You are on page 1of 4

ARIZONA VOCATIONAL

TRAINING CENTRE
MIKOCHENI A
P.o.Box 33158, Contact: Office. 0742-466965.
DAR ES SALAAM-TANZANIA

FOMU YA MAELEZO YA KUJIUNGA NA MAFUNZO


YA USHONAJI NA UBUNIFU WA MAVAZI (TAILORING AND FASHION
DESIGN) 2024/2025.

JINA LA MWANAFUNZI/MWOMBAJI…………………………………….
ARIZONA VOCATIONAL TRAINING CENTRE,MIKOCHENI A inakukaribisha sana
kujiunga na kozi ya Ushonaji na ubunifu wa mavazi ( Tailoring and fashion design) sekta hii
inakuwa kwa kasi kubwa hapa nchini, ni sekta inayo ajiri vijana wengi.
Malengo yetu Arizona vtc ni kutoa mafunzo kwa ubora wa hali ya juu hivyo kuwawezesha
wahitimu wetu kunufaika na fursa za ajira katika sekta hii inayokuwa kwa kasi hapa nchini.

MAZINGIRA YA CHUO.
Chuo chetu kipo kwenye mazingira tulivu, madarasa makubwa yenye mwanga na hewa safi. Ni
mazingira bora ya kujifunzia. Tunao walimu wenye taaluma ya kutosha kumuelisha na wenye
kiu ya mafakio ya wanafunzi wao.
FAIDA YA KUJIUNGA NA KOZI YA USHONAJI NA UBUNIFU WA
MAVAZI(TAILORING AND FASHION DESIGN)
1. AJIRA ya UHAKIKA: Wahitimu wetu wamekuwa wakifanya vizuri katika soko la
AJIRA hivyo kuacha sifa nzuri kila wanapoajiriwa katika viwandana taasisi mbalimbali.
2. Utafundishwa na walimu mahiri na wenye kipaji na uzoefu wa kufundisha
wanaozingatia taaluma ya ufundishaji.
3. Sekta hii ni pana sana hivyo kupitia maarifa na ujuzi atakaopata chuoni mhitimu
anauwezo wa kuamua kuajiriwa au kujiajiri.
4. Kupitia fani hii mhitimu anaweza kujiajiri kwa kufungua kiwanda kidogo cha kushona na
kubuni mitindo ya mavazi, hivyo kuunga mkono juhudi za serikali za kuanzisha na
kukuza viwanda nchini.
5. Baada ya kumaliza mafunzo kwa Nadharia na vitendo na kufaulu mitihani yake kwa
kupata alama nzuri mhitimu atatunukiwa cheti.
6.
MUDA WA KOZI NA GHARAMA ZAKE.
Kozi ya Ushonaji na ubunifu wa mavazi(Tailoring and fashion design) inatolewa kwa muda
miezi mitatu (3 months)
- Utasoma nadharia na vitendo
- Fomu ya kujiunga ni (10,000) tu
- Ada yake ni laki tisa tu(900,000/= tshs)

UTARATIBU WA KULIPA ADA


Ada yote ilipwe kwa awamu mbili ndani ya miezi mitatu kama ifuatavyo;
- Kiwango cha kuanzia kisipungue laki tano tu( 500,000/=tshs)
- Awamu ya pili shilingi laki nne (400,000/=tshs) ndani ya mwezi wa pili na wa tatu wa
masomo

GHARAMA NYINGINE ZINAZO FANYIKA KABLA YA KUMALIZA MASOMO


Malipo ya cheti cha kumaliza kozi ambayo ni elfu tano tu(5,000/=tshs)
Malipo ya ada yafanyike kabla ya kuanza masomo kwa kupitia M PESA lipa namba 5581313
jina la akaunti ARIZONA VTC

MAHITAJI MENGINE MUHIMU:


Mwanafunzi anatakiwa kuandaa vifaa vifuatavyo :
- Daftari kubwa moja, Kalamu za wino (blue) na kalamu ya risasi (pencil)
- Mkasi mkubwana Chaki
- Bobbin na bobbin case
- Futi kamba
- Kifaa cha kufumulia nguo (Lipa)
- Kitambaa kinachotokana na somo utakalosoma.
- Sindano za machine na Uzi utakaofanana na kitambaa ulichonunua

SHERIA NA TARATIBU AMBAZO MWANAFUNZI UNAPASWA KUZINGATIA

● Mwanafunzi anapaswa kutoa taarifa kama hata hudhuria darasani .

● Mwanafunzi anapaswa kuzingatia usafi wa darasa na mazingira yako

● Mwa nafunzi unapaswa kuwa mwangalizi wa mashine anayotumia pamoja na vifaa vyote
wanavyotumia.
● Mwanafunzi kama hata hudhulia wiki nzima bila taarifa yoyote huta hesabika kama
mwanafunzi wetu.
● Mwanafunzi anapaswa kizingatia muda wa kuingia darasani na kutoka darasani

● Haturuhusu matumizi ya lugha chafu darasani.


● Mwanafunzi haruhusiwi kutumia vileo mf. Pombe, uvutaji wa sigara au bangi n.k
uwapo chuoni au katika mazingira ya chuo.Ukibainika utasimamishwa masomo moja
kwa moja.

● Mwanafunzi anapaswa kulipa ada kupitia benki kwa akaunti ya chuo utakayopewa na mhasibu
hapa ofisini na si vinginevyo

● Mwanafunzi hakikisha unapewa risiti kwa malipo yote utakayofanya chuoni. Kama umefanya
malipo na hukupewa risiti unawajibu wa kuidai.

● Mwanafunzi unapaswa kuzingatia utaratibu wa kulipa ada kila ufikapo muda wa kufanya malipo
kama ulivyoelekezwa ofisini.

● Mwanafunzi atakayeshindwa kulipa ada kwa utaratibu wa kupunguza kila mwezi uliowekwa na
chuo atasimamishwa masomo mara moja.

● Mwanafunzi zingatia kutunza risiti zako za malipo ya ada ni muhimu mpaka utakapohitimu na
kutunukiwa cheti.

● Mwanafunzi unapaswa kukamilisha malipo yako ya ada kabla ya kufanya mitihani yako ya
mwisho.

● Ni lazima kila mwanafunzi afanye mazoezi yote atakayopewa na mwalimu


darasani,pamoja na mitihani yote itakayotolewa na shule.

● Mahusiano ya kimapenzi kati yamwanafunzi na Mwanafunzi au mwanafunzi na


mwalimu au na mfanyakazi yeyote wa shule ni marufuku kabisa

● Mwanafunzi atakayeghairisha masomo baada ya kulipa ada na kabla ya masomo kuanza


atarudishiwa asilimia hamsini (50%) ya ada aliyolipa. (gharama za fomu ya kujiunga
hazitarudishwa) Endapo utaamua kusitisha baada ya kuanza masomo ada haitarudishwa kwa
namna yoyote.

● Ni lazima mwanafunzi atii na kufuata sheria zote zilizoorodheshwa hapo juu na zile
nyingine utakazoendelea kupewa pindi awapo chuoni.

Baada ya kuhitimu hakikisha unachukua cheti chako mapema kabla ya kupita miezi miwili baada
ya hapo kutakuwa na TOZO kwa kuchelewa kuchukua cheti.
Mimi --------------------------------------------------- nimesoma na kuelewa maelezo yaliyotolewa
hapo juu na nimeamua kwa dhati kujiunga na masomo kwa kozi ya Ushonaji (tailoring)

---------------------------------- ----------------------------------
Sahihi Tarehe

(kwa matumizi ya ofisi)


Jina la mpokeaji form ( mkuu wa chuo) au kwa niaba

Jina --------------------------------------------------------- Sahihi ------------------------------ Tarehe


-------------------

You might also like