Professional Documents
Culture Documents
M K O A WA R U K WA
S.L.P. 128,
SUMBAWANGA.
2. MAFUNZO
Ndugu Wanahabari,
Mafunzo kwa Watendaji wetu ambao watahusika na zoezi hili
tayari yamekwisha fanyika kama ifuatavyo: Mafunzo kwa ajili ya Mratibu wa Mkoa, Maafisa
Waandikishaji na Maafisa Waandikishaji wasaidizi ngazi ya
jimbo yalifanyika tarehe 27 28/04/2015 yakifuatiwa na
Mafunzo ya Maafisa waandikishaji ngazi ya Kata
yaliyofanyika tarehe 18 19/05/2015 kwa Halmashauri zote
na mwisho Mafunzo ya BVR Opereta na Waandishi Wasaidizi
yaliofanyika tarehe 21 22/05/2015.
Nia kubwa ya Mafunzo haya yalikuwa ni kuwapa uelewa
wahusika na hasa namna ya kutumia Teknolojia mpya kwa
Mashine zijulikanozo kama BVR Kits lakini vile vile Mfumo
mpya utakaotumika.
3. VIFAA
Ndugu Wanahabari,
Katika zoezi hili la uboreshaji wa daftari vifaa mbalimbali
vimegawawiwa kwenye Halmashauri zetu na TUME YA
UCHAGUZI MKUU. Vifaa hivyo vitagawiwa kwa mujibu wa
maelekezo ya Tume kwa kuzingatia idadi ya vituo na idadi ya
wapiga kura wanaolengwa kuandikishwa katika maeneo husika.
Vifaa hivi vimegawiwa katika hatua mbili. Hatua ya kwanza ni
Tume kuvipeleka kwenye Halmashauri na hatua ya pili ni
Halmashauri kuvisambaza kwenye Vituo vya kujiandikisha.
Nimeambiwa baada ya zoezi hili kukamilika Afisa Mwandikishaji
ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri husika anatakiwa
kuvikusanya vifaa vyote na kuvihakiki na kuwasiliana na Tume
kwa ajili ya utaratibu wa kuvirudisha Tume. Vifaa hivyo ni:1. Fomu: Na1,Na.2 ,Na.3A, Na. 3B, Na.4, Na.5, Na.6, Na.7
2. Bango la Kituo cha kuandikisha wapiga kura
3. Kalamu ya wino mweusi
4. Kadi ya Plastiki (PVC)
5. Begi
2
6. Boksi
7. Utepe wa gundi
8. Gundi nzito na pini
9. Mfuko mdogo wa plastiki, na
10.
Sanduku la vifaa BVR. Vifaa vyote vimeshapelekwa na
Halmashauri zote na nimeelezwa wahusika wote
wameshapewa maelekezo ya namna ya kutumia vifaa hivyo.
Pia kama ilivyosisitizwa vifaa hivi vitunzwe vizuri katika hali
ya usafi na usalama. Hatua za Kisheria zitachukuliwa dhidi
ya wakaopoteza vifaa hivyo au kuviharibu kwa makusudi.
VITUO VYA KUANDIKISHA
Ndugu Wanahabari
Mkoa wetu una Vituo vya kuandikisha wapiga kura 748 kwa
mchanganuo ufuatao: Halmashauri ya Manispaa
218
Halmashauri ya Wilaya Nkasi 190
Halmashauri ya Wilaya Kalambo
158, na
Halmashauri ya Wilaya Sumbawanga 182 , Vituo hivi
vimeainishwa na Maafisa waandikishaji na vimesaidia sana
hasa kwa TUME kufanya maamuzi mbalimbali kwa
kuzingatia vituo hivyo. Kwa utaratibu wa TUME YA
UCHAGUZI Vituo vitafunguliwa saa 1.30 asubuhi hadi 12.00
jioni.
6. MAOTEO (PROJECTION) YA WATAKAO JIANDIKISHA
Ndugu Wanahabari,
Maoteo (Projection) ya wanaotegemewa kuandikishwa kwa Mkoa
wetu ni kama ifuatavyo:1.
2.
3.
4.
Halmashauri ya Manispaa
107,000
Halmashaurii ya Sumbawanga
141,000
Halmashauri ya Kalambo
124,000
Halmashauri ya Nkasi
152,000
3
8. SIFA ZA KUANDIKISHWA
Ndugu Wanahabari,
Ili mtu aweze kuandikishwa kuwa mpiga kura anapaswa kuwa na
sifa zote zitakazohitajika kwa mujibu wa Sheria. Sheria hizo ni
pamoja na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka
1977, Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura 343 na Sheria ya Uchaguzi
wa Serikali za Mitaa Sura 292. Kwa mujibu wa Sheria hizo
nilizotaja sifa kuu za mpiga kura ni:(a)
Kuwa raia wa Tanzania, na
(b)
Kuwa na umri wa Miaka 18 au zaidi vile vile kwa raia
wote watakaokuwa wametimiza umri wa Miaka 18 ifikapo
tarehe ya Uchaguzi.
Kwenye kipengele hiki cha sifa mtu anaweza kukosa sifa
kuandikishwa kuwa mpiga kura kwa mujibu wa Sheria ya Taifa
Uchaguzi Sura ya 343 Kifungu Na. 11(i) na Sheria ya Serikali
Mitaa Sura 292 Kifungu cha 9 (i) Mtu anakosa sifa
kuandikishwa kwa sababu zifuatazo:(i)
(ii)
(iii)
(iv)
(v)
za
ya
za
za
WATAZAMAJI
WA ZOEZI LA UBORESHAJI
Ndugu Wanahabari,
5
Kutakuwepo
na
watazamaji
wa
Ndani
na
Kimataifa
wanaoruhusiwa kutazama mchakato wa uboreshaji utakaofanyika
katika vituo mbalimbali. Watzamaji kabla ya kutembelea Vituo
mbalimbali vya uandikishaji ni lazima wapewe idhini na Tume ya
Uchaguzi. Mpaka sasa Mkoa wa Rukwa umepokea watazamaji wa
ndani watatu (3) na wanazo barua
za Tume ambazo
wameziwasilisha kwa Maafisa waandikishaji.
WITO WANGU
Ndugu Wanahabari,
Na Maafisa wa Tume, napenda kuchukua fursa hii kuwaomba
Kwanza, Wananchi kuwa watulivu wakati wote wa zoezi
Pili, kuwatakia watendaji wote wa Tume kuzingatia Miongozo
waliopewa
Tatu, kuvitaka vyama vyote vya siasa kufuata utaratibu
uliwasilishwa na Tume kwenye zoezi hili na kuwa kamwe
zoezi hili lisitumike kupotosha watu. Watu waachiwe
wajiandikishe kwa HIARI na UTASHI unaozingatia Sheria ya
nilizotaja hapo juu.
Nne, Changamoto yoyote itakayojitokeza iripotiwe mapema
kwa Maafisa waandikishaji na Mratibu wa Mkoa ili iweze
kuripotiwa kwenye TUME ili ipatiwe ufumbuzi.
Tano, Vyama vihamasishe watu kwa kuzingatia Sheria
zilizowekwa na TUME na Serikali kwa ujumla.
Mwisho,
Nichukue fursa hii kuwatakia wananchi ushiriki unaozingatia
Sheria na unaoendelea kudumisha mshikamano, umoja na Amani
tuliyo nayo.
6