Professional Documents
Culture Documents
TANZANIA GAME
TRACKERS
SAFARIS LTD
1.
2.
3.
4.
5.
1.
2.
3.
4.
5.
Vitalu vilivyoombwa
(2013-2018)
Moyowosi GR South
Lake Natron GCA
(North-South)
Lake Natron GCA (N)
Moyowosi GR Njingwe 2
Moyowosi GR Njingwe 3
Ugalla GR (South)
Ugalla GR (North)
Ugalla GR (Central)
Moyowosi GR Njingwe 1
Maswa Kimali
Vitalu vilivyogawiwa
(2013-2018)
1. Moyowosi GR South
2. Lake Natron GCA (NorthSouth)
1.
2.
3.
4.
5.
Ugalla GR (South)
Ugalla GR (North)
Moyowosi GR Njingwe 1
Maswa Kimali
Maswa Mbono
Jina la Kampuni
WENGERT WINDROSE SAFARIS
Kutokana na WWS kutogawiwa kitalu cha Lake Natron Game Controlled Area
(North) ambacho kampuni hiyo ilikuwa inakitumia hapo awali kwa shughuli za
uwindaji wa kitalii, iliwasilisha rufaa kwa Mhe. Waziri wa Maliasili na Utalii.
Tarehe 12 Desemba 2011, KUUV iliitisha kikao cha pamoja kati ya WWS na GMS
kujadili uwezekano wa kutafuta muafaka wa suala la umiliki wa kitalu cha Lake
Natron GCA (North).
Kutokana na hali hiyo WWS ilishauri KUUV iendelee kufikiria ombi lao la kubakia na
kitalu hicho kwa kuzingatia sheria, mikataba na masuala ya kiikolojia. Sababu za
kiikolojia zilizobainishwa na WWS ni pamoja na kupinga eneo la Lake Natron GCA
North kugawanywa kuwa vitalu viwili (Lake Natron GCA (North) na Lake Natron GCA
(North-South).
Jina la kitalu
North-South
North
South-West
MHJ1
MHJ2
MHJ3
Ramani za vitalu ziligawiwa mwezi Oktoba 2012 kwa kampuni za uwindaji wa kitalii
zikiwa na mabadiliko ya majina hayo. Baada ya mgawo ramani hizo, WWS ilikuja na
hoja mpya kuwa kitalu chake cha Lake Natron GCA North-South kimebalishwa
(swapped) na kupewa kampuni ya GMS. Ramani ya Lake Natron GCA North-South
iliyofanyiwa marekebisho ya jina ilionesha ukubwa wa kitalu ulibaki vile vile na katika
eneo na daraja lile lile pamoja na jira za mpaka (GPS coordinates) zikiwa zile zile.
WWS iligeuza madai hayo mapya kuwa hoja ya msingi badala ya hoja za awali.
Baada ya hapo suala hilo likageuka kuwa mgogoro kati ya Serikali, WWS na GMS
kwamba kuna udanganyifu umefanyika wa kubadilisha vitalu.
3
Katika kikao cha tarehe 24 Mei 2013, kati ya Idara ya Wanyamapori, WWS, GMS,
TAWIRI, na Kitengo cha Sheria cha Wizara; Mkuruguenzi wa GMS alitaarifu kuwa
katika mojawapo ya majadiliano kati ya GMS na WWS kuwa WWS iliiomba GMS
kuiuzia kitalu chake cha Lake Natron GCA North lakini GMS ilikuwa tayari kuiuzia safari
na siyo kitalu.
Baada ya GMS kukataa ombi lao, WWS ilianza kampeni za kuichafua kampuni ya GMS
ikiwa ni pamoja na tukio la Reno-Nevada, Marekani wakati kampuni hizo zikiuza safari
za uwindaji wa kitalii Januari, 2015. Katika tukio hilo WWS iliifanyia fujo GMS kuwa
kampuni hiyo inafanya utapeli kwa kusambaza vipeperushi vinavyopotosha kwamba
inamiliki kitalu cha Lake Natron GCA North.
Hatua hiyo iliichafua GMS na kusababisha Mkurugenzi wake Bw. Awadhi Abdallah atoe
taarifa Safari Club International (SCI). SCI iliingilia kati kutuliza mgogoro huo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009, kampuni zote
za uwindaji wa kitalii ikiwemo WWS zilitakiwa kuondoka katika vitalu tarehe 31 Machi,
2013 baada ya muhula wa umiliki wa vitalu kumalizika ili kupisha umiliki mpya ili
kutekeleza mabadiliko mapya yaliyoainishwa katika sheria hiyo. Hata hivyo, WWS
iligoma kuondoka na badala yake mwezi Mei 2013 iliamua kwenda Mahakamani kudai
haki.
Mmiliki mpya wa kitalu cha Lake Natron GCA North ambacho kilibadilishwa jina na
kuwa East, kampuni ya GMS aliwasilisha barua ya malalamiko kwa Mkurugenzi Idara
ya Wanyamapori kwamba anashindwa kuendeleza Kitalu pamoja na kujenga kambi ya
uwindaji kwa kuwa bado WWS wapo ndani ya Kitalu kinyume cha sheria. Mkurugenzi
wa Idara ya Wanyamapori aliiandikia WWS barua ya tarehe 20/05/2013 ya kuiamuru
kuondoka kwenye kitalu hicho katika muda wa siku tatu.
Amri hiyo haikutekelezwa na badala yake WWS ilirudi kwa Mhe Waziri wa Maliasili na
Utalii tarehe 23/5/2013 ikipinga amri ya kuondoka iliyotolewa na Mkurugenzi wa
Wanyamapori. Aidha, sambamba na hatua hiyo, WWS iliwasilisha Mahakama KuuKitengo cha Biashara kuomba zuio la GMS kufanya shughuli za uwindaji katika kitalu
cha Lake Natron GCA East.
Mhe. Waziri, alimwagiza Mkurugenzi wa Wanyamapori kuitisha kikao cha wadau wote
wanaohusika na mgogoro wa kitalu cha Lake Natron (GCA) (East) ili kulijadili tena suala
hili. Hata hivyo kikao hicho hakikufikia muafaka kutokana na WWS kuendelea kushikilia
msimamo wa kukitaka kitalu hicho kwa gharama yoyote ile.
Katika kikao hicho nyaraka zote muhimu ziliwasilishwa ikiwemo Ripoti ya Taasisi ya
Utafiti ya Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kuhusu Tathimini ya Vitalu vya Uwindaji wa
Kitalii Tanzania toleo la 3.1 ya Februari 2011. TAWIRI ndiyo Mamlaka ya kisayansi ya
utafiti wa wanyamapori Tanzania. Ikumbukwe kuwa, mabadiliko ya majina hayo
hayakuathiri ukubwa, mipaka na jira (GPS coordinates) za vitalu.
4
Katika kikao cha tarehe 24 Mei 2013 kilichotajwa awali, WWS iliwasilisha ramani
ambayo inadai kuipatia TAWIRI inayoonesha jina na mipaka kitalu cha Lake Natron
GCA (North-South) ili kuthibitisha uhalali wa madai yao. Ilipohojiwa kuwa imekuwaje
ipate ramani TAWIRI wakati Taasisi hiyo haina mamlaka ya kutoa ramani hizo kwa
kampuni za uwindaji, kampuni ya WWS ilieleza kuwa ililazimika kufanya hivyo kwa vile
haikuwahi kupewa ramani ya kitalu hicho na Idara ya Wanyamapori, jambo ambalo si
kweli.
Kampuni ya WWS iliendelea kufungua kesi mbalimbali katika Mahakama Kuu ya Ardhi
na Mahakama ya biashara bila mafanikio kama ifuatavyo;
i.
ii.
iii.
iv.
v.
vi.
vii.
viii.
kuzuia ndege za GMS zisitue; na walifunga barabara kwa magogo kuzuia magari ya
wageni waliokuja kuwinda yasipite.
ii.
iii.
iv.
v.
vi.
Wizara ya Maliasili na Utalii iliamua kuirejeshea leseni Kampuni ya Green Mile Safari
Ltd kufanya shughuli za uwindaji wa kitalii katika vitalu vyake vya Selous GR (MK1),
Lake Natron GCA (East zamani North), Gonabis/Kidunda WMA baada ya kupitia rufaa
yake dhidi ya Mkurugenzi wa Wanyamapori kupinga kunyanganywa leseni.
Kampuni ya GMS ilifutiwa umiliki wa vitalu na leseni zake zote za uwindaji kupitia
Taarifa ya Umma iliyotolewa tarehe 11 Julai, 2014. Uamuzi huo ulifikiwa kutokana na
ukiukwaji Sheria na Kanuni za Uwindaji wa Kitalii uliofanywa na wageni wa GMS wakati
wakiwinda kwenye kitalu cha Gonabis/Kidunda WMA mwaka 2012. Matukio ya
ukiukwaji yalibainishwa kupitia picha video (DVD) iliyowasilishwa Bungeni na Mhe.
Peter Msigwa (Mb) wakati wa Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2014.
Kampuni ya GMS ilirejeshewa leseni kunatokana na hoja zilizoainishwa kwenye rufaa
yake na tafsiri ya Sheria ya Wanyamapori Na.5 ya Mwaka 2009 katika kifungu 38(12)(c)
ikisomwa kwa pamoja na kanuni ya 17 (2) (b) ya Kanuni za Uwindaji wa Kitalii za
mwaka 2010 zilizofanyiwa marekebisho mwaka 2015.
Hukumu ya Mahakama
iliyotolewa tarehe 31 Machi, 2015 na Jaji Songoro dhidi ya Kampuni ya WWS pamoja
na tafsiri na ushauri kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa barua Kumb. Na.
AGC/A.130/2J/9 ya tarehe 14 Desemba, 2015 aliyoeleza kuwa kifungu cha 38(12)(c)
kinampa mamlaka Waziri wa Maliasili na Utalii kufuta umiliki wa kitalu endapo
Mahakama itakuwa imemtia hatiani mmiliki wa kitalu.
Ni kwa msingi huu Wizara ilitengua maamuzi yaliyotolewa na Mkurugenzi wa
Wanyamapori na kuirejeshea haki Kampuni ya GMS kufanya shughuli zake za uwindaji
wa kitalii. Aidha, Wizara ilitoa maelekezo kuwa waliohusika na uvunjifu wa sheria,
kanuni na taratibu za uwindaji zilizofanywa na wageni wa kampuni ya GMS huko
kwenye kitalu cha Gonabis/Kidunda WMA; wakiwamo Askari wa Wanyamapori
(waliosimamia uwindaji) pamoja na Mwindaji Bingwa wachukuliwe hatua za kisheria na
kinidhamu.
Pamoja na hatua hizi, Wizara ilielekeza kampuni ya Green Mile Safari Ltd, irudi
kwenye vitalu vyake na kuendelea na shughuli za uwindaji na kuwa Serikali itawapatia
ulinzi kila itakapohitajika. Kufuatia uamuzi huo, kampuni ya WWS ilifungua Shauri
tarehe 25 Mei 2016 katika Makahama Kuu, Kitengo cha Biashara kuomba zuio dhidi ya
utekelezaji wa amri ya Wizara ya kuiamuru kuondoka katika kitalu cha Lake Natron
GCA East ifikapo tarehe 31 Mei 2016. Shauri hilo lilisikilizwa na Jaji Mwambegele, J.
ambapo ombi hilo halikukubaliwa.
3. HITIMISHO
Maelezo haya yanabainisha mtiririko wa chanzo cha mgogoro na jitihada mbalimbali
zilizochukuliwa ili kufikia suluhu yake kama ifuatavyo;
i.
Taarifa za kukaribisha maombi kutoka kwa wadau wote wenye nia ya kufanya
biashara ya uwindaji wa kitalii zilitolewa kwa uwazi kupitia vyombo vya habari.
ii.
Kifungu cha 38(14) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009
kinatoa fursa kwa kampuni ambazo hazikuridhika na matokeo ya ugawaji kukata
rufaa kwa Mhe. Waziri na kusikilizwa kwa utaratibu wa mapitio ya kiutawala
(administrative review). Aidha, Kifungu cha 38(16) cha Sheria ya Kuhifadhi
Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 kinatoa fursa kwa kampuni ambazo
hazikuridhishwa na uamuzi wa Mhe. Waziri kukata rufaa Mahakama Kuu.
iv.
v.