A. Ayubu 40:10. Haya! Jivike sasa fahari na ukuu;Jipambe heshima na enzi.
Baba katika Jina la Yesu tunakushukuru kwa kutupamba kwa heshima na enzi katika mwezi wa chombo cha heshima.
B. Yoshua 5:9. BWANA akamwambia Yoshua, Siku hii ya leo nimeivingirisha
hiyo aibu ya Misri iondoke juu yenu. Kwa hiyo jina la mahali pale likaitwa Gilgali, hata hivi leo. Baba katika Jina la Yesu tunakushukuru kwa kuviringishia mbali nasi aibu na kutuvika heshima kwa kutufanya vyombo vya heshima na kutututumia kwa ajili ya utukufu wako katika Jina la Yesu.
2. Shukrani kwa Neno la Mwaka
A. Isaya 61:7. Badala ya aibu yenu mtapata maradufu, na badala ya fedheha
wataifurahia sehemu yao; basi katika nchi yao watamiliki maradufu; furaha yao itakuwa ya milele. Baba katika Jina la Yesu tunakushukuru kwa kumvika kila mshirika wa Huduma hii heshima maradufu kwenye kila eneo la maisha yake na kuondoa aibu ya magonjwa, utasa, umasikini na ukosefu wa kila namna katika Jina la Yesu.
Hesabu 23:19. Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo