Professional Documents
Culture Documents
html
T444ZZZ444
keni10000@yahoo.com
MCHANGANUO WA KILIMO CHA UFUTA/ SESAME CULTIVATION BUSINESS PLAN
1. MUHTASARI WA KILIMO BORA CHA UFUTA
Ufuta (sesamum indicum) ni zao linalolimwa kwa wingi katika mikoa ya Lindi, Mtwa
ra, Ruvuma, Pwani, Morogoro, Dodoma,
Tanga na ukanda wa chini katika mikoa ya Rukwa na Mbeya. Zao hili hulimwa kwa aj
ili ya chakula na biashara.
Mbegu za zao hili huwa na wastani wa mafuta kiasi cha asilimia 45.
Kwa sasa soko la ufuta Tanzania ni zaidi ya mara tatu ya uzalishaji wake, kwa ma
ntiki hiyo zao hili lina soko kubwa sana.
Uzalishaji wake unafanyika kwa kiasi kidogo kwa sababu wakulima wamekuwa wakili
ma zao hili la ufuta kwa mazoea na kutumia
mazao yake kama nafaka ya kutengeza vyakula mbalimbali kama kashata. Lakini kam
a utalima kibiashara ni zao ambalo linaweza kukomboa
jamii yetu kutoka katika dimbwi la umasikini.
2. UZALISHAJI WA ZAO LA UFUTA
MBEGU
Chagua aina ya mbegu inayotoa mazao mengi na bora, inayovumilia mashambulizi ya
magonjwa na wadudu, inayokomaa mapema na kutoa mafuta mengi.
Chagua mbegu inayokomaa kwa pamoja ili kurahisisha uvunaji na pia kuepuka upotev
u wa zao shambani.
Aina nyeupe ya mbegu ya ufuta hupendelewa zaidi kuliko aina nyeusi.
Mbegu bora ya ufuta inayopendekezwa ni LINDI 02, mbegu ambayo imefanyiwa utafiti
na chuo cha utafiti NALIENDELE.
Kwa wastani mbegu hii hutoa kati ya gunia 10 mpaka 15 ukifuata kanuni za kilimo
bora. Mbegu hii hukomaa ndani ya siku mia (100) mpaka mia na kumi(110).
Aina hii ya ufuta ina asilimia 55 ya mafuta. Hii ni habari njema kwa wakulima ku
toka kwa watafiti wetu wa Kilimo kutoka kituo cha Utafiti Naliendele, Mtwara.
UPANDAJI
Panda mbegu nusu inchi chini ya udongo, inchi sita umbali wa mbegu na mbegu na f
uti mbili nafasi ya msitari na msitari, kabla ya kupanda hakikisha ardhi
imelowana vya kutosha na upande mbegu masaa mawili au matatu baadae.
MBOLEA
Ufuta unahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao bora. Katika kudumisha rutuba
ya udongo, tumia kilimo cha mzunguko wa mazao au weka mbolea za asili pale inapo
bidi.
PALIZI
Dhibiti magugu kwa kupalilia ili kuruhusu ufuta kutumia vizuri unyevu na virutub
ishi. Magugu mengine huwa ni maficho ya wadudu waharibifu wa zao la ufuta.
MAGONJWA
Ufuta hushambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali ambao huweza kusababisha upu
ngufu na ubora wa mazao. Hivyo kagua shamba mara kwa mara hasa kwenye maua
na mapodo ili kuona dalili za mashambulizi. Endapo kuna dalili zamashambulizi, c
hukua tahadhari mapema kabla ya uharibifu mkubwa haujatokea.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNA
Kagua shamba kuona kama ufuta umekomaa. Ufuta hukomaa, kati ya miezi mitatu na m
inne tangu kupanda kutegemea aina. Aina ya ufuta usiokuwa na matawi
hukomaa mapema kuliko ile yenye matawi. Ni muhimu kuwahi kuvuna ili kuepuka ufut
a kupukutikia shambani.
6 Kuvuna 50,000
7 Usafiri 50,000
8 Gharama zingine 50,000
9 Jumla 400,000
10 Mapato (Forecasts) gunia 10*50kg*3000 1,500,000
11 Faida 1,100,000
4. SOKO LA UFUTA
Soko la ufuta kwa Tanzania ni mara tatu zaidi ya uzalishaji wake. Kuna makampuni
mbalimbali Tanzania ya unuzi wa ufuta. Makampuni hayo hununua na kusafirisha
nje ya nchi kama India na China. Makampuni hayo ni kama vile OLAM, Export Trader
s n.k.
Katika msimu wa mwaka 2014 bei ya ufuta kwa kilo ilikuwa sh 3000 ambayo ni sawa
na sh 300,000 kwa gunia lenye ujazo wa kilo 100. Kwa maana hiyo uhakika wa soko
upo na ni mkubwa sana.
DISCLAIMER
Mchanganuo huu ni matokeo ya kiutafiti wa kibiashara, ambayo jitihada zimefanyik
a kuifanya iendane na hali ya kiuchumi ya sasa, hivyo haitaathiri au kuathiriwa
na tamko la wazi au la kiutendaji wa mabadiliko ya kila siku ya kiuchumi duniani
hasa ndani ya soko letu la Tanzania. Matokeo yoyote utakayoyapata mtumiaji au m
somaji yatakayokuathiri moja kwa moja au kimchakato, bila kikomo cha muda maalum
u mpaka kuathiri faida iliyopangwa, hatutakua tayari kutupiwa lawama ya aina yoy
ote ile.