You are on page 1of 11

XAVERIAN STARS (YCS) CHOIR

ANIMATION OF WEDDING

MASS FOR

CECILIA AND JACOB

AT ST. MICHAEL CATHOLIC

CHURCH NAPETET ON 9TH MAY,

2015.

“Siondoki Kando
Yako Na Usiondoke Kando Yangu Hadi Kifo
Kitutenganishe.
1
PROCESSION.

TWENDE NYUMBANI MWA BWANA


TN: Twende nyumbani mwa bwana (hoye)
Twende nyumbani mwa bwana hoyetuimbe tushangilie
TN: Tupige vigelegele
Tupige makofi hoye hoye.
1. Twende tumsifu kwa nyimbo na zaburi wakristu -(hoye).
Tumsujududie twende tukamwabudu wakristu- (hoye)
2. Tujitayarishe kwa neno lake bwana wariest. - (hoye)
Tumsujudie twende tukamwabudu wariest. -(hoye)
3. Twende tumsifu kwa ngoma na kayamba wariest. -(hoye)
Tumsujudie twende tukamwabudu wariest. -(hoye)

NALIFURAHI SANA
Nalifurahi sana waliponiambia na twende nyumbani ,
Nyumbani mwake ee Bwana x2
1. Miguu yetu imesimama katika malango ya Yerusalemu oh
2. Yerusalemu mji uliyojengwa kama ule mji ulioshikamana oh
3. Makabila yote ya Israel, walishukuru jina lake bwana oh
4. Mmewekwa hukumu ya haki katika ukoo wa mfalme Daudi oh
5. Utakieni Yerusalemu amani , na wafanikiwe wakupendao oh
6. Kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu ninakuomba upate fanaka oh.

MWIMBIENI BWANA

1. Mwimbieni bwana (wimbo ule mpya) mwimbieni bwana (mataifa yote)


kwa maana bwana (mungu ametenda mambo ya ajabu)

Pazeni (sauti) imbeni (kwa shangwe) sifuni (jina lake takatifu)X2

2. Ingieni leo (malangoni mwake) ingieni nyote (kwa shukurani kubwa)


mshukuruni bwana (mungu wa majeshi kwa kuwa ni mwema).
3. Njooni tuabudu (njooni tusujudu) tupige magoti (mbele zake mungu)
tumfanyie shangwe (hekaluni mwake leo asubuhi)
4. Hubirini kwa (sauti ya kuimba) tangazeni hadi (mwisho wa dunia)
seemeni bwana (mungu amewakomboa watu wake.
5. Mbingu na dunia (mungu ameumba) bahari ni yake (na viumbe vyote)
mataifa yote (hata makabila sifuni milele.

2
UTUHURUMIE (Mitume mass)
Bwana utuhurumie
Sisi wakosefu Bwana – Bwana utuhurumie x2
Ee kristu (ee kristu) kristu utuhurumie-ie
Bwana utuhurumie
Sisi wakosefu Bwana – bwana utuhurumie x2.

UTUKUFU(MITUME MASS)

1. Utukufu kwa mungu juu,(kwa mungu juu) na amani kwa watu


wenye mapenzi memaX2

Tunakusifu na tunakuheshimu twakuabudu ee bwana


twakutukuzaX2

2. Tunakushukuru ee bwwana kwa ajili ya utukufu wako mkuu, wako


mkuu, ee bwana ee bwana mungu mfalme wa mbingu, mungu
babba ee mungu baba……baba mwenyezi.
3. Bwana yesu mwana wa pekee , ee bwana mungu, mwana kondoo
wa mungu baba, wa mungu baba… mwenye kuziondoa dhambi za
dunia, utuhurumie pokea maombi yetu.
4. Kwani ndiwe uliye pekee yako ee bwana, pekee yako mtakatifu
yeye kristu….uu pamoja naye roho mtakatifu, katika utukufu wa
mungu baba amina.

MASOMO

NASIKIA SAUTI.

1. Nasikia sauti nzuri kama ya malaria, Ni sauti toka mbinguni, sauti ya


Mungu
Aniita mimi niende nikamtumikie, Anitume shambani mwake nikavune
yote

Umeniita, nimeitika wito, nakuja kwako leo Najongea mbele zako Bwana
nipokee mimi Niko tayari, nimeyaacha yote, najikabidhi kwako Unitume
popote na mi nitakwenda haraka
3
2. Ninaenda mimi naenda, ninaenda mwenyewe, Ninaenda mbele za Bwana,
sitarudi nyuma
Ndugu zangu na marafiki, mniache niende, Nikafanye kazi ya Bwana,
nitakapotumwa
3. Nilitazama moyo wako, moyo wako mwanangu, Hata kabla hujazaliwa,
nilikutambua
Nilikuteua mapema kati ya ndugu zako, Uwe kuhani wangu mimi, kuhani
mkuu
4. Shamba lake Bwana ni kubwa na mavuno ni mengi, Wavunaji ndio
wachache nitakwenda mimi
Nakuomba sana ee Bwana, nipeleke shambani, Nikavune mavuno yote
yaliyo tayari.
5. Uwe nami siku kwa siku, Bwana usiniache, Unikinge na majaribu nilinde
daima
Nipeleke habari njema, ulimwenguni mwote, Watu wote wakutambue,
wakugeukie

KWA IMANI YANGU

(Kwa imani yangu pia matendo na maneno nitalihubiri injili ya bwana


siku zote) X2 Nitalitangaza neon hili pote , mataifa yote , yatakusifu wewe
(neon hili ndilo neon la wokovu) X2

1. Neno hili la bwana ndilo njia ya wokovu wetu, (yatupasa nasi sote
tulipokee)X2
2. Neno hili la bwana ni faraja ya watesekao, (yatupasa nasi sote
tulipokee)X2
3. Neno hili la bwana nit ulizo la moioyo yetu, (yatupasa nasi sote
tulipokee)X2

4.Neno hili la bwana ndilo taa la maisha yetu, (yatupasa nasi sote
tulipokee)X2

UNINYUNYIZIE MAJI
1. Uninyunyizie maji (Bwana) *2
Unioshe nitakate (kweli) Niwe mweupe kabisa *2
2. Mimi ni mwenye dhambi (Bwana) *2
Unioshe nitakate (kweli) Niwe mweupe kabisa *2
3. Natamani nije kwako (Bwana) *2
Unioshe nitakate (kweli) Niwe mweupe kabisa *2

4
4. Naingia nyumba yako (Bwana) *2
Unioshe nitakate (kweli) Niwe mweupe kabisa *2
5. Niuone uso wako (Bwana) *2
Unioshe nitakate (kweli) Niwe mweupe kabisa *2
6. Nifurahi milele (Bwana) *2
Unioshe nitakate (kweli) Niwe mweupe kabisa *2

WEDDING SONGS

HARUSI KIDEDEDEDE
1. Bwana harusi na bibi harusi , leo mmefunga ndoa ya maisha kaeni kwa
amani kidededede.
Tenor: upendo wenu umethihirika - Uyani kwenu bamba ishini
tototo
Uzuri wenu hakuna kifani……………….
Na nyumba yenu imebarikiwa……………
2. Jitulizeni mjizikie sukari, siku ya leoni yenu furahini mmepambwa maua
mnapendeza.
3. Bwana harusi pagawa changamka, Bibi harusi chachawa, chezacheza,
penzi lenu leo limekamilika.
4. Mapenzi yenu kweli yatasitawi, haiku yatasitawi yatamea kama ule
mwerezi wa Lebanoni.
5. Baraka zake Mungu ziwashukie, kaeni pasipo shida siku zote nyumba
yenu iwe hekalu la Mungu.

WEWE NI KIPENZI CHANGU


Wewe ni kipenzi changu, wewe ni kizuri changu tulizo la moyo wangu, chaguo
langu (chaguo langu).Tutaishi nawe daima, nitakufuata popote utakakokwenda
tutatembea pamoja (pamoja nawe).
1. Nakupenda ee mwenzangu, nimekupa pendo langu nawe nipe penzi lako
kwa moyo wako.
2. Jina langu ni kipenzi, jina lako ni kitulizo, njoo
3. Nakuita ee mwenzangu, nakuita njoo kwangu, njoo nipe agizo la moyo
wangu
4. Siondoki kando yako, siondoke kando yangu, kifo ndicho kitakacho
tutenganisha.

POKEA HII PETE

5
1. Pokea hii pete ee mwenzangu, iwe ishara ya pendo langu, na uaminifu
wangu kwako.
Nakupenda hakikaNakupenda ajabu Wewe wangu daima mimi wako
wewe
Tutahishi pamojaTutakula pamoja- hadi kifo kifike kitutenganishe
X2.
2. Jukumu langu ni kukupenda, wakati war aha na shida, na wewe kwangu
weka heshima.
3. Safari hii ndefu ya maisha,imeanza leo siogope tutatembea bila kuchoka.
4. Milima na mabonde ya maisha, tutapanda tena tutashuka tukiwa pamoja
siku zote.

HERI YENU
Heri yenu ninyi msitengane oh mkavunje ile agano x2
Mungu amewaonganisha binadamu asiwatenganishe x2
1. Na mwanamke atawacha wazazi wake, ataungana na yule mume wake x2
2. Na mwanamme atawacha wazazi wake , ataungana na yule mke wake x2
3. Na bwana Mungu alimuumba Adamu, akampa Hawa awemsaidizi wake
x2
4. Alicho unganisha Mungu baba mwenyezi hakuna atayeitenganisha x2
5. Mue na upendo mkaishi kwa amani, na Mungu baba ataibariki ndoa yenu.

TEMBEA POLEPOLE
1. Tembea polepole, tembea baba tembea kwa madaha, tembea mama
ingia hekaluni mwa mungu wetu mpate kutimiza ahadi zenu

Sikieni vigelegele, sikieni sauti nzuri tazameni maua hayo


yapendezayo, jongeeni mbele za bwana, jongeeni mfungwe pingu,
msivunje nadhiri zenu msitenganeX2

2. Harusi hii ya leo ni yako bwana, mapambo haya yote ni yako bibi,
upendo uzidishe kwa bibi yako heshima uongeze kwa bwana wako.

3.Harusi si chakula wala vinywaji, harusi ni furaha ya siku zote ,


maisha ni matamu mkipendana muendapo njiani mmeshikana.

4.Shetani ni mnyang’anyi asiingie asije ivuruga hii ndoa yenu


,mchunge mke wako asiponyoke,mlinde mume wako asitoroke.

6
5.Mkeo atakuwa kama zabibu ,uzaao matunda nyumbani mwako
,watoto muwapende na kuwalinda,muwafundishe yale ya uwinguni.

SADAKA
WE DO GIVE TO GOD
We do give to God, the splendid Lord; we do pray you Lord, our grand
joyous gifts, then Lord we shall sing of your gracious life.
1. Bread and wine we offer to the living Lord,
Together in joyful tide praise him God of love
2. Our hearts we offer to the living Lord
Together in joyful tide praise him Lord of love
3. Our joy we offer to the living Lord
Together in joyful tide praise him Lord of love
4. Our world …………………………………..
5. Our wealth …………………………………..
6. Our love ……………………………………….
7. Our lives …………………………………….

ACHENI VISINGIZIO
Bass: (Acheni visingizio wanadamu)X2
Wote:(Acheni visingizio kwamba hali ngumu)X2 (Nendeni mkatoe )X2
Nendeni mkatoe sadaka kwa bwana}X2

1) Siyo ninyi wenye magari ya kifahari…..(mnaodai hali ni ngumu)


Siyo ninyi wenye fedha nyingi mifukoni………

2) Siyo ninyi wenye majumba ya kifahari……….


Ndani yake mmejaza vitu vya thamani………..
3) Siyo ninyi mliovuna mazao mengi…………..
Siyo ninyi mnapokea mishahara…………….

4) Msidhani mmepata kwa uwezo wenu……….


Bali ni mungu aliye wajalia hayo……………

5) Kumbukeni mjane alotoa dinari……………..


Hakubakiza chochote mfukoni mwake………

7
ANAMIYIANG’O
Anamiyiang’o nyasae wuora madimo riga, inmichiwo ngima mane Adamu
wuora noseko gawito x2
(Abiro giilo (duto), Abiro ging’uono (bende)Abiro gimor (koro) akilo mich
mawangolo )x2
1. Pesa mawagole ofuke wan wakelogi gimor ye igweth gi jalamo
wanwakelogi giera
2. Cham mawagolo e pwothe…………………………..
3. Mwandu mawagolo e miere……………………………
4. Rombe mawagolo e kunde ……………………………..
5. Thok mawagolo e kunde …………………………………

BABA TWALETA VIPAJI

1. SP/ALT: baba tunaleta vipaji twakuomba sana pokea – baba tunaleta


twakuomba sana pokea
Twaja kushukuru kwa yote ulotujalia wanao – “ “

(SP:Baba tunasema) asante asante (ALT:kutupa uzima) asante asante

(TN: kwa kutukomboa) asante asante (BS: kutuweka huru) asante asante

2. Mkate na divai twaleta twakuomba sana pokea –


Ndiyo kazi yetu wanao twakuomba sana pokea –
3. Mazao ya mashamba twaleta twakuomba sana pokea –
Hata ni kidogo twaleta twakuomba sana pokea –
4. Nazo fedha zetu twaleta twakuomba sana pokea –
Utupe baraka twaleta twakuomba sana pokea –

MTAKATIFU(MITUME MASS)
Mtakatifu bwanaX3 Mungu wa majeshi, Mbingu na dunia( kweli zimejaa)X2
Utukufu wako.

T/A:HosannaX2 Juu mbinguni,


ALL: hosanna juu, Hosanna juu mbinguniX2
ALL:Mbarikiwa anaye kuja , anaye kuja kwa jina la bwanax2
T/A:HosannaX2 Juu mbinguni,
ALL: hosanna juu, Hosanna juu mbinguniX2

8
AMINA
Amina x5

AMANI
MAK’ TINGA
1. Bass; makting’a tingi, teyong’ x2
Ee rwoth’ rubang’ maktinga tingi teyong’
Menyut rwoth rubang’ moru wadutu x2
2. Makting’a ting’i aduong’ x2
3. Makting’a ting’i amin x2

KUPOKEA

AMETUALIKA

Ametualika kwenye karamu yake bwana tule mwili wake bwana tunye
damu yake, tumejaaliwa sote chakula cha roho zetu bwana anatuita kutushibisha
roho zetu.

i. Mwili wake bwana yesu ni chakula cha roho zetu, damu yake
bwana yesu ni kinywaji cha roho zetu, kilichoshuka kutoka kwa
baba waumini wote tujongee meza ya bwana tukale chakula cha
mbinguni.
ii. Njoni maskini maskini, viwete, vipovu na wagonjwa meza
imeandaliwa na bwana wetu yesu kristu kwa heshima kubwa kwa
upole na kwa unyenyekevu tujongee wote tupate chakula cha roho
ni mwili wake yesu kristu.

NIRUHUSU YESU WANGU


Niruhusu yesu wangu nijongee meza yako unisamehe dhambi
mwokozi uje rohoni mwangu uniokoee, Njoo kaa ndani yangu
name nikae ndani yako ili nipate amani tele ndani ya roho
yangu nifarijike.
SP:Wewe bwana wanijua, wanijua
A/T/B:Wewe bwana wanijua hata nafsini mwangu
ALL:Wewe ndiwe tabibu pekee wa roho yangu tena
ndiwe kimbilio languX2.

9
i. Tazama yesu wangu ninajongea karamu yako, pengine
kwako sikustahili kuijongea –unihurumie ee yesu wangu
unisamehe.
ii. Hakika kwako bwana makosa mengi nimeyatenda,
ubinadamu wangu siwezi kuficha kwako bwana-
unihurumie………….
iii. Ni wazi yesu wangu unaujua udhaifu wangu, sina cha
kujitolea mbele yako ee yesu wangu-
unihurumie………………

TWENDENI MEZANI
I. Angalieni wenyewe tazameni pendo la bwana,
(kweli) Amejitoa mwenyewe awe chakula, anatuita
twendeni tule mwili na tunywe damu, (kweli) ni cha
mbinguni che uzima.

Twendeni mezani pake


Twendeni atualika
Twendeni tule chakula kutoka mbinguni

II. Ni pendo kuu zaidi ni upendo wa kipekee (kweli) mtu


kutoa mwiliwe kwa ndugu zake, usisite ndugu twende
tule mwili na tunywe damu, (kweli) tuushiriki upendo
ule wa yesu.

III. Mwili wakeni chakula , damu yake ndicho kinywaji ,


tule tushibe na tunywe tuburudike , ni chakula chenye
nguvu ni chakula cha wasafiri, ni kinywaji chetu sisi
twendao kwetu.

IV. Tusipokula mwiliwe tena tusipokunywa damu,


hatutapata uzima ule wa mbingu, yeye ni chakula
kweli yeye ndiye kinywaji kweli, tule na tunywe
tupate uzima wa bure.

10
V. Milele tutafurahi tutaishi na bwana yesu, tukishinda
majaribu ya ulimwengu, tunapata nguvu nyingi
tunapokula mwili wake , tunashinda majaribu
tukinywa damu.

SHUKURANI

TUNAKUSHUKURU

(Ee bwana mungu baba wetu tunakushukuru kweli{hakika} kwa kutulinda wiki
nzima ee baba asante sana)X2

Kwa mwili wako tumeshiba, kwa damu yako tumeburudishwa twakushukuru


mungu wetu kwa wema wako woteX2

1) Umetupa uhai usio na kipimo(wanao twakushukuru kwa kutujalia)X2


2) Tumepata na neno kiroho tumejawa, (niseme nini baba bali
kukushukuru)X2
3) Aulae mwili wako pia anywae damu atapata uzima, (uzima wa milele)X2

MWISHO

Baraka za mungu zishuke na neema zake

Baraka za mungu zishuke na neema zakeX2

1) Mungu awajalie , maisha mazuri, muishi kwa amani, siku zenu zoteX2
2) Mkumbukeni mungu, siku zenu zote, ili azibariki, kazi zenu zoteX2
3) Uzao wenu wote, uwe na Baraka, mjaliwe watoto wenye afya njemaX2
4) Palipo na vikwazo, muiteni mungu, atawasaidia, siku zenu zoteX2

BY: ASINYEN LOBEI CAROLINE

CHOIRMISTRESS

EDITOR P. LOKS

11

You might also like