You are on page 1of 9

Bismillahir Rahmaanir Rahiim

Namba ya usajiliCU 130


S.L.P 2055 DAR ES SALAAM

MAFUNZO YA UALIMU
NA
UONGOZI WA SHULE YA AWALI NA MSINGI

MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA CHUO

2019/2020

Page | 1
NDUGU___________________________________

Assalaam alaykum Warahmatullah wabarakatuh,

YAH: KUCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NA


UONGOZI WA SHULE YA AWALI NA MSINGI KWA NGAZI YA CHETI

Shukurani zote zinamstahiki Allah (SW) na rehema na amani zimuendee


Mtume Muhammad (saw) na wafuasi wake wote.
Nakupongeza na kukuarifu kuwa umechaguliwa kujiunga na mafunzo ya
ualimu katika chuo hiki kwa mwaka wa masomo 2019/2020.

Chuo kitafunguliwa tarehe 01/04/2019 Unapaswa kusoma masharti ya


kujiunga na chuo kwa umakini na kuyakubali kabla ya kuripoti chuoni.
Unakaribishwa sana CHUO CHA UALIMU KIGOGO.

Wabillahit Tawfiiq.

………………………….

MKUU WA CHUO.

Page | 2
1. Utangulizi
Chuo cha Ualimu Kigogo ni kituo kinachotoa mafunzo ya ualimu na
uongozi wa shule ya Awali na Msingi.
Katika Chuo hiki maadili na elimu ni mambo yaliyopewa kipaumbele
kikubwa kabisa. Hii ni kutokana na ukweli kuwa Qur’an inatufahamisha
kuwa huwezi kusimamia jambo lolote kwa ufanisi sharti kwanza upate
elimu sahihi juu ya jambo hilo. Rejea Qur’an 2:31 na 96:1-5.
Kuhusu maadili, Qur’an inatufahamisha kuwa kwa mtu yeyote
anayetaraji malipo mema toka kwa Allah (sw) basi na aige mwenendo
wa Mtume Muhammad (s.a.w).
Misingi hii tuliyoainisha ndiyo kigezo kwa mwalimu anayeandaliwa
katika chuo hiki. Hii ni kwa sababu mwalimu ndiye wakala wa
mabadiliko yoyote ya maana katika jamii.

2. Lengo la Chuo
(i) Kuwaandaa walimu kwa kuwapatia elimu stahiki na kuwalea
kimaadili ili wakawe wasimamizi na walezi wa vijana katika suala la
elimu shuleni, vituo vya elimu na madrasa za aina zote katika eneo
lake la kazi. Huku wao wenyewe wakiwa wa kupigiwa mfano katika
jamii yetu hii ambayo maadili yamemomonyoka mno.
(ii) Kuwaandaa walimu watakao kuwa chachu ya mabadiliko katika
jamii ya waislamu na taifa kwa ujumla kwa kuwa na maadili na ari
ya kuitumikia dini na jamii kwa ujumla tukizingatia kuwa wengi wa
wanajamii hawakupata fursa ya kuyajua maadili ya dini yao.
(iii) Kuwaandaa walimu weledi watakaoweza kuanzisha,
kuendesha vituo vya elimu na kufundisha kwa ngazi ya awali na
msingi.
(iv) Kumwezesha mhitimu kuhifadhi juzuu moja kwa uchache.
(v) Malengo ya ujumla ni yale yapatikanayo kwa wahitimu wa
mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti.

Page | 3
3. MASOMO YATOLEWAYO.
Masomo yanayofundishwa ni yale yote ya lazima yaliyoainishwa katika
mtaala wa serikali. Kulingana na malengo ya chuo mchanganuo wa
masomo yanayofundishwa ni
1. Ualimu
2. Vitendo vya awali
3. Masomo ya kufundishia shule za msingi
4. Uongozi
5. Daawa
6. Montessori
7. Ujasiriamali
8. Computer
9. Lugha

10. Pia masomo yanaweza kuongezeka kulingana na hitajio ili kufikia


malengo na ndani ya masomo tajwa hapo juu yanabeba kozi mbalimbali.

4. GHARAMA ZA MAFUNZO
Gharama za mafunzo ni nafuu. Mwanachuo wa kutwa atalipia ada shilingi
600,000 na mwanachuo wa bweni atalipia Tsh 1,200,000 na zitalipwa kwa
awamu nne,au awamu 12 kwa wale watakaokopeshwa na benki ya
kiislamu ya AMANA.Na gharama nyingine zimeainishwa kama jedwali
linavyoonesha hapo chini:-
MALIPO APRIL-JUNE JULY - AUG SEPT - OCT NOV-DEC
BWENI KUTWA BWENI KUTWA BWENI KUTWA BWENI KUTWA
ADA 300,000 150,000 300,000 150,000 300,000 150,000 300,000 150,000
B.T.P 50,000 50,000 050555 050555
BIMA YA AFYA 050,55 050,55
OASILUBMATIK 050555 050555
AAI I AI 050555 050555 050555 050555 050555 050555
OALITKLK
ABLMI ,050,55 6250,55 0050555 6550555 ,550555 6050555 0050555 6550555

N.B:
 Malipo ya ada na mafunzo kwa vitendo (BTP) yanapaswa kufanyika
Benki kupitia Akaunti ya chuo na kuwasilisha Karatasi ya Malipo (Bank
Pay in Slip) kwa Mhasibu wa chuo.
 Na malipo ya bima ya afya na kitambulisho yatafanyika chuoni
mwanachuo anapowasili. Kwa wanachuo ambao wana Bima ya
afya hawatowajibika kulipia bima ya afya(NHIF)
Page | 4
 Kwa wanaosomeshwa na TESA watumie akaunti namba ya
(NMB) Jina la akaunti ni TESA mfuko wa elimu.

AKAUNTI YA MALIPO
BENKI JINA LA AKAUNTI NAMBA YA AKAUNTI
AMANA BANK CHUO CHA UALIMU KIGOGO 004120564370001
NMB BANK TESA MFUKO WA ELIMU 20310006554

5. MAHITAJI YA MWANACHUO
i. Vifaa
Wanafunzi wa Wanafunzi wa
KIKE KIUME
SN AINA YA KIFAA
BWENI KUTWA BWENI KUTWA
1 Seti ya vitabu vya maarifa ya uislamu darasa la watu wazima(7) √ √ √ √
2 Rimu 1 A4 √ √ √ √
3 Seti ya vitabu vya daawa (11) √ √ √ √
4 Nguo za kushindia zizingatie vigezo vya vazi la kiislam. √ X √ X
5 Nguo za kulalia √ X √ X
6 Mas’haf moja ya tafsiri (AL - FARSIY) √ √ √ √
7 Madaftari (Counter Book 2 quires) 20 √ √ √ √
8 Kalamu na penseli za kutosha √ √ √ √
9 Mkebe wa vifaa vya hisabati (Mathematical set) √ √ √ √
10 Saa ya mkononi √ √ √ √
11 Shuka na foronya TATU za rangi ya BLUE, PINKI NA NYEUPE √ X X X
12 Shuka na foronya TATU za rangi ya BLUE, PINKI NA KIJANI x X √ X
13 Godoro (fut 21/2 x 6) na mto √ X √ X
14 Ndoo ya kufulia √ X √ X
15 Sahani ya chuma yenye vyumba vya mboga, kijiko, kikombe √ X √ X
16 Sanduku la bati(Tranka) √ X √ X
17 Mkoba wa madaftari √ √ √ √

N.B. Katika kipengele namba 4 kwa wavulana wanatakiwa waje na nguo


za juu 3 na za chini 3 pamoja na taulo moja. Kwa wasichana wanatakiwa
waje na nguo za juu 4 za chini 4 pamoja na kitenge 1 na taulo 1.

Page | 5
ii. MAVAZI YA WANACHUO
Kwa sasa hakutakuwa na sare rasmi za chuo. Mwanachuo atatakiwa
kuvaa vazi linalozingatia miiko na maadili ya kiislam na fani ya
ualimu.
Wanachuo wa kiume wanaruhusiwa kuvaa shati, T-SHIRT yenye kola
na suruali za vitambaa sio jinsi. Na Mwanachuo wa kike atatakiwa
kuvaa baibui na juba au mtandio mrefu unaovuka kiwiko cha mkono.
Mavazi yote yazingatie sifa zifuatazo;
a) Vazi lisibane,lisiwe la mpira, lisishikane na mwili.
b) Lisiwe na mapambo, Maandishi wala Picha
c) Lisioneshe (transparent)
d) Liwe ni vazi la watu wema kwa asli
e) Lisitiri mwili wote.
f) Mwili (kucha, uso, miguu n.k) usiwe na mapambo

iii. MAVAZI YA MICHEZO KWA WANACHUO


Nguo za michezo track suit za bluu au zambarau na raba nyeusi kwa
wavulana.kwa wasichana juba na gauni la bluu bahari au damu ya
mzee, kitambaa kisiwe cha mpira na raba nyeupe.

6. GHARAMA ZA MAFUNZO KWA VITENDO (BTP)


Kutakuwepo na mazoezi ya vitendo kwa mwaka wa kwanza na mwaka
wa pili, BTP (Block Teaching Practice).
Kila mwanachuo atahudhuria mafunzo kwa vitendo katika mkoa na
wilaya atakayopangiwa. Mwanachuo atajitegemea kwa Gharama za
mafunzo kwa vitendo na atapaswa kulipia Tsh 100,000 kwa ajili ya
UKAGUZI.Fedha hii ilipwe ndani ya awamu ya tatu na ya nne na hivyo
kabla ya tarehe 15 Novemba iwe imekamilika.

7. UPIMAJI WA MAENDELEO YA MWANACHUO


Itakuwepo mitihani na majaribio ya kutosha ya ndani kwa kipindi chote
cha kuwepo chuoni ili kumuwezesha mwanachuo kusoma kwa bidii.
Hivyo mwanafunzi anapaswa kufaulu mitihani yote hiyo. Endapo atafeli
baadhi ya mitihani atapewa fursa ya kukariri mitihani hio
Page | 6
(supplementary) mwisho wa mwaka wa kwanzakwa gharama yake.
Kushindwa kupata wastani wa C au GPA 2.5 kwa matokeo ya jumla
mwanachuo atalazimika kurudia mwaka wa masomo. Kwa mwanachuo
atakaekosa kufanya mitihani bila ya sababu ya msingi zilizoafikiwa na
utawala atakuwa amejifukuzisha chuo au kupewa adhabu nyinginezo
kulingana na mazingira ikihusisha faini ya shilingi 15000 kwa kila
mtihani.

8. KANUNI NA MWENENDO BORA WA CHUO


Chuo hiki kinafuata misingi na maadili ya kiislamu.Hivyo mwenendo wa
Mwanachuo na wafanyakazi wote unatarajiwa uwe wa kiislamu. Kukiuka
maadili ya Qur’an na Sunnah ni sawa na kukiuka maadili ya chuo.
Atachukuliwa hatua za kinidhamu yeyote atakaekiuka kwa makusudi
maadili ya uislamu ikiwa ni pamoja na KUFUKUZWA chuo.
Zifuatazo ni kanuni muhimu kuzingatiwa na kila Mwanachuo;
(i) Kila Mwanachuo anapaswa kutambua kuwa yupo hapa kwa ajili
ya uislamu.Kwa hiyo chochote kilicho nje ya uislamu hakina
nafasi katika chuo hiki kiwe kwa maneno au kwa vitendo.
(ii) Kila Mwanachuo atakuza pendo lake kwa Allah (s.w) na Mtume
wake (s.a.w) dini yake pamoja na waumini wenzake.
(iii) Pamoja na haki za Muumba zilizo juu ya kila Muislamu,
yamwajibikia kila Mwanachuo achunge haki na nafasi yake na
atumie vipaji vyake katika uchamungu ndani na nje ya chuo.
(iv) Kila Mwanachuo atatumia muda wake vizuri katika kujielimisha
kwa ajili ya Allah (s.w) ikizingatiwa kuwa kujielimisha kwa ajili
ya Allah (s.w) ni amri ya kwanza kwa kila muislamu.
(v) Kila Mwanachuo analazimika kuhudhuria vipindi vya kila somo,
kufanya mazoezi, majaribio na mitihani yote itakayotolewa
chuoni.
(vi) Wakati wote wa kuwa chuoni au nje ya chuo, wanachuo
wanatakiwa kuvaa mavazi yanayochunga mipaka ya kiislamu.
(vii) Kupigana ni kosa kubwa, Mwanachuo atakaepigana atachukuliwa
hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kurudishwa nyumbani au
kufukuzwa chuo.

Page | 7
(viii) Ni marufuku kwa Mwanachuo wa Jinsia yoyote kuvaa mapambo
wakati akiwa chuoni na akiwa nje ya chuo.
(ix) Ni marufuku wanachuo kufuga kucha, kupaka rangi za kucha,
rangi za mikono, rangi za midomo, kupaka hina, kunyoa nyusi,
kuvaa viatu vya kuchuchumia au vinavyotoa sauti, kuweka
nywele dawa au kutia rangi au kusuka rasta n.k
(x) Ni marufuku Mwanachuo kuchochea,kushawishi,kuhamasisha au
kushiriki mgomo kwa namna yoyote.
(xi) Mwanachuo asionekane katika vilabu vya pombe, nyumba za
kupangisha wageni (guest house), kumbi za dansi na sinema.
(xii) Kila Mwanachuo ni mlinzi wa mali za chuo, mali zake binafsi na
mali za wenzake. Mwanachuo atakayeharibu au kusababisha
uharibifu au upotevu au wizi wa mali ya chuo atachukuliwa hatua
kali ikiwa ni pamoja na kulipa
(xiii) Kuiba ni kosa kubwa, Mwanachuo atakayethibitika kuiba mali ya
chuo au ya mwenzake atachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa ni
pamoja na kulipa.Hivyo Mwanachuo atakapogundua wizi wa mali
chuo, au mali ya mwenzake atoe taarifa kwa uongozi husika mara
moja.
(xiv) Kila Mwanachuo awe msafi na ahakikishe anashiriki vyema Usafi
wa Mazingira ya chuo.
(xv) Kelele za aina zozote hazitaruhusiwa iwe darasani, koridoni,
ndani ya bweni au popote katika eneo la chuo iwe kwa
Mwanachuo mmoja au wengi (kundi).Rejea Qur’an 31:19
(xvi) Mwanachuo hatoruhusiwa kutoka nje ya eneo la chuo bila kibali
maalum cha maandishi.
(xvii) Kila Mwanachuo analazimika kushirikiana na wanachuo wenzake,
wakufunzi na wafanyakazi wengine katika wema na uchamungu
ili kufikia lengo la chuo. Rejea Qur’an 05:02
(xviii) Hairuhusiwi kwa Mwanachuo kuja chuoni na vifaa vya ‘electronic’
kama vile TV,Redio, Simu ya mkononi, line za simu, n.k
(xix) Kila Mwanachuo atalazimika Kuswali swala ya Tahajjud
(Qiyaamul-layl) kila usiku wa ijumaa kuamkia Jumamosi na usiku
wa Jumamosi kuamkia jumapili.
(xx) Kusema uongo,kuficha uovu wa aina yoyote au kuzusha ni kosa
kubwa kwa mwanachuo na hatua za kinidhamu zitachukuliwa
ikibainika mwanachuo amefanya hayo .

Page | 8
(xxi) Ni marufuku kwa wanachuo wa Jinsia tofauti kukaa faragha
wakiwa wawili hata kama ni ndugu wa damu. Pia si ruhusa
kufanya shughuli yoyote ikiwemo kazi za makundi au group
discussion kwa wanachuo wawili wa Jinsia tofauti.

N.B: kwa makosa yote ya jinai na ya kinidhamu yatampelekea


mwanachuo kutoa faini, kumuita mzazi na ikibidi hatua za
kipengele namba 9 kuchukuliwa.

9. MAKOSA YANAYOSABABISHA MWANACHUO KUFUKUZWA


(i) Kutosimamisha swala.
(ii) Kuzini au kukaribia zinaa kwa namna yoyote.
(iii) Kugoma au kuchochea mgomo, kuongoza mgomo au kuvuruga
amani na usalama wa chuo na jamii inayozunguka.
(iv) Kukataa adhabu.
(v) Utoro wa aina yoyote.
(vi) Kukosa mtihani pasina sababu za msingi ikiwemo kutokamilisha
malipo ya ada na michango stahiki.
(vii) Kufanya makosa ya jinai mfano wizi, kupiga au kupigana n.k
(viii) Kutumia ulevi wa pombe, sigara au madawa ya kulevya ya aina
yoyote
(ix) Kwenda kwenye dansi, miziki, taarabu, fukwe zisizozingatia
maadili ya uislamu n.k
(x) Kutoroka kwenda kuangalia mpira katika mazingira hatarishi.
(xi) Kutohudhuria masomo pasi na sababu ya msingi.
(xii) Kusema uongo,kuficha uovu au uzushi wa aina yoyote.
(xiii) Kudharau au kukejeli kwa namna yoyote ile programu za
chuo,walimu na wafanyakazi wa chuo.
Nakutakia Masomo na Makazi Mema Hapa Chuoni

Wabillah Tawfiiq.

MKUUWA CHUO.

Page | 9

You might also like