Professional Documents
Culture Documents
Mzazi na mtoto
Mzazi: Amina leo mmejifunza nini shuleni?
Mtoto: Tumejifuna kiswahili mama.
Mzazi: Vizuri mwanangu, sasa kabadilishe nguo chakula
kiko jikoni,
alafu uoshe vyombo.
Mtoto: Sawa mama.
Hakimu na mshtakiwa.
Hakimu: Mshtakiwa una lolote la kujitetea?
Mshtakiwa: Ndio mweshimiwa hakimu.
Hakimu: Jitetee.
Mstakiwa: Mheshimiwa naomba mahakama
inipunguzie adhabu kwa
sababu nikosa langu la kwanza pia nina familia
inayonitegemea.
Daktari na mgonjwa.
Daktari: Meza mbili kutwa mara tatu (2×3×7)
Mgonjwa: Sawa daktari.
Daktari: Hakikisha unakunywa maji ya kutosha.
Mgonjwa: Sawa daktari.
Hivyo basi katika utumizi wa lugha uhusiano baina ya wahusika
huwawezesha kuteua aina ya mazungumzo yanayostahili kulingana na
mazungumzo husika.
Mada ya mazungumzo
Mfano;
Mada ya kisiasa.
Kiongozi: “People’s”
Wananchi: “Power”
Kiongozi: Leo ni siku pekee ya kuzungumza na
wananchi, naomba
mniskilize kwa makini.
Mada ya afya.
Bwana afya: Ndugu zangu chimbeni mashimo ili tuondokane na
magonjwa ya
kuambukiza kama yanayojitokeza katika kijiji chajirani.
Wanakijiji: Sawa mkuu, tutatekeleza.
Dhumuni la mazungumzo.
Mfano;
Dhumuni la kuelimisha;
Mshauri nasaha: Kutokana na majibu ya vipimo vyako, inabidi ule
vizuri chakula bora
ikiwa ni pamoja na matunda,pia upate muda wa kupumzika.
Ukizingatiahaya utaishi kwamatumaini.
Mgonjwa: Sawa.
Dhumuni la kuonya.
Mazungumzo kati ya mzazi na mtoto:
Mzazi: Siku hizi umekua ukichelewa kurudi nyumbani,
kinachokuchelewesha
kinachokuchelewesha
nini?
Mtoto: Usafiri mama.
Mzazi: Usafiri gani huo mpaka saa nne za usiku? mbona Aisha
amewahi
kurudi?
Mtoto: (kimya).
Mtoto: (kimya).
Mzazi: Mwanangu dunia haiko hivyo unavyodhani, umebadilika
sana siku hizi. Ujana
una mambo mengi, ni vyema uutumie ujana wako vizuri,
kumbuka kuna
magonjwa hatari na yasiyotibika.
Dhumuni la kuburudisha:
Mfano;
Mshereheshaji na wageni waalikwa:
Mshereheshaji: Piga vigelegele kwa maharusi wetu jamani.
Wageni waalikwa: Kilililiiiiiiiiiiiii ………………..
Mshereheshaji: Mwenye wivuuuuu…………...
Wageni waalikwa: Ajinyongeeeee ……………….
· Jinsi.
Tofauti za kimaumbile baina ya ke na me hupelekea wazungumzaji
wazawa wa lugha kuteua aina fulani ya lugha ya mazungumzo kutokana
na jinsi zao.
Mfano;
Mazungumzo kati ya mwanamke na mwanamke:
Asha: Mambo shosti?
Getrude: Safi tu shoga angu.
Asha: Nakuona umepodoka si mchezo?
Getrude: Mambo ya mfikemo hayooo ………..
Mazungumzo kati ya mwanaume na mwanaume,
Juma: Nambie kamanda.
Mifano,
Umbo la ndani Umbo la nje
Juma umwa maino. Juma anaumwa meno
Mama piki kiakula. Mama anapika
chakula
Kijana mwibi. Kijana mwizi.
Uchamko;
Uchamko ni utaratibu wa kutumia sheria fulani ambazo huweza
kutumika mara kwa mara katika kuunda sentensi ambazo zina urefu
usio na kikomo.Uchamko, hutokana na sentensi zaidi ya moja
kupachikwa katika Sentensi ile ya kwanza ili kuunda sentensi moja isiyo
na kikomo, uchamko hujitokeza katika aina kuu mbili, ambao ni
utegemezi na uambatanishaji.
Utegemezi;
Uteggemezi ni aina ya uchamko ambao hutokana na matumizi ya
maneno kama: kuwa, kwamba, kama, na ili. Pia hutokana na hali ya
kuwepo au kutokea kwa kipashio kimoja cha kiisimu ambacho
hutegemea uwepo wa kipashio kingine. Utegemezi huweza kutokana na;
Upachikaji kwa kutumia vijalizi na urejeshi ambao hutumiwa kuunda
sentensi changamano.
Mfano,
Mbuzi aliyechinjwa jana amepikwa leo.
S
KN KT
N βv T E
N1 T1 S2
KN2 KT2
N2 T2 U S3
KN3
KT3
N3 T3
Utegemezi
Ni uchamko ambao hutokana na hali ya kuwepo au kutokuwepo
Ni uchamko ambao hutokana na hali ya kuwepo au kutokuwepo
Uambatanishaji.
Ni aina ya uchamko ambao hudhihirishwa na uambatishaji wa sentensi
sahili mbili au zaidi. Kwahiyo, huu ni uchamko ambao hutokana na
sentensi ambatano.
Mfano;
Shangazi anapika, mama anaandaa chakula na baba anakula.
S1
KN KT
N T S2
Shangazi anapika KN KT
N T N U
S3
N
T
T
baba
anakula
Kama ilivyo kwa nadharia zingine, nadharia hii pia ina ubora na udhaifu
wake.
Ubora wa nadharia hii.
· Imeweza kuonesha umilisi alionao binadamu katika lugha yake, kuwa
anaweza kuzalisha tungo au sentensi mbalimbali kwa kutumia kanuni
chache zilizopo katika lugha yake.Umilisi huo humsaidia mtumiaji wa
lugha kuunda sentensi hizo hata kama hajui kusoma na kuandika.
· Pia nadharia hii inaonesha kuwa kila mzungumzaji wa lugha
huzifahamu vizuri kanuni chache zilizopo katika lugha yake na
kuzitumia kanuni hizi katika kuwasiliana na jamii inayomzunguka.
· Vilevile nadharia hii ya sarufi zalishi imeweza kuonesha kuwa
binadamu anao uwezo wa kufafanua kipi ni sahihi na kipi sio sahihi
katika uteuzi wa maneno wakati wa uzungumzaji.
· Nadharia hii inamchukulia binadamu kama kiumbe chenye uwezo
endelevu wa kuzalisha sentensi ambayo inaweza kueleweka kwa jamii
inayomzunguka.
· Pia nadharia inatuonesha kwamba upo uhusiano mkubwa kati ya akili,
kufikiri na lugha.Hususan katika dhana ya utendaji mtumiaji wa lugha
anatakiwa kutumia akili anapoteua lugha ya kutumia ili kuendana na
muktadha.
Udhaifu wa nadharia hii.
· Inafafanua namna au jinsi watu wanavyozungumza lugha na sio
kuwaeleza wazungumze vipi lugha hiyo itumike.
· Haitilii mkazo mabadiliko katika lugha hata kama yapo.
· Vipengele kama umbo la ndani na umbo la nje vinaweza kumchanganya
mtu anaejifunza lugha.
Hivyo ni kweli kwamba nadharia ya sarufi zalishi imeleta mapinduzi
makubwa katika taaluma ya sarufi miundo.
MAREJEO
Kapinga, (2012), Katika Dafina ya Lugha: Serengeti Education Publishers
(T) Ltd, Mwanza.
Kihore Y, M. Massamba, D.P. B na Msanjila, Y. P. (2012),Sarufi Maumbo ya
Kiswahili
Sanifu (SAMAKISA): TUKI, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Massamba, D. P. B, Kihore, Y, M na Hokororo, J. I,(2001), Sarufi Miundo ya
Kiswahili
Kiswahili Lugha
Sanifu(SAMIKISA): Tamu
TUKI: Duniani.
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Dar es Salaam.
Matinde, L. (2012),Dafina ya Lugha: Serengeti Education Publishers (T)
Ltd, Mwanza.
Pei na Gaynor, (2012), Katika Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu
(SAMAKISA): TUKI,
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
TUKI, (1999), Kamsi Sanifu ya Isimu ya Lugha: Chuo Kikuu cha Dar er
Salaam.
REPLY
Judikay nerfuler
REPLY
Hongera
REPLY
Enter comment
READ MORE
READ MORE
Powered by Blogger
Theme images by Galeries
trix titus