Professional Documents
Culture Documents
Zingatia
Hakikisha umesoma andiko unalosimamia kabla ya kuanza kuomba, kumbuka Mungu analiangalia
neno lake apate kulitimiza.
SIKU YA 11.
A) Kumiliki Malango Ya Mtaa
1. Kumbu 12:2-3. Baba katika jina la Yesu, ninaamuru moto wa Mungu juu ya miungu, sanamu,
matambiko, maashera na madhabahu ya uovu Kimara, tunaamuru malango ya Kimara kuifungukia
Redeemers Assembly katika jina la Yesu.
2. 1 Wafalme13:2.Kwa Damu ya Yesu ninatabiri kinyume cha madhabahu ya wachawi na kila mahali
pa juu katika mtaa wa Kimara, Ee madhabahu na kiti cha wachawi teketea kwa moto na kuwa majivu
katika jina la Yesu.
3. Waamuzi 7:18.Baba katika jina la Yesu tunatangaza upanga wa Bwana na upan ga wa Redeemers
Assembly juu ya makuhani wa giza Kimara wanaoshindana na mafanikio ya Redeemers Assembly
katika jina la Yesu.
SIKU YA 12.
A) Kongamano La Mwanzo Mpya Tarehe 15 Hadi 20 Mwezi Wa Nane.
1. 1 Samweli 3:21.Ee Baba katika jina la Yesu jifunue tena kwetu kwa viwango vipya, tuonyeshe
utukufu wako katika kongamano letu la mwanzo mpya mwaka huu katika jina la Yesu.
2. Isaya 45:8.Ee Baba katika jina la Yesu fungua mbingu zako juu ya kongamano letu la New
Beginning, sababisha kamba zetu kutuangukia mahali pema katika mipango yote katika jina la Yesu.
3. Isaya 41:15. Ee Baba mwandae mtumishi wako Emanuel kupita kawaida kwa ajili ya hili
kongamano, mfanye chombo kipya kikali cha kupuria na ukombozi katika jina la Yesu.
SIKU YA 13.
A) Kuombea Tanzania.
1. Mathayo 6:9.Ee Baba katika jina la Yesu, tunaomba ufalme wako uje Tanzania ndani ya Bunge,
Mahakama, Serikali, Vyuo vikuu, Mashuleni, Mikoani katika jina la Yesu.
2. Kumbu 12:1-3.Ee Baba inuka tuma malaika wako wavunje madhabahu ya uchawi na uganga
iliyolishilia Taifa la Tanzania na watu wake katika umasikini katika jina la Yesu.
3. 1 Wafalme 3:12.Ee Baba mpe Raisi Joseph Magufuli na Mawaziri wake hekima na akili ya
kulitawala na kiliongoza Taifa hili katika njia zako katika jina la Yesu.
SIKU YA 14.
A) Kuangusha Madhabahu Ya Uovu Katika Familia Yako.
1. 1 Wafalme 13:1-2. Ee Baba katika jina la Yesu, inuka kwa mfungo huu kwa ajili ya familia yangu,
ninalaani madhabahu ya uovu iliyotushikilia mateka katika ulevi, uzinzi, mitala, umasikini, uchawi,
teketea kwa moto na kuwa majivu katika jina la Yesu.
2. Isaya 49:24-26.Wewe kuhani muovu wa madhabahu ya ukoo wangu, unayenuiza na kutoa kafara
kinyume cha mafanikio yetu, Bwana Yesu anakupokonya familia yangu leo na wewe utalishwa nyama
yako na kunywa damu yako katika jina la Yesu.
3. Zekaria 9:11-12.Kwa Damu ya Yesu ninamuamuru kila mmoja katika familia yangu kutoka katika
gereza na shimo la mateso siku ya leo katika jina la Yesu.
SIKU YA 15.
A) Kuombea Kanisa la Kristo Dar es salaam.
1. Yoshua 5:9. Ee Baba inuka viringishia mbali aibu ya kanisa lako Dar es salaam majengo mabovu,
watu wachache, umasikini wa washirika na wachungaji, geuza umateka wetu katika jina la Yesu.
2. Isaya 2:2-3. Ee Baba inua mlima wa nyumba yako Dar es salaam, uweke imara juu ya madhabahu
za uchawi na uganga, acha watu walijilie kanisa lako Dar es salaam makundi makundi katika jina la
Yesu.
3. Mambo ya walawi6:12. Ee Baba katika jina la Yesu, washa moto wako juu ya madhabahu ya
kanisa lako Dar es salaam, usababishe uwake daima wala usizimike.