaraka yake. Binafsi Okello
akajitangaza kuwa Kiongozi wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Jumatatu Jan 14 1964 OSCAR KAMBONA ambaye alikuwa ni waziri wa mambo ya nje na
Ulinzi,akiwa nchini Kenya alimpigia simu Mwalimu na kumwambia serikali za Kenya na
Uganda zimeitambua Seikali ya mapinduzi Zanzibar ja ni yeye tu (MWALIMU) amebaki
kuitambua serikali hiyo. Mwalimu akamkatalia kwa kusema bado hana uhakika kama
Karume yupo madarakani.
Jumanne,January 15 Mwaka 1964 Mwalimu akasafiri kwenda Nairobi ili kukutana na Waziri
mkuu wa Kenya JOMO KENYATTA kujadili kuhusu shirikisho la Afrika Mashariki na
kuzungumzia msimamo wake juu ya Zanzibar
Jumatano, Jan 16 Sultan aliyepinduliwa Zanzibar akawa ametia nanga Dar Es salaam baada
ya Kenya kukataa kumpokea. Mwalimu akampokea ili akamilishe mipango ya kuhamia
Uhamishoni Uingereza
Siku mbili zilizofuata yaani ijumaa Tarehe 18 na Jumamosi Tarehe 19 zilikuwa za utulivu kwa
Mwalimu kwani hakuwa na fatiki yoyote. Katika kipindi hiki, askari wa FFU 300 waliwasili
Zanzibar wakitokea Tanganyika. Mwalimu hakujua kabisa kuwa alikuwa amejipunguzia Ulinzi
wake kwa Tukio ambalo lingefuatia tarehe 20 kuamkia tarehe 21.
Ni Tarehe 20 Ambapo Mwalimu Nyerere alikuwa Ikulu kwenye Mazungumzo na JOHN
OKELO ambaye ndiye aliyeongoza mapinduzi ya Zanziba(Mpaka leo haijasemwa kokote jinsi
Okelo alivyoondoka baada ya jaribio hili)
Maasi haya yalitokea wiki moja tu baada ya mapinduzi ya umwagaji damu ya Zanzibar,
Januari 12, 1964; na usiku huo wa maasi hayo, Kiongozi wa Mapinduzi ya Zanzibar “Field
Marshal” John Gidion Okello, alikuwa na mazungumzo na Mwalimu Nyerere Ikulu, Dar es
Salaam, katika hali ya kubadilishana mawazo juu ya hali ya Zanzibar ambapo Mwalimu,
alimshauri Okello afanye kazi kwa imani na Rais Abeid Amani Karume
Wakati jeshi hilo likiasi; siku hiyo hiyo, na saa hiyo hiyo, majeshi ya Kenya na Uganda nayo
yaliasi kwa staili hiyo hiyo. Maasi yote ya nchi tatu hizo yalizimwa na majeshi ya Uingereza
siku moja na wakati huo huo.
Alipotoka nje, aliona askari wake 12 wakikamatwa na wenzao wenye silaha na kutiwa
mahabusu. Ndipo alipofahamu kwamba, nusu ya askari 800 wa Kikosi hicho walikuwa
wameasi. Aliweza kutoroka yeye na familia yake hadi katikati ya jiji, akaiacha familia kwa
Balozi wa Australia, kisha akakakimbilia kwa Afisa mwenzake, eneo la Oyster Bay.
Akiwa huko, akampigia simu Oscar Kambona, akamwomba, naye akakubali, kupeleka ndege
tatu Kikosi cha Pili huko Tabora, kuleta askari waliokuwa bado waaminifu kwa Serikali.
Douglas na Kambona hawakujua kwamba, tayari waasi walikuwa wamefunga barabara
iendayo uwanja wa ndege; kwa hiyo, marubani walirudi mbio; naye Douglas akakimbilia
kwenye Ubalozi wa Uingereza, akajificha kwa siku tano hadi Januari 25.
Douglas alikuwa amempigia simu Mkuu wa Polisi, ambaye alikwenda moja kwa moja
nyumbani kwa Makamu wa Rais, Rashidi Kawawa, eneo la Ikulu na kumwamsha, kisha hao
wawili kwa pamoja, wakaenda kumpa habari Mwalimu.
Mwalimu alipoelezwa juu ya maasi hayo, alilipuka kwa hasira na ghadhabu kubwa papo
hapo; akataka kwenda yeye mwenyewe kukutana na Waasi hao ili wamweleze sababu za
kitendo hicho cha aibu. Mama Maria Nyerere, kwa machozi na kwa kupiga magoti, alimsihi
mumewe asitoke kwenda kukutana na watu wenye silaha, lakini hakufanikiwa kumgeuza
nia.
Ndipo watu wa Usalama walipojenga hoja nzito kumzuia, na hoja hiyo ikamwingia; akakubali
kuteremka dari ya chini, kisha yeye, Kawawa na Mama Maria Nyerere, wakatorokea mahali
kusikojulikana. Wakati huo, tayari waasi walikuwa kwenye lango kuu la Ikulu wakimtafuta.
Bado ni kitendawili kuhusu mahali Mwalimu na wenzake walikokuwa wamejificha. Wapo
wanaodai alijificha Misheni au Kanisani; wapo pia wanaosema alijificha kwenye nyumba ya
Balozi mmojawapo Jijini.
Wengine wanasema alijificha kwenye kibanda kidogo sana (Kigamboni?) karibu na Pwani; na
baadhi wanadai alikwenda Arusha au Nairobi. Lakini wapo pia wanaosema alijificha kwenye
meli. Wala haielezwi kama John Okello aliondokaje Ikulu usiku huo baada ya mazungumzo
au kama maasi yalimkuta Ikulu usiku huo.
Siku ya tatu baada ya maasi ya kikosi cha kwanza, Jumatano, Januari 23 asubuhi, ghafla
Nyerere akatokea hadharani amepanda gari la wazi akiwa na Mama Nyerere na Waziri wa
Mambo ya Ndani, Job Lusinde, akatembelea kila sehemu ya mji iliyoathiriwa na maasi.
Alhamis ya Januari 24, ilikuwa shwari; lakini Ijumaa, Januari 25, mazungumzo kati ya Serikali
na waasi yalionekana kuanza kuvunjika, wakaasi tena. Ni nani alikuwa kiongozi wa maasi
haya awamu ya pili? Sajini Higo Ilogi tena?
Siku hiyo ilipokelewa taarifa kwamba, Kikosi cha Pili cha Jeshi kilichokuwa Tabora nacho
kilikuwa kimeasi, baada ya kupata habari kwamba wenzao wa Collito walikuwa wameasi.
Inawezekana, ama walikuwa hawajapata taarifa kwamba wenzao wa kambi ya Colito
walikuwa wamerejea kambini; au walifahamu, lakini wakataka nao watekelezewe mambo
kadhaa kwenye Kikosi chao.
Wakati Kikosi cha Tabora kikiendelea na maasi, ilipokelewa hapo Tabora, simu ya maandishi
(telegraph) kutoka kwa Kambona, kwamba alikuwa amemteua Kapteni Mirisho Sam Hagai
Sarakikya, kuwa Mkuu wa Kikosi cha Tabora. Wakati huo Sarakikya na maafisa wengine
walikuwa wamekamatwa na kuwekwa mahabusu na askari walioasi hapo Tabora.
Sarakikya akatolewa mahabusu, akaomba simu hiyo isomwe kwa sauti; kisha akatoa amri
wasimame “Mguu sawa”, wafungue beneti na kutoa risasi. Nao wakamtii. Usiku huo,
Sarakikya alifanya mipango ya kuwasafirisha maafisa wa Kiingereza kutoka Tabora kwenda
Dar es Salaam na hatimaye makwao.
Tukio la Januari 21, na lile la Tabora pamoja na hali ya hatari ilivyokuwa huko Kenya, Uganda
na Zanzibar, lilifanya Serikali ya Uingereza ichukue tahadhari ya ziada kwa kupeleka askari
2,000 zaidi ukanda wa Afrika Mashariki.
Kwa hiyo, manowari iliyoitwa Rhy, ikawa imetia nanga hima Pwani ya Dar es Salaam, na
nyingine Centaur; iliyobeba ndege, iliwasili na askari 600.
Haielezwi ni jinsi gani Sajini Higo Ilogi aliweza kuponyoka, akaonekana mjini asubuhi hiyo
kwenye jumba la Simu za Nje za Kimataifa (Extelcoms), akituma simu ya mandishi kwa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) U Thant, kuomba msaada. Simu hiyo ilisomeka hivi:
“Majeshi ya Tanganyika yametekwa na askari wasiojulikana saidia haraka kuleta Majeshi
ya Umoja wa Mataifa LUTENI KANALI ILOGI, MKUU WA JESHI”.
Turejee kwenye swali letu la msingi: Nani alichochea maasi ya jeshi letu mwaka 1964? Oscar
Kambona? John Okello?
Kambona alikuwa Waziri mwenye dhamana ya ulinzi wakati huo, ambapo Jeshi lilikuwa chini
ya wizara yake. Kwa sababu hii, kushiriki kwake katika kutuliza maasi ya awamu ya kwanza,
hakuwezi kuchukuliwa kwamba alikuwa na hisa au kwamba alijua mpango huo wa maasi
hayo.
Ni ujasiri wake tu uliomtuma kukabiliana na hali hiyo. Kama kweli angekuwa na nia mbaya
kwa Serikali; na kwa kuzingatia pia jinsi alivyodhibiti hali hadi askari wakamkubali,
angeshindwaje kupindua nchi ambayo ilikuwa mikononi mwa Jeshi kwa siku mbili mfululizo
kama alikuwa na nia hiyo?
Je, ni Field Marshal John Okello? Hapa tena jibu ni HAPANA. Yeye hakuwa na muda huo, kwa
sababu kwa kipindi chote tangu Mapinduzi ya Zanzibar, alikuwa katika hati hati za kulinda na
kuimarisha utawala wake visiwani kutokana na tishio la kuenguliwa na wahasimu wake
ambao alidai hawakushiriki katika Mapinduzi. Okello aliongoza Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar kwa miezi miwili mfulilizo kabla ya kuenguliwa na Karume kwa kushirikiana na
Mwalimu Nyerere.
Wala haishangazi kwamba, maasi ya askari hawa yaliweza kuambukizwa kwa wenzao wa
Kenya na Uganda, ikizingatiwa kuwa majeshi ya nchi hizi tatu yamezaliwa na Jeshi la
Wakoloni wa Kiingereza waliotawala nchi hizo. Kwa hiyo, kwa kipindi hicho, na kwa
mazingira ya kazi ya wakati huo, malalamiko yao yalifanana kuwafanya wadai haki zao kwa
njia na kwa mtindo unaofanana.
Nakubaliana na maoni ya Balozi Abbas Kleist Sykes (akinukuliwa mahali fulani mwaka 2001),
kwamba, “Maasi ya Jeshi la Tanganyika Rifles (TR) mwaka 1964, yalitokana kwa sehemu
kubwa na kuchelewa kuwaondoa makamanda wa kizungu na kuwapandisha vyeo waafrika”,
kama ilivyofanyika kwa Jeshi la Polisi na watumishi wengine serikalini. Na ndivyo ilivyokuwa
kwa maasi ya Kenya na Uganda.
Wala haishangazi kwamba, viongozi wa vyama vya wafanyakazi waliungana na waasi awamu
hii ya pili kutaka kuiangusha Serikali, kutokana na ukweli kwamba, tangu Mwalimu
alipositisha zoezi la “Africanisation” Januari 1963, wao walikwishaapa mapema kutolala
usingizi “mpaka kieleweke”.
Kutokana na maasi hayo, Mwalimu alikifuta Kikosi chote cha Kwanza (Colito Barracks) na
kuwafukuza kazi askari 100 wa kikosi cha pili, Tabora. Alifukuza pia asilimia 10 ya askari
polisi 5,000 waliokuwapo, kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao wa kudhibiti maasi.
Hata wakati Mapinduzi ya Zanzibar yanafanyika, Hanga aliondoka haraka kwenda Dar es
Salaam kuzungumza na Kambona kuhusu matukio ya Zanzibar. Hadi leo mazungumzo hayo
yamekuwa siri.
Baada ya Mapinduzi Hanga alikataa kutoa sababu zozote za yeye kwenda kuonana na
Kambona na hakutaka kuzungumzia jambo walilojadiliana. Alichosema, alipohojiwa na
mwandishi wa Kiingereza, Keith Kyle, kwa mujibu wa gazeti The Spectator, Februari 14,
1964, “...Nilikuwa kazini.”
Kambona walikutana tena na Kassim Hanga siku moja kabla ya maasi ya kijeshi yaliyotokea
mjini Dar es Salaam usiku wa January 20, 1964 ambayo yalitokea juma moja tu baada ya
Mapinduzi ya Zanzibar.
Inawezekana Mwalimu Julius Nyerere alijua jambo fulani kuhusu mapendekezo ya Kambona
kumsaidia Kassim Hanga, lakini hakujua jambo lolote kuhusu maasi ya kijeshi yaliyotokea
Dar es Salaam na kumfanya yeye akimbilie mafichoni Kigamboni.
Kambona alijua kuhusu mpango wa maasi ya kijeshi na, kwa mujibu wa Anthony Clayton
katika kitabu chake, The Zanzibar Revolution, “...Kambona alitazamia kufaidika kisiasa
kutokana na machafuko ambayo yangetokea.”
Kwa maana nyingine kuna watu waliokuwa wamepanga kufanya mapinduzi huko Zanzibar
usiku wa Januari 20, siku ambayo kulitokea machafuko katika mji wa Dar es Salaam, lakini
John Okello akawazidi ‘kete’.
Kwamba Mapinduzi ya Zanzibar yalipangwa kufanywa na Kassim Hanga na watu wake huko
Zanzibar usiku wa Jumamosi ya Januari 18 kuamkia Jumapili ya Januari 19 na usiku huo huo
Kambona, au watu waliohusiana naye, wangefanya Mapinduzi ya Dar es Salaam ni jambo
lililozua gumzo wakati huo.
Kama yote hayo ni ya kweli, Mapinduzi ya Unguja na yale ya Dar es Salaam yalipangwa
kufanywa siku moja—usiku wa Januari 18—19, 1964. Mipango hiyo ilikuwa imeandaliwa
kwa muda mrefu.
Hata mijadala fulani fulani, kama ile ya kuwajadili Wacuba walioonekana Dar es Salaam na
Unguja katika kipindi hicho—ilifanyika Bagamoyo na maeneo mengine ambayo
hayakujulikana haraka.
Kwa kawaida Kambona alijua au alikuwa amearifiwa mapema kuhusu maasi ya Dar es
Salaam katika vitengo vya usalama vya Tanganyika na maofisa wa Kiingereza ambao bado
walikuwa wakiitumikia Serikali ya Tanganyika, lakini hakuchukua hatua yoyote kuikabili hali
hiyo hadi pale ilipotokea. Mmoja wa maofisa hao ni Luteni Kanali Rowland Mans.
Ilidaiwa kuwa mara kwa mara, Kambona, akiwa Waziri wa Ulinzi, alikuwa akiwatembelea
maofisa wa ngazi za chini katika kambi ya Colito, na mara nyingine bila kuonana na viongozi
wakubwa wa kambi hiyo.
Pia, kwa sababu zisizojulikana dhahiri lakini ambazo inawezekana ni njia ya kumsaidia
Kassim Hanga, Kambona alitenga silaha na zana nyingine za vita zilizotoka Algeria na
kuwasili Dar es Salaam Jumatano ya Januari 3, 1964 na kupakuliwa chini ya ulinzi maalum.
Silaha hizo ziliwasili siku tisa kabla ya Mapinduzi ya Zanzibar na wiki mbili kabla ya maasi ya
Dar es Salaam.
Silaha hizi, baada ya maasi yaliyotokea Dar es Salaam, inadaiwa—na hii inadaiwa tu—
zilichukuliwa na kutoswa baharini na Jeshi la Maji la Uingereza lililoombwa na Serikali ya
Tanganyika Jumamosi ya Januari 25, 1964, kukomesha maasi ya jeshi Dar es Salaam.
Hata hivyo nyingi za silaha hizo zilitumiwa wakati wa Vita Kuu II Kaskazini mwa Afrika.
Zilitumiwa na Waingereza, Wajerumani, na Waitalino na zingekuwa vigumu kutumiwa katika
miaka ya 1960 kwa kuwa hazikuwa na vipuri.
Inasemekana kwamba silaha hizo ziliagizwa na Serikali ya Tanganyika kwa ajili ya chama cha
Frelimo cha Msumbiji. Zilipowasili Dar es Salaam, pamoja na kwamba maofisa wakubwa wa
Jeshi la Tanganyika walikuwa ni Waingereza, silaha hizo zilipakuliwa na wanajeshi Waafrika
tu.
Inasemwa pia kwamba silaha hizo hazikuhifadhiwa kama ilivyopaswa, kwa hiyo zikawafanya
Waingereza washtuke. Walipozichunguza sana wakagundua kuwa zana nyingine zilitiwa
alama ya msalaba mweusi, wakachukulia kwamba hizo zilizotiwa alama zilikusudiwa
kupelekwa Zanzibar kumsaidia Kassim Hanga kulingana na tetesi walizokuwa wamezipata
hapo awali. Lakini silaha hizo hazikuwahi kufika Zanzibar. Je, zilikusudiwa kutumika wakati
wa maasi yaliyotokea Dar es Salaam?
Kwa mujibu wa utafiti wa Ndugu Nestor Luanda katika kitabu Tanganyika Mutiny, Kambona
alianza kufika mara kwa mara katika Makao Makuu ya Jeshi mwishoni mwa 1963 na
aliwaambia maofisa wa kijeshi wa Kiingereza kwamba alitaka wawe wameondoka nchini
ifikapo mwishoni mwa 1964.
Kambona alitaka maofisa wengi wa Kitanganyika wapewe vyeo haraka, jambo ambalo
Waingereza walidai haliwezi kutendeka kwa ghafla kama alivyotaka. Kuanzia hapo maofisa
hao wakaanza kuwa na wasiwasi kuwa chochote kinaweza kutokea.
Hata hivyo, usiku ule wa maasi maofisa wengi wa Kiingereza walikamatwa na ‘kutiwa ndani’
katika Kambi ya Colito’ ambako kwa wakati huo umeme tayari ulikuwa umekatwa.
Kikosi cha kiasi cha wanajeshi 25 waliondoka kambini hapo kwenda Ikulu kumfuata Rais
Julius Nyerere kikiongozwa na mwanajeshi machachari, Sajenti Francis Hingo Ilogi, mzaliwa
wa Bukene, Tabora.
Wakati huo huo, Mkuu wa Tawi Maalum, Emilio Mzena, baada ya kuambiwa yaliyotokea na
kwamba wanajeshi walio na silaha wameelekea Ikulu, aliwaarifu watu wake waliokuwa Ikulu
na kuwaambia wamtoroshe Rais.
Mzena aliambiwa kuhusu maasi hayo majira ya saa 8:00. Nusu saa baadaye, saa 8:30, baada
ya kuamshwa na walinzi wao, Rais Nyerere, akiongozana na Makamu wake, Rashidi
Kawawa, waliondoka Ikulu kupitia mlango wa nyuma. Walipishana na wanajeshi hao kwa
sekunde chache tu.
Baadaye wanajeshi hao walipelekwa kwa Oscar Kambona, wakamchukua kwenda naye
kambini kwao, Colito. Wakati huo ghasia na uporaji wa mali za raia tayari ulikuwa umetanda
katika mitaa ya mji wa Dar es Salaam.
Wakati hayo yakitokea, tayari walikuwa wameanza kupeana vyeo huko huko kambini.
Wengine walipokea vyeo hivyo lakini wengine hawakuharakisha kupokea. Kwa mfano, Ilogi
ambaye alikuwa na cheo cha Sajini alijikuta katika cheo cha Luteni Kanali na wengine
walimtaka mtu kama Kapteni Alex Nyirenda kuwa Brigedia.
Maasi hayo yalisababisha ghasia nyingi mitaani, hususan Mtaa wa Msimbazi maeneo ya
Kariakoo. Maeneo mengi ya katikati ya mji risasi zilirindima. Mwarabu mmoja eneo la
Magomeni, kwa kuona duka lake linavamiwa, alimpiga risasi mwanajeshi mmoja
aliyejulikana kwa jina la Kassim.
Koplo Nashon Mwita, ambaye alishuhudia mauaji hayo, alirudi kambini kujizatiti.
Akiongozana na askari mwingine, Luteni Mwakipesile, pamoja na wanajeshi wengine,
walifika Magomeni na kummiminia risasi Mwarabu huyo.
Kana kwamba haikutosha, waliiteketeza nyumba yake kwa moto. Katika nyumba hiyo,
inasemekana, Mwarabu huyo aliteketea na familia yake ya watu 15.
Maasi hayo yalianza kusambaa haraka. Siku moja baadaye, Jumatatu ya Januari 20, yalifika
hadi kambi ya jeshi ya Tabora ambako wanajeshi wengi, kama Mrisho Kapteni Sarakikya,
Luteni David Msuguri na Luteni Abdallah Twalipo walikuwa wamepandishwa vyeo.
Jumanne ya Januari 21, maasi hayo yakafika Nachingwea—kambi ambayo ndiyo kwanza tu
ilikuwa imeanzishwa, ikiongozwa na Meja Temple Morris.
Jumamosi ya Januari 25, 1964, baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya, Mwalimu Nyerere
aliomba msaada kutoka Serikali ya Uingereza kunyamazisha maasi ya kijeshi yaliyokuwa
yanazidi kusambaa katika Tanganyika. Hatimaye makomandoo wa Uingereza waliwasili kwa
helikopta na kuwanyang’anya silaha waasi. Jioni ya siku hiyo hiyo maasi ya Tabora nayo
yakazimwa.
Maasi hayo, hasa katika kambi ya Colito, yalizimwa baada ya makomandoo hao wa
Uingereza kutua na kuanza kulipua lango la mbele la kambi hiyo. Mara moja askari walioasi
walijisalimisha.
Kikosi cha Uingereza kiliongozwa na Brigedia Patrick Sholto Douglas. Waasi watatu waliuawa
katika operesheni hiyo. 20 walijeruhiwa na wengine 400 walikamatwa, kwa mujibu wa
‘TIME’ (Jan. 31, 1964). Wengine walitoroka.
Kwa njia hiyo Rais Nyerere alirejea madarakani, lakini historia ya Tanganyika ikabadilika
moja kwa moja.
Jioni ya Januari 25, baada ya kutembelea mitaa ya Dar es Salaam kujionea uharibufu
uliofanywa na wanajeshi walioasi, Mwalimu alisikika moja kwa moja Tanganyika
Broadcasting Corporation (TBC) akisema:
“Jana nililazimika kuomba msaada wa Mwingereza. Kwa bahati akakubali. Asubuhi hii kikosi
cha kwanza kikawasili …yote sasa ni shwari. Nasikia maneno ya wajinga kwamba eti
Waingereza wamerudi Tanganyika.”
Wiki tatu baada ya maasi (Feb. 16, 1964), aliitisha mkutano wa hadhara Viwanja vya
Jangwani na kuwaambia Watanganyika hivi: “…(Wanajeshi walioasi) Walidanganywa.
Wendawazimu walikuwa wawili, watatu. Wale wengine waliswagwa tu. Wakivutishwa
bangi, wakaja mjini kutenda maovu. Tukaenda kwa Mwingereza. Bwana Mwingereza
tusaidie utuondolee balaa hili.”
Baada ya maasi hayo, Mwalimu Nyerere alianza kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa
hakuna kosa linalorudiwa. Hatua ya kwanza, kwa mujibu wa jarida TIME (Feb. 07, 1964)
alianza kukamata wote waliohusika, kisha akapiga marufuku gazeti Nation la Kenya
linalomilikiwa na Aga Khan kutouzwa katika Tanganyika.
Kwanini marufuku hayo? TIME linasema hivi: “Gazeti hilo (Nation) lilitoa taarifa sahihi lakini
yenye raghba kuhusu kuangushwa kwa serikali yake. Kupunguza uwezekano wa mfarakano
wa mawazo, amewabadilisha makamanda wa Kiingereza akaweka wa Kiafrika. Wakati huo
huo, ameteua kamati ya kutafakari mabadiliko ya kikatiba ambayo yataifanya Tanganyika
kuwa nchi ya kidemokrasia ya ‘chama kimoja kisheria na kiuhakika.”
“…Uso wake ulikuwa na simanzi. Hakuna hata Mtanganyika mmoja aliyeuawa kwa miaka
yote 17 ya kupigania Uhuru wa Tanganyika. Lakini sasa baada ya uhuru Watangayika
wameuawa,” likasema TIME (Jan. 31, 1964)
Jumanne ya Aprili 21, Mwalimu Nyerere alimwapisha Sir Ralph Wildham ndani ya Ikulu ya
Dar es Salaam kuwa Jaji Mkuu wa Tanganyika, na kumwambia awashughulikie kikamilifu
wanajeshi waliofanya jaribio la kuipindua serikali yake hapo Januari 19, 1964. Ndipo Sir
Wildham akatangaza rasmi kuwa wanajeshi wa Kambi ya Colito waliotaka kuiangusha
serikali watafikishwa mahakamani siku ya Jumatatu, Aprili 27, 1964.
Wakati huo huo Rais alimteua Kapteni Abdallah Twalipo (35) na Kapteni Lukias Shaftaeli
(39), wote wakiwa ni wanajeshi wa jeshi la Wananchi, kuwa wajumbe wa mahakama ya
kijeshi. Sir Wildham akawa Rais wa mahakama hiyo. Baada ya uteuzi huo, Mkurugenzi wa
Mashitaka, Herbert Wiltshire Chitepo, alisema angewaita mashahidi 25.
Kesi hiyo iliendeshwa kwa siku chache na hatimaye hukumu ikatolewa. Ijumaa ya Mei 15,
1964, siku 19 baada ya kufanyika kwa Muungano wa Tanzania, wanajeshi walioasi katika
Kambi ya Colito walihukumiwa, lakini adhabu zao zilikuwa tofauti.
Sajini Francis Hingo Ilogi alihukumiwa kifungo cha miaka 15 jela, Koplo Aliche miaka kumi,
Koplo Baltazar miaka kumi, Private Jonas Chacha miaka kumi, Private Pius Francis miaka
kumi.
Wengine ni Private Patric Said John aliyehukumiwa miaka kumi, Sajini Lucas miaka kumi,
Kapteni Kamaka Mashiambi miaka kumi, Kapteni Benito Manlenga miaka kumi, Private
Dominicus Said miaka kumi, Kapteni Andrea Dickson miaka mitano, Private Hamidus miaka
mitano na Roger Mwanaloya miaka mitano.
********************
PART 2
JARIBIO LA PILI/UHAINI WA KWANZA(Bibi Titi,Kambona and co.)
Ilifikia hatua Mwalimu Nyerere alijiamini na kuweza kutoa kauli hii mwaka 1966 “I have
been one of the luckiest presidents in Africa.My colleagues are very loyal to me"
Mwalimu hakujua kama Upepo ulikuwa unaenda kubadirika kipindi cha miaka miwili tu
mbeleni.
Katika miaka hii miwili mbeleni,wengi wa waliokuwa kwenye baraza lake la mawaziri
walikuwa wamewekwa Vizuinini na zaidi ya yote,rafiki yake Mkubwa alikuwa amekimbilia
uhamishoni.
Inasemekana OSCAR KAMBONA ambaye ndiye alitajwa kama muhusika mkuu wa mpango
huu,alikuwa akiendesha harakati za kutaka kumpindua Mwalimu Nyerere akiwa huko huko
uamishoni Uingereza.
KAMBONA alinukuliwa na chombo kimoja cha habari akidai kuwa Rafiki yake wa
zamani(Nyerere) ameanza kuwa dictator.
Hivyo kambona akatajwa kuwa alikuwa akituma kiasi kikubwa sana cha pesa kwa watu
wanaomuunga mkono nchini Tanzania ili ziweze kusaidia katika nia yao ya kumng'oa
Nyerere madarakani.
Mipango yao ilifikia kilele kati ya tarehe 10 hadi 15 October 1969 ambapo waliendesha
vikao vyao mfululizo wakati Mwalimu Nyerere akiwa ameambatana na wasaidizi wake
wengi nje ya nchi akiwemo Major General wa JWTZ SAM SARAKIKYA.
Aliyelipua mipango hii sio mwingine,bali ni POTLAKO LEBALLO ambaye walimuingiza
kwenye mpango wao bila kujua kama jamaa alikuwa akiwachota baada ya kumwamini
na yeye akawa anatoa taarifa hizo kwa Usalama wa taifa.
Issue Ilianza Kubumbuluka Jijini Nairobi nchini Kenya ambapo POTLAKO LEBALLO alikutana
na GRAY MATTAKA ambaye alimwambia ana ujumbe wake kutoka kwa KAMBONA
aliyemtaka awaunge mkono kwenye Mpango wao wa mapinduzi. MATTAKA alimuhakikishia
POTLAKO kuwa watu wengi tu walio kwenye serikali ya Nyerere walikuwa nyuma ya
Mpango huo.
Watu wa Usalama walianza kwanza kwa kumkamata GRAY MATTAKA aliyekuwa Jijini
Nairobi.
POTLAKO alipoenda kukutana tena na KAMBONA Uingereza,KAMBONA akamwambia
wameamua kuachana na mpango huo baada ya GRAY MATTAKA kukamatwa. Kambona
hakujua kama alikuwa amekaa meza moja na mtu aliyekuwa akimuuza.
Baada ya hapo,Huku Tanzania,Watu walikuja kushangaa tu Mwezi October 1969 wahusika
wa mipango hiyo wanakamatwa.
Yalipotajwa majina ya wahusika watu walipigwa na butwaa hasa waliposikia jina la BIBI TITI
MOHAMED. Pia Wale kina ELIYA CHIPAKA na JOHN CHIPAKA watu walikuja kujua baadae
kuwa walikuwa ni Wapwa wa OSCAR KAMBONA.
Baada ya Kesi kuendeshwa kwa jumla ya siku 127, GRAY MATTAKA,ELIA CHIPAKA,JOHN
CHIPAKA na BIBI TITI MOHAMED walihukumiwa kifungo cha maisha.
Pia MICHAEL KAMALIZA na WILLIAM CHACHA walihukumiwa kifungo cha miaka 10
Kwa Upande wake ALFRED MILINGA aliachiliwa huru baada ya kutokutwa na hatia
akapokewa kwa furaha na ndugu zake baada ya kuwa Kizuizini kwa miezi zaidi ya 16 wakati
kesi hii ikiendelea.
Hata hivyo,Jaji katika kesi hii aliilaumu serikali kwa Kutunga sheria hiyo ya Kizuizi na kisha
ikapitishwa na Bunge kwani iliweza kumweka mtu kizuizini bila kumfikisha mahakamani kwa
hisia tu kuwa mtu anahatarisha usalama wa nchi.
OSCAR KAMBONA hakuhukumiwa kwa kuwa hakuwepo mahakamani hivyo hakujitetea .
Miaka saba baadae BIBI TITI aliachiwa kwa msamaha wa rais akiwa katika gereza la Isanga
dodoma. Inasemekana ni baada ya kumwandikia barua Nyerere ya kuomba msamaha
ambayo haikujibiwa.
Pia mwaka 1978 ndugu wa OSCAR KAMBONA waliokuwa wamewekwa kizuizini nao
Waliachiwa pamoja na wengine 22 waliokuwa kizuizini. Pia siku hiyo waliachiwa huru
Wote hawa waliachiwa huru katika maadhimisho ya kwanza ya kuzaliwa kwa CCM na miaka
hawakuhukumiwa, bali walikuwa wamewekwa kizuizini ambako walikaa kwa miaka 10 tangu
Desemba 1967 kwa sababu walikuwa wakimuunga mkono kaka yao, Oscar Kambona, na
Gazeti hilo lilikuwa likichapisha pia makala zilizoandikwa na Oscar Kambona akiwa
Aliendelea kukaa nchini Uingereza hadi aliporejea nchini kwa hiari yake mwenyewe mwaka
1992 ulipoanzishwa mfumo wa vyama vingi.
MWISHO WA PART 2
*********************
PART 3
1.Yassin Membar(21),
2.Mohammed Tahir(21),
3.Abdallah Ali Abdallah(22),
4.Mohammed Ally Abdallah(26)
na kiongozi wao
5.Musa Membar(26)
MWISHO
Wakiwa Wanaendelea na
manung'uniko huku wakiandaa
"mchoro" wa kumpiga "spana" Baba
mkuu, ndipo wakakutana na PIUS
MUTAKUBWA LUGANGIRA
ambaye alikuwa ni mfanya biashara
mkubwa mwenye asili ya kitanzania
nchini Kenya.
CHARLES KIZIGHA
akamuunganisha na Mkurugenzi wa
Usalama wa Taifa AUGUSTINE
MAHIGA