YA MUUNDO WA KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ____________________ Kamati ya Kanuni ya Bunge iliyoundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Job Ndugai hivi karibuni, leo imekutana Jijini Dar es Salaam na Kuridhia mapendekezo ya mabadiliko katika muundo wa kamati za Bunge yaliyowasilishwa na Mhe. Spika ili kuendana na mabadiliko ya Muundo wa Wizara katika Serikali ya awamu ya Tano. Mabadiliko hayo ambayo yamefanywa chini ya kanuni ya 155 (3) ya kanuni za Kudumu za Bunge yamezingatia madaraka aliyonayo Spika kufanya marekebisho kwenye nyongeza za kanuni kwa kushauriana na kamati hiyo. Akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo Mh. Ndugai ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati hiyo amesema amelazimika kufanya mabadiliko katika muundo wa kamati ili kuendana na mabadiliko ya Wizara na kwa kuzingatia kuwa muundo wa kamati umetajwa kwenye nyongeza ya nane.
Katika muundo huo Kamati mbili mpya zimeundwa ambazo ni
kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na kamati ya kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma. Akifafanua kuhusu maamuzi ya Kikao hicho, katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah amesema kikao hicho kimekuwa na mafanikio makubwa na kuridhia mapendekezo ya Mhe. Spika kama yalivyowasilishwa. Aidha Dkt. Kashililah aliongeza na kusema kuwa Kamati nyingine zimefanyiwa mabadiliko kwenye majina na nyingine mbili kuunganishwa na kufanya kamati mpya za Bunge kuwa kama ifuatavyo: Kamati zilizounganishwa ni: Kamati ya Huduma na maendeleo ya Jamii imeunganishwa kutoka iliyokuwa Kamati ya Maendeleo ya Jamii na kamati ya Huduma za Jamii Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama imeunganishwa kutoka iliyokuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama na kamati ya mambo ya Nje. Kamati zilizofanyiwa Marekebisho madogo kwenye majina ni: Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira (awali ilikuwa Kamati ya Viwanda na Biashara) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii (awali ilikuwa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira) Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa (awali ilikuwa Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa)
Kamati zilizobakia kama ilivyokuwa awali ni pamoja na:
Kamati ya Uongozi, Kamati ya Kanuni za Bunge, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Kamati ya Katiba na Sheria Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, Kamati ya Miundombinu Kamati ya Nishati na Madini. Kamati ya bajeti Kamati ya Masuala ya Ukimwi Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) Wabunge wote wanatakiwa kuwasili Dodoma tarehe 20 Januari, 2016 tayari kwa kuanza Vikao vya Kamati kabla ya Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza tarehe 26 Januari, 2016.
Imetolewa na,
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano.
Ofisi ya Bunge, S.L.P 9133, DAR ES SALAAM 15 Januari, 2016.
Hotuba Ya Mwenyekiti Wa Tume Ya Mabadiliko Ya Katiba, Mhe. Jaji Joseph Sinde Warioba, Akiwasilisha Rasimu Ya Katiba Ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Katika Bunge Maalum La Katiba, Machi 2014
RIPOTI YA KAMATI YA KUDUMU YA KATIBA, SHERIA NA UTAWALA YA BARAZA LA WAWAKILISHI – ZANZIBAR KATIKA KUFATILIA UTENDAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2008/2009 KATIKA MWEZI WA APRILI HADI JUNI NA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 KATIKA MWEZI WA JULAI HADI FEBRUARI
Hotuba Ya Waziri Kivuli Na Msemaji Mkuu Wa Kambi Rasmi Ya Upinzani Wizara Ya Fedha Na Uchumi Ndugu Kabwe Zuberi Zitto Kuhusu Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Ya Wizara Kwa Mwaka Wa Fedha 20122013
Hotuba Ya Waziri Wa Ujenzi, Uchukuzi Na Mawasiliano Mheshimiwa Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe (Mb), Akiwasilisha Bungeni Mpango Na Makadirio Ya Mapato Na Matumizi Ya Fedha Kwa Mwaka Wa Fedha 2019_2020