Professional Documents
Culture Documents
JINSI YA KUFANYA MAKADIRIO YA GHARAMA ZA UJENZI WA NYUMBA YAKO - S1 - by Judith Mwanri - Medium
JINSI YA KUFANYA MAKADIRIO YA GHARAMA ZA UJENZI WA NYUMBA YAKO - S1 - by Judith Mwanri - Medium
Judith Mwanri
Follow About
1. Uwe na ramani yenye vipimo ili kujua ukubwa wa jengo lako. Ramani inachorwa na
wasanifu majengo wataalamu ambao wanasomea — wataalamu hawa wanahitimu
katika vyuo vinne tu hapa nchi navyo ni Ardhi University (chuo kikuu), na vyuo vya kati
Ardhi Institute — Tabora, Ardhi Insitute — Morogoro, Institute of Lands Dar es Salaam.
2. Ufahamu aina ya material ama tofali utakazo tumia, kama ni hydraform, tofali za
kuchoma ama blocks, hii ni kwasababu tofali zina tofautiana size ama ukubwa hivyo
hata idadi yake itakuwa tofauti. Tofali zipo za aina tatu, ukubwa wake ni (length x width
x thickness/urefu x upana x unene)
HYDRAFORM; 90 mm x 240 mm x 40 mm
Get started Open in app
Hapa tuta tumia mfano wa nyumba hii yenye vyumba viwili-kimoja kikiwa na choo/bafu
ndani, sebule, jiko, choo cha wageni na vibaraza viwili; kufanya mahesabu ya tofali zetu.
Sasa kujua urefu wa kuta zote, utatakiwa kujumlisha urefu wa kuta zote
Kwenye mchoro wetu pale juu nime weka namba kila kuta hivyo itakuwa kama
ifuatavyo {vipimo vipo katika milimita (mm)}.
Ukuta 1= 6,500 mm; ukuta 2 = 9,150 mm; ukuta 3 = 4,000 mm; ukuta 4 = 4,000 mm;
ukuta 5 = 9,450 mm
Ukuta 6=11,046 mm, ukuta 7=6196 mm +3200 mm, ukuta 8=9,101 mm, ukuta 9
=3,060 mm, ukuta 10 = 2,900 mm
Hapa kama utajenga nyumba ya kozi 13 maana yake ni kimo cha 3000 mm
Sasa kumbuka tuna sehemu za wazi ambazo hizi hazihitaji tofali, mfano milango,
madirisha na sehemu za wazi za vibaraza
Tuna madirisha 6 yenye urefu 2,000 mm & kimo 1,800 mm= 2000 x 1800 sawa na
3,600,000 mm
sasa, tuna madirisha sita yenye vipimo sawa hivyo 3,600,000 x 6 = 21,600,000
Tumia dirisha 1 lenye urefu 1,400 na kimo 1,500 = 1,400 x 1500 sawa na 2,100,000
mm
Tuna dirisha 1 lenye urefu 1,000 na kimo 1,800 = 1,000x1, 800 sawa na 1,800,000 mm
Get started Open in app
Tuna madirisha 2 yenye urefu wa 800 na kimo 600 = 800x600 sawa na 480,000 mm
Tuna milango 9 yenye urefu wa 900 na kimo 2,400 = 900 x 2,400 sawa na 2,160,000
mm
Uwazi wa vibaraza jumla uref 10,010 kimo 2,400 =10,010 x 2,400 sawa na 24,024,000
mm
Sasa urefu wa msingi wako utategemea na nature ya eneo lakini tuchukulie utakuwa na
urefu wa 900 mm, ambapo ni sehemu tambarare (isiyo koro )
Kwahiyo kupata tofali tutalazimika kuchukua jumla ya ukubwa wa kuta ukiwa umetoa
uwazi na jumla ya eneo la kuta za msingi kisha tuta gawanya kwa eneo la tofali moja
135,885,000+61,742,700= 197,627,700 mm
Hapa utahitaji kuongeza asilimia kidogo ya tofali kwaajili ya zile zitakazo vunjika na
ngazi pia, tutatumia 5%, kwahiyo jumla ni tafali 1909+ 0.05(1909) = 2,004.45 ≈
2,000 tofali
NB: kumbuka haya huwa ni makadilio, hivyo sio lazima yawe sawa kwa asilimia 100,
lakini mara nyingi yanakaribia ukweli halisi kwa asilimia kubwa sana
Hapa nazungumzia tofali ambazo wengi wanaziita za block, ambazo kitaalamu zinaitwa
SAND CEMENT BLOCKS
-hivyo tofali hizi zitahitaji cement na mchanga Zaidi kuliko zile za kusimama (inch 5)
KANUNI
Hivyo ukichukulia zile tofali 700 za msingi kwenye ule mfano wetu itakuwa ifuatavyo
-Tofali hizi mara nyingi hujengwa kwa kusimama hivyo hazili mchanga na cement
nyingi kama zile za msingi
KANUNI
Hivyo ukichukulia tofali 1,300 za kuta kwenye ule mfano wetu, itakuwa kama ifuatavyo
NB: (ikumbukwe watu wengine hufanya mfuko 1 wa cement unajenga tofali 70 mpaka
90 za kuta, za kusimama), pia hii ni ili kupunguza gharama.
Karibu!
Get started Open in app
Ujenzi Nyumba Tanzania Makadirio Ya Gharama Construction Costing