Professional Documents
Culture Documents
UNIÃO AFRICANA
Addis Ababa, Ethiopia P. O. Box 3243 Telephone: +251 115 517 700 Fax: +251 115 517 844
Website: www.au.int
BARAZA KUU
Mkutano wa Kawaida wa Arobaini na Nne
15 Januari - 15 Februari 2024
Addis Ababa, ETHIOPIA
EX.CL/1476(XLIV)
Matini chanzi: Kingereza
KAULIMBIU:
Mwelimishe Mwafrika Amudu Karne ya 21: Kujenga mifumo thabiti ya
elimu, kuongeza upatikanaji wa ujifunzaji jumuishi, endelevu, bora, na
unaoendana na mazingira ya Afrika.
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 1
1
Repoti ya Taasisi ya Takwimu ya UNESCO (UIS) na Ripoti ya Ufuatiliaji wa Elimu Duniani (GEM) kuhusu
“Kufikia Malengo: Je, Nchi Zinajishughulisha Kufanikisha SDG4?”
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 2
13. Ni kwa mantiki hiyo kwamba pendekezo hili la kuchagua Elimu kuwa kaulimbiu ya
Mwaka 2024 liliwasilishwa kwa kujadiliwa na kupitishwa na Mkutano mkuu kwenye
mkutano wake wa 36 wa kawaida wa Februari 2023.
Mapitio ya hivi karibuni ya CESA (16-25) na Mpango Kazi wa Elimu 2030, ripoti ya kibara
kati ya Umoja wa Afrika na UNESCO ya CESA na SDG42 na ripoti ya pamoja kati ya
Umoja wa Afrika na UNICEF juu ya Mageuzi ya Elimu Afrika, yanaonesha ukweli kuwa
kwa miaka kumi iliyopita, Serikali za Kiafrika zimefanya programu nyingi na juhudi kwa
ngazi ya kisera kuhakikisha kuwa hakuna mtoto anabaki nyuma katika kupata elimu.
Kumekuwa na juhudi kubwa katika bara kuhakikisha, upatikanaji, uhitimishaji na elimu
msingi bora kwa wote.
Kwa ujumla, kiwango cha watoto wasiodahiliwa shule kilipungua mpaka kufikia mwaka
2010. Kiwango cha kuhitimu kiliongezeka kwa ngazi ya msingi na ngazi ya chini ya elimu
ya sekondari, pamoja na upatikanaji na ushiriki katika TVET. Vilevile maendeleo
yalionekana kwenye upatikanaji wa elimu ya awali na elimu ya watu wazima na elimu
endelevu. Kwa upande wa Chakula Shuleni, nchi za kipato cha chini zimeongeza
maradufu matumizi ya bajeti zao za kitaifa kwenye HGSF kutoka asilimia 17 mpaka
asilimia 33 kati ya mwaka 2013 na 2020. Katika nchi zenye kipato cha kati cha chini,
bajeti za kitaifa kwa sasa zimefikia asilimia 88 zaidi ya ufadhili wa fedha kwenye chakula
shuleni, kutoka asilimia mia 55 mwaka 2013.
Walakini, mbali na juhudi na maendeleo yaliyofikiwa, viashiria vikuu vitatu vinagonga
kengele ya tahadhari:
− Ingawa kiwango cha Wasiodahiliwa, yaani “idadi ya watoto na vijana wadogo
walio katika umri rasmi kwa ngazi husika ya elimu ambao hawajadahiliwa katika
ngazi ya awali, msingi, sekondari au ngazi za juu za elimu” inaendelea kushuka
mfululizo, hususani kwa ngazi ya msingi, idadi kamili imefikia kiwango cha hatari
cha dunia kinachokadiriwa kuwa milioni 98 katika Afrika3 (tazama kielelezo cha 1
hapo chini).
− Kiwango cha umasikini wa ujifunzaji, yaani “idadi ya watoto ambao hawawezi
kusoma kifungu rahisi cha maneno na kuelewa katika umri wa miaka 10 ilikuwa
ni kubwa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kabla ya janga la UVIKO-19,
kikiwa asilimia 86. Kiwango hiki kilikadiriwa kuwa kibaya baada ya janga,
kikikadiriwa kwa sasa kuwa asilimia 90. Hii humaanisha kuwa watoto tisa kati
watoto kumi hawaaezi kusoma kifungu rahisi cha maneno na kuelewa katika
umri wa miaka 10.4 (tazama kielelezo cha 2 hapo chini)
2
Elimu Afrika- Kuleta usawa kwenye kiini cha sera: https://unesdoc.unesco.org/ark:/48223/pf0000384479
3
UIS 2022 : https://unesdoc.unesco.org/ark:/48223/pf0000382577
4
Benki ya Dunia: The State of Global Learning Poverty: 2022 Update
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 4
− Afrika itahitaji nyongeza ya walimu milioni 175 ili kufanikisha elimu ya msingi na
sekondari kwa wote ifikaapo mwaka 2030.
Kwakutazama kwa ukaribu kwenye kila lengo mahususi kwenye CESA 16-25 au kwenye
SDG4, mtu anaweza kuona ulazima wa kufanya mageuzi na kuhuisha mfumo mzima wa
elimu katika bara, wakati huo akiweka umakini mkubwa kwenye makundi yaliosahaulika
wakiwemo wasichana, watoto maeneo ya vijijini, wale wanaoishi na ulemavu, na wale
wanaohamahama, wakiwemo wale walio kwenye nchi zenye hali na mazingira tete.
Kielelezo cha 1
5
UIS 2016: http://uis.unesco.org/en/files/fs39-world-needs-almost-69-million-new-teachers-reach-2030-education-
goals-2016-en-pdf
6
Tamko juu ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi iliyokubaliwa na STC-EST 4 ikifanyika Septemba 2022
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 5
Upper secondary
Total number: 98 million
Total: 98
Lower secondary
Primary
Kielelezo cha 2
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 6
Kwa ufupi,
Mbali na maendeleo makubwa yaliyofikiwa katika Afrika kwa miongo miwili iliyopita kwa
maana ya upatikanaji, uhitimishaji na ubora wa elimu msingi, tofauti zinaendelea kuwepo
kati ya nchi. Mafanikio katika kujifunza bado ni ya chini maeneo mengi ya Afrika.
Wasichana, watoto wanaotoka kwenye historia ya umasikini mkubwa, watoto wenye
ulemavu, na watoto wanaohama kama vile wanaohamishwa kwa nguvu, wanapata
changamoto ya kuipata haki yao ya elimu. Vilevile vikwazo bado vipo kwenye
kumwendeleza mwalimu katika Afrika pamoja na upungufu wa mara kwa mara wa walimu
ikitokea pamoja ukosefu wa fursa za kujiendeleza kitaalamu na hadhi na mazingira duni
ya kufanyia kazi. Dharura nyingi na za muda mrefu zimeathiri kwa kiasi kikubwa utoaji wa
elimu, ikiwemo ongezeko la mashambulizi ya shule. Kuna ulazima wa kuimarisha elimu
ya amani na kutengeneza utamaduni wa amani na uvumilivu katika ngazi zote za elimu-
inayofuata mfumo rasmi, isiyofuata mfumo na isiyo rasmi.
Changamoto hizi za kimfumo zinaanzia kwenye elimu ya awali ya utotoni, na kuendelea
elimu ya msingi na sekondari, elimu ya ujuzi na ufundi, na mafunzo kwenye ngazi ya vyuo
vya kati na elimu ya juu.
Janga la UVIKO-19 lilichochea vikwazo vya utekelezaji wa mbinu zilizopo za elimu kwa
ngazi zote, likizidisha kutokuwa na usawa katika elimu na moja kwa moja kutishia
kurudisha nyuma mendeleo yaliyopatikana kwa miongo kadhaa, ingawaje ni kidogo,
katika Afrika.
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 7
Katika muktadha huu, lisipofanyika jambo katika kuleta mageuzi na kuhuisha elimu katika
Afrika, mafanikio ya Mkakati wa Kibara wa Elimu kwa Afrika (CESA7 2016-2025), SDG
2030 na Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika hayatafikiwa. Pasipokuwa na suluhisho la ziada
la haraka, lilioratibiwa vizuri, shabaha za kupunguza umasikini wa ujifunzaji katika Afrika
hazitafikiwa. Matokeo yake kwa watoto na na jamii yatakuwa makubwa, na athari hasi za
muda mrefu kwenye matokeo ya maisha ya mtoto, ikiwemo kujifunza kwao, afya (kimwili
na kiakili), lishe na maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Dhana ya biashara kama siku zote
kwa ufupi haina mashiko.
Maendeleo katika Elimu yana athari inayofika mbali katika nyanja nyingine zote za
maendeleo ya raslimali watu. Idadi kubwa ya vijana wadogo katika Afrika ni chanzo
kikubwa cha ukuaji na maendeleo ya kiuchumi, endapo watapewa elimu bora na ujuzi
kwa fursa za ajira za karne ya 21.Hivyo kuwekeza kwenye elimu, ni uwekezaji mzuri
wenye tija katika kupambana na umasikini, kupunguza ukosefu wa usawa wa kijinsia,
kuwawezesha watu kujikimu kimaisha na kusitawi na kuendelea kusaidia kuboresha
maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Vilevile elimu inahusishwa na jamii zenye amani,
ushiriki mkubwa wa kiraia, na demokrasia imara.
Mwaka 2024 kutolewa kwaajili ya Elimu Afrika itakuwa ni fursa ya kipekee kwa Umoja wa
Afrika kuwaamsha Nchi Wanachama kuelekea kufanikisha shabaha za CESA na SDG4.
Muhimu, hii itakuja kama namna ya kufuatilia Matamko ya STC-EST4, AU-HLSE, Wito
wa Haraka wa Kuchukua Hatua wa Kamati ya Utendaji ya Ngazi ya Juu8 ya SDG4 na
Kauli ya Dira ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu ya Kuleta Mageuzi ya Elimu9.
Itahusisha Kamisheni ya Umoja wa Afrika kuwaweka pamoja Serikali na washirika wa
Maendeleo kutafakati mbinu za elimu na maendeleo ya ujuzi yanayohitajika kwa Afrika
tunayoitaka kwa karne ya 21.
7
CESA inakusudia “Kuunda upya mifumo ya elimu na mafunzo Afrika kufikia maaarifa, uwezo, ujuzi, uvumbuzi na ubunifu
vinavyohitajika kutunza mila zetu za msingi za Kiafrika na kukuza maendeleo endelevu katika ngazi za kitaifa, kanda ndogo na
kibara”
8
Kamati ya Utendaji ya Ngazi ya Juu ni chombo cha juu cha uratibu na ufuatiliaji wa dunia wa SDG 4
9
Kauli ya Dira ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ilijawa na michakato ya kina na jumuishi ya maandalizi
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 8
Mageuzi ya Elimu katika Afrika pamoja na Ilani ya Vijana juu ya Mageuzi ya Elimu katika
Afrika ambayo ilitokana na mashauriano ya vijana mwaka 2023 ambayo yaliwasilishwa
HLSE mjini New York.
4. Kaulimbiu Iliyopendekezwa
Kuwa na Elimu kama kaulimbiu ya mwaka 2024 itaongeza kasi kwenye msukumo
uliotokana na Mkutano wa Mageuzi ya Elimu (TES) na, kuendelea kufanya kazi na Nchi
Wanachama na washirika, kuangazia katika bara kwenye kurudi katika hali ya kawaida
baada ya UVIKO-19 na kujenga mifumo thabiti ili kuongeza upatikanaji wa Elimu jumuishi,
bora na inayoendana na mazingira katika Afrika. Hii itafanyika kwa njia hatua halisi na
zenye matokeo zinazochukuliwa na Wakuu wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Afrika
kuelekea kwenye mageuzi ya elimu Afrika.
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 9
Shughuli za kitaifa, kanda, na bara zitatekelezwa mwaka mzima katika kumbukizi ya kaulimbiu ya Umoja wa Afrika ya mwaka 2024.
Matukio haya ya kumbukizi itakuwa kama fursa ya kuthibitisha juhudi ya kisiasa kwa Serikali za Afrika kwenye Elimu. Miongoni mwa
mambo hayo ni pamoja na:
Kuwezesha/kujenga
uwezo wa walimu Historia Kuu ya Afrika (GHA) Programu za Kimkakati
kufundisha Historia ya zimeanzishwa na kutekelezwa UNESCO (ED, IBE, IICBA, PAX), Umoja wa Afrika,
Afrika, na kusaidia
Kamisheni za Kitaifa za UNESCO, ATUPA,
3 kuujumuisha mkataba
Mkakati wa Umoja wa Afrika wa ujumuishaji na matumizi ya ANCEFA, PAPS, ACERWC, AU ECOSOCC, and
wa Umoja wa Afrika wa
Mkataba wa Afrika wa Demokrasia, chaguzi na uongozi kwenye Save the Children
demokrasia, chaguzi na
uongozi kwenye mtaala mtaala wa shule umetekelezwa.
wa shule.
Suluhisho la elimu kwenye maeneo ya dharura na yaliyo tete ADEA, AU ESTI/ AfECN and National Advocacy
Utekelezaji wa uvumbuzi linapatikana na kuimarishwa, kuwezesha usawa na upatikanaji partners, AfECN/ WHO/UNICEF/EVAC/PLH, IED/
uliojikita kwenye wake. EU+ITU, UNICEF kwa kushirikiana na Airtel, EU,
5 ushahidi, suluhisho la Microsoft, Google, AUDA-NEPAD, SIFA FC & TC,
kidijitali yakinifu na Matokeo ya ujifunzaji yanaendelezwa na kujikita kwenye Save the Children, UNESCO-IICBA, UNESCO,
endelevu unaongezeka. ushahidi wa suluhisho la kidijitali la kiuvumbuzi na endelevu AfDB, Microsoft Philanthropies, AOSTI, ATUPA
kiuvumbuzi na endelevu AfroChampions Initiative, AfCFTA Secretariat,
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 11
Uletaji pamoja wa raslimali umefanyika kwa kupitia ushirikishwaji ANCEFA, UNICEF, AfECN, UNESCO, IF, AfDB,
Ongezeko la ufadhili
wa wafadhili na uhamasishaji, ikiwemo hafla za meza duara na UNECA, AU and GPE (inviting heads of UN
endelevu wa kifedha na
10 hafla za Hadhi ya Juu katika kufadhili kifedha mageuzi ya elimu Agencies, donor missions, regional orgs/banks),
uwekezaji wa kimkakati
katika Afrika na katika kuimarisha uongozi wa kibara kwenye WFP, UNAIDS, AUC-CIEFFA, Save the Children,
kwenye Elimu.
elimu. ATUPA, UNESCO-IICBA, ADEA and GEM Report,
EX.CL/1476(XLIV)
Ukurasa wa 14
Uzalishaji wa Mazao
Mkutano wa ya Maarifa na
Kiufundi na Machapisho
Kongamano
Inapendelewa
(Programu za ➢ Pamoja
Mazungumzo ya ana Kubadilishana) Kibara,kanda au
kwa ana ya Sera kwa nchi kadha
(Kati ya Nchi/Mabara)
Ngazi ya Juu (Ngazi ya kadhaa.
Rais na Mawaziri) Uratibu na ➢ Miradi ya
Ufuatiliaji majaribio yenye
tija kwa kwa
matokeo
makubwa,
yanayojirudia, na
kwa kwa ukubwa
Kichwa/Jina la tukio MUHUSIKA JAN FEB MAR APR MAY JUN JUL AUG SEP OCT NOV DEC