You are on page 1of 12

www.annuurpapers.co.

tz

Sauti ya Waislamu

ISSN 0856 - 3861 Na. 1071 RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Serikali yafuta kinyemela mtihani somo la Islamic


Waislam wapanga kumwona Katibu Ikulu
Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imepitisha uamuzi wa kutotahini tena mtihani wa somo la Dini kuanzia mwaka huu. Katika kupitisha uamuzi huo, Wizara ilikutana na taasisi za Kikristo pekee mwezi Machi mwaka huu na baadae kuwapa taarifa Bakwata juu ya maamuzi yaliyokiwa. Sisi tumefanya tu kupewa taarifa kuwa Serikali imepitisha uamuzi huo, lakini katika kujadili suala hilo hatukufahamishwa, Wizara ilikutana na wadau wa Kikristo pekee. Amesema asa mmoja wa Bakwata akielezea juu ya barua waliyoandikiwa na Kamishna wa Elimu juu ya uamuzi huo. Inaendelea Uk. 2

Askofu Tarcisius asigeuze mada

Uk. 6

Dk. Joyce Ndalichako

Wamwandikia barua Mwanasheria Mkuu Wataka Farid, Uamsho watendewe haki Wadai wanadhalilishwa huko korokoroni
Na Mwandishi Wetu

Maimamu Zanzibar wahoji udhalilishaji wa Masheikh


JUMUIYA ya Maimamu Zanzibar imemwandikia barua Mwanasheria Mkuu ikilalamika na kuhoji kwa nini Serikali ya Umoja wa Kitaifa inamdhalilisha na kumnyima haki Sheikh Farid Hadi pamoja na Masheikh wote wanaokabiliwa na kesi mahakamani. Jumuiya hiyo imesema imelazimika kuandika kuhoji kwa sababu wanaamini kuwa Masheikh hao wanadhulumiwa na kwamba ni jukumu la kila Muislamu kusimamia haki ikizingatiwa kuwa Muislamu nduguye Muislamu. Inaendelea Uk. 2

Sie ni hadithi ya mtoto kulilia wembe Tutafakari ya Umar Farouk Mutallab


Kuna wasiwasi na uwezekano mkubwa kwamba huenda tukio la bomu Kanisani Arusha, likatumika kujenga hoja kuwa sasa Tanzania inakabiliwa na kitisho cha ugaidi wa Al Shabab, Al Qaidah na magaidi wengine. Na hilo likifanyika, utakuwa ni msiba kwa taifa, lakini kwa wakati mwingine kuwa mafanikio makubwa kwa wale ambao kwa muda mrefu sasa walikuwa wakionyesha hamu ya kuona nchi hii kuwa nayo inasajiliwa kuwa na magaidi. Na hilo likitimia, itahalalisha uwepo wa kudumu wa FBI/CIA na hata vikosi vya kijeshi na droni. Inaendelea Uk. 10

Bomu Arusha kufungua mlango wa Al Shabaab

Sheikh Farid Had

IGP Said Mwema

2
S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786 Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: annuurpapers@yahoo.co.uk Osi zetu zipo: Manzese Tip Top Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

Tahariri/Habari
AN-NUUR

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

MAONI YETU

Serikali isiwe chanzo cha migogoro ya kidini


WAKATI serikali ikiwa katika harakati mbalimbali za kuhakikisha kwamba yanakuwepo mahusiano mema ya imani za kidini, na ili kuleta umoja na mshikamano wa kitaifa nchini, kuna haja sasa serikali hiyo hiyo kuwaacha huru Waislamu katika jumuiya zao. Isiwalazimishe kuwa mambo yao lazima ili yake Serikalini yapitie Bakwata. Na kwa upande mwingine Serikali iache msimamo kuwa haiwezi kukaa mezani na taasisi ya Kiislamu isiyo Bakwata wakati kwa Wakristo haifanyi hivyo. Tunasema hivyo kwasababu BAKWATA, limekuwa likilalamikiwa na Waislamu kuwa limeshindwa kutimiza wajibu wake wa kutetea, kulinda na kuendeleza maslahi ya Waislamu nchini, na badala yake limekuwa likishirikiana na serikali katika kutimiza maazimio na dhamira za serikali. Si hivyo tu, baraza hili pia limekuwa likilalamimkiwa kwamba limekuwa likifuja mali za Waislamu kwa maslahi ya watu wachache na kusababisha kudumaa maendeleo ya Waislamu na wakati huo huo kuleta migogoro baina ya Waislamu. Kwa mtazamo huo, sehemu kubwa ya Waislamu nchini inalitazama Baraza hili kama idara ya serikali na chumo la viongozi wachache wa baraza kuliko taasisi ya Kiislamu kwa ajili ya maslahi ya Waislamu wa nchi hii. Ni kutokana na udhaifu huo, mara kadhaa Waislamu wamejaribu kufanya juhudi za kuleta mabadiliko ili kuleta ufanisi wenye maslahi kwao, lakini juhudi hizo mara kadhaa zimekuwa zikizuiwa na nguvu ya serikali. Kimsingi, tunaona kwamba hali hii imeleta athari kubwa sana kwa jamii ya Kiislamu.

Inatoka Uk. 1 Afisa huyo akasema kuwa wao kama Bakwata wameshangaa na kushtuka sana. Akasema kuwa pamoja na kuwa hawakushirikishwa wanakuja kupewa tu taarifa, lakini wanashangaa pia kwa sababu hata walipopewa taarifa na Kamishna wa Elimu, wameambiwa jambo hilo liwe siri. Ni rai yetu kwamba, Jambo hili linafanywa madhali serikali imeonyesha SIRI, je Serikali inataka nia ya dhati katika kuleta Waislamu wasiambiwe? u m o j a n a u p e n d o k w a Kwanini? Kuna agenda gani? wananchi wake kidini, basi Amehoji asa huyo ambaye fursa hiyo pia itumike kwa hata hivyo hakutaka kutaja kuwaacha Waislamu. Iache jina lake akisema kuwa yeye kurasimisha kuwa msemaji sio msemaji wa Bakwata. Awali taarifa juu ya kikao wa Waislamu ni Bakwata. cha Wakristo na Wizara Kama kuna jambo linahitaji juu ya mitihani ya dini, mawazo ya Waislamu, basi zilianza kuvuja kupitia kwa m a w a z o y a o h a y a w e z i Wakristo waliohudhuria kuwasilishwa na BAKWATA ambao walipokutana na pekee. Lazima taasisi nyingine wadau kutoka upande wa zinazowakilisha Waislamu Waislamu waliwalaumu ni zisikilizwe. kwa nini hawakuhudhuria T u n a y a s e m a h a y a wakasaidiana kupinga uamuzi tukizingatia kauli za baadhi huo wa Serikali. ya Wabunge hivi karibuni Hata hivyo, wadau hao ambao kauli zao zinaonyesha kutoka Islamic Education kuwa hueda Muislamu akiwa Panel waliwafahamisha nje ya Bakwata, anatafsiriwa wadau hao wa Kikristo kuwa kama muhalifu au kavunja sheria za nchi. Lakini tunayasema haya pia tukizingatia kauli za wale waliosema kuwa hatua ya Serikali ya kuwadhibiti Waislamu chini ya Bakwata, na kwa namna moja au nyingine, kuingilia utendaji Inatoka Uk. 1 Muislamu ni ndugu wa Baraza hilo, ikiwa ni pamoja na kuhusika katika yake Muislamu ni haramu kuweka viongozi wa ngazi kumdhulumu na ni haramu kuacha kumnusuru za juu, ni ukandamizaji na akidhulumiwa. kinyume cha sheria kwa Wamenukuu Hadithi hiyo sababu haifanyi hivyo kwa Maimamu na kisha kumkabili taasisi za dini nyingine. Mwanasheria Mkuu kwa Wa k a t a k a Wa i s l a m u kusema kuwa wanamkishia w a a c h w e h u r u k a m a malalamiko yao kwa sababu walivyo huru Wakristo katika ndiye Msimamizi Mkuu madhehebu na taasisi zao. wa Sheria katika Serikali na Lakini kubwa zaidi ni utendaji wake kisheria. W a k a s e m a , kwa Serikali kuhakikisha kuwa kwa kauli na vitendo wanashangazwa sana kuiona h a i o n e k a n i k u p e n d e l e a Serikali ya Umoja wa Kitaifa ( SUT) ikiridhia kwa kukaa upande wowote wa jamii. Kwa hiyo, wakati inataka kimya juu ya dhulma na kukutana na viongozi wa kidini ukiukwaji wa kisheria na huku ikihimiza maelewano, udhalilishaji wanaofanyiwa ijitizame pia katika yale Viongozi wa Taasisi za i n a y o t u h u m i w a k w a y o Kiislamu nchini akiwemo kwamba inawapendelea Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar, Sheikh Wakristo. Farid Hadi Ahmed pamoja H a i t a s a i d i a s a n a na viongozi wa Jumuiya ya kuhangaika kuleta maelewano Mihadhara ya Kiislamu na b a i n a y a Wa i s l a m u n a Mashekhe (wengine). Wakristo ikiwa Serikali Jumuiya ya Maimamu yenyewe ndiyo chanzo cha Zanzibar (JUMAZA) inasema utengano kwa kuendesha kuwa Viongozi hao kumi ubaguzi na upendeleo. wa Kiislamu wamezuiliwa

Serikali yafuta kinyemela mtihani wa somo la Islamic


wao walikuwa hawakupewa taarifa. Kufuatia kuvuja kwa taarifa hizo, baadhi ya wajumbe wa Islamic Education Panel walifuatilia jambo hilo Bakwata wakidhani kuwa huenda Bakwata wao walipewa taarifa. Hata hivyo, maofisa wa Bakwata wakasema kuwa nao wanasikia tu, hawakualikwa. Kwa muda mrefu Serikali imekuwa ikitahini masomo ya Dini ya Kiislamu (Maarifa ya Uislamu) na Kikristo (Divinity) katika mitihani ya kidato cha nne na sita na pia katika Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada. Kwa upande wa Maarifa ya U is lamu , Wizara imekuwa ikishirikiana na Islamic Education Panel katika kuandaa mihutasari na mitihani kwa ngazi zote hizo. Vitabu vya mihutasari hiyo, kwa ngazi zote, katika jalada vimewekwa nembo ya Serikali na ile ya Islamic Education Panel na kusainiwa na Kamishana wa Elimu. H a t a h i v y o , Wi z a r a ya Elimu na Mafunzo ya

Ufundi, haikuwaita IEP katika kupitisha uamuzi huo mkubwa na wenye athari kubwa kwa vijana wa Kiislamu na vyuo vya Kiislamu. Hivi sasa Vyuo Vikuu kama kile cha Waislamu Morogoro (MUM), pamoja na wanafunzi wa kozi nyingine, huchukua wanafunzi waliomaliza kidato cha sita na kufaulu Somo la Islamic Knowledge kwa ajili ya kuchukua kozi ya Sheria na Sharia kwa pamoja. Aidha, huchukua pia wanafunzi hao kwa ajili ya kozi ya Masomo ya Dini na Ualimu, yaani BA Islamic Studies and Education. Kwa upande mwingine, Chuo Kikuu cha Elimu Zanzibar (Chukwani) na kile cha Tunguu, navyo vinachukua wanafunzi waliomaliza kidato cha sita na kufaulu somo la Maarifa ya Uislamu kwa ajili ya kozi zao mbalimbali. Vi p o p i a v y u o v i k u u vya Mbale Uganda, Sudan, Uturuki, Malaysia na sehemu nyingine ambapo wana kozi zinazohitaji somo la Maarifa ya Uislamu kama vile Islamic Banking. Inaendelea Uk. 5

Maimamu Zanzibar wahoji udhalilishaji wa Masheikh


na Jeshi la Polisi tokea tarehe 20/10/2012 mwaka jana na kukishwa Mahakamani kwa kesi za bandia zenye sura ya kutengenezwa ili kuwaweka ndani kwa muda mrefu kadiri itakavyowezekana. Jumaza ikadai kuwa Ushahidi wa hayo ni kuwa tokea siku waliofikishwa Mahakamani hadi leo huu sasa unaanza mwezi wa saba, hakuna haki yoyote waliotendewa zaidi ya udhalilishaji na usanii wa kuudanganya Umma wa Wazanzibari kuwa Mashekhe na viongozi wao hao wanakabiliwa na kesi kubwa ili wananchi waogope na warudi nyuma waachane na madai yao ya kudai Mamlaka kamili ya Nchi yao Zanzibar. Mhe, Mwanasheria Mkuu, kwa upande wa Mahakama, hadi hii leo imeshindwa hata kuwapangia Jaji kama taratibu zinavyoelekeza na kwa kipindi hicho chote kesi ya msingi imebaki kwa Mrajisi wa Mahakama ambaye amekuwa akiitaja kila wanapokishwa Mahakamani. Kutokana na kutokuwa na nia nzuri ya kutoa haki kama ambavyo mahakama inatakiwa ifanye, Mrajisi huyu alijipa uwezo wa kuzuia dhamana ya Masheikh na Viongozi hao licha ya kuwa hana uwezo kisheria kufanya hivyo; jambo ambalo limebainishwa wazi na katika hukumu ya Ombi la dhamana lilitolewa tarehe 11/3/2013. Imesema sehemu ya barua ya JUMAZA iliyosainiwa na Katibu Mtendaji wake Sheikh Muhidini Zuberi. Barua hiyo ikaongeza kudai kuwa kwa upande wa Osi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nao umekiuka utaratibu kwa hati ya kupinga dhamana na huku wakijua kuwa hawana sheria wala mamlaka ya kufanya hayo. (na kwamba) kinachoonekana wazi ni kujaribu kuridhisha utashi binafsi wa kisiasa ambao unaonekana kuwa umelengwa kufanikisha kuwaweka ndani Viongozi hao kwa muda mrefu na kuwanyima haki yao ya dhamana kwa kulifanya kosa Inaendelea Uk. 5

3
Na Bakari Mwakangwale
SHEIKH Ponda Issa Ponda, amesema kamwe Waislamu hawatorudi nyuma katika kudai haki zao hata kama itabidi kutoa uhai wao au kukabiliana na vifungo na mateso mengine. Sheikh Ponda ametoa msimamo huo, mbele ya maelfu ya Waislamu waliofurika katika Msikiti wa Mtambani, Kinondoni, Jijini Dar es Salaam, akiongea mara baada ya swala ya Ijumaa ya wiki iliyopita. Wakiwa na shauku kubwa kusikia kauli ya kwanza ya Kiongozi huyo wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, baada ya kuwa rumande kwa muda wa miezi saba, katika gereza la Segerea, Umma wa Kiislamu Msikitini hapo ulirindima kwa mvumo wa Takbirii, baada ya kusikia kauli hiyo. Waislamu hatutorudi nyuma, hakuna kurudi nyuma katika kupambana na madhalimu, haki ya Muislamu katika nchi hii lazima ipatikane. Muislamu haogopi jela, yupo tayari kuia dini yake na sisi ni seheme ya Waislamu hao. Alisema Ponda. Ponda alitahadharisha kwamba dhulma dhidi ya Waislamu nchini ni kubwa, kwani alidai matukio yote yanayotokea hivi sasa ni ya kutengeneza kwa lengo la kuuchafua Uislamu na Waislamu. Alisema, jambo ambalo Waislamu wanapaswa kulizingatia muda wote ni umoja wao, kwani alidai kukamatwa kwa viongozi wao lengo lake ni kuvunja umoja wa Waislamu. Ponda alisema hakuna vurugu za kidini nchini, bali Waislamu wanadai haki zao, badala ya kutafuta ufumbuzi wa madai yao, Serikali imekuwa

Habari

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013


linawafanya vinara wa dhulma hizo kujaribu kuwafumba mdomo. Hatuwezi kukubali sisi kama waja wa Allah (s.w) ambao tuna malengo na kufahamu tumeletwa katika Ulimwengu huu kwa sababu gani, halafu tukakubali yale yaliyotufanya Mwenyezi Mungu atulete hapa, iwe hayafanyiki au tunazuiwa kuyafanya. Alitanabaisha Sheikh Ponda. Akianisha kile alichookiita ni chuki na udini dhidi ya Waislamu, alisema, katika waliokamatwa katika vurugu za Mbagala, wapo waliokutwa na magita na laptop, lakini katika mchujo Polisi jamaa hao waliachiwa na waliobaki ni wale waliokuwa na alama za Uislamu. Ponda alisema, zimetokea vurugu Tunduma, na waliohusika ni Wakristo wakipinga Waislamu kuchinja, walipambana na Polisi na wakenda kuvunja Msikiti, lakini mpaka sasa hakuna shitaka lililofunguliwa kuhusu Wakristo hao. Hii sio nchi ya Kikristo ni nchi ya wote Waislamu na Wakristo ndivyo tunavyotaadharisha siku zote hatuwezi kukubali kuona kundi moja linadidimizwa na lingine likibebwa. Alisema Ponda. Leo Magereza yameja Waislamu, ukiuliza sababu za kufungwa au kunyimwa dhamana hazina sababu za msingi wala hazizingatii utawala wa sheria, ni vile wenye mamalaka wanavyo jisikia wanawahukumu Waislamu. Alilalamikia hali hiyo. Sheikh Ponda Issa Ponda, alihukumiwa kifungo cha nje miezi 12, huku Waislamu wengine 49, waliachiwa huru kufuatia mashitaka waliyokuwa wakikabiliwa nayo, katika Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam.

AN-NUUR

Ponda ahimiza Waislamu kupigania haki

Sheikh Ponda Issa Ponda inakuja na hoja za kupoteza malengo na kuwatisha Waislamu. Kiongozi huyo wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, alisema yote hayo yanakuja kutokana na Waislamu kuwa na agenda na madai ya msingi kwa Serikali yanayohitaji majibu na kufanyiwa kazi sio kupiga siasa za kuyeshusha mada. Mfano pale NECTA (Baraza la Mitihani) ameajiriwa Mchungaji kwa ajili ya maslahi ya wanafunzi wa Kikristo, swali linakuja kwa nini iwe ni Mchungaji tu, asiwepo na mtaalamu wa Somo la Dini ya Kiislamu, badala ya kujibu hoja hizi, wanasema ni uchochezi, huwezi kuigeuza NECTA kuwa Parokiya, sio nchi ya dini moja

hii, yapo mengi huu ni mfano tu. Alisema Ponda. Kuhusu mauwaji ya Mwembecha alisema kuwa ipo mikanda ya muda mrefu yenye maelezo ya Padri kupitia radio moja ya Kikristo, akiishawishi Serikali ikawashambulie Waislamu, lakini pia ipo CD, ambayo anasikika kiongozi wa Serikali akiliomba radhi Kanisa, na kuahidi kuchukua hatua. Mauaji yale ni mauaji ya kinyama kwa Waislamu, na yalifanyika mbele ya vyombo vya habari kumbukumbu zipo katika vyombo hivyo na mikanda ipo hakuna anayeliona hili kwa kuwa waliouwawa ni Waislamu. Alisema Ponda. Alisema, hivi karibuni zimepelekwa CD, Bungeni wabunge wakichachamaa kwa maneno yaliyomo ndani na kulalamika kuwa huo ndio udini, lakini alidai CD ya mauaji ya Waislamu Msikiti wa Mwembechai ipo tokea mwaka 1998, hakuna aliyestuka na mauaji hayo na kwamba Bunge lilikataa hata kuunda Tume ya Uchunguzi. Sheikh Ponda alisema kama si udini dhidi ya Waislamu na kutokujali haki za raia, basi hiyo CD, ya mauaji ndiyo ingestahili kupelekwa Bungeni na kuishinikiza Serikali ifanye uchunguzi na wahusika wachukuliwe hatua. Ndugu zangu, kipindi tunachopita hivi sasa ni kizito sana, si Tanzania tu, bali duniani kwa ujumla, hali ya Waislamu ni nzito. Alisema, yanayojiri hivi sasa nchini dhidi ya Waislamu ni kutokana na kuitambua dhulma dhidi yao na kuiweka hadharani jambo ambalo

Polisi wanajua kuna tatizo kati ya Waislam na Serikali


Na Bakari Mwakangwale WAISLAMU nchini wameelezwa kuwa yapo mambo ya kuzingatia katika kesi iliyokuwa ikiwakabili Waislamu wakiongozwa na Sheikh Ponda Issa Ponda. Akiongea na Waislamu katika Msikiti wa Mtambani, mwishoni mwa wiki iliyopita, Ustadhi Mukadam Swaleh, alisema kuwa moja ni kuwa wapo Polisi wanaotambua kuwa kuna tatizo la msingi kati ya Waislamu na Serikali. Alisema, hayo yametamkwa wazi na baadhi ya Polisi walipokuwa wanawahoji na kuchukua maelezo yao kabla ya kukishwa mahakamani na kuwekwa rumande. Hata hivyo akasema kuwa, Polisi hao walisema kuwa wao hawawezi kumaliza tatizo hilo na wala hatua wanazowachukuliwa Waislamu kama chombo cha dola haziwezi kuondoa tatizo la msingi. Alisema suala lingine ni kwamba wapo baadhi ya watendaji wa vyombo vya dola ambao hufanya kazi zao kwa chuki. Akitoa mfano akasema kuwa wakati wamo ndani, kuna Waislamu waliandamana baadhi wakakamatwa na kufikishwa Segerea. Alisema, wakiwa huko miongoni mwa wale walioandamana alichanganyikiwa akili na alipopelekwa Mahakamani kutokana na hali ile hakimu alimwachia. Lakini alisema kwamba Jeshi la Polisi lilimchukua na kuendelea kumshikilia matokekeo yake Muislamu yule alikosa huduma na kisha kufia mikononi mwa Polisi. H i l i n a l o Wa i s l a m u mlizingatie, muone ni namna gani watu wanafanya kazi kwa chuki, mtu dhahiri ameonekana kuchanganyikiwa, Mahakama imemwachia, lakini bado mtu haridhiki anamshikilia mpaka mwisho wa uhai wake. Alisema Ust Mukadam. Akizungumzia hali ya magereza, Ust. Mukadam, alisema wakati wameingi Segerea walikuta mahabusu 15 waliokuwa wakiswali, lakini baada ya kuka wao walianza kutoa daawa kwa wenzao, na kwamba kwa muda wote huo, mpaka wanatoka wameacha Waislamu wanaoswali wapatao 480, pamoja na waliowasilimisha. Ust. Mukadam, alisema kuwa katika gereza la Segerea panahitajika msaada wa kisima, kwani kuna shida kubwa ya maji kitu ambacho ni muhimu kwa Muislamu katika kuziendea ibada zake. Hivyo aliwataka Waislamu na wote wenye mapenzi mema na watu wajitolee kuchumba kisima.

SAFARI YA UMRAH PAMOJA NA KUTEMBELEA JIJI LA ISTAMBUL, UTURUKI KWA DOLA 1850,
KUONDOKA TAREHE 17 JUNE NA KURUDI TAREHE 30 JUNE 2013 GHARAMA INAJUMUISHA: TIKETI YA NDEGE YA KWENDA NA KURUDI DAR-MADINA, JEDDAH- DAR MALAZI SIKU 4 MADINA KATIKA HOTELI YA NYOTA TATU YA AL ANSAAR NEW PALACE MALAZI SIKU 6 MAKKAH KATIKA HOTELI YA NYOTA TATU YA NAWRAT SHAMS ZIYARAH SEHEMU ZA KIHISTORIA MADINA NA MAKKAH MATEMBEZI YA SIKU 3 KATIKA JIJI LA ISTAMBUL, UTURUKI MALAZI HOTELI YA NYOTA TATU KUTEMBELEA SEHEMU ZA KIHISTORIA IKIWEMO: MAKUMBUSHO AMBAMO KUMEHIFADHIWA NGUO, UPANGA NA PETE YA MTUME SAW. KUZURU KABURI LA ABI AYUB ANSAARI, MSIKITI WA MEHMET (BLUE MOSQIE) PAMOJA NA SEHEMU MBALIMBALI KATIKA JIJI LA ISTAMBUL CHAKULA MILO MITATU NA VIZA YA UTURUKI SIKU YA MWISHO YA KUJISAJILI NI TAREHE 29 MAY 2013 SAFARI YA UMRAH YA SIKU 15 KATIKA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI KWA DOLA 3400 KUONDOKA TAREHE 23 JULY (15 RAMADHAN) NA KURUDI TAREHE 7 AUGUST (29 RAMADHAN) GHARAMA INAJUMUISHA: TIKETI YA NDEGE YA KWENDA NA KURUDI DAR-MADINA, JEDDAH- DAR MALAZI MADINA SIKU 4 KATIKA HOTELI YA NYOTA TATU YA AL ANSAAR NEW PALACE MALAZI MAKKA SIKU 10 KATIKA HOTELI YA NYOTA TATU YA NAWRAT SHAMS ZIYARAH SEHEMU ZA KIHISTORIA MADINA SIKU YA MWISHO YA KUJISAJILI NI TAREHE 20 JUNE 2013. HUDUMA YA UMRAH KWA MTU BINAFSI, FAMILIA NA KIKUNDI INAPATIKANA WAKATI WOWOTE HADI MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI. PIA TUNATOA HUDUMA YA KUOMBA VIZA ZA NCHI MBALIMBALI DUNIANI KWA MAWASILIANO ZAIDI NA USAJILI WASILIANA: PEACE TRAVEL, MTAA WA MAFIA INATAZAMANA NA MASJID MANYEMA. NAMBA YA SIMU 0655/0784 411 788, 0777 411 020, 0713 530 036 Barua pepe: peacetraveltz@gmail.com. Tovuti: http// www.peacetraveltz.com

UMRAH 2013 / 1434

4
Na Kassim I. Chubwa

Makala

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

Kuna maneno mazuri ya Kiingereza husema Every thing has happened there is the reason to be, ukiwa na maana kuwa kila kitu kinachotokea kuna sababu ya kuwa hivyo. Katika hali ya utando na giza iliyotanda katika baadhi ya vichwa vya Watanzania juu ya hali ya hatari inayolinyemelea Taifa, na watu kuzidi kuipalilia mbegu ya chuki ya kimahusiano kati ya Wakristo na Waislamu nchini, kwa kuzingatia msemo huu wa Kiingereza h ay a y an ay o to k ea ip o sababu ya kuwa hivi! Kunahitaji umakini ili kumjua ni nani mhandisi (Architect) wa propaganda na chuki za kidini na hatari inalolinyemelea Taifa letu. Hebu tuitizame historia kidogo baina ya Waislamu na Wakristo nchini, na nani chanzo cha chokochoko zinazoendelea. Ni kianzia na makala maarufu ya mwanahistoria Mohamed Said aliyoipa jina Tusiwalaumu wa Zanzibar kwa kukosa subra turejee Historia, nitamnukuu sehemu ya manneo katika makala hiyo si kweli kuwa Waislamu wana chuki na Wakristo anaetaka kujua ukweli rejea katika histori ya uhuru wa Tanganyika. Ajiulize vipi Mkatoliki Mwalimu Nyerere aliweza kupokelewa na Waislamu Dar es Salaam na wakampa uongozi na baadae kumfanya Waziri Mkuu wa Tanganyika mwaka 1961? Waislamu wangekuwa na chuki na Wakristo Mwalimu Nyerere asingekuwa kama mtoto wa Bi MLUGURU BINT MUSSA akiingia nyumbani kwake Kirki Street akila, kulala na kufuliwa nguo zake pale. Mama zetu wangelikuwa wana chuki na Wakristo, TATU BINT MZEE asingelimwita Nyerere kaka. Waislamu wangelikuwa wana chuki na Wakristo, wasingelikuwa wanakula n a Wa k r i s t o w e n g i n e katika harusi za misiba yao, wangelikuwa na chuki

wasingeliwapangisha Wakristo katika nyumba zao Kariakoo, Ilala, Temeke na kwingineko. Kama hali ilikuwa hivyo, nini kimetokea hadi leo tumekuwa maadui? Jibu ni kuwa ulipopatikana uhuru roho ya Mwl Nyerere ikabadilika akawa si yule aliyeletwa osi ya TAA na Abdulwahid Sykess akawa si Nyerere yule aliyekuwa mkono wa kulia kwake kuna Sheikh Hassan Bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir, Mshume Kiyate, Mwinjuma Mwinyikambi na wengineo. Kisa ni kirefu sitaki kukuchosha matokeao ya kubadilika roho ya Nyerere na uadui wake si kwa wale tu waliomfadhili kama Abbdulwahid Sykes na Sheikh Hassan Bin Ameir na wengineo bali na Waislamu wote kwa ujumla. Nyerere kaenda mbali zaidi akaja na njama kwanza kudhalilisha Uislamu na pili kufuta historia ya kudai uhuru wa Tanganyika. Laiti watu wangejua historia ya Waislamu na Nyerere huenda hali ingekuwa tofauti kidogo. Mwisho wa kunukuu. Nasikitishwa na kejeli na matusi nisomayo katika mitandao ya kijamii, na magazeti mbali mbali y a k w a m b a Wa i s l a m u hawajasoma, Waislamu ni magaidi, Waislamu wanapeleka nchi pabaya! Najiuliza nini kimetokea, kulikoni. Haya ni matokeo ya mbegu ya chuki iliyopaliliwa na kumea vizuri na sasa kuanza kuchipua vyema. K i u h a l i s i a Wa i s l a m u hawana ugomvi na Wakristo isipokuwa Wakristo na Waislamu ni mithili ya watoto wawili wa mama mmoja na baba mmoja, mtoto mmoja ambaye ni Wakristo amedekezwa na kupendelewa na babaye

Hakuna ugomvi kati ya Waislamu na Wakristo


ambaye ni serikali kwa kupewa Memorandum of Understanding (MoU) fursa katika elimu fursa katika ajira, na kusikilizwa kwa yale anayoyadai na kukubaliwa kwa yale anayoyapinga kama vile Mahakama ya Kadhi, Tanzania kujiunga na OIC, na mengine mengi. Mtoto huyu kwa kupewa fursa adhimu ya kustawi na kutotonoka vyema amekuwa yuko tayari kumkejeli nduguye hata kwa kumpaka kamasi ili aendelee kuwa dhalili na hata siku moja asikubaliwe shida zake. Mtoto wa pili ambaye ni Muislamu, amevumilia kwa kipindi kirefu tangu mauaji ya Mwembechai, kuvunjwa kwa jumuiya ya EAMWS, ubaguzi na dhulma za Baraza la Mitihani tangu 1973, mgawanyo sawa wa madaraka hayo ni baadhi aliyoyataja mtoto huyu anayenyanyapaiwa na kunyongeshwa mpaka akafikia kumueleza Mzee wake maneno yaliyowahi kusemwa na Desmond Tutu. Alisema hivi, There can be no Real Peace and Security in (SoA) until there be rst Justice enjoyed by all the inhabitants of that beautiful Land. Tafsiri hakutakuwa na amani ya kweli na usalama (Afrika ya Kusini) hadi kwanza kuwe na haki yenye kufurahiwa na wakazi wote wa nchi hiyo nzuri. (Tazama the Noble Peace Prize lecture Desmond M.Tutu 1986) Kwa maneno mengine, nchi ambayo sehemu ya Raia wake wanalalamika kutokutendewa haki pasi na kusikilizwa na serikali ya nchi hiyo, Amani ya Kweli itakuwani Ndoto. Hapa tunajifunza kumbe kuna amani ya kweli. Matokeo ya kupendelewa kwa Wakristo wamefikia kumwambia wazi wazi baba wa familia (Ambaye ni serikali) nguo alizovaa hazikufai zinakubana na ukiacha kufanya hivyo mimi mwanao hata Bakora. Bado naedelea kusisitiza kuwa Wakristo na Waislamu wangekuwa na chuki kubwa kama inavyosimuliwa na b aad hi ya vy ombo vya habari kutokana na kile kinachodaiwa ni bomu kulipuka Arusha kwenye uzinduzi wa Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, nchi hii isingekuwa inakalika. Mahusiano ya Waislamu na Wakristo katika nchi hutafsiriwa katika maisha yao ya kila siku mitaani, kazini na harakati mbalimbali za kimaisha; sio kulipuliwa nyumba za ibada. Haiwezekani watu waishi vizuri pamoja mitaani na hata katika nyumba moja kisha wakitoka hapo wakalipuliane Misikiti na Makanisa. Serikali ichunguze vizuri iseme ni nani hawa waliolipua kanisa ili kutuharibia mahusiano yetu mazuri kati ya Waislamu na Wakristo nchini. (Kassim_Ibrahimu@yahoo. com)

Ahlul Daawa Hajj And Travel Agency


Inawatangazia Waislamu wote Kuwa Imeandaa Safari ya Hijja Mwaka 2013 Sawa na Mwaka 1434 Hijria kwa Dola US$ 3550 tu. Umra kwa Mwezi wa Ramadhani itakuwa ni Dola US$ 1995 Fomu zinapatikana katika osi zifuatazo:1. Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam Mtaa wa Dosi na Mkadini Nyumba Namba 26 Mkabala na Showroom ya Magari Tel 0713 730 444, au 0773 804101 au 0785 930444 na 0773 930444. 2. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo Tel 0777 484982 au 0777 413 987. 3. Abubakar Maulana wa Markaz Kiwalani Dar es salaam 0784 453838 4. Abdallah Salehe Mazrui ( HOKO) Dar es salaam 0715 724 444 5. Salim Is-haq Dar es salaam 0754 286010 au 0774 786101 6. Dukani kwa Abdala Hadh Mazrui wete pemba 0777 482 665 7. Dukani kwa Mohamed Hadh Mazrui Mkoani Pemba 0777 456911 8. Sheikh Daudi khamis sheha 0777 679692 9. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar 0777 417736 Wahi kulipia. Osi ya Ahlul Daawa Dar es salaam 0713 730 444 au 0773 804101 au 0785 930444. Osi ya Ahlul Daawa Zanzibar Rahaleo 0777 484982 au 0777 413 987. Maalim Seif Humoud Hamed Kijichi Zanzibar 0777 417736 Sheikh Salim Mohamed Salim 0774 412974 au Kupitia A CCOUNT NAMBA 048101000030 NBC Tanbih: Atakae maliza Taratibu zote kuanzia sasa Mpaka 15 July 2013 atapata Punguzo la asilimia 16% atalipia $ Dola 2982 tu. Atakae maliza Taratibu zote kuanzia Tarehe 16-july Hadi Tarehe 15 Augost 2013 atapata Punguzo la Asilimia sita 6% atalipia Dola $3337 tu. Kutakuwa na umra ya utangulizi kabla ya Umra ya Hijja kwa atakae maliza kufanya hivyo. Atakae maliza taratibu zote mwanzo ndie atakae shughulikiwa mwanzo. Ukilipia kwa njia ya Account kwanza piga simu 0774 412975. Kumbuka Kikundi cha Ahlul Daawa Kwa Bei nafuu kuliko wote na Huduma bora Kuliko wengi. Nyote mnakaribishwa

Makala

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

Serikali yafuta kinyemela mtihani wa somo la Islamic

Kwa uamuzi huu wa Serikali, ina maana kuwa sasa itakuwa vigumu kwa MUM na Chukwani kupata wanafunzi wenye sifa kwa hiyo huenda vikalazimika kufuta kozi hizo. Hii maana yake ni kuwa uamuzi huu unapunguza idadi ya wanafunzi wa Kiislamu wanaokuwa na sifa za kupata elimu ya juu. Kinachosikitisha ni kuwa Serikali imeamua kukaa na Wakristo pekee kupitisha maamuzi mazito kama haya bila kujali athari yake kwa vijana wa Kiislamu na taasisi za Kiislamu nchini. Amesema mjumbe mmoja wa Islamic Education Panel akizungumzia suala hilo. Hii ni dharau iliyopitiliza kiwango, Serikali inachukuaje maamuzi kama haya bila kujali kuwa kuna shule za Kiislamu na Vyuo vya Ualimu vya Kiislamu pamoja na Vyuo Vikuu ambavyo vinategemea kupata wanafunzi kutokana na wanafunzi wanaomaliza kidato cha sita wenye somo la Maarifa ya Uislamu? Amesema mjumbe huyo wa Islamic Education Panel ambaye hata hivyo hakutaka kutajwa jina lake gazetini. Kama Serikali imeona kuna mantiki kujitoa katika kutahini somo hili, kwa nini ifanye kinyemela? Kwa nini isiwashirikishe wadau husika ili kujua, ni utaratibu gani mwingine utafanyika ili vyuo vya Kiislamu vilivyopo visiathirike? Kwa nini wasikae pamoja na Panel? Mbona waliwaita Wakristo? Kitu gani kiliwafanya wakwepe kuwaita Waislamu, ni dharau, UDINI, au kuna agenda ya siri? Mdau mmoja wa Kikristo aliyekuwa katika kikao hicho cha Machi kati ya Serikali na wadau wa Elimu wa Kikristo alipoulizwa kuwa katika kikao hicho Serikali imetoa

Inatoka Uk. 2

Dk. Joyce Ndalichako, Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani hoja gani ya kufuta mtihani huo alisema kuwa, hakuna jambo lililoelezwa la kujenga hoja madhubuti, lakini yeye binafsi anadhani ni kutokana na masuala ya Waislamu toka walipopinga matokeo ya Islamic mpaka ikabidi Baraza la Mitihani liyabadili. Wajumbe wa Islamic Education Panel wanasema kuwa, wakati Waislamu wametimiza matakwa yote ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya kuwa na Mihutasari na vitabu kwa ngazi zote, Wakristo hawakuwa w ametimiza matakwa hayo, hawakuwa hata na mihutasari, lakini somo lao lilikuwa likitahiniwa. Hata hivyo, akasema, hao hao ambao hawakuwa wametimiza matakwa ya Wizara na Baraza la Mitihani, ndio walioitwa kupitisha uamuzi wa Serikali kujitoa katika kutahini mtihani huo. Waislamu wakilalamika kuwa kuna ubaguzi, udhalilishaji, uonevu na udini, wanaambiwa wanafanya uchochezi, hivi Serikali inaweza kukaa na Waislamu pekee na kufanya maamuzi makubwa yenye kugusa masilahi ya Kanisa Katoliki na Wakristo wote, halafu ifanye tu kuwapelekea taarifa Baraza la Maaskofu juu ya maamuzi hayo? Alihoji. Wachambuzi wa masuala ya kidini na kijamii nchini wanasema kuwa huenda Serikali imeamua kujitoa katika suala hili ili ipate fursa ya kuweka mkakati mwingine wa kuibuka na somo la dini mseto baada ya kukwama huko nyuma. Hata hivyo wengine wanasema kuwa hii ni moja tu ya mikakati ya kupunguza idadi ya vijana wa Kiislamu wenye sifa za kujiunga na vyuo vikuu. Wengine wakakumbusha kuwa zilipoanzishwa shule za kwanza za seminari za Kiislamu, Serikali ilitangaza kuwa shule hizo sio shule zinazotambulika. Ni Madrasa. Kwa hiyo wanafunzi wake wakimaliza kidato cha nne wasingepatiwa nafasi za kusoma kidato cha tano katika shule za Serikali. Na kwamba kwa wale watakaomaliza kidato cha sita, wasingechaguliwa kuingia vyuo vikuu na vyuo vingine vya Serikali. Kwa vile isingewezekana kutangaza kuwa wasiotakiwa ni Waislamu pekee, ilibidi tangazo liguse shule zote pamoja na seminari za Kikristo. Hata hivyo, baadae walilazimka wenyewe kuondoa tena kimya kimya sera hiyo kabla haijafanyiwa kazi, baada ya kuona kuwa watakao athirika zaidi ni vijana wa Kikristo kwa sababu ni taasisi za Kikristo zilizokuwa na shule nyingi za seminari. Ni kwa sababu ya matukio kama hayo, baadhi ya wachambuzi wanasema kuwa huenda kuna agenda ya siri inayowalenga Waislamu na ndio maana waliitwa Wakristo pekee ili waelimishwe kuwa wawe radhi kutoa muhanga mtihani wa Divinity. Kwa upande mwingine huenda hawakuitwa Waislamu kwa kuhowa kuwa wangehoji mambo ambayo yasingeweza kupatiwa majibu moja likiwa ni utaratibu gani umeandaliwa kuhakikisha kuwa MUM, Chukwani na

vyuo vingine vya Kiislamu vyenye kozi za Islamic Studies, Shariah na Islamic Banking, vitapata wanafunzi kulingana na vigezo vya Mamlaka ya Vyuo VikuuTanzania Commission for Universities (TCU). Habari kutoka ndani ya Bakwata na Islamic Education Panel zinasema kuwa taarifa kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi juu ya suala hilo, imeeleza kuwa nao Wizara wamefanya kupewa maelekezo na Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu. N a k w a m b a Wi z a r a ilitakiwa kukaa na wadau, kwa maana ya taasisi za kidini kuangalia suala hilo. Hata hivyo, haikuweza kufahamika kuwa uamuzi wa kutokuwashirikisha Waislamu na badala yake kukaa na Wakristo pekee, ilikuwa ni maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi au ulikuwa uamuzi wa Kamishna wa Elimu. Wa d a d i s i w e n g i n e wanasema kuwa jambo hili limetokea Baraza la Mitihani ( N E C TA ) n a k w a m b a kama ambavyo Baraza hilo liliona umuhimu wa kuajiri Mchungaji wa kutizama masilahi ya wanafunzi wa Kikristo na kugoma kuajiri Muislamu, ndio mtindo huo huo umetumika katika kuita kikao cha Wizarani. Kutokana na hali hiyo, Waislamu kupitia taasisi zao, wamepanga kumuona Katibu Mkuu Kiongozi kupata ufafanuzi juu ya suala hilo. Na kwa kuwa suala hili linagusa masilahi ya Waislamu wote nchini, litafanyiwa taratibu za kujadiliwa na kupitishwa maamuzi ya pamoja. Hadi jana tukienda mitamboni juhudi za kuwapata wahusika Wizara ya Elimu na NECTA kuzungumzia suala hili, hazikuweza kufanikiwa.

Maimamu Zanzibar wahoji udhalilishaji wa Masheikh


Inatoka Uk. 2

ambalo halipo kuwa ni kosa kubwa na la kutisha kinchi. Wa k i m t u p i a l a w a m a Mwanasheria Mkuu, JUMAZA wakamkabili wakisema: We w e n i m w e l e d i zaidi wa mambo ya sheria na hivyo unafahamu fika kuwa dhamana ni haki ya mtuhumiwa kwa kesi kama hiyo, lakini bado Mashekhe wanaendelea kunyimwa dhamana hiyo na kupigwa

danedane. Sheria zinachezewa huku Serikali ya Umoja wa Kitaifa ikibariki ukiukwaji huo kwa ukimya wake na kupongeza Jeshi la Polisi. Mbali ya kuwa dhamana ni haki yao, kesi yenyewe unafahamu wewe na Serikali kuwa kisheria kesi hiyo ililazimika isikilizwe ndani ya miezi minne na Sheria inaelekeza ikishindikana, basi kesi ifutwe, la kusikitisha leo ni mwezi wa sita udhalilishaji unaendelezwa huku wananchi

wakifanywa waamini kuwa nchi hii ina Utawala Bora na Kuheshimu Sheria. Wakikamilisha maelezo yao JUMAZA wakasema k u w a Wa i s l a m u w a Zanzibar hawajawahi kuona viongozi wa dini ya Kikristo wakidhalilishwa kwa namna yoyote ile kama wanavyofanyiwa viongozi wa Waislamu. Na wakamaliza kwa kuwataka wananchi kuungana na kutoa sauti moja ya

kupinga dhulma, uonevu na udhalilishaji kwa sababu hiyo sio yaliyotarajiwa kuletwa na kufanywa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Jumuiya ya Maimamu inatoa wito kwa Serikali na Wawakilishi wa wananchi kusimamia Utawala wa Haki na Sheria bila ubaguzi na kushirikiana pamoja na wananchi kutanguliza utetezi wa maslahi ya nchi kwanza. Maslahi ya vyama, vikundi vya watu na mtu binafsi

yatafuatia baadae. Walimaliza JUMAZA katika barua yao waliyoinakili kwa Waziri wa Sheria, Baraza la Mapinduzi, Jaji Mkuu, Baraza la Wawakilishi na Mkurugenzi wa Mashitaka. Wengine waliopewa nakala ni Shirika la Kimataifa la Kutetea Wafungwa (Amnesty International), Umoja wa Majaji na Makadhi Zanzibar, East Africa Law Society, Zanzibar Law Society na Waandishi wa Habari.

6
Na Omar Msangi
The Church is now totally dependent on State aid for the administration of these schools. If this aid were withdrawn the church will be forced to close its schools. Hii ni kauli ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) Fr Robbinson, D. W miaka ya 1960. Kauli hiyo inamaanisha kuwa Kanisa limekuwa tegemezi kabisa kwa Serikali katika kutoa pesa za kuendesha shule zake na kwamba ikiwa Serikali itasita kutoa fedha kwa shule hizo, basi Kanisa litalazimika kuzifunga. Hiyo ilikuwa ni mwaka 1965 ambapo inaelezwa kuwa hadi kukia mwaka 1964, kiasi cha asilimia 60 ya bajeti ya Kanisa Katoliki katika kuendesha shule zake ilikuwa inategemewa kutoka Serikalini. Kutoka katika Hazina yenye kuchangiwa na Watanzania wote. Kwa mujibu wa taarifa ya Padiri Robbinson, kufika mwaka huo wa 1965, ndio ikawa kwa asilimia mia moja (100%), ndio kanisa likawa linategemea kuchotewa pesa kutoka Hazina. Kwa upande mwingine, Padiri Dr. John Sivalon anasema kuwa, kutokana na ukweli kuwa wahitimu wengi wa shule za Kanisa za St. Marys Tabora na St. Francis Pugu, ndio walishika serikali, iliwezesha kukua kwa uhusiano kati ya viongozi wa Kanisa na wa Serikali na Chama (TANU/CCM). Na kwamba hali hii imefanya matendo, msimamo na uamuzi wa viongozi wa Serikali ufanane mara kwa mara kwa namna moja au nyingine na mafundisho na mwelekeo wa Kanisa. Na nini ulikuwa mwelekeo, mtizamo na msimamo wa Kanisa? Padri Sivalon anasema kuwa ulikuwa ule wa kupinga kuenea kwa dini ya Kiislamu na kwamba walifanya makusudi kujenga uhusiano na viongozi wa Serikali ili wawe na nafasi nzuri katika kujihami dhidi ya uenezi wa Uislamu. Padiri Sivalon anasema kuwa moja ya mambo ambayo maaskofu hawakupenda kuona, ni kuwepo kwa taasisi madhubuti za Waislamu zinazowajengea umoja na kuwaleta maendeleo. Waliitaja kwa jina Jumuiya ya Maendeleo ya Waislamu ya Afrika Mashariki-East A f r i c a M u s l i m We l f a r e Society (EAMWS). Na baada ya kuonyesha kuwa hawataki kuiona EAMWS, kilichofuatia ni Mwalimu Nyerere kupiga marufuku taasisi hiyo na Serikali kusimamia kuundwa kwa Bakwata kule Iringa. Nikutokana na historia hiyo, ndio maana mpaka leo akina Mheshimiwa Anna Abdallah bado hawaoni vibaya kusimama bungeni kuitaka Serikali iendelee kuwadhibiti Waislamu chini ya Bakwata. Ijumaa wiki iliyopita wakati wa mazishi ya watu waliokufa katika mlipuko wa Bomu

MAKALA

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013


Waziri wa Fedha Basil Pesambili Mramba akiwa pia ni Mbunge wa Rombo, alipokea jumla ya shilingi 76,200,000 kutoka katika kampuni ya kuchimba gesi iitwayo Rak Gas ya Falme za Kiarabu na kuzipeleka kuendeleza shule za Rombo. Kwa kawaida makampuni kutoka nje hushauriwa na Serikali kutoa misaada ya kimaendeleo katika eneo ambalo ndiko kampuni husika hufanya shughuli zake. Kampuni ya Rak Gas ilikuwa ikijishughulisha na utati wa gesi Lindi, lakini msaada waliotoa badala ya kuwanufaisha watu wa Lindi (kwenye Waislamu wengi), pesa zikapelekwa Rombo kwenye Wakristo wengi. Kutokana ile ahadi aliyotoa Mwalimu kuwa atalipa Kanisa fursa bora hapa Tanzania, Dr. Sivalon anasema kuwa Mwalimu alikuwa na uhusiano wa karibu sana na maaskofu akikutana nao mara kwa mara na alikuwa kiungo muhimu katika utume wao. Na kwamba alifanya kila awezalo kuwaimarisha kiuchumi jambo lililolifanya Kanisa Katoliki kuwa na nguvu za kiuchumi wakati taifa likiwa kwenye hali mbayana kwamba Kanisa likawa ndicho chombo pekee kilichoweza kushindana na Chama na Serikali katika sehemu zote za Tanzania Bara. Na kwa nguvu hizo na kwa kutokana na ukweli kuwa karibu taasisi zote muhimu za kiserikali zimeshikwa na Wakristo, ndio anasema Padiri John Sivalon kuwa wakati mwingine katika utendaji wa Serikali inakuwa vigumu kujua ni lipi la Kanisa na lipi la Serikali. A s k o f u Ta r c i s i u s Ngalalekumtwa, huu ndio mfumokristo wanaozungumzia Wa i s l a m u n a k a m a ilivyoonyeshwa umeasisiwa na Hayati Mwalimu Nyerere. Ni mfumo wa UDINI dhidi ya Uislamu na Waislamu. Kwa misingi ya kiserikali, katiba na sheria za nchi, mfumo huu haupo rasmi. Lakini kiutendaji mfumo huu umefanywa kuwa ndio mila, desturi na utamaduni wa watendaji walio wengi serikalini na katika taasisi za nchi ambako unatumika kukandamiza na kudhulumu haki za Waislamu. Jaribio la Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa kutaka kuunganisha madai ya Waislamu kuhusu mfumokristo na bomu la Arusha au kujaribu kuleta madai kuwa Muislamu kupinga dhulma kama walivyosema wakiwa Diamond Jubilee, ni sawa na kutaka Waislamu wakubali kuwa dhalili, wenye kudhulumiwa, kubaguliwa, kukandamizwa, raia daraja la pili na hohe hahe, daima dumu. Hili hatudhani kuwa kuna binadamu yeyote anayeweza kulikubali. Kwa hiyo, kama ni kuvuruga amani ya nchi, wataivuruga wale ambao watajaribu kuwapakazia uhalifu Waislamu wanaopinga dhulma kama mkakati wa kuwanyamazisha.

AN-NUUR

Bomu lisiunganishwe na madai ya Waislam Yaliyosemwa Diamond Jubilee haya hapa Na huu ndio Waislam wanaita Mfumokristo
Kanisani Arusha, Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa alihusisha tukio la kulipuliwa bomu Kanisani na Waislamu. Katika maelezo yake mbele ya Waziri Mkuu, Askofu Ngalalekumtwa amesema kuwa katika miongo mitatu hali ya usalama nchini imetoweka na hili linafanywa na baadhi ya watu wasiolitakia mema taifa hili na wapinga Ukristo. Akifafanua na kuwataja hao wasiolitakia mema taifa hili na wapinga Ukristo, akasema kuwa ni wale waliofanya vikao vingi na cha mwisho kilikuwa Oktoba 16 mwaka 2011 katika ukumbi wa Diamond Jubilee na kuazimia kuuwa ili kutokomeza Ukristo. Akifafanua zaidi akasema kuwa katika kongamano la Diamond walichochea chuki ya kidini kati ya Waislamu na Wakristo kwa kudai kuwa Serikali ya Tanzania inaongozwa kwa mfumokristo ulioasisiwa na Hayati Mwalimu Nyerere. Akinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari Askofu Ta r c i s i u s N g a l a l e k u m t w a alisema kuwa katika kongamano hilo, washiriki waliaminishwa kuwa Serikali inatoa fedha za ruzuku kujenga shule na taasisi za Kanisa kutokana na kuwapo mkataba maalum kati ya Kanisa na Serikali, jambo ambalo siyo kweli. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba Serikali haikukanusha madai na uchochezi huo, licha ya mambo hayo kufanyika na kusemwa hadharani kwa wahusika kuzunguka nchi nzima kueneza chuki na uchochezi huo. N i s e m e k u w a , kinachosikitisha ni kuwa Serikali haijajibu wala kutekeleza madai haya ya Waislamu. Sio kuwa haijakanusha kama anavyosema Askofu Ngalalekumtwa. Serikali haiwezi kukanusha kwa sababu ni madai ya kweli. Na kama anavyosema Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, Waislamu walikutana Diamond Jubilee. Hawakujicha. Walitembea nchi nzima na kueleza madai yao hadharani. Walifanya hivyo kwa sababu hawakuwa wakitangaza biashara ya bangi wala kusema mambo ya kuzua na kuchochea chuki wala kutangaza ubaya na Wakristo. Waliyosema yote yalikuwa ya kweli. Kwa bahati mbaya Serikali ikaona namna ya kujibu ni kukaa kimya. Labda tumuulize Askofu Ngalalekumtwa, hivi ingekuwa n i k w e l i k u w a Wa i s l a m u waliokutana Oktoba 16 mwaka 2011 katika ukumbi wa Diamond Jubilee waliazimia kuuwa (Wakristo) ili kutokomeza Ukristo na wakatembea nchi nzima kutangaza azma hiyo, leo 2013, bado nchi ingekuwa salama? Kwa wanasiasa kusema mambo ya kuzua kama haya na hata makubwa zaidi, inaweza isiwe ni jambo la kushangaza sana; lakini inapokuwa ni kiongozi wa Kidini, kidogo hapo inaleta maswali mengi na utata mwingi! Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Kamati Maalumu iliyoandaa Makongamano ya Waislamu Dhidi ya Mfumokristo na wakaandaa lile kongamano la Ukumbi wa Diamond Jubilee Oktoba 16, 2011, katika mwaka wa fedha wa 2009/10 Serikali ilitumia jumla ya shilingi 85,776,373,200 katika hospitali na taasisi nyingine za huduma ya afya zinazomilikiwa na makanisa na zile zinazomilikiwa na Serikali kwa ajili ya kulipa mishahara wafanyakazi na gharama za uendeshaji. Kati ya fedha hizo, shilingi 46,624, 820, 500 ambazo ni sawa na asilimia 54.4 ya fedha zote, zilipelekwa katika hospitali na taasisi nyingine za huduma za afya zinazomilikiwa na makanisa. Hospitali na taasisi zinazomilikiwa na Serikali zilipatiwa shilingi 39,151,552,700 sawa na asilimia 45.6 Lakini ukiacha taarifa hizi za kiutati, Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika hotuba yake katika Misa ya kusimikwa Askofu wa Jimbo la Dodoma , Gervas Nyaisonga, Machi mwaka 2011 alisema kuwa mwaka 2010 Serikali yake iliwapa Wakristo ruzuku ya shilingi bilioni 61.9 (61,900,000,000). Na kwamba kwa mwaka 2011 ruzuku hiyo ilitarajiwa kukia shilingi bilioni 112. Yote haya yanafanyika kwa sababu toka huko nyuma kama alivyosema Fr. Robbinson, Serikali ilikuwa imejiwekea utaratibu wa kuwapa Wakristo fedha kutoka hazina ya nchi kuendesha shughuli zao na kufika mwaka 1992 ndio

Askofu Tarcisius asigeuze mada


utaratibu huo ukawekewa makubaliano maalum ya kisheria. Makubalinao hayo kama yalivyosainiwa na Mheshimwa Edward Lowassa kwa niaba ya Serikali ndiyo yanayojulikana kama Memorandum of Understanding (MoU) ambapo Serikali inalazimishwa kutenga kiasi cha fedha za walipa kodi na kuzipa taasisi za afya na elimu zinazomilikiwa na Wakristo. Lakini pia chini ya MoU, Serikali inatakiwa kusaidia taasisi zinazomilikiwa na Makanisa kupata misaada kutoka kwa wafadhili wa nje ya nchi, pamoja na kutenga nafasi maalum za masomo katika shule na vyuo kwa ajili ya kusomesha watu watakaofanya kazi katika taasisi za elimu na afya zinazomilikiwa na makanisa. Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa, kama huu ndio ukweli, na hii ndio hali ya mambo katika nchi hii inayodaiwa kuwa hakuna ubaguzi wala upendeleo wa kidini, Serikali ikanushe nini? Mwandishi Bergen P kwenye kitabu kiitwacho, Development and Religion in Tanzania ukurasa wa 334 anamnukuu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akisema manneo yafuatayo: Im a layman but I try to do what I can anda will not go against my own church. I want to give the church a better chance here. Tell the Bishops that I have established in TANU a department of political education and have put a Lutheran minister in charge; he was not a greater politician I selected him because of his strong faith. Yaani, Mimi si mjuzi wa dini lakini huwa najaribu kufanya kile niwezacho na kamwe sitoenda kinyume na Kanisa langu. Nataka kulipa Kanisa fursa bora hapa. Waambie maaskofu kwamba nimeunda Idara ya Elimu ya Siasa katika Chama cha TANU na kumweka waziri ambaye ni Mlutheri kuwa kiongozi wa Idara hiyo. Yeye si mwanasiasa mahiri, hasha, nimemuweka kwa sababu ni muumini thabiti wa Kikristo. Katika taarifa yao, Waislamu waliokutana Diamond Oktoba 16, 2011 wakisherehesha kauli hii ya mwalimu Nyerere walisema kuwa ni kutokana na mawaziri na watumishi wengine wa Serikali wanaoteuliwa kwa kuzingatia umadhubuti wao katika Ukristo, ndio maana aliyewahi kuwa

Tangazo

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

Yakitekelezwa yaliyosemwa Diamond ndio amani ya kweli itapatikana nchini


Na Hashim Saiboko

Makala

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

Vipi hii inakufaa? Inaonekana inafanana sana na rangi (ya njano) ya kile chama chako. Lakini sasa hivi ni kuchagua mtu siyo mambo ya chama-Askofu Alex Malasusa. Ndugu mhariri naomba unipatie nafasi katika gazeti lako ili niweze kuwatahadharisha wale wanaodhani kwamba vuguvugu la Waislamu la kudai mfumokristo ukomeshwe zinaweza kunyamazishwa na propaganda na uongo na unaoenezwa na baadhi ya Maaskofu na mawakala wao. Tumeearifiwa kupitia katika vyombo vya habari kwamba siku ya maziko ya watu waliouwawa katika mlipuko wa bomu uliotokea kanisani Arusha, Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa alinukuliwa akidai kwamba walipuaji wa bomu wana uhusiano na Waislamu waliokutana Diamond Jubilee tarehe 16 Oktoba, 2011 kuzungumzia mfumokristo. Aidha juma hili Dr Kitima ambaye ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Saint Agustino (SAUTI) aliiambia Star Television katika kipindi kimoja cha TV hiyo kwamba viko vyuo hapa nchini kimojawapo kikiwa huko Morogoro ambavyo vinatoa magaidi. Huu ndiyo ninaosema ni uongo na propaganda za wale wanaofaidika na mfumokristo. Tuliona jinsi mara baada ya mlipuko wa bomu kutokea Arusha ambavyo haraka haraka ilikimbiliwa kuwakamata Waarabu. Hii ilikuwa ni kuweka taswira kwamba walipuaji walikuwa ni Waislamu. Hatujaambiwa kwamba hakuna Wazungu waliokuwa Arusha siku ile ya tukio. Bila shaka watu wamejengewa dhana potofu kwamba Wazungu ni Wakristo hivyo hawawezi kufanya uovu ule! Kuhusu kongamano la Diamond Jubilee ni kweli kwamba lilifanyika na kufuatiliwa na makongamano ya nchi nzima. Yaliyosemwa pale yamo katika kijitabu na katika CD/DVD. Kijitabu kilisambazwa katika osi zote za serikali. Kwa hiyo kongomano lile halikuwa na siri yoyote na wala maudhui yake kamwe hayawezi kusemwa kwamba ni siri. Viongozi wa serikali, maaskofu wanatambua wazi kwamba maudhui ya kongamano la Diamond ilikuwa ni kujaribu kuwazindua wale wanaodhani kwamba kunaweza kuwepo amani ya kweli na ya kudumu katika taifa ambalo baadhi ya watu wake wanabaguliwa kwa misingi ya dini yao. Kijitabu kile kimesheheni mifano kadha wa kadha ya kuonesha jinsi serikali inavyotumia rasilimali za nchi kuwanufaisha Wakristo huku Waislamu wakibanwa. Mwito ulitolewa kwa serikali kukomesha upendeleo huo ambao ndiyo ulioitwa mfumokristo. Wa i s l a m u h a w a k u k u t a n a Diamond kutangaza vita dhidi ya Wakristo. Wanajua kwamba Wakristo wengi wa kawaida hawajui uwepo wa mfumokristo kwa maana ya ubaguzi dhidi ya Waislamu. Wamezoea kujiona wakiwa wengi katika shule na vyuo vya umma. Wamezoea kuwaona baba zao na shangazi zao wakiwa katika maosi ya umma peke yao. Wengi wa Wakristo wa kawaida wameelewa kwamba Waislamu hawako shuleni, vyuoni na maosini kwa sababu

Maaskofu waache kupiga propaganda haisaidii

kama inavyosemwa mara kwa mara na wakuu wa mfumokristo kuwa (eti) Waislamu hawapendi kusoma. Wote tuliokuwa Diamond tunatambua ukweli huu na hivyo hatuna sababu ya kutangaza vita na Wakristo wala nyumba zao za ibada. Na kwa kuwa kijitabu kipo na DVD pia zipo na hilo halimo, ni dhahiri basi kwamba uongo na propaganda za Maaskofu lengo lake ni kuwazuia Waislamu kufahamamishana ukweli kuhusu uwepo wa mfumokristo na kuwataka waupinge kwa nguvu zao zote ili kuihakikishia Tanzania amani ya kweli na ya kudumu. Ifahamike pia kwamba Waislamu wote tuliokuwa Diamond Jubilee tunafahamu wazi kwamba maaskofu wote wanajua uwepo wa mfumokristo na namna ambavyo wao binafsi na makanisa yao yatakavyoathirika kama mfumokristo hautaendelea kuwepo. Lakini pia tunajua wote tuliokwenda Diamond Jubilee kwamba sio wote wanaodai kuwa wanaipenda nchi na kuitakia amani, wanasema kweli. Tazama gazeti la Mwananchi la Oktoba 17, 2010 ambalo liliripoti kwamba MKUU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk Alex Malasusa amewataka Watanzania kuchagua kiongozi makini badala ya chama. Ona jinsi alivyowahamasisha waamini wake kuinyima CCM kura mwaka 2010, rejea maneno yafuatayo yaliyonukuliwa kutoka Gazeti la Mwananchi la tarehe niliyoitaja, Wakati akipiga mnada wa khanga, ambayo ilikuwa na rangi ya njano, Askofu Malasusa alimtazama mmoja wa watu waliotaka kununua khanga hiyo na kumuuliza: Vipi hii inakufaa? Inaonekana inafanana sana na rangi ya kile chama chako. Lakini sasa hivi ni kuchagua mtu siyo mambo ya chama. Ifahamike pia kwamba wote tuliokuwa Diamond tunafahamu ka lipi lilikuwa chaguo la Maaskofu katika uchaguzi wa mwaka 2010

na kipi chama kilikuwa chaguo lao na kwa nini. Na kwa bahati nzuri hawakujicha. Wote tuliokuwa Diamond tunaelewa kwamba maana ya udini ambayo sisi tumeiita mfumokristo ambayo in dhana inayoelezea upendeleo unaofanywa na serikali kuwapendelea Wakristo huku ikiwabana Waislamu siyo sawa na dhana ya udini inayotamkwa na maaskofu. Kwa watumishi hawa wa Bwana maana ya udini ni Muislamu kupata haki yake! Rais akimteua Muislamu kuongoza taasisi au kuwa katika cheo fulani huo ni udini. Na neno hili kuwa udini ni kumpa Muislamu nafasi limedhihirika hata katika Bunge linaloendelea hivi sasa. Waziri wa nchi Osi ya Rais Prof. Mark Mwandosya alisimama kumtetea Rais wetu Mheshimiwa Jakaya Kikwete kwamba hana udini na kutoa ushahidi kuwa Osi ya Rais imejaa mawaziri, makatibu na wakurugenzi Wakristo. Kwa mtazamo wa wenzetu hawa kuwepo Wakristo wenyewe katika osi moja ya umma, huo si udini! Lakini huko UDOM kumejaa udini na bunge limeelezwa kwa sababu tu yuko kiongozi mmoja Muislamu tena Profesa! Wote tuliokwenda Diamond Jubilee tunafahamu kwamba maaskofu wanapozungumzia umoja wa kitaifa wanazungumzia maslahi yao serikalini. Kila anayepinga maslahi ya kanisa serikalini anaonekana kuhatarisha amani. Maneno yatatungwa ili kuwapiga vita. Katika tukio la kuchomwa makanisa Mbagala, maaskofu walitumia fursa hiyo kuitaka serikali ifikirie uwezekano wa kupiga marufuku vazi la hijabu katika osi za umma na mashuleni. Katika tamko lao la tarehe 18 Oktoba 2012 wanasema, Kulazimisha uvaaji wa alama za kidini katika taasisi za umma ili kurahisisha na kuratibisha tofauti za Watanzania. Tunajiuliza: Likitokea la Mbagala

katika mashule yetu na vyuo vya umma, watachomwa wangapi na kuuawa wangapi? Kwa maaskofu kupinga maadili ya dini za wengine ndio utaifa wenyewe. Maaskofu wanapinga vazi la hijab kwa hoja ya Utanzania. Hata siku moja hawapingi makasisi na watawa kuvaa nguo na misalaba mikubwa inayoashiria dini zao. Kwa maaskofu dini ya Tanzania ni Ukristo na Watanzania wenye haki mbele ya serikali ni Wakristo. Wengine sisi ni kama wapagazi tu au wapangaji. Tunaweza kutakiwa kuondoka wakati wowote. Kwao wao lazima tuwe na adabu! Hili si udini! Kwa sisi tuliokuwa Diamond Jubilee, tungependa kutambuliwa kama Waislamu wa Tanzania badala ya Watanzania Waislamu. Wote tuliokwenda Diamond Jubilee tunatambua dhamira njema tuliyo nayo hata sasa kwa taifa hili. Tuna yakini kwamba Waislamu hawataweza kuendelea kusubiri kwa miaka mingine 50 wakiwa watazamaji tu na wengine wakifaidi maliasili na rasilimali za nchi yetu. Hawatakubali kuendelea kulipa kodi na kuiacha serikali kuendelea kutoa sehemu ya kodi zao kuwapa makanisa kuendeshea taasisi zao za elimu na afya kupitia muafaka wa MoU. Wote tuliokuwa Diamond Jubilee hatuwezi kusema kwamba hatuna wasiwasi kwamba huenda baadhi ya maaskofu hulipwa mishahara yao kupitia pesa za MoU kwa ulaghai wakijifanya kama watumishi wa afya katika hospitali za kanisa wakati hawafanyi kazi hizo. Kwa maaskofu hili la kupewa pesa za serikali kuendeshea mambo yao si udini! Ningependa kuishauri serikali yangu na maaskofu na wale mawakala wa mfumokristo kwamba amani ya Tanzania itakuwa endelevu kwa kuzingatia haki sawa kwa wote. Ingekuwa amani inadumishwa kwa kuwakamata wanaosema dhidi ya maovu na kuwafunga, basi

wangefanikwa Makaburu wa Afrika Kusini. Waislamu waliokwenda Diamond hawawachukii Wakristo japo wasitegemewa kuwapenda maaskofu ambao kila uchao dua yao ni kuona Waislamu wakikwa na mabalaa. Kila linalotakiwa na Waislamu: Iwe Mahakama ya Kadhi, OIC, haki sawa, elimu kwa Waislamu, uteuzi na ajira bila ubaguzi, wao hutoa kauli za kupinga. Japo maaskofu hawategemei siku moja serikali iwaaambie waache kuhubiri hadharani uungu wa Yesu, lakini kila siku wanaichagiza serikali iwazuie Waislamu kuhubiri kuwa Issa bin Mariam (Yesu) si Mungu! Wa i s l a m u w a l i o k w e n d a Diamond Jubilee kuupinga mfumokristo na kuchukua azimio la kukisha ujumbe ule nchi nzima hawakutegemea maaskofu waje na kauli yenye heri nao. Hivyo kama ambavyo hatukushangaa Makaburu na wakoloni wa Kireno walivyowaua akina Steve Biko, Solomoni Mahlangu na Edward Mondlane, hatuwashangai maaskofu wanapoitaka serikali kuwashughulikia walikwenda Diamond kuupinga mfumokristo. Mfumokristo ndiyo lifeline yao! Mwenye kutaka kuingia hapo anatafuta ugomvi. Waislamu waliokwenda Diamond wako tayari kwa ugomvi huo kwa sababu hapo ndiko kwenye salama ya Tanzania ya sasa na ya baadaye. Tutaitwa magaidi, wachochezi, mujahidina, siasa kali n.k., lakini hatuaacha kusema dhidi ya mfumokristo kwa sababu hii ni haki yetu ya kikatiba ya kutoa maoni yetu na pia haki yetu ya kibinaadamu na ya kiungwana ya kujaribu kuiepusha nchi yetu na machafuko. Maneno ya waliokwenda Damond Jubilee hayatofautiani na yale ya Shahid Malcom X aliyepigania haki za watu weusi huko Marekani. Wakati anatafakari hali yake na watu Weusi wenzake kama wahanga wa mfumo wa ubaguzi ulikuwepo kule aliposema: Im one of 22 million black people who are the victims of Americanism. I see America through the eyes of a victim. I do not see American dream, I see American nightmare. Kuhusu nini cha kufanya ili kujikomboa na hali ya Weusi wa Marekani Malcom X alipinga kuwakumbatia wabaguzi na kuwashauri Weusi wenzake hivi: . Everything, anything that you beg other men to set you free you will never be free. Freedom is something that you have to do for yourself. And until the American Negro let the white men know that we are real ready and willing to pay the price necessary for freedom our people will always be walking around here second class citizen which we call 20 century slaves.. The price of freedom is death! Wa i s l a m u w a l i o k w e n d a Diamond Jubilee wanaamini kuwa Waislamu wa nchi hii wanadhulumiwa, wanabaguliwa na kunyimwa haki zao za msingi. Wanaamini kuwa inawabidi kufanya juhudi kubwa na kujitolea muhanga kama walivyofanya kuzunguka nchi nzima kulieza jambo hili, ndio watapata haki zao. Tunatoa mwito kwa Watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi yao tuungane kuuondoa mfumo unaoendeleza ubaguzi na dhulma nchini.

Obama alivyovuruga haki za binadamu, utawala wa sheria Marekani


Na Paul Craig Roberts Mei 9, 2013 - Mtandao wa kupashana habari Rais mpya wa Venezuela, Nicolas Maduro, ana mtazamo unaofanana na Chavez. Hapo Mei 4, alimwita Rais Obama wa Marekani mangi mkuu wa majini. Obama, ambaye ameisaliti demokrasia nchini Marekani, akipania kuuawa kwa wananchi wa Marekani bila kupitia mkondo wa sheria na bila kuidhinishwa na Bunge, alisababisha alichosema Maduro kwa kudai kuwa serikali mpya ya Maduro iliyochaguliwa inawezekana ilichaguliwa kwa udanganyifu. Ni wazi kuwa Obama hana raha kutokana na mamilioni ya dola za Marekani ambazo utawala wake ulitumia kuwezesha kuchaguliwa kibaraka wa Marekani badala ya Maduro, kushindwa. Kama kuna mtu ameisoma Marekani vyema, ni wa-Venezuela. Nani atakayemsahau Chavez akiwa amesimama katika jukwaa la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York akimzungumzia George W. Bush? Kunukuu kutoka kumbukumbu: Hapa tulipo, jana, katika jukwaa hili hili alisimama Shetani mwenyewe, akizungumza kana kwamba dunia ni mali yake. Bado unaweza kuisikia harufu ya sulphur. Mbabe Marekani alitupa pesa nyingi katika uchaguzi uliopita wa Venezuela, akifanya aliloweza kuwasilisha utawala wa nchi hiyo kwa kibaraka wa Marekani aitwaye Henrique Caprilles, kwa maoni yangu msaliti kwa Venezuela. Kwanini huyu kibaraka wa Marekani asikamatwe kwa uhaini? Kwanini mawakala wa Marekani wanaohujumu nchi huru - balozi wa Marekani, washauri, maosa wa USAID/CIA, mashirika yasiyo ya kiserikali yanayopata fedha kutoka Marekani wasitakiwe kuondoka Venezuela haraka au wakamatwe na kukishwa mahakamani kwa ujasusi na uhaini mkuu? Kwanini kuruhusu uwepo wowote wa Marekani nchini Venezuela wakati ni wazi kuwa nia ya Marekani ni kuigeuza Venezuela nchi kibaraka kama Uingereza, Ujerumani, Canada, Australia, Uturuki, Japan na nyingine. Kulikuwa na wakati, kama ule wa Allende na Pinochet, ambako wapenda maendeleo wa Marekani na vyombo vya habari vilivyopotea vya ukosoaji wangekuwa wanaichachafya Marekani kwa uingiliaji usio halali wa mambo ya nchi huru. Sivyo tena. Kama mwandishi Jeffrey St. Clair wa gazeti la CounterPunch alivyoweka wazi hivi karibuni, wapenda maendeleo wa Marekani bado hawana hisia halisi ya utovu wa kimaadili na kikatiba wa uhalifu unaofanywa na championi wao - rais wa kwanza mweusi, au nusumweusi, wa Marekani - kumwacha Rand Paul (mjumbe mwandamizi wa Baraza la Wawakilishi) atoe pingamizi rasmi dhidi ya operesheni za kibabe za Marekani dhidi ya mataifa huru. Dhidi ya vitendo vya ugaidi wa kimataifa na wa ndani wa serikali ya Obama, wataalamu wa mageuzi kuanzia wanademokrasia hadi roboti wa Moveon.org hawainui pingamizi zozote na hawafanyi maandamano. St. Clair ameandika makala yenye nguvu, Isome kwa wakati wako: http://www. counterpunch.org/2013/05/03/thegame-of-drones/print Nadhani wapenda maendeleo wa Marekani walipoteza hamasa wakati Urusi ilipoanguka na wakomunisti wa China na India wakageukia ubepari. Kila mtu aliisoma vibaya hali hiyo, hasa wapumbavu wa mwisho wa historia (dhana ya Prof. Francis Fukuyama, kuwa mjadala wa kihistoria umekwisha na ubepari, demokrasia vimeshinda). Matokeo yake ni kuwa na dunia isiyo na upinzani mkali dhidi ya vitendo vya Marekani na nchi vibaraka wake vya uhalifu wa kivita, mauaji, kuharibiwa kwa uhuru wa raia na haki za binadamu, na propaganda za wazi za uwongo: Jana usiku majeshi ya Poland yalivuka mpaka na kuishambulia Ujerumani, ndivyo alivyowahi kusema Adolf Hitler. Madai ya Marekani ya silaha za maangamizi ni uwongo wa wazi zaidi ya huo. Lakini hakuna anayejali. Serikali za nchi za Magharibi na Japan zimelipwa na kununuliwa, na zile ambazo hazijanunuliwa zinaomba kununuliwa kwa sababu nao pia wanahitaji fedha hizo. Ukweli, uadilifu, haya yote ni maneno yasiyo na uhai. Hakuna tena anayefahamu yana maana gani. Zezeta George W. Bush alisema, katika kujikanganya mfano wa Animal Farm ya George Orwell, wanatuchukia kwa uhuru wetu na demokrasia. Hawatuchukii kwa sababu tunawapiga mabomu, tunawavamia, tunawaua, tunaua mfumo wao wa maisha, utamaduni, na miundombinu. Wanatuchukia kwa sababu sisi ni wema sana. Hivi mtu awe mpumbavu kuasi gani aweze kuamini mkorogo huu? Marekani na Israel zinaleta katika dunia uovu usiofichika. Sihitaji kusimama katika jukwaa la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa baada ya Bush au Obama. Napata harufu ya maovu ya Washington nikiwa kilomita 1000 kutoka hapo, hapa Florida. Jeffrey St. Clair anapata harufu hiyo akiwa katikati ya Marekani huko Oregon, Nicolas Maduro anapata harufu hiyo nchini Venezuela. Evo Morales anaisikia harufu hiyo nchini Bolivia ambako aliwafukuza maofisa wa USAID waliojaziwa majasusi wa CIA. Putin anasikia harufu hiyo Russia, licha ya kuwa bado anaruhusu wahaini wa upinzani wa Russia unaofadhiliwa na fedha za Marekani kuiwekea vikwazo serikali ya Russia. Wa-Irani wanapata harufu hiyo katika Ghuba ya Uajemi, Wa-China wanaipata kutoka mbali, jijini Beijing. Idara ya Usalama wa Ndani, inayofanana na Gestapo, polisi wa siri wa Hitler, ina wanaofuatilia hatari kusaidia kudanganya wananchi katika operesheni zake za kuigiza. Soma: http://www. governamerica.com/black-ops/ boston-bombings/110-fema-hiringactors-to-run-live-terror-drills Utawala wa Obama una droni

Makala

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

Mwandishi Ibn e Abdul Haq anakamilisha uchambuzi wa ushahidi wa mashirika ya upepelezi ya Marekani kuhusu kuhusika kwa Waislamu, na Al Qaeda, katika shambulio la Septemba 11 mwaka 2001 nchini humo. 7 . Wa s h i r i k a w a A l Q a e d a walikamatwa katika video za usalama katika uwanja wa ndege? Mojawapo ya ushahidi kwa madai kuwa washirika wa Al Qaeda walikuwa katika ndege hizo ni fremu za picha za mikanda ya video, zinazosemekana zilichukuliwa na camera za usalama zinazodaiwa kuonyesha watekaji waliingia katika viwanja vya ndege (ndege hizo zilikotokea). Muda mfupi baada ya mashambulio, kwa mfano picha zinazomwonyesha Mohamed al-Atta na al-Omari katika uwanja wa ndege zilizungushwa duniani kote. Hata hivyo, ingawa ilikuwa inadhaniwa kuwa picha hizo zilipigwakatika uwanja wa ndege wa Boston, ukweli ni kuwa zilipigwa katika uwanja wa ndege wa Portland. Hakuna picha zinazomwonyesha Atta au mwingine kati ya wanaodaiwa kuteka nyara ndege katika uwanja wa ndege wa Logan mjini Boston ziliwahi kutolewa. Sana sana tuna ushahidi wa picha kuwa Atta na al-Omari walikuwa katika uwanja wa ndege wa Portland. Hivyo, uthibitisho wa video kuwa watekaji hao waliingia viwanja vya ndege siku hiyo 9/11 haupo. 8. Majina ya watekaji yalikuwa katika orodha ya abiria? Je, nini kuhusu orodha za walioingia katika ndege, ambazo zinaweka majina ya abiria wote? Kama wanaodaiwa ni watekaji walinunua tiketi na kuingia

Je, Waislamu waliishambulia Marekani Septemba 11 2001?


kwenye ndege, majina yao yangeonekana katika orodha ya abiria wa ndege hizo. Orodha za abiria ambazo zilitolewa katika vyombo vya habari hazikuwa na majina 19 ya wanaodaiwa waliteka nyara ndege hizo, na hata majina ya watu wa Mashariki ya Kati hayakuwepo kabisa. Orodha hizi, kwa hiyo, zinatoa ishara kuwa hapakuwa na watekaji wa al Qaeda katika ndege hizo. 9. Vipimo vya DNA (vinasaba) vilionyesha watekaji watano kati ya waliokufa katika shambulio la Pentagon? Kama ndege ya Boeing 757 ingekuwa inasari katika mwendo wa maili 500 kwa saa ikiwa ardhini, ingeharibu sana majani na ardhi inapopita, ikiwa ni pamoja na kusababisha mashimo kutokana na mikwaruzo ya injini zinazoninginia, lakini picha zilizochukuliwa mara baada ya athari hiyo kudaiwa kutokea inaonyesha hali ya majani kuwa ni nzuri bila doa. Malundo ya mabaki yalianza kuonekana baadaye na huenda ilishushwa kutoka dege la mizigo la C-130 ambalo lilionekana likizunguka jengo hilo. Isitoshe, kutokuwepo kwa uonyeshaji halisi wa wanaodaiwa kuteka nyara katika vipimo vya DNA kunashabihiana na taarifa ya uchunguzi wa maiti, ambayo ilitolewa kwa Dk. Thomas Olmsted, ambaye alipeleka maombi ya taarifa hiyo kwa idara ya serikali ya Marekani ya usari wa ndani wa ndege. Kama ilivyokuwa kwa orodha ya abiria ya Safari namba 77, alichua, taarifa hii pia haina majina ya Kiarabu. 10. Madai kuwa baadhi ya wanaodaiwa kuteka ndege bado wako hai imekanushwa? Tatizo jingine la madai kuwa watekaji 19 walikuwa wametambuliwa mnamo Septemba 11, au tuseme siku chache baadaye, ni kuwa baadhi yao walionekana katika orodha ya mwisho ya FBI walionekana hao baada ya 9/11. Mnamo Septemba 22, 2001, shirika la utangazaji la BBC lilichapisha makala ya David Bamford yenye kichwa Mtuhuhiwa utekaji nyara yuko salama Morocco. Ilimwonyesha Waleed alSehiri aliyetajwa na FBI kama mmoja wa wateka nyara akiwa mzima. Kesho yake BBC ikachapisha makala nyingine, Watuhumiwa utekaji nyara wako hai na salama. 11. Bin Laden na Al Qaeda wangeweza kufanikisha mashambulio hayo? Ili waendesha mashitaka wadhihirishe kuwa washitakiwa wametenda jinai,, inabidi waonyeshe kuwa walikuwa na uwezo (pamoja na nia ya nafasi) ya kufanya hivyo. Lakini wataalamu kadhaa wa masuala ya kisiasa na kijeshi wa nchi nyingine wamesema kuwa Bin Laden na Al Qaeda kwa vyovyote wasingeweza kuendesha mashambulio hayo. Jenerali Leonid Ivashov, ambaye mwaka 2001 alikuwa Mkuu wa Majeshi ya Russia aliandika: Ni mashirika ya kijasusi pekee na wakuu wake wa sasa au waliostaafu ambao bado wana ushawishi katika taasisi za dola wana uwezo wa kupanga, kuratibisha na kutekeleza mpango wa aina hiyo.. Osama bin Laden na al Qaeda hawawezi kuwa watayarishaji au watekelezaji wa mashambulio ya 9/11. Hawana uwezo wa mipango, raslimali au viongozi wanaohitajika. Mohammed Hassanien Heikal, aliyekuwa zamani Waziri wa Mambo ya Jje wa Misri, aliandika: Bin Laden hana uwezo wa operesheni ya kiwango hiki. Ninapomsikia Bush akizungumza kuhusu Al Qaeda kana kwamba ni Ujerumani ya kifashisti au chama cha Kikomunisti cha Urusi, nacheka kwa sababu najua kilichopo. Maelezo kama hayo yametolewa pia na Andreas van Bulow, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi nchini Ujerumani, Jenerali Mirza Aslam Beg, aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Pakistan, na hata Jenerali Musharraf, rais wa Pakistan hadi hivi karibuni. 12. Jengo la WTC 7 : Bunduki inayotoa moshi ya 9/11 Kwa vile jengo la WTC 7 (lingine katika kituo cha kimataifa cha biashara) haikugongwa na ndege, kuanguka kwake kwa kasi ya kutokuwa na kizuizi, ambako kulitanguliwa na milipuko na kuyeyushwa chuma, lilikuwa mfano wa wazi wa kuangusha jengo kwa mpangilio. Kwa mfano , Jack Keller, profesa mstaafu wa uhandisi katika Chuo Kikuu cha Utah, ambaye amepewa wajibu maalum na jarida la Scientic American, alisema: Ni wazi ilitokana na uangushaji jengo kwa mpangilio. Pia, Danny Jowenko, mtaalamu wa uangushaji majengo kwa mpangilio alipotakiwa kuzungumzia video ya kuanguka kwa jengo hilo alisema: Walilipua tu mihimili na yaliyosalia yaliachia punde. . Ni mlipuko wa ndani. Kundi la wataalamu lilifanya hivyo. Uteketezaji wa jengo namba 7 la kituo cha kimataifa cha biashara ilikuwa

ambazo inazitumia kuwanyamazisha raia wa Marekani bila kupitia mkondo wa sheria. Soma: http://www.salem-news.com/ articles/may042013/drones-bostonwh.php Idara ya Usalama wa Ndani ina risasi zaidi ya bilioni moja, vifaru, kikosi maalum cha kijeshi. Kambi za wafungwa zimejengwa. Bunge la Marekani lina fedha za walipakodi kuilipa FBI (Shirika la Upelelezi) kuwabambika wasio na hatia na kuwapeleka jela. Hii ndiyo nchi ambayo Marekani imekuwa. Haya ndiyo mashirika ya usalama iliyo nayo, ikijaza mifuko yao kwa kuteketeza maisha ya wasio na hatia na wanyonge. In God we trust (Katika Mungu tunatumaini) ndiyo nembo ya serikali ya Marekani. Ingefaa isomeke: In Satan we follow. (Katika Shetani tunafuata). (Paul Craig Roberts alikuwa Naibu Waziri wa Fedha na Sera za Uchumi na Mhariri mshiriki wa jarida la Wall Street Journal. Amekuwa mwanasafu wa jarida la kiuchumi la Business Week, mtandao wa habari wa Scripps Howard. na Creators Syndicate (jukwaa la waandishi). Amekuwa na miito mingi kufundisha katika vyuo vikuu, Makala zake katika mtandao zimewavutia wasomaji kote duniani. Kitabu chake kipya Kushindwa kwa ubepari usio na mpaka na kuyeyuka kiuchumi kwa ukanda wa Magharibi (The Failure of Laissez-Faire Capitalism and Economic Dissolution of the West) sasa kinapatikana. Mfasiri kwa Kiswahili Anil Kija)

lazima ni kazi ya ndani. Hitimisho: Baada ya muongo mmoja wa vita vilivyoanzishwa kwa madai ya uwongo kukaribia kumalizika nchini Afghanistan, kuanzia 2014, suala la nani aliyefaidika na 9/11 halipo tena mashakani. Katika miaka 12 iliyopita, dunia imeona faida kubwa waliyopata Marekani, Ulaya Magharibi na Israel kisiasa, kidiplomasia, udhibiti wa maeneo na uchumi kutokana na vita hivyo. Afghanistan, Irak na majirani zao wa Kiislamu, kwa upande mwingine, wamekuwa waathirika wa utumiaji nguvu, umwagaji damu na uharamia uliofanywa na Marekani na washirika wake wa NATO. Mfumo wa kijeshi wa nchi za Magharibi umekuwa ukikanyaga kila mahali duniani miguu yake ikiwa na madoa ya damu ya mamilioni ya Waislamu wasio na hatia. Maelezo rasmi na ushahidi wote uliotoa kuwa Marekani ilishambuliwa na Waislamu mnano Septemba 11, yakiangaliwa kwa undani, yanaelekea kuwa yametengenezwa. Kama hilo litathibitishwa, matokeo yake yatakuwa ya kutisha. Kuwagundua na kuwapeleka mahakamani wahusika halisi wa mashambulio ya Septemba 11 bila shaka kungekuwa na umuhimu mkubwa. Uhakika wa watu katika uadilifu na usahihi kisiasa wa nchi za Magharibi ungeporomoka. Matokeo ya kwanza, hata hivyo, ingekuwa kugeuza mielekeo na sera zilizojengwa juu ya mtazamo kuwa Marekani ilishambuliwa na Waislamu hapo Septemba 11.

10

Sie ni hadithi ya mtoto kulilia wembe Huenda nasi tunataka tuletewe droni Tutafakari ya Umar Farouk Mutallab
Na Omar Msangi

Bomu Arusha kufungua mlango wa Al Shabaab


kwa hiyo, matukio mengi ya kigaidi yamekuwa ya kubuni na kutengenezwa ili ipatikane sababu. Makachero, wasomi, wanasayansi, watati wataalamu mbalimbali, kwa muda sasa wamekuwa wakiandika na kuhoji maswali mengi pamoja na kuchua siri zilizojicha katika matukio yaliyotikisa ulimwengu yakidaiwa kuwa ni ugaidi uliofanywa na kundi hili au lile. Matukio hayo ni pamoja na lile mashuhuri Septemba 11, Anthrax Terror Attack, Bali, London Bombing, kulipuliwa Balozi za Marekani Dar es Salaam na Nairobi, mgogoro wa Libya na huu wa Syria hivi sasa n.k. Kwa upande wa Al Shabab tatizo linafahamika kuwa ni Wasomali wasiotaka kuona nchi yao ikitawaliwa na watu wa nje au watu vibaraka wanaotumiwa na mabeberu. Al shabab ni matokeo ya hatua ya Marekani na Ethiopia kushirikiana kungoa utawala wa Umoja wa Mahakama za Kiislamu uliokuwa umeiletea amani Somalia baada ya miaka zaidi ya 15 ya vita na uharamia wa wenyewe kwa wenyewe. Waliongolewa madarakani wakashika silaha kupambana na serikali waliyoiita ya kisaliti. Kama itatokea kuwa na uadui na watu wa nje, basi itakuwa ni wale wanaoshiriki vita ndani ya nchi yao. Lakini sasa suala linageuzwa kuwa hao ni kundi la kigaidi, ni wenzao Alqaida wanaofanya vitendo vya kigaidi Afrika Mashariki. Na kwa maana hiyo, tunalazimishwa kuamini kuwa ni maadui wa Kenya, Uganda, Tanzania na eneo lote la Afrika Mashariki na Kati. Mambo haya yanakwenda hatua kwa hatua. Kwanza unapigwa propaganda ukubali kuwa kuna gaidi anakuvizia na ashaingia nyumbani kwako. Propaganda hiyo inaonekana ishakolea Tanzania. Hatua ya pili, ni kukuthibitishia kuwa kweli adui sasa yupo na ni hatari kweli. Likitokea tukio kama lile la kuuliwa Padiri Mushi kule Zanzibar au hili la Arusha, hata kama lina chanzo na malengo tofauti, laweza kutumika kulazimisha kuwa waliohusika ni Al Shabab au Al Qaidah. Hilo likishafanikiwa, kinachofuatia sasa ni kupewa msaada wa kupambana na magaidi. Utathibitishiwa uwepo wa FBI/CIA, Marines na droni. Lakini ukifikishwa hapo, basi ujue pamoja na msaada huo na mwingine utakaopewa wa kitaalamu, vifaa, mafunzo na fedha, hupo salama tena. Matukio ya kutisha kama la Arusha yataendelea kuwepo ili kudumisha kitisho na hivyo kuhalalisha uwepo wa walinzi wako wa usalama kutoka nje. Hii ndiyo hali inayoikuta Pakistan, Yemen, Afghanistan, Iraq n.k. Ni kutokana na hali kama hii ndio nasema kuwa, itakuwa msiba iwapo tukio la Arusha litatumika kuwafungulia milango Ashabab na Alqaidah. Hakuna hata nchi moja duniani, iliyonasa katika mtego huu ambayo ipo salama. Hata hiyo Marekani yenyewe haipo salama kwa sababu ili kitisho cha ugaidi kiendelee kuwepo, ni lazima ziendelee kuwepo hizi Boston Marathon Bombing. Tukio la Arusha na jinsi Ubalozi wa Saudi Arabia ulivyoshughulika kutaka kujua uhakika wa kuhusishwa raia wa nchi hiyo, imeonyesha kuwa sio Serikali zote duniani ambazo hazijali watu wake. Serikali hiyo imesimama madhubuti kuona kuwa raia wake anatendewa haki na maadhali alikuwa hahusiki, ameachiwa. Katika kesi ya kulipuliwa Ubalozi wa Marekani, hatukuweza kufanya lolote kumtetea Ghailani wala kutaka kama ni kushitakiwa ashitakiwe katika ardhi ya Tanzania ambapo ndipo uhalifu ulifanyika. Matokeo yake ni kuwa taarifa tulizo nazo ni zile za kuambiwa. Tumeambiwa tumekubali, wala haikutushughulisha kuhoji ukweli wa madai kuwa Ahmed Khalfani Ghailani anahusika. Nyaraka muhimu ya mashitaka dhidi ya Ghailani inasema kuwa kijana huyo Mtanzania aliingiza vifaa vya kutengenezea bomu nchini. Kisha akakusanya watu wa kumsaidia wakatengeneza bomu likakamilika. Lilipokamilika, wakawa wanalihamisha kutoka nyumba moja hadi nyingine ili lisigundulike mpaka ilipoka siku ya kwenda kulipua. Mtu yoyote anayetumia akili yake japo kwa asimia moja tu, hawezi kukubali maelezo kama haya. Lazima atahoji, iliwezekanaje yote hayo kufanyika bila ya vyombo vya nchi kujua. Lakini tumekaa kimya, tunaona fahari kutangaza kuwa Mtanzania amehusika kulipua Ubalozi wa Marekani! Inakuwa kana kwamba tunaona fahari kutangaza kuwa Mtanzania ni gaidi. Katika ile kadhia ya siku ya Krismasi 25 Desemba, 2009, kijana wa ki-Nigeria, Umar Farouk Abdulbutallab, maarufu Underwear Bomber akisafiri katika ndege ya shirika la ndege la Northwest Airlines, Flight 253, kutoka Amsterdam kuelekea Detroit, Michigan, alidaiwa kujaribu kulipua ndege hiyo. Ikadaiwa kuwa kijana huyo alificha milipuko katika nguo yake ya ndani (chupi) na alipotaka kulipua ndege, ikamuunguza yeye mwenyewe. Kiasi wiki mbili zilizopita nililazimika kuacha kichupa changu kidogo cha manukato Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Dar es Salaam kilichokuwa katika begi kwa sababu kiligunduliwa na machine za ukaguzi. Sheria za sasa za usalama katika viwanja vya ndege, haziruhusu abiria kuingia katika ndege na chupa ya paumu, hata na chupa ya maji ya kunywa. Nimewahi kusari na ndege za Mashirika ya Kimarekani, ndani na nje ya Marekani ikiwemo hii Northwest Airlines kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Schiphol, Amsterdam kwenda Washington (baada ya Septemba 11), kwa hiyo najua ni kiasi gani cha upekuzi unaofanyika na hasa ukiwa Muislamu au Muarabu. Leo inaposemwa kuwa Muislamu, Mweusi kutoka Nigeria kaingia katika ndege ya abiria na milipuko bila kutambulika, ni jambo linalozua maswali mengi sana na utata mwingi. Lakini ukiacha hilo, wapo wasafiri mtu na mkewe, Kurt Haskell na Lori Haskell ambao nao walikuwa wakisari katika ndege aliyopanda Umar. Wao wanasema walipokuwa katika sehemu ya maosa wa Uhamiaji na ukaguzi wa mwisho kabla ya kuingia katika ndege, walishuhuduia mtu mmoja akimpitisha Umar Farouk bila kupitia hatua za kawaida za ukaguzi. Wanahoji, ni nani yule mtu, Smartly dressed man, aliyempitisha Umar Farouk Abdumutallah uwanja wa ndege wa Schiphol, Amsterdam, Uholanzi bila ya kupitia taratibu za kawaida za kiusalama katika viwanja ya ndege? Hoja yao ni kuwa mtu yule aliyempitisha akipatikana itajulikana Umar ni nani na kwa nini alipitishwa bila kupekuliwa. Na kwamba inavyoonekana wanausalama katika uwanja wa ndege walikuwa wamearifiwa juu ya kupita kwake. Kurt na Lori walijitahidi sana kuita vyombo vya habari kueleza tukio hilo, lakini habari hizo zikawa zinafukiwa. Kinyume chake TV na magazeti yakakazana kuelezea kuwa Umar alipokuwa chuoni alikuwa kiongozi wa vijana wa Kiislamu. Alikuwa akianza siku yake kwa swala ya Subhi, kisha kusoma

Makala

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

Kuna wasiwasi na uwezekano mkubwa kwamba huenda tukio la bomu Kanisani Arusha, likatumika kujenga hoja kuwa sasa Tanzania inakabiliwa na kitisho cha ugaidi wa Al Shabab, Al Qaidah na magaidi wengine. Na hilo likifanyika, utakuwa ni msiba kwa taifa, lakini kwa wakati mwingine kuwa mafanikio makubwa kwa wale ambao kwa muda mrefu sasa walikuwa wakionyesha hamu ya kuona nchi hii kuwa nayo inasajiliwa kuwa na magaidi. Na hilo likitimia, itahalalisha uwepo wa kudumu wa FBI/CIA na hata vikosi vya kijeshi na droni. Kauli ya hivi karibuni ya Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Saidi Mwema kwamba katika kuchunguza tukio la Arusha wanashirikiana na makachero wa Kenya kwa sababu wao wana uzoefu wa mambo haya, yaweza kwa upande mmoja isiwe na tatizo. Kwa maana kuwa ikaonekana ni kauli ya kuonyesha tu kusaidiana majirani katika shida kama hii. Hata hivyo, kutokana na kauli za wanasiasa huko nyuma na hata vyombo vya usalama ambazo zimekuwa zikionyesha wazi kuwa kulikuwa na hamu ya kutangaza kuwa tuna ugaidi wa Al Shabab na Al Qaidah, huenda kuwepo k w a m a k a c h e r o wa Kenya kukakamilisha azma hiyo. Wasiwasi ni kwamba iwapo makachero hao watasema kuwa bomu la Arusha linafanana na yale yaliyokuwa yakilipuliwa Kenya ambayo yalidaiwa kuwa ni ya Al Shabab, basi hiyo itatosha kutangaza kuingia kwa Al Shabab Tanzania na mengine kufuatia. Wasiwasi huu unapata nguvu zaidi kwa sababu ni kiasi wiki mbili tu zilizopita, Polisi wetu walisema kuwa wana taarifa za ki-intelijinsia zinazoonyesha kuwa Tanzania inakabiliwa na kitisho cha ugaidi wa al Shabab na al Qaidah. Hoja hapa sio kuwa vyombo vyetu vya usalama visifanye kazi na kutekeleza wajibu wao kutizama kuwa nchini kuna vikundi vyovyote vya kigaidi na kuchukua hatua. Lakini ukiacha propaganda, ukweli uliokwisha dhihirika mpaka sasa ni kuwa kinachoitwa vita dhidi ya ugaidi imekuwa kama mkakati na mipango ya mabeberu ya kutimiza malengo yao katika nchi mbalimbali duniani. Na

Quran hadi wakati wa kwenda darasani. Wakasema pia kuwa Umar alikuwa akitumia kumi la mwisho la mwezi mtukufu wa Ramadhani kukaa Itiqaaf Msikitini na kwamba alikuwa akiwapa nasaha vijana wenzake wasiwe na mahusiano na wasichana ya uboy na girl friends, labda kama ni kutaka uchumba. Kwamba madai haya juu ya Uislamu wa Umar ni sahihi au ya uwongo, sio muhimu. Muhimu hapa ni mambo mawili. Moja ni hilo la kuunganisha Uislamu na ugaidi. Na pili, jinsi watu walivyopumbazwa na kuathiriwa katika kukiri kwao kiasi kwamba hawataki tena kujua ukweli. Wanachoshikilia ni propaganda wanayopewa na makachero wa Serikali. Hawana haja ya kuwasikiliza akina Kurt Haskell walioshuhudia tukio. Watu wamepumbazwa kwa propaganda hawaoni, hawahoji wala hawasikii. Mwaka 2005 liliwahi kuandika gazeti moja katika ukurasa wake wa mbele kuwa Waislamu walikuwa wameingiza majambia, mapanga na silaha nyingine kwa ajili ya kupambana na Wakristo. Likasema kuwa silaha hizo zilikuwa zimehifadhiwa katika Misikiti Dar es Salaam na Morogoro. Taarifa kama hizi ambazo zimekuwa zikirejewa kwa namna tofauti tofauti, hazikuwahi kukanushwa wala kukemewa na Serikali hata mara moja. Wakati ule baada ya kuona kuwa Serikali imekaa kimya, gazeti la An nuur liliandika likihoji kuwa mchezo kama huo ukiachwa, je, jamii haioni kuwa kama itatokea tu vurugu, au akatokea kichaa mmoja kupiga mtu jiwe kanisani au kutia moto Kanisa, hatuoni kuwa Wakristo watakimbilia kusema kuwa ni Waislamu kwa sababu walishaambiwa kuwa wameandaa silaha? Mantiki ya hoja ya An nuur ilikuwa kwamba kama madai yale yalikuwa ni kweli, basi wahusika wakamatwe wakishwe mahakamani. Lakini kama ilikuwa ni mambo ya kuzua, yakemewe, yasiachwe yakaathiri ufahamu, uelewa na uoni wa watu wetu. Hilo halikufanyika. Hivi watu waliopiga propaganda chafu kama hizi, wanashindwa kupanga tukio ili kutaka kuthibitisha madai yao? Na hata wakishindwa kupanga na kutekeleza, hivi likitokea tukio lolote la kihalifu kama ilivyotokea Zanzibar au hili la bomu Arusha (na hata kilichodaiwa kuwa ni kuchomwa makanisa Mbagala katika maandamano), watashindwa kutumia tukio hilo kupiga propaganda kujenga uwongo kuwa wahusika ni wale walioingiza majambia mwaka 2005?

11

Mwaka wa 65 wa Ufedhuli wa Israel


Na Saeb Erekat Kila mwaka tarehe 15 Mei, taifa la Palestina linaadhimisha janga lililoikumba mwaka 1948. Mnamo mwaka huo Wapalestina walilazimishwa kwa mtutu wa bunduki kuiacha nchi yao na kuelekea ukimbizoni. Nchi ya Palestina ikafutwa katika ramani ya dunia. Takriban vijiji 418 viliteketezwa na asilimia 70 ya watu wetu wakawa wakimbizi. Tangu wakati huo imepita miaka 65, tumekuwa tunaishi maisha ya kuhangaika na kudhalilishwa tukiwa ndani na nje ya nchi yetu. Leo tunaendelea kudai haki ya Wapalestina wote ulimwenguni, haki ya kuirudisha nchi yetu katika ramani, na haki yetu ya kurudi nchini mwetu kwa mujibu wa sheria ya kimataifa. Leo tukiadhimisha siku hii ya Janga la 1948, kila Mpalestina popote alipo anaendelea kusononeka na kudhalilika, kitu ambacho kinapaswa kiwe ni aibu kwa ulimwengu mzima. Hii ni kwa sababu, baada ya miaka yote hii pamoja na maazimio kemkem kupitishwa yakidai haki ya kimsingi ya Wapalestina, Israel inaendelea kupuuza kwa jeuri na ufedhuli. Kwa muda wa miaka 25 Wapalestina wamediriki hata kukubali (kwa shingo upande) kuitambua Israel na kukubali iendelee kuikalia asilimia 78 ya ardhi ya mababu zetu. Licha ya yote hayo Israel siyo tu imekataa kuitambua Dola ya Palestina, bali inaendelea kupanua himaya yake kwa kuvamia ardhi yetu tunamoishi. Israel inafanya uvamizi huu kinyume cha sheria ya kimataifa wakati ikifaidika kwa kuwa na uhusiano wa kirafiki na nchi nyingi ulimwenguni. Mwaka 1949, Umoja wa Mataifa (UN) ulikubali kuiruhusu Israel iwe mwanachama wa UN kwa masharti mawili. Sharti la kwanza ni kuwa wakubaliane na azimio namba 181 la kuwa na mataifa mawili ya Israel na Palestina. Sharti la pili ni kukubaliana na azimio 194 la kuwaruhusu Wapalestina wakimbizi wote kurudi kwao walikofukuzwa. Inasikitisha kuwa hata azimio moja kati ya haya mawili halijatekelezwa. Si hayo tu, bali miaka 65 baada ya Nakba, Israel inakataa kuungama dhulma ilizotenda mnamo 1948. Kibaya zaidi ni kuwa Israel imeunda sheria inayokataza Wa p a l e s t i n a w a l i o r a i a wa Israel kuadhimisha siku ya Nakba. Ukweli ni kuwa hakuna sheria inayoweza kufuta ukweli wa Nakba. Kukataa kuwaruhusu wakimbizi warudi kwao hakumaanishi kuwa wakimbizi hawatakuwepo. Kitakachofanyika ni kuwa upatikanaji wa suluhu na amani ya kudumu utazidi kuwa mgumu Ndio maana leo Nakba inaendelea kukumbukwa miongoni mwa Wapalestina milioni 11 kote duniani. Mfano mmoja ni wakimbizi wa Kipalestina wanaoishi Iraq na Syria, ambao wanateseka kutokana na vurugu za wenyewe kwa wenyewe ambazo haziwahusu. Katika hali kama hii ni muhimu sana kwa ulimwengu kuingilia kati na kuhakikisha kuwa wakimbizi hao wanarudi nchini mwao, kwani usalama wa maisha yao hauwezi kuhakikishwa bila ya haki yao ya kurudi Palestina. Ili kuhakikisha kuwa amani inapatikana, tumejitahidi sana kugeuza msimamo wetu. Ndio maana tumekubaliana na mpango wa amani uliopendekezwa na nchi za Kiarabu, tukakubali kuishi kwa amani na Israel. Tunachodai ni kuwa Israel ituachilie ardhi iliyovamia na kuikalia tangu mwaka 1967 pamoja na kuwaruhusu wakimbizi warudi makwao kwa mujibu wa azimio 194. Kwa bahati mbaya, tunakabiliwa na mvamizi asiyetaka amani, tunakabiliwa na utawala wenye msimamo mkali unaowaunga mkono na kuwawakilisha walowezi

Janga la Palestina (Al Nakba)


wanaokalia ardhi yetu waliyoivamia mwaka 1967. Hii ni serikali ambayo inakataa fursa ya kuishi kwa amani na badala yake inangangania ardhi yetu. Hii ni serikali ambayo mawaziri wake wanakataa katu katu kuitambua Dola ya Palestina na kutangaza azma ya kuongeza walowezi wa Kiyahudi hadi kukia milioni moja katika ardhi iliyovamiwa. Ndio maana kuna umuhimu wa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Bw John Kerry. Baada ya miaka 65 ya Nakba, ulimwengu unapaswa sasa useme kwa nguvu zake zote Imetosha! badala ya kuendelea kutoa maneno matupu bila ya vitendo. Wa k a t i u m e f i k a s a s a kusahihisha makosa ya kihistoria, kwa kuruhusu Palestina irudi katika ramani ya dunia, ikiwa taifa huru na linalojitegemea, linaloishi jirani na Israel kwa amani na maelewano, ili kutimiza haki za kimsingi za kila Mpalestina popote alipo. Ili kuhakikisha kuwa malengo haya yanatekelezwa, ni lazima ulimwengu uachane na mbinu zilizoshindwa na kusahauliwa. Kusema kuwa mazungumzo ya amani yafanyike bila ya kuwa na hadidu rejea na bila ya kuilazimisha Israel itekeleze majukumu yake kama tulivyokubaliana, ni sawa na kuendelea na mazungumzo kwa

Makala/Tangazo

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

AN-NUUR

miaka 20 ijayo, wakati Israel inaendelea na uvamizi wa ardhi bila ya kikwazo. Mwishowe mazungumzo hayatafanikiwa na hakutakuwa na amani tunayotarajia. Tumemaliza zaidi ya nusu karne. Hii ni mara ya kwanza tunaadhimisha Nakba wakati Palestina imetambuliwa kama Dola katika Umoja wa Mataifa. Ingawa tungali tuko chini ya ukoloni wa Israel, tumechukua hatua thabiti kuelekea tunakokusudia. Tutaendelea kuelekea huko ili kushinda haki yetu ya kimsingi kama taifa. Ni lazima tukomeshe miaka 65 ya ufedhuli wa Israel. Ulimwengu hauwezi kuendelea kuadhimisha siku kama hii bila ya kuchukua hatua thabiti. Ni lazima Israel itanabahi kuwa kukataa kuwapa Wapalestina haki yao kutawagharimu sana. Kukubali kuishi kwa amani ni njia pekee waliyo nayo. Hawana njia nyingine. Bahati mbaya, jambo hili halijaingia katika akili za Waisrael na ndio maana wanaendelea kujidanganya. Saeb Erekat ni Mkuu wa Mazungumzo ya amani kwa niaba ya Chama cha Ukombozi cha Palestina (PLO). Contact us: P.O Box 20307, 612 UN Road Upanga West, Dar es Salaam Tel: 2152813, 2150643 Fax: 2153257 Email: pict@pal-tz.org Website: www. pal-tz.org

FAIR LAND DISTRIBUTION


NAFASI ZA KAZI Inawatangazia nafasi ya kazi upande wa wauzaji (Salesman) Sifa za muombaji Awe kijana wa kitanzania Awe na umri kati ya miaka 25-45 Awe tayari kuweka dhamana ya mali isiyohamishika Awe na wadhamini watatu ( 3) wenye ajira zinazotambulika kiserikali Awe na elimu siyochini ya kidato cha nne Awe na uzoefu wa kazi usiopungua miaka mitatu katika fani hiyo.

TANZANIA MUSLIM PROFESSIONAL ASSOCIATION


CAREER GUIDANCE KWA WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA JUMUIYA YA WATAALAMU WA KIISLAMU TANZANIA (TAMPRO) INAWAALIKA WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA KUHUDHURIA CAREER GUIDANCE JUU YA UOMBAJI WA UNDERGRADUATE SCHOLARSHIPS NJE YA NCHI. TAMPRO IMEPATA WAHISANI WA KUFADHILI MASOMO NGAZI YA SHAHADA YA KWANZA. SIKU: JUMAPILI, TAREHE 19/05/2013 MUDA: SAA 3:00 ASUBUHI 6:00 MCHANA MAHALI: TAMPRO MAKAO MAKUU, MAGOMENI, DAR ES SALAAM TAFADHALI UKIIPATA TAARIFA HII WAJULISHE WENGINE KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA: 0713 521147, 0764 024441, 0715 822332 AU EMAIL: suke75@yahoo.com, info@tampro.org SADIKI S. GOGO MKURUGENZI MTENDAJI

MAWASILIANO Zaidi: Piga Simu: 0789 272 737 Maombi yote yatumwe katika mtandano. Email: fairlandcom@yahoo.com Au kwa Barua S.L.P 4804- DSM MAOMBI YAAMBATANISHWE NA PASSPORT SIZE.

12

AN-NUUR
MAKALA

MAULID!!! MAULID!!!

Ni nasaha za Hay-atul Ulamaa


Na Mwandishi Wetu Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu (Hay-atul Ulamaa) umewataka Waislamu kuwa makini na kuchukua tahadhari kubwa katika kipindi hiki tete. Wametoa tamko hilo kufuatia tukio la Mei 5 la kurushwa bomu kanisani Arusha lililosababisha vifo vya watu watatu na wengi kujeruhiwa. Tunawataka Waislamu wote nchini kuwa watulivu na kamwe wasichokozeke na matamshi yanayotolewa na baadhi ya watu au baadhi ya vyombo vya habari ambavyo vina malengo yasiokuwa bayana. Imesema taarifa ya Hayatul Ulamaa iliyotolewa tarehe 7 May, na kusainiwa na Mwenyekiti wake Sheikh Sulaiman Amran Kilemile. Taarifa hiyo ya Hay-atul Ulamaa, imewataka Watanzania kwa ujumla wao kutolihusisha suala hili na taasisi, kikundi, dhehebu, dini na wala chama chochote na kuviacha vyombo husika vifanye uchunguzi wake na hatimae wahusika kukishwa katika vyombo vya kisheria. Kwa muktadha huo, wakavitaka vyombo hivyo kufanya shughuli zake bila kuathiriwa na misukumo yoyote ile ikiwa ni ya kisiasa, kidini au vinginevyo na kwamba viweke wazi matokeo ya uchunguzi wa tukio hili na yanayofanana na hili kama

Waislamu watakiwa kuchukua tahadhari


Nyote Mnakaribishwa

12

RAJAB 1434, IJUMAA MEI 17-23, 2013

Masjid Allah Karim Kazimzumbwi Kisarawe Inawaalika waislamu wote katika Maulid ya Mtume Muhammad (S.A.W) Kazimzumbwi Kisarawe, Tarehe 25/05/2013, siku ya Jumamosi Saa 2:30 Baada ya Swalatul Ishaa , Inshaalah. Wafadhili wa maulidi Hii ni. 1. Sheikh Juma Sadiki Muyenga 2. Mohamed Rak Nurmohamed Satya 3. Ndugu wa Familia ya Madenge

Balozi wa zamani wa utawala wa Kizayuni wa Israel nchini Ujerumani, Av i P r i m o r, a m e k i r i kwamba Shirika la Kijasusi la Israel MOSSAD, ndilo lililopanga na kutekeleza njama za kumuua Emad Mughniya, kamanda wa Hizbullah Februari mwaka 2008 mjini Damascus, Syria. Avi Primor ameyaeleza hayo kwenye mahojiano na televisheni moja nchini Ujerumani na kusisitiza kwamba, utawala wa Israel ndio uliotekeleza shambulio la kumuua kigaidi kamanda Mughniya. Hayo yanajitokeza katika hali ambayo utawala wa Kizayuni wa Israel mara zote umekuwa ukikanusha

Israel yakiri kumuua Kamanda wa Hizbullah


kumuua Mughniya au kuhusika katika kupanga njama za kutekeleza shambulio hilo la kigaidi. Waziri Mkuu wa utawala huo, Benjamin Netanyahu, amekuwa akiwataka viongozi wa utawala huo wasizungumze na vyombo vya habari vya Israel kuhusiana na suala hilo. Wakati hali ikiwa hivyo, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Nabil al Arabi, amekiri kushindwa jumuia hiyo kuulinda mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu na Israel. Al Arabi amesema jumuiya hiyo haina uwezo wala vifaa vya kuweza kuzuia jinai zinazotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel.

yale ya Zanzibar, ili kuondoa hisia zinazoweza kusababisha chuki na kudhaniana vibaya kati ya watu wa dini tofauti hapa nchini. Awali, Wanazuoni hao wametoa kauli ya kulani shambulizi hilo la kihalifu na ukatili. Hay-atul Ulamaa inachukua nafasi hii kulaani vikali kitendo hicho ambacho hakikubaliki kidini na kibinaadamu (na) tunatumia fursa hii kuwapa

pole wale wote walioathirika kwa njia moja au nyengine na tukio hilo na kuwaombea waliojeruhiwa wapate nafuu haraka ili waweze kuendelea na shughuli za kila siku za ujenzi wa Taifa. Imesema taarifa hiyo huku ikivitaka vyombo vya habari kuwa makini pale vinaporipoti matukio kama haya, bila kusindikizwa na mitazamo ya kiitikadi walizo nazo ili kuzuia uwezekano wa kusababisha kutokea machafuko hapa nchini.

Amesema hayo katika mkutano wa Jumuiya hiyo mjini Cairo, ambako pia ametaka kuanza kuchukuliwa hatua za kisiasa na kidiplomasia za kuulazimisha utawala wa Kizayuni kusimamisha hujuma zake dhidi ya Wapalestina. Baraza Kuu la Jumuiya ya Arab League lilihitimisha kikao chake hicho cha saa mili kujadili jinai za kila siku za Israel katika mji wa Quds Tukufu, bila kutoa tamko lolote rasmi juu ya suala hilo. Hayo yanajiri huku utawala wa Kizayuni wa Israel ukizidisha jinai za kila aina dhidi ya wananchi wa Palestina wasio na ulinzi wowote.

TEHRAN Chombo cha kutegua bomu baharini kilichotengenezwa na wataalamu wa Iran kimezinduliwa. Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Admeli Habibullah Sayyari, amezindua chombo hicho na amesema, Iran ni kati ya nchi chache duniani zenye uwezo wa kutegua na kuondoa mabomu baharini. Kamanda huyo amesema hayo wakati wa mazoezi ya kutegua mabomu baharini, yanayofanyika baharini kusini mwa Iran ambako mfumo huo umezinduliwa. Sayyari amesema Jeshi la Wanamaji la Iran linafuatilia kwa karibu

Iran yazindua chombo cha kutegua mabomu baharini

harakati za vikosi vya kigeni katika eneo la Ghuba ya Uajemi, ili kuhakikisha kuwa hakuna tishio lolote dhidi ya nchi hiyo. Amesema Jamhuri ya Kiislamu imethibitisha kuwa nchi za eneo hilo zinaweza kusimamia usalama wa eneo hilo bila kuwepo vikosi vya kigeni. Hivi karibuni Jeshi la Wanamaji la Iran lilianzisha mazoezi ya kutegua mabomu baharini Mashariki mwa Lango la Bahari la Hormuz na Ghuba ya Oman. Iran mara kwa mara imezihakikishia nchi za eneo hilo kuwa uwezo wake mkubwa wa kijeshi si tishio na kwamba lengo lake ni kujihami.

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

You might also like