You are on page 1of 36

KISIMA CHA

TATU
Toleo la 1

Na Mwl. Oscar Samba


Tangazo la Haki na Hati Miliki.

Kitabu hiki hakiuzwi, ila ukiguswa kuichangia huduma hii unaweza kutumia namba
zifuatazo za M-Pesa

+255 (0) 759859287

Angalizo

Pia kumbuka au fahamu kitabu hiki kimetolewa kwa njia ya “ki-elektroniki” kwa hiyo
ubadilishwaji “convert” kwa njia au namna yoyote ile, au uzaji wowote ule na kwa nia
yoyote ikiwemo ya nia ya wizi ama kujinufaisha ni kosa kisheria na kiroho pia.

©Haki Zote Zimeifadhiwa, 2023.

KISIMA CHA TATU,


Toleo la Kwanza, Kimechapishwa na
Haleluya Press, December 2023,
Rombo Kilimanjaro Tanzania.
Na Mwl. Oscar Samba.
Yaliyomo

Tangazo la Haki na Hati Miliki. ...................................................................................................................... 2

1. Mukutadha wa Kufukuwa Visima. ........................................................................................................ 4

Mambo Kadhaa Yakuzingatia:................................................................................................................... 5

1. Zitazame Changamoto Zinazokukuta Kwa Jicho Chanya. ..................................................................... 5

2. Unapaswa Kuwa na Imani Dhabiti, lakini pia na Nia au Utayari wa Urejesho ...................................... 9

2. Mukutadha wa Kugombaniwa kwa Visima na Ushindi Katika Kisima cha Tatu. ..................................... 12

Msaada: Ukipanda Mua Panda na Majivu .......................................................................................... 17

Kanuni ..................................................................................................................................................... 18

1. Omba Rehema. ................................................................................................................................... 18

2. Fukuwa Malango Watu Waliofukiwa Kama Kisima............................................................................. 26

3. Fahamu Hatua Mbalimbali za Vita. ..................................................................................................... 28

Sala ya Toba ................................................................................................................................................ 31

Orodha ya Vitabu Vyetu .............................................................................................................................. 32

Mawasiliano ................................................................................................................................................ 35
1. Mukutadha wa Kufukuwa Visima.

Inawezekana kwenye maisha yako kuna vitu vimefukiwa na adui kama Wafilisti
walivyofukia visima vya Ibrahimu. Mwanzo 26:15 Na vile visima vyote walivyochimba
watumwa wa baba yake, siku za Ibrahimu babaye, Wafilisti walikuwa wamevifukia, wakavijaza
kifusi.

18 Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu
babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu;
naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

Yamkini hukuchimba wewe na hata yawezekana aliyevichimba ni wewe pia; la muhimu hapa
ni kufahamu ya kuwa vipo visima katika familia yako, au kwenye maisha yako binafsi
vilivyopaswa kukupatia riziki lakini vimefukiwa.

Ipo miradi mbalimbali ambayo enzi za baba au mzazi wako, au zama fulani ilikuwa ikifanya
kazi lakini kwa sasa imefukiwa. Usijali, upo upako wa kifukuwa visima siku ya leo. Kitabu hiki
kimekuwa kama sehemu ya huo upako. Umesota vya kutosha, lazima sasa ifike mahali uanze
kufukuwa visima. Umeishi maisha ya taabu vya kutosha sasa ni wakati wa kunywa maji ya
kisima chako mwenyewe.

Umenyanyasika na ajira za watu vya kutosha, sasa ni wakati wa kufukuwa kisima au visima
vya kale ambavyo zama hizo vilitumika kama njia ya kupitishia kipato kwa familia, wazazi
na hata wewe binafsi.

Lakini pia inawezekana ni eneo la kihuduma; kipawa au karama fulani iliyokuwa ikifanya
vyema sana hapo zamani lakini sasa imeuawa na adui, au ulishindwa kuichochea na mwenye
kufukia akapata mwanya akaifukia: nayo au navyo pia huhitaji kufukuliwa.

Kisima chako inawezekana kikawa na mahusiano, kila unapochumbia unakwama. Au ni mke


au mume, aliyekuacha; nawe umefahamu kabisa kisima hicho kimefukiwa na adui, sasa ni
wakati wa kukifukuwa.

Yamkini ni mahusiano yako na ndugu, mzazi, jamaa; rafiki na hata mtu wako wa karibu sana
kikazi au kihuduma; nacho kisima hicho kinahitaji kufukuliwa. Kufilisika, au mtu aliyesimama
kama mchonganishi na mashitaka yake ya uongo na kukuvurugia mahali. Hata kama ni kweli
ulikosea, ninachofahamu ni kwamba kwa Mungu kuna msamaha; na kisha tunakifukua hicho
kisima.

Nataka ukae mkao wa kufukuwa visima vilivyofukiwa na Wafilisti, na kumbuka hata


mpendwa au mchungaji wako anaweza kugeuka kuwa Mfilisti wako. Mke au mume, rafiki au
mfanyabiashara mwenzako, haijalishi ni nani ila ninachojua ni kwamba hapa upo upako wa
urejesho; upako wa kufukuwa vilivyofukiwa.

Mambo Kadhaa Yakuzingatia:


1. Zitazame Changamoto Zinazokukuta Kwa Jicho Chanya. Kuna mambo
ambayo hutokea yakiwa na nia njema kabisa ya kukusaidia ili kuhuisha akili zako kama mwana
mpotevu kwa ajili ya kufukua visima. Mfano unaweza kufukuzwa kazi, lakini Mungu akawa ana
nia ya kukutaka uamuwe kujiuliza mbona zamani nilikuwa na kazi yangu binafsi; mbona zamani
nilikuwa nimejiajiri? Ni aina ya maswali ambayo hunuia kukusaidia au kuzisaidia akili zako ili
uweze kufukuwa visima. Ni kuamshwa kwa fikra, ni kuhuishwa.

Mwana mpotevu alipotapanya mali, aliona ni jambo jema tu. Ila njaa ilipoingia, naye
kuteseka ndipo akili zilipomjilia na kuamua sasa kururea nyumbani. Kwa hiyo, taabu
ilikuja ili kumjulisha umekosea! Unaishi chini ya kiwango cha maisha uliyopaswa kuishi
hapo awali; unaishi maisha yasiyo yako.

Maana roho ya kufukia visima haifukii tu visima vya mwili, bali huwa inavifukia rohoni;
kwa maana kwamba akili nazo huwa zinakamatwa. Roho inayokufunga jela, haiishi tu
kukufunga ikakuacha bali huwa inakulinda ili usije ukatoka!

Wakati na Petro au Petro, Paulo na Sila walipokuwa jela bado kulikuwa na ulinzi
maalumu dhidi yao. Na alikadhalika visima vikifukiwa, uwe na hakika na akili au fahamu za
muhusika nazo huletewa usingizi mzito. Ndio maana utamuona ni mtu mwenye furuksa kubwa
tu, lakini shamba lake amelitelekeza kijijini. Wakati angeweza hata kulilima akiwa mjini, na
bado maisha yake yakaenda sawa. Kasoma lakini ukimshauri atafute kazi kwenye "fani" au ujuzi
aliosomea bado anakuwa mkali. Sasa Mungu akitaka kukusaidia, huwa ana ruhusu dhoruba zije
ili kukufanya ufikiri kwa upya moyoni mwako; Luka 15:15 Akaenda akashikamana na mwenyeji
mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe.

16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu
aliyempa kitu. 17 Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba
yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.

Shika sana haya maneno, "akazingatia moyoni mwake!" Alafu tazama


kilichofuata! Utagundua ni fikra mpya, zilizonuia kurejesha uhusiano mwake na
baba yake. Ghafula akagundua maisha ninayoishi siyo yangu, kuna kitu
kimefukiwa kwenye maisha yangu. Haijalishi Mfisti wake ni mimi mwenyewe
kwa kutapanya mali, ila ninachojua baba atanisamehe. Akaamua kufanya
matengenezo.

Nawe usikubali kutazama kila tatizo kwa sura hasi, kama kikwazo au vita. Bali mengine
yanakuja yakiwa na sababu ya kunuia kuzisaidia akili zako ili kufanya marejesho kwa
ulivyopoteza. Ukiweza kusoma kitabu chetu cha USIFIE JANGWANI, basi nenda moja kwa
moja kwenye ujumbe unaoitwa Majira ya Farao Asiyemjua Yusufu. Utakutana na ujumbe na
somo litakalokusaidia kuyaona haya majira kwa sura pana zaidi.

Kwa nini haya majira?


Mungu alishawahaidia toka awali ya kuwa watakaa utumwani miaka 400, lakini hadi wakati huo
mwaka wa/ni miaka ya 430, hawajatoka bado. Maana walikuja kutoka mwaka huo. Ilibidi
ayaruhusu haya majira ambayo sijui sana yalichukuwa muda gani, ila ninalofahamu ni kwamba
yaliwasukuma katika hatua za kudai uhuru wao. Waliteswa na baada ya kuteswa ndipo walipolia
mbele za Mungu na Mungu akasikia kilio chao. Kwa nini hawakulia toka miaka ya 390? Ni kwa
sababu hawakutambua ya kuwa wapo katika eneo ambalo hawahitajiki tena baada ya miaka 10
inayo.
Kwa kifupi ni kwamba akili zao hazikuweza kusoma alama za nyakati. Unaniuliza
Mwalimu umejuaje? Kwani Danieli alijuaje ya kuwa muda umeisha wa kukaa Babeli? Ni
kwa sababu alikuwa akisoma vitabu, alikuwa akimsoma na kumfuatia Mungu. Wao
walishindwa nini kufuatilia ahadi za Ibrahimu pale Mwanzo 15 kuhusu muda huo?
Inawezekana hali yao ya kiroho au mahusiano yao na Mungu hayakukaa vizuri, lakini pia
kuridhika na maisha, tatu kukosa mtu wa kujisomea, kama Danieli; ukifikia ukomo wa
kutaka maarifa ni umekubali kufukia akili zako wewe mwenyewe! Kuna watu ni
Wafilisti wa visima vyao wenyewe kwa uzito tu wa kutaka kujua zaidi.

Miaka hiyo ya 390 ndipo Musa alipokuwa akiibukia. Alikuwa na nia ya kuwakomboa,
alipokuwa akimua au tukio lile la kumuamua Mwebrania mwenzake dhidi ya mzawa liloishilia
na hatua ya kumuua huyo Mmisri lilikuwa na maana ya ukombozi wao. Lakini wakamkataa
kama Stefano anavyotuambia kwenye Matendo ya Mitume; 7:35 Musa huyo waliyemkataa,
wakisema, Ni nani aliyekuweka kuwa mkuu na mwamuzi? Ndiye aliyetumwa na Mungu kuwa
mkuu na mkombozi, kwa mkono wa yule malaika aliyemtokea katika kile kijiti.

Katika kumkataa huko kulionyesha dhairi ya kuwa akili zao hazikuwa tayari kutoka
utumwani. Hawakuwa tayari kufukuwa kisima cha ahadi ya nchi ya Kanani kama Bwana
alivyowahaidia wazee wao. Utumwa ule ulifunika akili zao. Ilibidi Musa akae utumwani
miaka 40.

Mungu alipoona sasa imepita miaka kadhaa toka ahadi iachiliwe, ndipo akayaruhusu
haya majira ya Farao asiyemjua Yusufu ili kuhuisha akili zao. Danieli aliyaomba maombi ya
urejesho kwa wakati kabla ya muda kuzidi na bila utumwa kuzidishiwa makali, ni Daniel 9.
Wakati Wengine walilazimika kuyaomba baada ya taabu kukazwa; Kutoka 1:8 Basi akainuka
mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu.

10 Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao
wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii. 11 Basi
wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji
ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi.

Kutendwa kwa akili maana yake ni jambo ambalo lilihusha fahamu au akili zao pia!
Ashukuriwe Mungu aliyeliruhusu hilo, hata kama adui hakufahamu moja kwa moja alichokuwa
akikifanya, ila Mungu alilitumia kama sehemu ya kuziamsha akili zao. (Wakati wa taabu usione
haya au aibu kumkumbuka Mungu. Usiseme mimi huwa "namtafutaga" mtumishi wakati na
shida tu! ) Huwa "nawaambiaga" sisi ni kama hosipitali; sasa ukiwa unakuja wakati ukiwa
mgonjwa tu hatuwezi kushangaa! Na usipokuja pia hatuna kazi. Furaha na ajira yetu ni kuona
tunatatua matatizo ya watu. "Lakini pia unaweza kwenda hosipitalini kwa ajili ya kufanya
'chekapu' ya afya. Kwa hiyo, wakati mwingine nikutie moyo kuwakumbuka wakufunzi au
walimu wako na kuwashirikisha mema yako wakati wa mafanikio. Japo imizo hapa ni kwamba
ukikwama au kubanwa usiache kurudi kwao kwa kuona haya.

Taabu yao iliamsha akili zao; Kutoka 2:23 Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa
Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao
kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa.

Kutoka 2:24 Mungu akasikia kuugua kwao, Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya
na Ibrahimu na Isaka na Yakobo. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya
makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na
Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. 7
Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia
kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;

8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi
njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori,
na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena
nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.

Sijui kama umeona jambo hapo? Hii ni faida kubwa sana ya haya majira. Ninakutaka
kuwa makini maana hata wao kidogo wangekwama hapa. Badala ya kutazama faida ya hili pito
kama ninavyokufunza kwenye kile kitabu chetu cha MUONE MUNGU NYUMA YA PITO
LAKO, wao waliishilia kuwa na uchungu na maumivu yaliyotaka kuziba maskio yao ya ndani;
hawajui Mungu amenuia kutumia kilio hicho kama sehemu ya kuwatoa utumwani. Kwa hiyo
Musa alipowaendea ugumu ukajidhiirisha; Kutoka 6:6 Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni
YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na
utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa;

7 nami nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ni
YEHOVA, Mungu wenu, niwatoaye mtoke chini ya mizigo ya Wamisri. 8 Nami nitawaleta hata
nchi ile ambayo naliinua mkono wangu, niwape Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; nitawapa iwe
urithi wenu; Mimi ni YEHOVA. 9 Musa akawaambia wana wa Israeli maneno haya; lakini
hawakumsikiliza Musa kwa ajili ya uchungu wa moyo, na kwa ajili ya utumwa mgumu.

Kuwa makini uchungu wa jaribu lako usijekufanyika kikwazo, au kwazo katika safari
yako. Mungu anaweza akaja na ujumbe wa kukutoa kifungoni lakini ukajikuta
unasukumia mbali sauti yake. Fikra zako mwenyewe za kukata tamaa zikakuzuilia
kufukuwa kisima. Ukaanza kujisema lakini hii biashara nimeifanya miaka mingi bila
mafanikio, nimeingia hasara na kujikuta nakuwa mtu wa madeni tu. Nimeomba au
nimetuma barua za maombi ya kazi hadi mwenyewe nimechoka: kwa hiyo sioni haja au
sipo tayari. Uwe na hakika kuna mahali unajikwamisha. Lazima uweze kutambua
kubadilika kwa majira. Muda wa kukaa utumwani umeshapita, sasa ni wakati wa kutoka.

Japo kwenye kutoka nako sio kwepesi, lazima uwe tayari kupambana na askari
waliowekwa kaburini kukulinda ili usifufuke kutoka kwenye kaburi la uchumi, kwenye kaburi
lililozika ndoa au kibali chako kihuduma. Lazima uwe na huo utayari. Niposa tukakuwekea
mada ya pili ili kukupa mukutadha au picha hii kiwazi zaidi. Maarifa ni muhimu sana, ili uweze
kutenda vyema katika kila hatua ya maisha yako.

Isaka alilitambua hilo, kufukuzwa kwake na Wafilisti katika mji au eneo alilokwapo
ilikuwa furuksa ya kufukua visima. Nawe tazama mambo kwa jicho kama hilo. Kuna muda
kufukuzwa kazi, kusimamishwa huduma, kuondolewa kwenye nyumba ya kupanga ni sehemu ya
kuinuliwa. Sio kuzalilishwa na kuabishwa, bali ni ngazi na mwanzo wa kufufua karama na
vipawa, ni mlango wa kazi nzuri na hata ajira yako, pia ni mlango wa kupata nyumba yako.

Hukuwahi kusikia ule msemo usemao ya kwamba mlango mmoja ukifungwa mingine
saba inafunguliwa! Unafikiri ni maneno ya kawaida tu! Tunapaswa kutazama mambo
kwa jicho chanya! Katikati ya tatizo unatakiwa kuuona utukufu wa Mungu nyuma yake!
Ndiposa ninakutaka kuendelea kumuabudu Mungu au kuendeleza uhusiano wako na
Mungu vyema unapokuwa upo mahali pagumu katika kitabu chetu kile cha KATIKATI
YA SHIMO MKUMBUKE MUNGU.

Muone Isaka; Mwanzo 26:16 Abimeleki akamwambia Isaka, Utoke kwetu, maana wewe una
nguvu sana kuliko sisi. 17 Basi Isaka akatoka huko akapiga kambi katika bonde la Gerari,
akakaa huko. 18 Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za
Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu;
naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

Neno ondoka wakati mwingine huwa na maana ya nenda kafanikiwe zaidi. Huwa na
maana ya kwa nini unakaa hapa na unaendelea kuteseka na maisha haya magumu wakati
zipo nafasi nyingi za kukufanikisha! Ndio maana wanakufukuza kazi ili sasa ukanzishe
kampuni yako itakayo ajiri maelufu ya watu.
Uliwahi kulielewa hili andiko? Kutoka 1:12 Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo
walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli.

Lazima ujifunze kuiona roho ya maongezeko katikati ya roho ya kukuzuia


kuongezeka kwa sababu tu ya kuwa umeanza kuwa na nguvu! Hii tumeiona pia kwa Isaka,
ya kwamba alipoanza kupanuka na kuwa na nguvu, mfalme anamuondoa kwa sababu ya uwezo
wake. Ukisoma kwa umakini utagundua hili jambo kiupana sana, lakini hata hapo pia Mungu
alikuja kumnufaisha zaid, na zaidi.

Yaani mimi siri kubwa ninayokumegea ni kwamba, ukihitaji kufanikiwa vyema, au


kuvuka vyema hapa; jribu likikupata wewe endelea kumshukuru Mungu. Endelea kumtafakakari
yeye, usikubali kunung'unika wala kuvunjika moyo. Mambo hayo niliyokukataza hapo,
ukiyafanya yatakupiga upofu. Hutaweza kuviona visima, na kama Roho akijaribu kukumbusha
uchungu utaongezeka zaidi. Badala ya kutaka kuvifukuwa utajikuta unalia kwa kusema kwamba
sijui nina mkosi gani, niliwahi fanya biasha fulani nayo ikafa, nikanunua shamba nalo
nikazulumiwa, niliwahi tengeneza "bekari" au tanuru la mikate nalo ni hasara tupu, nimesomea
kitu fulani lakini kila nikifanya au nikikifanya sifanikiwi! Hujui kuwa ni majira ya kuvifukuwa.
Na hujui ya kuwa ni Roho Mtakatifu anakukumbusha ili uanze sasa kufukuwa hivho visima!

Lazima ujiulize kwa nini hapo awali ulikiwa huyakumbuki hayo yote? Ile umekumbuka
ni kwamba ni ishara ya msimu mpya. Ni ishara ya kwamba kuna jambo linapaswa
kuzaliwa. Kwa kifupi ni kwamba roho ya manung'uniko itapofusha fikra zako na kuziba
maskio yako yasiweze kusikia na kusikia.

Ni kwamba, marejesho au ufukuaji wa visima unahitaji upako maalumu. Sasa hakikisha


unakuwa na hali ya ibada moyoni mwako ili huu upako uweze kufanya kazi, ukijitenga na
Mungu ni unakaa mbali na chanzo cha upako wa kukuvusha.

2. Unapaswa Kuwa na Imani Dhabiti, lakini pia na Nia au Utayari wa


Urejesho. Ndugu zake na Lazaro walikuwa wamefiwa na kaka yao. Yesu alisimama katika
nafasi kubwa sana ili kumfufua. Walikata tamaa kiasi chakutaka hata kumzuilia Yesu pale
kaburini walipoambiwa waliondowe jiwe na kujikuta Martha akijibu kuwa ananuka sasa. Kwa
rehema zake Yesu akaanza tena kumjenga kiimani. Sio kila mara utakutana na neema ya namna
hii; japo ni kweli ameketi hata sasa mkono wa kuume kwa Mungu Baba akituombea: lakini pia
kadhalika Roho Mtakatifu hutuombea kwa kuugua tena kwa jinsi isivyotamkika! Lakini nafasi
yako ni muhimu sana. Ukisoma kisa hiki chote utagundua ya kuwa muda mwingi Yesu
alipokuwa akiongea na Dada huyu wa Lazaro alikuwa akijikita katika kumjenga kiimani.

Alitamani ajaye imani, awe na utayari pamoja na nia dhabiti ya kufufuka kwa ndugu yake.
Na aliwekeza kwa Martha zaidi hata ya kwa Miriamu; japo inafahamika Martha ndiye mkubwa,
lakini funzo moja wapo hapa ni kwamba Mungu muda mwingi hutafuta mtu, na sio sana sana
watu wengi; kuna muda huhitaji mtu mmoja tu ili asimame kwenye nafasi yake.
Hii ikupe kuniona ya kuwa wewe ni mtu muhimu katika kuisaidia familia, kanisa au hata
ukoo wako ama timu yako ya kwaya kanisani. Acha kulalamika bali simama sasa kwenye nafasi
yako. Nikutie moyo kupitia tukio zima, ila hapa nakumegea tu mara haya ya ufufuo; Yohana
11:39 Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana,
ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa


Mungu? 41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba,
nakushukuru kwa kuwa umenisikia. (Baada ya jiwe kuondolewa ndipo Yesu anachukua
hatua. Kwa hiyo kuna mambo hayawezi fikia hatua nyinge hadi utimize wajibu fulani.)
43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.

44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake
amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.

Unajua ni kwa nini Yesu alikuwa akiuliza maswali kama haya alipokuwa akihitaji
kumuombea mtu! Ama hata kuibua changamoto fulani!

Kwa Kipofu Bartimayo:


Marko 10:51 Yesu akamjibu, akamwambia, Wataka nikufanyie nini? Yule kipofu akamwambia,
Mwalimu wangu, nataka nipate kuona. 52 Yesu akamwambia, Enenda zako, imani yako
imekuponya. Mara akapata kuona; akamfuata njiani.
Kwani Yesu hakujua ana shida gani! Sialikuwa anaonekana kabisa ya kuwa haoni.
Swali hili lilikuwa linahitaji mambo haya muhimu ninayokufunza hapa. Mahojiano
mengi kati ya muombaji na muhitaji yananuia kupata kumjengea haya mambo,
ikitangulia na kufahamu au kutaka kuyachunguza kama yamo ndani yake kwa kiwango
gani!

Kisa cha Mwanamke Myunani:


Nia ilikwepo, utayari ulikwepo...na imani pia...Yesu alikuwa akivitafuta hivyo. Mambo
hayo yakiwepo mtu atavuka kila kikwazo hata kama ni kutoboa dari atakuwa radhi kupishana
matofali ili tu mujiza utokee. Marko 7:25 Ila mara mwanamke, ambaye binti yake yuna pepo
mchafu, alisikia habari zake, akaja akamwangukia miguuni pake.26 Na yule mwanamke ni
Myunani, kabila yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika binti yake.
27 Akamwambia, Waache watoto washibe kwanza; maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto,
na kuwatupia mbwa. 28 Naye akajibu, akamwambia, Naam, Bwana, lakini hata mbwa walio
chini ya meza hula makombo ya watoto.

29 Akamwambia, Kwa sababu ya neno hilo, enenda zako, pepo amemtoka binti yako. (Neno
hilo! Lilibeba ni imani yake. Unanijliza najuaje, twende huku;Mathayo 15:28 Ndipo Yesu
akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona
binti yake tangu saa ile.)
Nia ilimsukuma kung'ang'ania mujiza. Lakini pia utayari ulimzulia kukata tamaa.
Alikuwa radhi kuvuka kila kikwazo.

Marko 7:30 Akaenda zake nyumbani kwake, akamkuta yule kijana amelazwa kitandani, na yule
pepo amekwisha kumtoka.

Baba wa Mtoto Mwenye Kifafa:


Kwa mtu huyu Yesu alihitaji kwanza kumsaidia kiimani, na mtu huyu nampenda sana
maana alipogundua udhaifu wake alimuhitaji Yesu amsaidie katika madhaifu hayo ya
kupungukiwa na imani! Ni baada ya kufanya kosa la kumwambia Yesu kama akiweza....mtu
huyu aliadhiriwa na kushindwa kwa wanafunzi wake Yesu...(nataka ujifunze umuhimu wa imani,
nia na utayari!) Mtu huyu alikuwa na nia dhabiti, na utayari pia.
Lakini imani yake ilipelea au ilitindika. Na inawezekana hali hii ilijitokeza ikiwa ni matokeo ya
wanafunzi wake kushindwa kumtoa au kumsaidia hitaji lake... Na wengi leo imani zao
zimetindika na kuadhiri aidha imani, nia au utayari wao wa kuendelea kumtegemea Mungu au
kumuamini. Kwa kuwa tu umeshaombewa maeneo kadhaa na waombaji kadhaa na hujapona au
hujapata mpenyo basi unaishilia kukata tamaa!

Unaenda hata sasa kwenye maombi lakini kiukweli ndani kumepunguka..na moyoni
unamwambia Yesu kupitia muhubiri wake ya kwamba ukiweza waweza tusaidia..! Maana hata
ukiambiwa uelezee tatizo linalokusibu unajikuta unaelezea tu kushindwa kwa waombaji
waliotangulia...Juwa sana yule kiwete wa mlango mzuri alikaa pale muda mwingi...na Yesu
alimfahamu...lakini hakumponya kipindi hicho...maana wakati wake ulikuwa ni kipindi cha
Yohana na Petro...tazama pale jinsi muujiza ule ulivyoleta badiliko la kiinjili ndipo utakapoona
umuhimu wake kwa muda ule. Maana ulitikisa baraza zima la mji. Maana yake kuna namna
misingi ya mji ilitikisika. (Ukiona umefanya jambo la kiroho na eneo fulani kutikisika uwe na
hakika kuna jambo limetokeo. Usiwaone viongozi wanaokuinukia bali ona vitu vilivyotikiswa
vilivyokuwa chini yao.)

Tujione nilipoanzia msingi wa nasaha hii; Marko 9:22 Na mara nyingi amemtupa katika moto,
na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia. 23 Yesu
akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. 24 Mara babaye yule kijana
akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
2. Mukutadha wa Kugombaniwa kwa Visima na Ushindi Katika
Kisima cha Tatu.

Kuna mambo kadhaa na muhimu unayohitaji kufahamu kwanza kuhusu kisima cha tatu.
Ni kwamba ni kisima cha ushindi, katika hili hakuna anayeweza kukupokonya au
kukunyanganya tena. Maana kisima cha kwanza walikigombania, hakufa moyo
akafukuwa cha pili nacho wakakipigania, napo hakukata tamaa bali aliendelea kufukua
na cha tatu ambacho hawakukiweza tena. Mwanzo 26:19 Watumwa wa Isaka
wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.

20 Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu.


Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.

21 Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna. 22
Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake
Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.

Inawezekana umekuwa na mchumba wa kwanza, adui akakupokonya na kusikia kaolewa


au kashaowa mtu mwingine; usife moyo endelea kufukua na kingine. Kuna mtu yamkini
amefanya kazi au ametafuta ajira ya kwanza na hata ya pili wakamfanyia fitina. Wala
hutakiwi kukata tamaa. Maana kisima cha tatu kinakuja, ambacho adui hataweza
kukupokonya tena.

Mukutadha mkuu wa kitabu hiki nikukutaka kutokukata tamaa. Maana inawezekana huyo
mchumba ni kisima tu cha pili, wala usijione una mkosi, maana yamkini alikuwa haonekani, ila
kwa maombi yako akaanza kuonekana machoni pa watu, ndipo wakamuona na kumnganyania.
Kwani kabla yako hakuwa hata na kibali, ila baada ya kuwa naye kwenye mahusiano ni kama
vile nyota imeanza kung'aa ama kung'ara. Wala usijiulize maswali mengi, maana waliogombania
visima hawakujua tena kama vilikwepo hapo? Ninaamini kabisa historia waliijua, hata kufukia
inawezekana walihusika kabisa. Lakini macho yao na fikra au akili zao zilifukiwa pamoja na
kisima. Lakini vilipoanza kufukuliwa ndipo waliposhituka na kuanza kusema hivi ni vyetu,
mashindano yakazaliwa hapo.

Na wewe u sawa na mtu aliyefukuwa kisima au visima, awali hakusifika wala kuuona
uzuri wake. Kwa nini? Ni kisima chenye kifusi, lakini sasa kwa kuwa kinatoa maji ndipo
wanaanza kuona uzuri wake na kuanza kugombania. Wala usiwasuate na kuwauliza kwani hapo
awali mlikuwa hamumuoni? Wala usitake kumuuza huyo mpenzi wako wa zamani ya kwamba
ni kwa nini asijliuze hapo awali walimchukia na kumuona wa kawaida ila sasa iweje ang'ae
machoni pao? Wewe fahamu ni kisima kilichofukuliwa. Kila akionaye atakipenda tu. (Zamani
walikikanyaga nakupita juu yake, wakaona ni njia. Na pengine kilipofukiwa kikawekwa na jiwe;
kwa hiyo wakisafiri na kuchoka walikaa juu yake. Lakini wewe ukawa sawa na wale wenye
mashine za kupima aridhi kama chini kuna madini au maji yanapatikana; ukaona na kuanza
kufukuwa.) "Songa mbele kisima chako cha tatu kipo."

Usijiulize sana kwamba eneo hilo lilikaa muda mrefu bila biashara, iweje sasa umeanza
tu wewe kila mtu ameanza kulipigania. Kwani hapo awali walikuwa hawalioni? Uliwahi kupita
aneo mjini ukatamani kama ungefungua hapo biashara; kisha baada ya muda ukakuta kuna mtu
kashawahi! Uwe na hakika kuna namna ulifukuwa kisima, ile uliona na kwenda kuombea, au
kutamka neno; rohoni umefukuwa kisima. Na ukitaka kujua utakuta biashara ile ile uliyoitaka
kuifanya ndiyo iliyokuja kufunguliwa. (Kweli adui anaweza kukuibia wazo, ndio maana
unahitajika kujifunza kufunika mawazo yako kwa damu ya Yesu, ila yote katika yote kufukuwa
visima kupo.)

Hutakiwi kukata tamaa kisa adui amegombania kisima chako, fahamu kuna visima
vinakuja na hataweza kuvigombania tena. Kubwa zaidi ni kuhakikisha unakaza katika
kuvifukuwa.

Kisima cha tatu kina mambo makuu mawili, ambapo Isaka aliyabainisha na kutujuza,
mosi ni nafasi na pili ni baraka za kuzidi au baraka za maongezeko. Rehobothi yako imebeba
nafasi, na kisha baraka za maongezeko, ukishindwa kufukuwa kisima cha pili ni unanizuilia
kuipata Rehobothi yako, usikubali kukwamia Eseki ambacho ni kisma cha kwanza wala Sitna
ikiwa ni chapili bali nenda hadi katika Rehobothi yako ili ujipatie nafasi pamoja na roho ya
maongezeko; Mwanzo 26:22 Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho
hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa Bwana
ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.

Inawezekana fika kabisa wewe ni mchungaji, na umefungua ama kuchunga kanisa la


kwanza, napo wamekufanyia vita na kukunyanganya. Usife moyo, tazama Rehobothi
wako yupo. Unapofika hatua ya kushindwa kuendelea kumtumikia Mungu, au kujaribu
kususa huduma ni unajizulia kufika katika kituo chako ambacho utafika mahali kama
Isaka pa kusema; "... Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa Bwana
ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi."Mwanzo 26:22 .

Kuna mambo mengine yanaachiliwa ili kukutoa Eseki yako au Sitna kwa nia njema
kabisa ya kukufikisha Rehobothi kwako. La muhimu ni macho yako ya ndani kuwa tayari
kumsikia Mungu. Akikwambia hapa ni Edeni usitoke hicho ni kitu kingine. Ila kama ni jambo tu
la ubishi wako, na upofu wako wa kutokuona mbele kuna Rehobothi yako; uwe na hakika
utakwama.

Narudia tena ya kwamba, ni lazima kujifunza kumuona Mungu katika mambo magumu,
macho yako yaone uchanya wa mapito na matukio magumu maishani mwako. Kuna
muda unasalitiwa na mchumba kumbe Mungu ameshajua mbele kuna Rehobothi yako.
Kwa hiyo usikubali kuumia sana, ila jifunze kuisubiria na kuipigania Rehobothi yako.
Najua ujumbe huu hautakupa kuachilia kila kitu kizembe. Maana hata Isaka
hakuachilia kizembe, alijua vipo visima viwili mbele. Na ole wao wangesubutu
kumfutilia tena akiwa Rehobothi! Uwe na hakika angewatoa kwa makali ya
upanga hapo. Adui akikufuata Edeni au katika Rehobothi yako lazima uwe mkali.
Na mlango wa vita au upako wa ukali utauona tu. Ila wakija Eseki ama Sitna
wewe kuwa muungwana tu na usonge mbele. Watashangaa walitarajia kukuona
umekonda, umenywea umepoteza matumaini kumbe ndo kwanza unanawiri na
kuchanua. Kwa nini? Unajua Rehobothi yako ipo.

Kwa Isaka maneno Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi yalikuwa na
maana gani? Ni utimizwaji wa Ahadi ya kiagano juu yao. Kuhusu kumiliki, na kuzaana. Nafasi
maana yake kwa mara ya kwanza anapata eneo ambalo ataishi bila bugudha. Fahamu huko awali
alikuwa akihamishwa na kukimbizwa na mfalme na hata wenyeji wa nchi kumbugudhi yeye au
babaye. Lakini sasa anapokea hakikisho la kuwa na umiliki wa kisehemu chakekwa wakati ule;
na nchi yao kwa wakati ujao.

Kwa hiyo, havikuwa vita vya urithi vya kawaida, haikuwa vita vya kugombania
mali vya kawaida au vya kumfilisi tu. Bali kiroho alikuwa anafukuzwa katika nchi.
Ili nini? Asiwe na makao wala asizae na kuongezeka.

Hawakuwa wanafukia visima tu, kama visima bali walikuwa wanazika ndoto zake au za
uzao wao wa kuja kuishi hapo. (Hii ikufungue macho sana, usije kutazama vita unavyokutana
navyo kama vya kawaida, kwa kuona ni jambo dogo kumbe kiroho unazuiliwa jambo kubwa
sana.) Ndio maana alipopata cha tatu kichoitwa Rehobothi hakuna namna aliendelea
kunyanyaswa tena. Na ndipo mkuu wa nchi alipomfuata na kufanya naye mapatano.

Hii inatupa kufahamu ya kuwa walipokuwa wanafukia visima vya baba yake Ibrahimu
hawakuwa wanafukia mali za marehemu bali walikuwa wanafukia ahadi za Mungu au
mbaraka wa Mungu kwa uzao wake. (Japo walisahau ya kwamba katika baraka hizo
walihaidiwa nao pia: kama mataifa kufaidi pale kwenye Mwanzo 22 ndiyo maana
Eseki..na Tasna... yaani kisima cha kwanza na cha pili vilikuwa vyao.)

Visima vile vilikuwa ni ishara ya mbaraka wa Mungu kwa uzao wa Ibrahimu. Na adui
akijua kuwa kwako kuna baraka ya namna hii, vita vyake sio vidogo. Kwa wengine ndoa ni hii
ishara, na ukiwa na ndoa ya namna hiyo uwe na hakika utakutana na vita vikali sana. (Hii ikupe
pia kupigania visima vyako, wala usikubali kuvipoteza kirahisi.)

Baraka za uzao na kumiliki nchi zisingeweza kuwa kwa Isaka mpaka amefukuwa visima.
Na kwa mataifa ikiwemo taifa la Filisti baraka hizi zisingeweza kuwa hai hadi visima
vimefukuliwa.

Hukuwahi kuona hata ndugu waliokupiga vita nao wamefanikiwa mara tu baada ya wewe
kuanza kufanikiwa? Uwe na hakika walifukia na visima vyao; (wapokufukuza, walifukuza
mbaraka! Ulipokaza na kufanikiwa: nao pia wakaanza kula matunda ya mbaraka) yaani kile cha
kwanza na cha pili. Sema tu hawakujua wanajua. Na adui tabia yake ni moja, yupo tayari
asababishe ajali itakayouwa watu wote kwenye ndege au basi, akinuia kumua mtu mmoja tu
ambaye ni muhubiri wa injili. Kama Mungu alivyokuwa radhi kufanya lolote bila kujali kuna
wafanya biashara wenye mkopo wa Kabaila au benki kwenye melikebu aliyopanda Yona
akimtafuta tu Yona!

Sasa Shetani yu radhi kuhakimisha na wao visima vyao vinafukiwa akinuia tu kukuzuilia
wewe usiifikie Rehobothi yako. Ndio maana kupenya kwako ni muhimu ili na ndugu
zako nao waweze kupokea mpenyo. Nje ya hapo utasalia unalalamika tu mbona ndugu
zako nao wamekwama eneo ulilokwama wewe! Wenyeji wa nchi hawezi pata visima
vyao viwili hadi wewe umeamua kuvifukuwa; kuna muda wataweza kufukia lakini
wasiweze kufukua. Adui kuna muda anajua kuloga lakini hajui kuagua. Kule Misri
kipindi cha Musa waganga wa Farao walitengeneza na wao vyura ili kumuiga Mungu
wetu, na wakashindwa kuwaondoa ikabidi Musa aje kuwasaidia. Kwa hiyo usishangae
kushindwa kwao.

Tukio hili la wana wa Israel walipokuwa wakisafiri wakielekea Moabu na wakitokea


Misri, linatupa kufahamu kuwa upako wa fimbo ya enzi ulitumika. Upako wenye maana ya
uwezo wa kisheria au kimahakama katika kupigania jambo hilo. Ndio maana rehema ni muhimu
ili kukupatia haki mbele ya sheria za ulimwengu wa roho na Roho. Hesabu 21:17 Ndipo Israeli
wakaimba wimbo huu; Bubujika Ee kisima; kiimbieni;

18 Kisima walichokichimba wakuu, Ambacho wakuu wa watu wakakifukua, Kwa fimbo za


enzi, kwa fimbo zao. (Kilichimbwa na Wakuu na kikafukiwa na Wakuu! Tazama silaha ya
kukifukia; uwe na hakika ndo ya kuchimbia na kufukulia!)

Ikupe kufahamu pia ya kwamba kipindi kama hiki usikubali kikupite, maana upako huu
huja ili kukuwezesha kupokea mpenyo. Vita vya namna hii bila Mungu kuingilia kati huwezi
penya maana adui anafahamu thamani yake, hawezi kukuachilia kirahisi.

Kikifukiwa na fimbo yao ya enzi, uwe na hakika kuwa inahitajika mamlaka ya fimbo ya
enzi ya Rohoni pia ili kupambana na fimbo yao ya rohoni. Ikupe kufahamu kuwa unaopigana
nao hupigani nao kikawaida, hushindani nao kikawaida. Bali nyuma yao ipo roho, kuna fimbo ya
enzi pia. Sasa rehema itawanyima uhalali tu lazima.

Kumbuka au Fahamu Kibiblia Kisima pia Huwakilisha Wokovu. Hii inatupa


kufahamu Isaka alikuwa akipigania pia jambo la wokovu kwa uzao wake pamoja na mataifa;
Isaya 12:3 Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu.

Kwa hiyo, kama angekwama ni ishara ya kukwama kwa jambo kubwa sana. Maana ahadi
za Mungu kwa Ibrahimu zilihusisha pia wokovu kwa uzao wake. Uzao kama mchanga wa bahari
ni watu kweli wa kwake, lakini zaidi ni uzao hata kwa wale ambao watakuja kuunganishwa naye
kumpitia Yesu Kristo kama Isaka wa pili; kama Wagalatia 3 inavyotujiza. Mimi na wewe tulio
okoka ni sehemu ya kisima kilichofukuliwa.

Sasa kama hujaokoka, tafadhali hii iwe ni nafasi yako ya kumuamini huyu Yesu sasa ili
uweze kunufuka na dhima hii ya womovu. Hayo maandiko niliyokupatia hapo
"commentary" moja wapo ya Matthew Henry imeunganisha hayo maandiko ya Hesabu
21:10-20 na kisima kama wokovu, uzima wa milele, ikitupeleka kwenye maji ya Yohana
7:38-39 (huwakilisha Roho Mtakatifu) na hata hiyo Isaya 12:3 inayonena habari za
wokovu.

Kitabu hiki kimenikumbusha mbali sana! Miaka fulani nilishangaa (nikiwa mdogo
kwenye miaka kumi naa..) nilitoka safarini na kukuta ndugu yangu mmoja au mtu wa karibu
kang'oa maua yangu. Na anatoa sababu fulani tu japo ni za kiroho. Sasa leo ndo ufahamu
unanijia kumbe na mimi nilikuwa nang'olewa kwenye urithi! "Sikuhitajika juu ya nchi."

Kingine nilipotaka kufuga kuku upinzani ulikuwa mkubwa sana kutoka kwa mtu mmoja,
anadai hawana faida. Mara ukienda chuo utamuachia nani, sijui unamtwisha mama mzigo. Mtu
anakuwa mkali hadi unashanga! Sasa ukimya ukanisaidia. Japo haikuishia hapo...uwe na hakika
ya kwamba vita kama hivi havitaki uwe sehemu ya urithi wa familia. Havitaki kukuona ukiwa
unatumia rasilimali za kifamilia kupiga hatua.

Kuna kipindi nilikuwa nachukiwa mimi pamoja na mauwa yangu. (Maana sikuja kuchoka
kupanda mengine.) Unafikiri ni maua ndo yalikuwa yanachukiwa la! Kwani hili sio kwa mtu
mmoja. (Sasa usiulize ni wakina nani!) Ila fahamu ya kuwa lilikuwa ni jambo la kiroho.
Hukuwahi kupitia mahali pagumu kwenye kilimo na ufugaji hadi maua nyumbani yakakauka!
Hadi ukifuga paka aidha wafe au wakimbie, ama wadumaye! Jaribu kufuga mbwa utakutana na
kesi kama hiyo hiyo! Zinakufa biashara na paka nao wanakufa na maua yananyauka tu bila
sababu ya msingi. Lazimisha bustani ndo utaelewa au miti ya matunda.

Upinzani mwingine ni ishara ya kukufahamisha ya kuwa upo vitani, na vita hivyo kuna
kitu vinanuia kufanya. Alipokufa baba ndipo nilipoanza kuelewa maana ya vile vita. Sasa
bahati nzuri nilishapambana navyo toka mapema, ila adui alikusudia jambo gumu kweli
kweli.

Fahamu:
Uchimbaji wa Ibrahimu kama mvumbuzi, au mwanzilishi; na "strago" au kuteseka ama
kupambana kwa Isaka katika kufukuwa vilivyofukiwa kulikuwa ni mtaji kwa ajili ya uzao wake
ujao. Nawe usiache kupambana maana ni nani ajauye kuwa mapambano yako ni mbegu kwa ajili
ya washirika wako au watu ambao Mungu atakupa kuwachunga ama kuwaongoza na hata uzao
wako; Kumbukumbu la Torati 6:10 Tena itakuwa atakapokwisha Bwana, Mungu wako,
kukuleta katika nchi aliyowaapia babu zako, Ibrahimu na Isaka na Yakobo, ya kuwa atakupa;
miji mikubwa mizuri usiyoijenga wewe; 11 na nyumba zimejaa vitu vyema vyote usizojaza
wewe, na visima vimefukuliwa usivyofukua wewe, mashamba ya mizabibu na mizeituni
usiyoipanda wewe, nawe utakula na kushiba.

Msaada: Ukipanda Mua Panda na Majivu. Sijui aridhi ya kwenu, ila huku kwetu
nilijikuta naingia hasara mara kadhaa. Niliwahi kuleta mbegu ya mua kutoka Singida, nikiipokea
Dodoma na kuifadhi kisha kuja kuipanda huku Rombo-Kilimanjaro nayo cha ajabu ikaliwa.
Sikujua maana mbegu kadhaa nazo zilikuwa zikiliwa.

Afadhi ioteshwe kipindi ambacho sicho cha mvua nyingi, au eneo husika liwe halina maji
mengi. Likiwa tu na maji mengi ni kosa. Maana kuna aina fulani ya wadudu ambao hushambulia
sio mbegu au kipande kilichopandwa bali chipukizi likiwa teke, yaani bado changa.

Lakini, ukiotesha na majivu, hakika hawawezi kusogelea. Hii ni siri hata kwa wale
bacteria au wadudu wanaoshambulia migomba hususani maaeneo ambayo siyo ya mvua nyingi
na unapoamua kuimwagilia basi hujirundika hapo. Na kuna aina fulani ya migomba
hushambuliwaga zaida katika maeneo mbalimbali (tunaita ndizi kisukari.)

Sasa ili uwe salama wewe ukiiotesha otesha na majivu.

Je nataka kukwambia nini hapa!


Kuna jamii tunaishi nazo ni sawa na aridhi yenye hawa wadudu. Hawataki kuona muwa, wala
ndizi kisukari. Kuna roho zinakaa kwa watu wetu wa karibu; kwenye baadhi ya familia au asili
yetu nazo hukinzana na kila mbegu inayopandwa aridhini ya mafanikio ikiwemo miradi na hata
wazo la maendeleo ya kawaida nje ya lile la uchumi. (Baya zaidi kuna madhabahu za makanisa
yetu zimekamatwa na hizi roho, au makanisa yenye mawakala "maajeti" wa kuzimu/wachawi,
katika makanisa mengi eneo la uvhumi au ndoa, karama na vipawa; ufahamu wa kumjua Mungu
hukamatwa sana.) Huzuia watu pia kuokoka, ama kila wakiokoka hawadumu kwenye wokovu.
Ukitaka kufanya mradi wa biashara, kabla ya kupanda tanguliza majivu shimoni. Leo muda
mchache uliopita nimetoka kupanda miwa, na nje ya mbolea ya kuku, nimeweka na majivu pia.

Usikubali kuanza mradi bila maombi ya kutosha. Maombi ni majivu kwa muwa na
ndizi kisukari. Maombi ni ulinzi kwa hilo wazo. Hata unapochipuza endelea kuhakimisha
unauzingira kwa maombi. Asubuhi na mchana. Uwe na tabia hii hadi pale majira
yatakapobadilika. Ni kweli majira hubadilika, lakini hata kabla ya kubadilika unaweza
kupanda mbegu jangwani au eneo la ukame na ukavuna kama Isaka.

Isaka katika sura hiyo hiyo ya kufukuwa visima, alitokewa na Mungu na kuonywa
kuwa asielekee Misri kusaka chakula bali atafanikiwa akiwa hapo hapo. Alipotii,
ndipo alipokuja na kufukuwa visima. Maandiko hutujuza kuwa alipanda mbevu
na kuvuna sana. Ni nchi kame lakini kwake ikapandwa. Na wewe ukipanda weka
na majivu.
Kanuni
1. Omba Rehema. Rehema ni sawa na kufungua njia ya kupita kwenye eneo ambalo njia
haikwepo. Rehema humpatia Mungu uhalali wa kukupigania, rehema hurejesha neema
uliyowahi kuipoteza au ambayo iliondoka kutokana na uzembe wa kutokuitumia. Lakini pia
rehema huwa na kazi ya kuachilia ama hata kuongeza nguvu za Mungu ambazo hukusaidia
katika kufukuwa visima. Rehema huondosha uhalali wa adui au ile haki ya adui katika kuvifukia,
kuvilinda visifukuliwe na kadhalika.

Kwa hiyo hakikisha unafanya toba kwa muda. Kufa kwa Ibrahimu kuliwafanya
Wafilisti kufukia visima! Sio jambo la kawaida maana Isaka tu fahamu ndiye mrithi pekee wa
Ibrahimu, kivyovyote vile ipo sababu iliyopelekea ucheleweshaji wa urithi huu juu yake.

Je, nataka kukufunza nini hapa!


Migogoro mingi ya miradhi ni matokeo ya kukosekana kwa kitu kama hiki. Ni urithi wako au
wenu sana, ni haki yenu sawa lakini mnaweza kucheleweshwa aidha na mahakama au na ndugu
katika kuipata. Lazima ujifunze kuyatazama haya mambo kiroho. Na wengine sio ndugu bali ni
wabia tu wa biashara na marehemu. Na pengine ukapokonywa kabisa, lazima sasa utambue ya
kuwa hivyo ni visima vilivyofukiwa mara baada ya Ibrahimu kufa. Ndivyo maandiko
yanavyotuambia ya kuwa alipokufa Wafilisti wakafukia visima.
Lakini pia wafuatiliaji wa mambo haya wanajua Isaka ndiye mrithi. Swali ni kwamba alikwepo
wapi hadi vikafukiwa! Maana vilikuwa ni mali yake hapana shaka, kwani wale wana wengine
walipewa vizawadi tu, na Ishmael tunafahamu ya kuwa alishapewa urithi wake huko
walikokimbilia na mamaye. Na Mungu alimpatia kisima chache au chemichemu yake huko
jangwani.

Kuna vitu tunaitaga zuio kwenye upande wa urithi. Zuio hili huweza kuwa ni laana,
au aina fulani ya maneno yaliyowahi kuachiliwa ama ni aina pia ya kifungo kwa watu ambao
wapo kwenye aridhi au eneo husika ama ni swala la kifungo kinachotembea kizazi na kizazi.
Lakini pia kama mali hiyo haikuwa halali, nikimaanisha ilitokana na msaada wa miungu ya
kigeni, uwe na uhakika kuna uwezekano wa kuwepo kwa mashariti ya mganga au ya kishirikina
hapo. Mashariti hayo yanaweza kuwa na vigezo kadhaa, ambavyo mtapaswa kuvitimiza. Na
nyingine huwa na agizo au zuio la kutokurithiwa na yeyote kabisa, ama ikachagua mrithi, yaani
kubagua wengine.

Wakati Joshua anaibomoa Yeriko aliweka mashariti kwa atakayetaka kuja kuijenga upya.
Mashariti hayo yalihitaji sadaka ya mtoto wa kwanza katika misingi yake. Na malango yake ni
sadaka ya mtoto wa mwisho. Kwa hiyo, ukitoa sadaka moja ya mtoto wa kwanza utafanikiwa
kuujenga mji, au ukuta wake. Lakini usipotoa ya mtoto wa mwisho maana yake malango yake
hayawezi jengwa.

Kwa hiyo, kama malango hayajajengwa ni mji usio na ulinzi, na ni mji ambao hauwezi
kupenyeza baraka maana hauna malango au mafanikio hayawezi patikana kwa watu wa mji huo.
Maana Isaya 60:11-13 hutaumbia kuhusu malango ya kwamba yawe wazi ili watu waweze
kumuletea utajiri wakiongozwa na wafalme wao.

Swala la ukiwa pia litatawala maana ni mji ambao hakuna anyeutaka. Kwa sababu
malango yake hayajajengwa. Haya ni mambo muhimu sana ya rohoni unapaswa kuyajua. Kwa
hiyo kama ni fedha au mali zenye mashariti kadhaa ya marehemu kama ilivyokuwa kwa Yoshua,
lazima ajaye yaani mfalme Ahabu akitaka kujenga ayajue na ayatimize hayo mashariti. Nje ya
hapo hiyo mali ya marehemu itapuputika tu au itapotea tu! Sikwambii haya bure maana hata
Isaka alichimbua visima baada ya Mungu kumtokea kiagano kama Mungu wa Ibrahimu babaye.
(Na mali ya mashiriti ya upande wa pili huhitaji kujua namna ya kutembea kiagano au katika
agano la marehemu ili naye Mungu wa marehemu akutoke kiagano; ila ni kama hujaamua
kuokoka au kumkabidhi Yesu hiyo kesi).Hii ina maana kwamba swala la visima kama urithi
halikuwa la kawaida kama alivyorithi mali nyingine kirahisi.

Tuanze na Yoshua dhidi ya Ahabu kama aliyekuja kupaswa kutimiza mashariti. Yoshua;
Yoshua 6:26 Naye Yoshua akawaapisha kiapo wakati ule, akasema, Na alaaniwe mbele za
Bwana mtu yule atakayeinuka na kuujenga tena mji huu wa Yeriko; ataweka msingi wake kwa
kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake, tena atayasimamisha malango yake kwa kufiliwa na mtoto
wake mwanamume aliye mdogo.

Ahabu;1 Wafalme 16:33 Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha


Bwana, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia. 34 Katika
siku zake, Hieli Mbetheli akajenga Yeriko; akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu
mzaliwa wake wa kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake
mdogo Segubu; sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa Yoshua mwana wa Nuni.

Nathani umeona! Ndio maana kama umeokoka, na unataka kurithi mali ambayo hujui vyanzo
vyake kiuhalisia. Hunabudi kuwekeza muda wa kutosha kwenye rehema; ( ya namna
ilivyopatikana). Pili inunue hiyo mali kwa Damu ya Yesu, na katika kuinunua hakikisha
unaitumia hiyo damu kufuta mashariti yoyote yaliyowekwa kama sehemu ya kuirithi hiyo mali.
Kisha vunja maagano yote yanayoambatana na hiyo mali. Pangua kila kafara iyowahi kuyolewa
au sadaka kwa miungu mingine. Ondoa zui juu yako kuihusu, kisha tangaza wewe ndiwe
mmiliki mpya na halali wa hiyo mali. Yaombe kwa muda na usiache kuambatanisha na sadaka
maombi haya. Maana sadaka huwa na tabia ya kupambana na sadaka nyingine.

Kumbuka damu ya Yesu huwa na uwezo wa kusafisha kama 1 Yohana 5:7b


inavyotuambia, pia kama Waebrania 9, kwa hiyo kama inasafisha inaweza pia kufuta,
mashariti yaliyoachwa na Yoshua wa upande wa pili.

Ukifeli hapa au nje ya hapo, ujiandae kusota na kesi hiyo mahakamani sana huku
mali ikipuputika yenyewe. Na wengine wanakosa kabisa utayari wa kufuatilia hizi mali hadi
zinapotea kabisa. Utakuta tu hajui ni kwa nini hataki kuifuatilia, au kila akipanga anakutana na
kikwazo, atakosa hata nauli au udhuru wowote utamkwamisha tu. Akilazimisha anajikuta
ugomvi mkubwa umeibuka baina yake na ndugu zake kiasi cha kutokuwapa mwanya wa kulijadi
kwa muda huo. Uonapo dalili hizo huna budi kuliweka magotini.

Sio kiroho hata kidogo kukataa kurithi mali za unayostahi kurithi kwa kujisemea kuwa
hujui chanzo chake! Huku nako ni aina fulani ya kulogwa akili. Unaweza kujiona upo
kiriho sana na ikawa ni kweli ni kiroho lakini ni kiroho kile cha giza. Kuna giza
limefukia akili zako katika huo urifhi kwa kubana fahamu au fikra zako mahali.

Unawezaje kurithi jina la baba alafu ugomee kurithi mali zake? Hata kama una
uhakika sio halali, chukua hatua ya kuziombea na kuzihalalisha ili uweze kuzimiliki. Narudia
tena ni kulogwa akili kugoma na hata kuzembea kurithi mali za mzazi. Ukishindwa pia
kuzigombania au kuzipambania/kuzipigania kwa njia ya maombi na mhakama kwa kusema
unaachilia nako pia ni kufungwa fahamu. Isaka angeachilia visima vyake bila kuvifukuwa
angekwama tu. Na huwezi pata kisima cha tatu kama hukufukua cha kwanza na cha pili. Hili
lishike daima.

Umewahi kukutana na wapendwa waliozulumiwa viwanja au mashamba na hata nyumba


za urithi na wakaachilia? Alafu wanatumia na maandiko kabisa ya mwamba ukinyanganywa
kwanzu mpe na joho! Ukipigwa shavu hili geuza la upande wa pili! Ni vyema kukosa yote ila
ukaupata ufalme wa mbinguni!

Sijui sana ila nijualo ni kwamba mambo ya rohoni ni lazima tujifunze kufukuwa visima
vilivyofukiwa na Wafilisti, Isaka angewaza hivyo angekwama tu. Na hayo maandiko
yanatumiwa vibaya na hila ya adui kama nyoka amekaa hapo. Fahamu hata alipomtokea Yesu
alimsomea maandiko tena kwa usahihi, lakini Yesu aligundua hila yake na kumpa tafsiri sahihi
kimaandiko pia. Yakwamba hakubisha malaika huweza kuagizwa kweli ili kumuokoka, ila
inategemea na mazingira, kama itakuwa yu hatarini kuangushwa na adui sawa. Ila sio katika
mazingira ya Yesu kujiangusha, huko ni kumjaribu Mungu. Na wewe lazima uwe na maandiko
ya kukinzana na hizi hila.

Na maandiko ya Isaka kuchimbua visima ni jibu tosha kwa fikra kama hizi. Ni lazima
kuhakikisha ya kuwa adui hapewi mwanya wa kutuzuilia mibaraka yetu.

Nasikia mtu kwenye ulimwengu wa roho akisema ya kuwa lakini kuna migogoro!
Nisikilize, Damu ya YESU iingize vitani. Omba, na baada ya muda urithi utakufuata. Migogoro
mingine ni matokeo ya zuio lililokaa kwenye urithi.

Miungu mingine ilishasema atakayeokoka ni ametusaliti, kwa hiyo haruhusiwi kurithi


mali kwenye hii jamii yetu. Sasa usipojifunza kupambana kiroho na kisheria utakwama tu.
Hujawahi ona watu walionyimwa mali kisa wameokoka? Sio jambo la kawaida, ni vita
vya kimiungu.
Lakini Mungu wetu ni mkuu kuliko hiyo miungu, na swala la urithi ni kanuni ya
Kibiblia. Na dunia na mali, au na vyote viumbwavyo ni mali yake Mungu wetu; kama Zaburi ya
24 inavyosema. Kwa hiyo ukiomba lazima uliambie hilo zuio ya kwamba hujakaa kihalali,
ninaye Mungu mkuu ambaye ndiye anipaye urithi, ulipokabithiwa pale Edeni kumbuka Yesu
alishakunyanganya pale Msalabani. Akakupokonya na funguo za mamlaka. Alipofufuka alisema
amekabithiwa mamlaka au amekabithiwa vyote! Vyote maana yake ni vyote ikiwemo na vile vya
Edeni ulivyopewa na Adamu kwa kosa lile. Baada ya ukiri huo kemea. (Mathayo 28:18 Yesu
akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.)

Mambo ya rohoni na maagano unahitaji kuyafahamu sana, tutazame Isaka maana


nalikwambia hapo awali ya kuwa hakuanza kufukuwa visima mpaka alipokutana na Mungu
kiagano; Mwanzo 26:1 Ikawa njaa katika nchi hiyo, mbali na njaa ile ya kwanza iliyokuwa siku
za Ibrahimu. Isaka akamwendea Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, huko Gerari. 2 Bwana
akamtokea, akasema, Usishuke kwenda Misri, kaa katika nchi nitakayokuambia.

3 Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa
wewe na uzao wako nchi hizi zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba
yako. 4 Nitazidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, nami nitawapa uzao wako nchi hizi zote,
na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.

Mwanzo 26:6 Isaka akakaa katika Gerari....18 Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji
walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada
ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.

Hapo awali nilikwambia pia uenda zuio hilo ni laana au aina fulani ya maneno
yaliyowahi kuachilia. Huku kwetu na jirani yetu kuna aridhi moja iliyonenewa maneno kwa
kichagga ya kwamba, "nelaa mwesha." Ya kwamba atalala au ataishi hapo mtu mgeni, "wakuja."

Kwa hiyo kuna zuio la mwenyeji kuishi hapo. Yaani ndugu au mtu wa damu. Sababu ni
kwamba huyo bibi aliyekuwa anaishi hapo walimtesa na njaa, akafa njaa, katika kuelekea nakufa
aligundua kuwa urithi ule utatwaliwa tu na watu ambao walipaswa kumtunza; ndiposa akaachilia
hilo zuio. Sasa wewe unakuja kama mjukuu, au hata ndugu mwingine tu na ukapewa hiyo aridhi
iwe urithi wako, ghafula unashangaa kila unachokifanya hapo hakiendi. Wanakuja watu
wanakwambia hapa bibi yako au ndugu huyu alisema hivi na hivi na ukitazama ni kweli hakuna
kinachoenda. Utafanyaje? Na ukijaribu kuuza uwe na hakika fedha ya namna hiyo hailiki.

Mungu aliwahi kughadhabishwa na maisha ya watoto na malezi ya baba yao kuhani Eli.
Akaachiliana laana kama hii juu ya uzao wao (kama kuna laana huwa siipendi, kuiogopa ni ile ya
uzao, maana inaadhiri hata watu ambao kiuhalisia wanazaliwa hatiani au wanaingia hatiani kwa
kosa la mwingine). 1 Samweli 2:30 Kwa sababu hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema, Ni
kweli, nalisema ya kuwa nyumba yako, na nyumba ya baba yako itakwenda mbele zangu milele;
lakini sasa Bwana asema, Jambo hili na liwe mbali nami; kwa maana wao wanaoniheshimu
nitawaheshimu, na wao wanaonidharau watahesabiwa kuwa si kitu.
31 Angalia, siku zinakuja, nitakapoukata mkono wako, na mkono wa mbari ya baba yako, hata
nyumbani mwako hatakuwako mzee. 32 Nawe utalitazama teso la maskani yangu, katika utajiri
wote watakaopewa Israeli; wala nyumbani mwako hatakuwako mzee milele.

33 Tena mtu wa kwako, ambaye sitamtenga na madhabahu yangu, atakuwa mtu wa kukupofusha
macho, na kukuhuzunisha moyo; tena wazao wote wa nyumba yako watakufa wapatapo kuwa
watu wazima. 36 Kisha itakuwa, ya kwamba kila mtu atakayesalia katika nyumba yako
atakwenda kumsujudia, apate kipande kidogo cha fedha, na mkate mmoja; na kumwambia,
Tafadhali unitie katika kazi mojawapo ya ukuhani, nipate kula kipande kidogo cha mkate.

Hapo kuna paka laana ya watu kutokuwa wazee. Kuna mchungaji mmoja ambaye mama
(36), dada (20’s) na baba (56) walifariki wakiwa tu na umri wa kawaida, hawakufikilia uzee,
tena kama mama na dada ndo mapema zaidi. Anasema kabla ya baba kufa roho ya mauti
ilimuwinda yeye, na aliikemea ndotoni: ndipo baba yake akaja kufa. Alipoona hivyo likawa
ishara kwake baada ya kuokoka, (mama alifariki akiwa bado hajaokoka) na kuwa na huu
ufahamu. Aliamua kuingia kwenye maombi ya muda na kuikomesha hii hali huko kwao. Baba
alikuwa mganga kwa hiyo huwezi juwa sana kuna damu nyingi kiasi gani zilikuwa zikipiga
kelele juu yao, na wengineo walisema baba ndo alimuua mama. Nakujuza haya ili kama na
kwako kuna vitu vya namna hiyo ujifunze kuvishughulikia.

Jambo mojawapo ninalotaka ulione hapo ni hili la kuachiliwa laana kwenye eneo la
kutokurithi nafasi ya ukuhani. Mungu anasema maneno magumu ya kuwa mkono wa Eli
utakatwa, na ule wa baba yake yaani urithi na baraka za kiurithi au uweza huo utakatwa.
Ukuhani ulikuwa ni kisima cha baraka kwa uzao huu wa Eli kuhani; ambapo naye aliridhi
ikitokea kwa Haruni babu yao. Ni njia na mkondo wa baraka pia. Lakini kwa bahati mbaya
kisima hiki kinafunikwa. Sasa hapa mfunikaji ni Mungu, kwako inawezekana mfukiaji ni Shetani.

Lakini hata kama mfukiaji ni Mungu bado kuna nafasi ya matengenezo! Tazama jambo
hili lilivyokuja kutimia hata mikaa kadhaa baadae, sijui ni baada ya uzao wa ngapi ila
inawezekana ni wa tatu hata wa nne baada ya kuhani Eli, ilipita hesabu ya miaka au kipindi cha
kutoka utawala wa kuhani na mwamuzi Samweli, kisha Sauli aliyetawala miaka 40 na Daudi 40,
unaweza kupata miaka hiyo au uweza kutafuta kwa kufuatilia pia uzao huo zaidi. Kipindi cha
mwanzo cha utawala wa mfalme Sulemani mambo huja kujidhiirisha; 1 Wafalme 2:27 Hivyo
Sulemani akamtoa Abiathari asiwe kuhani wa Bwana; ili alitimize neno la Bwana, alilonena juu
ya nyumba ya Eli katika Shilo.

Kwa hiyo kuna nafasi unaweza kuondolewa na kumbe kwenye ulimwengu wa roho kuna
maneno au zuio la kilaana limesababisha. Ni muhimu ujue cha kufanya unapopitia nafasi
kama hii. Kumjua Mfilisti wako ni jambo muhimu sana.

Kijana mmoja alifukuzwa kazi, kumbe ni matokeo ya mke wake kusimama kama Mfikisti na
kinywa kibaya. Mke huyu alikuwa amemkosea mumewe vya kutosha, na mumewe kumrudisha
kwa wazazi kwa muda ili wamfundishe na kumsaidia ili ajue kuishi na mume. Usiku mmoja
akaota anamuuza mumewe kwa "bosi" au muajiri wake mumewe kwa shinlingi elufu 30 za
kitanzania. Babaye alikuwa ni mchungaji na alimuonya. Tafsiri yake ilikuwa ni roho ya usaliti
kwa mumewe katika eneo la kazi au nafasi, maana fedha hiyo iliwakilisha vipande thelathini vya
fedha alivyopewa Yuda. Sio jambo la kawaida, bali kuna roho ilimpa majukumu hayo ya usaliti,
(kwani hata Yuda hizo fedha alipewa na Wakuu wa Makuhani na baraza lao.) Haikuchukuwa
siku kadhaa mumewe alifukuzwa kazi na kupita sana kiuchumi.

Siku moja kijana huyu naye akaja akaota ndoto babu yake ambaye ni marehemu
anamkabithi huyu mwanamke pochi ya kiume yaani ya huu mume, "waleti" lakini iliyochaka
chakaa. Na aliiota baada ya muda akiwa kwenye mapambano ya kiuchumi.

Kumbe Wakuu wake wa Makuhani ni roho za kifamilia, ambazo zilimuwekea zuio la


kutokufanikiwa kiuchumi. Maana hakuwa babu kama babu, ila ni miungu ya nyumbani. Ambapo
ilitumia mlango wa mke. Yaani mke alifanyika kuwa lango la kuzimu. (Kitabu chetu cha
MALANGO KWENYE ULIMWENGU WA ROHO kitakusaidia.)

Kuna kitu kingine kimenihuzunisha hapa kwa Eli na kuniongezea pia ufahamu. “..
atakuwa mtu wa kukupofusha macho, na kukuhuzunisha moyo;..” Unajua maana yake? Kuna
familia ambazo huko kwao au jamii zao, lazima kuwe na mtoto ambaye ni teso kwa mzazi au
wazazi ama jamii. Tumezoea kuwaita “pasua kichwa.”

Ndio chanzo hata cha ugonjwa au magonjwa ya moyo ama kisukari kwa mzazi.
Amekuwa sehemu ya huzuni kwenye familia. Shule akatae yeye, kesi mtaani na polisi ni yeye,
magomvi pia ufujaji wa mali ni yeye. Kutukanana na kupiga wazazi pia ni huyu huyu.

Hapa tunajuzwa ni aina ya laana. Ukiona boma au jamii ama kaya na hata ukoo wenye
uzao wa namna hii. Tazama sasa kwa jicho la laana au kifungo fulani ama kama adhabu ya
kiungu au miungu imekaa hapo. (Adhabu za miungu sijui kama unazielewa. Mara nyingi ni
matokeo ya uzao ujao kuasi mashariti ya namna ya kuishi na mizimu au miungu ya baba zao.
Nikutie moyo kuwa ukiiasi, basi amua kuokoka. Na ukiokoka; simama au maanisha. Lakini pia
ukiyaona haya yashughulikie kwa haraka maana hupaswi kuonewa nayo kwani wewe
ulishahama kihalali kutoka kwenye miliki yao.)

Roho Mtakatifu ananijulisha ya kuwa, kuna mtazamo usio wa Kibiblia miongoni mwa
wapendwa wengi kuhusu laana,.. Ni kama vile laana haiwezi kuwa juu yao. Unapaswa
kubadilika. Utofauti ni kwamba tuliokoka tuna nafasi nzuri na bora ya kushuhulika nazo kuliko
walio nje. Ukibisha, tazama matatizo yanayozunguka familia za ndugu zako utayaona na kwako.
Ukiona haya iwe ni ishara kwako. Ingia katika mombi ya rehema na uanze kujitoa kwenye hivyo
vifungo wewe na wanao au na watu wa kwenu kumbuka hata Lazaro alivyotoka kaburini
alipaswa kufunguliwa sanda.

Alipomfufuka Yesu hakuondoa kila kitu. Mengine tunaachiwa ili tujifunze vita. Ndiposa
ulipookoka kuna mambo yaliondoka papo hapo, na kuna mengine ni hatua kwa hatua. Andiko la
ya kale kupita na tazama yamekuwa mapya; unapaswa kulielewa kwa upana wake. Epuka
kuokoka kuliko Biblia. Na kial andiko la kwenye Biblia linapaswa kushikamana na mengine. Hii
ni kanuni ya kutafsiri maandiko, kwa walioenda vyuo vya Theoojia huweza kunielewa kirahisi.
Kuna watu wamejitengenezea misimamo yao na kulazimisha iwe ya Kibiblia. Hii ndo
imewazuilia wengine kupuuzia ndoto. Wakati hata babaye mlezi wa Yesu kwenye gano Jipya
aliongozwa au alipewa mara kama tatu hivi maelekezo muhimu kumuhusu Yesu na mamye kwa
kupitia ndoto! Tunahitaji kuwa na fundisho sahihi kutoka katika msimamo wa Kibibia sio
msimamo na mtazamo wa mtu au dhehebu ama Imani na hata mrengo fulani. Tuendee pale
ulipoishia ka kuhanu Eli;

Sijui kama umefanikiwa kupata picha hapo?


Lazima uwe makini na kutazama roho unapokuwa ukipambana na jambo fulani ambalo una
uhakika kabisa umewekewa zuio ni nini huwa unakiona rohoni! Macho yako lazima yawe
makini. Mwingine yupo mjini lakini huwa anaota sana akiwa kijijini kwao au maeneo ya
nyumbani kwao. Binti mmoja akawa anaota sana akiwa chini ya mti fulani wa kwao. Kuja
kuuliza akafahamu ni eneo la madhabahu ya mila zamani. Kwa hiyo ni ishara ya kuwa kuna
kifungo cha kimaagano kimemshikilia hapo. Hata wanaota vyakula au wanakula ama kunywa,
uwe na hakika wanajulishwa ushirika wa kiagano na kifungo fulani.
Wapo ambao huota shule wilizo soma au marafiki, kitabu chetu cha NGUVU YA NDOTO
KWENYE ULIMWENGU WA ROHO kitakusaidia sana. Sio ndoto za kawaida, kuna namna
umekamatiwa hapo, kuna kifungo kimekushikilia hapo. Ukiona unamuota mtu fulani mara kwa
mara uwe na hakika kuna nira mmefungiwa pamoja, ukitaka kwenda huku anakuvuta. Tazama
sana kwa umakini kuna eneo mtakuwa mnafanana, mnapambana wote kwa pamoja kujinasua
hapo. Au malepo yanatumia nafasi yake katika uhalali walionao kukutesa. Si kila mara huwa na
maana ya kulogwa au kufungwa na huyo mtu. Mara nyingine huwa ni kicungo cha aina fulani,
kama ulisoma naye basi kilikuingia jkiwa shuleni au kiliwafunga pamoja kipindi hicho. Kama ni
ndugu huwa ni roho za mashetani eneo la familia; "family spirit" Ambazo huwa zinafanyika zuio
kubwa sana.

Kuna mfalme mmoja kipindi kile cha Yeremia aliwahi kutamkiwa maneno kama haya,
sio kwake yeye tu, bali hata manaye hataketi hapo. Na nchi yaani aridhi ikaambiwa iandike hayo
maneno. Bi lia ya kingereza imetumia neno aridhi. Yeremia 22:29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie
neno la Bwana.

30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu
hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi
katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.

Hata akiketi hapo huyo mtoto hatafanikiwa! Ni muhimu kutaka kujua ugumu au tatizo
fulani limeanzia wapi na lini? Mengine yameanza tu toka uliporithi kiwanja au nyumba fulani.
Lazima utake kujua ya kuwa kuna maneno yatakuwa yalisemwa au kusemewa ama lipo zuio la
ulimwengu wa roho katika hiyo nafasi. Nalo sio jepesi, panahitaji matengenezo makubwa, sasa
rehema ninavyokufunza humu kitabuni itakusaidia.

Jana nilikumbuka mambo muhimu sana, chanzo cha kuandika vitabu ni matokeo ya aina
fulani ya kisima cha urithi. Ni kweli toka nikiwa mdogo (hata kabla ya kumaliza chuo cha
uandishi wa habari) nilikuwa nasema mimi ni mwandishi wa vitabu, lakini kiukweli sikuwahi
kuanza kuandika.

Siku niliyoanza kuandika niliota ndoto baba yangu mzazi (kipindi hicho bado akiwa hai)
akinipa kitu kama kashata eneo la huku nyumbani kwetu Rombo, katika aridhi ambayo zamani
ilimilikiwa na wazee wetu wa karibu kabisa, japo kwa sasa bado ipo mikononi mwa ndugu wa
ukoo. Nipoamka tu upako wa kuandika ukanizukia.

Sasa maana yake ni nini? Baba yangu alikuwa ni mpenzi wa vitabu, japo sio mwandishi
ila ni msomaji mkubwa sana alikuwa. Baba yangu mdogo ambaye alifariki mwaka 1985 akiwa ni
msomi wa kwanza huku kwetu wa chuo kikuu, alikuwa mwandishi wa vitabu; waliniambia.
Lakini pia kwa upande wa bibi mzaa baba kwao wapo au yupo mwandishi. Ambapo vitabu
vyake vikitajwa hapa vinaweza kufahamika maana serekalini nimewahi somwa mashuleni.

Sasa hii inamaanisha nini kwa upande wa hiyo ndoto!


Kuna kitu cha urithi nilikabidhiwa ambacho Mungu anakitumia kama lango lake katika
huduma hii ya uandishi wa vitabu. Kama Isaka alirithi visima vya maji, wengine pia tunaridhi
visima vya uandishi wa vitabu. Mungu akitaka kukupitishia baraka lango moja wapo ambalo
hulitumia ni la urithi. Sasa adui akifanikiwa kulidhibiti ni atakuwa amefanikiwa kukuzuilia
jambo kubwa na muhimu sana hapo.
Hata hayo maandiko ya Isaka ni matokeo ya urithi. Ndio maana Mungu anajitokeza kama
Mungu wa Ibrahimu. Alifanya hivyo pia kwa Yakobo. Kwa Isaka mara baada ya kujitokeza
ndipo anapokuja kumwambia ya kuwa nitakubariki. Sababu sio kwa sababu ni Isaka bali ni kwa
sababu ni uzao wa Ibrahimu. Hii ikupe pia kuhakikisha unatembea vizuri na Mungu kwa ajili ya
familia na uzao wako. Eli alipomkorofisha: pamoja na huyo mfalme waliathiri na familia au na
uzao wao.

Sasa kwako wewe ambaye unateseka na familia ya namna hii hujui hujinashueje kutoka
katika vifungo vya kilaana au maneno ya namna hii ni muhimu kwako kujua umuhimu wa
rehema. Tubia kosa lao, tubia sababu za kuachiliwa kwa laana au kifungo hicho. Kikatae kwako
au jitoe kwenye orodha ya watu wanatamkwa kuwa chini ya hivyo kifungo. Kataa jina lako
kuwepo, kisha tangaza mujiondoa kwenye maisha au huo uruthi wako mbaya.

Ununue huo urithi au hiyo nafasi kwa damu ya Yesu. Ukitaka kusaidia na wengine basi
waombee pia hivyo. (Kitabu au vitabu vyetu vya Namna ya kutoka kwenye vigungo
vitakusaidia.)
Sasa ukitaka kuamini kuwa ni kweli jambo hili la visima lilihusisha nguvu ya kiagano,
basi nenda toka enzi za Ibrahimu na huyo mfalme wa Wafilisti. Utagundua kuwa yalikwepo
mapatano, kiapo na sadaka. Ambapo sadaka hiyo inabebwa na ishara ya kondoo saba wa wakike.
Mambo hayo manne hukamilisha agano, moja ni ishara, pili ni mapatano, tatu ni sadaka na nne
ni kiapo. Alafu mwishowe Ibrahimu tunamuona akimfanyia Mungu ibada au madhabahu. Kwa
hiyo ni dhairi kuwa ni Agano kati yake na Mungu lakini na nchi, aridhi ikiwakilishwa na mkuu
wa nchi au mkuu wa hiyo aridhi pamoja na mkuu wa majeshi.

Mwanzo 21:25 Kisha Ibrahimu akamlaumu Abimeleki kwa sababu ya kisima cha maji ambacho
watumwa wa Abimeleki wamekinyang'anya. 27 Ibrahimu akatwaa kondoo na ng'ombe akampa
Abimeleki, na hao wawili wakafanya mapatano.

28 Ibrahimu akaweka wana kondoo wa kike saba peke yao. 29 Abimeleki akamwambia
Ibrahimu, Hawa wana kondoo wa kike saba, uliowaweka peke yao, maana yake nini?

30 Akasema, Hawa wana kondoo wa kike saba utawapokea mkononi mwangu, wawe ushuhuda
ya kuwa ni mimi niliyekichimba kisima hiki. 31 Kwa hiyo akapaita mahali pale Beer-sheba, kwa
sababu waliapa huko wote wawili.

32 Basi wakafanya mapatano huko Beer-sheba. Abimeleki, na Fikoli mkuu wa jeshi lake,
wakaondoka wakarudi hata nchi ya Wafilisti. 33 Ibrahimu akapanda mkwaju Beer-sheba,
akaliitia huko jina la Bwana Mungu wa milele. (Kuliitia jina la Bwana kunawakilisha ibada, na
hakuna ibada kipindi kile bila madhabahu.) Mti wa mkwaju uliopandwa hapo uliwakilisha
madhabahu, eneo la kiibada. Kamusi moja wapo katika tafsiri moja wapo ya huo mti huo
imetumia neno Ashera. :34 Ibrahimu akakaa hali ya ugeni katika nchi ya Wafilisti siku nyingi.

2. Fukuwa Malango Watu Waliofukiwa Kama Kisima. Kuna muda adui huwa
anatutenga na watu muhimu sana ambao walipaswa kutusaidia au kutuvusha mahali au watu
ambao wanapaswa kufanyika baraka kwenye maisha yetu. Mtunga Zaburi anasema kuwa
ametengwa na mpenzi wake. Akimaanisha rafiki wake wa karibu sana. Zaburi 88:8 Wanijuao
umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka.

Hayo maandiko ni magumu sana, mosi ametengwa nao, pili wametupiwa roho ya
kumchukia, yaani hali ya kukataliwa. Tatu amefungwa wala hawezi kutoka ili yamkini
aweze kujipigania ili kuchomoka hapo.

Tazama msitari mwingine katika sura hiyo hiyo; 18 Mpenzi na rafiki umewatenga nami, Nao
wanijuao wamo gizani.

Hapa tunapata jambo la nne ya kwamba wamo gizani. Muhusika kafungwa (jambo la 3)
kwa hiyo hawezi kujipigania, alafu ambao yamkini wangemuona ili waweze kumsaidia
nao wapo gizani. Kwa maana hawawezi muona; alafu usisahau wanamchukia.
Hii ikupe kuwa makini sana unapojikuta ghafula watu wako muhimu wameamua
kukuchukia, wamejikuta wanakuchukia tu bila sababu. Umakini unahitajika sana tena mno. Watu
ambao walikuwa wakikusaidia, au ambao unafahamu fika ya kwamba walipaswa kukusaidia
alafu wanakupita kama vile hawakuoni uwe na hakika ya kuwa wapo gizani. Hawawezi kukuona.

Ni muhimu kuyajua haya maana watu wengi hawajui ni kwa nini wanatengwa au
marafiki huwa wanawasahau wanapopita katika njia au mahali pagumu. Mara nyingi huwa ni
vita vya namna hii. Na adui hukutenga nao kwa makusudi ili kukuzuilia kuvuka.

Fahamu sana kuwa hata uwe ni mtu mzuri, mwenye uwezo au ubora mkubwa kiasi gani
bado unawahitaji watu watakaokusemea vizuri. Watu watakao kuvusha mahali. Narudia tena ya
kwamba kila mtu anahitaji mtu ili kutimiza ndoto zake, sio watu kama wasaidi tu, bali watu
kama wakina Yohana Mbatatizaji. Watu ambao watajitoa ili wewe uvuke. Yesu na Uungu wake
alimuhitaji Yohana Mbatatizaji. Sasa jaribu kufikiri nini kitatokea kama Yohana wako
amekwamishwa mahali!

Paulo alimuhitaji Barnaba. Nawe pia kuna mtu unamuhitaji. Wakati nasoma maandiko
haya mwaka jana muda ama mwezi kama huu na juma kama lijalo niliamua kuingia kwenye
maombi ya siku nne, nilipoyahitimisha tu katika tarehe 24 ya mwezi wa 12 ndipo kesho yake ya
25 nilipokea majibu yangu. Nilikuwa kwenye vita kali na uongozi wangu wa sehemu, na hapo
awali nilipoteza maelewano na mchungaji wangu wa zamani.

Ghafla akanipigia na kurejesha uhusiano, nikajikuta namueleza maisha ninayopitia. Kwa


kuwa alifahamiana na Mwangalizi basi wakateta na hatimaye kuyamaliza vyema kabisa. Na
ilipita miaka mingi toka tupotezani, na hatukuachana vyem pia. Ni miaka kama 5 au 4, ghafula
nikarejesha uhusiano na hatimaye kunivusha mahali. Tazama maombi yangu; ni yakurejesha
mpenzi au rafiki ama mtu muhimu niliyetengwa naye. Maana niliposoma nikajikuta napokea
ufunuo, najisemea ooh ooh! Kumbe kuna mtu muhimu nimetengwa naye? Nikamrudisha kwenye
maombi tena bila mimi kumjua alikuwa ni nani? Nichojua tu ni kwamba hapa ninapopitia lazima
yupo mtu wa kunitoa jela, sema tu kanisabau kama Yusufu, nimetengwa naye. Sasa maombi
kama haya yanamtoa gizani, yanaondoa kila roho ya chuki aliyotupiwa. Kila roho ya kukataliwa
iliyojuu yako inaondoka.

Yusufu alipokuwa jela igundua kabisa huyu ni lango mtu, huyu ni mtu kama mlango wa
mimi kutoka gerezani. Ndio maana aliweza kumwambia haya maneno; Mwanzo 40:14 Ila
unikumbuke mimi, utakapopata mema, ukanifanyie fadhili, nakuomba, ukanitaje kwa Farao, na
kunitoa katika nyumba hii. 15 Kwa sababu hakika naliibiwa kutoka nchi ya Waebrania, wala
hapa sikutenda neno lo lote hata wanitie gerezani.

Akili kama hizi za Yusufu tunazihitaji sana! Ili zikupe kunufaika na haya malango watu.
Wapo kila mahali, na katika kila hatua ya maisha. Sema tu adui huwa ana tabia ya kutangulia
mbele na kututenga nao. Ndio maana unapochukiwa na mtu muhimu wako bila sababu huna budi
kuhitaji matengenezo. Maombi ni njia muhimu sana, tengeneza kwa njia ya maombi na utaona tu
mlango mwilini wa kutengeneza pia.

Hata kama hujui sababu, huwajui kwa majina wewe omba tu kama mimi, ya kwamba
ninarejesha au ninarejesha mlenzi ama rafiki au mtu wangu wa muhimu niliyetengwa naye.
(Ukisoma hayo maandiko kwenye Biblia mbalimbali za kingereza utagundua maneno
yaliyotumika hapo pa mpenzi au rafiki ni yenye maana kubwa sana katika mahusiano.)

Kwa Yusufu huyu mtu alifukiwa au kufunikwa na roho au hali ya kumsahau Yusufu. Ila
Bwana alihakikisha analeta uhitaji uliomfanya Yusufu kukumbukwa. Nawe ukikaza kuomba
utakuta tu unakumbukwa; Mwanzo 41:8 Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu
kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia
ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo.

9 Basi mkuu wa wanyweshaji akamwambia Farao akisema, Nayakumbuka makosa yangu leo.
12 Na huko pamoja nasi palikuwa na kijana; Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari,
tukamhadithia, naye akatufasiria ndoto zetu; akamfasiria kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake.

14 Ndipo Farao akapeleka watu, akamwita Yusufu, wakamleta upesi kutoka gerezani. Akanyoa,
akabadili nguo zake, na kuingia kwa Farao.

3. Fahamu Hatua Mbalimbali za Vita. Watu wengi hususani waombaji au wapiganaji


wa vita vya kiroho wanapoingia vitani kwa maombi waliyoyapanga kwao kumaliza maombi au
zile siku ni kipaumbele kikubwa kuliko kujirithisha kama vita vimeisha au la! Kuna wakati
unaingia kwenye maombi ya siku 7, au 21 na hata 40. Yamkini pia ni ya siku tatu na kadhalika;
alafu akishamaliza hapo anashangaa vita vikali vinaibuka.

Wengine wameamua kutokuomba tena maana kila wakiomba vita huibuka kubwa zaidi.
Kwa hiyo, anaamua kuacha kabisa kuomba ili kuepuka hivyo vita. Wengine wakiomba na
wakikaribia kumaliza hahelewi anapolala na kuota ndoto au kuona maono kuwa kuna mtu
alikuwa anapigana au kuna kitu alikuwa anapambana nacho na aliamka akiwa bado hajamaliza
mapambano. Njozi au maono hayakuisha na ushindi. Mwingine yanaisha akiwa amejeruhiwa au
amelemewa na vita.

Ukiona umelemewa hakikisha unaongeza "gia" au omba msaada kwa waombaji wengine.
Kuongeza "gia" kunakutaka kuhakikisha kama yalikuwa ni maombi ya masaa 24 basi unaingia
magumu zaidi. Kama mlikuwa wawili, ongeza waombaji wengine, usipowapata basi huna budi
kuongeza muda zaidi wa maombi na uzito wa mfungo.

Musa alipokuwa mlimani katika maombi au kuzungumza na Mungu (katika kuliandika


Agano) na kushuka na kukuta wana wa Israel wamejenga ndama na kuiabudu, hakukata tamaa.
Bali alirejea tena mlimani na kuingia tena kwenye maombi ya siku hizo au kama hizo hizo.
Kumbukumbu la Torati 9:16 Nikaangalia, na tazama, mlikuwa mmefanya dhambi juu ya Bwana,
Mungu wenu; mmefanya ndama ya ng'ombe ya kusubu; mmekengeuka upesi katika njia
aliyowaamuru Bwana.

17 Nikazishika zile mbao mbili, nikazitupa kutoka katika mikono yangu miwili, nikazivunja
mbele ya macho yenu. 18 Nikaanguka nchi mbele za Bwana siku arobaini usiku na mchana,
kama pale kwanza; sikula chakula wala kunywa maji; kwa sababu ya makosa yenu yote
mliyokosa, kwa kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, kwa kumkasirisha.

Kwa hiyo, kama kanisani mlikuwa mmeingia kwenye maombi ya siku 40 na


mkayamaliza au wakati mnakaribia kuyamaliza kukaibuka vita vikali sana; hakikisha
unaingia kwenye maombi mengine kama hayo tena. (Uwe na akili kama zile za Musa.)

Kuna wakati unaombea jambo la ndoa kwa muda wa siku tatu, na ukimaliza tu
mwenzako anachachamaa kana kwamba ndo Shetani kashuka mzima-mzima kutoka kuzimu!
Suluhu ni kurudi tena mlimani kwa siku nyingine tatu tena.

Kwa kifupi sana ni kwamba unapopambana vita hakikisha unaipigana hadi inaisha. Usifanye
vita kwa muda uliouweka tu! Uwe na nia na akili zakupigana vita hadi viishe. Sio hadi siku
40 ziishe, ni hadi upate usbindi.

Siku moja nikiwa kanisani, na muhubiri mmoja mgeni alisoma au alihubiri kutoka kwenye
jambo lile la Wafilisti kuiba sanduku la Agano la Bwana, yule mgeni akanitaka nisome akisema;
Mwalimu tusomee..wakati nasoma, alikuwa akiniwekea kituo na kusemea mstari kabla ya mimi
kuendelea... nikiwa nimesimama huku nasoma na muda ule wa kituo Roho Mtakatifu
alinifunulia jambo zuri sana na mimi kutikisa kichwa.

Ni kuhusu Dagoni yule mungu wao, kuna pigo la kwanza alipigwa la kuanguka kifudifudi na
kumsujudia Mungu aliye hai, ikiwa ni ishara kwao kukubali kusalimu amri kabla ya lile la pili la
kukatika baadhi ya viungo...makuhani wa ile dini hawakumuacha, hawakukubali kuwa
wameshindwa vita dhidi ya Mungu wa Waebrania bali walimsimamisha tena!

Roho Mtakatifu akaniambia kuwa vita dhidi ya miungu mara nyingi huwa na hatua au "face"
zaidi ya moja. Na tatizo kubwa la wapendwa huishia ile ya kwanza. Ndugu yangu ni kwamba
ukiingia siku arobaini wakati mwingine ni umepigana hatua ya kwanza, na makuhani
wamemsimamisha tena Dagoni hata kama wameshapwa isara a ni yupi n Mungu mkuu, kati ya
Mungu wa Waebrani na Dagoni. Hapa ndipo pale ambapo vita vikali huibuka na kushamiri sana.
Na kwa bahati mbaya walio wengi huvunjika moyo na hata kukata tamaa kabisa.

Ukiwa hapa, epuka kutumia midomo, nguvu au akili zako kujipigania. Tuliwahi maliza
maombi ya simu 40 kanisani zamani ningali tu kijana mdogo, na kuliibuka vita vikali
vilivyoacha majeraha hadi leo. Kanisa hadi leo imepita miaka zaidi ya kumi natumai; lakini
halijakaa sawa! Mzee wa kanisa Kiongozi alishindwa kuelewana na mchungaji. Wakatofautiana.
Baya zaidi kilichofuata ni kutupiana maneno. Na kwa vita vya maneno adui akapata pakukaa.
Laiti tungekuwa na akili hizi leo! Kitu ambacho kingefuata ni ukimya, alafu tunarudi tena
mlimani kwa siku 40, labla Mungu mwenyewe aseme kwa kweli kipande kilichosalia ni siku
21: _tungeweza kuimalizia ile vita.

Kuna mzungu mmoja ambaye alikuwa ni mwindaji hapa nchini, siku moja akampiga simba
risasi kadhaa. Simba akajifanya amekufa, "wazoefu wanasema wanyama kama hao huwa na hiyo
mbinu." Mzungu akamfuata ili kuendelea na nia yake, simba alipoona amemkaribia alimrukia na
kumrarua kifuani. Walimkimbiza mzungu wa watu Nairobi na helkopta kwa haraka lakini
alifariki. Naye simba alikufa tu punde maana alikuwa amezidiwa sana.

Lazima uwe na akili ya kujua huyu adui amemalizika! Simba alikuwa amezidiwa, ila alisalia
na nguvu ambapo angeachwa mwenyewe muda angejifia. Kwa kuwa alisogelewa kwa haraka,
aliweza kujilipizia kasasi. Mzungu angejua angemuongeza risasi nyingine moja. Inawezekana
alishazoea simba wengine huuawa kwa risasi kama kwa huyo kiidadi. Ni kweli hata wewe vita
vingine umeshinda kwa maombi ya siku 21, lakini hivi usiishi au usiingie kwa kukarili.

Tazama maandiko haya ya Dagoni; 1 Samweli 5:1 Basi Wafilisti walikuwa wamelichukua
sanduku la Mungu, wakaenda nalo kutoka Eben-ezeri hata Ashdodi. 2 Wafilisti wakalichukua
sanduku la Mungu, wakalitia katika nyumba ya Dagoni, wakaliweka karibu na Dagoni.

3 Na watu wa Ashdodi, walipoamka alfajiri siku ya pili, kumbe! Dagoni imeanguka chini
kifudifudi, mbele ya sanduku la Bwana. Wakaitwaa Dagoni, wakaisimamisha mahali pake tena.
(Unaona hapo!) Ni ni hatua. Hapa ndo panachemshaga vita sana. 4 Hata walipoamka kesho yake
asubuhi, kumbe! Dagoni ilikuwa imeanguka chini kifudifudi, mbele ya sanduku la Bwana; na
kichwa chake Dagoni na vitanga vya mikono yake vyote viwili vimekatika, vipo vimelala
kizingitini; Dagoni ikasalia kiwiliwili chake tu.

5 Kwa hiyo makuhani wa Dagoni, na mtu awaye yote aingiaye nyumbani mwa Dagoni,
hawakanyagi kizingiti cha nyumba ya Dagoni huko Ashdodi, hata leo.

Maandiko yanayofuata yanaonyesha au yanatufunza kuwa, huwezi wagusa adui zako,


wala kuwatikisa hadi pale ambapo umefanikiwa kuipiga miungu yao. Dagoni alipopigwa na
makuhani ambao huitumikia hiyo miungu kukosa kazi ambayo ilikuwa ikiwalinda watu; ndipo
Mungu alipoanza kuwagusa watu.

Na wakristo wengi wanashindwa kumiliki na kutawala kwa kufanya vita na watu, na


kuacha kuipiga miungu yao inayowanufaisha au kuwalinda. Wakikushinda sauti, wewe pambana
na wanaowapa sauti rohoni. Huwezi kuwatawala hadi umempiga Dagoni wao hadi makuhani
wao, au waganga wao kuacha au kushindwa kuendelea na huo utumishi.1 Samweli 5:6 Lakini
mkono wa Bwana ulikuwa mzito juu ya watu wa Ashdodi, akawaharibu, akawapiga kwa majipu,
huko Ashdodi na mipakani mwake. 7 Kisha hao watu wa Ashdodi, walipoona ilivyokuwa,
walisema, Hilo sanduku la Mungu wa Israeli halitakaa kwetu; kwa maana mkono wake ni mzito
juu yetu, na juu ya Dagoni, mungu wetu.
Sala ya Toba

Na Yamkini haujaokoka, nawe umeguswa na ujumbe huu na unatamani


kuokoka (kumbuka wokovu maana yake ni kumkataa Shetani na mateso
yake, dhambi na taabu zake na kumkubali Yesu na Uzima ama mbingu).
Inawezekana pia, Uliwahi Kuokoka Ukarudi Nyuma; Changamkia Hii
Nafasi.
Kama ndivyo basi nikutie moyo kufuatisha Sala hii ya Toba kwa imani,
Sema;

EWE MUNGU BABA, MIMI NI MWENYE DHAMBI,

NIMEGUNDUA MAKOSA YANGU, NISAMEHE YESU, FUTA

MAJINA YANGU KWENYE KITABU CHA HUKUMU,

NIANDIKE KWENYE KITABU CHA UZIMA WA MILELE,

Amen.

Hongera kwa Kuokoka na tafadhali tafuta kanisa la watu waliokoka

ukasali hapo, Ameni.

a
Orodha ya Vitabu Vyetu

Vya Ndoa/Familia:

1. Ndoa na Utumishi. 2.Saikolojia ya Ndoa. 3. Mwanamke Mwenye Busara, 4. Mwanaume


Mwenye Hekima 5. Mwana Mwenye Hekima, 6. Jibu la Ndoa, 7. Ishi Salama Kwenye Ndoa
Changa 8. Misingi ya Ndoa, 9. Familia Katika Kristo Yesu, 10.Watoto na Biblia, 11.Mwanangu.
12. Nafasi ya Wanamke Katika Familia, Jamii na Kanisa. 13. Karibu Kwenye Ndoa (Jiandae kwa
Ajili ya Ndoa) 14. Uchumba Salama Katika Kristo Yesu. 15. Mambo Muhimu Kiroho kwa
Mama Mjamzito. 16 .Vuka Ujana Salama. 17.Ndoa Ni Zaidi Ya Pendo

Vya Uongozi:

18. Hekima ya Uongozi Kihuduma, 19. Nafasi Ya Ulimwengu Wa Roho Katika Uongozi. (Kiti
Cha Enzi.) 20. Siasa, na Uongozi Uliotukuka, 21. Wito wa Kitumishi. 22. Ujuwe Wito na
Huduma ya Mwinjilisti. 23. Ujuwe Wito na Huduma ya Mchungaji. 24. Ujuwe Wito na Huduma
ya Mtume. 25. Ujuwe Wito na Huduma ya Mwalimu. 26. Ujuwe Wito na Huduma ya Nabii. 27.
Ijuwe Huduma ya Uimbaji. 28. Usizike Ndoto Zako 29. Utumishi na Mtumishi, 30.Uwe Hodari
Shujaa na Mwenye Moyo Mkuu,

Utoaji:

31. Sadaka kama Mbegu, 32. Sadaka Iliyotukuka Mbele za Mungu.

Faraja:

33. Usifie Jangwani, 34. Neno la Faraja, 35. Mtu wa Nne. 36. Ipo Nguvu kwa Mwenye Tumaini.
37. Jipe Moyo. 38.Usiogope, 39.Katikati ya Shimo Mtafute Mungu, 40. Usikate Tamaa. 41.
JANGWANI MAJI YAPO. 42. Bwana Yu Pamoja Nawe, 43 . Katikati ya Shimo Mtafute Mungu,
44. Nguvu ya Kuomba Bila Kukoma. 45. Mungu Ni Kimbilio na Msaada ! 46. Mungu
Amekusamehe na Kusahau, 47. Mungu Anakupenda, 48. Nguvu ya Kuomba Bila Kukoma, 49.
Mwaka wa Urejesho. 50. Majaribu ni Mtaji 51. Imani Ya Kusubiria Na Kupokelea Majibu 52.
Namna ya Kuishi wakati wa Majaribu au Mapito.

53. Cha Kufanya Unapokuwa Njia Panda 54. Muone Mungu Nyuma ya Pito au Jaribu Lako. 55.
Vumilia Wamjue Mungu Wako, 55. YESU NI RAFIKI WA KWELI WAKATI WA TAABU

57. Hata Jela Yesu Yupo 58. CHAKUFANYA UNAPOLEMEWA NA MZIGO AMBAPO
MUNGU BADO ANATAKA UENDELEE KUUBEBA. 59. Kesho Yako Ni Bora Kuliko Leo
Yako. 60. Siku Ya Tatu. 61. Nina Siri Kwa Waliao. 62. Kisima cha Tatu

b
Mfumo wa Fahamu:

63. Saikolojia ya Mtu wa Ndani. 64. Moyo Wa Fahamu, 65. Nguvu ya Fikra Katika Kukufanya
Uishi na Utakavyo Ishi, 66. Nafasi ya Akili Katika Kukunufaish Aua Kukufanikisha Kimaisha,
67. Nafasi ya Hekima Katika Kukufanikisha Kimaisha. 68. Thamani ya Muda wa Uanafunzi au
Elimu kwa Mwanafunzi. 69. Maana Yakumpenda Mungu kwa Akili Zako Zote.

Ukuaji:

70. Namna Ya Kuomba, 71. Nafasi ya Imani Katika Kukufanikisha Maishani . 72. Kuwa Kiroho.
73. Maana ya Mbegu Iliyodondoka Kando ya Njia, 74. Ukulie Wokovu, 75. Muongozo Maalumu
wa Kiroho kwa Waalimu wa Waongofu Wapya, 76. Kwa Nini Unapaswa Kuokoka. 77. Kwa
Nini Kusamehe Ni Muhimu 78. Nguvu Ya Neno La Mungu Kwenye Maisha Ya Mwanadamu.
79. Sauti ya Mungu

Uungu/Utumishi:

80. Moyo Safi, 81.Tunu za Tunda la Roho 82. Utumishi Wenye Matunda Mbele za Mungu,
83. Thamani ya Muda Katika Kufanikisha Ndoto Zako. 84. Sababu Za Damu ya Yesu Kuwa na
Nguvu Iliyo Nayo, 85. Mjuwe Yesu Kristo. 86. Kweli na Neema Kama Kristo. 87. Nafasi Ya
Roho Mtakatifu Katika Kukufanikisha Kimaisha Au Kihuduma ( Siri Ya Upako). 88. Hila za
Shetani. 89. Thamani ya Kukaa Kwenye Mapenzi ya Mungu. 90. Zijuwe Ajenda Muhimu za
Maombi kwa Mtumishi na Utumishi. 91. Ijuwe Thamani na Mamlaka Uliyo Nayo kwa Mungu,
(Jione kama Mungu Anavyokuona.) 92 . Nafasi ya Viungo vya Mwili wa Mwanadamu katika
Ulimwengu wa Roho. 93. Maana ya Kumuabudu Mungu Katika Roho na Kweli. 94. Mtumikie
Mungu. 95.Nafasi Ya Roho Mtakatifu Katika Kufanikisha Ndoto au Maono Yako. 96. Zijue na
Uzishinde Roho za Maajenti wa Kuzimu Makanisa 97. Karama Na Neema Za Roho Mtakatifu
98. Wasifu Wa Yesu Kristo. 99. Fikra Sahihi Katika Shamba la Bwana.

Uchumi/Mafanikio:

100. Tajirika Kibiblia. 101. Utumishi na Mali au Fedha. 102. Nafasi ya Fedha Katika
Kukufanikisha au Kukuangamiza Kiroho na Kimaisha ( Faida na Hatari ya Fedha). 103. Timiza
Maono Kibiblia. 104. BARAKA 105. Msaada Wa Kimaarifa Kwa Anayemuona Mungu
Amechelewa Kumbariki 106. Kwa Nini Mungu Anataka Umkabidhi Njia Zako

Vifungo/Ukombozi:

107. Msaada kwa Waliokosa Mpenyo Kihuduma na Kimaisha, 108.Namna ya Kutoka Kwenye
Vifungo (Kuvunja Nira), 109. Namna ya Kutoka Katika Kifungo au Hali ya Kukataliwa,
110.Teka, Miliki na Utawale, 111. Zijuwe na Uzishinde Roho za Kaburi na Mauti. 112.Ondoa
Zuio. 113. Ijuwe Na Uishinde Hasira, 114. Nguvu ya Ndoto Kwenye Ulimwengu wa Roho.

c
115. Malango kwenye Ulimwengu wa Roho. 116. Nguvu ya Agano Kiroho,

117. Uponyaji wa Mtu wa Ndani. 118. Nguvu ya Ukiri wa Kinywa. 119. Zijue na Uzishinde
Roho za Mapepo Mahaba. 120. Nguvu ya Kinywa au Maneno, 121. Mambo Muhimu ya
Kufanya au Kuzingatia Kunapokuwa na Adhabu ya Kiungu Inyoijumuisha Eneo Ulilopo au
Jamii.

Matendo ya Miujiza:

122. Majira ya Kulisimamisha Jua.

Vinginevyo:

123. Uzuri wa Mbinguni, 124. Ole Wafu Wafao Nje ya Bwana. 125.Furuksa, 126. Jiandae na
Uishi Vyema katika Msimu Wako Mpya wa Kiroho, 127.Wanatheolojia Wanapokesea, 128.
Mjuwe Mwalimu Oscar Samba.

E-Book:

129. Watu AMBAO MUNGU ANAWATAFUTA

d
Mawasiliano

Tutembele ama Wasiliana Nasi

http://www.ukombozigospel.blogspot.com

Tumeunda Channel ya WhatApp, Tufolo;


https://whatsapp.com/channel/0029Va827LBJENy9u6Enke1h

Kundi letu la WhatsApp https://chat.whatsapp.com/E0eD0xegh1eIGMjRykPyRD

Telegram https://t.me/+fft3GHXC9xIzYjhk

Subscribe YouTube yetu: https://www.youtube.com/@ukombozigospeltv

Kwa Maombi +255759859287, Email: ukombozigospel@gmail.com

Usiache Kutembelea na Ku-Like Page Yetu Ya Mafundisho ya Neno la Mungu Facebook:


https://www.facebook.com/MafundishoyanenolaMungunamwalimuoscarsamba?mibextid=ZbW
KwL

Tuandikie pia Maoni Yako; mwalimuoscarvitabu@gmail.com


TAFADHALI Kitabu hiki kikutie moyo;
Siwezi kueleza kila kitu humu; maana
kuna tukio lilinikuta punde tu: katika pito
ambalo nimelipitia takribani mwaka wa
kumi sasa. Nami nalisema nimepata
pumziko, lakini adui akaamua
kunivurugia.

Wakati haya yanatokea, kabla ya


kulitafakari au kulifikiria ndipo moyoni
mwangu kikanijia hiki kitabu! Kwa hiyo;
kama vile ujumbe huu ulivyonivusha.
Mwl. Oscar Samba Ninatamani nawe iwe hivivyo kwako.
(Toleo letu la pili litabeba huo usuhuda.)

…Kuna mambo kadhaa na muhimu unayohitaji kufahamu kwanza kuhusu kisima


cha tatu. Ni kwamba ni kisima cha ushindi, katika hili hakuna anayeweza kukupokonya
au kukunyanganya tena. Maana kisima cha kwanza walikigombania, hakufa moyo
akafukuwa cha pili nacho wakakipigania, napo hakukata tamaa bali aliendelea kufukua na
cha tatu ambacho hawakukiweza tena.

Mwanzo 26:22 Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho


hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa
Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi…

Usife Moyo maana #Kesho_Yajo_Ni_Bora_Kuliko_Leo_Yako. Hakika.

Jesus Loves You

You might also like