Professional Documents
Culture Documents
Katika kipindi chake cha utawala wa eneo la ufipa, chifu Mwene Kiatu
hakujaliwa kupata watoto na alipokufa, milki ilichukuliwa na dada yake,
Mwene Ngalu ambaye ndiye mwanzilishi wa Sumbawanga.
Hata hivyo Chifu Mwene Ngalu alijaliwa kupata watoto saba ambao
wote aliwazalia katika nyumba yake ya utawala iliyojengwa kwa kipindi
cha miaka miwili katika mwaka 1918 hadi 1920 chini ya usimamizi wa
Mabruda wa dhehebu la Roma yaani wakatoliki ambao walikuwa
Wajerumani.
Nyumba hiyo hivi sasa imebomoka na limebaki gofu ambalo kwa nje
kuna sehemu ya makaburi yanayotumika kuzika kizazi cha utawala
huo, na jambo la ajabu kwenye gofu hilo wapo nyuki waliojenga
kwenye pango na wapo kwa muda mrefu tangu kipindi cha uhai wa
baadhi ya watawala wa kizazi hicho.
Katika kipindi cha utawala wake, Chifu Kapufi wa Tatu, alijaliwa kupata
watoto watatu ambako mkewe wa kwanza alijaliwa kupata mtoto
mmoja wa kike aliyeitwa Ntalu na mke mdogo alijaliwa kupata watoto
wawili wa kiume ambao ni Oscar na Apolinary. Hata hivyo baada ya
kifo cha Kapufi wa Tatu, hivi sasa ukoo huo wa kichifu uko kwenye
mchakato wa kutafiti mrithi wa kiti hicho.
Kwa kijiji cha Milanzi baadhi ya wakazi wake hutumia mapango yaliyo
kwenye mlima uitwao Itwelele kwa kufanya matambiko na mambo
mengine ya kishirikina kwa imani kuwa mizimu iliyopo huko huwasaidia
kutekeleza mahitaji yao na kumdhuru mtu au watu waliotenda makosa
na kuyakana.