Professional Documents
Culture Documents
3. Fani inayotendwa: Ni ile sanaa yenyewe, kwa mfano hadithi, wimbo, methali,
kitendawili au utenzi ambao unawasilishwa na fanani.
Kwa kawaida, fasihi simulizi hutungwa kichwani kabla ama wakati ule ule wa
kutambwa.
Tungo fupi fupi, kwa mfano nyimbo na baadhi ya majigambo, huweza kutungwa
kabla ya kuhifadhiwa kichwani hadi wakati wa uwasilishaji. Hata hivyo, fanani
(msanii) huwa na uhuru wa kubadilisha matini (maneno) ya tungo hizo wakati
wowote ili kukidhi mahitaji ya muktadha wa utendaji. Kwa upande wa tungo
ndefu za kimasimulizi, kwa mfano ngano na tendi, kwa kawaida kiini cha hadithi
hubuniwa kabla ya uwasilishaji, napengine hupokewa na fanani kutoka kwa wasanii
waliomtangulia,lakini matini na mbinu za kisanii hutungwa papo kwa papo wakati wa
uwasilishaji. Hivyo tungo hizo hazikaririwi kama baadhi ya watu wanavyofikiri.
i). Mazungumzo: Baadhi ya tanzu zilizomo katika kundi hili ni; Hotuba,
Malumbanoyawatani, soga, mawaidha.
ii). Masimulizi: Tanzu mbalimbali za hadithi zinaingia hapa, kwa mfano ngano,
hekaya, hurafa,. Kadhalika simulio za kihistoria na kiasili kamavile visakale, mapisi,
tarihi, kumbukumbu na visasili.
iii). Maigizo: Hapa zinaingia tanzu mbali mbali kutegemea shabaha na miktadha
Fasihi simulizi na fasihi andishi zina mambo fulani yanayofanana. Baadhi ni haya
yafuatayo:
Uhusiano
Tofauti: Tofauti za aina hizi mbili za fasihi zimeorodheshwa katika jedwali ifuatayo:
Kwa kawaida hutungwa papo kwa papo Hutungwa kwa utulivu kwa kipindi kirefu
wakati wa utendaji. kabla ya kuwasilishwa kwa hadhira.
ii.Uwasilishaji
iv.Hadhira
v.Umri:
vi.Umilikaji:
vii.Lugha
Hutumia lugha ya hadhira inayohusika. Hutumia lugha anayoimudu zaidi mtunzi au ile
ya wasomaji waliokusudiwa.
viii.Kuhifadhika
x.Marekebisho/Masahihisho
xi.Wahusika:
Hitimisho
Aina zote hizi mbili za fasihi zina dhima kubwa kwa umma, jamii ikitumiwa
inavyopasika. Kauli hiiya mwisho ni muhimu sana kwa kuzingatia ukweli kwamba
sio kila kazi ya fasihi inaweza kuletamchangochanya kwaumma.
Ziko kazi zafasihi zinazoweza kuleta athari hasa kwa jamii. Kwa msingi huo, inafaa
uchambuzi wandaniufanyweilikubaininiainaganiyafasihi huleta mchango mzuri
kwa umma na zipi ni chanzo cha vurugu na matatizo. Umma wenyewe ukipevuka
katika masuala mbalimbali ya kifasihi unayo nafasi kubwa ya kujiamulia nini
kinafaa, na nini hakifai.
Wanafasihi hawa wanaonesha kuwa kila kimoja cha kigezo cha fani na
maudhui kimo ndani yachenziwe, kushirikiana na kuathiriana katika ama kijenga
vizuri au kubomoa kazi ya sanaa.
Kama kazi ya fasihi itakuwa na fani duni, lakini maudhui yake ni mazuri basi
hata maudhuiyaliyokusudiwahayatatoaujumbeunaokusudiwaipasavyo.Mfano mzuri
ni riwaya ya kikasuku zilizoandikwa baada ya Azimio la Arusha zinazojadili
dhamira ya ujenzi wa jamii mpya kama vileShida, Mtu ni Utu, Ufunguo Wenye
Hazina, Njozi za Usiku, Ndoto za Ndaria n.k. zilisisitiza zaidi maudhui na
kuupuzia kipengele cha fani.
Vile vile, kama maudhui ni duni na fani ni bora, pia jamii itapata hasara ya
kufikiwa na maudhui yasiyo na maana. Mfano mzuri ni riwaya pendwa zote
zimeweka msisitizo kwenye fani na kusahau kipengele cha maudhui. Katika riwaya
pendwa kama vile riwaya za upelelezi, mapenzi na uhalifu,zina wahusika ambao
hawaaminiki kwani wanapewa sifa ambazo si rahisi kuziona kwa binadamu
wakawaida.(Toa mifano ya riwaya hizo).
Pili, mtindo ambao ni upangaji wa fani na maudhui katika kazi ya fasihi andishi
kwa njia ambayohatimaye huonesha nafsi au labda upekee wa mtungaji wa kazi
hiyo. Katika riwaya, mtindo unawezakuwa na masimulizi, monolojia au dayolojia
na katika tamthilia mtindo wake ni dayolojia (majibizano). Katika ushairi
mtindo unaweza kuwa wa kimapokeo au wa kisasa.
Kipengele cha tatu ni wahusika ambao hutumiwa na msanii kufikisha ujumbe kwa jamii yake.
Kipengele kingine ni jarada: Kazi za fasihi huwa na michoro au picha na hata rangi
kwenye
majaradayake.Inawezekanamajaradahayoyakawanauhusianonadhamiraaumaudh
uiyakazizinazohusika.Picha hizi huweza kuwa kielekezi muhimu cha fani
kwenye uchambuzi wa kazi yakifasihi. Mfano picha za majarada ya Nyota ya
Rehema ya M.S.Mohamed,Kufa KuzikanaK.Walibora,Babu alipofufuka
M.S.Mohamed na Bina-AdamuK.W.Wamitila na nyingi nyinginezo. Hata hivyo
ni muhimu kutambua kuwa sio kazi zote za kifasihi ambazo zinaonesha uwiano
kati ya majarada yake na yaliyomo.