Professional Documents
Culture Documents
STADI ZA KAZI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
ii
YALIYOMO
DIBAJI ............................................................................................................................................ IV
1.0 UTANGULIZI ..................................................................................................................... 1
2.0 TATHMINI YA UFAULU WA WATAHINIWA KWA KILA SWALI ........................ 2
2.1 SEHEMU A: MASWALI YA MAJIBU MAFUPI .................................................................... 2
2.1.1 Swali la 1: Maandalizi ya Ufundishaji.......................................................................... 2
2.1.2 Swali la 2: Ushonaji wa Nguo ...................................................................................... 4
2.1.3 Swali la 3: Kilimo, Ufugaji na Uvuvi ........................................................................... 7
2.1.4 Swali la 4: Biashara Ndogo Ndogo .............................................................................. 9
2.1.5 Swali la 5: Ufundishaji ............................................................................................... 12
2.1.6 Swali la 6: Udobi ........................................................................................................ 15
2.1.7 Swali la 7: Kilimo, Ufugaji na Uvuvi ......................................................................... 18
2.1.8 Swali la 8: Sanaa za Maonesho .................................................................................. 22
2.1.9 Swali la 9: Muziki ...................................................................................................... 24
2.1.10 Swali la 10: Sanaa za Maonesho ............................................................................ 27
2.2 SEHEMU B: MASWALI YA INSHA................................................................................... 29
2.2.1 Swali la 11: Kilimo, Ufugaji na Uvuvi ....................................................................... 30
2.2.2 Swali la 12: Upishi ..................................................................................................... 34
2.2.3 Swali la 13: Ufundishaji ............................................................................................. 39
2.2.4 Swali la 14: Upimaji ................................................................................................... 42
3.0 UCHAMBUZI WA UFAULU WA WATAHINIWA KATIKA MADA....................... 48
4.0 HITIMISHO ...................................................................................................................... 48
5.0 MAPENDEKEZO ............................................................................................................. 49
KIAMBATISHO .............................................................................................................................. 50
iii
DIBAJI
Baraza la Mitihani la Tanzania limeandaa taarifa ya uchambuzi wa majibu ya
watahiniwa wa Mtihani wa Kuhitimu Mafunzo ya Ualimu Daraja la A kwa somo la
Stadi za Kazi. Taarifa hii imeandaliwa ili kutoa mrejesho kwa wanachuo,
wakufunzi, waandaa sera, wadau wa elimu na jamii kwa ujumla jinsi watahiniwa
walivyojibu maswali ya mtihani.
Athumani S. Amasi
KATIBU MTENDAJI
iv
1.0 UTANGULIZI
Mtihani wa somo la Stadi za Kazi kwa watahiniwa wa mtihani wa Ualimu
Daraja la IIIA uliofanyika Mei 2022, uliandaliwa kwa kuzingatia muhtasari
wa somo la Stadi za Kazi wa mwaka 2009 na fomati ya mtihani ya mwaka
2022.
Taarifa hii inachambua maswali yenye ufaulu mzuri, wastani na hafifu kwa
kina ili kuongeza kiwango cha ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji wa
somo la Stadi za Kazi. Aidha, taarifa hii inaonesha sababu zilizowafanya
watahiniwa kupata ufaulu mzuri, wastani au hafifu katika majibu ya
maswali ya baadhi ya mada. Sampuli za majibu ya watahiniwa
1
zimeambatishwa ili kuonesha kile walichofanya. Hivyo, uchambuzi huu
utasaidia kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji wa somo la Stadi za Kazi
kwa mada ambazo ufaulu ulikuwa hafifu ili kuinua kiwango cha ufaulu
kwa watahiniwa katika mitihani yao. Aidha, inategemewa kuwa matokeo
ya uchambuzi huu yatawanufaisha wanachuo, wakufunzi, waandaaji wa
sera na wadau wote wa elimu kwa ujumla.
N = 3,274
2
Uchambuzi wa majibu ya watahiniwa unaonesha kuwa, watahiniwa 2,754
sawa na asilimia 84.1 waliopata alama kuanzia 0 - 1.5, hawakuelewa
matakwa ya swali, hivyo kupelekea kutoa majibu yasiyo sahihi. Baadhi ya
watahiniwa waliainisha faida za kutumia muhtasari badala ya taarifa
muhimu zilizo katika ukurasa wa haki miliki. Watahiniwa wengine
waliainisha maudhui yaliyomo ndani ya muhtasari. Mfano, mtahiniwa
mmoja aliandika;
(i) Mada Kuu: Huonesha jambo kuu ambalo litatakiwa kubeba mada
ndogo.
(ii) Mada ndogo: Huonesha vipengele mbalimbali kutoka kwenye
mada kuu.
(iii) Njia /mbinu za kufundishia: Huonesha namna ya kuwasilisha
somo.
(iv) Muda na Matumizi ya Zana: Huonesha wakati unaopaswa
kutumia na zana.
3
Kielelezo Na. 1.1: Sampuli ya jibu lisilo sahihi katika swali la 1.
4
alama kuanzia 2.0 hadi 4.0. Chati Na. 1 inaonesha ufaulu wa watahiniwa
katika swali hili.
6
vigezo kwa vipimo sahihi, kukata vigezo, kushona vigezo hatua kwa hatua
na kushona nguo kwa kutumia vigezo. Watahiniwa wengine walitoa majibu
yaliyohusu aina za mishono ya kutarizi. Mfano, mtahiniwa mmoja
aliandika; Mwiba wa samaki, Kikonyo na Mnyororo. Hii ilipelekea
watahiniwa kupata alama za chini na hivyo kuwa na ufaulu hafifu.
Kielelezo Na. 2.2 kinaonesha sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeshindwa
kujibu swali hili kwa usahihi.
N=3274
7
Jedwali Na. 2 linaonesha kuwa, watahiniwa 3,109 (95.0%) walipata alama
kuanzia 3.0 hadi 4.0 ambazo ni ufaulu mzuri, watahiniwa 25 (0.8%)
walipata alama kuanzia 2.0 hadi 2.5 ambazo ni ufaulu wa wastani na
watahiniwa 140 (4.2%) walipata alama kuanzia 0.0 hadi 1.5 ambazo ni
ufaulu hafifu.
8
Katika Kielelezo Na. 3.1, mtahiniwa aliweza kubainisha na kuzielezea kwa
usahihi mbinu zinazoweza kutumika katika kufundisha ufugaji wa bata kwa
wanafunzi wa Darasa la Nne, hivyo kupata alama za juu katika swali hili.
9
lilijibiwa na watahiniwa 3,274 (100%). Kwa ujumla ufaulu wa swali hili
ulikuwa ni mzuri kwani watahiniwa 3,093 (94.5%) walipata alama kuanzia
2.0 hadi 4.0. Chati Na. 2 inaonesha ufaulu wa watahiniwa katika swali hili.
11
Kielelezo Na. 4.2 kinaonesha sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeshindwa
kujibu swali hili kwa usahihi.
12
Jedwali Na. 3: Ufaulu wa watahiniwa katika swali la 5
N=3274
13
kinaonesha sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeweza kujibu swali hili kwa
usahihi.
14
usafi na mpangilio maalum mfano matumizi ya jiko, Kutunza mazingira
yanayokuzunguka mfano upakaji wa rangi kwa brashi na Kujifunza mahiri
mbalimbali muhimu kwa njia ya sauti mfano ngoma. Kielelezo Na. 5.2
kinaonesha sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali hili
kwa usahihi.
15
Chati Na. 3: Ufaulu wa watahiniwa katika swali la 6
Katika Kielelezo Na. 6.1, mtahiniwa aliweza kuelezea kwa ufupi, umuhimu
wa kupitisha pasi kwenye kitambaa cha kujaribia kabla ya kuanza kupiga
pasi nguo, hivyo alipata alama za juu katika swali hili.
18
Chati Na. 4: Ufaulu wa watahiniwa katika swali la 7
19
nchini. Aidha, uchambuzi zaidi unaonesha kuwa, watahiniwa wachache
waliweza kutoa hoja mbili au tatu na wengine walichanganya hoja sahihi na
zisizo sahihi hivyo kupata ufaulu wa wastani. Kielelezo Na. 7.1 kinaonesha
sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeweza kujibu swali hili kwa usahihi.
Katika Kielelezo Na. 7.1, mtahiniwa aliweza kutoa hoja nne na kuelezea
kwa usahihi umuhimu wa kudumisha afya njema ya ng’ombe wa maziwa,
hivyo alipata alama za juu katika swali hili.
20
(i) Kuhakikisha kuwa vyombo vya kuwalishia ng’ombe wa maziwa ni
visafi na vinapatikana sehemu husika
(ii) Kuwapatia chakula cha kutosha ambacho kitawezesha ng’ombe
hao wa maziwa kuwa na afya njema
(iii) Kuwapatia chanjo ili kuweza kudhibiti magonjwa nyemelezi kwa
ng’ombe hao wa maziwa.
21
2.1.8 Swali la 8: Sanaa za Maonesho
Swali hili liliwataka watahiniwa kuainisha mambo manne ambayo Bwana
Ambilikile anatakiwa kuyazingatia wakati wa kughani shairi kwenye
maadhimisho ya siku ya wanawake duniani. Swali lilijibiwa na watahiniwa
3,274 (100%). Kwa ujumla ufaulu wa swali hili ulikuwa hafifu kwani jumla
ya watahiniwa 1,250 (38.2%) ndio waliopata alama kuanzia 2.0 hadi 4.0.
Chati Na. 5 inaonesha ufaulu wa watahiniwa katika swali hili.
23
Kielelezo Na. 8.2: Sampuli ya jibu lililo sahihi katika swali la 8.
24
Chati Na. 6 inaonesha kuwa, watahiniwa 2,072 (43.8%) walipata alama
kuanzia 3.0 hadi 4.0 ambao ni ufaulu mzuri, watahiniwa 637 (19.5%)
walipata alama kuanzia 2.0 hadi 2.5 ambao ni ufaulu wa wastani na
watahiniwa 1,202 (36.7%) walipata alama kuanzia 0.0 hadi 1.5 ambao ni
ufaulu hafifu.
25
Katika Kielelezo Na. 9.1, mtahiniwa aliweza kubainisha kwa usahihi mbinu
nne za kuwaelekeza washiriki wa mashindano ya Bongo Star Search ili
waweze kuimba vizuri. Hivyo kupata alama za juu katika swali hili.
26
Katika Kielelezo Na. 9.2, mtahiniwa alibainisha mbinu zinazotumika katika
kufundisha mada husika badala ya kubainisha mbinu atakazowaelekeza
washiriki wa shindano la Bongo Star Search ili waimbe vizuri, hivyo
kupata alama za chini katika swali hili.
N=3274
27
mwanafunzi na mwanafunzi, Husaidia kutunza kumbukumbu endelevu,
Inakuza ari ya kupenda somo, Huleta motisha na kukuza ari ya kujifunza,
Huibua fikra, udadisi na vipaji kwa wanafunzi, Wanafunzi wanakuwa
wasikivu na wanaburudika na Husaidia kutatua matatizo/changamoto za
wanafunzi kwa haraka. Majibu haya yalipelekea watahiniwa hawa kupata
alama za juu katika swali hili.
Kielelezo Na. 10.1: Sampuli ya jibu lililo sahihi katika swali la 10.
28
(iv) Husaidia kufanya majaribio kabla ya kwenda kufanya vitendo
mbele ya hadhira.
29
2.2.1 Swali la 11: Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
Swali hili liliwataka watahiniwa, kwa kutumia hoja sita kuelezea ni
kwanini ni muhimu kwa mkulima kutumia mbegu bora katika ustawishaji
wa mboga shambani. Swali lilijibiwa na watahiniwa 3,274 (100%). Kwa
ujumla ufaulu wa swali hili ulikuwa mzuri kwani jumla ya watahiniwa
3,262 (99.6%) walipata alama kuanzia 6.0 hadi 15.0. Chati Na. 7 inaonesha
ufaulu wa watahiniwa katika swali hili.
Kielelezo Na. 11.1: Sampuli ya jibu lisilo sahihi katika swali la 11.
31
Katika Kielelezo Na. 11.1, mtahiniwa alimudu kuelezea umuhimu kwa
mkulima kutumia mbegu bora katika ustawishaji wa mboga shambani
ingawa katika baadhi ya hoja maelezo hayakujitosheleza sana. Hivyo,
alishindwa kupata alama zote 15 katika swali hili.
32
Kielelezo Na. 11.2: Sampuli ya jibu lisilo sahihi katika swali la 11.
33
Katika Kielelezo Na. 11.2, mtahiniwa aliainisha hatua za kuandaa shamba
na kupanda mbegu shambani badala ya kuelezea umuhimu wa mkulima
kutumia mbegu bora katika ustawishaji wa mboga shambani. Hii
ilisababisha mtahiniwa kupata alama za chini katika swali hili.
35
Kielelezo Na. 12.1: Sampuli ya sehemu ya jibu lililo sahihi katika swali la
12.
36
Uchambuzi zaidi unaonesha kuwa, watahiniwa 261 (0.8%) waliopata
ufaulu hafifu, walishindwa kuelewa matakwa ya swali hivyo kutoa majibu
yasiyo sahihi. Baadhi ya watahiniwa waliainisha mbinu mbalimbali za
kufundishia badala ya kuelezea hatua mbalimbali watakazowaelimisha
wanafunzi wa Darasa la Tano kuhusu upishi wa ugali. Mfano, mtahiniwa
mmoja alitoa majibu kama vile; Kwa kutumia mbinu ya mhadhara, Kwa
kutumia mbinu ya maswali na majibu, Kwa kutumia mbinu ya majadiliano,
Kwa kutumia mbinu ya maelezo na Kwa kutumia mbinu ya onesho mbinu.
Aidha, mtahiniwa mwingine aliainisha njia mbalimbali za kupika kama
vile; Kukaanga, Kuchemsha, Kubanika, Kuoka na Mvuke. Kadhalika,
watahiniwa wengine walibainisha kanuni za usafi katika mapishi. Mfano,
mtahiniwa mmoja aliandika; Eneo liwe safi, Mpishi awe safi, Mavazi yawe
safi, Chakula kiwe safi, Chakula kifunikwe na Vifaa viwe visafi. Majibu
haya yanaonesha kuwa, watahiniwa walishindwa kuelewa matakwa ya
swali hivyo kutoa majibu yasiyo sahihi. Kielelezo Na. 12.2 kinaonesha
sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeshindwa kujibu swali hili kwa usahihi.
37
Kielelezo Na. 12.2; Sampuli ya jibu lisilo sahihi katika swali la 12.
38
2.2.3 Swali la 13: Ufundishaji
Swali hili liliwataka watahiniwa kufafanua faida sita anazozipata mwalimu
wa somo la Stadi za Kazi anapotumia Andalio la Somo wakati wa
ufundishaji. Swali lilijibiwa na watahiniwa 3,274 (100%). Kwa ujumla
ufaulu wa swali hili ulikuwa mzuri kwani jumla ya watahiniwa 3,254
(99.6%) walipata alama kuanzia 6.0 hadi 15.0. Chati Na. 9 inaonesha
ufaulu wa watahiniwa katika swali hili.
39
kuboresha ufundishaji wake, Humsaidia mwalimu kufanya tathmini ya
wanafunzi wameelewa kwa kiasi gani na Humsaidia mwalimu kujua namna
ya kutumia zana. Majibu sahihi yalitokana na uzoefu waliopata watahiniwa
katika kufanya mazoezi ya kuandaa somo wakati wa kipindi cha mazoezi
ya muda mrefu. (Block Teaching Practice). Kielelezo Na. 13.1 kinaonesha
sampuli ya jibu la mtahiniwa aliyeweza kujibu swali hili kwa usahihi.
40
Kielelezo Na. 13.1: Sampuli ya sehemu ya jibu lililo sahihi katika swali la
13.
Katika Kielelezo Na. 13.1, mtahiniwa aliweza kufafanua kwa usahihi faida
sita anazozipata mwalimu wa somo la Stadi za Kazi anapotumia Andalio la
Somo hivyo aliweza kupata alama za juu katika swali hili.
41
kuhusianisha mazingira na mahiri anayofundisha na Mwalimu ataanza na
mada rahisi kabla ya ngumu. Mtahiniwa mwingine alitoa hoja kama vile;
Humsaidia mwalimu kuvuta usikivu wa wanafunzi, Humsaidia mwalimu
kukuza hali ya wanafunzi kupenda somo lake, Humsaidia mwalimu
kueleweka kwa haraka. Hata hivyo mtahiniwa alishindwa kuelewa kuwa
hoja alizotoa zilihusu faida za kufundisha kwa kutumia zana hivyo
kushindwa kupata alama katika swali hili. Aidha, baadhi ya watahiniwa
hawakujibu swali hili. Majibu haya yanaonesha kuwa, watahiniwa
hawakuelewa swali hivyo kupelekea kupata ufaulu wa chini katika swali
hili.
43
44
Kielelezo Na. 14.1: Sampuli ya sehemu ya jibu lililo sahihi katika swali la
14.
46
Kielelezo Na. 14.2: Sampuli ya sehemu ya jibu lisilo sahihi katika swali la
14.
47
Katika Kielelezo Na. 14.2, mtahiniwa aliandika baadhi ya mambo muhimu
ya kuzingatia mwalimu anapochagua njia za kufundishia badala ya
kufafanua kanuni sita anazopaswa kuzingatia katika kuandaa maswali ya
kuchagua jibu sahihi.
Uchambuzi zaidi uliofanyika ulibaini kuwa, ufaulu mzuri katika mada hizo
umetokana na watahiniwa kuwa na maarifa ya kutosha, uwezo mzuri wa
kujenga hoja pamoja na kuelewa matakwa ya swali. Hata hivyo, baadhi ya
watahiniwa walishindwa kupata alama za juu hususani katika mada ya
Maandalizi ya Ufundishaji, hii ilisababishwa na watahiniwa hawa
kutokuwa na maarifa ya kutosha kuhusu dhana iliyoulizwa, kushindwa
kujenga hoja hasa katika kujibu maswali ya insha na kushindwa kuelewa
matakwa ya swali.
4.0 HITIMISHO
Matokeo ya uchambuzi wa takwimu za ufaulu kwa watahiniwa
yanathibitisha kuwa, kwa ujumla, ufaulu kwa watahiniwa katika somo la
Stadi za Kazi ulikuwa mzuri. Maswali ambayo watahiniwa wengi walipata
alama za juu yalikuwa kumi (10), wastani maswali mawili (02) na hafifu
maswali mawili (02). Aidha, majibu ya watahiniwa yaliyonukuliwa au
kuambatishwa kama vielelezo vya majibu mazuri yameonesha kuwa
umahiri wa watahiniwa katika dhana zilizoulizwa ulikuwa mzuri. Kwa
upande mwingine, mada moja (01) tu ndio iliyokuwa na ufaulu hafifu,
jambo linaloonesha kuwa watahiniwa wengi walikuwa na umahiri wa
kutosha katika mada za somo husika.
48
5.0 MAPENDEKEZO
Ili kuongeza kiwango cha ufaulu katika mada ya Maandalizi ya Ufundishaji
iliyokuwa na ufaulu hafifu na mada zenye ufaulu wa wastani yafuatayo
yanashauriwa.
49
Kiambatisho
Asilimia ya Ufaulu
Namba
Na. Mada Waliopata Maoni
ya swali
alama 40 na Wastani
zaidi
1. Ufundishaji 5 99.5
99.45 Vizuri
13 99.4
2. Udobi 6 95.5 95.50 Vizuri
3. Biashara Ndogo
4 94.5 94.50 Vizuri
Ndogo
4. Upishi 12 92.0 92.00 Vizuri
5. Kilimo, Ufugaji 11 99.6
na Uvuvi
3 95.8 90.23 Vizuri
7 75.3
6. Upimaji na
14 79.4 79.40 Vizuri
Tathmini
7. Sanaa za 10 99.7
Maonesho 68.95 Wsatani
8 38.2
8. Muziki 9 63.3 63.30 Wastani
9. Ushonaji wa
2 40.8 40.80 Wastani
Nguo
10. Maandalizi ya
1 15.9 15.90 Hafifu
Ufundishaji
50