Professional Documents
Culture Documents
ORGANISATION,
IMEANDALIWA NA:
WAZIRI - FRED A. BUZIKA
CALL : 0623025002.
NAIBU WAZIRI - FAUZIA SULEIMAN
CALL : 0685822989.
SALAMU, NA NENO LA UFUNGUZI.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Naibu spika, Mheshimiwa katibu wa bunge,
Mheshimiwa Waziri Mkuu, Baraza la Mawaziri, Waheshimiwa Wabunge, Habari za
Wakati huu.
Awali ya yote Natanguliza shukrani zangu kwa Mola wetu mlezi aliyetuwezesha sisi
kukutana hapa siku ya leo katika bunge la pili la ISRC. Napenda kutumia nafasi hii
kumshukuru Mheshimiwa Rais wa serikali ya wanafunzi IFM, Mh. Al-Haidary
Khamis Ngomero kwa Imani aliyonayo juu yangu na kuniteua kuwa katika baraza
lake. Vilevile ninamshukuru Mh. Makamu wa Rais, Mh. Philemoni Mwakanyamale
na Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mh.Shwaibu kwa iman zao na kunipokea katika
baraza hili wanaloliongoza. Aidha ninawashukuru kwa dhati kabisa viongozi
wenzangu katika baraza la mawaziri kwa ushirikiano wao wakipekee katika
majukumu yetu ya kila siku.
MUHTASARI.
Mheshimiwa Spika, Ripoti hii ninayokwenda kuisoma ni ripoti ya utendaji kazi wa
wizara ya kampasi na malazi katika muhula wa kwanza wa masomo wa mwaka
2021/2022. Ripoti hii imegawanyika katika sehemu tano, sehemu ya kwanza ni
utangulizi, shemu ya pili malengo wizara, sehemu ya tatu ni mafanikio ya wizara,
sehemu ya nne ni changamoto zinazoikumba wizara na sehemu ya tano mwisho wa
ripoti yaani hitimisho.
SEHEMU YA KWANZA
UTANGULIZI.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya kampsi na malazi yaani “Ministry of campus and
accomodation” ni moja ya wizara tisa zilizounda serikali ya wanafunzi IFM mwaka
2021/2022. Wizara hii imetengwa na wizara ya Afya kwa kulinganisha na mwaka
jana ambapo ilikuwa ni wizara moja.
Wizara inaundwa na viongozi wawili ambao ni waziri na naibu waziri, Kwa sasa
waziri mwenye dhamana ni Fred Abely Buzika, na naibu waziri ni Fauzia suleimani
.
SEHEMU YA PILI
MALENGO YA WIZARA.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya kampsi na malazi katika serikali ya wanafunzi IFM
mwaka 2021/2022 ina malengo kadhaa yakuyafikia kabla muda wake kuisha.
Malengo haya ni muhimu kwetu ili kuweza kuboresha mazingira na afya za
wanafunzi wa IFM pamoja na jamii nzima ya IFM kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika, malengo katika wizara hii ni kama yalivyoainishwa hapa chini
na nitayasoma kama ifuatavyo.
i. Kuhakikisha unafanyika ukarabati wa Block C & D kwenye maeneo mbali
mbali
ii. Kuhakikisha ubadilishwaji wa madawati na viti vibovu vya Block A
Unafanyika kwa weredi na ukamilifu
iii. Kuhakikisha upatikanaji wa decoda ya Azam na Dstv vinapatikana na
kulipiwa kifurushi ili wanafunzi wasiteseke katka kuangalia kandanda safi la
mwamba wa Lusaka
iv. Kuhakikisha tunalinda na kuboresha mazingira ya chuo chetu cha IFM na
maeneo yanayozunguka chuo.
v. Kuhakikisha kunapatikana ufumbuzi au utatuzi wa changamoto yeyote ile ya
kimazingira ndani ya chuo chetu haraka iwezekanavyo kila pale changamoto
itakapojitokeza. Hapa tunakusudia zaidi zile changamoto zinazotokana na
uharibifu wa baadhi ya miundombinu au vitu
vi. Kuhakikisha tunalinda na kuboresha mazingira yote ya canteen na yanayo
izunguka canteen ili kulinda maslahi ya wanafunzi wetu.
vii. Kuhakikisha kunapatikana Vimbweta eneo la Maktaba ya Taifa ili wanafunzi
waweze kupata sehemu ya kujisomea
Kuhakikisha tunawapa wakazi wa hostel za kijichi huduma ambazo
zinapatikana apa main campus vifaa vya michezo na huduma zingine kama
television na mengine pia
SEHEMU YA TATU
MAFANIKIO YA WIZARA.
SEHEMU YA NNE.
CHANGAMOTO ZINAZOIKUMBA WIZARA.
Mheshimiwa Spika, Kama ilivyosehemu nyingine sehemu yeyote yenye mafanikio
haikosi changamoto, hivyo wizara ya kampasi na malazi inakumbana na
changamoto kadhaa katika utendaji wake. Miongoni mwa changamoto hizo ni
pamoja na;
SEHEMU YA TANO.
MWISHO.
Mheshimiwa Spika, Wizara inapenda kutoa shukrani za dhati kwa wale wote
wanaliohusika na wanaoendelea kutoa ushirikiano katika utendaji kazi wa wizara.
Kwa kipekee wizara ingependa kutambua mchango wa viongozi wenzetu kutoka
wizara mbalimbali ndani ya serikali ya wanafunzi pamoja na wawikilishi wa
madarasa (CRs) kwa ushirikiano wenu.
Email: ministryofcampusifmso@gmail.com
Imeandaliwa na wizara
Waziri:Fred A.Buzika