You are on page 1of 3

Kutoka kwa; Juma T.

Salum
Kwenda kwa; Mkurugenzi
Tarehe; 1.02.2021

Assalaam Aleikum Mkurugenzi


Nimepitia dokezo la uanzishwaji na uendeshaji wa mradi wa mafuta na kwa heshima na
unyenyekevu mkubwa naomba kuwasilisha mchango wangu kwa maandishi kama
ifuatayo;
1. Eneo la mradi limewekewa TZS;360,000,000=, kuonyeshwe mchanganuo kwamba
kitajumisha ununuzi wa eneo lenyewe, gharama za ufutiliaji, gharama za uhaulishaji
kutoka katika jina la muuzaji kuja katika jina la UTAHIZA, gharama za Sheha,
mwanasheria na kwa kuwa katika dokezo hakuna kipengere cha usafishaji/
ushindiliaji wa eneo, nashauri kijumuishwe katika gharama hii kama kikihitajika.
2. Ujenzi wa ofisi imewekewa TZS;107,591,000=, mchanganuo uboreshwe kuonyesha
idadi ya vyumba vya ofisi na ukubwa, flour itakuwa ya saruji, terazo au tiles, kama ni
tiles zitakuwa za ceramic, porcelain au granite, madirisha yatakuwa PVC, aluminium
au mbao, kama ni mbao basi tuseme ya mninga, mkongo na kadhalika, katika paa
tusema kama bati za kawaida, slab tukitegemea kuongeza kitu kingine juu, na
kadhalika. Muhimu kila kipengere katika ofisi kiguswe wajumbe wawe na taswila ya
ofisi wanayotarajia kumiliki.
3. Samani (Furniture and fittings) kimewekewa TZS;2,000,000= kwa tano na kupata
jumla TZS;10,000,000=, mchanganuo uwepo kuonyesha samani zinazotarajiwa aina
na idadi ya viti, meza, makabati, fittings, na kadhalika, zitakuwa mbao au fibreboard
au chuma na kadhalika.
4. Ujenzi wa uzio umewekewa TZS;35,000,000= mchanganuo unahitajika kuonyesha
urefu wa ukuta, idadi ya tofali, lovers, na kadhalika zitakazohitajika na kutumika
katika ujenzi wa uzio.
5. Uwekaji wa interlock umewekewa TZS; 25,000,000=, mchanganuo unahitajika
kuonyesha idadi ya squire meters zitakawekewa na gharama kwa kila squire meter.
6. Uchimbaji na uwekaji wa matank umewekewa TZS; 10,000,000= kwa kila moja na
kwa matatu kutagharimu TZS; 30,000,000=, kunatakiwa maelezo kuonyesha kama
kwamba bila kujali ukubwa wa tank za gharama za uchimbaji na uwekaji wa matank
ziko sawa.
7. Usimamizi wa mradi umewekewa TZS;10,000,000=, kunahijika mchanganuo
kuonyesha matumizi yatakavyokuwa yanafanywa kwa kila week na kila mwezi,
hatimae kupata ya mwaka mzima.
8. Matumizi;
a) Kumeonyoshwa mishahara jumla ya TZS; 7,000,000=, kunatakiwa mchanganuo
kuonyesha gharama kwa mwezi hatimae kupata ya mwaka, kwa kuwa
TZS;7,000,000=, ukigawa kwa miezi kumi na mbili, TZS;583,333=, hivyo,
kumaanisha kwamba muundo wetu wa mishahara haiko constant throughout the
year.
b) Kumeonyeshwa michango ya ZSSF asilimia 10% ya TZS;700,000= kunahitajika
mchanganuo kuonyesha gharama kwa mwezi na hatimae kupata ya mwaka,
hata mishahara yetu haiku constant throughout the year.
c) Kumeonyeshwa malipo ya umeme ya TZS;500,000=, kunahitajika mchanganuo
kuonyesha gharama kwa mwezi na hatimae kupata ya mwaka, hata hivyo, kiasi
hicho ni sawa na TZS;41,667=, kwa matumizi ya kituo cha mafuta ni kidogo
sana.
d) Kumeonyeshwa malipo ya ZRB ya dola 1000 kuzidisha exchange rate ya
TZS;2,300, utapata TZS;2,300,000=, lakini katika matumizi kumewekwa
TZS;191,666.67, kunahitajika maelezo.
e) Kumeonyeshwa malipo ya ZURA ya dola 500 kuzidisha exchange rate
TZS;2,300=, utapata TZS;1,150,000=, lakini katika matumizi kumewekwa
TZS;95,833.33, kunahitajika maelezo.
f) Haukupunguza gharama za usimamizi wa mradi, ambazo umeweka
TZS;10,000,000=, ni sehemu ya gharama za uendeshaji zitapunguza faida
tarajiwa.
g) Haukuonyesha gharama za maji, kwa mwezi na hatimae mwaka, ni sehemu ya
gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
h) Haukuonyesha gharama za BIMA, kwa mwezi na hatimae mwaka, ni sehemu ya
gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
i) Haukuonyesha gharama za SDL, ambazo ni asilimia 5% kwa kila mwezi kwa
jumla mishahara yote kwa mwajiri mwenye wafanyakazi kuanzia wanne, hivyo,
5% ya TZS;7,000,000= na kupata TZS;350,000=, jumla TZS;4,200,000= kwa
mwaka, ni sehemu ya gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
j) Haukuonyesha gharama za ulinzi, haukusema kwamba katika mishahara kuna
sehemu ya malipo ya mishahara ya ulinzi, kama haipo ionyeshwe, ni sehemu ya
gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
k) Hakuonyesha depreciation formula na rates zitakazotumika, ni sehemu ya
gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
l) Haukuonyesha gharama za auditors, ni sehemu ya gharama za uendeshaji,
zinapunguza faida tarajiwa.
m) Haukuonyesha gharama za simu, ni sehemu ya gharama za uendeshaji,
zinapunguza faida tarajiwa.
n) Haukuonyesha gharama za stationary, wino, kalamu na kadhalika, ni sehemu ya
gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
o) Haukuonyesha gharama za viburudisho katika vikao vya wawekezaji au
wafanyakazi, ni sehemu ya gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
p) Haukuonyesha gharama ya vifaa usafi, cleaning materials, ni sehemu ya
gharama za uendeshaji, zinapunguza faida tarajiwa.
9. Haukuonyesha baada ya kupunguza matumizi na kupata faida, malipo
yatakayofanywa TRA kama kodi, income tax katika biashara ya mradi wa mafuta
ambayo ni asilimia 30% ya faida yote.
10. Haukuonyesha mgawanyiko wa faida baada ya kodi, asilimia ya kubaki katika mradi,
kuwa sehemu ya mtaji wa kuendeshea mradi na asilimia itakayogawanywa kwa
wawekezaji, ambao utawakata kila mmoja 10% katika malipo yao ya kuwasilisha
TRA, kama interest on dividends.
11. Haukuonyesha mchanganuo wa mishahara kurahisisha kutambua wanaowajibika
kukatwa PAYE na kuwasilisha TRA, kwa kuwa kisheria, mwajiri yeyote anaelipa
mshahara kupindukia TZS;180,000= kwa Zanzibar, lazima akate kwa kiwango
kilichobainishwa katika jedwali na kuwasilisha TRA, lakini sio sehemu ya gharama
za uendeshaji, hivyo, halipunguzi faida tarajiwa.
12. Dokezo lionyeshe mchanganuo wa mradi kikamilifu katika kila kipengere pamoja na
haki, mipaka, wajibu na yawepo makubaliano ya uwekezaji, yawepo maandishi
kabla ya uchangiaji watu wajipime na waamue kuwekeza, liwe specific liondoshe
maelezo ya jumla jumla.
13. Nashauri kila kipengere kijadiliwe kwa kina, kieleweke, penye mapungufu/ utata
pajazwe/ patatuliwe, kurahisisha utekelezaji kulingana na makisio, kuepusha
kuvuruga makisio tuliopitisha, tuzingatie kwamba tukishindwa kupanga tumepanga
kushindwa.

Naomba kuwasilisha kwa hatua zifaazo

You might also like