Professional Documents
Culture Documents
Mwanamke ajitoa kufa akishikilia bendera Amwambia polisi ina jina la Allah nakufa nayo Aumizwa jicho, mguu anyimwa matibabu
Ushauri kwa Ndalichako, Serikali Kuchoma kichaka cha wahujumu Vinginevyo ni kudumisha dhulma
miezi miwili baada ya walimu kusahihisha? Katika usahihishaji, wanakuwepo walimu wengi na kunakuwepo na uwazi na uhakiki. Katika hali hii ya watu wachache kujifungia mahali kwa siri, kutakuwa na uhakika gani kwamba majibu wanayokuja kutoka ndio yale yale yanayotokana na makisi walizotoa wasahihishaji? (Soma Uk. 2)
Jussa atoa darsa Yametimia. Askofu hatawanunia tena Polisi: Waislamu washushiwa kipigo kikali muhimu Barazani
Mwadini Suleiman Juma alipigwa na polisi katika eneo la Mahonda Mkoa wa Kaskazini Unguja kabla ya kuka Donge kulikoandaliwa mkutano.
KUMKABIDHI mtu mmoja au kikundi cha watu matokeo yote ya nchi nzima kwenda kukaa nayo kwa muda mrefu bila kuyatangaza, ndio chanzo cha hujuma. Kwa nini matokeo hayatangazwi pale pale yanapomalizika kufanyiwa kazi? Baraza linafanya nini na matokeo kwa zaidi ya
Msikiti wavurumishiwa mabomu, wavunjwa vioo Wanawake wavuliwa shungi, wapigwa mabuti Watu Donge wataka kutolewa kifungoni Misri
TAHARIRI/HABARI
uliopo kama ambavyo wana haki hiyo Watanganyika (Tanzania Bara). Ni kweli pia kuwa wananchi wa Zanzibar wana haki kutaka uhuru wa nchi yao na Dola yao yenye mamlaka kamili ndani ya Muungano. Kwamba Muungano uwe wa nchi mbili kila moja yenye uhuru na mamlaka yake (sovereignty) kamili ndio pawe na ushirikiano unaotowa haki sawa kwa nchi zote mbili. Hata hivyo, tunachosema ni kuwa pamoja na uhuru na haki hiyo, Wazanzibari watambue kuwa mfumo wa serikali mbili uliopo haunganganiwi kwa bahati mbaya tu au sio kwamba una masilahi makubwa ya kisiasa na kiuchumi kwa Zanzibar. Unanganganiwa kwa sababu ndio unaotakiwa na mfumokristo. Wakishatambua hilo, watambue pia nguvu ya mfumo huo. Zanzibar ina Rais wake ambaye huchaguliwa na wananchi wa Zanzibar na huapishwa kuwa ni Rais wa nchi inayoitwa Zanzibar. Lakini Rais huyo huyo wa nchi, huingia katika Baraza la Mawaziri la Tanzania akivaa gwanda la Mawaziri. Hata hivyo, serikali ya Zanzibar, Wazanzibari na Rais anayekuwa madarakani, hahisi tatizo. Anakula kiapo na kuhudhuria vikao. Sisi hatudhani anafanya hivyo kwa kuridhia. Anaangalia nguvu iliyompitisha kule Dodoma kugombea Urais na ikamsimamia hadi kuapishwa. Hiyo ndiyo nguvu na athari ya mfumo ulioshikilia Muungano huu. Labda tutaje mfano mwingine ulio wazi zaidi. Katika suala la OIC ambalo Mheshimiwa Mwakilishi Raza alilikumbusha Barazani hivi karibuni. Waziri wa
AN-NUUR
Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa Mheshimiwa Benard Membe alishalitolea ufafanuzi Bungeni Dodoma kuwa halina tatizo. Kwamba baada ya serikali kulifanyia utati ilikuwa tayari kujiunga kwa sababu ya faida zake na kwamba halina tatizo lolote. Lakini mara tu baada ya kutoa msimamo huo rasmi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Mheshimiwa aliitwa na Askofu wake Mkuu wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kadinali Pengo na kuambiwa marufuku OIC. Sasa ukitaka kugombana na Mheshimiwa Membe, mkumbushie juu ya ule msimamo wa serikali kwamba haina tatizo kujiunga na OIC! Hiyo ndiyo nguvu ya mfumokristo ulioshikilia Muungano huu ambao Uamsho (na Wazanzibari wengine) wanasema hawautaki.
S.L.P. 55105, Simu: Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110148, 0755 260 087, DSM. www.ipctz.org E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam
AN-NUUR
MAONI YETU
KWA mara ya kwanza nilipatwa na mshangao mkubwa kusikia kuwa ati mitihani ya wanafunzi wa shule za Kiislamu na pia za serikali na watu binafsi waliofanya mtihani wa Maarifa ya Uislamu (Islamic Knowledge) takriban wote w a k i w a n i Wa i s l a m u imekosewa. Habari hizi zilinijia wakati nikiwa siamini kuwa madai ya Wakuu wa Shule za Kiislamu kuwa wanapinga matokeo yale ni ya kweli. Imekuwa muda mrefu Wa i s l a m u w a m e k u w a wakilalamika nchi nzima kuwa wamekuwa wakinyimwa haki sawa za elimu na ajira hasa serikalini na kwenye mashirika yake. Kwa hiyo kutokana na ukweli huo, inajenga taswira ya kuamini baadhi ya malalamiko hata kama hayana uhusiano wa karibu. Imenitisha zaidi kusikia kuwa kilichotokea ni kosa la Asa anayeingiza hesabu hizo kwenye Komputa au tuseme mtu anayehusika na IT- (Information Technology) kugawanya matokeo kwa tatu badala ya mbili. Na baada ya hapo kilichofanyika ni kutoa majibu mengine
AN-NUUR
HABARI
GARI alilokuwemo Sheikh Farid Had likiwa na matundu ya risasi. na ndipo Masheikh hao walipoingia Msikitini. Taarifa kutoka eneo la tukio zinafahamisha kuwa polisi waliwafuata huko huko Msikitini kuwatawanya kwa mabomu ambapo Sheikh Farid na wenzake waliruka ukuta na kukimbia kwa miguu katika pori kutoka Mahonda kuelekea njia ya Mwangapwani. Huku nyuma, wakidhani Sheikh Farid yupo ndani ya gari alilokuja nalo, watu wasiofahamika walilifukuza gari hilo na kulipiga risasi ambapo lilipinduka na kuharibikia vibaya. Sijui kama walitaka kutuuwa au vipi, lakini bahati mimi sikuwemo katika ile gari ingawa wanadhani kwamba ile gari ni yangu, lakini niseme mimi ile gari sio yangu ila nilipewa kwa kutumia kwa ajili ya shughuli za kuendeleza hizi harakati zetu, alisema Sheikh Farid muda mfupi baada ya kurudi katika hekaheka hizo ambapo walifanya mhadhara wao Mbuyuni baada ya kutokufanikiwa kupenya kwenda Donge. Akielezea juu ya kilichomfika Bi Riziki anasema kuwa kwa vile alikuwa kashikilia bendera, ilikuwa rahisi kwake kufuatwa na polisi. Mimi nilikuwa nimekamata bendera yangu polisi alipokuja kunichukua akanikamata mkono ananipeleka kituoni alipoka mbele kuna polisi mwenzake akawambia unampeleka kituo kama Bi Harusi, mpige virungu, yule polisi akajibu kwa nini tumpige wakati amekubali kutii amri halali? Mwenzake akasema, haiwezekani hao hawana adabu lazima apigwe, yeye ndio akaanza kunipiga huku akinambia nimpe bendera yangu ya Uamsho mimi nikamwambia nipige lakini bedera yangu sikupi ndio akaendelea kunipiga na kunipiga, alisema Bi Riziki. Wakawa wanatuambia maneno ya ovyo kwamba tutakoma, kwa hivyo yule polisi mmoja akawa anaendelea kunipiga alipokuja polisi mwenzake akawambia unampigia nini huyo wakati yeye amekubali umpeleke kituoni ndipo waliponichukua na kunipiga tena. Riziki ambaye aliumia sehemu ya jicho baada ya kupigwa kibao na jicho lote kupiga wekundu, anasema kilichomshangaza ni kwamba kila kituo cha polisi alipokwenda alikataliwa kupewa barua ya kwenda kupata matibabu. Tunafanywa kama sio raia wa nchi hii tulipokwenda kituo walikataa kutupa barua wakati wanajua hatuwezi kutibiwa kama tumeumia mpaka tupate barua ya polisi, tulipotoka Mahonda tukaja mjini tulikwenda Kituo cha Polisi Mkunazini wakakataa kutupa kibali tukenda Malindi pia wakatwambia nyinyi nendeni tu huko huko hospitali wambieni madaktari kuwa mmepigwa na polisi hawakutupa. Bi Riziki ambaye aliumia mkono na jicho anasema hata walipokwenda hospitali walikataliwa kupewa tiba hadi watakapokwenda na barua ya polisi. Naye Hafsa Mohammed Mahfoudh (19) mkaazi wa Kinuni, Magogoni anasema katika zahma hizo watu wengi walikimbilia Msikitini na ndipo walipoona Polisi wakiingia Msikitini na kuwapiga wanawake na wanaume na kuwatoa nje huku wakitaka wanawake wote wavuliwe mashungi yao. Walikuwa wakisema maneno mabaya mabaya huku wakituvuta mashungi yetu wakitwambia tokeni hapa Waislamu, Waislamu, Waislamu nini, wanafiki wakubwa, na kuna askari wa kike alinivuta sana shungi na kunipiga sana kwa
Inaendelea Uk. 7
MAKALA
AN-NUUR
Inatoka Uk. 4
makosa ya daraja hiyo, nilipata maelezo kutoka kwa mtu mmoja wa Baraza na pia haswa kutoka kwa Mwalimu ambaye miaka mingi amehusika na usahihishaji wa mitihani ya sekondari nchini. Kutokana na maelezo yake ya kina, mitihani husahihishwa kwa makini sana kwani huhusisha waalim takriban 400 na zaidi na kila mmoja anasahihisha swali moja la mtihani wa somo analohusika. Baada ya hapo kuna mkaguzi anayepitia swali hilo na kuhakikisha kuwa mwalimu huyo amesahihisha vizuri na kuweka maksi husika kikamilifu. Baada ya kila mwalimu kusahihisha swali lake na kuweka alama ya maksi na kupitiwa na wakaguzi wote, anachukua mwalimu teule kujumlisha alama zote na kuweka jumla ya alama zote za mwanafunzi. Zoezi hili hupitiwa na waalim wakaguzi wengine wawili kuthibitisha kuwa mweka alama huyo hakufanya makosa na kama yapo hurekebishwa mara moja. Matokeo yote ya alama za kila mwanafunzi yanakusanywa pamoja na waalimu wawili wateule na kuyaweka pamoja kwa orodha ya watahiniwa wote kulingana na mitihani yao iwe ni mmoja miwili au zaidi. Kazi hii ya kuweka pamoja matokeo hayo hukaguliwa
ISMAIL Jussa ametaka irudi Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, kisha ndio uundwe muungano wa kimkataba. Jussa ameyasema hayo jana Barazani akichangia Hotuba ya Bajeti ya Makamo wa Pili wa Rais, Zanzibar. Mwakilishi huyo wa Jimbo la Mji Mkongwe, alikuwa kama anatoa darsa kwa Wawakilishi ambapo alitumia muda
kimkataba. Akasema, kinachotakiwa ni kuwa na Tanganyika, Zanzibar, zote zikiwa nchi huru zenye mamlaka yake kamili ya kidola, kisha nchi na serikali hizo mbili ziangalie namna ya kushirikiana kimkataba. Hali Bungeni ilikuwa kama Jussa ndio katoa kauli ya siku iliyoakisi hisia na matakwa ya Wa w a k i l i s h i w e n g i kwa jinsi walivyopokea uchambuzi na maoni yake.
(Haya ni maoni yangu, mwananchi, msamaria mwema wa nchi hii nzuri Tanzania)
AN-NUUR
Makala
TANZANIA imeamua kuandika upya katiba yake. Mchakato huu wa Katiba na suala la muungano umeanza kwa kupitishwa sheria n o 8 / 2 0 1 1 . Ta y a r i mwanzo mbaya (falsestart) imeonekana katika mchakato unaoundwa na sheria hiyo. Kasoro kubwa ya sheria hii ni kuwa HAITOI FURSA YA WAZI kwa wananchi (wamiliki na wadhamini wa Katiba) kuujadili muungano na ukweli ni kuwa muungano ni nguzo kuu ya katiba yenyewe. Hasa kwa upande wa Zanzibar, ambako wananchi wa Zanzibar uhusiano wao juu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kupitia muungano. Yote yaliyo nje ya mambo ya muungano, upande wa Zanzibar hawana haki nayo kama ambavyo Watanzania bara hawana haki na mambo ya Zanzibar (yasiyokuwa ya muungano). Ukisoma vifungu vya 8, 9 na 17 vya sheria hiyo ambavyo vimeainisha hadidu rejea (terms of reference) au mipaka (na kuna umuhimu gani wa kuwekea wananchi mipaka kuhusiana na mjadala wa Katiba yao?) ya kazi za tume ya katiba hamna hadidu rejea yo yote inayaotaja kuangalia suala la muungano. Na baya zaidi vifungu vya 9(1) (C) na 17(1) na 17(2)(d) vimeielekeza tume kutayarisha na kuwasilisha ripoti kwa kuzingatia hadidu za rejea hivyo ni kuwa
HATA kama wananchi watazungumza sana juu ya suala la muungano, lakini kwa mujibu wa sheria hii, Tume haitoandika cho chote kuhusu mambo haya ya muungano. Tukizingatia ukweli wa kuwa wananchi wa nchi mbili hizi hawajawahi kupata fursa ya kutoa maoni yao juu ya suala la muungano, ilitegemewa muungano uwe ndio hoja kuu ya mjadala wa katiba na kuacha kabisa kuendeleza utamaduni wa muda mrefu wa kulitenga suala la muungano na wananchi wenyewe kulifanya halifikiki, halijadiliki wala haligusiki. Ni busara tusome alama za nyakati. Jambo jengine ni kuwa tatizo lililojitokeza mwaka 1977 kuhusu kukosekanwa kwa uwiano wa wajumbe katika kuunda Bunge la Katiba la wakati ule, linajikoteza tena mwaka 2012 katika kosa hilo hilo la kukosekanwa uwiano wa kuunda Bunge la Katiba la sasa. Yaani hatukujifunza hata baada ya miaka karibu 35 au ndio muendelezo wa ile dhana ya kuwa lengo la Muungano ni nchi moja (Tanganyika) kuitawala nchi nyengine (Zanzibar)? Bunge la Katiba la 1977 lilikuwa na wajumbe 207: ambapo wajumbe 45 tu walitoka Zanzibar na wajumbe 162 walitoka
Tanganyika. Na Bunge la Katiba la sasa kwa mujibu wa Sheria nambari 8 ya 2011 ya mchakato wa marekebisho ya Katiba linaeleza kuwa; kutakuwa na wajumbe takriban 600 wa Bunge la Katiba: ambapo wajumbe kutoka Zanzibar watakuwa kama 200, na wajumbe kutoka Tanganyika watakuwa kama 400. SUALA la kujiuliza: Mbona tunapoingia katika ushirikiano wa kimataifa na nchi nyengine, principle ya equality of membership inafuatwa na kuheshimiwa? Kwa mfano Bunge la Afrika Mashariki lenye nchi wanachama: Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi: kila nchi wanachama imepeleka wajumbe tisa (9) tu katika Bunge la Katiba la Jumuia hii. Haikusemwa kwamba Tanzania kwa sababu tuko wengi kwa idadi ya watu milioni 43 hivyo inabidi tupeleke wajumbe wengi zaidi kulinganisha na Rwanda yenye watu milioni nane? Nchi zote hizo zilipeleka wajumbe tisa bila ya kujali wingi wa idadi ya watu wake au ukubwa wa eneo kwa sababu si demograpy wala geography zinazotumika katika kuzingatia vipimo vya mamlaka (sovereignity) ya nchi. Sasa kwa nini Bunge la Katiba la Tanzania liwe
na wajumbe wachache kutoka Zanzibar; lakini liwe na wajumbe wengi k u t o k a Ta n g a n y i k a ? Mbona Tanzania hiyo hiyo inaifuata principle ya usawa wa uwiano ikiwa nje ya nchi (kimataifa) lakini kwa makusudi inaipuuza ikiwa ndani ya nchi? Tatizo kubwa jengine ambalo linajirudia kama ilivyotokea mwaka 1977: lile Bunge la Katiba la 1977 na hili la sasa kwa mujibu wa sheria nambari 8: YOTE mawili ni mabunge ya kuteuliwa si Mabunge ya kuchaguliwa. Kwa nini Mabunge haya yasichaguliwe na wananchi wenyewe na badala yake Rais ayateue? Je, yataweza ku - reflect wishes za wananchi? Wa s h i r i k i w a k u u wa mchakato huo wa marekebisho ya Katiba ni WANANCHI ambapo mamlaka ya kuendesha nchi yanatokana na wananchi wenyewe. Universal declaration of human rights inasema hivyo. Hiyo Katiba ya Muungano ya 1977 nayo inasema vivyo hivyo. Na Katiba ya Zanzibar ya 1984, Toleo la 2010 nayo inalitambua hilo pia. Ibara ya tisa inaeleza kuwa uwezo, nguvu na mamlaka yote ya kuendesha nchi yatatoka kwa wananchi wenyewe na si kwengineko. Kama
hivyo ndivyo, iweje Tume ya Katiba iweke hadidu rejea (terms of references) ambayo maana yake ni MIPAKA? Unawawekeaje mipaka wananchi ambao sio tu ndio wamiliki wa Katiba; bali ndio walio na MAMLAKA na HAKI kuhusiana na mustakbal wa taifa lao kama ibara ya 21 (2) ya Katiba ya Zanzibar inavyoeleza? Sheria nambari 8 ya 2011 ya marekebisho ya Katiba haiwezi KUWA JUU YA Katiba ya Zanzibar. Wanaoutetea Muungano kwa madai kuwa ni mzuri na hauna matatizo na kwamba tuendelee nao kama tulivyo - wanaonekana sio tu ni wahafidhina wasiojua mambo (political naives); bali hawajui hata kusoma alama za nyakati na mahitaji na kwamba wanaonekana ni politicians with NO politics. Essence ya marekebisho ya Katiba ya Muungano maana yake nn? Maana ya marekebisho ni kuwa kuna mapungufu na kasoro. Kitu kikiwa kizuri hakihitaji marekebisho. Ila, Muungano una kasoro na kero nyingi ambazo wao wenyewe wamekiri kushindwa kuzipatia ufumbuzi. Kwa wengine, Muungano umekuwa ndio kero yenyewe kutokana na kuonekanwa una dhamira ya nchi mmoja kuitawala nchi nyengine. Kwa mfano, ibara ya 55 (1) ya Katiba ya Muungano inasomeka: Mawaziri wote ambao ni wajumbe wa Baraza la Mawaziri kwa mujibu wa ibara ya 54, watateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Waziri Mkuu. Sasa tujiulize, nani Rais na nani Waziri Mkuu? Rais ni Kikwete, Waziri Mkuu ni Pinda iko wapi Zanzibar hapo? Eti hiyo ndiyo cabinet inayoamua sera za mambo ya Muungano huu. Kwa nini ibara isiseme kuwa Rais atateua Mawaziri baada ya kushauriana na Makamo wa Rais ambayo ndiyo formula katika Katiba isemayo kwamba - Rais akitoka upande mmoja wa Muungano, Makamu wa Rais anatoka Inaendelea Uk. 8
HABARI
AN-NUUR
MOSHI na moto uliotanda eneo la Donge baada ya polisi kurusha mabomu ya moshi. unyama na uhalifu wa hali ya juu kwa kuunajisi Msikiti wa Ijumaa wa Mahonda kwa kuwahujumu raia wasio na silaha ndani ya Msikiti kwa kuwarushia mabomu ya machozi yasiojulikana idadi yake ambapo hadi hii leo Msikiti huo hausaliki ndani kutokana na harufu kali ya mabomu. Pia askari hao walipiga risasi pamoja na kuingia ndani ya Msikiti na viatu na kuvunja kwa makusudi vyombo ikiwa ni pamoja na Vespa, Pikipiki na Baskeli vilivyoegeshwa eneo la Msikiti huo wa Ijumaa pamoja na kuiba viatu vya waumini kwa kunyanganyiana. Imesema sehemu ya Tamko la Uamsho. Maelezo ya wananchi waliokuwa katika eneo la tukio wanasema kuwa ilikuwa kama wakati ule wa Janjawed maana Polisi walikuwa wakitolea hasira zao mpaka kwenye vyombo vilivyoegeshwa nje ya Msikiti na majumbani mwa watu. Jambo la kushtusha zaidi ni kitendo cha kuwadhililisha wanawake na kufikia hadi kuwakashifu kwa kuwachania nguo zao na kuwavua mashungi yao pia hata watoto wadogo mitaani wako walopata kipigo, kitendo cha kuwatimba wanawake kwa viatu bila ya huruma na kuwapiga marungu na kuwajeruhi vibaya sehemu za usoni na mwilini kwa ujumla, huo wote ni unyama na ukiukwaji wa haki za binaadamu. Imesema taarifa ya Uamsho. Awali mara tu baada ya kutokea vurugu ambapo baadhi ya makanisa yalichomwa, Askofu Mokiwa alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa anataka kuona watuhumiwa (Uamsho)
wakikamatwa wapigwe bakora na polisi na baadaye wakishwe kwenye vyombo vya sheria. (Nipashe, Mei 31 2012) Lakini kabla ya hapo alisema pia kuwa hajaridhika na utendaji wa Polisi kwa sababu hajaona kasi yao kwa vitendo wakiwashughulikia Uamsho. Kwa kukujua nguvu ya mfumokristo na kwa kuzingatia uzoefu wa kadhia ya mauwaji ya Mwembechai, gazeti hili katika toleo lake namba 1015 la Juni 1-7, 2012 lilielezea wasiwasi wake kuwa huenda Polisi Zanzibar wakafanya hujuma kubwa kwa Waislamu ili kuitikia na kutekeleza matakwa na shinikizo la Kanisa. Naam, yametimia. Uamsho, Waislamu na waumini ndani ya Msikiti wa Mahonda, wamepigwa bakora kabla ya kuhukumiwa kama alivyotaka Askofu Vallentino Mokiwa. Baada ya bakora hizo, sasa waliokamatwa ndio watakishwa mahakamani. Kwa upande mwingine, Kule Donge nako, Waislamu waliokuwa wamekusanyika katika Msikiti ulipokuwa ufanyike mkutano, hawakunusika. Walipa mgao wao wa kipigo. Walivamiwa na kupigwa sana. Ilipofikia wakati wa Laasiri Jeshi la Polisi walianza kupiga mabomu ndani ya Msikiti wa Donge Pwani pamoja na kuuhujumu Msikiti na waumini wakiwa wanaswali na kuvunja vioo vya msikiti huo. Inasema taarifa moja. Kwa mujibu wa maelezo ya wananchi walioongea na mwandishi, Polisi walikuwa na hasira na kisirani ambacho hakijulikani sababu yake ilikuwa nini. Wakifafanua walisema kuwa walishangaa kuona baadhi ya polisi wakiharibu vyombo ya usafiri vya waumini waliokuwa ndani ya Msikiti. Japo taarifa ya Polisi inasema kuwa hakuna mtu aliyejeruhiwa, lakini mwandishi ameshuhudia na kuongea na watu kadhaa wenye majeraha yaliyotokana na virungu au mabomu ya machozi. Mmoja wa majeruhi Mzee Kassim Sheha aliyepigwa wakati akiswali swala ya Laasir na kujeruhiwa vibaya miguuni kwa mlipuko wa bomu la machozi akiwa ndani ya swala. Inaendelea Uk. 7
AN-NUUR
HABARI
zao Wazanzibari? Jambo hilo limegusiwa pia katika Tamko la Uamsho lililotolewa tarehe 19 Jun, 2012 ambalo pamoja na mambo mengine limesema kuwa: Wananchi wa Donge wanaomba ufafanuzi kutoka Baraza la Wawakilishi kwani kwa miaka yote wanajiona kuwa wanabaguliwa wakati wananchi wenzao wa Mashamba yote mengine katika wilaya tofauti wakipata haki kikamilifu, jee wao si Wazanzibari? Ni dhambi gani waliyotenda hata wakabaguliwa kiasi hicho? Au Donge ni nchi
yenye mfalme kama wafalme wa ki-Misri wakijulikana kwa jina la Firauni? (Soma Tahariri Uk. 2)
Mwanamke wa Kiiaslamu aliyekuwa akishikilia bendera ya Uamsho yenye maandishi Laaila ha ilallah, aLIshushiwa .
MAKALA
AN-NUUR
upande mwengine? Halafu wahadhina hawa watuambie tusiuzungumze Muungano huu uliojaa viini macho!? (To them politics is just a business; not a mission) ! Vil vile, Sheria nambari 8 ya 2011 ya marekebisho ya Katiba imeweka suala la makosa na adhabu. Sheria ime creates makosa ya jinai kupitia kifungu cha 21 cha sheria ile. Makosa yenyewe ni pamoja na kuzuia Tume isifanye kazi ambapo kufanya hivyo ni kosa la jinai na utashitakiwa. Kuchochea mtu yo yote kuzuia Tume isifanye kazi zake au sekretarieti au mjumbe wa Tume asifanye kazi zake pia ni kosa la jinai na utashitakiwa chini ya kifungu hicho cha 21. Kubwa zaidi, yo yote anaetaka kufanya mikutano au makongamano nk yenye lengo la kuelimisha umma (public awareness programme) - kwa mujibu wa sheria hiyo analazimika afuate taratibu za sheria hiyo zinavyotaka. Hapo maana yake nini? Maana yake ni kuwa; sheria nambari 8 ya 2011 ya marekebisho ya Katiba inakana na kunyima haki ya wananchi ya Kikatiba ya kutoa maoni yao kwa uhuru kwa kuwalazimisha wafuate taratibu za sheria hiyo. Baada ya kuyaona hayo, ukweli ni kuwa sio tu kuwa suala la muungano liwe ni msingi katika mjadala wa katiba; lakini suala la muungano lilistahiki kuamuliwa mwanzo na ndiyo baadae lije suala la katiba. Vipi tusiuzungumze Muungano ambao ndio uliozaa Katiba? Tuliungana kwanza kabla ya kuwa na Katiba. Muungano ndio uliozaa katiba tulizonazo, katiba zote mbili (ya Zanzibar 1984 na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977) ni matokeo ya muundo wa muungano huu. Muundo ambao uliunda mamlaka tatu (three Jurisdictions): ya Tanganyika, ya Zanzibar, na ya Muungano na baada ya hapo mamlaka mbili za Tanganyika na ya Muungano
zikachanganywa (fused) na kuwa chini ya serikali moja na mamlaka ya Zanzibar kuwa chini ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Hivyo pakawa na Serikali mbili na katiba mbili. Na huu ndio msingi unaowafanya wengi (Aboud Jumbe, 1994 & Dourado, 1999 nk) wakasisitiza kuwa mkataba wa muungano ulikusudia mamlaka 3 na serikali 3 na ule utaratibu wa mamlaka 3 chini ya serikali 2 na hivyo katiba mbili ulikuwa ni wa muda wa mwaka mmoja tu mpaka utapoundwa mfumo wa katiba mpya ndani ya mwaka mmoja kuanzia siku uliposainiwa mkataba wa muungano. Mkataba wa Muungano unataja kipindi hicho kuwa ni interim period Angalia kifungu (iii) cha Mkataba wa Muungano: During the interim period, the Constitution of United Republic shall be the constitution of Tanganyika so modied as to provide for . Mkataba ulielekeza kuundwa kwa tume ya katiba (kifungu vii) ambayo ingeundwa kwa makubaliano kamili ya Marais wawili wa nchi zilizoungana. La kushangaza ni kuwa hilo lilikwepwa kabisa, tena kwa amri ya upande mmoja tu (Tanganyika chini ya Nyerere) alipoamua kivyake - vyake tu (uniletarally) kupitisha sheria (Act no 18 of 1965) na kuliakhirisha hilo kwa muda usiojulikana mpaka hapo lilipoibuka tena miaka 14 baadae kwa kuunda katiba ya 1977 wakati huo ikiwa ni sawa na kuvuta shuka wakati kumeshakucha kwani mkataba wenyewe ulishajeruhiwa vya kutosha. Sheria hii ndio iliyovuruga kabisa Mkataba wa Muungano na ikafungua milango kwa upande mmoja wa Muungano kuamua watakalo. K. Sasa tujiulize endapo Wa z a n z i b a r i a m b a o wataamua, katika maoni yao, kuwa hawataki muungano na kwamba muungano kwao ndio kero yenyewe ni vipi bunge la katiba litakuwa na wajumbe kutoka Zanzibar? Inakuaje
leo wanaodai kuukataa Muungano waonekana maadui na hata ikie hadi kukamatwa na kupigwa mabomu? Huku si ni kwenda kinyume na Katiba ambazo zinaeleza kuwa mamlaka, uwezo na nguvu zote za Serikali zitatoka kwa wananchi? Na hata Nyerere mwenyewe wakati akiwa Uingereza, tarehe 20 April, 1968 alisema na maneno yake kunukuliwa ndani ya makala ya London Observer akisema: If the mass of the people of Zanzibar should, without external manipulation, and for some reason of their own, decide that the union was prejudicial to their existence, I Nyerere could not BOMB Zanzibaris into submission. The union would have ceased to exist when the consent of its constituent members was with drawn; yaani, Endapo umma wa Wazanzibari wataamua bila ya ushawishi kutoka nje kwa hoja zao wenyewe, wakaamua kukoma kwa Muungano, mimi Nyerere sitoweza kuwapiga mabomu. Muungano utasita pale tu utakapokosa ridhaa ya wananchi. Sasa kama hivyo ndivyo, iweje leo viongozi wa Serikali wawapige MABOMU wananchi halali kwa kuitumia haki yao hiyo Kikatiba na ya right to self - determination kuukataa Muungano uliowagharimu kila kilicho chao? Wanaodai kuwa wao ni watetezi wa Muungano wanadai kuwa tuudumishe Muungano ili kuwaenzi marehemu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume wakiwa ni waasisi wa Muungano huo. Suala: Vipi tuwaenzi marehemutena wawili kwa kuwadhulumu waliohai kwa mamilioni? Je, ni nani alie na maana na thamani zaidi kati ya marehemu na aliehai? Tuwaenzi kwa kuudumisha hata kama unatugharimu kila kilicho chetu? Muhimu si kuwaenzi marehemu; muhimu ni MASLAHI ya waliohai. (The damage is HERE; the damage is NOW).
Na kwa hakika Wazanzibari walio wengi kama ni kumuenzi Karume basi wanamuenzi sio tu kwa maneno matupu; bali wanamuenzi kwa vitendo kwa kuisimamia hoja yake kuwa Muungano ni sawa na kushona koti, ukiona linakubana, UNALIVUA,
hoja ambayo aliizungumza wakati bado Nyerere yuhai! Lakini na Watanganyika nao watamuenzi Nyerere kwa kuwaachia Wazanzibari wajiamulie walitakalo bila ya kuwapiga mabomu kama alivyoeleza Nyerere alipokuwa Uingereza 1968.
VIROBA MURUA
Kwa mahitaji ya viroba bora vipya kabisa kwa matumizi mbalimbali sasa unaweza kupata kwa bei ya jumla na rejareja kwa saizi zote kwa bei nafuu zaidi, kwa BANDO. Tupo mtaa wa Likoma na Pemba Kariakoo, Dar es Salaam (nyuma ya Msikiti wa Idrisa). Kwa mawasiliano zaidi wasiliana kwa simu: 0557 800999/0683 800999.
AN-NUUR
MAKALA
Na Ibrahim Mohammed Hussein MAMBO yanataka mipango. Jambo lolote lile linataka mipango. Inawezekana watu wakawa na nguvu, wakawa na mali na wakawa wengi na wakashinda kwa kishindo, lakini wakakosa mipango na hapo mambo yao yote yakaharibika. Tu l i j i n a s i b u t u l i f a n y a Mapinduzi yenye lengo la kuwakomboa Wazanzibari kutokana na hali mbaya ya maisha na kutaka kunyanyua uchumi wa visiwa hivi pamoja na kujiamulia mambo yao. Sio lengo la Mapinduzi kuwafukuza watawala wa Kiarabu ili Waafrika wa Bara watawale Visiwa hivi. Lakini kutokana na mipango na mikakati madhubuti ya majirani zetu ilioanzishwa tokea miaka ya sitini ya kutoiona Zanzibar kama ni nchi walifanya mipango ya kujishirikisha katika siasa za Zanzibar kwa malengo maalum. Ni wao waliopika Mapinduzi na kuyasaidia kwa hali na mali ili kuhakikisha mipango iliyopangwa kwa ustadi inatimia. Wakafanya juu chini kulipora Taifa la Zanzibar kupitia katika mtego wa Muungano, na kuanzia hapo Zanzibar ikawa iko chini ya Serikali moja yenye nguvu ya Muungano yenye kuongozwa na Serikali ya Tanganyika iliyosokomezwa ndani ya Muungano. Inabidi hivi sasa tutafakari na kujiuliza nani alihusika kuuwawa kwa watu kama Marehemu Othman Sharif. Marehemu huyu nae ni miongoni mwa Viongozi walioutumikia mpango maalum wa kupindua Zanzibar. Alipokuja shituka ndipo aliposema: Wa n a n c h i S e r i k a l i ishatwawa, ishakuwa Bara. Tunamnyanganya Muengereza, tunampa Songoro Hereza, kashampa Mjombawe Mali Jeza. Sasa ataka tuangamiza. Wapiii:- Hatamu zote za Uongozi ziko upande wa pili:1. Rais wa Jamhuri ya
10
MAKALA
AN-NUUR
Jengo la Kanisa ambalo lina ramani ya ukubwa wa kushinda Kanisa lolote katika Visiwa hivi. Mikusanyiko mikubwa inayoonekana hapo kila Jumapili kwa sasa inawajumuisha takriban watalii wote wa Ukanda wa Pwani ya Mashariki mwa Kisiwa cha Unguja, anzia Paje, Jambiani, Uroa, Chwaka, Matemwe, Pwani Mchangani, Pongwe, hadi Kiwengwa; wote hao hujumuika hapo, kunogesha wimbo wasioujua maana yake wa udumu Muungano. Kwa wimbo huo wananchi wametakiwa waendelee kuwa watulivu na watoto wao watakuwa wakipatiwa huduma ya maziwa na uji kila siku watakayohudhuria ndani ya kituo cha Maandalizi kiliopo Kanisani hapo, na yeyote atakayebisha huyo ataitwa UAMSHO na Adui Nambari Moja wa Muungano, hivyo ndivyo linavyotaka Kanisa. (Abu Hassan Ally Makame)
HAKUNA Muislamu, Mzanzibari, mwenye busara yeyote katika nchi ambaye haelewi kwamba Kanisa na wafuasi wake hawako radhi kuona Zanzibar ikiwa tulivu na yenye kutengamaa. Huenda huo ndio mwelekeo uliompelekea hata Raisi\ Mstaafu wa Awamu ya Tatu ya Uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Benjamin William Mkapa hata akashindwa kucha hisia zake juu ya shaka ya kuviwacha Visiwa hivi vikitanafasi. Msimamo huo ambao ni kama ufuasi wa njia ambayo ilishazoeleka kabla na baada ya Uhuru kwamba isifike wakati Zanzibar ikaishi kwa murua, kutokana na shaka iliyotawala nafsi za waliokereketwa na nuru ya neema ya Visiwa hivi, ulikuwa si mzaha katika hima ya kuimeza na ikibidi kuifutilia mbali jamii ya watu hawa wa Pwani ikibidi na vizazi vyao popote walipo Ulimwenguni. Kama inawezekana natamani kuvikunjakunja vijisiwa hivi na kuvitupilia mbali baharini kutokana na ..............., hiyo ni miongoni mwa dalili za mawingu ya hisia nzito za watawala waliopita dhidi ya visiwa vya Unguja na Pemba na watu wake. Haikuwa mzaha kwani ni muda mfupi wa Miongo isiyozidi Miwili ya Utawala wa Bw Mkapa pekee tuliposhuhudia Zanzibar ikigeuka ghaa kutoka safari ya kuelekea Dubai ndogo kibiashara hadi katika jangwa la idhilali lisilokuwa na hali wala mahali. Mpaka inakuja Serikali ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar, chini ya Uongozi wa akina Dr. Shein, Maalim Seif, na Balozi Idd, Biashara
yao. Mbona hakuna kelele kwamba msikiti hadi leo hausaliki, Waislamu wanaswali nje kutokana na harufu ya mabomu na damu iliyotapakaa, ya Waislamu waliopigwa mabomu na risasi ili kuridhisha mlingano wa ile vita ya panzi. Ni lipi ilitakalo Kanisa katika Visiwa hivi... Tafakari: Hebu funga safari mpaka Kijiji kimoja kinachoitwa
ASKOFU Mokiwa kutoka Zanzibar kwenda Bara, hali ambayo haikuwahi kujiri tangu asili ya Nchi hii, ilikuwa ni ya thamani ya Sh. bilioni 2 ukilinganisha na bilioni 60 kutoka Bara kwenda Zanzibar. Tunabaini kwa mujibu wa takwimu sahihi ndani ya takriban kipindi cha mwaka mmoja hali imekuwa ya kujiuliza wakati ambao maagizo ya kibiashara kutoka Bara kwenda Zanzibar yakisalia kwenye bilioni 60, kutoka Zanzibar kwenda Bara yameruka hadi bilioni 70 na kuwacha pengo si dogo; huku ndiko kupumua inakohitaji Zanzibar sasa. Hayo ni ya upande wa uchumi pekee, na mengi memgineyo yapo chini ya azma njema tokea pale watu wa Visiwa vya Unguja na Pemba walipokubali Maridhiano, chini ya Serikali ya sasa ya Umoja wa Kitaifa. Bila shaka hayo yameanza kupiga kengele ya tahadhari kwa Kanisa na kila asiyeitakia mema Nchi hii ya Waislamu, ambayo hayana ubishi yakisikika kwenye hadhara za siri na za dhahiri, kwamba hawa wasije wakaelewana hali itakuwa mbaya. Utashangaa sana visingizio vilivyopo mara vya Uamsho, mara vya Wapemba, na mara vya Waislamu kuchoma m ak an is a , a lm u r ad i nyimbo tu za kuwazuga watu, lakini linalotakiwa halisemwi; hili hili la vita vya panzi neema kwa kunguru. Usishangae kwa nini ni Waislamu waliosimama barabarani Mahonda, Wilaya ya Kaskazini B, Unguja wakawajeruhi vibaya vibaya Waislamu wenzao, pamoja na kuuteketeza Msikiti Mkubwa wa gharama uliopo hapo, kisa Uamsho wasiende Donge, ambako tayari umma wa Wakaazi wa huko na wa maeneo ya jirani walishasheheni kiwanjani kungojea tafakari murua ya nchi
Hanyegwa Mchana, k a t i k a Wi l a y a y a Kati, Mkoa wa Kusini Unguja. Ni eneo mashuhuri kutokana na gereza la muda mrefu, ingawa si wengi wanaopafahamu hapo, miongoni mwa wakaazi wa visiwa vya Unguja na Pemba. Waislamu wachache ambao wanalitumia eneo hilo kwa harakati zao za kujitafutia riziki za halali, hivi karibuni walipigiwa upatu ili wakaelimishwe juu ya matunda ya Muungano. Walichoshuhudizwa hapo ni harakati ya
Kiwanja kikubwa kinauzwa. Kipo katika eneo zuri la kuweza kufanya biashara, makazi au shughuli nyingine yoyote muhimu ya kimaendeleo. Kimepimwa na kupewa Namba Knd/tnd/ktb3/9. Kipo Mtaa kwa Tumbo Kata ya Tandale Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam. Kwa mawasiliano zaidi: 0787 463400
KIWANJA KINAUZWA
AN-NUUR
MASHAIRI/MAKALA
11
Inatoka Uk. 12
Universities (AAU) na na mtandao wa vyuo vikuu vya jumuiya ya madola yaani Commonwealth Universities (CU). Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kina walimu wenye uzoefu na utaalamu wa kutosha kutoka ndani na nje ya nchi. Chuo kina walimu wa sayansi toka nchini Cuba, Australia na pia Chuo kinatarajia kupata
kipaumbele kinatolewa kwa wanafunzi wa kike, walemavu na wanafunzi kutoka nje ya nchi. Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kina mpango wa kuanzisha masomo ya ngazi ya Masters katika eneo la Kigamboni Dar es Salaam, kuanzisha masomo ya cheti na diploma na pia kuanzisha Chuo cha utati wa urithi wa mambo ya kale Kilwa Masoko, Mkoani Lindi.
AN-NUUR
SHABAN 1433, JUMANNE JUNI 26-28, 2012 CHUO Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) kilianzishwa rasmi mwaka 2004, Chuo kinamilikiwa kisheria na Taasisi ya Maendeleo ya Waislamu nchini (Muslim Development Foundation MDF). Chuo kilianza udahili mwaka 2005 na kilianza na jumla ya wanafunzi 167 kikiwa na degree program tatu ambazo ni Bachelor of Arts (Education), Bachelor of Arts (Mass C o m m u n i c ation) n a Bachelor of Islamic Studies with Education. Miaka minne baadae, Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kiliongeza degree programu nne na kufanya jumla ya program hizo kuwa saba. Programu zilizoongezwa ni pamaja na Bachelor of Science (Education), Bachelor of Law with Shariah, Bachelor of Business Studies na Bachelor of Languages and Interpretation. Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kina jumla ya wanafunzi 3093 ikiwa ni pamoja na wanaume 1196 na wanawake 1897. Ta n g u k u a n z i s h w a Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro kimeshatoa wahitimu zaidi ya 900 ambapo wanafanya kazi sehemu mbalimbali serikalini, mashirika ya umma na katika taasisi binafsi. Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro ni mwanachama wa jumuiya mbalimbali zilizopo ndani na nje ya nchi. Jumuiya hizo ni pamoja na Tanzania Commission for Universities (TCU), Tanzania Association for Private Universities (TAPU), Committee of Vice Chancellors and Principals in Tanzania (CVCPT). Jumuiya za nje ni pamoja na Inter University Council for East Africa (IUCEA), Association of African
Inaendelea Uk. 11
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagaration Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.