Professional Documents
Culture Documents
2
1. MFUKO WA SELF – SELF MF
Walengwa
Walengwa wa Mfuko wa SELF, ni wajasiriamali wadogo hasa wale waishio sehemu za
vijijini; ikiwa ni pamoja na wanawake, vijana, walemavu, wakulima ambao wamekuwa
wakikosa huduma rasmi za kifedha, na hivyo kushindwa kushiriki kikamiifu kwenye
shughuli za uzalishaji.
(b) Kujenga Uwezo wa Asasi Ndogo na za Kati za Fedha kwa njia ya Kutoa
Mafunzo na Vitendea Kazi: Mafunzo haya yanafanya wadau wa SELF waweze
kutoa huduma bora na endelevu kwa wajasiriamali walengwa wa Mfuko wa
SELF. Aidha, Mfuko huwajengea uwezo wajasiriamali wadogo ili waweze kufanya
shughuli za uzalishaji mali kwa tija na kwa ufanisi zaidi, ikiwa ni pamoja na
kuitumia mikopo hiyo vizuri, ili hatimaye waondokane na umasikini.
3
1. Iwe imesajiliwa kisheria. Katika kuthibitisha hilo, nakala ya Hati ya kuandikishwa,
leseni ya biashara, MEMARTS, malipo ya kodi, share certificates na Katiba ya
Asasi husika vinapaswa kuwasilishwa Mfuko wa SELF.
10. Iwasilishe barua toka kwenye Bodi/Wadhamini inayotoa ridhaa kwa uongozi
kukopa. Kwa vyama vya Akiba na Mikopo, kumbukumbu za kikao cha mkutano
mkuu wa wanachama ulioridhia uongozi kukopa fedha zinahitajika.
4
ambayo ni Mwanza, Shinyanga, Kigoma, Tabora, Simiyu na Geita na Ofisi ya Kanda -
Arusha, inayotoa huduma kwenye mikoa ya kanda ya Kaskazini ambayo ni Arusha,
Kilimanjaro, Manyara, Tanga na Singida.
5
Tovuti: www.self.or.tz, Barua pepe: selfmf@self.or.tz
Barabara ya Kenyatta, Jengo la NSSF, Jengo la NSSF, Mafao House2nd Floor,
S.L.P: 3172, Mwanza, Simu: + 255 282505049, Old Moshi Arusha, S.L.P.1611, Arusha,
Fax: +255 282505050. Simu. 027 25 20154
Dhumuni la Mfuko ni kutoa mikopo yenye masharti nafuu hasa kwa wanawake wasio
na vigezo au sifa za kukopesheka katika taasisi za fedha ili waweze kujikwamua
kiuchumi na kupambana na Changamoto mbalimbali zinazowakabili kulingana na nafasi
yao katika familia na jamii.
Mfuko huu unaendesha shughuli zake katika halmashauri zote Tanzania Bara.
Walengwa wa Mfuko
Walengwa wanaotarajiwa kunufaika na Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake ni:
(i) Wanawake wenye umri wa miaka 18 na kuendelea au wanawake walio chini ya
umri huo ambao wana watoto, watakaokidhi sifa za walengwa;
(ii) Kikundi, au mwanamke mmoja mmoja kutoka katika makundi maalumu; na
(iii) Wanawake wajasiriamali waliojiunga katika vikundi vya kijamii (VICOBA, VSLAs,
SILC, ROSCAs) na SACCOS wanaofanya shughuli za kiuchumi zikiwemo; kilimo,
uvuvi, ufugaji, viwanda vidogo, usafirishaji, madini na biashara mbalimbali halali.
Sifa za wanawake walengwa wa Mfuko
Awe mjasiriamali katika eneo husika, kwa muda usiopungua mwaka mmoja;
6
Wasiokuwa na sifa za kukopesheka katika Taasisi za fedha;
Mwananke asiyekuwa na ajira rasmi;
Mwenye mtaji usiozidi shilingi 200,000 katika mradi anaofanya.
Vigezo vya Utoaji wa Mikopo kwa Walengwa
Vigezo vya utoaji wa mikopo katika Mwongozo huu vitakuwa kama ifuatavyo:
i. Mikopo itatolewa kwa miradi ya kilimo cha mazao ya biashara na chakula,
ufugaji, uvuvi, biashara, usindikaji, viwanda vidogo, wachimbaji wadogo wa
madini, n.k. Kila mradi uwe na andiko la mradi;
ii. Uwepo wa fomu ya maombi iliyojazwa na mwombaji na kuwasilishwa kwa afisa
maendeleo ya jamii;
iii. Uthibitisho wa dhamana ya wanakikundi au kikundi cha mwombaji au
mwanakikundi mmoja mwenye umri wa miaka 18 au chini ya umri huo na
mwenye mtoto kudhaminiwa na wenzake wanne. Muda wa udhamini ni miaka
miwili na isizidi miaka mitano;
iv. Dhamana ya mali isiyohamishika au wadhamini wawili wenye mali
zisizohamishika kwa mkopaji binafsi;
(a) Mikopo itatolewa kwa riba ya asilimia 10 kwa mwaka.
(b) Riba hiyo katika ngazi zote itatumika kwa ajili ya kugharamia uendeshaji na
usimamizi chini ya udhibiti wa Afisa Masuuli (Accounting Officer) katika ngazi
husika;
v. Kabla ya kukopa vikundi vya Kijamii na SACCOS au mwanamke mmoja mmoja
wanatakiwa kufungua akaunti na kuweka asilimia 10 ya fedha inayokopwa;
vi. Kiwango cha utoaji wa mkopo kwa mwanamke mmoja mmoja kitategemea
andiko la mradi na kisizidi shilingi 1000,000/= Kwa vikundi vya kijamii au
SACCOS isizidi 20,000,000/-;
vii. Uthibitisho wa taarifa ya ushiriki wa mafunzo ya ujasiriamali na biashara kutoka
kwa Afisa Maendeleo ya Jamii;
viii. Usajili wa Kikundi cha wanawake na utambulisho wa Serikali ya Mtaa au kijiji;
ix. Mwombaji kuwa na vitambulisho vinavyotambulika kisheria.
7
Fomu ya Maombi ya Mkopo
Mwombaji wa mkopo anatakiwa kujaza fomu ya maombi ya mkopo na kuambatisha
mchanganuo wa mradi. Fomu hizo zinapatikana kwa Afisa Maendeleo/Mtendaji wa kata.
Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) umeanzishwa kisheria (chini ya Sheria ya Misitu Sura
323 ya mwaka 2002), kama njia endelevu ya kuwezesha uhifadhi, usimamizi na
uendelezaji wa rasilimali misitu katika Mikoa
yote ya Tanzania Bara. Mfuko huu umeanzishwa
kwa lengo la kukabiliana na changamoto za
usimamizi wa rasilimali ya misitu hasa katika
kuimarisha utekelezaji wa Sera na Sheria ya
Misitu. Mfuko wa Misitu Tanzania ni Mfuko wa
Umma uliopo chini ya Wizara ya Maliasili na
Utalii. Mfuko huu unasimamiwa na Bodi ya
Wadhamini na utekelezaji wa shughuli za kila
siku hufanywa na Sekreatarieti ya Mfuko. Mfuko
8
wa Misitu Tanzania ulizinduliwa rasmi kupitia Waraka wa Hazina Na. 4 wa mwaka 2009
na ulianza rasmi utekelezaji wa majukumu yake Julai 2011. Mfuko wa Misitu Tanzania
unatoa aina tatu za uwezeshaji kulingana na mahitaji ya walengwa. Uwezeshaji huo ni:
Uwezeshwaji wa fedha; vifaa; na Stadi/Utaalam
Mfuko unatoa ruzuku katika maeneo matatu ya kipaumbele ambayo ni:
Mfuko wa Misitu Tanzania unatoa aina tatu za ruzuku za ambazo kama ifuatavyo:
Ruzuku Ndogo: kiasi cha fedha kisichozidi Shilingi za Kitanzania (TZS) milioni
tano;Ruzuku ya Kati: kiasi cha fedha kinachozidi TZS milioni tano (5) lakini haizidi TZS
milioni 20;na Ruzuku Kubwa:kiasi cha fedha kinachozidi TZS milioni 20 lakini haizidi
TZS milioni 50
9
taasisi za utafiti, wizara, Idara, na wakala za serikali, pamoja na mamlaka za serikali za
mitaa. Hata hivyo, vikundi/asasi/taasisi zote zinatakiwa kuwa zimesajiliwa na mamlaka
zinazotambulika kisheria, wakati waombaji binafsi wanatakiwa kuwa na wadhamini
wawili wanaotambulika/wanaoaminika. Mfuko wa Misitu Tanzania huitisha/hukaribisha
maandiko ya miradi ya kuomba ruzuku kila mwaka hususan tarehe mosi ya mwezi
Februari na maandiko hayo hupokelewa kwa vipindi vitatu tofauti.
Mfuko wa Misitu Tanzania unatoa ruzuku kwa miradi itakayotimiza vigezo vifuatavyo:
Mradi unatoa faida ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja katika uhifadhi na
usimamizi wa rasilimali misitu; Mradi unatoa faida moja kwa moja au isiyo ya moja kwa
moja kwa walengwa; Shughuli ziwe wazi na kuwepo na uwajibikaji; Mradi wenye
ubunifu; Miradi ambayo matokeo yake yatatumika kuboresha usimamizi wa rasilimali
misitu; Uwezo wa mwombaji kufanikisha malengo na shughuli zilizopendekezwa; Uwezo
wa mwombaji kutekeleza na kusimamia shughuli za mradi; Uendelevu wa shughuli za
mradi zitakazotekelezwa; Ushiriki wa wadau; Mwombaji wa ruzuku ya kati na kubwa
aahidi kuwa atachangia asilimia 20 (fedha taslimu au hali na mali) ya jumla ya fedha
yote inayoombwa; na Mwombaji wa ruzuku aahidi uwepo wa watumishi wenye ueledi
wa aina ya mradi unaombwa ili kurahisisha utekelezaji..
Miradi iliyowezeshwa kupitia ruzuku ya Mfuko imesambaa katika mikoa yote Tanzania
Bara na imeoneshwa kwenye ramani ya Tanzania kama Kiolezo Na.1
10
RAMANI YA TANZANIA IKIONYESHA MIRADI INAYOFADHILI
NA MFUKO WA MISITU
Jumla ya Miradi : 2 Jumla ya Miradi : 12 Jumla ya Miradi : 9 Jumla ya Miradi : 4 Jumla ya Miradi : 13
Midogo: 2 Midogo: 6 Midogo: 5 Midogo: 2 Midogo: 10
Kati: 0 Kati: 5 Kati: 4 Kati: 1 Kati: 2
Mikubwa : 0 Mikubwa : 1 Mikubwa : 0 Mikubwa : 1 Mikubwa : 1
Hadi kufikia Mwezi Juni, 2016 Jumla ya mikopo yenye thamani ya shilingi 478.6 Milioni
ilitolewa kwa wajasiriamali 761, ambapo wanawake walikuwa 575 na wananume 186 .
1. DIRA YA MFUKO
“Tumedhamiria kuwa taasisi ya kifedha ambayo ni chaguo la vijana na
wanawake katika kuleta mabadiliko bora ya kiuchumi nchini Tanzania”
2. DHIMA YA MFUKO
“Kujenga uwezo kwa vijana na wanawake wa Tanzania kwa kuwapatia
huduma bunifu za kifedha na zisizo za kifedha kupitia wafanyakazi weledi,
ili kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa walengwa.”
3. MADHUMUNI YA MFUKO
Madhumuni ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea ni kuwa na chombo
mahsusi cha kutia msukumo wa maendeleo katika jamii hasa ya wale wenye kipato cha
chini, wakina mama na Vijana, na wafanyabiashara ndogondogo waweze kujiajiri
wenyewe hatimae waweze kujitegemea.
4. WALENGWA WA MFUKO
i. Vijana ambao wamehitimu mafunzo mbalimbali ikiwemo ufundi stadi
unatambuliwa na VETA,SIDO na vyuo vingine vya ufundi stadi.
ii. Wanawake wajasiriamali walio katika sekta ya uzalishaji mali.
iii. Kundi maalum la Vijana walemavu
12
5. VIGEZO VYA MIKOPO
a. Mikopo ya vijana
i. Uwe mkazi wa eneo lililolengwa
ii. Uwe na shughuli ya ujasiriamali inayoendana na fani uliyosomea
iii. Ujiunge katika kikundi cha watu kati ya watano hadi kumi waliotimiza masharti
kwa Mikopo ya UMOJA na VIFAA.
iv. Uwe mhitimu katika chuo kinachotambulika na VETA, NACTE, ama umepata
mafunzo ya ujasiliamali toka SIDO ama Taasisi za kijasiriamali.
v. Uhudhurie mafunzo ya Mikopo ya Ujasiriamali yatolewayo na Mfuko wa Rais wa
Kujitegemea kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali.
b. Mikopo ya akina mama
i. Uwe umepatiwa mafunzo ya ujasiriamali toka SIDO, VETA au Taasisi
inayotoa mafunzo ya ujasiriamali.
ii. Uwe mkazi wa eneo lililolengwa
iii. Uwe mjasiriamali katika sekta ya uzalishaji na sio ya uchuuzi.
iv. Ujiunge katika kikundi cha watu 5 hadi 20 waliotimiza masharti Kwa Mikopo ya
UMOJA na VIFAA.
v. Uhudhurie mafunzo ya siku saba ya Mikopo na Ujasiriamali yatolewayo na Mfuko
wa Rais kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.
6. RIBA:
Mfuko unatoza Riba kulingana na aina ya Walengwa wetu. Mikopo ya Vijana Riba ni
asilimia 1% kwa mwezi sawa na asilimia 12% kwa mwaka, na Mikopo ya Wanawake
wazalishaji mali ni asilimia 1.25% kwa mwezi , sawa na asilimia 15% kwa mwaka.
7. MUDA WA MAREJESHO: Muda wa marejesho kwa sasa ni kati ya miezi 4 hadi 12
kwa mikopo ya UMOJA na kwa mikopo ya Vifaa ni hadi miezi 24.
13
BAADHI YA BIDHAA ZA ASILI ZINAZOTENGENEZWA
NA KIKUNDI CHA WANAWAKE KIITWACHO
HANDCRAFT KILICHOPO NJOMBE ENEO LA
SABASABA KATIKA JENGO LA SIDO.
Walengwa wa Mfuko
Mtu binafsi, vikundi vilivyosajiliwa, vyama vya wakulima au kampuni zinazojishughulisha
na miradi mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa kilimo (mazao,mifugo na uvuvi).
14
Vigezo vya Mikopo
a) KwaWaombaji wote
i. Kujaza fomu ya maombi ya huduma za PASS.
ii. Taarifa ya benki kwa miezi 12
iii. Ainisha mradi/biashara na mahitaji na Gharama zote zinazotakiwa katika mradi
wako.
iv. Kuchangia asilimia 25 ya gharama za mradi/biashara
v. Ainisha uzoefu katika mradi au biashara hiyo.
vi. Utambulisho kutoka mamlaka husika mahali mradi unapofanyika
vii. Uthibitisho wa Dhamana ya mkopo (kama leseni za makazi, dhamana za
kuhawilishwa, Hati ya nyumba na nyinginezo)
viii. Cheti cha usajili wa biashara Kama mradi/biashara imesajiliwa
ix. Leseni ya biashara (kama ipo)
x. Kulipia Ada ya maombi ya huduma za PASS
b) Mtu binafsi
d) Makampuni
i. Mahesabu ya Kampuni ya miaka 3 iliyopita yaliyokaguliwa
ii. Mahesabu ya kampuni ya mwaka husika mpaka mwezi wa mwisho kabla ya
maombi.
15
iii. Makadirio yote ya mradi kwa kipindi cha mkopo
iv. Wasifu wa Wakurugenzi
v. Mwongozo wa kampuni
vi. Marejesho ya kampuni ya mwaka ulioisha yaliyowasilishwa BRELA
vii. Cheti cha usajili wa kamapuni
viii. Leseni ya biashara na cheti cha kulipa kodi
ix. Makubaliano ya kikao cha bodi ya kampuni kuomba dhamana ya PASS
x. Mchanganuo wa biashara
xi. Dhamana za mkopo
xii. Uthaminishaji wa dhamana inayowekwa
Kabla Baada
Nyumba bora iliyotokana na kipato cha familia kuongezeka baada ya kuwezeshwa na PASS kupata
mkopo wa kunenepesha ngombe huko Monduli, Arusha
16
6. MFUKO WA KILIMO KWANZA
(AGRICULTURE FINANCING WINDOW)
UTANGULIZI
Mnamo mwaka 2009, Serikali ilifikia uamuzi wa kukuza
sekta ya kilimo na kuboresha uzalishaji kupitia azma ya
Kilimo Kwanza. Ili kutekeleza azimio hilo, Serikali ilitenga kiasi cha fedha shilingi
bilioni 42 za kitanzania kwa ajili ya kukopesha katika miradi yakilimo. Serikali iliiteua
benki ya TIB Development ltd na kuipa mamlaka ya kukopesha na kusimamia fedha
hizo kwa kufungua Dirisha maalumu la mikopo ya kilimo. Dhumuni kubwa ikiwa ni
kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali ya serikali katika kuwaletea wananchi
maendeleo ya kiuchumi na kupunguza umaskini.
2. Walengwa
i) Riba inatozwa kwa kiwango cha asilimia tano (5%) kwa mwaka kwa wakopaji wa
moja kwa moja toka benki (direct borrowers). Taasisi zinazokopa kwa ajili ya
kukopesha (on-lenders) zinatozwa asilimia nne (4%) kwa mwaka ambapo
zitatakiwa kukopesha kwa asilimia isiyozidi nane (8%) kwa wakulima/wateja
wao. Viwango vya riba vinaweza kubadilika itakapobidi.
ii) Ada za kibenki (bank charges)zote zinazohusiana na mkopo ikiwa ni pamoja na
gharama za ushuru wa stampu, usajiri wa hati za dhamana, mikataba na
huduma mbalimbali zikiwemo za kisheria zitalipiwa na mkopaji.
iii) Kwa taasisi za kifedha (on-lenders), ada zote (bank charges) za mkopo
zitakazotozwa kwa mkulima (final borrower) zinatakiwa zisizidi asilimia mbili
(2%).
17
4. Muda wa Marejesho ni kati ya miezi sita hadi miaka kumi na tano (15) kwa
kutegemea aina ya mradi wa kilimo pamoja na makadirio ya hesabu (financial
projections).
5 Kipindi cha rehema (Grace period) kinatolewa kulingana na kipindi cha kukomaa
kwa mazao husika pamoja na makadirio ya mtiririko wa fedha (projected cash flow).
Katika kipindi hicho mkopaji atatakiwa kulipia riba ya mkopo ingawa malipo yatazingatia
msimu wa mapato.
Masharti husika kwa mkopaji atapatiwa na wahusika katika tawi na kanda husika.
Kwa maelezozaidiwasilianana :
MkurugenziMtendaji
TIB Development Bank,
S L P 9373,
DAR ES SALAAM
Katika juhudi za kukabiliana na changamoto hizo, mnamo mwaka 2002/03, Serikali kwa
kushirikiana na Benki Kuu ilianzisha Mfuko wa kudhamini mikopo kwa ajili ya mauzo ya
18
bidhaa za Tanzania nje ya nchi (Export Credit Guarantee Scheme (ECGS)).Madhumuni
ya mfuko huu ni kuhamasisha uzalishaji kwa ajili ya mauzo nje ya nchi ili kuchangia
kukuza pato la Serikali. Halikadhalika, katika mwaka wa fedha wa 2004/05, Serikali
ilianzisha Mfuko wa Udhamini wa mikopo ya miradi midogo na ya kati(Small and
Medium Enterprise – Credit Guarantee Scheme (SME-CGS)). Mfuko huu unalenga
kukuza na kuendeleza miradi midogo na ya kati (SMEs) kwa kujenga mazingira ya
kuwezesha wajasiriamali wenye miradi midogo na ya kati kupata mitaji kwa njia ya
mikopo ili kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuzaji wa uchumi, kukuza ajira na
kupunguza umaskini. Mifuko hii inasimamiwa na Benki Kuu chini ya makubaliano na
Serikali (Agency Agreement) kama njia ya mpito hadi hapo itakapoanzishwa taasisi
inayojitegemea.
19
iii. Benki au taasisi ya fedha itafuata taratibu zote za kibenki kabla ya kupitisha mkopo,
ikiwa ni pamoja na upembuzi makini wa mradi husika, kuangalia taarifa za muombaji
kuhusu taarifa ya mikopo mingine, aliyokwishawahi kupata na kusajiliwa (Credit
Information Bureau).
iv. Baada ya benki au taasisi ya fedha husika kuridhika na ubora wa mradi wa mkopaji
na kuridhia kutoa mkopo, benki au taasisi ya fedha itawasilisha maombi ya udhamini
kwenye mifuko husika ya udhamini, endapo mkopaji hatokuwa na dhamana ya
kutosha kupata mkopo.
v. Baada ya udhamini kutolewa, benki au taasisi ya fedha husika inawajibika kufuatilia
maendeleo ya mradi na marejesho na kuwasilisha taarifa kwenye mfuko wa
udhamini.
Mfuko huu unasimamiwa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) kupitia ofisi
zake za mikoa.
20
iv. Muombaji wa mkopo awe ndie mmiliki halali wa Mradi
v. Muombaji awe na uwezo na nia ya kurejesha mkopo kwa muda uliopangwa
vi. Muombaji wa mkopo awe tayari kufungua akaunti ya Benki kwa jina la biashara
yake
vii. Kwa mikopo ya mtu mmoja mmoja muombaje awe na wadhamini wawili wenye
dhamana
viii. Kwa Mikopo ya Vikundi muombaji awe tayari kujiunga kwenye vikundi vya
mshikamano na kuweka akiba ya mkopo kama dhamana ya mkopo
Muundo wa Mkopo
21
9. MFUKO WA MAENDELEO YA VIJANA (YDF)
(i) Kikundi cha Vijana ndicho huomba mkopo ambao hutolewa kupitia SACCOS ya
Vijana ya Halmashauri ya Wilaya husika.lengo ya kupitisha fedha hizi kwenye
SACCOS ni kuwapa vijana wenyewe umiliki na kujenga tabia ya kuweka na
kukopa miongoni mwa vijana
(ii) Wizara hupeleka fedha kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Wilaya (DED) ambaye
naye huzipeleka kwenye SACCOS husika. Wizara humwelekeza kwa maandishi
ni kikundi gani kinastahili kupewa mkopo.
(iii) Kikundi cha Vijana kabla ya kupewa mkopo, hubuni mradi na kuandaa andiko
ambalo hufanyiwa uchambuzi na kuthibitishwa na DED husika. Baadaye mradi
na taarifa za uhalali wa kikundi hupelekwa kwa RAS ambaye ndiye huleta
maombi hayo kwa Katibu Mkuu – Wizarani.
(iv) Wizara hufanya uchambuzi wa mradi, huchunguza taarifa za Halmashauri na
Mkoa kupitia fomu maalum iliyoandaliwa. Inapoonekana mradi unaoombewa
mkopo unafaa, hupewa mkopo.
(v) Mkopo urejeshwa Wizarani kupitia kwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya
Halmashauri ya Wilaya husika baada ya kupokea fedha hizo kutoka kwenye
SACCOS ya Vijana ya Halmashauri yake.
22
(vi) Muda wa marejesho kwa sasa ni miaka miwili (2)
(vii) Riba ya mkopo ni 10% ambapo 5% ubakizwa kwenye SACCOS ya Vijana ili
kuiongezea mtaji. Aidha, 2% ubakizwa kwenye Halmashauri husika ili
kuwezesha usimamiaji, ufuatiliaji na uratibu wa mikopo itolewayo na Mfuko
katika maeneo yao. Aidha, 3% inayobaki urejeshwa kwenye Mfuko ili
kuuwezesha kuwa endelevu.
Kwa huduma hii, tafadhali tembelea Halmashauri yeyote iliyo karibu nawe.
Mfuko wa Pembejeo (The Agricultural Inputs Trust Fund) ulianzishwa mwaka wa 1994
kwa Sheria ya Bunge Na. 9 ya mwaka wa 1994.Hivyo, kazi ya Mfuko wa Pembejeo ni
pamoja na:-
Kutoa mikopo ya masharti nafuu kwa ajili ya
kugharamia usambazaji wa pembejeo za kilimo, uvuvi,
dawa za mifugo na zana ndogondogo zinazotumiwa
katika sekta hizo.
Kuhakikisha kuwa pembejeo zinawafikia wakulima,
wavuvi na wafugaji kwa wakati na kwa bei nafuu.
Kutoa mikopo ya matrekta mapya, matrekta madogo (power tiller) na kukarabati
matrekta machakavu ili kuboresha na kupanua maeneo ya kilimo nchini.
Kufuatilia marejesho ya mikopo iliyotolewa ili Mfuko uwe endelevu (Revolving) na
waombaji wengine waweze kukopeshwa.
i. Pembejeo za kilimo, Uvuvi na Ufugaji, muda wa mikopo ni miaka miwili kwa riba
ya asilimia nane (8%) kwa mwaka.
ii. Mikopo ya matreka mapya, muda wa mikopo ni miaka mitano kwa riba ya 6-7 %
kwa mwaka.
iii. Mikopo ya matrekta madogo ya mkono (Power tiller), muda wa mikopo ni miaka
mitatu kwa riba ya 6-7% kwa mwaka.
iv. Mikopo ya kukarabati matrekta; muda wa mikopo ni miaka mitatu, riba 6-7%
kwa mwaka.
vi. Mikopo ya nyezo za usindikaji wa mazao, muda wa mkopo ni miaka mitatu kwa
riba ya asilimia 6-7% kwa mwaka.
24
vii. Fomu iliyoambatanishwa na vielelezo vyote itawasilishwa kwa afisa Kilimo wa
wilaya hsuiaka ili ipitishwe.
viii. Fomu za maombi zilizopitishwa na Halmashauri ya Wilaya/Mji/ Manispaa
zitawasilishwa Mfuko wa Pembejeo.
Mkurugenzi Mtendaji
Mfuko wa Pembejeo
S. L .P 32081
DAR ES SALAAM
Simu: 022 2700191
Nukushi: 022 2774850
Barua pepe: agitif@kilimo.go.tz
Tovuti: www.agitf.go.tz
25
Vigezo vya wanufaika wa mfuko
Mfuko wa Nishati Vijijini unasimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini kwa niaba ya Bodi.
Sheria pia imebainisha uwepo wa Wakala wa Amana (Trust Agent) pamoja na
majukumu yake. Wakala wa Amana huratibu upelekeji wa fedha kwa watekelezaji
pamoja na ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa miradi husika mara baada ya
mikataba kusainiwa kati ya mtekelezaji na Bodi ya Nishati Vijijini.
Majukumu ya Wakala
26
ii. Kuainisha na kutathmini miradi ya nishati inayostahili ufadhili wa Mfuko wa
Nishati vijijini;
iii. Kuwajengea uwezo waendelezaji wa miradi ili kutekeleza mipango endelevu ya
nishati vijijini;
iv. Kuibua, kuhamasisha na kuwezesha utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini;
v. Kuhamasisha matumizi ya nishati bora katika shughuli za uzalishaji mali, kilimo,
viwanda vidogo na vya kati na biashara ili kukuza uchumi vijijini;
vi. Kuwezesha upatikanaji na matumizi ya nishati bora kwa ajili ya huduma za
ustawi wa jamii vijijini kama vile afya, elimu, maji na mawasiliano.
Wakala hutekeleza majukumu yake kwa kushirikiana na taasisi za umma, sekta binafsi,
asasi zisizo za kiserikali na taaisisi za jamii ili kuhakikisha kuwa wananchi wengi wa
vijijini wanapata huduma za nishati bora.
Fursa za Fedha
a. Ruzuku (Grants)
i. Ruzuku kabla ya uwekezaji (pre investment grants)
ii. Ruzuku wakati wa uwekezaji (development stage)
b. Mikopo ya Muda Mrefu (credit line facility);
c. Malipo ya kupunguza Hewa ya Ukaa (Carbon credits/Clean Development
Mechanism)
d. Kushindanisha Miradi yenye Ubunifu, mfano Lighting Rural Tanzania Grant
Competition.
27
Fursa za Mafunzo
Vigezo vya kuzingatia kwa mwombaji anayeaka ruzuku kutoka kwenye mfuko wa nishati
vijijini ni kama ifuatavyo;
28
iv. Awe na hati/kibali cha kumiliki Ardhi;
v. Awe na kibali cha kutumia maji (kwa miradi ya small hydropower);
vi. Awe amekubalika na serikali ya kijiji/kata au wilaya ya mahali anapokusudia
kutekeleza mradi;
vii. Awe na kibali cha mazingira;
viii. Aonyeshe kuwa mradi wake ni shirikishi kwa jamii.
Mkurugenzi Mkuu,
Wakala wa Nishati Umeme Vijijini,
SLP 7990,
Dar es Salaam.
Awamu ya pili ya (TASAF II) ilitekelezwa kwa miaka nane kuanzia mwaka 2005 hadi
2013, katikaHalmashauri zote Tanzania Bara pamoja na Unguja na Pemba. Jumla ya
miradi ipatayo 14,437 ya sekta mbalimbali yenye hamani ya Shilingi Bilioni 430
ilitekelezwa.
Kutokana na haja ya kuhakikisha kuwa kaya maskini sana zinawezeshwa kutumia
huduma za jamii zilizopo, Serikali ilianzisha Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika
Awamuya Tatu ya TASAF (TASAF III) ambayo ilizinduliwa rasmi Mwezi Agosti, 2012 na
utekelezaji unaendelea mpaka sasa.
29
Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF III)
Ni Mpango wa kuwezesha kaya Maskini kuongeza kipato, fursa na uwezo wa
kugharamia mahitaji muhimu. Utekelezaji unahusisha halmashauri zoteza Tanzania Bara
na Unguja na Pemba. Muda wa utekelezaji ni miaka kumi ambapo patakuwa na awamu
mbili za miaka mitano kilamoja.
Mpangounasehemukuunne:
Walengwa wa Mpango
Ni kaya maskini sana zinazo ishi katika mazingira duni na hatarishi zilizotambuliwa
na kuorodheshwa kwenye daftari la walengwa
30
Kwa maelezo zaidi wasiliana Na:
Mkurugenzi Mtendaji
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
S L P 9381
Kilwa / Malindi Rd
Simu: +255-22-2123583(Tel)
Nukushi: +255-22-2123582(Fax)
DAR ES SALAAM
Historia ya Mfuko
Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ilianzishwa kwa Sheria ya Mfuko wa Elimu Na.8 ya
mwaka 2001 Sura ya 412 ikiwa na jukumu la kusimamia uendeshaji wa Mfuko wa Elimu
wa Taifa. Madhumuni ya Mfuko wa Elimu ni kuongeza nguvu za serikali katika
kugharimia miradi ya elimu ili kuinua ubora wa elimu na upatikanaji wake kwa usawa,
katika ngazi zote za Elimu kwa Tanzania Bara na Elimu ya Juu kwa Tanzania Zanzibar.
Sifa za mwombaji
Mfuko wa Elimu hutoa ufadhili kwa njia ya ruzuku na mkopo nafuu kwa shule na taasisi
za elimu za umma na binafsi ambazo zenye usajili wa Mamlaka husika kama ifuatavyo:
a) Vyuo Vikuu – Kamisheni ya Vyuo Vikuo Tanzania (TCU) angalau usajili wa muda
b) Vyuo vya Ufundi – Baraza la Taifa la Vyuo vya Ufundi (NACTE) angalau usajili wa
muda.
c) Vyuo vya Ualimu, shule za sekondari, msingi na awali- Wizara ya Elimu na
mafunzo ya Ufundi (Usajili kamili)
31
Maeneo ya Ufadhili
Katika kutekeleza jukumu la utoaji ufadhili, Mamlaka imeweka vipaumbele vya ufadhili
ambavyo huboreshwa kila Mwaka kwa kuzingatia Sera na Mahitaji ya Kisekta. Aidha
Maeneo haya hujadiliwa kwa pamoja na Wizara Mama ya Elimu, Sayansi Teknolojia na
Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Maeneo ya kipaumbele kwa ujumla wake yamekuwa ni:-
Vifaa vya kufundishia na kujifunza kama vitabu, vifaa vya Maabara, mashine na
mitambo mbalimbali, vitabu vya kiada na zana nyingine za kufundishia.
Upatikanaji wa vifaa vya TEHAMA, kufunga mitandao
Mafunzo kwa Wakufunzi katika fani Maalum kwa taasisi za elimu ya Juu;
Vifaa zaidizi na vile vya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wenye mahitaji
maalum (wenye ulemavu)
Programmu maalum kuwezesha wanafunzi wa kike kujiunga na michepuo ya
sayansi katika ngazi ya Vyuo vikuu na Vyuo vya Ufundi;
Ujenzi wa miundombinu ikiwemo mabweni, kumbi za mihadhara, madarasa,
maktaba na ofisi
Mikopo kwa ajili ya Ujenzi, upanuzi na ukarabati wa majengo kwa shule binafsi
na vyuo vya elimu ya juu.
32
c) Mpango wa ulipaji mkopo ukitaja pia fedha hizo zinapatikana vipi (Details of
repayment plan)
d) Dhamana ya mkopo mali isiyo hamishika (Collateral of immovable asset 150% of
the value of the loan)
e) Gharama za ujenzi
Kati ya Mwaka 2003/4 na 2015/16 Mamlaka ya Elimu Tanzania imeweza Kwa ujumla
kufadhili na kutekeleza miradi 2,161 yenye thamani ya TZS Billion 109,954,926,454.00.
Miradi iliyofadhiliwa mingi. Baadhi ya miradi iliyotekelezwa katika kipindi cha karibuni ni
pamoja na:-
33
Vyumba vya mihadhara, vyuo vikuu
xi. Mamlaka pia hutoa ufadhili kwa upande wa Zanzibar ,ikiwemo miradi ya Ufadhili
Mafunzo ya awali (pre entry) wanafunzi wa kike katika Sayansi
xii. Kuiongezea uwezo Idara ya Uthibiti ubora wa Elimu Msingi na Sekondari katika
kutekeleza majukumu yake kwa kuanzia na ukaguzi wa shule zilizopata ufaulu
hafifu katika mwaka wa 2014;
Kwa maelezo zaidi wasiliana Na:
Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Elimu Tanzania
S L P 34578
DSM
34
15. MFUKO WA UTT-MFI Plc
Malengo ya Mfuko
Kutoa huduma shirikishi za kifedha (financial inclusive services) kama vile; uwakala wa
bima, uwakala wa benki, uwakala mkuu wa miamala ya fedha kupitia mifumo ya
Tehama
35
Na. Huduma Nia na Madhumuni Walengwa Malengo
/Mkopo
2 Pamoja Kukidhi Mahitaji ya mitaji Wafanyabiashara Kuwezesha na
loan kwa wafanyabiashara ndogo ndogo kuimarisha biashara na
wadogo wadogo ambao ambao ukuzaji/uwekaji akiba
kwa namna moja au wamedhaminiwa na kutoa ajira –
nyingine hawakopesheki na wenzao katika husussani akina mama
katika mabenki vikundi. na vijana
3 Taasisi kuziba nakisi ya kifedha na SACCOS na Kuzijengea uwezo
loan kuziwezesha SACCOS na Taasisi ndogo za taasisi hizo kutimiza
taasisi ndogo za kifedha kifedha malengo ya utoaji
zinazo zijihushisha na huduma za kifedha na
ukopeshaji ili ziweze kuwafikia
kuendelea kutoa mikopo wananchi/wahitaji
kwa wanachama wao walio wengi zaidi
4 Mshahar Kuwawezesha watumishi wa Wote Walio Kusaidia watumishi wa
a Loan Serikali kutimiza mahitaji katika utumishi umma kupata rasilimali
yao ikiwemo ununuzi wa wa umma na vifaa mbali mbali
vifaa vya mahitaji ya (Watumishi wa Fursa kwa watumishi
nyumbani kama vile Serikali, kujiwekea akiba
vyombo vya usafiri, Samani Mashirika na (Forced saving)
za ndani n.k. Taasisi za
Umma)
5 Hati Kuwawezesha watoa Watoa huduma Kuwawezesha watoa
Malipo huduma na wakandarasi na wakandarasi huduma na
loan (waliopewa mikataba na waliohakikiwa na wakandarasi
(Contrac Serikali na Taasisi za UTT MFI wazalendo/wazawa
t Umma) kupata fedha za katika jitihada za
financin kukidhi mahitaji ya mtaji kukuza ajira nchini
g) kwa kuzingatia kazi
walizopewa.
6 Bima Kutoa fedha kwa ajiri ya Wakopaji katika Kusambaza huduma za
loan kukidhi mahitaji ya bima ya mkopo wa bima nchini kote ili
Afya, mali, maisha n.k kwa Pamoja; Wamiliki kupunguza hasara
watanzania wenye mapato wote wa zitokanazo na
ya chini na kati. vipande, hisa na majanga/madhira
hati fungani mbalimbali yakiwemo
zilizosajiliwa magonjwa na uharibifu
36
Na. Huduma Nia na Madhumuni Walengwa Malengo
/Mkopo
katika Soko la wa mali usiotarajiwa.
Hisa la Dsm,
wafanyabiashara
wadogo wadogo
na watumishi
walio katka sekta
binafsi
7 Salary Kuwasaidia watumishi walio Watumishi wote Kutimiza mahitaji ya
Advance katika sekta ya umma walio katika dharura ya kifedha
loan kukidhi mahitaji ya dharura sekta ya umma
(Serikali na
Taasisi zake)
8 Special Kutoa mikopo kwa miradi Wamiliki wa Kusaidia kukuza
Projects mahususi ambayo inalenga viwanda vidogo ujasiriamali na
loan kuzalisha bidhaa vidogo vya uzalishaji wa ajira mpya
zinazoongeza thamani ya usindikaji, kwa vijana.
mazao na kuzalisha ajira usagishaji,
mpya. ufumaji,
utengenezaji
nguo, na
utengenezaji
bidhaa n.k
9 Micro Kuwawezesha Wafanyabiashara Kutoa huduma mbadala
Leasing wafanyabiashara wadogo wadogo na wa ili kusaidia ujasiriamali
loan kukidhi mahitaji yao ya kati; walio katika na uzalishaji wa ajira
kifedha ili kupata vifaa ushirikiano wa kwa Wananchi wa
wezeshi vya biashara kibiashara na; kawaida
zikiwemo mashine Makampuni
mbalimbali zitakazo tumika mbalimbali
kama nyenzo na kuleta tija
na ufanisi katika kazi/
biashara.
10 Micro Kuwawezesha wananchi wa Wananchi wa Kuunga mkono jitihada
Housing kawaida waishio mijini na kipato cha chini za Serikali katika
Loan vijijini kumiliki nyumba bora na cha kati na kuhakikisha wananchi
za kuishi watumishi wote wa kawaida wanakuwa
37
Na. Huduma Nia na Madhumuni Walengwa Malengo
/Mkopo
walio katika na Makazi Bora
Utumishi wa
Umma
11 School Kutoa mikopo inayolenga Wamiliki wa Kuisaidia sekta ya elimu
Improve kukidhi mahitaji ya upanuzi Shule binafsi na katika kuboresha
ment wa huduma ya elimu kwa za Serikali mazingira ya
Loan shule husika ikiwemo ufundishaji na utoaji wa
kujenga madarasa mapya, elimu iliyo bora kwa
ununuzi wa samani, ujenzi wanafunzi
wa uzio nk.
12 Sanitatio Kuwawezesha Wafanyabiashara Kutekeleza sera za
n Loan wafanyabiashara wa wadogo na wa Serikali katika
huduma za usafi kukidhi kati;wanaojishug kuhakikisha mazingira
mahitaji yao ya kifedha ili hulika na bora kwa kila
kupata vifaa wezeshi vya biashara za mwananchi na kuepuka
biashara zikiwemo mashine huduma za usafi magonjwa ya mlipuko.
na nyenzo mbalimbali za wa
usafi. mazingira,maji
taka na maji safi.
13 SME's Kuwawezesha Wafanyabiashara Kusaidia Serikali kutimiza
Industrial wafanyabiashara wenye au wamiliki wa malengo ya kukuza uchumi
Loan Viwanda vidogo na vya kati Viwanda vidogo kupitia viwanda na
kukidhi mahitaji yao ya na vya kati. biashara.
kifedha ya uendeshaji wa
kila siku.
14 Agri- Kuwawezesha wakulima Wakulima Kuwawezesha wakulima
Business wadogo wadogo waliopo wadogo wadogo kupata Pembejeo,mbegu,
Loan katika vikundi kupata ambao mbolea na vitendea kazi
mikopo ili kukidhi mahitaji wamedhaminiwa mbalimbali ili kuboresha
ya kilimo cha biashara. na wenzao katika kilimo cha biashara.
vikundi.
38
Hadithi za Mafanikio
Mteja wa Pamoja Loan: John Malima
Kwa majina naitwa John Malima,ni mteja ambaye nimenufaika na mkopo wa vikundi.
Nilijiunga na UTT Microfinance miaka miwili iliopita. UTT Microfinance imenisaidia
kukuza biashara yangu ya kutengeneza fredge ambazo zinatumika motuary. Nimeweza
kununua vifaa mbalimbali ambavyo nisingeweza bila mkopo. Nilianza UTT MFI na
mkopo wa TZS 500,000 na sasa nimefikia hatua ya kupata mkopo wa TZS 3,000,000.
Mafanikio mengine ni kwamba nimeweza kuajiri watanzania wenzangu nilianza biashara
yangu nikiwa na watu wawili na sasa nina watu sita ambao nimewaajir
Egom Investment Ltd ilianzishwa mnamo July 2013. Tulijiunga na UTT Microfinance Plc
2014 kama wateja wa mkopo wa Hati Malipo [Contract Financing]. Mkopo huo
ulituwezesha kufanya kazi mbali mbali za UTT Microfinance Plc. Tulifanya marekebisho,
matengenezo na ukarabati wa tawi lao la Zanzibar pamoja na Makao makuu ya UTT
Microfinance. Hii imetupa fursa ya kupanua wigo wetu wa biashara na kukutana na
39
fursa chanya kwa kampuni yetu. Kutaja wachache tumeweza kufanya kazi na UTT PID,
World Lung Foundation , NSSF na Amend ORG ( NGO ya kimarekani) . Binafsi
tumeweza kukuza kampuni yetu kwa kuajiri zaidi ya wafanyakazi wa msimu 300 kwa
mwaka na wafanyakazi wakudumu wawili. Kampuni yetu pia iko katika hatua za mwisho
za kupanda daraja kutoka daraja la 6 kwenda la 4. Tumeona mafanikio makubwa ya
kujiunga na UTT Microfinance Plc
40
16. MFUKO WA UWEZESHAJI WA MWANANCHI (MEF)
Mfuko wa Uwezeshaji wa Mwananchi (MEF) ni moja ya mifuko ya uwezeshaji ambayo
inatumiwa na Serikali katika kusaidia utekelezaji wa jitihada mbalimbali za uwezeshaji
wananchi kiuchumi. Mifuko huu ulizinduliwa tarehe 23 Januari,
2008 ambapo malengo yake makuu yamekuwa ni kuondoa
tofauti za kiuchumi baina ya watanzania.Katika utekelezaji wa
malengo hayo Mfuko huu umekuwa ukiwezesha utoaji wa mitaji
kwa wajasiriamali kupitia program ya udhamini wa mikopo
inayopelekea uanzishwaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi
miongoni mwa watanzania.
MEF iko chini ya usimamizi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi
(NEEC) , ambayo ni taasisi ya Serikali iliyoanzishwa mwaka 2005 kwa Sheria ya Taifa
ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (sheria namba 16 ya mwaka 2004) ikiwa na jukumu
la kusimamia, kufuatilia na kuratibu masuala yote yanayohusika na uwezeshaji
wananchi kiuchumi.
Mfuko huu unafanya kazi katika Mfumo wa kutoa dhamana za Mikopo kwa kushirikiana
na Mabenki na Taasisi za Fedha, ambapo kwa sasa unafanya kazi kwa kushirikiana na
Benki ya TPB(TPB Bank Plc), katika programu ya udhamini wa mikopo kwenda kwa
vikundi vya VICOBA na vyama vya Ushirika wa Kuweka na Kukopa (SACCOS).
Walengwa wakuu wa Mfuko huu ni vikundi vya kiuchumi kama vile Vikundi vya VICOBA
pamoja na Vyama vya Ushirika wa Kuweka na Kukopa (SACCOS) hususani SACCOS za
Wanawake, Vijana na Bodaboda.
.
Vigezo vya Utoaji wa Mikopo
1. SACCOS
i. SACCOS iwe imesajiliwa kwa mujibu wa sheria ya vyama vya ushirika.
ii. Iwe na Bodi iliyochaguliwa kidemokrasia na kupata mafunzo kuhusu uendeshaji
wa SACCOS.
iii. Iwe na kamati ya mikopo iliyopata mafunzo ya namna ya kujadili, kutoa,
kusimamia na kufuatilia mikopo yote inayotolewa na chama.
iv. Iwe na katiba na sera zinazosimamia uendeshaji wa shughuli za chama kama
mikopo n.k
v. Iwe na Kamati ya Usimamizi iliyopata mafunzo ya namna ya kusimamia SACCOS.
vi. Iwe na uzoefu wa kukopeshana usiopungua mwaka mmoja na kuwa na kiwango
kizuri cha marejesho kisichopungua asilimia 95.
vii. Iwe na mfumo mzuri wa utunzaji wa kumbukumbu za kiuhasibu za chama.
41
viii. Iwe na Ofisi inayotambulika.
ix. Utoaji wa mikopo uzingatie taratibu za ushirika kama kuwa na hisa na akiba
zinazotosha mkopo unaoombwa na mwanachama.
x. SACCOS itatakiwa kuweka asilimia 30(Cash Cover) ya kiwango cha Mkopo
itakayomba ambayo itatumika kama sehemu ya Dhamana yake kwa Mkopo
iliouomba
xi. Muda wa marejesho ya mkopo ni kati ya mwaka 1-2, hivyo hautazidi miaka
miwili.
xii. Kiwango cha Mkopo kwa Mwanachama mmoja mmoja katika SACCOS hakitazidi
Shilingi milioni 5.
xiii. Riba ni asilimia 13 kwa mwaka
xiv. Ada ya Mkopo ni asilimia 2
xv. SACCOS itakayohitaji kupata Mikopo katika Baraza la Uwezeshaji ni sharti ifungue
akaunti katika Benki ambayo inashirikiana na Baraza katika utekelezaji wa
Programu husika.
xvi. Mikopo yote itakayodhaminiwa na Baraza itatakiwa kukatiwa bima ya maisha ya
mkopo.
42
x. Kikundi kitatakiwa kuweka asilimia 30 (Cash Cover) ya kiwango cha Mkopo
kitakachomba ambayo itatumika kama sehemu ya Dhamana yake kwa mkopo
iliouomba.
xi. Muda wa marejesho ya mkopo ni kati ya mwaka 1-2 hivyo hautazidi miaka
miwili.
xii. Kiwango cha Mkopo kwa Mwanachama mmoja mmoja katika Kikundi cha VICOBA
hakitazidi Shilingi milioni 3.
xiii. Riba ni asilimia 13 kwa mwaka.
xiv. Ada ya Mkopo ni asilimia 2.
xv. Kila kikundi cha VICOBA kitakachohitaji kupata udhamini wa Mikopo katika
Baraza la Uwezeshaji ni sharti kifungue akaunti katika Benki ambayo
inashirikiana na Baraza katika utekelezaji wa Programu husika.
xvi. Mikopo yote itakayodhaminiwa na Baraza itatakiwa kukatiwa bima ya maisha ya
mkopo.
Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi
12 Barabara ya Kivukoni
S.L.P. 1734 Dar-Es-Salaam
Simu: +255 22 2137362
Simu/Nukushi: +255 22 2125596
Barua Pepe : neec@uwezeshaji.go.tz
Tovuti : www.uwezeshaji.go.tz
Makao Makuu
LAPF Towers
Bagamoyo Road
P. O. Box 9300
Dar Es Salaam
Tanzania
Simu: +255 22 2110621/2
Nukushi: +255 22 2114815
Barua Pepe : corporateaffairs@postalbank.co.tz
au tembelea Tawi lolote la Benki ya Posta lililopo karibu nawe
43