Professional Documents
Culture Documents
Maana Ya Saumu Za Sunna
Maana Ya Saumu Za Sunna
Saumu za Sunna
Saumu yoyote amabayo sio ya lazima na mtu anaifunga ili kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu U
Na saumu ya sunna ina fadhila kubwa na malipo makubwa. Katika Hadithi Al-Qudsy kutoka kwa Abu
Hureirah t Anasema: Amesema Mtume (saw): “Kila kitendo chema cha mwanadamu malipo yake
huongezwa, jema moja hulipwa kwa kumi mfano wake mpaka kufikia mara sabini. Anasema Mwenyezi
Mungu Mtukufu: Isipokuwa saumu, kwani hiyo ni yangu mimi, na mimi ndiye mwenye kuilipa”
[Imepokewa na Bukhari na Muslim.].
Kwa kauli ya Mtume (saw): (Atakayefunga Ramadhani, kisha akafuatiliza kwa kufunga siku sita za
Shawwaal, itakuwa ni kama aliyefunga mwaka mzima) [Imepokewa na Muslim.].
Sawasawa awe amezifunga siku sita hizi kwa pamoja kufuatana au siku mbalimbali zisizofuatana.
Kwa kauli ya Mtume (saw): (Hakuna masiku ambayo matendo mema ni bora zaidi mbele ya Mwenyezi
Mungu kuliko masiku haya – yaani masiku kumi ya Dhulhijjah – wakasema (maswahaba): hata jihadi kwa
njia ya Mwenyezi Mungu? Akema (Mtume): “Hata jihadi kwa njia ya Mwenyezi Mungu, isipokuwa mtu
aliyetoka (kwenda jihadi) yeye mwenyewe na mali yake, wala asirudi na chochote (yaani akafa vitani)”
[Imepokewa na Bukhari.].
Na masiku haya yakatiliwa nguvu zaidi na siku ya A’rafa kando na hajj – nayo ni siku ya tisa ya mwezi wa
Dhulhijjah; kwa kauli ya Mtume (saw): (Kufunga siku ya A’rafa nataraji kwa Mwenyezi Mungu
kusamehewa mtu madhambi ya mwaka kabla yake, na mwaka uliyo baada yake) [Imepokewa na
Muslim.].