Professional Documents
Culture Documents
PRESIDENTS OFFICE, THE STATE HOUSE, P.O. BOX 9120, DAR ES SALAAM.
Tanzania.
kifo cha mtumishi wa Chama chetu kwa miaka 14 hadi alipoomba kustaafu mwenyewe na kiongozi wa CCM kwa nafasi alizowahi kuzishikilia katika Baraza Kuu la Wazazi na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama chetu kwa miaka 10 kuanzia 1992. Aidha, kupitia kwako, nakuomba unifikishie salamu zangu za pole kwa viongozi, wanachama, makanda na wapenzi wa CCM ambao wameondokewa na mwenzao na ambaye wanajua fika pengo lake litakuwa gumu sana kuzibika. Nakuomba pia ufikishe pole zangu nyingi kwa wanafamilia ambao wameondokewa na mhimili wa familia. Wajulishe wanafamilia kuwa naungana nao katika kuomboleza, niko nao katika msiba huu mkubwa na pamoja nao namwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, aiweke pema roho ya Marehemu Salum Shomvi Tambalizeni. Amin. Imetolewa na: Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, DAR ES SALAAM.
14 Oktoba, 2013