Professional Documents
Culture Documents
Halmashauri ya Manispaa imekuwa ikiongeza juhudi za kukusanya mapato yake ya ndani. Katika
mwaka wa fedha wa 2010/2011 Halmashauri ilikisia kukusanya jumla ya Sh. 16,110,130,000,
mapato halisi yaliyokusanywa mwisho wa mwaka yalifikia Sh. 13,059,508,452 sawa na Asilimia
81% ya lengo lake. Kiwango hicho kimekuwa kinaongezeka na kufikia mwaka huu wa fedha
2014/2015, makisio yalikuwa ni Sh. 30,450,000,000 hadi kufikia Juni, 2015 makusanyo halisi
yamefikia Sh. 30,862,178,729.90 sawa na Asilimia 103 ya lengo la mwaka. Aidha kwa mwaka
unaofuata wa 2015/2016 Halmashauri imepanga kukusanya Sh. 54,258,100,000 kutoka mapato ya
ndani.
Takwimu za walipa kodi, mpango unaolenga kubaini idadi ya walipa kodi wa Halmashauri na
hivyo kuwa na makadirio halisi ya mapato. Aidha kutokana na kukua kwa Tekinolojia ya
mawasiliano Manispaa imeanza kuwasiliana na Walipa kodi wake kwa njia ya simu zao za
mkononi kwa ajili ya kuwahimiza na kuwakumbusha ulipaji wa Kodi/Tozo na Ushuru mbalimbali.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi
Usimamizi mzuri ambao umekuwa ukifanywa na Waheshimiwa Madiwani katika kuhakikisha
kuwa kanuni za matumizi ya fedha zinazingatiwa, umeiwezesha Halmashauri kuendelea kupata
Hati safi za Ukaguzi wa Mahesabu. Uthibitisho wa karibu ni taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za
Serikali ya mwaka wa fedha wa 2014/15 ambapo Manispaa ya Ilala ni miongoni mwa
Halmashauri zilizopata hati safi ya Mahesabu.
MASOKO
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Manispaa ya Ilala ina jumla ya masoko 18, masoko makubwa ni Matano (5), masoko
madogomadogo ni 8 na maeneo matano (5) yasiyotumika kikamilifu. Kati ya masoko matano
makubwa, masoko matatu (3) ya Kisutu, Ilala na Buguruni ni masoko yaliyojengwa miaka ya
1960 hivyo kwa sasa hayakidhi mahitaji makubwa ya Wafanyabishara walioko katika masoko
hayo. Katika kipindi hiki cha miaka mitano Halmashauri ya Manispaa imeweka mazingira
mazuri kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Sekta za Biashara na Masoko kwa lengo la kuzalisha
ajira, hususani kwa wafanyabiashara wadogo. Halmashauri imeweza kuanisha maeneo 17 ya
kuendelezwa ikijumuisha shughuli za wafanyabiashara wadogo. Lengo kuu likiwa kuwafanya
wafanyabiashara wadogo kuondokana na uchuuzi mdogo mdogo na kuwa wajasiriamali. Aidha
2
ambapo hadi kufikia mwaka 2015 vimeongezeka na kufikia 29. Aidha katika kipindi hiki baadhi
ya Hospitali na Zahanati zimeingizwa kwenye mchakato wa kupandishwa hadhi. Hospitali ya
Amana imepanda hadhi na sasa ni Hospital ya Mkoa ambapo Kituo cha Afya Mnazi Mmoja
kimepandishwa hadhi kuwa Hospital. Zahanati ya Pugu Kajiungeni inaendelea na mchakato wa
kupandishwa hadhi kuwa kituo cha afya. Kumekuwa na kuimarika kwa ushirikiano kati ya Idara
ya Afya na Wadau wa Afya hususan Taasisi zinazojihusika na utoaji wa Tiba. Utoaji wa Chanjo
kwa Watoto na Kina Mama Wajawazito umevuka lengo la Kitaifa la asilimia 90 na kufikia
asilimia 100 kwa chanjo karibu zote. Mafanikio haya yote yanaonesha ni jinsi gani Waheshimiwa
Madiwani pamoja na Watendaji wameweza kuelekeza jitihada zao katika eneo hili muhimu la
huduma linalogusa moja kwa moja maisha ya Wananchi, kwani inaaminika kuwa Mtu mwenye
Afya bora anao mchango mkubwa katika familia yake na Taifa lake.
USAFI NA HIFADHI YA MAZINGIRA
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Katika eneo hili, Halmashauri inaendelea na juhudi za kuliweka Jiji katika hali ya usafi. Takwimu
zinaonesha wakazi wa Manispaa ya Ilala wanazalisha tani 1,100 za taka ngumu kila siku wakati
uwezo wa kuzoa na kusafirisha hadi dampo la Kigogo Fresh katika Kata ya Pugu ni Tani 676
kufikia Juni, 2015 kiwango hicho ni sawa na Asilimia 61% ya uzalishaji. Mwaka 2010
Halmashauri pamoja na Wakandarasi wengine wa kuzoa taka waliweza kuzoa wastani wa Asilimia
50% za taka ngumu kwa siku. Aidha Halmashauri ina uwezo wa kufagia Km. 136 za barabara
kwa siku dhidi ya Km. 126 za mwaka 2010. Uwezo huu mdogo wa uzoaji wa taka umechangiwa
kwa kiasi kikubwa na ukosefu wa vitendea kazi hususani, malori yenye uwezo mkubwa wa kuzoa
taka. Baraza hili la Madiwani linavunjwa likiwa tayari limetoa idhini ya kukopa Sh. 2.55 Bilioni
kwa ajili ya kununua malori 17 ya kusafirisha taka ili kuboresha zaidi hali ya usafi Jijini.
Kwa kushirikiana na Sekta binafsi Halmashauri inaendelea kutunza jumla ya Ha. 137.4 za misitu
katika bonde la Zingiziwa, Kinyerezi, Kivule dhidi ya majanga ya moto na uvunaji usio endelevu
wa mazao ya misitu. Vikundi 7 vinaendelea na ufugaji nyuki kutumia mizinga ya 157
iliyotundikwa katika misitu ya asili, na ya kupandwa katika maeneo mbalimbali ya Manispaa.
Kupitia Kamati za mazingira za Kata, Wananchi wamekuwa wakielimishwa juu ya umuhimu wa
kutunza Vyanzo vya maji na Uoto wa asili hususani kwenye maeneo ya miinuko.
MIPANGOMIJI
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Kama inavyofahamika Manispaa ya Ilala ndiyo yenye kubeba taswira ya Jiji la Dar es Salaam,
hivyo katika kipindi hiki cha miaka mitano (5) jitihada zimefanyika za kuhakikisha kuwa ujenzi
wa nyumba na majengo unazingatia Sheria na kupunguza makazi holela. Kumekuwa na mipango
ya kubadilisha taswira ya eneo la Manispaa ambapo mipango ya uendelezaji upya wa maeneo
mbalimbali imeidhinishwa. Jumla ya viwanja 29,243 vimemilikishwa kwa wananchi na viwanja
9,123 vimepimwa katika maeneo ya umma, leseni mpya za makazi 1,568 zimesajiliwa. Aidha
wananchi 62,000 wamepata elimu ya sheria za ardhi, Mipango miji na matumizi bora ya ardhi.
UJENZI WA MIUNDOMBINU
Kupitia Idara ya Ujenzi, Halmashauri ya Manispaa imeweza kuboresha zaidi miundombinu yake
ya Barabara, ambapo imeweza kuongeza urefu wa Km. 71.31 za barabara za lami kutoka jumla ya
Km. 190.32 zilizokuwepo mwaka 2010 kufikia Km. 261.63 mwaka 2015. Urefu wa barabara za
Changarawe umeongezeka kwa Km. 56.77 kutoka Km. 76.6 za mwaka 2010 kufikia Km. 133.37
mwaka 2015 na barabara za udongo zenye urefu wa Km. 638.95. zimetengenezwa. Aidha,
makalavati 37 nayo yameweza kujengwa. Katika kipindi hiki Manispaa imeweza kununua Greda
mbili (2) kwa njia ya mkopo ikilenga kuhakikisha kuwa barabara zake zote zinapitika katika
vipindi vyote vya mwaka.
HUDUMA ZA MAJI
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Sote tunatambua kuwa maji ni rasilimali muhimu. Katika kipindi hiki cha miaka mitano (5)
jitihada za kusambaza maji safi na salama katika Manispaa zimefanyika ambapo Halmashauri
imechimba visima virefu 42 na kufanya jumla ya visima vyote vilivyopo kufikia 247. Visima
vifupi nane (8) vilichimbwa na kufikia jumla ya visima 69. Vituo vya kuchotea maji 1,239
Mifumo 9 ya kuvuna maji ya mvua imejengwa. Vikundi vya watumia maji 15 na kamati za maji
50 zimeundwa. Hadi kufikia Juni, 2015 idadi ya wakazi wanaopata maji safi na salama
wanaohudumiwa na visima vya Halmashauri wamefikia Asilimia 52% ya wakazi wote wa
Manispaa wanaokadiriwa kuwa 1,220,611 (Sensa ya 2012).
MAENDELEO NA USTAWI WA JAMI
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Katika kipindi cha kuanzia 2010 hadi 2015 Manispaa ya Ilala imeendelea kutekeleza mipango
mbalimbali ya Ustawi wa Jamii ambapo upo mfumo mzuri wa kuendeleza vikundi vya Wanawake
na Vijana. Makundi haya yamekuwa yakinufaika kwa kupatiwa mikopo kutoka Benki yetu ya
DCB ambapo Halmashauri ina hisa, pia Mfuko wa Wanawake na Vijana umeendelezwa kwa
Halmashauri kutenga fedha kukopesha makundi hayo. Hadi kufikia Juni 2015 vikundi 37 vilifikia
hatua za mwisho za kukopeshwa mitaji ya biashara. Aidha Manispaa ya Ilala imeweka mfumo
mzuri wa kuhudumia Watoto waishio katika mazingira hatarishi kupitia Timu ya Ulinzi na
Usalama wa Mtoto. Dawati la kuwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu
lililofunguliwa Hospital ya Amana limewezesha kuokoa idadi kubwa ya Watoto waliokuwa
wakifanyiwa ukatili wa kijinsia.
MAHUSIANO NA WADAU
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Tunapopima mafanikio ya Manispaa ya Ilala hatuwezi kuacha kuzungumzia eneo la mahusiano.
Dhana ya maendeleo kwa njia ya kushirikisha Wadau wakijumuisha Wafadhili imeendelea
kutekelezwa ndani ya Manispaa ya Ilala. Ofisi ya Mstahiki Meya imeweza kushawishi Shirika la
KOICA kujenga Hospitali eneo la Chanika. Mkataba wa Makubaliano ya kuanza ujenzi
umeshasainiwa. Ujenzi wa Hospital hii utasaidia kusogeza huduma karibu na Wananchi na
kupunguza msongamano wa Wagonjwa katika Hospitali ya Amana. Katika kipindi hiki mipango
ya Maendeleo inayoibuliwa imekuwa Shirikishi. Kata zote 26 zimeunda Kamati ya wananchi
zenye jukumu kuu la kuibua vipaumbele vya ngazi ngazi ya Kata ambavyo baada ya kuidhinishwa
na Kamati za Maendeleo za Kata inajumuishwa katika Mipango na Bajeti ya Halmashauri ambako
inatengewa fedha. Aidha Halmashauri imesimamia na kuendeleza mahusiano yaliyopo kati ya
6