You are on page 1of 170

Dua

za
Mwezi wa Ramadhan

Kimekusanywa na:
Tayyiba Publishers – Canada

Kimetarjumiwa na:
Ustadh Haji Hemedi Lubumba Selemani
Na
Al-Haj Ramadhani S. K. Shemahimbo

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 1 6/16/2016 4:29:21 PM


© Haki ya kunakili imehifadhiwa na:
AL-ITRAH FOUNDATION

ISBN: 978 – 9987 – 17 – 035 – 7

Kimekusanywa na:
Tayyiba Publishers - Canada
Barua Pepe: tayyiba.publishers@gmail.com

Kimetarjumiwa na:
Ustadh Haji Hemedi Lubumba Selemani
Na
Al Hajj Ramadhani S. K. Shemahimbo

Toleo la Kwanza: June, 2016


Nakala: 1000

Kimetolewa na kuchapishwa na:


Alitrah Foundation
S.L.P. 19701 Dar es Salaam, Tanzania
Simu: +255 22 2110640 / 2127555
Barua Pepe: alitrah@yahoo.com
Tovuti: www.alitrah.info

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 2 6/16/2016 4:29:21 PM


Yaliyomo
Neno la Mchapishaji........................................................................ 1

Dua katika Mwezi wa Ramadhani Tukufu....................................... 3

Dua Uuonapo Mwezi Mwandamo Wa Ramadhani.......................... 5

Dua Za Usiku wa Ramadhani.......................................................... 8

Dua ya Kwanza................................................................................ 8

Dua ya Pili...................................................................................... 12

Maelezo Mafupi Juu Ya Dua Ya Al-Iftitah:.................................... 15

Kumtukuza Mwenyezi Mungu: .................................................... 16

Msisitizo Juu Ya Upweke (Tawhiid) Wa Allah: ............................ 16

Ukarimu Wa Mwenyezi Mungu: ................................................... 16

Mahusiano Ya Allah Na Wanadamu: ............................................ 17

Kumswalia Mtukufu Mtume (Salawat): ....................................... 17

Rehma Na Amani Juu Ya Ma’sumiin: ........................................... 18

Jukumu La Imam Wa Kumi Na Mbili (A.S.): ............................... 15

Dua Ya Tatu.................................................................................... 20

Dua Ya Nne : Dua Al-Iftitah.......................................................... 22

Dua Ya Tano................................................................................... 55

Dua Ya Sita.................................................................................... 60

Dua Ya Saba................................................................................... 63

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 3 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua Ya Sahri (DAKU)................................................................... 64

Ziyara Al-Waritha.......................................................................... 68

Ziyara Ya Ali Akbar (A.S.)............................................................. 74

Ziyara Ya Wahanga Wote............................................................... 75

Ziyara Ya Abul-Fadhli Abbas (A.S.).............................................. 78

Dua Baada Ya Ziyara..................................................................... 80

Dua Za Kila Siku Ya Ramadhani................................................... 83

Mwezi Mosi:.................................................................................. 83

Mwezi Pili: .................................................................................... 84

Mwezi Tatu: .................................................................................. 84

Mwezi Nne: ................................................................................... 85

Mwezi Tano: ................................................................................. 86

Mwezi Sita: ................................................................................... 87

Mwezi Saba: .................................................................................. 87

Mwezi Nane: ................................................................................. 88

Mwezi Tisa: ................................................................................... 89

Mwezi Kumi: ................................................................................ 89

Mwezi Kumi Na Moja: ................................................................. 90

Mwezi Kumi Na Mbili: ................................................................. 91

Mwezi Kumi Na Tatu: ................................................................... 92

Mwezi Kumi Na Nne: ................................................................... 92

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 4 6/16/2016 4:29:21 PM


Mwezi Kumi Na Tano: .................................................................. 93

Mwezi Kumi Na Sita: ................................................................... 94

Mwezi Kumi Na Saba: .................................................................. 94

Mwezi Kumi Na Nane: ................................................................. 95

Mwezi Kumi Na Tisa: ................................................................... 96

Mwezi Ishirini: .............................................................................. 96

Mwezi Ishirini Na Moja: ............................................................... 97

Mwezi Ishirini Na Mbili: .............................................................. 98

Mwezi Ishirini Na Tatu: ................................................................ 99

Mwezi Ishirini Na Nne: ................................................................ 99

Mwezi Ishirini Na Tano: ............................................................. 100

Mwezi Ishirini Na Sita: ............................................................... 101

Mwezi Ishirini Na Saba: ............................................................. 101

Mwezi Ishirini Na Nane: ............................................................. 102

Mwezi Ishirini Na Tisa: .............................................................. 103

Mwezi Thelathini: ....................................................................... 104

Dua Ya Mikesha Kumi Ya Mwisho.............................................. 105

Kithirisha Maneno Haya: ............................................................ 111

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Moja................................. 112

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Mbili................................. 116

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Tatu................................... 121

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 5 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Nne................................... 125

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Tano.................................. 130

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Sita................................... 134

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Saba.................................. 138

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Nane................................. 143

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Tisa................................... 147

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Thelathini............................................ 151

vi

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 6 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ٰ َ ْ َّ َّ ْ
‫ِبس ِم الل ِه الرحم ِن الر ِح ِيم‬
Neno La Mchapishaji

K itabu kilichoko mikononi mwako ni tarjuma ya kitabu cha


dua (Kiarabu/Kingereza) kwa jina la A Manual of Ramadhan
­Devotion. Sisi tumekiita, Du’a za Mwezi wa Ramadhani.
Kitabu hiki ni mkusanyiko wa dua maarufu zinazosomwa katika
mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Jambo bora kabisa ambalo muumini anaweza kuomba wakati
wa mwezi huu ni maghfira na msamaha kutokana na dhambi zake
zilizopita. Nyingi ya dua maalumu kwa mwezi wa Ramadhani ni
za kuomba msamaha wa mzigo mkubwa wa dhambi ambao mtu
­ameubeba.
Ramadhani ni nafasi nzuri sana aliyopewa yeye kufanya
­madhambi yake yafutwe na kujipatia cheo cha juu mbele ya macho
ya Mwenyezi Mungu.
Kutokana na umuhimu wa dua hizi, tumeamua kukichapi-
sha kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili, kwa lengo letu lile lile la
­kuwahudumia ndugu zetu Waislamu wazungumzaji wa Kiswahili.
Tunamshukuru ndugu yetu Ustadh Al Haji Hemedi Lubumba
Selemani na Al Haji Ramadhani S. K. Shemahimbo, kwa kukubali
jukumu hili la kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale
wote walioshiriki katika kusahi­hisha na kukipitia hadi kufanikisha
kuchapishwa kwake. Ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitaku-
wa ni chenye manufaa kwa wasomaji wetu na kuzidisha upeo wao
wa ibada na elimu katika dini.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 1 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Shukrani Maalumu

Wachapishaji wa kwanza wa kitabu hiki katika lugha ya Kiarabu /


Kiingereza ni:
Tayyiba Publishers
Canada
Barua pepe: tayyiba.publishers@gmail.com

Taasisi yetu ya Al-Itrah Foundation inaishukuru sana Taasisi hii


kwa kutukubalia tuki­tarjumi kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili.
­Tunamuomba Allah ‘Azza wa Jalla awazidishie kila la kheri wazidi
kuendeleza kazi hii ya tablighi ulimwenguni kote -Amin.

Mchapishaji:
Alitrah Foundation.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 2 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ٰ َ ْ َّ َّ ْ
‫ِبس ِم الل ِه الرحم ِن الر ِح ِيم‬
Dua Katika Mwezi wa
­Ramadhani Tukufu

M wezi wa Ramadhani ni fursa iliyotolewa na Muumba Mwenye


huruma kwa ajili ya waja wake kujikurubisha karibu Naye,
kuomba msamaha kwa ajili ya dhambi zao, na ukidhiwaji wa haja
zao. Ndani ya Qur’ani Tukufu, katikati ya mjadala muhimu juu ya
mwezi wa Ramadhani, Aya ifuatayo, ambayo ni dhahiri kwamba
haina uhusiano wa moja kwa moja na Ramadhani, imeingizwa: “Na
waja wangu watakapokuuliza juu yangu basi hakika mimi nipo
karibu, nayaitika maombi ya muombaji anaponiomba, basi
­waniitikie na waniamini, ili wapate kuongoka. (2:186)
Wafasiri wanakubaliana kwamba hii ni Aya yenye nguvu sana
kati ya Aya zote juu ya uhusiano wa ki-ungu na binadamu. Aya yote
imesima­ma katika kiwakilishi nomino cha umoja (singular) nafsi ya
kwanza, ambayo imerudiwa mara saba. Ni uthibitisho wa ule uhu-
siano wa karibu sana baina ya mwanadamu na Muumba wake, na
uhakikisho kwamba yeye atasikilizwa pale atakapokuwa anamuom-
ba Yeye (s.w.t).
Kwamba Aya kama hii ni lazima ijumuishwa miongoni mwa Aya
zina­zozungumzia umuhimu wa mwezi wa Ramadhani, na baadhi ya
kanuni zake (tazama 2:182-7), ni dalili ya dhima muhimu ya Dua
katika mwezi wa Ramadhani. Kujizuia kutokana na kukidhi mata-
manio ya kimwili kuna­chochea kuongezeka kwa imani ya kiroho, na
kunasababisha mwelekeo juu Swala na ibada kwa jumla.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 3 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Waumini hujihisi kuwa karibu na Mwenyezi Mungu, na Mun-


gu huwakumbusha kwamba na Yeye pia yuko karibu, na atayajibu
maombi na Dua zao. Masiku (mikesha) ya mwezi wa Ramadha-
ni hutumika kwa kukesha katika swala na Dua kwa wingi. Hata
wale waumini ambao kwa kawaida hawana muda mwingi kwa ajili
ya Dua, wanajaribu kufanya hivyo katika mwezi huu. Hii ni kwa
sababu ya msisi­tizo wa utukufu wa mwezi huu, na ile ahadi ya
thawabu za ziada, na vilevile ule uhakikishiwaji wa majibu ma-
zuri ya mafanikio. Anasema Mtukufu Mtume (s.a.w.w.): “…..fanya
maombi ukiwa umenyanyua mikono yako juu ….. kwani hizi ndio
nyakati bora zaidi, ambazo kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu
anawaangalia waja wake kwa huruma, anajibu Dua zao kama
wakiomba, anaitika kama wanamwita, anatoa kama wakiomba na
anawakubalia kama wakimsihi ….. (hadithi ya Mtume anapoukari-
bisha mwezi wa Ramadhani).
Jambo bora kabisa ambalo muumini anaweza kuomba waka-
ti wa mwezi huu ni maghfira, msamaha juu ya dhambi zake zi-
lizopita. Nyingi ya Dua maalum kwa mwezi wa Ramadhani ni
za kuomba msamaha wa mzigo mkubwa wa dhambi ambao mtu
ameubeba. Ramadhani ni nafasi nzuri sana aliyopewa yeye kufan-
ya madhambi yake yafutwe, na kujipatia cheo cha juu mbele ya
macho ya Mwenyezi Mungu. Hivyo watu wengi wanasame­hewa
katika mwezi huu kiasi kwamba ni wale wasio na bahati tu am-
bao wanakoseshwa. Mtukufu Mtume anasema katika hadithi hiyo
hiyo: “Hakika mwenye majuto ni yule ambaye anakosa msamaha
wa Mwenyezi Mungu katika mwezi huu mashuhuri.” Mambo men-
gine ya kuomba ni pamoja na kukidhiwa haja, kuondolewa mateso,
na mafanikio katika akhera.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 4 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Uuonapo Mwezi Mwandamo Wa


Ramadhani

Mwenyezi Mungu ameagiza kwamba Waislamu watumie mwendo


wa mwezi ili kutambua upitaji wa miezi na miaka. Wakati wale
Waislamu wa mwanzo walipoulizwa juu ya mwezi mpya (mwanda-
mo), Mwenyezi Mungu akashusha Aya isemayo: Mwenyezi Mungu
asema:

َّ ُ َ َ َ ْ ُ َّ َ ْ‫َ ْ َ ُ َ َ َ أ‬
‫اس‬
ِ ‫يسألونك ع ِن ال ْ ِه َل ِة ۖ قل ِهي موا ِقيت ِللن‬
}189{ ۗ ‫َوالح ِ ّج‬
“Wanakuuliza juu ya miezi: Sema : Hivyo ni (vipimo
asilia) vya nyakati kwa ajili ya
(mfumo wa maisha ya) watu na Hijja .(2:189)
Mwezi mwandamo wa Ramadhani ni makhsusi kwa Waislamu.

Unatangaza kuanza kwa mwezi mtukufu huo na kuanza kwa reh-


ma na neema zinazohusiana na Ramadhani. Kwa mujibu wa Mtuku-
fu Mtume (s.a.w.w.) yeyote yule anayeuona mwezi mwandamo wa
Ramadhani ana­paswa kusoma Dua ifuatayo.*

ْ َّ ٰ َ ْ َّ َّ ْ
‫ِبس ِم الل ِه الرحم ِن الر ِحي ِم‬
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema
Mwenye ­kurehemu.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 5 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫هللا َر ُّب ْال َع مَال ْين‬


ُ ‫َرّب ْي َو َر ُّب َك‬
ِ ِ
Mlezi wangu na Mlezi wako ni Allah, Mwenyezi
­Mungu, Mola Mlezi wa viumbe.

َ ْ ْ‫َ ّ ُ َّ َ َّ ُ َ َ ْ َ أْ َ ْ َ إ‬
‫اليم ِان‬ِ ‫اللهم ا ِهله علينا ِبالم ِن و‬
Ewe Mungu wangu! Uandamishe kwetu kwa amani
na imani.
َ ْ ْ‫َ َّ َ َ َ إ‬
‫السال ِم‬
ِ ‫والسالم ِة و‬
Kwa salama na unyenyekevu.

َ‫َو مْالُ َسا َر َعة إ َلى َما ُتح ُّب َو َت ْر�ضى‬


ِ ِ ِ
Na kwa kuharakisha kuyaendea yale uyapendayo na
kuyaridhia.
َ َ َ ْ َ ْ َ َ ْ َ َّ ُ ّ َ
‫اللهم با ِرك لنا ِفي شه ِرنا هذا‬
Ewe Mungu wangu! Tupe baraka ndani ya mwezi
wetu huu.

ُ‫َو ْار ُز ْق َنا َخ ْي َر ُه َو َع ْو َنه‬


Turuzuku kheri yake na msaada wake.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 6 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫ض َّر ُه َو َش َّر ُه َو َبلاَ َئ ُه َوف ْت َن َته‬


ُ ‫اصر ْف َع َّنا‬
ْ ‫َو‬
ِ ِ
Na tuepushie madhara yake, shari yake, balaa lake na
mtihani wake.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 7 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Za Usiku Wa Ramadhani

K ila usiku wa mwezi wa Ramadhani ni wakati wa kumwabudu


Allah (s.w.t.). kwa kumuomba na kutaka msamaha Wake.
Mwenyezi Mungu ana­jua kwamba wanadamu wana uwezekano wa
kutenda dhambi, na wanahi­taji fursa na wasaa wa kutubia na ku-
jirekebisha.
Hivyo mwezi wa Ramadhani ni msimu wa Dua na kuomba
maghufira ambapo Waislamu wanajivua mizigo ya dhambi. Dua
zinazofuata zimefundishwa na Ma’sumiin (a.s.) na zinatuonyesha
sisi namna ya kutafuta msamaha na Huruma za Allah katika mwezi
huu.

Dua Ya Kwanza

Baada ya kumtukuza Mwenyezi Mungu, Dua inayofuata inaelezea


ubora wa mwezi wa Ramadhani, na sifa zake bainifu. Wenye
kuabudu na wenye kuomba wanapata upendeleo maalumu ikiwa
wataomba ndani ya mwezi huu. Dua hii imependekezwa pia baada
ya Swala za wajibu.

َّ ‫الر ْح َٰمن‬ َّ ْ
َّ ‫الل ِه‬
‫الر ِح ِيم‬ ِ ‫ِبس ِم‬
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 8 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

‫َيا َع ِل ُّي َيا َع ِظ ْي ُم‬


Ewe Uliye juu! Ewe Mwenye uwezo!
َ
‫َيا غ ُف ْو ُر َيا َر ِح ْي ُم‬
Ewe Msamehevu! Ewe Mrehemevu!

َّ ‫َأ ْن َت‬
ُ‫الر ُّب ْال َع ِظ ْيم‬
Wewe ni Mola Mlezi uliye na uwezo,

ٌ‫س َكم ْثله َش ْيئ‬


َ ْ‫َا َّلذ ْي َلي‬
ِٖ ِ ِ
Ambaye hakuna yeyote mfano Wake,

ُ‫السم ْي ُع ْال َب ِص ْير‬


َّ ‫َو ُه َو‬
ِ
Na Yeye ni Msikivu, Mjuzi.

ُ‫َو َه َذا َش ْه ٌر َع َّظ ْم َت ُه َو َك َّر ْم َته‬


Huu ni mwezi ulioutukuza na kuupa heshima,
ُّ َ َ ُ َ ْ َّ َ َ ُ َ ْ َّ َ َ
ْ‫الش ُهور‬
ِ ‫وشرفته وفضلته على‬
Ulioupa sharafu na ubora kuliko miezi mingine,

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 9 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ‫ض َت ِص َي َام ُه َع َلي‬


ْ ‫الش ْه ُر َّالذ ْي َف َر‬
ِ
َ ََُ
‫وهو‬
Nao ni mwezi ambao umefaradhisha funga juu yangu,

َ‫ان َّالذ ْي َأ ْن َ ْزل َت ف ْيه ْال ُق ْر َءان‬


َ ‫ض‬َ ‫َو ُه َو َش ْه ُر َر َم‬
ِ ِ ِ
Nao ni mwezi wa Ramadhan ambao ndani yake
­umeteremsha Qur’an,

َ ْ ُ ْ َ َ ُ ْ َ ّ َ ّ َ َ َّ ً ُ
‫ات ِمن الهدى والفرق ِان‬ ٍ ‫اس وب ِين‬
ِ ‫هدى ِللن‬
Ili kuwa mwongozo kwa watu, na dalili zilizo wazi za
mwongozo na upambanuzi.

ْ َ ْ َ ََْ ْ َ َْ َ َ
‫وجعلت ِفي ِه ليلة القد ِر‬
Ndani yake umeweka Laylatul-Qadri,

ْ َ َْ ْ ً ْ َ َََْ َ َ
‫ف شه ٍر‬ِ ‫وجعلتها خيرا ِمن أل‬
Na ukaufanya kuwa bora kuliko miezi elfu.

َ‫َف َيا َذا مْالَ ّن واَل ُي َم ُّن َع َل ْيك‬


ِ ِ
Ewe Mwenye fadhila na wala hakuna yeyote mwenye
kukufadhili,

10

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 10 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫النار ف ْي َم ْن َت ُم ُّن َع َليه‬


َّ ‫ُم َّن َع َل َّي ب َفكاك َر َق َبت ْي م َن‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Nifanyie fadhila kwa kuniepusha na moto. Niwe
­miongoni mwa wale uwafanyiao fadhila,

َ‫الراحم ْين‬
َّ َ‫َو َأ ْدخ ْلني ْال َج َّن َة ب َر ْح َمت َك َيا َا ْر َحم‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Na niingize Peponi kwa rehema zako ewe Mbora wa
wenye ­kurehemu.

11

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 11 6/16/2016 4:29:21 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Pili

(Kwa ajili ya kila usiku wa Ramadhani na kwa nyakati zote):

M oja ya taratibu za Dua ni kuwaombea wengine, kuwakumbuka


wale ambao wana shida.
Ni kitendo kisicho na ubinafsi, kuonyesha ubinadamu na ku-
wafikiria wengine. Mwenyezi Mungu anampenda sana yule mtu
anayewaombea wengine kwanza, halafu ndipo ajiombee yeye mwe-
nyewe. Imam wa sita (a.s.) anasema: “Wakati Mwislamu anapomu-
ombea ndugu yake, (nyongeza katika) riziki inatolewa kwake kwa
wingi, mateso husukumiliwa mbali na yeye, na malaika wanam-
wambia: “Utapata nawe pia kama hayo hayo.”
Watu wengi duniani kote wanapatwa na matatizo yasiyoelezeka.
Dhulma na uonevu vimeenea katika nchi nyingi. Ni kidogo sana
tunachoweza kufanya ili kuyaondoa mateso hayo.
Hata hivyo, tunaweza angalau kuwaombea kwa kweli ya dhati,
tukitegemea kwamba Mwenyezi Mungu atawasaidia kwani anao
uwezo juu ya kila kitu. Na sisi vilevile tuna­muomba Allah (s.w.t.),
atatupatie nia na uwezo wa kuwasaidia wengine kwa njia yoyote
tutakayoweza.

َّ ٰ َ ْ َّ َّ ْ
‫ِبس ِم الل ِه الرحم ِن الر ِح ِيم‬
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

12

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 12 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ َ ُ ٰ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد وا ِل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mpe rehema Muhammad na Aali
Muhammad.

ُّ ‫َا َّلل ُه َّم َا ْد ِخ ْل َع َلى َا ْهل ْال ُق ُب ْور‬


‫الس ُر ْو َر‬ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Wape furaha watu wa
­makaburini.

ْ‫َا َّلل ُه َّم َا ْغن ُك َّل َفقير‬


ٍ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Mtajirishe kila fakiri.

ُ ْ َ َّ َ
‫الل ُه َّم اش ِب ْع ك َّل َجا ِئ ٍع‬
Ewe Mungu wangu! Mshibishe kila mwenye njaa.

َ ْ ُ َّ ُ ُ ْ َّ ُ َّ َ
‫اللهم اكس كل عري ٍان‬
Ewe Mungu wangu! Mvishe kila aliye tupu.

ُ ْ َّ ُ َّ َ
‫ض َد ْي َن ك ِ ّل َم ِد ْي ٍن‬
ِ ‫اللهم‬
‫اق‬
Ewe Mungu wangu! Mlipie deni kila mwenye deni.

13

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 13 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ ُ ْ َ ّ ُ ْ َ ْ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ف ِرج عن ك ِل مكرو ٍب‬
Ewe Mungu wangu! Mfariji kila mwenye matatizo.

ْ َ َّ ُ َّ ُ َّ ُ َّ َ
‫اللهم رد كل غ ِري ٍب‬
Ewe Mungu wangu! Mrejeshe nyumbani kila mgeni.

ْ‫َا َّلل ُه َّم ُف َّك ُك َّل َاسير‬


ٍ ِ
Ewe Mungu wangu! Mwachie huru kila mateka.

َ‫صل ْح ُك َّل َفاسد م ْن ُا ُم ْور مْالُ ْسلم ْين‬ْ َ َّ ُ َّ َ


ِِ ِ ِ ٍ ِ ِ ‫اللهم ا‬
Ewe Mungu wangu! Sahihisha kila lisilo sawa
­miongoni mwa mambo ya Waisila­mu.

ْ َ َّ ُ ْ َ َّ ُ َّ َ
‫ض‬
ٍ ‫ف كل م ِري‬ِ ‫اللهم اش‬
Ewe Mungu wangu! Mponye kila mgonjwa.

َ‫َا َّلل ُه َّم ُس َّد َف ْق َرَنا بغ َناك‬


ِِ
Ewe Mungu wangu! Ziba ufakiri wetu kwa utajiri
Wako.

14

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 14 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫ؤء َحال َنا ب ُح ْسن َحالك‬


َ ُ‫َا َّلل ُه َّم َغ ّْي ْر س‬
ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Badili ubaya wa hali yetu kwa
uzuri wa hali Yako.

ْ َ ْ َ َ ْ َ َ ْ َّ َّ َ ْ َّ ُ َّ َ
‫ض عنا الدين واغ ِننا ِمن الفق ِر‬
ِ ‫اللهم اق‬
Ewe Mungu wangu! Tulipie deni na tusaidie dhidi ya
ufakiri.

ْ‫إ َّن َك َع َلى ُك ّل َش ْيئ َقدير‬


ٍ ِ ٍ ِ ِ
Hakika Wewe ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu.

Maelezo Mafupi Juu Ya Dua Ya Al-­Iftitah:


Dua al-Iftitah ilifundishwa na Imam wetu wa kumi na mbili (a.s.) kwa
ajili ya Mashia kusoma kila usiku wakati wa mwezi wa Ramadhani.
Dua hii ni bora sana kwa ajili ya kujenga mwelekeo wa mwanadamu
kwa Mola Wake kwa vile inazungumzia vipengele vingi vya udhaifu
wa binadamu, na neema za Allah. Dua hii inaweza ­kugawanyika ka-
tika sehemu mbili:

1. Uhusiano wa binadamu na Mwenyezi Mungu.


2. Viongozi wa ki-Ungu watakatifu.
Sehemu ya kwanza ya Dua hii inaelezea sifa mbalimbali za
Mwenyezi Mungu, na inadhihirisha hali ya huruma na upendo wa
Mwenyezi Mungu juu ya wanadamu. Sehemu hii ya Dua inaweza
kugawanywa zaidi katika vifungu vifuatavyo:

15

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 15 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Kumtukuza Mwenyezi Mungu:


Kama ilivyo taratibu ya Dua, Dua hii ya al-Iftitah inaanza na kum-
sifu na kumtukuza Mwenyezi Mungu. Hii sio kwa sababu kwamba
Mwenyezi Mungu anahitajia kusifiwa kabla ya Yeye kujibu Dua
zetu, bali ni kumkumbusha muombaji juu ya yule Muweza wa yote
anayeongea naye, na hatimaye kuweka hofu juu ya Allah katika
nyoyo ambazo mara nyingi zinakuwa hazizingatii.
Uanzaji wa Dua hii unamuweka muombaji katikati ya matumai-
ni na hofu, mtazamo bora wakati unapoomba. Mwenyezi Mungu
ni Mwingi wa huru­ma, lakini pia ni mkali wa kuadhibu. Binadamu
wasiwe wenye kukata tamaa, wala wasijiamini sana bali wadumu
katika Njia Yake.

Msisitizo Juu Ya Upweke (Tawhiid) Wa Allah:


Mwenyezi Mungu hana mshirika wala mtoto, na anayo mamlaka
kamili na udhibiti usiogawanyi­ka, juu ya viumbe. Wakazi wa angani
na mbinguni wanamtegemea Yeye. Hii ni kuimarisha utegemeaji wa
muombaji juu ya Mwenyezi Mungu, kwani hakuna mwingine tena
anayeweza kumgeukia.

Ukarimu Wa Mwenyezi Mungu:


Hazina za Mwenyezi Mungu hazifilisi­ki wala haziishi, na wakati
wote zinatolewa kwa ukarimu juu ya viumbe Wake. Shida za binad-
amu ni nyingi mno, na kwa kuuwacha wazi mlango wa Du’a, Mwe-
nyezi Mungu amewapa ufunguo wa kwenye hazina Zake. Milango
Yake wakati wote iko wazi, na hakuna maombi yoyote Kwake ya-
nayokataliwa bila ya majibu fulani.

16

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 16 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Lakini mara nyingi mwanadamu ni mtovu wa shukurani, na


wakati wote ni mlafi. Anategemea kwamba Du’a zake siku zote zi-
tajibiwa mara moja. Wakati kuridhika kama huko hakupatikani, yeye
anageuka, badala ya kujikumbusha yeye mwenyewe juu ya neema
zote anazozifaidi.

Mahusiano Ya Allah Na Wanadamu:


Ni uhusiano wa ajabu kweli kweli! Ingawa ni mwanadamu anayem-
hitaji Allah, na anapaswa kujitahidi kumuelekea Yeye; ni Mwenyezi
Mungu anayemualika na kumhimiza yeye kuja, ambaye anaonyesha
upendo na huruma na anaendelea kumpendelea kwa njia nyingi.
Kama anavyosema Imam wa nne katika Dua ya Abu Hamza
Thumali: “Shukurani zimwendee Allah ambaye huniitikia mimi pale
ninapomwita, ingawa mimi ninasitasita pale anaponiita, na sifa ni
kwa juu Yake Allah ambaye hunipa mimi wakati ninapomuomba,
ingawa mimi ni bakhili pale anaponiomba.” Hii inafaa kuitafakari
kwa wale wanaomdha­nia Mwenyezi Mungu kwamba ni bwana wa
kidhalimu anayeweka sheria juu ya wanaadamu.
Sehemu hii ya Dua ni somo bora sana katika mtazamo wa Ki-
islam wa sifa za Mwenyezi Mungu. Mola wa Uislam ni mwenye
upendo, Mungu mwenye huruma anayewatendea wanadamu kwa
ubora zaidi kuliko wanavyostahili. Msingi wa uhusiano kati ya
Mwenyezi Mungu na mwanadamu ni upendo wa Muumba juu ya
viumbe Wake. Ni juu ya mwanadamu kuupekua moyo wake kwa
ajili ya mwitiko wa kutendeana. Sehemu ya pili ya Du’a hii inamta-
kia rehema na amani Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) na Ma’asuumin
wote, na halafu inazungumzia jukumu la Imam wa kumi na mbili
(a.s.).

17

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 17 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Kumswalia Mtukufu Mtume (Salawat):


Baada ya imani juu ya Mwenyezi Mungu, sehemu muhimu ya dini
inayofuata ni imani juu ya wale aliowatuma. Hivyo baada ya kukiri
Ukuu na Upole wa Muumba, Du’a hii inatufundisha sisi kuwakiri
wale viongozi wa Ki-Ungu watukufu kama viongozi wetu kuelekea
kwa Allah (s.w.t.) Rehma na amani zina­tumwa kwa Mtukufu Mtume
(s.a.w.w.) kama ishara ya mapenzi na shuku­rani kwa Mtukufu Mtume
(s.a.w.w.) na kutambua kwamba yeye ni binadamu na anahitaji hu-
ruma na neema kutoka kwa Allah. Inaimarisha vilevile ukumbusho
kwa Mtume (s.a.w.w.) na msukumo wa kuifuata njia yake.

Rehma Na Amani Juu Ya Ma’sumiin:


Baada ya Mtukufu Mtume (s.a.w.w.) warithi waandamizi wake wa-
nakumbukwa na kuombewa. Hawa ndio viongozi halisi wa umma
wa Kiislam ambao waliteuliwa na Mwenyezi Mungu. Imani juu yao,
na upendo kwao ni sehemu muhimu ya imani ya ki-Shi’a.

Jukumu La Imam Wa Kumi Na Mbili (A.S.):


Katika kila zama Mwenyezi Mungu huwa anaye mwakilishi Wake
ambaye anawaongoza viumbe Wake kwenye kusimamisha haki na
uadilifu katika ardhi. Huyo Imam wa Kumi na mbili ndiye kiongozi
wa zama zetu hizi, ambaye atakuja kudhihiri na dini ya Mwenyezi
Mungu itashinda (dini zote) duniani.
Sehemu ya mwisho ya Dua al-Iftitah inazungumzia kuhusu kuja
kwake, kuwaandaa waumini juu ya kusimama kwa utawala wa Allah
unaotarajiwa juu ya ardhi. Kuomba msaada na ushindi kwa ajili ya
Imam wa Kumi na mbili kunatukumbusha sisi kwamba tunamngojea
yeye, na tunahitaji kujiandaa kwa ajili ya kuja kwake. Tunakuwa tu-
natambua wajibu wetu katika wakati wa kughibu (kufichika) kwake,

18

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 18 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

na umuhimu wa kujifundisha sisi wenyewe kama wasaidizi wake.


Tunaomba kwa ajili ya ndoto ya mwisho ya Mwislam, hali ambayo
dini ya Mwenyezi Mungu inapata umuhimu mkubwa, na ukafiri na
unafiki vinadhalilishwa.
Dua al-Iftitah inatukumbusha sisi kwamba imani na vitendo vy-
ote ni muhimu na vya lazima ili kuwa muumini halisi na wa kweli.
Imani juu ya Mwenyezi Mungu inafungamana na kuufanyia kazi
ujumbe Wake ulioku­ja na Mtume Wake, na kusimamisha dini Yake
duniani. Wakati ambapo hilo linaweza kufanyika tu kupitia kwa
Imam, sisi tunapaswa kufanya kazi na kuomba kwa ajili ya kudhihiri
kwake. Wanadamu wanaweza kufaidi uadilifu na amani halisi, na
kutimizwa kwa haja zao, chini ya kiongozi huyo Mtukufu.
Dua al-Iftitah sio maombi tu kwa ajili ya shida na haja zetu, bali
ni ufundishaji wa mizizi ya imani, na upangaji kwa ajili ya namna ya
maisha. Inabakia kwetu sisi kuandaa jedwali la maisha yetu wakati
tunapoisoma du’a hii nzuri katika kila usiku wa Ramadhani.

19

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 19 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Tatu

Dua Hii Kwa Kawaida Husomwa Kabla Ya Dua Al-Iftitah

H ii ni Du’a fupi lakini yenye manufaa makubwa sana. Ndani


yake tuna­muomba kwamba Mwenyezi Mungu atujaalie fursa
ya kwenda Hijja, na kwamba atusamehe dhambi zetu. Kuhiji kwe-
nye nyumba ya Allah (s.w.t.) ni tendo kubwa sana la ibada na tamaa
kuu ya kila Muislam. Imam Ali (a.s.) anasema kuhusu hujaji: “Yule
anayekwenda Hijja na Umra ni mgeni wa Mwenyezi Mungu, na ni
haki juu ya Mwenyezi Mungu kwamba amheshimu mgeni Wake, na
anaonyesha mapenzi Yake kwake kupitia msamaha (wa dhambi).”

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬ ْ
ِ ‫ِبس ِم‬
ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫ص ِلي َعلى ُم َح َّم ٍد َّو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ ‫اللهم‬
Ewe Mungu wangu! Mpe rehema Muhammad na Aali
za ­Muhammad.

َ‫ان َّالذ ْي َا ْن َ ْزل َت ف ْيه ْال ُق ْرآن‬


َ ‫ض‬َ ‫َا َّلل ُه َّم َر َّب َش ْهر َر َم‬
ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Mola Mlezi wa mwezi wa
­Ramadhan, ambao ndani yake uliteremsha Qur’an,

20

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 20 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ّ ‫ض َت َع َلى ع َباد َك ف ْيه‬


َ‫الص َيام‬ ْ ‫َو ْاف َت َر‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Na humo ukafaradhisha funga kwa waja Wako.
َ َّ
‫ص ِلي َعلى ُم َح َّم ٍد َّو ِآل ُم َح َّم ٍد‬
Mpe rehema Muhammad na Aali za Muhammad.

َ َ ْ َ ْ َ َّ َ ْ ْ ُ ْ َ
‫وارزق ِني حج بي ِتك الحر ِام‬
Niruzuku kwenda kuhiji nyumba yako tukufu,
ُ َ
‫ِف ْي َع ِام ْي َهذا َو ِف ْي ك ِ ّل َع ٍام‬
Ndani ya mwaka huu na kila mwaka.

َ‫الذ ُن ْو َب ْالع َظام‬


ُّ َ ْ ْ ْ ْ َ
‫واغ ِفر ِلي ِتلك‬
ِ
Nisamehe dhambi hizo kubwa.
َ ْ َ َ
‫ف ِإ َّن ُه ال َيغ ِف ُر َها غ ْي ُر َك‬
Kwa hakika hakuna yeyote asiye Wewe awezaye
­kuzisamehe,

ُ‫َيا َر ْح ٰم ُن َيا َعلاَّ م‬


Ewe Mwingi wa rehema Uliye Mjuzi mno.

21

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 21 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Nne : Dua Al-Iftitah

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mpe rehema Muhammad na Aali
Muhammad.

َّ ُ َ ْ َ ْ ّ َّ ُ َّ َ
َ‫الث َن َاء ب َح ْمدك‬
ِ ِ ‫اللهم ِإ ِني افت ِتح‬
Ewe Mungu wangu! Hakika mimi naanza kukutukuza
kwa hamdi Yako,

َ‫لص َواب ب َم ّنك‬


َّ ٌ ّ َ ُ َ ََْ
ِ ِ ِ ‫وأنت مس ِدد ِل‬
Nawe ni Mwenye kuelekeza kwenye usahihi kwa
wema Wako.

ْ َ ْ ْ َ ْ َ ْ َّ ُ َ ْ َ َ ْ َ َ َّ َ ُ ْ َ ْ َ َ
‫وأيقنت أنك أنت ارحم الر ِاح ِمين ِفي مو ِض ِع العف ِو‬
َّ ‫َو‬
‫الر ْح َم ِة‬
22

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 22 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Nina yakini kuwa hakika Wewe ndiye Mbora wa


warehemevu pale pana­postahiki msamaha na rehema.

َ ْ َّ َ َ َّ ْ ْ َ ْ َ ْ َ ُ ْ‫َ َ َ ُّ م‬
‫واشد العا ِق ِبين ِفي مو ِض ِع النك ِال والنقم ِة‬
Lakini ni mkali wa adhabu pale panapostahiki onyo
na adhabu.
َ ْ ْ ُ ْ‫َ َ م‬
‫َوا ْعظ ُم ال َت َج ِّب ِرْي َن ِف ْي َم ْو ِض ِع ال ِك ْب ِرَي ِاء َوال َعظ َم ِة‬
Na ni mwenye nguvu kuliko majabari pale
­panapostahiki kiburi na nguvu.
َ‫َا َّلل ُه َّم َاذ ْن َت ل ْي ف ْي ُد َعائ َك َو َم ْس َئ َلتك‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Umenipa idhini ya kusoma dua
na kukuomba,

ْ ‫َف‬
‫اس َم ْع َيا َس ِم ْي َع ِم ْد َح ِت ْي‬
Hivyo sikiliza utukuzo wangu ewe Msikivu!

ْ‫َو َاج ْب َيا َر ِح ْي ُم َد ْع َو ِتي‬


ِ
Nijibu ombi langu ewe Mrehemevu!
ْ َ َ
‫َوا ِق ْل َيا غ ُف ْو ُر َعث َرِت ْي‬
Samehe makosa yangu ewe Msamehevu!

23

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 23 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ ‫َف َك ْم َيا ِا‬


َ‫لهي ِم ْن ُك ْرَب ٍة َق ْد َف َّر ْج َتها‬
Matatizo mangapi ewe Mungu wangu umeyafariji,

َ‫َو ُه ُم ْوم َق ْد َك َش ْف َتها‬


ٍ
Na tabu ngapi umeziondoa,

َْ َ َ ْ
‫َو َعث َر ٍة ق ْد اقل َت َها‬
Makosa mangapi umeyaondoa,
َ َ َ
‫َو َر ْح َم ٍة ق ْد نش ْ َرت َها‬
Rehema ngapi umezieneza,

َ‫َو َح ْل َق ِة َبلاَ ٍء َق ْد َف َك ْك َتها‬


Na milolongo mingapi ya balaa umeitawanya.
ً َ َ َ‫َ ْ َ ْ ُ ّٰ َّ ْ َ ْ َ َّ ْ َ َ ً َّ ا‬
‫الحمد ِلل ِه ال ِذي لم يت ِخذ ص ِاحبة ول ولدا‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye hana
mke wala mtoto.
ْ ُ ْ‫َ َ ْ َ ْ َ ُ َ ْ ٌ م‬
‫ولم يكن له ش ِريك ِفي الل ِك‬
Hana mshirika katika ufalme,

24

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 24 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً ْ ْ َ ُ ْ ّ َ َ ّ ُّ َ ٌّ َ ُ َ ْ َ ْ َ َ
‫ولم يكن له و ِلي ِمن الذ ِل وك ِبره تك ِبيرا‬
Hana msaidizi kwa udhalili, hivyo mtukuze mno.

َ‫َا ْل َح ْم ُد ِل ّٰل ِه ب َج ِم ْيع َم َح ِام ِد ِه ُك ِّل َها َع َلى َج ِم ْيع ِن َع ِم ِه ُك ِّلها‬


ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu kwa yote
anayostahili ­kusifiwa juu ya neema Zake zote.

ْ َ ْ ُ َ َ َ ُ َ َ ْ ُ ْ ُ َ َّ َ ُ َ ّٰ ُ ْ َ ْ َ
‫الحمد ِلل ِه ال مضاد له ِفي مل ِك ِه وال من ِازع له ِفي أم ِر ِه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu asiye na
­mkabala katika ufalme Wake, wala mpinzani katika
amri Yake.

ُ‫َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َّالذ ْي َال َشرْي َك َل ُه ف ْي َخ ْلقه َواَل َشب ْي َه َله‬


ِ ِِ ِ َ ِ ِ ِ ِ
َ
‫ِف ْي عظ َم ِت ِه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu ambaye hana
mshirika katika kuumba Kwake, wala mwenza katika
utukufu Wake.

ُ ‫َا ْل َح ْم ُد ِل ّٰل ِه ْال َفا�ش ْي في ْال َخ ْلق‬


ُ‫امر ُه َو َح ْم ُده‬
ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu mwenye
­kueneza miongozo kwa viumbe.

25

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 25 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫الظاهر ب ْال َك َرم َم ْج ُده‬


َّ
ِ ِ ِ ِ
Na utukufu wake uko dhahiri kwa uzuri wa ukarimu
Wake.

ُ‫ْال َباسط ب ْال ُج ْود َي َده‬


ِ ِ ِ ِ
Mwenye kufumbua mkono Wake kwa ukarimu Wake.

ُ‫ص َخ َزائ ُنه‬


ُ ُ‫َا َّلذ ْي َال َت ْنق‬
ِ ِ
Ambaye hazina Yake haipunguki.

ً‫َواَل َتزْي ُد ُه َك ْث َر ُة ْال َع َط ِاء إ اَّل ُج ْو ًدا َو َك َرما‬


ِ ٍ
Wala wingi wa utoaji hauzidishi ila ukarimu.

ُ‫إ َّن ُه ُه َو ْال َعزْي ُز ْال َو َّهاب‬


ِ ِ
Hakika Yeye ni Mwenye uwezo na Mtoaji.

ْ‫م ْن َكثير‬ ً‫َ َّ ُ َّ ّ ْ َ ْ َ ُ َ َ ْ لا‬


ٍ ِ ِ ‫اللهم ِإ ِني أسئلك ق ِلي‬
Ewe Mungu wangu! Hakika mimi nakuomba
­kichache toka kwenye kingi,

26

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 26 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ ْ َ ْ َ َ ََ
‫مع حاج ٍة ِبي ِإلي ِه ع ِظيم ٍة‬
Japokuwa haja yangu kwacho ni kubwa.

ٌ‫اك َع ْن ُه َق ِد ْي ٌم َو ُه َو ِع ْن ِد ْي َك ِث ْير‬
َ ‫َوغ َن‬
ِ
Na kutokukihitaji Kwako ni kwa kudumu, nacho
kwangu ni kingi,

ٌ‫َو ُه َو َع َل ْي َك َس ْه ٌل َي ِس ْير‬
Na kwako ni chepesi na rahisi.

ْ‫َا َّلل ُه َّم إ َّن َع ْف َو َك َع ْن َذ ْنبي‬


ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Hakika msamaha wako wa
dhambi zangu,

َ َ َ
‫َوت َج ُاو َز َك َع ْن خ ِط ْيئ ِت ْي‬
Na usamehevu Wako makosa yangu,

ْ‫ص ْف َح َك َع ْن ُظ ْل ِمي‬
َ ‫َو‬
Usamehevu Wako wa dhulma yangu,

27

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 27 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫َو ِس ْت َر َك َع َلى َقب ْيح َع َم ِلي‬


ِ ِ
Na sitara Yako juu ya ubaya wa amali yangu,
َ ْ
‫َو ِحل َم َك َع ْن ك ِث ْي ِر ُج ْر ِم ْي‬
Na upole Wako dhidi ya wingi wa makosa yangu,

ْ‫ان ِم ْن َخ َط ِا ْي َو َع ْم ِدي‬
َ ‫ع ْن َد َما َك‬
ِ
Pindi nikukoseapo kwa bahati mbaya na makusudi,
َ َ‫ا‬ ََ َ َ ْ َ
‫اط َم َع ِن ْي ِف ْي ا ْن ا ْسئل َك َما ل ا ْس َت ْو ِج ُب ُه ِم ْن َك‬
Yamenitamanisha nikuombe yale nisiyopaswa kutoka
kwako.
َ‫َا َّلذ ْي َر َز ْق َتني م ْن َر ْح َمتك‬
ِ ِ ِ ِ
Ambayo umeniruzuku toka kwenye rehema Zako,
ُ َ
‫َوا َرْي َت ِن ْي ِم ْن ق ْد َرِت َك‬
Na umenionyesha toka kwenye uwezo Wako,
َ‫َو َع َّر ْف َتن ْي م ْن ا َج َابتك‬
ِ ِ ِ ِ
Na umenitambulisha toka kwenye majibu Yako.

28

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 28 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً‫َفص ْر ُت َا ْد ُع ْو َك آمنا‬
ِ ِ
Hivyo nimekuwa nikikuita huku nikiwa ni mwenye
amani,
ْ َُ َ
‫َوا ْسئل َك ُم ْس َتا ِن ًسا‬
Na nikukuomba huku nikiwa sina upweke.

َ َ‫اَ َ ً َ ا‬
‫ل خا ِئفا ول و ِجل‬
Sina khofu wala woga,
َ َ ‫ُمد اًّل َع َل ْي َك ف ْي َما َق‬
‫ص ْد ُت ِف ْي ِه ِال ْي َك‬ ِ ِ
Bali nina imani juu Yako kuhusu yale niliyokusudia
Kwako.

َ‫َفإ َّن َا ْب َط َأ َع ّن ْي َع َت ْب ُت ب َج ْهل ْي َع َل ْيك‬


ِ ِ ِ ِ
Likawiyapo (jibu) hukulalamikia kwa ujinga wangu
juu Yako,

ْ‫َو َل َع َّل َّال ِذ ْي َا ْب َط َأ َع ّن ْي ُه َو َخ ْي ٌر لي‬


ِ ِ
Na huenda ulilolikawiza kwa ajili yangu ndio kheri
kwangu.

29

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 29 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ْ‫ْ َ َ َ أ‬
ْ‫ال ُمور‬
ِ ‫ِل ِعل ِمك ِبعا ِقب ِة‬
Kwa kuwa Wewe ndiye Mjuzi wa matokeo ya
baadaye.
َ َ َ ْ َ ً ْ َ ً ْ َ ََ ْ ََ
‫ص َب َر َعلى َع ْب ٍد ل ِئ ْي ٍم ِم ْن َك َعل َّي‬ ‫فلم ار مولى ك ِريما ا‬
Sijamwona bwana mkarimu mwenye kumvumilia mja
muovu kushinda Wewe ulivyo juu yangu.

َ‫َيا َ ّب ْي إ َّن َك َت ْد ُع ْون ْي َف َأ ْو َلي َع ْنك‬


ِ ِ ِ‫ر‬
Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika wewe waniita, nami
nakukimbia.
َ ُ َّ َ َ َ َ َّ َ ُ َّ َ َ َ َ
‫ض ِإل ْي َك‬ ‫وتتحبب ِإلي واتبغ‬
Unaonyesha huba kwangu, nami naonyesha chuki
kwako.

َ‫َو َت َت َو َّد ُد إ َل َّي َفلاَ َا ْق َب ُل م ْنك‬


ِ ِ
Unaonyesha mapenzi kwa ajili yangu lakini sikubali,

َّ ‫َك َأ َّن ل َي‬


َ‫الت َط ُّو َل َع َل ْيك‬
ِ
Kana kwamba nina nguvu juu Yako.

30

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 30 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫الر ْح َم ِة لي‬
َّ َ‫َف َل ْم َي ْم َن ْع َك َذال َك من‬
ِ ِ ِ
Lakini hayo yote hayajakuzuia kunipa rehema Zako

َّ‫َو ْاإل ْح َسان إ َلي‬


ِ ِ ِ
Na ihsani Yako.
َ‫ضل َع َل َّي ب ُج ْود َك َو َك َرمك‬ ُّ ‫الت َف‬
َّ ‫َو‬
ِ ِ ِ ِ
Wala kunifanyia fadhila kwa ukarimu wako na wema
Wako.

َ‫َفا ْر َح ْم َع ْب َد َك ْال َجاهل‬


ِ
Basi mrehemu mja Wako mjinga.
َ‫ضل ا ْح َسانك‬ْ ‫َو ُج ْد َع َل ْيه ب َف‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Mkirimu kwa fadhila za ihsani Yako.

ٌ‫إ َّن َك َج َو ٌاد َكرْيم‬


ِ ِ
Hakika Wewe ni Mkarimu, Mwema.
ْ ُ ْ ْ ُ ْ ُ ْ‫َ ْ َ ْ ُ ّٰ َ َ م‬
‫الحمد ِلل ِه م ِالك الل ِك مج ِري الفل ِك‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, Mmiliki wa
ufalme, Mwendeshaji wa meli,

31

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 31 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ ْ َ َّ ّ َ ُ
‫الري ِاح ف ِال ِق ا أِلصب ِاح‬
ِ ‫مس ِخ ِر‬
Mpelekaji wa pepo, Mletaji wa machweo,
َ‫ْ م‬
‫الد ْي ِن َر ِ ّب ال َع ِال ْي َن‬
ّ ‫َد َّيان‬
ِ ِ
Mamlaka ya siku ya malipo na Mola Mlezi wa
­viumbe.
ْ َ ْ َ ْ َ َ ّٰ ُ ْ َ ْ َ
‫الحمد ِلل ِه على ِحل ِم ِه بعد ِعل ِم ِه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu kwa
­ustahmilivu Wake baada ya elimu Yake.
ُ َ ّٰ َْ
‫َو ال َح ْم ُد ِلل ِه َعلى َع ْف ِو ِه َب ْع َد ق ْد َرِت ِه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu kwa msamaha
Wake baada ya uwezo Wake.

َ َ ْ َ َ ‫َ َ ْ َ ْ ُ ّٰ َ َ ُ ْ ل‬
‫و الحمد ِلل ِه على طو ِ انا ِت ِه ِفي غض ِب ِه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu kwa urefu wa
subira Yake ana­poghadhibika,
َ َ
‫َو ُه َو ق ِاد ٌر َعلى َما ُي ِرْي ُد‬
Na Yeye ni Mwenye uwezo juu ya lile alitakalo.

32

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 32 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َْ ْ َ ّٰ ُ ْ َ ْ َ
‫الحمد ِلل ِه خ ِال ِق الخل ِق‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Muumba wa
viumbe,

ْ ‫الر ْزق َفالق ْال‬


‫ص َب ِاح‬ ّ ‫اس ِط‬ َ
‫ب‬
ِ
ِ‫ِ ِ ِ إ‬ ِ
Mtoaji wa riziki, Mletaji wa machweo,

َ ْ ْ‫ْ َ لاَ َ إ‬
‫الكر ِام‬ِ ‫ِذي الج ِل و‬
Mwenye utukufu na heshima,

ْ ْ‫َ ْ َ ْ َ إ‬
‫الن َع ِام‬
ِ ‫والفض ِل و‬
Mwenye fadhila na neema.

َ‫َ لا‬ َّ َ
‫ال ِذ ْي َب ُع َد ف ُي َرى‬
Ambaye kajiweka mbali hawezi kuonekana,

َّ ‫َو َق ُر َب َف َشه َد‬


‫الن ْج َوى‬ ِ
Ambaye yu karibu ashuhudia siri.

33

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 33 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ ََ َ َ ََ
‫تبارك وتعالى‬
Ametakasika na kutukuka jina Lake.

ُ‫س َل ُه ُم َناز ٌع ُي َعاد ُله‬


َ ْ‫َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َّالذ ْي َلي‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, ambaye hana
mpinzani anayelingana naye,

ُ‫َواَل َشب ْي ٌه ُي َشاك ُله‬


ِ ِ
Wala shabihi wa namna Yake,

ُ‫َواَل َظه ْي ٌر ُي َعاض ُده‬


ِ ِ
Wala msaidizi ampaye nguvu.

َّ َ ْ َّ َ َ َ
‫قهر ِب ِعزِت ِه األ ِعز ِاء‬
Kwa nguvu Zake kuwatenza nguvu wababe,

ُ‫اض َع ِل َع َظ َم ِت ِه ْال ُع َظ َماء‬


َ ‫َو َت َو‬
Na kwa utukufu Wake wamenyenyekea wakuu.

34

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 34 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫َف َب َل َغ ب ُق ْد َرِت ِه َما َي َشاء‬


ِ
Hivyo kwa uwezo Wake akayafikia ayatakayo.

ْ‫َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َّالذ ْي ُيج ْي ُبن ْي ح ْي َن ُا َناديه‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, ambaye
­hunijibu nimwitapo,

ْ‫َو َي ْس ُت ُر َع َل َّي ُك َّل َع ْو َر ٍة َو َأ َنا َا ْعصيه‬


ِ ِ
Husitiri kila aibu yangu ilihali mimi namuasi,

ْ‫الن ْع َم َة َع َل َّي َفلاَ ُا َجازيه‬


ّ ‫َو ُي َع ّظ ُم‬
ِ ِ ِ ِ
Huongeza neema kwangu na wala simlipi.

ْ‫َف َك ْم ِم ْن َم ْو ِه َب ٍة َه ِن ْي َئ ٍة َق ْد َا ْع َطا ِني‬


Kwani ni hiba ngapi tulivu amenipa.

ْ‫وف ٍة َق ْد َك َفا ِني‬


َ ُ َ َْ َ َ
‫وع ِظيم ٍة مخ‬
Ni makubwa mangapi ya kukhofisha ameniondolea.

35

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 35 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫َو َب ْه َج ٍة ُم ْو ِن َق ٍة َق ْد َا َرا ِني‬


Ni furaha ngapi changamfu amenionyesha.

ً َ َُْ
‫فاث ِن ْي َعل ْي ِه َح ِامدا‬
Hivyo namtukuza kwa kumsifu,

ً‫َو َا ْذ ُك ُر ُه ُم َس ّبحا‬
ِ
Na ninamtaja kwa kumsabihi.

َ‫ّٰ َّ ا‬ َْ
‫ال َح ْم ُد ِلل ِه ال ِذ ْي ل ُي ْه َت ُك ِح َج ُاب ُه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, ambaye pazia
Yake ­hairaruriwi.

ُ‫َواَل ُي ْغ َل ُق َب ُاب ُه َواَل ُي َر ُّد َسائ ُله‬


ِ
Wala mlango Wake haufungwi, Wala muombaji
Kwake hanyimwi.

ُ َ َ‫ا‬
‫َول ُيخ َّي ُب ِآمل ُه‬
Wala matumaini yake hayafelishwi.

36

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 36 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َّالذ ْي ُي ْؤم ُن ْال َخائف ْين‬


ِِ ِ ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, ambaye
­huwapa amani wenye hofu.

َّ ‫َو ُي َن ّجي‬
‫الص ِال ِح ْي َن‬ ِ
Huwaokoa waja wema.

ْ ‫َو َي ْر َف ُع مْالُ ْس َت‬


َ‫ض َعف ْين‬
ِ
Huwanyanyua waliodhoofishwa.

َ‫ض ُع مْالُ ْس َت ْكبرْين‬


َ ‫َو َي‬
ِِ
Huwafedhehesha wenye viburi.

َ ُ ْ َ ْ ََ ً ْ ُُ ُ َُْ
َ‫آخرْين‬
ِ ‫ويه ِلك ملوكا ويستخ ِلف‬
Huwaangamiza wafalme, na (sehemu zao) huwaweka
wengine.

َ‫َو َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َقاصم ْال َج َّبارْين‬


ِ ِ ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu. Mwenye
­kuwafutilia mbali majabari,

37

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 37 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ْ ُ
َ‫الظال ْين‬
ِ ِ‫م ِبي ِر م‬
Mwenye kuwaangamiza madhalimu,

َ‫ُم ْد ك ْال َها ب ْين‬


ِ‫ِر‬ ِ ‫ِر‬
Mwenye kuwafikia wanaomkimbia,

َّ
َ‫الظال ْين‬ ََ
ِ ِ‫نك ِال م‬
Mtoa adhabu kwa madhalimu,

َ‫صرخ ْين‬ ْ ‫صرْيخ مْالُ ْس َت‬


َ
ِِ ِِ
Msaidizi wa wenye kulia kwa ukelele wakiomba
msaada.

َّ
َ‫الطالب ْين‬ َ ‫موضع َح‬َ
ِِ ‫ات‬
ِ ‫اج‬ ِِ
Na kwake yeye ndiko kwenye mahitaji ya watafutaji,

َ‫ُم ْع َت َمد مْالُ ْؤمن ْين‬


ِِ ِ
Na Yeye ndiye tegemeo la waumini.

38

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 38 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ‫َا ْل َح ْم ُد ِل ّٰل ِه َّال ِذ ْي م ْن َخ ْش َي ِت ِه َت ْر َع ُد‬


َ‫الس َم ُاء َو ُس َّك ُانها‬ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, Ambaye kwa
kumwogopa Yeye mbingu na wakazi wake hutikisika,

َ‫ض َو ُع َّما ُرها‬ َ ْ‫َ َ ْ ُ ُ أ‬


ُ ‫ال ْر‬ ‫وترجف‬
Na milima na wakazi wake hugwaya,

َ‫َو َت ُم ْو ُج ْالب َح ُار َو َم ْن َّي ْس َب ُح ف ْي َغ َم َر ِاتها‬


ِ ِ
Na bahari hufanya mawimbi ikiwa na waogeleaji
wake.

ْ‫َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َّالذ ْي َه َد َانا ل َه َذا َو َما ُك َّنا ل َن ْه َتد َي َل ْو اَل َأن‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
ُ‫َه َد َانا هللا‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, Ambaye
­ametuongoza kwenye hili, na tusingeweza kuongoka
lau Mwenyezi Mungu asingetuongoza.

ْ‫َا ْل َح ْم ُد ل ّٰله َّالذ ْي َي ْخ ُل ُق ُو َل ْم ُي ْخ َلق‬


ِ ِ ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu, Ambaye
­huumba na hajaumbwa,

39

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 39 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫َو َي ْر ُز ُق َواَل ُي ْر َزق‬


Huruzuku na wala hapewi riziki,

ُ‫َو ُي ْط ِع ُم َواَل ُي ْط َعم‬


Hulisha na wala halishwi,

َ‫َو ُيم ْي ُت ْا َأل ْح َياء‬


ِ
Huwafisha walio hai,
َ ْ َ ْ‫َ ُ ْ م‬
‫ويح ِيي الوتى‬
Huwapa uhai walio wafu,

ُ‫َو ُه َو َح ٌّي اَل َي ُم ْوت‬


Yeye ni hai asiyekufa,

ُ‫ب َي ِد ِه ْال َخ ْير‬


ِ
Kheri iko mkononi mwake.

ْ‫َو ُه َو َع َلى ُك ّل َش ْيئ َقدير‬


ٍ ِ ٍ ِ
Na Yeye ni Muweza wa kila kitu.

40

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 40 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad.

‫بد َك َو َر ُس ْوِل َك‬


ِ ‫ع‬
َ
Mja Wako na Mtume Wako,

َ‫صف ّي َك َو َحب ْيبك‬َ ‫َو َأم ْين َك َو‬


ِ ِ ِِ ِ ِ
Mwaminifu Kwako, mteule Wako na hababi Wako,

ََ َ
‫َوخ َي َرِت َك َم ْن خل ْق َك‬
Chaguo Lako bora kati ya viumbe Wako,

َ‫َو َحافظ س ّر َك َو ُم َب ّلغ ر َس َالتك‬


ِ ِ ِِ ِ ِ ِ ِ
Muhifadhi wa siri Yako na mfikishaji wa ujumbe
Wako,

َ‫ض َل َو َا ْح َس َن َو َا ْج َم َل َو َا ْك َمل‬
َ ‫َا ْف‬
Aliye mbora zaidi, mwema zaidi, mzuri mno,
­mkamilifu zaidi,

41

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 41 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َو َا ْز َكى َو َا ْن َمى َو َا ْط َي َب َو َا ْط َه َر َو َا ْس َنى َو َا ْك َثر‬


Takasifu zaidi, itukuzwayo zaidi, tukufu mno na safi
mno,
َ َّ ْ َ َ ْ َّ َ
‫صل ْي َت َو َب َارك َت َوت َر َّح ْم َت َوت َح َّنن َت َو َسل ْم َت َعلى‬ ‫ما‬
َ َْ َ
‫ا َح ٍد ِّم ْن ِع َب ِاد َك َوان ِب َيا ِئ َك َو ُر ُس ِل َك َو ِص ْف َو ِت َك َوا ْه ِل‬
َْ َ َْ
‫الك َر َام ِة َعل ْي َك ِم ْن خل ِق َك‬
Kushinda ile uliyemrehemu, kumbariki, kumhurumia
na kumtakia rehma yeyote miongoni mwa waja Wako,
Manabii Wako, Mitume Wako, wateule Wako na we-
nye heshima Kwako miongoni mwa ­viumbe Wako.

َ‫ص ّلي َع َلى َعل ّي َأم ْير مْالُ ْؤمن ْين‬َ ‫َا َّلل ُه َّم‬
ِِ ِ ِ ٍ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Ali Jemedari wa
Waumini,

َ‫َو َو�ص ّي َر ُس ْول َر ّب ْال َع مَال ْين‬


ِ ِ ِ ِ ِ
Wasii wa Mtume wa Mola Mlezi wa viumbe.

‫َع ْب ِد َك َو َو ِل ِّي َك‬


Mja Wako na kipenzi Chako.

42

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 42 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َو َاخي َ ُس ْول َك َو ُح َّجت َك َع َلى َخ ْلقك‬


ِ ِ ِ ‫ِ ر‬
Binamu wa Mtume Wako na hoja Yako juu ya viumbe
Wako.

ْ ْ ُْ
‫َو َآي ِت َك الك ْب َرى َوال َن َب ِأ ال َع ِظ ْي ِم‬
Alama Yako kubwa na habari kuu.

َّ
َ‫الط ِاهر ِة‬ َّّْ ََ َّ َ
‫الص ِديق ِة‬
ِ ‫وص ِلي على‬
Na mrehemu mkweli, mtoharifu,
َ‫ْ م‬ َّ ‫َفاط َمة‬
‫الز ْه َر ِاء َس ِّي َد ِة ِن َس ِاء ال َع ِال ْي َن‬ ِ ِ
Fatima Zahra, Bibi mbora kushinda wanawake wote
wa ulimwengu.

َ ْ َّ َ ْ ََ َّ َ
‫وص ِلي على ِسبط ِى الرحم ِة‬
Warehemu wajukuu wawili wa rehema,

ْ َ َ َ
‫اي ال ُه َدى‬
ِ ‫وِامام‬
Na maimamu wa uongofu,

43

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 43 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ‫َا ْل َح َسن َو ْال ُح َس ْين َس ّي َد ْي َش َباب َا ْهل ْال َجنة‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Hasan na Husein, Mabwana wawili wa vijana wa
Peponi.
َ ْ ْ ُ ْ‫َ َ ّ َ َ َ َّ م‬
، ‫وص ِلي على أ ِئم ِة الس ِل ِمين‬
Warehemu maimamu wa waislamu:

ْ َ ُ ْ ّْ َ
‫ع ِل ِي ب ِن الحسي ِن‬
Ali bin Husein,

‫َو ُم َح َّم ِد ْب ِن َع ِل ّ ٍي‬


Muhammad bin Ali,
َ
‫َو َج ْعف ِر ْب ِن ُم َح َّم ٍد‬
Jafar bin Muhammad,
َ
‫�سى ْب ِن َج ْعف ٍر‬
َ ‫َو ُم ْو‬
Musa bin Jafar,

َ ‫َو َعل ّي ْبن ُم ْو‬


‫�سى‬ ِ ِ ِ
Ali bin Musa,

44

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 44 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

‫َو ُم َح َّم ِد ْب ِن َع ِل ّ ٍي‬


Muhammad bin Ali,

‫َو َع ِل ّ ِي ْب ِن ُم َح َّم ٍد‬


Ali bin Muhammad,

ّ‫َو ْال َح َسن ْبن َع ِلي‬


ٍ ِ ِ
Hasan bin Ali,

ّ‫ف ْال َه ِادي مْالَ ْه ِدي‬ ََ ْ َ


ِ ‫والخل‬
ِ ِ
mrithi na mwongozaji, Mahdi

َ‫ُح َّجت َك َع َلى ع َبادك‬


ِ ِ ِ
Hoja Wako juu ya waja Wako,
َ‫َ ُ َ َ َ ْ لا‬
‫ِد َك‬ ‫وأمنا ِئك ِفي ِب‬
Na waaminifu katika nchi Yako.
ً َ َ ًَْ َ ً َٰ
‫صلوة ك ِثيرة دا ِئمة‬
Warehemu rehema nyingi za kudumu.

45

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 45 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫ص ّلي َع َلى َول ّي َا ْمرك‬َ ‫َا َّلل ُه َّم َو‬


ِ ِِ ِ
Ewe Mungu wangu! Mrehemu mwangalizi wa jambo
Lako,

َ ُ ْ‫م‬ َْ
‫القا ِئ ِم الؤ َّم ِل‬
Mwakilishi mwenye kutarajiwa,

َ َ ْ ُ ْ‫َ ْ َ ْ م‬
‫والعد ِل النتظ ِر‬
Na mwadilifu mwenye kungojewa.

َ ُ ْ‫م‬ َ َ‫َ ُ َّ ُ َ لا‬


‫ِئك ِت َك الق َّرِب ْي َن‬ ‫وحفه ِبم‬
Mzungushie Malaika Wako walio wa karibu,

ُ ُ ْ ُْ ُ ْ ََّ
‫وأ ِيده ِبرو ِح القد ِس‬
Msaidie kwa Raho mtakatifu,

َ‫ْ م‬
‫َيا َر َّب ال َع ِال ْي َن‬
Ewe Mola Mlezi wa viumbe.

46

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 46 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ ‫َا َّلل ُه َّم‬


َّ ‫اج َع ْل ُه‬
َ‫الداع َي إ َلى ك َتابك‬
ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Mfanye awe mlinganizi kwenye
Kitabu Chako,

َ
‫َوالقا ِئ َم ِب ِد ْي ِن َك‬
Na msimamizi wa dini Yako,

ْ َ ْ َ ْ َّ َ ْ َ ْ َ ْ َ َ ْ َ ْ ُ ْ ْ َ ْ
‫ض كما استخلفت ال ِذين ِمن قب ِل ِه‬ِ ‫ِاستخ ِلفه ِفي األر‬
Mfanye Khalifa ardhini kama ulivyowafanya
­makhalifa wale wa kabla yake.

َ ‫َم ّك ْن َل ُه د ْي َن ُه َّالذي ا ْ َت‬


ُ‫ض ْي َته‬
‫ِ ر‬ ِ ِ
Mwimarishie dini yake uliyoiridhia.

ً ْ َ َ ْ َ ْ َ ْ ُ ْ َْ
‫اب ِدله ِمن بع ِد خو ِفه امنا‬
Mpe amani baada ya khofu.

ً ْ َ َ ُ ْ ُ َ‫َ ْ ُ ُ َ ا‬
‫يعبدك ل يش ِرك ِبك شيئا‬
Akuabudu bila kukushirikisha na chochote.

47

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 47 6/16/2016 4:29:22 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ ْ َ َ ُ َّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ا ِعزه واع ِزز ِب ِه‬
Ewe Mungu wangu! Mpe nguvu na kupitia yeye wape
wengine nguvu,

ْ ُ ‫َو ْان‬
‫ص ْر ُه َوان َت ِص ْر ِب ِه‬
Msaidie na kupitia yeye wasaidie wengine.

ً ْ َ ً ْ َ ُْ ُ ْ َ
‫وانصره نصرا ع ِزيزا‬
Msaidie msaada uliotukuka.

ً ً َ َ ْ
‫َواف َت ْح ل ُه ف ْتحا َي ِس ْيرا‬
Mpe ushindi kirahisi.

ً ْ ًَ َ ُْ َ َُْ ْ َُ ْ َ ْ َ
‫واجعل له ِمن لدنك سلطانا ن ِصيرا‬
Mpe mamlaka saidizi kutoka Kwako.

َ َ ْ َ َّ َ
‫الل ُه َّم اظ ِه ْر ِب ِه ِد ْي َن َك َو ُس َّنة ن ِب ِّي َك‬
Ewe Mungu wangu! Kupitia yeye idhihirishe dini
Yako na Sunna ya Nabii Wako,

48

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 48 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫�ش ْيء م َن ْال َح ّق َم َخ َاف َة َا َحد ّمن‬


َ َ ْ َ ْ َ َ‫َ َّ ا‬
‫حتى ل يستخفى ب‬
ِ ٍ ِ ْ َِ ْ ٍ ِ ِ
‫الخل ِق‬
Mpaka sehemu yoyote ya haki isifichikane kwa
­kumwogopa yeyoye kati ya viumbe.

َ ْ َ َ ْ َ ْ َ ْ َ ُ َ ْ َ َّ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ِإنا نرغب ِإليك ِفي دول ٍة ك ِريم ٍة‬
Ewe Mungu wangu! Hakika sisi tuna hamu mno na
dola ya heshima toka Kwako,

ُ‫ُتع ُّز ب َها ْال ْسلاَ َم َو َا ْه َله‬


ِ‫ِ ِ إ‬
Ambayo kwayo Uislamu na watu wake utapata nguvu,

ُ‫اق َو َا ْه َله‬ ّ ‫َو ُتذ ُّل ب َها‬


َ ‫الن َف‬
ِ ِ ِ
Na unafiki na watu wake utadhalilika.

َ ‫الد َعاة إ َلى َط‬


َ‫اعتك‬ ُّ ‫َو َت ْج َع ُل َنا ف ْي َها م َن‬
ِ ِِ ِ ِ
Utujalie humo tuwe walinganizi kwenye utii Wako,

َ‫َو ْال َق َادة إ َلى َسب ْيلك‬


ِ ِ ِِ
Na viongozi kwenye njia Yako.

49

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 49 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫الد ْن َيا َو آْال ِخر ِة‬


ُّ ‫َو َت ْر ُز ُق َنا ب َها َك َر َام َة‬
ِ
Uturuzuku kwayo heshima ya Dunia na Akhera.

ُ‫َا َّلل ُه َّم َما َع َّر ْف َت َنا م َن ْال َح ّق َف َح ّم ْل َناه‬


ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Haki uliyotuelimisha tusaidie
tuitekeleze,

ُ‫ص ْرَنا َع ْن ُه َف َب ّل ْغ َناه‬


ُ ‫َو َما َق‬
ِ
Na tuliyoipuuzia tujaalie tuifikie.

َ‫ص ْد َعنا‬ ْ َ َ َ َ َ ْ ُ ْ‫َ َّ ُ َّ َ م‬


َ ‫اش َع ْب به‬
ِِ ‫اللهم الم ِب ِه شعثنا و‬
Ewe Mungu wangu! Kupitia yeye tusuluhishie mambo
yetu na u
­ nganisha makun­di yetu.

َ‫َوا ْ ُت ْق به َف ْت َق َنا َو َك ّث ْر به ق َّل َتنا‬


ِ ِِ ِ ِِ ‫ر‬
Weka pamoja mtengano wetu na kithirisha uchache
wetu.

َ‫اغن به َعائ َلنا‬


ْ َ َ َ َّ ْ ْ ََ
ِ ِ ِ ِ ‫واع ِزز ِب ِه ِذلتنا و‬
Upe heshima udhalili wetu na tajirisha familia zetu.

50

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 50 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ََ ْ َ ْ ُ ْ َ َ َ ْ َ ْ َ ْ َ
‫ض ِب ِه عن مغر ِمنا واجبر ِب ِه فقرنا‬
ِ ‫واق‬
Mlipie deni mdaiwa wetu na ondoa ufakiri wetu.
َ َ ْ ُ ْ ّ َ َ َ َ َّ َ َّ ُ َ
‫وسد ِب ِه خلتنا وي ِسر ِب ِه عسرنا‬
Ziba pengo la mahitaji yetu na rahisisha mazito yetu.
َ َ ْ َ َّ ُ َ َ َ ْ ُ ُ ْ ّ َ َ
‫وب ِيض ِب ِه وجوهنا وفك ِب ِه اسرنا‬
Zing’arishe nyoyo zetu na wape uhuru mateka wetu.
َ ْ َ َ ْ ََْ َ ََ ََ ْ ََْ
‫اعي ِدنا‬
ِ ‫وان ِجح ِب ِه طلبتنا وان ِجز ِب ِه مو‬
Tufanikishie maombi yetu na tutimizie ahadi yetu.

َ‫اس َتج ْب به َد ْع َو َت َنا َو َا ْعط َنا به ُس ْؤ َلنا‬


ْ ‫َو‬
ِِ ِ ِِ ِ
Tujibu dua yetu na tupe maombi yetu.

َ‫الد ْن َيا َواآلخ َرة َآم َالنا‬


ُّ ‫َو َب ّل ْغ َنا به م َن‬
ِ ِ ِ ِِ ِ
Tutimizie matarajio yetu duniani na Akhera.

َ‫َو َا ْعط َنا به َف ْو َق َر ْغ َبتنا‬


ِ ِِ ِ
Na utupe zaidi ya mategemeo yetu.

51

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 51 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َيا َخ ْي َر مْالَ ْس ُؤ ْول ْي َن َو َا ْو َس َع مْالُ ْعط ْين‬


ِ ِ
Ewe mbora wa waombwaji na mkuu wa watoaji.
َ َْ ْ ْ ََ ََْ ُ ُ
َ‫ظ ُق ُل ْوبنا‬ ْ
ِ ‫ي‬‫غ‬ ‫ه‬ ‫ب‬
ِِ ِ‫ب‬ ‫ه‬ ‫ذ‬ ‫ا‬‫و‬ ‫ا‬ ‫ن‬ ‫ر‬‫و‬ ‫د‬ ‫ص‬ ‫ه‬
ِ ِ ِ ‫ِا‬
‫ب‬ ‫ف‬ ‫ش‬
Kupitia yeye viponye vifua vyetu na ondoa vinyongo
vya nyoyo zetu,

َ‫ف ف ْيه م َن ْال َح ّق بإ ْذنك‬


َ ُْ َ
‫ل‬ ‫ت‬ ‫اخ‬ ‫ا‬ ‫ل‬
َ ْ َ
ِ ِِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ‫واه ِد ِ ِ م‬
‫ه‬ ‫ب‬ ‫ا‬ ‫ن‬
Tuongoze kwa idhini Yako kwenye haki
­waliyotofautiana,

ْ َ ْ ُ َ َ ُ َ َ ْ َ ْ َ َ َّ
‫اط مست ِقي ٍم‬ٍ ‫ِإنك ته ِدي من تشاء ِإلى ِصر‬
Hakika wewe humwongoza umtakaye kwenye njia
nyoofu.
َّ ُ َ َ َ ّ ُ َ ََ َ ُ ْ َ
‫ص ْرنا ِب ِه على عد ِوك وعد ِونا‬ ‫وان‬
Na kupitia yeye tusaidie dhidi ya adui Wako na adui
wetu.
ْ ٰ
‫ِإل َه ال َح ِ ّق ِآم ْي َن‬
Ewe Mungu wa haki, amin.

52

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 52 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ َ َ ُ َ َ َ َ ّ َ َ ْ َ َ ْ َ ُ ْ َ َّ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ِإنا نشكو ِإليك فقد ن ِب ِينا صلواتك علي ِه و ِآل ِه‬
Ewe Mungu wangu! Hakika sisi tunakushtakia
­kutoweka kwa Mtume wetu, rehema
Zako ziwe juu yake na juu ya kizazi chake,

َ َ َْ َ َ
‫َوغ ْي َبة َوِل ِّي َنا َوكث َرة َع ُد ّ ِونا‬
ghaiba ya walii wetu na uwingi wa maadui zetu,

َ‫َوق َّل َة َع َدد َنا َوش َّد َة ْالف َتن بنا‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ
uchache wa idadi yetu na ukali wa fitina kwetu,
َ َّ ‫َو َت َظ ُاه َر‬
‫الز َم ِان َعل ْي َنا‬
na ushindi wa zama dhidi yetu.

َ َّ َ ُ ََ ّ َ َ
‫فص ِل على محم ٍد و ِآل ِه‬
Hivyo mrehemu Muhammad na kizazi chake,
ُ ُ َ َ َ َ
‫َوا ِع َّنا َعلى ذ ِل َك ِبف ْت ٍح ِم ْن َك ت َع ِ ّجل ُه‬
Na tusaidie katika hilo kwa ushindi wa haraka toka
Kwako.

53

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 53 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫ض ّر َت ْكش ُفه‬


ُ ‫َوب‬
ِ ٍ ِ
Na kwa kutuondolea madhara,
ُ ْ ََ
‫ص ٍر ت ِع ُّز ُه‬ ‫ون‬
Kwa msaada uupao nguvu,

ُ‫َو ُس ْل َطان َحق ُت ْظه ُره‬


ِ ٍ ِ
Kwa mamlaka ya haki uidhihirishayo,
ُّ ُ
‫َو َر ْح َم ٍة ِم ْن َك ت َج ِلل َن َاها‬
Kwa rehema utupazo heshima kwazo toka Kwako,
ُْ
‫َو َعا ِف َي ٍة ِم ْن َك تل ِب ُس َن َاها‬
Na kwa afya utuvalishayo toka Kwako.

َّ ‫ب َر ْح َم ِت َك َيا َا ْر َح َم‬
‫الر ِاح ِم ْي َن‬ ِ
Kwa rehema Zako ewe mbora wa warehemevu.

54

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 54 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Tano

D ua hii inazungumzia starehe za Peponi na adhabu za ndani


ya Jahannam. Kuamini juu ya Akhera ndio mzizi wa mwisho
muhimu wa dini na Dua hii ni ufuatiliaji unaostahili wa Dua al-Ifti-
tah ambayo inazungumzia juu ya misingi mingine ya Imani.
Thawabu na mateso yanayowangojea wanadamu yanaelezewa
kwa kina­ganaga kwa ajili ya muumini kuweza kuyabaini hayo.
Haitoshi tu kibusara kuamini juu ya Akhera. Kama vile tu inavyo-
pendekezwa mtu kujifikiria anavyokufa ili aweze kujiandaa kwa
kifo kwa uhakika, ni muhimu vilevile kujifikiria mtu kwam­ba
yuko Peponi au Jahannam kwa ajili ya uimarishaji wa imani juu
ya Akhera.

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa kurehemu.
َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫ص ِلي َعلى ُم َح َّم ٍد َو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ ‫اللهم‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad, na Aali
Muhammad.
ْ ََ َّ ‫َا َّلل ُه َّم ب َر ْح َم ِت َك في‬
‫الص ِال ِح ْي َن فا ْد ِخل َنا‬ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Kwa rehema Zako tujumuishe na
wachamungu.

55

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 55 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َوف ْي ع ّل ّي ْي َن َف َا ْ َف ْعنا‬
‫ِ ِِ ِ ر‬
Tunyanyue tuwe pamoja na wenye heshima.

ْ ‫َوب َك ْأس م ْن َمع ْين م ْن َع ْين َس ْل َسب ْيل َف‬


َ‫اسقنا‬
ِ ٍ ِ ٍ ِ ٍ ِ ِ ٍ ِ
Tunyweshe kwa kikombe cha maji toka chemchem ya
Salsabili.

َ‫َوم َن ْال ُح ْور ْالع ْين ب َر ْح َمت َك َف َز ّو ْجنا‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Kwa rehema Zako tuozeshe hurulaini.

َ‫ال َخ َّلد ْي َن َك َأ َّن ُه ْم ُل ْؤ ُل ٌؤ َم ْك ُن ْو ٌن َف َا ْخد ْمنا‬


ُ ْ‫َ َ ْ ْ َ م‬
‫و ِمن ال ِولد ِان‬
ِ ِ
Tupe wahudumu miongoni mwa wavulana
­wasiochakaa walio kama lulu zilizofichwa.

َ‫َوم ْن ث َمار ْال َج َّنة َو ُل ُح ْوم ْال َّط ْير َف َا ْطع ْمنا‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Tulishe matunda ya Peponi na nyama za ndege.

َ‫الس ْن ُدس َو ْال َحرْير َو إْال ْس َت ْب َرق َف َا ْلب ْسنا‬


ُّ ‫َوم ْن ِث َياب‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Na tuvishe nguo za hariri nzito na laini.

56

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 56 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ ْ َ ْ َ َّ َ َ ْ َ ْ َ َ ْ َ َ
‫وليلة القد ِر وحج بي ِتك الحر ِام‬
Tuwafikishe tuipate Laylatul-Qadri, Tuhiji nyumba
Yako tukufu.

َ‫َو َق ْت ًال ف ْي َسب ْيل َك َف َو ّف ْق َلنا‬


ِ ِ ِ ِ
Tuuwawe katika njia Yako.

ْ ‫الد َع ِاء َو مْالَ ْس َئ َلة َف‬


َ‫اس َتج ْب َلنا‬ ُّ ‫صال َح‬َ ‫َو‬
ِ ِ ِ
Na utujibu dua na maombi mema.

َ‫َوإ َذا َج َم ْع َت ْا َأل َّول ْي َن َو آْالخرْي َن َي ْو َم ْالق َي َامة َفا ْ َح ْمنا‬


‫ِ ِ ر‬ ِ ِ ِ ِ
Uturehemu utakapowakusanya wa zamani na wa
mwisho siku ya Kiyama.

َ‫النار َف ْاك ُت ْب َلنا‬


َّ ‫َو َب َر َائ ًة م َن‬
ِ ِ
Tuandikie tuepukane na moto.

َ‫َوف ْي َج َه َّن َم َفلاَ َت ُغ َّلنا‬


ِ
Usituzamishe ndani ya Jahannam.

57

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 57 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َوف ْي َع َذاب َك َو َه َوان َك َفلاَ َت ْب َتلنا‬


ِ ِ ِ ِ
Na usitujaribu ndani ya adhabu Yako na udhalili
Wako.

َ‫الضرْيع َفلاَ ُت ْطع ْمنا‬


َّ ‫الز ُّق ْوم ّو‬
َّ ‫َوم َن‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Usitulishe mti wa Zaquum wala wa Dharii.

َ‫الش َياط ْي َن َفلاَ َت ْج َع ْلنا‬


َّ َ َ َ
‫ومع‬
ِ
Usituweke pamoja na mashetani.

َ‫النار َع َلى ُو ُج ْوه َنا َفلاَ َت ْك ُب ْبنا‬


َّ ‫َوفي‬
ِ ِ ِ
Usiziangushie nyuso zetu juu ya moto.

َ‫النار َو َس َراب َيل ْال َقط َران َفلاَ ُت ْلب ْسنا‬


َّ ‫َوم ْن ث َياب‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Usituvishe nguo za moto na kanzu zenye lami.

ُ ّ ُ ْ َ
‫وء‬
ٍ ‫و ِمن ك ِل س‬
Na kila kwenye baya tuepushe.

58

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 58 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َيا اَل إ ٰل َه إ اَّل َأ ْنت‬


ِ ِ
Ewe Ambaye hapana Mungu wa haki ila Wewe.

َ‫ب َح ّق اَل إ ٰل َه إ اَّل َأ ْن َت َف َن ّجنا‬


ِ ِ ِ ِ ِ
Tuokoe kwa utukufu wa tamko ‘hapana Mungu wa
haki ila Wewe’.

59

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 59 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Sita

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫ِهللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali za
Muhammad.

ُ‫َا َّلل ُه َّم إ ِّني َا ْس َئ ُل َك َأ ْن َت ْج َع َل ِف َي َما َت ْق�ضي َو ُت َق ِّدر‬


ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Hakika mimi nakuomba uweke
katika yale ­unayopitisha na kukadiria,

ْ َ ْ ْ َ ْ ْ ُ ْ َ ْ‫َ ْ َ ْ م‬
‫ِمن األم ِر الحتو ِم ِفي األم ِر الح ِكي ِم‬
Miongoni mwa mambo ya uhakika yenye hekima,

ُ‫ض ِاء َّال ِذي اَل ُي َر ُّد َواَل ُي َب َّدل‬


َ ‫م َن ْال َق‬
ِ
Toka kwenye pitisho lisilokataliwa wala kubadilishwa.

60

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 60 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ ْ َ ْ َ َّ ُ ْ ْ َ ُ ْ َ ْ َ
‫أن تكتبني ِمن حج ِاج بي ِتك الحر ِام‬
Uniandike miongoni mwa mahujaji wa nyumba Yako
tukufu,

ْ‫مْالَ ْب ُر ْور َح ُّج ُه ْم مْالَ ْش ُك ْور َس ْع ُي ُهم‬


ِ ِ
Ambao Hijja yao imekubaliwa, juhudi zao zimeth-
aminiwa,

ْ‫مْالَ ْغ ُف ْور ُذ ُن ْو ُب ُه ْم مْالُ َك َّفر َع ْن َس ّي َئ ِاتهم‬


ِ ِ ِ ِ
Dhambi zao wamesamehewa na makosa yao yamefut-
wa.

ُ‫َو َأ ْن َت ْج َع َل ِف ْي َما َت ْق�ضي َو ُت َق ِّدر‬


ِ
Na uweke katika yale unayopitisha na kukadiria,

َ‫َأ ْن ُتط ْي َل ُع ْمر ْي ف ْي َخ ْير َو َعافي ٍة‬


ِ ٍ ِ ِ ِ
Kwamba umri wangu urefuke katika kheri na afya,
ُ
‫َوت َو ِ ّس َع ِف ْي ِر ْز ِق ْي‬
Na riziki yangu ipanuke.

61

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 61 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َو َت ْج َع َلني م َّم ْن َت ْن َتص ُر به لد ْينك‬


ِ ِِ ِِ ِ ِ ِ
Niweke miongoni mwa wale ambao, kupitia kwao
­unaipa ushindi Dini Yako.
َ َ َ‫ا‬
‫َول ت ْست ْب ِد ْل ِب ْي َغ ْي ِر ْي‬
Na wala usimweke mwingine badala yangu.

َ‫الراحم ْين‬
َّ َ‫َيا َا ْر َحم‬
ِ ِ
Ewe mbora wa Warehemevu.

62

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 62 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Saba

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫ِهللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

ْ َ ْ َ ْ َ َ‫َ ُ ْ ُ َ لا‬
‫أعوذ ِبج ِل وج ِهك الك ِري ِم‬
Najikinga kupitia utukufu wa heshima Yako kuu,

َ ‫َأ ْن َي ْن َق�ض َي َع ّني َش ْه ُر َر َم‬


َ‫ضان‬
ِ ِ
Usimalizike mwezi wa Ramadhani,

َ َْ َ ْ ُ ْ َ ْ َ ُْ َ ْ َ
‫أو يطلع الفجر ِمن ليل ِتي ه ِذ ِه‬
Au kuchomoza alfajiri ya usiku wangu huu,

ْ‫َو َل َك ق َبلي َتب َع ٌة َأ ْو َذ ْن ٌب ُت َع ِّذ ُبني َع َليه‬


ِ ِ ِ ِ ِ
Na wewe Kwangu una la kufuatilia au dhambi
­utakayoniadhibu kwa ajili yake.

63

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 63 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Sahri (DAKU)

H ii ni Dua moja nzuri sana. Lugha yake ya kishairi na ujumbe


wake unao­gusa moyo unafanya iwe ni Dua nzuri sana. Rehema
ya Mwenyezi Mungu inayozunguka kila kitu inafananishwa na uku-
bwa mpana sana wa bahari, ambapo wenye haja na shida ni wasafiri
katika meli wakingojea kuvuka.
Unyenyekevu ni sehemu muhimu sana ya taratibu na adabu za
Dua.
Utambuzi wa dhambi zake mtu na mapungufu mengine kunafaa
sana kwa muombaji. Hili linaelezwa kwa ufupi na uwazi katika Dua
ifuatayo:

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫ِهللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mwenyezi Mungu! Mrehemu Muhammad na
Aali Muhammad.
ُ َّ َ َ َ
‫السا ِئل ْو َن ِب َب ِاب َك‬ ‫ِإلهي وقف‬
Ewe Mungu wangu! Waombaji wamesimama
­mlangoni Kwako.

64

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 64 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َواَل َذ ْال ُف َق َر ُاء ب َج َنابك‬


ِ ِ
Mafukara wamekimbilia kwenye heshima Yako.

َ‫َو َو َق َف ْت َسف ْي َن ُة مْالَ َساك ْي َن َع َلى َساحل َب ْحر ُج ْودك‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ
َ‫َو َك َرمك‬
ِ
Safina ya masikini imesimama kwenye mwambao wa
bahari ya u
­ karimu Wako na wema wako.

َ ‫َي ْر ُج ْو َن ْال َج َو َاز إ َلى َس‬


َ‫احة َر ْح َمت َك َون ْع َمتك‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Wanataraji kuvuka kwenda kwenye uwanja wa
­rehema Zako na neema Zako.
َّ‫ْ ُ ْ َ اَ َ ْ َ ُ ْ َ َ َّ ْ َّ ْ ا‬
‫ف ِإل‬ِ ‫ِإلهي ِإن َكن َت َل تر َحم ِفي هذا الشه ِر الش ِري‬
َ ‫ل ْن ا ْخل‬
‫ص ل َك ِف ْي ِص َي ِام ِه َو ِق َي ِام ِه‬ ِ‫م‬
Ewe Mungu wangu! Ukiwa humhurumii ndani ya
mwezi huu ­mtukufu ila mwenye ikhlasi kwako katika
funga yake na Swala yake,
َ َ ْ ُ ُ ْ َ ْ َ َ َ ّ َ ُ ْ‫م‬ ُْْ ْ ََ
‫ق‬
‫فمن ِللمذ ِن ِب الق ِص ِر ِإذا غ ِر ِفي بح ِر ذنو ِب ِه وآث ِام ِه‬
Basi ni nani atamhurumia mwenye dhambi mzembe
anapozama kwenye bahari ya dhambi zake na makosa
yake!?

65

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 65 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫إلهي إ ْن ُك ْن َت اَل َت ْر َح ُم إ اَّل مْالُط ْيع ْي َن َف َم ْن ل ْل َعاص ْين‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mola wangu! Ukiwa huwahurumii ila watiifu,
basi ni nani atawahu­rumia waasi!?

ّ ‫ َف َم ْن ل ْل ُم َق‬،‫َوإ ْن ُك ْن َت اَل َت ْق َب ُل إ اَّل م َن ْال َعامل ْي َن‬


‫ص ِرْي َن‬ِ ِ ِِ ِ ِ ِ
Na ukiwa hupokei ila kutoka kwa wenye matendo ma-
zuri, Basi ni nani atawahurumia wenye kuzembea!?

‫الصا ِئ ُم ْو َن‬
َّ ‫إلهي َرب َح‬
ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Wenye Swaumu wamefaulu,
ُ ْ‫َ َ َ ْ َ ُ ْ َن َ َ َ م‬
ُ ‫ال ْخل‬
، ‫ص ْو َن‬ ِ ‫وفاز القا ِئمو ونجى‬
Wenye kusimama kwa ajili ya Swala wamefuzu, Na
wenye ikhlaswi wameokoka.
ْ‫م‬
‫َو َن ْح ُن َع ِب ْي ُد َك الُ ْذ ِن ُب ْو َن‬
Na sisi ni waja Wako wenye dhambi,
َ
‫فا ْر َح ْم َنا ِب َر ْح َم ِت َك‬
Hivyo turehemu kwa rehema Zako.

66

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 66 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫النار ب َع ْفو َك َيا َكرْيم‬


َّ ‫اعت ْق َنا م َن‬
ْ ‫َو‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Na tutoe motoni kwa msamaha Wako ewe Mkarimu.

َ‫الراحم ْين‬
َّ َ‫َيا َا ْر َحم‬
ِ ِ
Ewe mbora wa Warehemevu.
َّ
َ‫الطاهرْين‬ َّ َّ َ ُ َ ُ َّ َ َ
ِ ِ ‫وصلى هللا على محم ٍد و ِآل ِه‬
Na mrehemu Muhammad na Aali zake watoharifu.

67

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 67 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Ziyara Al-Waritha

َ ْ َ َ َ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عـليك يا وا ِرث آدم صـفـو ِة‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Adam mteule wa
Mwenyezi Mungu!

ّ َ ْ ُ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عـليك يا وا ِرث نـو ٍح نب ِـ ِي‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Nuh Nabii wa
Mwenyezi Mungu!
ْ َ َ َ ْ َ ْ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عـليك يـا وا ِرث ِإبـر ِاهيـم خـليـ ِل‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Ibrahim kipenzi
cha Mwenyezi Mungu!

ْ َ َ ْ ُ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عـليك يا وا ِرث موســى ك ِـلي ِم‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Musa aliyesema na
Mwenyezi Mungu!

ْ ُ َ ْ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
ِ ‫الس م عـليك يـا وا ِرث ِعـيـ�سى رو ِح‬
‫هللا‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Isa roho wa
­Mwenyezi Mungu!

68

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 68 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ َ ّ َ ُ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عـليك يا وا ِرث مـحـمـ ٍد حـ ِبـي ِب‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Muhammad
­kipenzi cha ­Mwenyezi Mungu!

ّ َ َ ْ ْ ُ ْ َ َ َ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عـليك يـا وا ِرث ا ِمي ِر املؤ ِم ِنين و ِل ِي‬
Amani iwe juu yako ewe mrithi wa Jemedari wa
Waumini walii wa Mwenyezi Mungu!

َ َ ْ ُ ْ‫َّلاَ ُ َ َ ْ َ َ ْ َ ُ َ َّ َ م‬
‫الس م عـليك يابـن مـحـم ٍـد الـصـطـفـى‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Muhammad
­Al-Mustafa!

َ ‫السَّلاَ ُم َع َـل ْي َك َي ْاب َـن َعـل ّي مْالُ ْرَت‬


‫ـضـى‬ ِ ِ
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Ali Al-Murtadha!

َ ْ َّ َ َ َ َ ْ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫اطـمة الزهر ِاء‬
ِ ‫الس م عليك يابـن ف‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Fatima Zahraa!
ُْ َ َ َ‫َّلا‬
‫الس ُم َعل ْي َك َي ْاب َـن َخ ِد ْي َجة الك ْب َـرى‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Khadija
­Al-­Kubra!

69

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 69 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫السَّلاَ ُم َع َل ْي َك َيا َث َار هللا َو ْاب َـن َثاره َو ْالو ْت َـر مْالَ ْو ُت ْـور‬
ِ ِِ ِ
Amani iwe juu yako ewe ambaye kisasi chake
­kitalipizwa na ­Mwenyezi Mungu. Na mwana wa
­ambaye kisasi chake kitalipizwa na yeye! Na aliye wa
pekee kwake.
َ َ َّ َ ْ َ َ َ َ‫َ ْ َ ُ َ َّ َ َ ْ َ َ ْ َ َّلا‬
‫اشـهد انك قد اقمت الص ة وآتيت الزكاة‬
Nakiri kuwa hakika wewe umesimamisha Swala na
umetoa Zaka.
َ ْ ُ ْ‫َ َ َ ْ َ مْ َ ْ ُ ْ َ َ َ ْ َ َ م‬
‫وامرت بِـالعرو ِف ونهيت ع ِـن النك ِر‬
Umeamrisha mema na kukataza mabaya.

َ ‫َو َاطَـ ْع َـت‬


َ ‫هللا َو َر ُس ْـو َل ُه َح َّـتى َا َت‬
ُ‫اك ْال َيق ْـين‬
ِ
Na umemtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake
­mpaka yakini ­ilipokufika.
َ‫هللا ُا َّم ًة َق َت َـل ْتـك‬
ُ ‫َف َـل َع َـن‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliokuua.
َ‫هللا ُا َّم ًة َظ َل َم ْتك‬
ُ ‫َو َل َع َن‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliokudhulumu.

70

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 70 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ َ َ َ َ َ ْ َ َ ً َّ ُ ُ َ َ َ َ
‫ولعن هللا امة س ِمعت بِـذ ِلك فر ِضيت ِب ِـه‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliosikia hayo kisha
ukayaridhia.

ْ َ َ َ َ َ َ‫َ َ ْ ا‬
‫هللا‬
ِ ‫يا مولي يا ابا عب ِد‬
Ewe bwana wangu! Ewe Abu Abdillah!
َ َّ َ‫أْ َ ْ لا‬ ً ْ ُ َ ْ ُ َ َّ َ ُ َ ْ َ
‫اشهد انك كنت َنورا ِفي الص ِب الش ِامخ ِة‬
َ‫َو أْال ْر َحـام مْالُ َط َّهر ِة‬
ِ
Nakiri kuwa hakika wewe ulikuwa nuru kwenye
­mifupa ya migongo ya juu na matumbo ya uzazi
­yaliyo tohara.

َ‫ـاسـها‬َ‫َل ْم ُت َـن ّج ْـس َـك ْال َجـاهل َّي ُة بـ َا ْنج‬


ِ ِ ِِ ِ
Ujahiliya haujakuchafua kwa uchafu wake.

َ‫ات ثـ َيابـها‬ َّ َْ ُ ْ َ ْ ُْ ْ ََ
ِ ِ ِ ‫ولم تـلبِـسك ِمن مدل ِهم‬
Wala giza halikukufunika kwa shuka lake.
ّ ‫َو َا ْش َـه ُد َأ َّن َك م ْن َد َعائم‬
َ‫الد ْين َو َا ْر َكان مْالُ ْؤمن ْين‬
ِِ ِ ِ ِ ِِ ِ
Nakiri kuwa hakika wewe unatokana na nguzo za dini
na viongozi wa waumini.

71

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 71 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ‫ـام ْال َب ُّر‬


َّ ‫الت ِق ُّـي‬
ُّ‫الر ِضـي‬ ُ ‫َو َا ْش َه ُد َا َّن َك إْال َم‬
ِ
Nakiri kuwa hakika wewe ni Imam mwema,
­mchamungu mwenye kuridhiwa.

ُّ‫الز ِك ُّي َا ْل َه ِادي َا مْلَ ْه ِدي‬


َّ
Mtakasifu, kiongozi muongozaji kwa haki.
َ ْ‫َ َ ْ َ ُ َ َّ أ‬
َّ ‫الئ َّم َة م ْن ُو ْلد َك َكل َم ُة‬
‫الت ْق َـوى‬ ِ ِ ِ ِ ‫واشـهد ان‬
Nakiri kuwa hakika Maimamu toka kwenye kizazi
chako ni neno la ucha­mungu,

َ ْ ُ ُ ‫َ َ ْ لاَ ُ ْ ُ َ َ ْ ُ ْ َو‬
‫واعـ م الهدى والعـر ة الوثـقى‬
Alama za uongofu, shikio imara,

ُّ ‫َو ْال ُح َّـج ُة َع َـلى َا ْهل‬


َ‫الد ْنيـا‬
ِ
Na hoja juu ya watu wa duniani.

ُ‫ئ َك َت ُه َو َا ْنبـ َي َائ ُه َو ُر ُس َـله‬ َ‫َ ُ ْ ُ َ َ َ لا‬


ِ ِ ‫واش ِـهد هللا ومـ‬
Namshuhudisha Mwenyezi Mungu na malaika Wake,
Manabii Wake na Mitume Wake,

72

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 72 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫َا ِّن ْي ب ُـك ْـم ُم ْؤم ٌن َوبـ َايابـ ُكم‬


ِ ِِ ِ ِ
Kuwa hakika mimi ni mwenye kuwaamini nyinyi, na
ni mwenye yakini na kurudi kwenu,

ْ‫ُم ْو ِق ٌن بَـ َش َرا ِئع ِد ْين ْي َو َخ َوا ِت ْيم َع َم ِلي‬


ِ ِ ِ
Sheria za dini yangu, na matokeo ya matendo yangu.

ٌ‫َو َق ْلب ْي ِل َق ْلب ُك ْم ِس ْلم‬


ِ ِ
Moyo wangu ni wenye kujisalimisha kwenye nyoyo
zenu.

ُ َ َ
‫َوا ْم ِر ْي اِل ْم ِرك ْـم ُم َّت ِب ٌـع‬
Na mambo yangu ni yenye kufuata mambo yenu.

ْ‫هللا َع َل ْي ُكم‬ ُ‫ص َل َوات‬


َ
ِ
Rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yenu,

ُ َ َ ُ َ َ ُ َ َ
‫َو َعلى ا ْر َو ِاحـك ْم َو َعلى ا ْج َـس ِـادك ْم َو َعلى ا ْج َـس ِـامك ْم‬
Na juu ya roho zenu, miili yenu, na viwiliwili vyenu.

73

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 73 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫َو َع َلى َشـاه ِد ُك ْم َو َع َلى غَـا ِئبـ ُكم‬


ِ ِ
Juu ya anayeonekana na asiyeonekana,
ُ َ ََ َ ْ ُ َ ََ َ
‫ـاطـ ِنـك ْـم‬
ِ ‫وعـلى ظ ِـاه ِركم وعـلى بـ‬
Aliye dhahiri na asiye dhahiri.

Ziyara Ya Ali Akbar (A.S.)

ْ ُ َ َ ْ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫ل‬
ِ ِ ‫الس م عليك يابــن رسـو‬
‫هللا‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Mtume wa
­Mwenyezi Mungu!

ّ َ َ ْ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّ لا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عليك يابـن نبِـ ِي‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Nabii wa
­Mwenyezi Mungu!
َ‫السَّلاَ ُم َع َل ْي َـك َي ْاب َـن َام ْير مْالُ ْؤمن ْين‬
ِِ ِ ِ
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Jemedari wa
Waumini!

ْ َّ ْ َ ُ ْ َ ْ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّ لا‬
‫الس م عليك يابـن الحسـي ِن الش ِـهي ِد‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa Husein shahidi!

74

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 74 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ َّ َ ْ َ ُ ْ َّ َ ُّ َ َ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫الس م عليك ايها الش ِهيد وابـن الش ِـهي ِد‬
Amani iwe juu yako ewe shahidi na mwana wa
shahidi­!

ْ ُ ْ َ ْ‫َّلاَ ُ َ َ ْ َ َ ُّ َ مْ َ ْ ُ ْ ُ َ ْ ُ م‬
‫الس م عليك ايها الـظـلوم وابـن الظـلو ِم‬
Amani iwe juu yako ewe uliyedhulumiwa mwana wa
­aliyedhulumiwa!
ُ ‫َل َع َن‬
َ‫هللا ُا َّم ًة َق َت َـل ْتـك‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliokuua.
َ‫هللا ُا َّم ًة َظ َل َم ْتـك‬
ُ ‫َو َل َع َن‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliokudhulumu.
ْ َ َ َ َ َ ْ َ َ ً َّ ُ ُ َ َ َ َ
‫ولعن هللا امة س ِـمعت بِـذ ِلك فر ِضيت بِـ ِه‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliosikia hayo kisha
ukayaridhia.

Ziyara Ya Wahanga Wote


ُ‫السَّلاَ ُم عَـ َل ْي ُكم َيا َا ْول َي َاء هللا َو َاحـبَّـ َائه‬
ِ ِ ِ
Amani iwe juu yenu enyi mawalii wa Mwenyezi
­Mungu na vipenzi Vyake!

75

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 75 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ ‫السَّلاَ ُم َع َل ْي ُك ْم َيا َا‬


ُ‫صـف َي َاء هللا َو َاو َّد َائه‬
ِ ِ ِ
Amani iwe juu yenu enyi wateule wa Mwenyezi
­Mungu na vipenzi Vyake!

‫هللا‬ ‫ن‬ ‫ي‬ َ ‫السَّلاَ ُم َع َل ْي ُك ْم َيا َا ْن‬


ْ ‫ص َـار د‬
ِ ِ ِ
Amani iwe juu yenu enyi wasaidizi wa dini ya
­Mwenyezi Mungu!

‫ل‬ ْ ُ َ َ َ ْ َ َ ْ ُ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
ِ ِ ‫الس م عـليكم يا انـصـار رسو‬
‫هللا‬
Amani iwe juu yenu enyi wasaidizi wa Mtume wa
Mwenyezi Mungu!

ْ ُ ْ‫َّلاَ ُ َ َ ْ ُ َ َ ْ َ َ م‬
‫ـص َـار ا ِم ْي ِر الؤ ِم ِن ْـي َن‬ ‫الس م عـليـكم يـا ان‬
Amani iwe juu yenu enyi wasaidizi wa Jemedari wa
Waumini!

َّ ‫ـص َـار َفـاط َم َة‬


َ‫الز ْه َراء َس ّيدة‬ َ ‫السَّلاَ ُم َع َـل ْي ُك ْم َيا َا ْن‬
ِ ِ ِ ِ
َ‫ن َساء ْال َع مَـال ْين‬
ِ ِ ِ
Amani iwe juu yenu enyi wasaidizi wa Fatima, Bibi
mbora kushinda wanawake wote wa ulimwengu!

76

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 76 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ّ‫ـص َـار َابـي ُم َح َّم ٍد َا ْل َح َسن ْبـن َع ِـلي‬ َ ‫السَّلاَ ُم َع َل ْي ُك ْم َيا َا ْن‬
ٍ ِ ِ َّ ِ َْ
َ
‫اص ِح‬ِ ‫الو ِل ّ ِي الن‬
Amani iwe juu yenu enyi wasaidizi wa Abu Muham-
mad Hasan ibnu Ali, walii mtakasifu na mnasihi!

ْ َ َ َ َ ْ َ َ ْ ُ ْ َ َ ُ َ‫َّلا‬
‫هللا‬
ِ ‫الس م عليكم يا انصار ابِـي عب ِـد‬
Amani iwe juu yenu enyi wasaidizi wa Abu Abdillah!

ْ‫بـ َابـ ْي َا ْن ُت ْم َو ُا ِّمي‬


ِ ِ
Baba yangu na mama yangu ni fidia kwenu.

ْ‫ض َّال ِت ْـي ِف ْـي َها ُد ِف ْن ُـتم‬ َ ْ‫ْ ُ ْ َ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْر‬ ‫ِطبـتم وطاب ِت‬
Hakika mmesafika na imesafika ardhi mliyozikwa.
ً ْ َ ً ْ َ ْ ُْ ُ َ
‫وفزتم فـوزا ع ِـظـيما‬
Na mmefuza kufuzu kukubwa mno.

ْ‫َف َيا َل ْي َتني ُك ْن ُت َم َع ُك ْم َف َا ُف ْو َز َم َع ُكم‬


ِ
Natamani laiti ningelikuwa pamoja nanyi nikafuzu
pamoja nanyi.

77

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 77 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Ziyara Ya Abul-Fadhli Abbas (A.S.)


ْ‫اس ْاب َن َأمير‬
َ َ‫ضل ْالعب‬
َّ ْ ‫الس َال ُم َع َل ْي َك َيا َأ َبا ْال َف‬
َّ
ِ ِ ِ َ ْ ُ ْ‫م‬
‫الؤ ِم ِن ْين‬
Amani iwe juu yako ewe Abul-Fadhli Abbas! Mwana
wa Jemedari wa Wau­mini!
ْ َ َ َّ
‫السال ُم َعل ْي َك َيا ْاب َن َس ِّي ِد ال َو ِص ِّي ْي َن‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa bwana wa mawasii!

ْ‫الس َال ُم َع َل ْي َك َيا ْاب َن َأ َّول ْال َق ْوم إ ْس َال ًما َو َأ ْق َدمهم‬
َّ
ِِ ِ ِ ً ِ
‫ِإ ْي َمانا‬
Amani iwe juu yako ewe mwana wa wa kwanza kuwa
mwisilamu, na wa mwanzo kuamini.
َ ْ ْ‫َ َ ْ َ ْ ْ َّ َ َ ْ َ ْ َ َ إ‬
‫السال ِم‬
ِ ‫و أقو ِم ِهم ِب ِدي ِن الل ِه و أحو ِط ِهم على‬
Aliye imara mno kwenye dini ya Mwenyezi Mungu na
mjuzi mno juu ya Uisilamu.

َ ‫َأ ْش َه ُد َل َق ْد َن‬
َ‫ص ْح َت ل َّله َو ل َر ُس ْوله َو َلخ ْيك‬
ِ ِ‫ِ ِ ِ ِ ِ أ‬
Nakiri kuwa umetoa nasaha kwa ajili ya Mwenyezi
Mungu, Mtume Wake na kaka yako.

78

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 78 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ُ ْ‫َ ْ َ أْ َ ُ م‬
‫ا�سي‬
ِ ‫ف ِنعم الخ الو‬
Ni uzuri ulioje kwa wewe kuwa ndugu mfariji!

َ‫ك‬ ْ َ َ َ ً َّ ُ ُ َّ َ َ َ َ
‫فلعن الله أمة قتلت ‏‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliokuuwa.

َ‫الل ُه ُأ َّم ًة َظ َل َم ْتك‬


َّ َ َ َ َ
‫ولعن‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliokudhulumu.

َ ْ‫َ َ َ َ َّ ُ ُ َّ ً ْ َ َ َّ ْ ْ َ م‬
َ‫ال َحارم‬
ِ ‫و لعن الله أمة استحلت ِمنك‬
Mwenyezi Mungu aulani umma uliohalalisha haramu
dhidi yako,

َ ْ ْ‫َ ْ َ َ َ ْ ُ ْ َ َ إ‬
‫السال ِم‬
ِ ‫و انتهكت حرمة‬
Na ukavunja heshima ya Uisilamu.

ُ ْ‫َ ْ َ َّ ُ مْ ُ َ ُ م‬
َّ ‫ال َحامي‬
‫اص ُر‬
ِ ‫الن‬ ِ ‫ف ِنعم الص ِابر الج ِاهد‬
Ni uzuri ulioje kwa wewe kuwa mvumilivu,
­Mpiganaji, muhami na msai­dizi,

79

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 79 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ْ‫َ أْ َ ُ َّ ُ َ ْ َ ْ م‬
َ ‫الج ْي ُب إ َلى َط‬
ّ‫اعة َربه‬
ِِ ِ ِ ِ ‫و الخ الدا ِفع عن أ ِخي ِه‏‬
Ndugu mtetezi kwa ndugu yake na mtiifu kwa Mola
wake,

ُ‫الراغ ُب ف ْي َما َزه َد ف ْيه َغ ْي ُره‬


ِ ِ ِ ِ ِ َّ
Mwenye kupendelea yale waliyoyapa mgongo
­wengine,

ْ َ ْ َ َّ َ ْ َ ْ َ َّ َ
‫اب الج ِزي ِل و الثن ِاء الج ِمي ِ ‏ل‬
ِ ‫ِمن الثو‬
Kuanzia thawabu njema hadi sifa jamili.

َّ َ َ َ َ َ َ ُ َّ َ َ َ ْ َ َ َ َ َ ْ َ َ
‫ات‬
ِ ‫و ألحقك (فألحقك) الله ِبدرج ِة آبا ِئك ِفي جن‬
َّ
‫الن ِع ْي ِم‏‬
Mwenyezi Mungu akuweke kwenye daraja la baba
zako ndani ya pepo yenye neema.

Dua Baada Ya Ziyara


َ‫ض ُت لزَيا َ ة َأ ْول َيائ َك َر ْغ َب ًة في َث َوابك‬
ْ َّ َ َ ّ َّ ُ َّ
ِ ِ ِ ِ ِ ‫اللهم ِإ ِني تعر ِ ِ ر‬
Ewe Mungu wangu! Nimekusudia mwenyewe
­kuwazuru mawalii Wako kwa ajili ya kutamani tha-
wabu Zako.

80

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 80 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫ك‬ َ ْ ْ َ َ َ َ َْ ً َ َ َ
‫و رجاء مِلغ ِفرِتك و ج ِزي ِل ِإحسا ِن ‏‬
Na kutaraji msamaha Wako na ihsani Yako njema.
َّ
َ‫الطاهرْين‬ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ ََ
ِ ِ ‫فأسألك أن تص ِلي على محم ٍد و ِآل ِه‬
Hivyo nakuomba mrehemu Muhammad na Aali zake
watoharifu.
ًّ َ ْ ْ َ َ ْ َ ْ َ َ
‫و أن تجعل ِرز ِقي ِب ِهم دارا‬
Na kupitia kwao ifanye maridhawa riziki yangu.
ً َ
‫َو َع ْي ِ�شي ِب ِه ْم قا ّرا‬
Fanya maisha yangu yawe yenye kupendeza.
ً َُْ ْ َ ْ
‫َو ِزَيا َرِتي ِب ِهم مقبولة‬
Ziyara yangu ikubalike.
ً ََّ ْ
‫َو َح َيا ِتي ِب ِهم ط ِيبة‬
Na maisha yangu yawe ya kufurahisha.

َ ‫َو َأ ْدر ْجني إ ْد َر‬


َ‫اج مْالُ َك َّرم ْي ‏ن‬
ِ ِ ِ ِ
Niweke pamoja na wale wenye kuheshimiwa.
81

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 81 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫اج َع ْلني م َّم ْن َي ْن َقل ُب م ْن زَيا َ ة َم َشاهد َأح َّبائك‬


ْ ‫َو‬
ِ ِ ِ ِ ‫ر‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Nijalie niwe miongoni mwa wale wanaorudi toka ku-
zuru
makaburi ya wapenzi Wako,
ً ُْ ً ُْ
‫مف ِلحا من ِجحا‬
Huku wakiwa ni wenye kufaulu na kufuzu.
ُ ُّ َ َ ْ ُ َ ْ ُ ْ َ
‫وب‬
ِ ‫ق ِد استو ِجب غفران الذن‬
Ambao wamewajibika kusamehewa dhambi,

ْ ُ ُ ْ َ ْ َ َ ُُْ ْ َْ َ َ
‫و‬
‫و ستر العيو ِب و كشف الكر ِب‬
Kusitiriwa aibu na kuondolewa matatizo.

َ ْ َ ْ‫َّ َ َ ْ ُ َّ ْ َ ى َ َ ْ ُ م‬
. ‫ِإنك أهل التقو و أهل الغ ِفر ِة‬
Hakika Wewe ni mwenye kupokea uchamungu na
kumiliki ­msamaha.

82

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 82 6/16/2016 4:29:23 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Za Kila Siku Ya Ramadhani

Mwezi Mosi:
َ‫الصائم ْين‬
َِّ ْ ‫َا َّلل ُه َّم‬
َ‫اج َع ْل ص َيامي ف ْيه ص َيام‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Ijalie funga yangu katika mwezi
huu iwe ni funga ya wenye kufunga kwa dhati.

َ‫َوق َيامي ف ْيه ق َي َام ْال َقائم ْين‬


ِِ ِ ِ ِ ِ ِ
Na kisimamo changu cha ibada kiwe ni kisimamo cha
wenye kusimama kwa ibada ya dhati.

َ‫َو َن ّب نْهي ف ْيه َع ْن َن ْو َمة ْال َغافل ْين‬


ِِ ِ ِ ِ ِِ
Niepushe na usingizi wa wavivu,

َ‫َو َه ْب لي ُج ْرمي ف ْيه َيا إ َله ْال َع مَال ْين‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Samehe dhambi zangu humo ewe Mola wa viumbe.

ُ ْ‫َ ْ ُ َ ّ َ َ ً َ م‬
َ‫ال ْجرم ْين‬
ِ ِ ‫واعف ع ِني يا عا ِفيا ع ِن‬
Na uniafu ewe mwenye kuwasamehe wakosaji.

83

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 83 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Pili:
َ ‫َا َّلل ُه َّم َق ّرْبني ف ْيه إ َلى َم ْر‬
‫ضا ِت َك‬ ِ ِ ِ ِِ
Ewe Mungu wangu! Nikurubishe kwenye radhi ndani
ya mwezi huu.

َ َ
‫َو َج ِّن ْب ِني ِف ْي ِه ِم ْن َسخ ِط َك َون ِق َما ِت َك‬
Niepushe na hasira Zako na maangamizo Yako ndani
ya mwezi huu.

ٰ َ ّ
‫َو َو ِف ْق ِني ِف ْي ِه ِل ِق َرآئ ِة ا َيا ِت َك‬
Na uniwafikishe niweze kukisoma Kitabu Chako.

َّ ‫ب َر ْح َم ِت َك َيا َا ْر َح َم‬
‫الر ِاح ِم ْي َن‬ ِ
Kwa rehema Zako ewe mbora wa warehemevu.

Mwezi Tatu:

َ‫الت ْنب ْيه‬ ّ ْ ْ ُ ْ َّ ُ َّ َ


َّ ‫الذ ْه َن َو‬
ِ ِ ‫اللهم ارزق ِني ِفي ِه‬
Ewe Mungu wangu! Niruzuku uelevu na uzinduko,

84

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 84 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ‫الس َف َاهة َو‬


‫الت ْم ِو ْي ِة‬ َّ َ ‫َو َباع ْدني ف ْيه م‬
‫ن‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Niepushe na ubaradhuli na upumbavu,

ْ‫اج َع ْل ل ْي َنص ْي ًبا م ْن ُك ّل َخ ْير ُت ْنز ُل فيه‬


ْ ‫َو‬
ِ ِ ِ ٍ ِ ِ ِ ِ
Na niwezeshe kupata fungu la kila kheri itakayoshuka,
َ ْ‫ُ ْ َ َ َ ْ َ َ أ‬
َ‫ال ْج َود ْين‬
ِ ‫ِبجو ِدك يا اجود‬
Kwa ukarimu Wako ewe mbora wa wakarimu.

Mwezi Nne:
َ َ َ َ َّ َ
‫الل ُه َّم ق ّ ِو ِني ِف ْي ِه َعلى ِاق َام ِة ا ْم ِر َك‬
Ewe Mungu wangu! Nipe nguvu za kuniwezesha
kutekeleza amri Zako.

َ‫َو َاذ ْقني ف ْيه َحلاَ َو َة ذ ْكرك‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Nionjeshe humu utamu wa utajo Wako.

َ‫َو َا ْوز ْعني ف ْيه َل َداء ُش ْكر َك ب َك َرمك‬


ِ ِ ِ ِ ِ‫ِ ِ ِ ِ أ‬
Niwezeshe kutekeleza wajibu wa kukushukuru kwa
neema Zako.

85

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 85 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫اح َف ْظني ف ْيه بح ْفظ َك َو َس ْترك‬


ْ ‫َو‬
ِ ِ ِِ ِ ِ ِ
Na nihifadhi humu katika ulinzi Wako na sitara Yako.

َ ‫َيا َأ ْب‬
َّ ‫ص َر‬
َ‫الناظرْين‬
ِ ِ
Ewe mwenye kuona zaidi ya waoni.

Mwezi Tano:
َ‫اج َع ْلني ف ْيه م َن مْالُ ْس َت ْغفرْين‬
ْ ‫َا َّلل ُه َّم‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Nijalie ndani ya mwezi huu niwe
miongoni mwa wanaoom­ba maghofira.
َْ َّ ‫اج َع ْلني ِف ْي ِه م ْن ِع َب ِاد َك‬
‫الص ِال ِح ْي َن القا ِن ِت ْي َن‬ ِ ِ
ْ ‫َو‬
Nijalie niwe miongoni mwa waja Wako wema
­wanyenyekevu.
َ‫اج َع ْلني ف ْيه م ْن َأ ْول َيائ َك مْالُ َق َّرب ْين‬
ْ ‫َو‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Na nijaalie niwe miongoni mwa mawalii Wako wa
karibu.
َ‫الراحم ْين‬
َّ َ‫ب َ ْرأ َفت َك َيا َا ْر َحم‬
ِ ِ ِ ِ
Kwa huruma Yako ewe mbora wa wenye huruma.

86

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 86 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Sita:

‫ض َم ْع ِص َي ِت َك‬ ُّ ‫َا َّلل ُه َّم اَل َت ْخ ُذ ْل ِني ِف ْي ِه ِل َت َع‬


‫ر‬
ِ
Ewe Mungu wangu! Usinitelekeze kwa kukuasi.
َ َ
‫اط ن ِق َم ِت َك‬ ‫ي‬‫س‬ ‫ب‬ ‫ي‬ ‫ن‬ ‫ب‬ ْ ‫َواَل َت‬
ْ‫ضر‬
ِ ِ ِ ِِ
Wala usinipige kwa mjeledi wa adhabu Yako.

َ ْ ْ ََ
‫ات َسخ ِط َك‬ ْ
ِ ‫وزح ِزح ِني ِف ْي ِه ِمن ُم ْو ِج َب‬
Niepushe na mambo yote yawezayo kuniwajibishia
hasira Zako.

َ‫الراغب ْين‬
َّ َ‫ب َم ّن َك َو َا َياد ْي َك َيا ُم ْن َتهى َر ْغبة‬
ِِ ِ ِ ِ ِ
Kwa ukarimu Wako na baraka Zako ewe uliye raghba
ya wenye raghba.

Mwezi Saba:

َ َ َ ََ ْ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ا ِع ِني ِفي ِه على ِصي ِام ِه و ِقي ِام ِه‬
Ewe Mungu wangu! Nisaidie niweze kuufunga na
kusimama kwa ajili ya ibada.

87

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 87 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ َ َ َ ْ ْ َّْ َ
‫وج ِنب ِني ِفي ِه ِمن هفوا ِت ِه وآث ِام ِه‬
Niepushe na matelezo na madhambi.
ْ ْ
‫َو ْار ُزق ِني ِف ْي ِه ِذك َر َك ِب َد َو ِام ِه‬
Na niruzuku nidumu katika utajo Wako.

َ‫ب َت ْوف ْيق َك َيا َهاد َي مْالُض ّل ْين‬


ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Kwa tawfiki Yako ewe Mwongozaji wa waliopotea.

Mwezi Nane:
َ ْ َ ْ‫َ َّ ُ َّ ْ ُ ْ ْ َ ْ َ َ أ‬
‫اللهم ارزق ِني ِفي ِه رحمة اليت ِام‬
Ewe Mungu wangu! Niruzuku hali ya kuwaonea
­huruma mayatima,
َ‫َ ْ َ َ َّ َ َ ْ َ َ َّ لا‬
‫الس ِم‬ ‫وِإطعام الطع ِام وِإفشاء‬
Kulisha vyakula, kutoa salamu, na kusuhubiana na
watu wema.

َ‫ص ْح َب َة ْالك َرام َيا َم ْل َج َأ آْالمل ْين‬


ُ ‫َو‬
ِِ ِ ِ
Kwa utajiri Wako ewe kimbilio la wenye matarajio.
88

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 88 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Tisa:
ْ ً َ ْ ‫َا َّلل ُه َّم‬
‫اج َع ْل ِلي ِف ْي ِه ن ِص ْيبا ِم ْن َر ْح َم ِت َك ال َو ِاس َع ِة‬
Ewe Mungu wangu! Nijalie nilipate fungu la rehema
Zako pana.

‫اط َع ِة‬ َّ
‫الس‬ َ ‫َو ْاهدني ف ْيه ل َب َراه ْين‬
‫ك‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ِِ
Uniongoze kwenye buruhani Zako zing’arazo.

ْ َ ‫َو ُخ ْذ ب َناص َيتي إ َلى َم ْر‬


‫ضا ِت َك ال َج ِام َع ِة‬ ِ ِ ِ ِ
Na nishike mkono kuelekea kwenye radhi Zako kuu.

َ‫ب َم َح َّبت َك َيا َأ َم َل مْالُ ْش َتاق ْين‬


ِ ِ ِ
Kwa mahaba Yako ewe uliye matarajio ya wenye
shauku.

Mwezi Kumi:
َ‫اج َع ْلني ف ْيه م َن مْالُ َت َو ّكل ْي َن َع َل ْيك‬
ْ ‫َا َّلل ُه َّم‬
ِِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Nijalie niwe miongoni mwa
­wenye kukutegemea.

89

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 89 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫اج َع ْلني ف ْيه م َن ْال َفائزْي َن َل َد ْيك‬


ْ ‫َو‬
ِِ ِ ِ ِ ِ
Nijalie niwe miongoni mwa wenye kufuzu mbele Yako.

َ‫اج َع ْلني ف ْيه م َن مْالُ َق َّرب ْي َن إ َل ْيك‬


ْ ‫َو‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Na nijalie niwe miongoni mwa wenye ukuruba
­Kwako.
َّ َ َ َ َ َ َ ْ
َ‫الطالب ْين‬
ِ ِ ‫ِب ِإحسا ِنك يا غاية‬
Kwa ihsani Yako ewe uliye lengo la waombaji.

Mwezi Kumi Na Moja:


َ‫َا َّلل ُه َّم َح ّب ْب إ َل َّي ف ْيه إْال ْح َسان‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Nijalie nipende sana kutenda
mema.

ْ ‫َو َك ّر ْه إ َل َّي ف ْيه ْال ُف ُس ْو َق َو ْالع‬


َ‫ص َيان‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Na niwezeshe kuchukia kutenda uovu na uasi.

َ‫الن ْي َران‬ َ َ َّ ْ َّ َ َ ْ ّ َ َ
ّ ‫ط َو‬
ِ ‫وح ِرم علي ِفي ِه السخ‬
Na niepushe na hasira Zako na moto.

90

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 90 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫اث مْالُ ْس َتغث ْين‬


َ َ َ َ َْ
‫ِبعو ِنك يا ِغي‬
ِِ
Kwa msaada Wako ewe uliye nusra ya watakao nusra.

Mwezi Kumi Na Mbili:

ََْ َ ّْ ْ ‫َا َّلل ُه َّم َزّي ّني ف‬


‫اف‬
ِ ‫ف‬ ‫ع‬ ‫ال‬‫و‬ ‫ر‬ ‫ت‬ ‫الس‬ ‫ب‬ ‫ه‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِِ‫ي‬
Ewe Mungu wangu! Nipambe kwa sitara na utawa.

ََْ َ ُُْْ َ ْ ْ ُْ َ
‫اف‬
ِ ‫اس القنو ِع والعف‬
ِ ‫واسترِني ِفي ِه ِب ِلب‬
Nipambe kwa vazi la ukinaifu na utoshekevu.

‫اف‬ َ ‫اح َم ْلني ف ْيه َع َلى ْال َع ْدل َو إْال ْن‬


‫ص‬ ْ ‫َو‬
ِ ِ ِ ِ ِ ِ
Nielekeze kwenye uadilifu na insafu.

ُ َ َ َ ّ ُ ْ ْ ّ
‫وآم ِني ِفي ِه ِمن ك ِل ما اخاف‬
ِ
Na nisalimishe dhidi ya kila ninachohofia.

َ ْ َ ْ َ َ َْ
‫ص َمة الخا ِئ ِف ْي َن‬ ‫ِب ِعصم ِتك يا ِع‬
Kwa kinga Yako ewe uliye kinga ya wenye hofu.

91

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 91 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Kumi Na Tatu:


َ ْ َ ْ‫َ َّ ُ َّ َ ّ ْ ْ َ َّ َ َ أ‬
‫س والقذ ِار‬ ِ ‫اللهم ط ِهرِني ِفي ِه ِمن الدن‬
Ewe Mungu wangu! Nitakase dhidi ya taka na uchafu.

َ ْ َ ْ‫َ َ ّ ْ ْ َ َ َ َ أ‬
‫ات القد ِار‬ ِ ‫وص ِبرِني ِفي ِه على كا ِئن‬
Nipe subira juu ya matukio ya kadari Zako.

َ ْ َ ْ‫َ َ ّ ْ ْ ُّ َ َ ُ ْ َ أ‬
‫وو ِفق ِني ِفي ِه ِللتقى وصحب ِة البر ِار‬
Na niafikishe kwenye uchaji na kusuhubiana na watu
wema.

َ‫ب َع ْون َك َيا ُق َّر َة َع ْين مْالَ َساك ْين‬


ِ ِ ِ ِ
Kwa msaada Wako ewe kiburudisho cha walio
­masikini.

Mwezi Kumi Na Nne:

َ َ َ ْ ْ ْ َ ُ َ‫َ َّ ُ َّ ا‬
‫ات‬
ِ ‫اللهم ل تؤ ِاخذ ِني ِفي ِه ِبالعثر‬
Ewe Mungu wangu! Usinihukumu kwa yale
­niliyojikwaa.

92

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 92 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ َْ َ َ َ َ ْ َ ْ ْ ََ
‫ات‬
ِ ‫وا ِقل ِني ِفي ِه ِمن الخطايا والهفو‬
Niepushe na makosa na matelezo.

َ ْ‫َ اَ َ ْ َ ْ ْ َ َ ً ْ َ لاَ َ َ آ‬
‫ات‬
ِ ‫ول تجعل ِني ِفي ِه غرضا ِللب يا والف‬
Na wala usinifanye shabaha la balaa na maafa.

َ‫بع َّزت َك َيا ع َّز مْالُ ْسلم ْين‬


ِِ ِ ِ ِِ
Kwa utukufu Wako ewe uliye utukufu wa Waislamu.

Mwezi Kumi Na Tano:


َ ‫َا َّلل ُه َّم ْار ُز ْقني ف ْيه َط‬
َ‫اع َة ْال َخاشع ْين‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Niruzuku utiifu wa wenye
­unyenyekevu.
ُ ْ‫َ ْ َ ْ ْ َ ْ ْي َ َ م‬
َ‫ال ْخبت ْين‬
ِ ِ ‫واشرح ِفي ِه صد ِر ِب ِاناب ِة‬
Na kikunjue kifua changu kwa toba ya wenye
­kujisalimisha.

َ‫ان ْال َخائف ْين‬


َ ‫ب َا َمان َك َيا َا َم‬
ِِ ِ ِ
Kwa amani Yako ewe uliye amani ya wenye hofu.
93

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 93 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Kumi Na Sita:

َ ْ َ ْ‫َ َّ ُ َّ َ ّ ْ ْ ُ َ َ َ أ‬
‫اللهم و ِقف ِني ِفي ِه مِلوافق ِة البر ِار‬
Ewe Mungu wangu! Niafikishe niafikiane na watu
wema.

َ ْ َ ْ‫َ َ ّ ْ ْ ُ َ َ َ َ أ‬
‫وج ِنب ِني ِفي ِه مرافقة الشر ِار‬
Niepushe kurafikiana na waovu.
َْ َ
‫َو ِآو ِني ِف ْي ِه ِب َر ْح َم ِت َك ِإلى َد ِار الق َر ِار‬
Na uniweke kwa rehema Zako kwenye nyumba ya
utulivu.
َ‫باله َّيت َك َيا إ َله ْال َع مَال ْين‬
ِ ِ ِ ِ ِِ
Kwa utukufu Wako ewe Mungu! wa viumbe.

Mwezi Kumi Na Saba:


َ ْ َ‫ْ َ ْ أ‬ ْ َّ ُ َّ َ
‫اللهم اه ِد ِني ِفي ِه ِلص ِال ِح العم ِال‬
Ewe Mungu wangu! Niongoze kwenye amali njema.

َ‫َو ْاقض لي ِف ْي ِه ْال َح َوا ِئ َج َو آْال َمال‬


ِ ِ
Na nitekelezee haja zangu na matarajio yangu.

94

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 94 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ُّ َ ْ ْ َّ َ ُ َ ْ َ َ‫َ َ ْ ا‬
‫يا من ل يحتاج ِإلى التف ِسي ِر والسؤ ِال‬
Ewe usiyehitaji ufafanuzi na kuuliza.
َ‫ْ م‬ ُ ‫َيا َعال ًا ب َما في‬
‫ص ُد ْو ِر ال َع ِال ْي َن‬ ِ ِ ِ‫م‬
Ewe Mjuzi wa yale yaliyomo vifuani mwa viumbe.
َّ
َ‫الطاهرْين‬ َ َّ َ ُ ََ ّ َ
ِ ِ ‫ص ِل على محم ٍد و ِآل ِه‬
Mrehemu Muhammad na Aali zake watoharifu.

Mwezi Kumi Na Nane:


َ َ َ َ ْ ْ‫َ َّ ُ َّ َ ّ ن‬
‫ات ا ْس َحا ِر ِه‬
ِ ‫اللهم ن ِب ِهي ِفي ِه ِلبرك‬
Ewe Mungu wangu! Nizindue ili nipate baraka za
masiku yake.

َ ْ َ َ ْ ْ َ ْ ‫َ َ ّ ْر‬
‫ون ِو ِفي ِه قل ِبي ِب ِضي ِاء انوا ِر ِه‬
Ung’arishe moyo wangu kwa mwangaza wa nuru
zake.
َ ّ َ َ ْ َ ّ ُ ْ ُ
‫ضا ِئي ِإلى ِات َب ِاع آثا ِر ِه‬ ‫وخذ ِبك ِل اع‬
Na vishike mkono viungo vyangu vyote vifuate athari
zake.

95

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 95 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫ب ُن ْور َك َيا ُم َن ّو َر ُق ُل ْوب ْال َعا ف ْين‬


ِ ‫ِر‬ ِ ِ ِ ِ
Kwa nuru Yako ewe Mwangazi wa nyoyo za wakujuao.

Mwezi Kumi Na Tisa:


َ َ َ ْ ّ َ ْ ْ ّ َ َّ ُ ّ َ
‫اللـهم و ِفر ِفي ِه ح ِظي ِمن بركا ِت ِه‬
Ewe Mungu wangu! Niongezee fungu langu la baraka
za mwezi huu.
َ َ
‫َو َس ِّه ْل َس ِب ْي ِلي ِالى خ ْي َرا ِت ِه‬
Nisahilishie njia ya kuzifikia kheri zake.
َ َ َ َ ْ ُ َ ْ ْ َ َ
‫ل‬
‫وال تح ِرم ِني قبو حسنا ِت ِه‬
Wala usininyime kabuli ya mema yake.
ُ ْ‫م‬ ْ َ ً
‫َيا َه ِاديا ِإلى ال َح ِ ّق ال ِب ْي َن‬
Ewe uongozaye kwenye haki iliyo wazi.

Mwezi Ishirini:
َ ْ َ َ ْ َ ْ ْ َ ْ َّ ُ ّ َ
‫اللـهم افتح ِلي ِفي ِه ابواب ال ِجن ِان‬
Ewe Mungu wangu! Nifungulie milango ya Peponi.

96

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 96 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ ّ َ َ ْ َ ْ َّ ْ ْ ََ
‫النير ِان‬ ِ ‫واغ ِلق عني ِفي ِه ابواب‬
Unifungie milango ya moto.
ْ َ‫لا‬ ّ
‫َو َو ِف ْق ِني ِف ْي ِه ِل ِت َو ِة ال ُق ْر ِآن‬
Na niafikishe niweze kuisoma Qur’an.

َ‫السك ْي َنة فى ُق ُل ْوب مْالُ ْؤمن ْين‬


َّ َ
‫ل‬ ‫ز‬
ُْ َ
ِِ ِ ِِ ِ ِ ‫يا م‬
‫ن‬
Ewe Mwenye kutia utulivu nyoyoni mwa waumini.

Mwezi Ishirini Na Moja:


ً ْ َ َ َ ْ َ َ ْ ْ َ ْ َّ ُ ّ َ
‫اللـهم اجعل ِلى ِفي ِه ِالى مرضا ِتك د ِليال‬
Ewe Mungu wangu! Niwekee mwongozo wa kufikia
radhi Zako.
ً َ َ ْ َّ ْ َ ْ َ َ‫َ ا‬
‫فيه َعل َّي َسبيال‬
ِ ِ ‫ول تجعل ِللشي‬
‫ان‬‫ط‬
Usimpe shetani nafasi juu yangu.
ً ْ َ َ ً ْ َ َ َّ َ ْ َ ْ َ
‫واجع ِل الجنة ِلى من ِزال وم ِقيال‬
Na ifanye Pepo iwe ndiyo mashukio yangu na
­mapumziko.
97

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 97 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ
َ ‫الطالب ْين‬ َ َ َ َ َ
ِ ِ ‫ا�ضي حوا ِئ ِج‬
ِ ‫يا ق‬
Ewe mwenye kukidhi haja za wakuombao.

Mwezi Ishirini Na Mbili:

َ‫ضلك‬ َ ‫َا ّلل ُـه َّم ْاف َت ْح لى ف ْيه َا ْب َو‬


ْ ‫اب َف‬
ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Nifungulie milango ya fadhila
Zako.

َ‫َو َا ْنز ْل َع َل َّي ف ْيه َب َر َكاتك‬


ِ ِ ِ ِ
Niteremshie baraka Zako.

َ ‫َو َو ّف ْقني ف ْيه لُ ْوج َبات َم ْر‬


َ‫ضاتك‬
ِ ِ ِ ِ‫ِ ِ ِ ِ م‬
Niafikishe nitende viwajibishi vya radhi Zako.

َ‫َو َا ْسك ّني ف ْيه ُب ْح ُب ْو َحات َج َّناتك‬


ِ ِ ِ ِ ِِ
Na unipe makazi kwenye maliwazo ya Pepo Yako.

ْ ُ‫َيا ُمج ْي َب َد ْع َوة مْال‬


َ‫ض َط ّرْين‬
ِ ِ ِ
Ewe Mwitika wa maombi ya wenye dhiki.

98

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 98 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Ishirini Na Tatu:

ْ ُ ُّ َ ْ ْ ْ َّ ُ ّ َ
‫اللـهم اغ ِسلني ِفي ِه ِمن الذنو ِب‬
Ewe Mungu wangu! Nisafishe dhidi ya madhambi.

ْ ُ ُ ْ َ ْ ْ َّ َ
‫وط ِهرِني ِفي ِه ِمن العيو ِب‬
Nitakase na aibu.

ْ ُُْ َ َْ ْ َْ ْ َ ْ َ
‫وامت ِحن قل ِبي ِفي ِه ِبتقوى القلو ِب‬
Na uonjeshe moyo wangu uchaji wa kweli.
َ‫َيا ُمق ْي َل َع َث َرات مْالُ ْذنب ْين‬
ِِ ِ ِ
Ewe Msamehevu wa matelezo ya wenye dhambi.

Mwezi Ishirini Na Nne:


َ‫َا ّلل ُـه َّم ا ّني َا ْس َأ ُل َك ف ْيه َما ُي ْرض ْيك‬
ِ ِ ِ ِِ
Ewe Mungu wangu! Nakuomba yale
­yanayokuridhisha.
َ‫َو َا ُع ْو ُذب َك م َّما ُي ْؤذ ْيك‬
ِ ِ ِ
Na ninajikinga Kwako na yale yanayokuudhi.

99

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 99 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ‫َو َا ْس َأ ُل َك‬
َ‫الت ْوف ْي َق ف ْيه َل ْن ُاط ْي َع َك َواَل َا ْعص ْيك‬
ِ ِ ِ‫ِ ِ ِ ا‬
Na ninakuomba uniwafikishe niweze kukutii na wala
nisikuasi.

‫السا ِئ ِل ْي َن‬ َ ‫َيا َج‬


َّ ‫واد‬
Ewe uliye mkarimu kwa waombao.

Mwezi Ishirini Na Tano:

ْ ‫َا ّلل ُـه َّم‬


َ‫اج َع ْلني ف ْيه ُمح َّب ًا َل ْول َيائك‬
ِ ِ ِ‫ِ ِ ِ ِ ا‬
Ewe Mungu wangu! Nijalie niwe mwenye kuwapenda
mawalii Wako.
َ ً
‫َو ُم َع ِاديا اِل ْع َدا ِئ َك‬
Mwenye kuwachukia maadui Zako.
َ‫ُم ْس َت ّن ًا ب ُس َّنة َخ َاتم َا ْنب َيائك‬
ِ ِ ِ ِ ِ
Na mwenye kufuata mwenendo wa hitimisho la
­Mitume Wako.
َّ ‫َيا َعاص َم ُق ُل ْوب‬
‫الن ِب ِّي ْي َن‬ ِ ِ
Ewe mwenye kuzitakasa nyoyo za Mitume.

100

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 100 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Ishirini Na Sita:


ً ْ ُ ْ َ ْ ْ َ ْ َ ْ َّ ُ ّ َ
‫اللـهم اجعل سع ِيي ِفي ِه مشكورا‬
Ewe Mungu wangu! Jalia juhudi zangu ziwe ni zenye
kuthaminiwa.
ً ْ ُْ َ ْ َْ َ
 ‫وذن ِبي ِفي ِه مغفورا‬
Dhambi zangu ziwe ni zenye kusamehewa.
ً
‫َو َع َم ِلي ِف ْي ِه َم ْق ُب ْوال‬
Na amali zangu ziwe ni zenye kukubaliwa.
ً ُْ ْ َ ْ َْ َ
‫وعي ِبي ِفي ِه مستورا‬
Na aibu zangu ziwe ni zenye kusitiriwa.
َ‫السامع ْين‬
َّ َ‫َيا َا ْس َمع‬
ِ ِ
Ewe Mbora wa wasikivu.

Mwezi Ishirini Na Saba:


ْ َ ْ َ ْ َ َ ْ َ ْ ْ ‫َ ّ ُ َّ ْ ُز‬
‫اللـهم ار ق ِني ِفي ِه فضل ليل ِة القد ِر‬
Ewe Mungu wangu! Niruzuku fadhila za usiku wa
Laylatul-Qadri.

101

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 101 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ ُ ْ َ ْ ُْ َ ْ ْ ُ ُ َّْ َ
‫وص ِير امو ِري ِفي ِه ِمن العس ِر ِالى اليس ِر‬
Humo uyageuze mambo yangu mazito yawe mepesi.

‫َو ْاق َب ْل َم َع ِاذ ْي ِري‬


Zikubali nyudhuru zangu.

َ‫الذ ْن َب َو ْالو ْزر‬


َّ ّ َ َّ ُ َ
‫وحط عن ِي‬
ِ
Na uniondolee mzigo wa dhambi.

َّ ‫َيا َر ُؤ ْو ًفا ب ِع َب ِاده‬


‫الص ِال ِح ْي َن‬ ِ ِ
Ewe uliye Mpole kwa waja wema.

Mwezi Ishirini Na Nane:


َّ ‫َا ّلل ُـه َّم َو ّف ْر َح ّظي ف ْيه م َن‬
‫الن َوا ِف ِل‬ ِ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mungu wangu! Niongezee fungu langu la ibada
za ziada ndani ya mwezi huu.

َ َ ْ‫َ َ ْ ْ ْ ْ َ م‬
‫واك ِرم ِني ِفي ِه ِب ِاحض ِار السا ِئ ِل‬
Nikirimu kwa kuweza kuhudhurisha maombi.

102

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 102 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ ْ َْ ْ َ َْ َْ َ ْ ْ ّ َ َ
‫وق ِرب ِفي ِه و ِسيل ِتى ِاليك ِمن بي ِن الوسا ِئ ِل‬
Nisogezee njia miongoni mwa njia za kukufikia.
ُ ْ‫َ َ ْ اَ َ ْ َ ُ ُ ْ َ ُ م‬
‫ـاح ال ِل ِ ّح ْي َن‬ ‫يا من ل يشغله ِالح‬
Ewe Ambaye hushughulishwi na mahimizo ya
­wahimizao.

Mwezi Ishirini Na Tisa:

َّ ‫َا ّلل ُـه َّم َغ ِ ّش ِني ِف ْي ِه ب‬


‫الر ْح َم ِة‬ ِ
Ewe Mungu wangu! Nifunike kwa rehema Zako.
َ َ ْ ْ َ َ ْ ْ َّ ْ ْ ُ ْ َ
‫وارزق ِني ِفي ِه التو ِفيق وال ِعصمة‬
Niruzuku tawfiki na hifadhi.

ُّ ‫َو َط ّه ْر َق ْلبي م ْن َغ َياهب‬


‫الت ْه َم ِة‬ ِ ِ ِ ِ ِ
Na utakase moyo wangu dhidi ya giza la shaka.

َ‫ما بع َباده مْالُ ْؤمن ْين‬


ً ْ َ َ
ِ ِ ِ ِ ِ ِ ‫يا ر ِحي‬
Ewe Uliye Mrehemevu kwa waja Wake waumini.

103

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 103 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Mwezi Thelathini:
ْ ُ َ ْ َ ْ ُّ ْ َ ْ َ ْ َّ ُ ّ َ
‫اللـهم اجعل ِصي ِامى ِفي ِه ِبالشك ِر والقبو ِل‬
Ewe Mungu wangu! Ijalie Saumu yangu iwe ni yenye
kukubaliwa na kuthami­niwa.

‫ل‬ُ ْ ُ َّ ُ َ ْ َ َ ُ َ ْ َ َ ََ
، ‫على ما ترضاه ويرضاه الرسو‬
Yenye kulingana na yale uyaridhiayo na ayaridhiayo
Mtume.

ْ ُ ُ ْ‫ُ ْ َ َ ً ُ ُ ْ ُ ُ ا‬
‫محكمة فروعه ِبالصو ِل‬
Na ambayo matawi yake yameshikana madhubuti na
shina.

َّ
َ‫الطاهرْين‬ َ َّ َ ُ َ ّ َ ّ َ
ِ ِ ‫ِبح ِق س ِي ِدنا محم ٍد و ِآل ِه‬
Kwa haki ya bwana wetu Muhammad na Aali zake
watoharifu.

َ‫َو ْال َح ْم ُد هللِ َر ّب ْال َع مَال ْين‬


ِ ِ
Na kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Mola Mlezi
wa viumbe.

104

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 104 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Mikesha Kumi Ya Mwisho

V ile mwezi wa Ramadhani unapoingia hatua yake ya mwisho,


waumini wanatambua kwamba zile neema zilizotolewa ndani
ya mwezi huu zinafikia mwisho.
Wanaombea kwamba mwezi huo usingekwisha bila ya wao
kusamehewa na kujibiwa.
Dua hii ina namna ya haraka ndani yake, kana kwamba mwito wa
mwisho usio na matumaini kabla ya mwezi huo unaponyoka zake.

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬ ْ
ِ ‫ِبس ِم‬
ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

ْ‫م‬ ْ ُ َ َّ َّ ُ ّ َ
‫تاب َك الُ ْن َز ِل‬ َ
ِ ‫اللـهم ِانك قلت في ِك‬
Ewe Mungu wangu! Hakika Wewe umesema ndani ya
Kitabu Chako ulichokite­remsha:

105

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 105 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ً ُ ُ ْ ُ ْ ْ َ ْ ُ َّ َ َ َ َ ُ ْ َ
ِ ‫ان َال ِذي ا َن ِز ْل َِفي ِه ال ْق ُرآن هدى ِللن‬
‫اس‬
ّ ‫َو َب‬
‫شهر رمض‬
‫قان‬ ْ ‫ات ِمن ال ُهدى َوالف‬
‫ر‬ ٍ ‫ن‬ ‫ي‬
ِ ِ
“Ni mwezi wa Ramadhani ambao humo iliteremshwa
Qur’an kuwa mwon­gozo kwa watu, na dalili zilizo
wazi za mwongozo na upambanuzi.”

َ‫ان ب َما َا ْن َ ْزل َت ف ْيه من‬


َ ‫ض‬ َ ‫َف َع َّظ ْم َت ُح ْر َم َة َش ْهر َر َم‬
ِ ِ ِ ِ ِْ
ُ
‫القر ِآن‬
Ukaitukuza heshima ya mwezi wa Ramadhani kwa
sababu ya ile Qur’ani uliyoiteremsha humo,

ْ َ ْ ََْ ُ َ ْ َ َ َ
 ‫وخصصته ِبليل ِة القد ِر‬
Ukaufanya makhsusi kwa usiku wa Laylatul-Qadri,

ْ َ َْ ْ ً ْ َ ََْ َ َ
‫ف شه ٍر‬ِ ‫وجعلتها خيرا ِمن ال‬
Nao ukaufanya ni bora kuliko miezi elfu.

َ ‫ان َقد ْان َق‬


ْ‫ضت‬ َ ‫ض‬َ ‫َا ّلل ُـه َّم َوهذه َا ّي ُام َش ْهر َر َم‬
ِ ِ ِِ
Ewe Mungu wangu! Hivi sasa siku za Mwezi wa
­Ramadhani zimekwisha,

106

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 106 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ‫َو َل َيال ْيه َق ْد َت‬


ْ‫ص َّر َمت‬
ِ ِ
Na nyusiku zake zimetuacha,

ّ‫َو َق ْد ص ْر ُت َيا الـهي م ْن ُه ا َلى َما َا ْن َت َا ْع َل ُم به مني‬


ِ ِِ ِ ِ ِ ِ
Nawe ewe Mola wangu wajua zaidi kuliko mimi ni
hadhi gani niliyofikia humo.

َ‫َو َا ْح�صى ل َع َدده م َن ْال َخ ْلق َا ْج َمعين‬


ِ ِ ِِ ِ ِ
Nawe ndiye uwezaye kuhesabu idadi yake kuliko
­viumbe wote.
ْ‫م‬ َ َ‫لا‬ ََ َُ ََ
‫فا ْسأل َك ِب َما َسأل َك ِب ِه َم ِئك ُت َك الُ َق َّرُب ْو َن‬
Nakuomba kupitia yale waliyokuomba malaika Wako
wakuruba,

َّ ‫ َو ِع َب ُاد َك‬،‫َو َا ْنب َي ُاؤ َك مْالُ ْر َس ُل ْو َن‬


‫الص ِال ُح ْو َن‬ ِ
Manabii Wako wajumbe na waja Wako wema,

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ
‫ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Umrehemu Muhammad na Aali Muhammad.

107

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 107 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ َ َ َ َ َّ ُ َ َ َ
‫وأن تفك رقب ِتي ِمن الن ِار‬
Na uniepushe na moto,

َ ْ َ ُ
‫َوت ْد ِخل ِني ال َج َّنة ِب َر ْح َم ِت َك‬
Na uniingize Peponi kwa rehema Zako.

َّ ‫َو َا ْن َت َت َف‬
َ‫ض َل َع َّلي ب َع ْفو َك َو َك َرمك‬
ِ ِ ِ
Na unifanyie fadhila kwa msamaha Wako na ukarimu
Wako.

َ ََ َ َ
‫ت َتق َّب َل تق ُّرِبي َو ت ْس َت ِج ْي َب ُد َعا ِئي‬
Kubali kujikurubisha Kwangu na jibu dua yangu.

ْ َ ْ َ ْ َ ْ َ ْ‫َ ُ َّ َ َ َّ ا‬
‫وتمن علي ِبالم ِن يوم الخو ِف‬
Nikirimu kwa kunipa amani siku yenye khofu,

ْ َ َ ُ
‫ِم ْن ك ِ ّل َه ْو ٍل ا ْع َد ْدت ُه ِل َي ْو ِم ال ِق َي َام ِة‬
Dhidi ya kila lenye kutisha uliloliandaa kwa ajili ya
siku ya Kiyama.

108

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 108 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ َ ْ َ ْ َ ُ ْ ُ ََ
‫ِالـهي واعوذ ِبوج ِهك الك ِري ِم‬
Ewe Mola wangu! Najilinda kupitia heshima Yako
tukufu,
ْ َ‫لا‬
‫َو ِب َج ِل َك ال َع ِظ ْي ِم‬
Na utukufu Wako wenye nguvu,

ْ‫ان َو َل َياليه‬
َ ‫ض‬َ ‫َا ْن َي ْن َق�ض َي َا َّي ُام َش ْهر َر َم‬
ِ ِ ِ ِ
Zisiishe siku za mwezi wa Ramadhani na nyusiku
zake,
ُ َُ َْ َ ٌ َ َ
‫َول َك ِق َب ِلي ت ِب َعة ا ْو ذن ٌب تؤ ِاخذ ِني ِب ِه‬
Bila kunisamehe haki au dhambi utakayoniadhibu
kwayo.

َ ْ ْ َ ْ َ ّ َ َّ َ ْ َ ْ َ ُ ْ ُ ٌ َ ْ َ ْ َ
‫او خ ِطيئة ت ِريد ان تقتصها ِم ِني لم َتغ ِفرها ِلي‬
Au kosa utakalolipiza kwangu bado haujanisamehe.

‫َس ِّي ِدي َس ِّي ِدي َس ِّي ِدي‬


Bwana wangu, Bwana wangu, Bwana wangu,

109

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 109 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َأ ْس َأ ُل َك َيا اَل ال َـه إالَّ َا ْنت‬


ِ
Nakuomba ewe Ambaye hapana Mungu wa haki ila
Wewe,

ْ َ ّ َ‫ا‬ َ‫ْ ا‬
‫ِاذ ل ِال َـه إل ان َت‬
Kwani hakuna Mola wa haki ila Wewe.
ً ّ َ ْ َ ْ َ ْ َّ َ َ َ َ ْ َ َ ْ ُ ْ
‫ِان كنت ر ِضيت ع ِني ِفي هذا الشه ِر فازدد ع ِني ِرضا‬
Ikiwa umeniridhia ndani ya mwezi huu basi niongezee
ridhaa Yako.

َ ‫َوا ْن َل ْم َت ُك ْن َرض ْي َت َع ّني َفم َن ْا‬


َ ‫آلن َفا ْر‬
‫ض َع ِ ّني‬ ِ ِ ِ ِ
Na ikiwa hujaniridhia basi tokea sasa niridhie.

َ‫الراحم ْين‬
َّ َ‫َيا َا ْر َحم‬
ِ ِ
Ewe Mbora wa warehemevu.

َ ‫هللا َيا َا َح ُد َيا‬


‫ص َم ُد‬ ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Mmoja wa pekee, ewe Mwenye
­kukusudiwa.

110

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 110 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ‫َيا َم ْن َل ْم َيل ْد َو َل ْم ُي ْو َلد‬


ِ
Ewe Ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa.

ٌ‫َو َل ْم َي ُك ْن َل ُه ُك ُف ًوا َا َحد‬


Wala hana yeyote anayefanana naye.

Kithirisha Maneno Haya:

ُ‫السلاَ م‬
َّ ‫َيا ُم َل ّي َن ْال َح ِد ْي ِد ِل َد ُاو َد َع َل ْي ِه‬
ِ
Ewe uliyelainisha chuma kwa ajili ya Daud, amani iwe
juu yake.

ْ‫الض ّر َو ْال ُك َرب ْالع َظام َع ْن َا ُّي ْو َب َع َليه‬


ُ ‫ف‬ َ َ َ
‫اش‬
ِ ِ ِ َ‫ِ لا‬ ِ ِ ‫يا ك‬
‫الس ُم‬
َّ
Ewe uliyeondoa madhara na shida kubwa kwa Ayyub,
amani iwe juu yake.

َّ ‫َيا ُم َف ّر َج َه ّم َي ْع ُق ْو َب َع َل ْي ِه‬
ُ ‫الس‬
‫الم‬ ِ ِ
Ewe uliyemfariji Yakub, amani iwe juu yake.

111

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 111 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ ‫ف َع َل ْي ِه‬
ُ‫السالم‬ َ ُ ُْ ّ َ َ َُّ َ
‫يا من ِفس غ ِم يوس‬
Ewe uliyemuondolea simanzi Yusuf, amani iwe juu
yake.

َ َ
‫على ُم َح َّم ٍد َو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ َ ‫ص ِ ّل‬
Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad,
َ‫ع َل ْيه ْم َأ ْج َمع ْين‬ َ ‫ص ّل َي‬َ ‫ت‬ ُ ‫َك َما َأ ْن َت َأ ْه ُل ُه َأ ْن‬
ِ ِ ِ
Kama unavyostahili kuwarehemu wote.
ُ‫َو ْاف َع ْل ب ْي َما َأ ْن َت َأ ْه ُل ُه َواَل َت ْف َع ْل ب ْي َما َأ َنا َأ ْه ُله‬
ِ ِ
Nifanyie yale unayostahiki, wala usinifanyie yale
­ninayostahili.

Dua Ya Usiku Wa Mwezi


Ishirini Na Moja

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
112

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 112 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali


Muhammad.

َ َّ ْ َّ َ ْ ُ َ
‫يا موِلج اللي ِل ِفي النه ِار‬
Ewe Mwenye kuutia usiku katika mchana
َّ َّ ‫َو ُم ْول َج‬
‫الن َه ِار ِفي الل ْي ِل‬ ِ
Na Mwenye kuutia mchana katika usiku.

ّ َ ْ‫َ ُ ْ َ ْ َ ّ َ م‬
‫يامخ ِرج الح ِي ِمن ال ِي ِت‬
Ewe Mwenye kukitoa kilicho hai toka kwenye kilicho
maiti
ْ َ ْ‫ْ م‬
‫َو ُمخ ِر َج ال ِّي ِت ِم ْن ال َح ّ ِي‬
Na Mwenye kukitoa kilicho maiti toka kwenye kilicho
hai.

‫اب‬ َ ‫َيا َراز َق َم ْن َي َش ُاء ب َغ ْير ح‬


‫س‬
ٍ ِ ِ ِ ِ
Ewe Mwenye kumruzuku umtakaye bila kipimo.

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا َر ْح ٰم ُـن‬
Ewe Allah, ewe Mwingi wa rehema.

113

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 113 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا َر ِح ْي ُم‬
Ewe Allah, ewe Mrehemevu.

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ ا‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬
َ‫ا‬
ُ‫َو اْاللء‬َ
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba umrehemu Muhammad na Aali Muham-
mad,

َ ُّ ْ َ ْ َّ َ ْ َ َ ْ َ ْ ََ
‫داء‬
ِ ‫وان تجعل ِاس ِمي ِفي ه ِذ ِه الليل ِة ِفي السع‬
Na uliweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri.
ُّ
‫َو ُر ْو ِح ْي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema.

114

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 114 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َوا ْح َسان ْي في ع ّل ّي ْين‬


ِ ِِ ِ ِ ِ
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu.
ً ْ
‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.
َْ ُ َُ ًَْ َ َ ََ ْ ََ
‫اشر ِب ِه قل ِبي‬
ِ ‫وان تهب ِلي ي ِقينا تب‬
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu.
َّ ْ ً
‫َوِا ْي َمانا ُيذ ِه ُب الش َّك َع ِ ّني‬
Na imani itakayoniondolea shaka.

ْ‫ُت ْر ِض َيني ب َما َق َس ْم َت لي‬


ِ ِ ِ
Na uniridhie kwa kile ulichogawa kwa ajili yangu.
ً َ ْ‫ا‬ ً ْ ُّ
‫الدن َيا َح َس َنة َّو ِفي ال ِخ َر ِة َح َس َنة‬ ‫َوآ ِت َنا ِفي‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na utuepushe na moto uchomao.

115

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 115 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬


ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫الن َاب َه‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

ً َّ َ ُ َ َ ً َّ َ ُ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محمدا‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad,

َ َّ ُ ْ َ َ َ ْ َ َ
‫السال ُم‬ ‫علي ِه وعلي ِهم‬
Amani iwe juu yake na juu yao.

Dua Ya Usiku Wa Mwezi


Ishirini Na Mbili

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

116

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 116 6/16/2016 4:29:24 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِل على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.
َّ َّ ‫َيا َسال َخ‬
‫الن َه ِار ِم َن الل ْي ِل‬ ِ
Ewe Mwenye kuutoa mchana toka kwenye usiku,
ْ َ َ
‫ف ِاذا َن ْح ُن ُمظ ِل ُم ْو َن‬
Na hatimaye ghafla tunakuwa kwenye giza.

َ ُ ْ َّ ‫َ ُ ْ ي‬
‫س مِل ْس َتق ّ ِر َها ِب َت ْق ِد ْي ِر َك‬
ِ ‫ومج ِر الشم‬
Na Mwenye kulipeleka jua kwenye kituo chake kwa
uwezo Wako.

‫َيا َع ِزْي ُز َيا َع ِل ْي ُم‬


Ewe Mwenye nguvu, ewe Mjuzi.

َْ ْ َ َْ َ
‫َو ُمق ِّد َر الق َم ِر َم َن ِاز َل َح َّتى َع َاد كال ُع ْر ُج ْو ِن الق ِد ْي ِم‬
Na Mwenye kuupimia mwezi vituo mpaka ukarudia
kuwa kama kole la mtende kuukuu.

117

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 117 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ ّ ُ ََُْ ُْ ّ ُ َُْ َ
،‫ ومنتهى ك ِل رغب ٍة‬،‫يا نور ك ِل نو ٍر‬
Ewe Nuru ya kila nuru na kilele cha kila raghba.

َ ْ ّ ُ َّ َ َ
،‫وو ِلي ك ِل ِنعم ٍة‬
Na Mmiliki wa kila neema.
ُ ‫َيا‬
،‫هللا َيا َر ْح ٰم ُـن‬
Ewe Allah! Ewe Mwingi wa rehema.

ُ ْ ُّ ُ َُ َ
،‫يا هللا يا قدوس‬
Ewe Allah, ewe Mtakatifu.
ُ‫ َيا َف ْرد‬،‫َيا َا َح ُد َيا َواح ُد‬
ِ
Ewe mmoja, ewe wa pekee, ewe mpweke.
ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ ا‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬
ُ،‫اللء‬ َ‫ا‬ َ ْ‫َ ا‬
‫و‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

118

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 118 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ َ ُ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
‫وآل محم ٍد‬ِ ‫اسألك ان تص ِلي على محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

َ ‫الس‬
ُّ َ ْ َّ َ ‫َو َا ْن َت ْج َع َل ا ْسم ْي في‬
،‫داء‬
ِ ‫ع‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫ة‬
ِِ ‫ل‬ ‫ي‬ ‫الل‬ ‫ه‬ ‫ذ‬ ‫ه‬
ِِ ِ ِ ِ
Na uliweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri.

َ ُّ َ َ ْ ‫َو ُر‬
،‫داء‬
ِ ‫ه‬ ‫الش‬ ‫و ِحي مع‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema.
ّ
،‫َوِا ْح َسا ِن ْي ِفي ِع ِل ِّي ْي َن‬
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu.

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.
َْ
،‫اش ُر ِب ِه قل ِبي‬ َ ‫َو َا ْن َت َه َب لي َيق ْي ًنا ُت‬
‫ب‬
ِ ِ ِ
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu.

119

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 119 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ّ َ َّ َّ ُ ْ ُ ً َ ْ َ
،‫وايمانا يذ ِهب الشك عني‬
Na imani itakayoniondolea shaka.
َ ْ َ َ َ َ ُْ
،‫تر ِضي ِني ِبما قسمت ِلي‬
Na unifanye niridhike na kile ulichogawa kwa ajili
yangu.
ً َ َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ ا‬
‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفى ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na utuepushe na moto uchomao.
َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬
ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako.
َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako.

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ ُ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali Muhammad.

120

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 120 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫السلاَ م‬
َّ ‫َع َل ْي ِه َو َع َل ْيه ُم‬
ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

Dua Ya Usiku Wa Mwezi


Ishirini Na Tatu

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِل على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.

ْ َ ْ َ ْ َ َّ َ َ
‫يا رب ليل ِة القد ِر‬
Ewe Mola Mlezi wa usiku wa Laylatil-Qadri.

ْ َ َْ ْ ً َْ ََ َ َ
،‫ف شه ٍر‬ِ ‫اعلها خيرا ِمن ال‬
ِ ‫وج‬
Na uliyeufanya kuwa mbora kuliko miezi elfu.

121

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 121 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ ْ َ َ َّ ْ َّ َّ َ َ
،‫ وال ِجب ِال وال ِبح ِار‬،‫ورب اللي ِل والنه ِار‬
Mola Mlezi wa usiku na mchana, milima na
­mabahari,

َ َّ َ ْ َ ْ‫َ ُّ ْ َ أْ َ ْ َ َ أ‬
،‫ض والسم ِاء‬ِ ‫ والر‬،‫والظل ِم والنو ِار‬
Giza na nuru, ardhi na mbingu.

َ ‫َيا َبار ُئ َيا ُم‬


،‫ص ّ ِو ُر‬ ِ
Ewe Muumbaji, ewe Msanifu maumbo.
ُ ‫ان َيا َم َّن‬
،‫ان‬ ُ ‫َيا َح َّن‬
Ewe mwenye huba, ewe mwenye huruma.

ُ ‫َيا‬
،‫هللا َيا َر ْح ٰم ُن‬
Ewe Allah, ewe Mwingi wa rehema.
َ ُ َ
‫هللا َيا ق ُّي ْو ُم‬ ‫يا‬
Ewe Allah, ewe Mwenye kusimamia mambo.

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا َب ِد ْي ُع‬
Ewe Allah, ewe Muumbaji.

122

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 122 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬
َ‫اْ َ ا‬
،‫َوالل ُء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

ُّ ‫الل ْي َل ِة في‬
،‫الس َع َد ِاء‬
َّ
‫ه‬ ‫هذ‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫ي‬‫م‬ ْ ‫َو َا ْن َت ْج َع َل ِا‬
‫س‬
ِ ِِ ِ ِ
Na uliweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri.

ُّ
‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema.
ّ
،‫َوِا ْح َسا ِني ِفي ِع ِل ِّي ْي َن‬
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu

123

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 123 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.
َْ ُ َُ ً ْ َ َ ََ ْ ََ
‫اشر ِب ِه قل ِبي‬
ِ ‫وان تهب ِلي ي ِقينا تب‬
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu.
َّ ً َْ َ
،‫ذه ُب الش َّك َع ّني‬
ِ ‫ي‬ُ ‫انا‬ ‫وايم‬
Na imani itakayoniondolea shaka.
َ ُ
،‫ت ْر ِض َي ِني ِب َما ق َس ْم َت ِلي‬
Na uniridhie kwa kile ulichogawa kwa ajili yangu.
ً َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ آ‬
،‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفي ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.
ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na utuepushe na moto uchomao.
َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬
ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

124

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 124 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,
ً َّ َ ُ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ َ َ ْ َّ َ
‫آل ُم َح َّم ٍد‬
َ ‫دا َو‬ ‫والتوبة والتو ِفيق مِلا وفقت له محم‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad,

ُ‫السلاَ م‬
َّ ‫َع َل ْي ِه َو َع َل ْيه ُم‬
ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Nne

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬ ْ
ِ ‫ِبس ِم‬
ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.
َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫ص ِلي َعلى ُم َح َّم ٍد َو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ ‫اللهم‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.
ً َ َّ َ ‫ َو‬،‫ص َباح‬ ْ‫َ َ َ ا‬
،‫اع َل الل ْي ِل َسكنا‬
ِ ‫ج‬ ْ ‫ال‬
ِ ِ ‫يا ف ِالق‬
Ewe Mpasuaji wa asubuhi na Mwenye kuufanya
usiku uwe kitulizo,

125

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 125 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً َ ْ ُ َ َ ْ َ ْ َّ َ
،‫س والقم ِر حسبانا‬
ِ ‫والشم‬
Na jua na mwezi kwa ajili ya hesabu.

‫َيا َع ِزْي ُز َيا َع ِل ْي ُم‬


Ewe Mtukufu Mjuzi,

ْ َّ َ ّ َ ْ‫َ َ م‬
‫ل‬
، ِ ‫يا ذا ال ِن والطو‬
Ewe Mwenye ukarimu na uwezo,

ْ َ ْ َ َّ ُ ْ َ
‫ل‬
، ِ ‫والقو ِة والحو‬
Nguvu na ujanja,

َ ْ ْ‫َ ْ َ ْ َ ا‬
،‫النع ِام‬ِ ‫والفض ِل و‬
Fadhila na neema,

َ ْ ْ‫َ ْ َ لاَ َ ا‬
،‫الكر ِام‬ِ ‫والج ِل و‬
Utukufu na uungwana.

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا َر ْح ٰم ُن‬
Ewe Allah, ewe Mwingi wa rehema.

126

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 126 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ،‫هللا َيا َف ْر ُد َيا و ْتر‬


ُ ‫َيا‬
ِ
Ewe Allah, ewe Wa pekee, ewe Mmoja.

،‫اط ُن‬ َ ‫هللا َيا َظاه ُر َيا‬


‫ب‬ ُ ‫َيا‬
ِ ِ
Ewe Allah, ewe Uliye dhahiri, ewe Uliye wa siri.

َ ْ َ ّ َ‫َ َ ُّ اَ َ ا‬
،‫يا حي ل ِالـه ِإل انت‬
Ewe Hai, hakuna Mola wa haki ila Wewe.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ أْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬
َ‫اْ َ ا‬
،‫َوالل ُء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba umrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad,

َ ‫الس‬
ُّ َ ْ َّ َ ‫اسمي في‬
ْ َ َ ‫َو َا ْن َت ْج‬
،‫داء‬
ِ ‫ع‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫ة‬
ِِ ‫ل‬ ‫ي‬ ‫الل‬ ‫ه‬ ‫ذ‬ ‫ه‬
ِِ ِ ِ ‫ل‬ ‫ع‬
Na uliweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

127

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 127 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُّ
،‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,

ّ
،‫َوِا ْح َسا ِني ِفي ِع ِل ِّي ْي َن‬
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.

َْ
،‫اش ُر ِب ِه قل ِبي‬ َ ‫َو َا ْن َت َه َب لي َيق ْي ًنا ُت‬
‫ب‬
ِ ِ ِ
Nakuomba unipe yakini ambayo itaugusa moyo
­wangu.

ّ َ ّ َّ ُ َ ْ َ ً َ ْ َ
،‫وِايمانا يذهب ِبالش ِك ع ِني‬
Na imani itakayoniondolea shaka.

َ ُ
،‫ت ْر ِض َي ِني ِب َما ق َس ْم َت ِلي‬
Na unifanye niridhike na kile ulichogawa kwa ajili
yangu.

128

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 128 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً َ َ َ َ َ ً َ َ َ ْ ُّ َ
 ،‫اآلخر ِة حسنه‬
ِ ِ ‫ي‬ ‫ف‬ ‫و‬ ‫ة‬ ‫ن‬‫س‬ ‫ح‬ ‫يا‬ ‫ن‬ ‫الد‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫نا‬
ِ ِ‫ت‬ ‫آ‬‫و‬
Tupe wema duniani na Akhera.

َّ َ ََ َ َ
‫و ِقنا عذاب الن ِار‬
Na utuepushe na moto uchomao.

َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬


ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫ و‬،‫والرغبة ِاليك‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ ُ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ َ ْ َّ َ
‫والتوبة والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad,

ُ‫السلاَ م‬
َّ ‫َع َل ْي ِه َو َع َل ْيه ُم‬
ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

129

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 129 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na


Tano

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye Kurehemu.
َ َ َّ ُ َّ َ
‫ص ِ ّل َعلى ُم َح َّم ٍد َّو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ ‫اللهم‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.
ً َ َ َ َّ َ ً َ ْ َّ َ َ َ
،‫ والنه ِار معاشا‬،‫اعل اللي ِل ِلباسا‬
ِ ‫يا ج‬
Ewe Uliyeufanya usiku vazi na mchana maisha,
ً ََْ َ ْ َ ً َ ْ َ ْ‫َ ا‬
،‫ وال ِجب ِال اوتادا‬،‫ض ِمهادا‬
ِ ‫والر‬
Ardhi tandiko na milima vigingi.

ُ‫هللا َيا َق ِاهر‬


ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Kahari,

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا َج َّب ُار‬
Ewe Allah, ewe Jabari.

130

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 130 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا َس ِم ْي ُع‬
Ewe Allah, ewe Msikivu.
َ ُ َ
‫هللا َيا ق ِرْي ُب‬ ‫يا‬
Ewe Allah, ewe Uliye karibu.

ُ ‫َيا‬
‫هللا َيا ُم ِج ْي ُب‬
Ewe Allah, ewe Mwenye kujibu.

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬ 
ُ،‫َو آْال اَلء‬
Una majina mazu­ri, na mifano bora, hadhi na neema.
َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫ص ِل َي َعلى ُم َح َّم ٍد َو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ ‫اسالك ان ت‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

131

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 131 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ ُّ َ ْ َّ ْ َ َ ْ َ ْ ََ
،‫هذ ِه الليل ِة ِفي السعد ِاء‬
ِ ‫وان تجعل اس ِمي ِفي‬
Na liweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

ُّ
،‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,

َ،‫َوا ْح َساني في ع ّل ّي ْين‬


ِ ِِ ِ ِ ِ
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu,

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.

َْ ُ َُ ً ْ َ َ ََ ْ ََ
،‫اشر ِب ِه قل ِبي‬
ِ ‫وان تهب ِلي ي ِقينا تب‬
Nakuomba unipe yakini ambayo itaugusa moyo
­wangu.

َّ ْ ً
،‫َوِا ْي َمانا ُيذ ِه ُب الش َّك َع ِ ّني‬
Na imani itakayoniondolea shaka.

132

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 132 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ َ َ َ َُْ
،‫وتر ِضي ِني ِبما قسمت ِلي‬
Na uniridhie kwa kile ulichogawa kwa ajili yangu.
ً ْ‫آ‬ ً ْ ُّ
‫الدن َيا َح َس َنة َو ِفي ال ِخ َر ِة َح َس َنة‬ ‫َوآ ِت َنا ِفي‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na utuepushe na moto uchomao.
ْ ُ ْ ْ
‫َو ْار ُزق ِني ِف ْي َها ِذك َر َك َوشك َر َك‬
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,
َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako na kurejea Kwako,
ً َّ َ َ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫آل ُم َح َّم ٍد‬
َ ‫دا َو‬ ‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محم‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad.

ُ‫َع َل ْيه َو َع َل ْيه ُم السَّلاَ م‬


ِ ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

133

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 133 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Sita

َّ ‫الر ْحمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِل على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.
َّ َ َ َ
،‫الن َه ِار َآي َت ْي ِن‬
َّ ‫الل ْيل َو‬
ِ ‫اعل‬ ِ ‫يا ج‬
Ewe Uliyefanya usiku na mchana kuwa alama mbili.
ً َ ْ ُ َ َّ َ َ َ َ َ َ ْ َّ َ َ َ َ ْ َ َ
‫يا من محا آية اللي ِل وجعل آية النه ِار مب ِصرة‬
Ewe Uliyefuta alama ya mchana na ukafanya alama
ya usiku ni yenye kuangaza,
ً ْ َ ُ ْ ً ْ َ ُْ ََْ
،‫ض َوانا‬ ‫ِلتبتغوا فضال ِمنه و ِر‬
Ili humo mtafute fadhila na radhi.
ً ْ َْ َْ ّ ُ َ ّ َُ َ
،‫يا مف ِصل ك ِل �شي ٍء تف ِصيال‬
Ewe Uliyetenganisha kila kitu peke yake.

134

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 134 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ‫َيا َماج ُد َيا َو ّه‬


،‫اب‬ ِ
Ewe Mwenye kusifika kwa uzuri, ewe Mpaji.

،‫هللا َيا َج َو ُاد‬


ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Mkarimu.

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ أْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬
َ‫آْ ا‬
،‫َوالل ُء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

ُّ ‫الل ْي َل ِة في‬
،‫الس َع َد ِآء‬
َّ
‫ه‬ ‫ذ‬ ْ ‫َو َا ْن َت ْج َع َل‬
َ ‫اسمي في‬
‫ه‬
ِ ِِ ِ ِ
Na liweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

135

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 135 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُّ
‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,

َ،‫َوا ْح َساني في ع ّل ّي ْين‬


ِ ِِ ِ ِ ِ
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu,

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.

َْ ُ َُ ً ْ َ َ ََ ْ ََ
‫اشر ِب ِه قل ِبي‬
ِ ‫وان تهب ِلي ي ِقينا تب‬
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu.

ّ َ َّ َّ ُ ُ ً َ ْ َ
،‫ذهب الشك عني‬ِ ‫وايمانا ي‬
Na imani itakayoniondolea shaka.

َ ْ َ َ َ َ َُْ
،‫وتر ِضي ِني ِبما قسمت ِلي‬
Na niridhie kwa kile ulichogawa kwa ajili yangu.

136

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 136 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ آ‬
،‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفي ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na tuepushe na moto uchomao.

َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬


ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako na shukrani Yako,

َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ ُ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad.

ُ‫السلاَ م‬
َّ ‫َع َل ْي ِه َو َع َل ْيه ُم‬
ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

137

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 137 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Usiku Wa Mwezi


Ishirini Na Saba

َّ ‫الر ْح ٰمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬ ْ
ِ ‫ِبس ِم‬
ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.

ً َ ُ َ ْ َ َ َ َ ْ ْ َ َ ّ ّ َّ َ َ
،‫الظ ِل ولو ِشئت لجعلته س ِاكنا‬
ِ ‫يا ماد‬
Ewe Mwenye kukiongeza kivuli, na lau ungetaka basi
ungekifanya kision­gezeke.

ً ْ َ ْ َ َ َ ْ َّ َ ْ َ َ َ
‫وجعلت الشمس علي ِه د ِليال‬
Umelifanya jua kuwa dalili juu yake,

ً ْ َ ً ْ َ َ ْ َ ُ َ ْ َ َ َّ ُ
،‫ثم قبضته ِاليك قبضا ي ِسيرا‬
Kisha ukakichukua Kwako kwa wepesi kabisa.

138

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 138 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َ َ ْ ُ ْ َ َّ ْ َ ْ ْ َ َ آْ ا‬
،‫يا ذا الجو ِد والطو ِل وال ِكب ِري ِاء والل ِء‬
Ewe Mwenye ukarimu na nguvu, heshima na neema.
َّ َْ ْ َ َّ‫ال‬ َ‫ا‬
‫ل ِال َـه ِإ ان َت َع ِال ُم الغ ْي ِب َوالش َه َاد ِة‬
Hapana Mungu wa haki ila Wewe Mjuzi wa
­yasiyoonekana na yanayoo­nekana.

ُ ‫الر‬
،‫حيم‬ ُ ‫الر ْح‬
َّ ‫من‬ َّ
Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.
ّ َ َ‫ا‬
ُ ‫إال َا ْن َت َيا ُق ُّد ْو‬
‫س‬ ‫ل ِإله‬
Hapana Mungu wa haki ila Wewe, ewe Mtakatifu.

ُ‫َيا َسلاَ ُم َيا ُم ْؤمن‬


ِ
Ewe Mwenye salama, ewe Mtoaji wa amani.

‫َيا ُم َه ْي ِم ُن َيا َع ِزْي ُز‬


Ewe Mwangalizi, ewe Mwenye nguvu.
ّ ‫َيا َج ّب ُار َيا ُم َت‬
‫كب ُر‬
ِ
Ewe Jabari, ewe Mkubwa.

139

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 139 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ُ َ
‫هللا َيا خ ِال ُق‬ ‫يا‬
Ewe Allah, ewe Muumbaji.

َ ‫َيا َبار ُئ َيا ُم‬


،‫ص ّ ِو ُر‬ ِ
Ewe Mtengenezaji, ewe Msanifu wa umbo.

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬ 
َ‫آْ ا‬
،‫َوالل ُء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

ُّ ‫الل ْي َل ِة في‬
،‫الس َع َد ِاء‬
َّ
‫ه‬ ‫هذ‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫ي‬‫م‬ ْ ‫َو َا ْن َت ْج َع َل‬
‫اس‬
ِ ِِ ِ ِ
Na liweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

140

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 140 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُّ
،‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,
ّ
،‫َوِا ْح َسا ِني ِفي ِع ِل ِّي ْي َن‬
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu,
ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.
َْ
،‫اش ُر ِب ِه قل ِبي‬ َ ‫َو َا ْن َت َه َب لي َيق ْي ًنا ُت‬
‫ب‬
ِ ِ ِ
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu.
ّ َ َّ َّ ُ ْ ُ ً َ ْ َ
،‫وِايمانا يذ ِهب الشك ع ِني‬
Na imani itakayoniondolea shaka,
َ ُ
،‫َوت ْر ِض َي ِني ِب َما ق َس ْم َت ِلي‬
Na niridhie kwa kile ulichogawa kwa ajili yangu.
ً َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ آ‬
‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفي ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.

141

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 141 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na tuepushe na moto uchomao.

َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬


ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬


ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ َ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali Muhammad.

ُ‫َع َل ْيه َو َع َل ْيه ُم السَّلاَ م‬


ِ ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

142

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 142 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Dua Ya Usiku Wa Mwezi


Ishirini Na Nane

َّ ‫الر ْحمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِل على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.

َ َ ْ ْ َّ َ َ َ
،‫يا خ ِازن اللي ِل ِفي الهو ِاء‬
Ewe Uliye uhifadhi usiku katika anga,

ُّ ‫َو َخاز َن‬


َّ ‫الن ْور في‬
،‫الس َم ِاء‬ ِِ ِ
Na uliyehifadhi nuru katika mbingu,

ْ َّ‫َ َ َ َّ َ َ ْ َ َ َ َ َ اْ َ ْ ال‬
 ‫ض ِإ ِب ِاذ ِن ِه‬
ِ ‫وما ِنع السم ِاء أن تقع على الر‬
Na Uliyezuia mbingu isiidondokee ardhi ila kwa idhini
Yake,

143

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 143 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َ َ َ ُ َ َ ْ َ ُ ْ ا‬
،‫وح ِابسهما ان تزول‬
Na Mwenye kuzishika zisitoweke.
َ
،‫ َيا غ ُف ْو ُر َيا َدا ِئ ُم‬،‫َيا َع ِل ْي ُم َيا َع ِظ ْي ُم‬
Ewe Mjuzi, ewe Mtukufu, ewe Msamehevu, ewe Wa
daima.

ْ ُ ُ ْ ْ َ َ َ َ ُ َ َُ َ
 ،‫اعث من ِفي القبو ِر‬
ِ ‫ يا ب‬،‫يا هللا يا وا ِرث‬
Ewe Allah, ewe Mrithi, ewe Mwenye kuwafufua
­waliyomo makaburini.

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ أْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬
َ‫ا‬
ُ،‫َو آْاللء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

144

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 144 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ َ ُّ َ ْ َّ َ ْ َ َ ْ َ ْ ََ
،‫وان تجعل اس ِمي ِفي ه ِذ ِه الليل ِة ِفي السعد ِآء‬
Na liweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

ُّ
،‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,

َ،‫َوا ْح َساني في ع ّل ّي ْين‬


ِ ِِ ِ ِ ِ
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu,

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.

َْ ُ َُ ً ْ َ َ ََ ْ ََ
،‫اشر ِب ِه قل ِبي‬
ِ ‫وان تهب ِلي ي ِقينا تب‬
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo itaugusa
moyo wangu,

ّ َ َّ َّ ُ ْ ُ ً َ ْ َ
،‫وِايمانا يذ ِهب الشك ع ِني‬
Na imani itakayoniondolea shaka,

145

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 145 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ َ َ َ َُْ
،‫وتر ِضي ِني ِبما قسمت ِلي‬
Na nifanye niridhike na kile ulichogawa kwa ajili
yangu.

ً َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ آ‬
‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفي ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫الن ِار ال َح ِرْي ِق‬ ‫و ِقنا عذاب‬
Na tuepushe na moto uchomao.

ْ ُ ْ ْ
‫َو ْار ُزق ِني ِف ْي َها ِذك َر َك َوشك َر َك‬
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ َ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali Muhammad.

146

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 146 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫َع َل ْيه َو َع َل ْيه ُم السَّلاَ م‬


ِ ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Ishirini Na Tisa

َّ ‫الر ْحمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬ ْ
ِ ‫ِبس ِم‬
ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye kurehemu.

َّ َ ُ َّ َّ َ ُ َ َ ّ َ َّ ُ َّ َ
‫اللهم ص ِل على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.

َّ َ َ ْ َّ َ ّ َ ُ َ
ِ ‫يا مك ِور اللي ِل على الن‬
،‫هار‬
Ewe Mwenye kuukunja usiku juu ya mchana,

ْ َّ َ َ َ َّ َ ّ َ ُ َ
،‫ومك ِور النه ِار على اللي ِل‬
Na Mwenye kuukunja mchana juu ya usiku.

‫َيا َع ِل ْي ُم َيا َح ِك ْي ُم‬


Ewe Mjuzi Mwenye hekima.

147

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 147 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ ْ َ ْ‫َ َ َّ ا‬
‫اب‬
ِ ‫يا رب الرب‬
Ewe Mola Mlezi wa walezi.

،‫ات‬ ‫اد‬ َ ‫َو َس ّي َد‬


َ ‫الس‬
ِ ِ
Ewe Bwana wa mabwana.

َ‫اَل ا َله إالَّ َا ْنت‬


ِ
Hakuna Mungu wa haki ila Wewe.

ْ َ َْ
،‫َيا اق َر َب ِال َّي ِم ْن َح ْب ِل ال َو ِر ْي ِد‬
Ewe Uliye karibu nami kuliko mshipa wa moyo.

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬ 
َ‫آْ ا‬
،‫َوالل ُء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

148

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 148 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

ُّ ‫الل ْي َل ِة في‬
،‫الس َع َد ِاء‬
َّ
‫ه‬ ‫هذ‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫ي‬‫م‬ ْ ‫َو َا ْن َت ْج َع َل‬
‫اس‬
ِ ِِ ِ ِ
Na liweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

ُّ
،‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,
ّ
،‫َوِا ْح َسا ِني ِفي ِع ِل ِّي ْي َن‬
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu,

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.
َْ
،‫اش ُر ِب ِه قل ِبي‬ َ ‫َو َا ْن َت َه َب لي َيق ْي ًنا ُت‬
‫ب‬
ِ ِ ِ
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu,

149

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 149 6/16/2016 4:29:25 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ّ َ َّ َّ ُ ْ ُ ً َ ْ َ
،‫وِايمانا يذ ِهب الشك ع ِني‬
Na imani itakayoniondolea shaka,
َ ْ َ َ َ َ َُْ
،‫وتر ِضي ِني ِبما قسمت ِلي‬
Na nifanye niridhike kwa kile ulichogawa kwa ajili
yangu.
ً َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ آ‬
‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفي ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َ ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫و ِقنا عذاب الن ِار الح ِري ِق‬
Na tuepushe na moto uchomao.
َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬
ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,
َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ َ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad.

150

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 150 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ‫َع َل ْيه َو َع َل ْيه ُم السَّلاَ م‬


ِ ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

Dua Ya Usiku Wa Mwezi Thelathini

َّ ‫الر ْحمن‬
‫الر ِح ْي ِم‬ َّ ‫هللا‬
ِ ‫م‬ ْ‫ب‬
‫س‬
ِ ِ ِ
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema,
Mwenye ­kurehemu.

َ َ َّ ُ َّ َ
‫ص ِ ّل َعلى ُم َح َّم ٍد َّو ِآل ُم َح َّم ٍد‬ ‫اللهم‬
Ewe Mungu wangu! Mrehemu Muhammad na Aali
Muhammad.

ُ،‫ْال َح ْم ُد هللِ اَل َشرْي َك َله‬


ِ
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu asiye na
mshirika yeyote.

ْ َ َ َ ََْ َ َ ُ ْ َ ْ
‫الحمد هللِ كما ينب ِغي ِلكر ِم وج ِه ِه‬
Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu kama inavyo-
pasa kwa utukufu wa heshima Yake,

151

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 151 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ،‫َوع ّز َجالله َو َك َما ُه َو َا ْه ُله‬


ِِ ِِ
Na nguvu ya utukufu Wake, na kama anavyostahiki.

ْ ُ ْ َ ْ ُ َ ُ ْ ُ َ ُ ْ ُّ ُ َ
،‫يا قدوس يا نور يا نور القد ِس‬
Ewe Mtukufu, ewe Nuru, ewe Nuru ya utukufu.
َّ
،‫َيا ُس ُّب ْو ُح َيا ُم ْن َتهى التس ِبي ِح‬
ْ ْ
Ewe Mtukuka, ewe kilele cha utukuzo.

َ ْ َّ َ َ َ ُ َْ َ
،‫اعل الرحم ِة‬ِ ‫يا رحمـن يا ف‬
Ewe Mwingi wa rehema, ewe Mtendaji wa rehema.

ُ ْ َ َ ُْ َ َُ َ
 ،‫يا هللا يا ع ِليم يا ك ِبير‬
Ewe Allah, ewe Mjuzi, ewe Mkubwa.
ُ ْ َ َُ َ
ُ،‫ف َيا َج ِل ْيل‬ ‫يا هللا يا ل ِطي‬
Ewe Allah, ewe Mpole, ewe Jalili.

ُ ‫َيا‬
،‫هللا َيا َس ِم ْي ُع َيا َب ِص ْي ُر‬
Ewe Allah, ewe Msikivu, ewe Mwenye kuona.

152

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 152 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ُ ‫هللا َيا‬
‫هللا‬ ُ ‫هللا َيا‬
ُ ‫َيا‬
Ewe Allah, ewe Allah, ewe Allah.

ُ‫ َو ْال ِك ْبرَياء‬،‫ال ْال ُع ْل َيا‬ َ ْ‫َ َ اْ َ ْ َ ُ ْ ُ ْ َ َ أ‬


ُ ‫ال ْم َث‬
ِ ‫ و‬،‫لك السماء الحسنى‬ 
َ‫آْ ا‬
،‫َوالل ُء‬
Una majina mazuri, na mifano bora, hadhi na neema.

َّ َ ُ َ َّ َ ُ ََ َ َّ ُ ْ َ َ َُ ْ َ
،‫اسالك ان تص ِلي على محم ٍد و ِآل محم ٍد‬
Nakuomba mrehemu Muhammad na Aali
­Muhammad.

ُّ ‫الل ْي َل ِة في‬
،‫الس َع َد ِاء‬
َّ
‫ه‬ ‫هذ‬ ‫ي‬‫ف‬ ‫ي‬‫م‬ ْ ‫َو َا ْن َت ْج َع َل‬
‫اس‬
ِ ِِ ِ ِ
Na liweke jina langu usiku huu katika watu wenye
kheri,

ُّ
،‫َو ُر ْو ِحي َم َع الش َه َد ِاء‬
Roho yangu pamoja na wahanga wema,
ّ
،‫َوِا ْح َسا ِني ِفي ِع ِل ِّي ْي َن‬
Matendo yangu ndani ya daftari la watukufu,

153

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 153 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

ً ْ
،‫َوِا َس َاء ِتي َمغ ُف ْو َرة‬
Na makosa yangu yafutwe.

َْ
،‫اش ُر ِب ِه قل ِبي‬ َ ‫َو َا ْن َت َه َب لي َيق ْي ًنا ُت‬
‫ب‬
ِ ِ ِ
Nakuomba unipe yakini ambayo kwayo utaugusa
moyo wangu,

ّ َ َّ َّ ُ ْ ُ ً َ ْ َ
،‫وِايمانا يذ ِهب الشك ع ِني‬
Na imani itakayoniondolea shaka,

َ ُ
،‫َوت ْر ِض َي ِني ِب َما ق َس ْم َت ِلي‬
Na niridhie kwa kile ulichogawa kwa ajili yangu.

ً َ َ َ َ ْ‫ُّ ْ َ َ َ َ ً َ آ‬
‫َوآ ِت َنا ِفي الدنيا حسنة و ِفي ال ِخر ِة حسنة‬
Tupe wema duniani na Akhera.

ْ َّ َ َ َ َ َ
،‫الن ِار ال َح ِرْي ِق‬ ‫و ِقنا عذاب‬
Na utuepushe na moto uchomao.

154

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 154 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

َ‫َو ْار ُز ْقني ف ْي َها ذ ْك َر َك َو ُش ْك َرك‬


ِ ِ ِ
Niruzuku humo utajo Wako, shukrani Yako,

َ َ َ ْ‫َ َّ ْ َ َ َ ْ َ َ ا‬
‫النابة‬
ِ ‫والرغبة ِاليك و‬
Raghba ya kuelekea Kwako, kurejea Kwako,

َّ َ ُ َ َ ً َّ َ َ ُ َ َ ْ َّ َ َ َ ْ ْ َّ َ
‫والتو ِفيق مِلا وفقت له محمدا وآل محم ٍد‬
Na tawfiki katika yale uliyomwafikisha Muhammad
na Aali ­Muhammad,

ُ‫َع َل ْيه َو َع َل ْيه ُم السَّلاَ م‬


ِ ِ
Amani iwe juu yake na juu yao.

155

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 155 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

Orodha Ya Vitabu Vilivyo ­Chapishwa Na


Al-Itrah Foundation

1. i) Qur’ani Tukufu – Pamoja na Tarjuma ya Kiswahili


ii) Qur’an Al-Kariim - Tafsir Al-Kashif Juzuu ya kwanza mpaka Thelathini
2. Uharamisho wa Riba
3. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Kwanza
4. Uharamisho wa uwongo Juzuu ya Pili
5. Hekaya za Bahlul
6. Muhanga wa Imamu Husein (A.S.)
7. Mikingamo iliyomzunguka Imamu Ali (a.s.)
8. Hijab vazi Bora
9. Ukweli wa Shia Ithnaashari
10. Madhambi Makuu
11. Mbingu imenikirimu
12. Abdallah Ibn Saba
13. Khadijatul Kubra
14. Utumwa
15. Umakini katika Swala
16. Misingi ya Maarifa
17. Kanuni za Ndoa na maadili ya Familia
18. Bilal wa Afrika
19. Abudhar
20. Usahihi wa Historia ya Uislamu na Waislamu
21. Salman Farsi
22. Ammar Yasir
23. Qur’an na Hadithi
24. Elimu ya Nafsi
25. Yajue Madhehebu ya Shia

156

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 156 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

26. Ukusanyaji na Uhifadhi wa Qur’an Tukufu


27. Al-Wahda
28. Ponyo kutoka katika Qur’an
29. Uislamu mfumo kamili wa maisha ya kijamii
30. Mashukio ya Akhera
31. Al Amali
32. Dua kwa Mujibu wa Ahlulbayt (a.s)
33. Udhuu kwa Mtazamo wa Qur’ani na Sunna
34. Haki za wanawake katika Uislamu
35. Mwenyezi Mungu na sifa zake
36. Kumswalia Mtume (s)
37. Nafasi za Ahlul Bayt (a.s)
38. Adhana
39. Upendo katika Ukristo na Uislamu
40. Qur’ani na Kuhifadhiwa Kwake
41. Maana ya laana na kutukana katika Qur’ani Tukufu
42. Kupaka juu ya khofu
43. Kukusanya Sala Mbili
44. Bismillah ni sehemu ya Qur’ani na husomwa kwa Jahara
45. Kuwaongoza vijana wa kizazi kipya
46. Kusujudu juu ya udongo
47. Kusheherekea Maulidi Ya Mtume (s)
48. Tarawehe
49. Malumbano baina ya Sunni na Shia
50. Kupunguza Swala safarini
51. Kufungua safarini
52. Umaasumu wa Manabii
53. Qur’an Yatoa Changamoto
54. as-Salaatu Khayrun Mina -’n Nawm
55. Uadilifu wa Masahaba
56. Dua e Kumayl

157

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 157 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

57. Sauti Ya Uadilifu wa Binadamu


58. Umaasumu wa Mitume - Faida Zake Na Lengo Lake
59. Umaasumu wa Mitume - Majibu Ya Aya Zenye Utata
60. Umaasumu wa Mitume - Umaasumu wa Mtume Muhammad (s)
61. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Kwanza
62. Nahju’l-Balaghah - Juzuu ya Pili
63. Kuzuru Makaburi
64. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Kwanza
65. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Pili
66. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tatu
67. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Nne
68. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Tano
69. Maswali Na Mishkili Elfu - Sehemu ya Sita
70. Tujifunze Misingi Ya Dini
71. Sala ni Nguzo ya Dini
72. Mikesha Ya Peshawar
73. Malezi Ya Mtoto Katika Uislamu
74. Ubora wa Imam ‘Ali na Ushia ndio njia iliyonyooka
75. Hukumu za Kifikihi zinazowahusu Wanawake
76. Liqaa-u-llaah
77. Muhammad (s) Mtume wa Allah
78. Amani na Jihadi Katika Uislamu
79. Uislamu Ulienea Vipi?
80. Uadilifu, Amani na Mtume Muhammad (s)
81. Dhana ya Ndoa ya Mitala na Ndoa za Mtume Muhammad (s)
82. Urejeo (al-Raj’ah)
83. Mazingira
84. Utokezo (al - Badau)
85. Hukumu ya kujenga juu ya makaburi
86. Swala ya maiti na kumlilia maiti
87. Uislamu na Uwingi wa Dini

158

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 158 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

88. Mtoto mwema


89. Adabu za Sokoni Na Njiani
90. Johari za hekima kwa vijana
91. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Kwanza
92. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Pili
93. Maalimul Madrasatain Sehemu ya Tatu
94. Tawasali (AT- TAWASSUL)
95. Imam Mahdi katika Usunni na Ushia
96. Hukumu za Mgonjwa
97. Sadaka yenye kuendelea
98. Msahafu wa Imam Ali
99. Maimamu wa Ahlul Bait – Ujumbe na Jihadi
100. Idi Al-Ghadir
101. Kusoma sura zenye Sijda ya wajibu
102. Hukumu zinazomuhusu mkuu wa kazi na Mfanyakazi
103. Huduma ya Afya katika Uislamu
104. Sunna za Nabii Muhammad (saww)
105. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Kwanza)
106. Historia na sera ya viongozi wema (Sehemu ya Pili)
107. Shahiid Mfiadini
108. Mwanamke Na Sharia
109. Ujumbe -Sehemu ya Kwanza
110. Ujumbe - Sehemu ya Pili
111. Ujumbe - Sehemu ya Tatu
112. Ujumbe - Sehemu ya Nne
113. Mariamu, Yesu na Ukristo kwa mtazamo wa Kiislamu
114. Hadithi ya Thaqalain
115. Ndoa ya Mutaa
116. Ukweli uliopotea sehemu ya Kwanza
117. Ukweli uliopotea sehemu ya Pili
118. Ukweli uliopotea sehemu ya Tatu

159

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 159 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

119. Ukweli uliopotea sehemu ya Nne


120. Ukweli uliopotea sehemu ya Tano
121. Mkutano wa Maulamaa wa Baghdad
122. Safari ya kuifuata Nuru
123. Fatima al-Zahra
124. Myahudi wa Kimataifa
125. Kuanzia ndoa hadi kuwa Wazazi
126. Visa vya kweli sehemu ya Kwanza
127. Visa vya kweli sehemu ya Pili
128. Elimu ya Ghaibu ya Maimamu
129. Mwanadamu na Mustakabali wake
130. Imam Ali (‘a) Ndugu wa Mtume Muhammad (s) (Sehemu ya Kwanza)
131. Imam Ali (‘a) Ndugu wa Mtume Muhammad (s) (Sehemu ya Pili)
132. Khairul l’Bariyyah
133. Uislamu na mafunzo ya kimalezi
134. Vijana ni Hazina ya Uislamu
135. Adhana ni Ndoto au ni Wahyi?
136. Tabaruku
137. Saada Kamili – Kitabu cha Kiada cha Maadili
138. Vikao vya furaha
139. Shia asema haya Sunni asema haya Wewe wasemaje?
140. Visa vya wachamungu
141. Falsafa ya Dini
142. Kuhuzunika na Kuomboleza
143. Sunna katika Kitabu Fiqhi al-Sunnah
144. Mjadala wa Kiitikadi
145. Kuonekana kwa Allah
146. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Kwanza)
147. Tabia njema kwa Mujibu wa Ahlul-Bayt (Sehemu ya Pili)
148. Ndugu na Jirani
149. Ushia ndani ya Usunni

160

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 160 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

150. Maswali na Majibu


151. Mafunzo ya hukmu za ibada
152. Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 1
153. Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 2
154. Ahlul Bayt ndani ya tafsiri za Kisunni No 3
155. Abu Huraira
156. Vipengee kadhaa katika Swala ya Jamaa na Msikiti.
157. Mazingatio kutoka katika Qur’an - Sehemu ya Kwanza
158. Mazingatio kutoka kaitka Qur’an - Sehemu ya Pili
159. Mazingatio kutoka katika Uislamu - Sehemu ya kwanza
160. Mazingatio kutoka katika Uislamu - Sehemu ya Pili
161. Shia na Qur’ani – Majibu na Maelezo
162. Falsafa ya Mageuzi ya Imam Husein (a.s)
163. Amali za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
164. Elimu ya Tiba za Kiislamu - Matibabu ya Maimamu
165. Uislamu Safi
166. Majlisi za Imam Husein Majumbani
167. Je, Kufunga Mikono
168. Uislam wa Shia
169. Amali za Makka
170. Amali za Madina
171. Asili ya Madhehebu katika Uislamu
172. Sira ya Imam Ali kuhusu Waasi
173. Ukweli uliofichika katika neno la Allah
174. Uislamu na Mifumo ya Uchumi
175. Umoja wa Kiislamu na Furaha
176. Mas’ala ya Kifiqhi
177. Jifunze kusoma Qur’ani
178. as-Sahifatul Kamilah as-Sajjadiyyah
179. Hayya ‘Alaa Khayri’l-’Amal Katika Adhana
180. Ukweli kuhusu Funga ya Siku ya Ashura

161

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 161 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

181. Dua za Miezi Mitatu Mitukufu (Rajabu, Shaabani na Ramadhani)


182. Uadilifu katika Uislamu
183. Mahdi katika Sunna
184. Maswali Ya Uchunguzi Kuhusu Uislam
185. Kazi na Bidii ni njia ya maendeleo
186. Abu Talib – Jabali Imara la Imani
187. Ujenzi na Utakaso wa Nafsi
188. Vijana na Matarajio ya Baadaye
189. Historia maana na lengo la Usalafi
190. Ushia – Hoja na Majibu
191. Mateso ya Dhuria wa Mtume (saww)
192. Maombolezo – Msiba wa Bwana wa Mashahidi (a.s.)
193. Shahidi kwa Ajili ya Ubinadamu
194. Takwa
195. Upotoshaji Dhahiri katika (Turathi) Hazina ya Kiislamu
196. Amirul Muuminina (as) na Makhalifa
197. Tawheed Na Shirki
198. Kuvunja hoja iliyotumika kutetea Uimamu wa AbuBakr
199. Adabu za vikao na mazungumzo
200. Hija ya Kuaga
201. Uwazi baina ya Maslahi na Vikwazo
202. Fadhila za watukufu watano katika Sahih Sita
203. Mdahalo baina ya Mwanachuoni waKisunni na Kishia (Al- Muraja’aat)
204. Utawala na Uendeshaji katika Sera ya Imam Ali (as)
205. Imam Husain ni Mfumo wa Marekebisho na Mageuzi
206. Mtazamo kuhusu msuguano wa Kimadhehebu
207. Nchi na Uraia – Haki na wajibu kwa Taifa
208. Mtazamo wa Ibn Taymiyyah juu ya Imam Ali (as)
209. Uongozi wa Kidini – Maelekezo na Utekelezaji wa Kijamii
210. Maadili ya Ashura
211. Mshumaa – Shahidi na Kifo cha Kishahidi

162

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 162 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

212. Mizani ya Hekima – Hadithi za Ahlul Bait (as) – Sehemu ya Kwanza


213. Imam Ali na Mambo ya Umma
214. Imam Ali na Mfumo wa Usawa
215. Uimamu na Tamko la Kutawazwa
216. Mfumo wa Wilaya
217. Vipi Tutaishinda Hofu?
218. Kumswalia Mtume ni Ufunguo wa Utatuzi wa Matatizo
219. Maeneo ya Umma na Mali Zake
220. Nahju ‘L-Balagha– Majmua ya Khutba, Amri, Barua, Risala,
Mawaidha na Semi za Amirul-Muuminin Ali bin Abu Talib (a.s.)
221. Mukhtar – Shujaa aliyelipiza kisasi dhidi ya wauaji
wa Imam Husein (as) hapo Karbala
222. Mazingatio Katika Swala
223. Imam Hasan na Mfumo wa Kujenga Jamii
224. Vyakula Na Vinywaji
225. Kuelewa Rehema ya Mwenyezi Mungu
226. Imam Mahdi na Bishara ya Matumaini
227. Mtazamo Mpya - Wanawake katika Uislamu
228. Shia Na Sahaba - Majibu na Maelezo
229. Majanga Na Jukumu la Jamii
230. Shia Na Hadith - Majibu na Maelezo
231. Upotofu Ndani ya Kitabu cha Mitaala kwa Shule za Sekondari
232. Ugaidi Wa Kifikra Katika Medani Ya Kidini
233. Yafaayo kijamii
234. Uswalihina Dhahiri Na Batini Yake
235. Mkakati wa Kupambana na Ufakiri
236. Mwanamke Katika Harakati Za Mageuzi
237. Jihadi
238. Hija Katika Maneno Na Ujumbe Wa Imam Khomeini (R.A)
239. Tiba Ya Maradhi Ya Kimaadili
240. Yusuf Mkweli

163

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 163 6/16/2016 4:29:26 PM


Dua za Mwezi wa Ramadhan

241. Taqiyya Kwa Mujibu Wa Sheria Ya KIISLAMU


242. Imam Mahdi (A.S) Imam Wa Zama Hizi Na Kiongozi Wa Dunia
243. Talaka Tatu
244. Safari Ya Kuelekea Kwa Mwenyezi Mungu
245. Hotuba Za Kiislamu Juu Ya Haki Za Binadamu
246. Mashairi Ya Kijamii
247. Ngano Ya Kwamba Qur’ani Imebadilishwa
248. Wito Kwa Waumini: “Enyi Mlioamini”
249. Imam Husain (a.s) ni Utu na Kadhia
250. Imam Husain ni Kielelezo cha Kujitoa Muhanga na Fidia
251. Imam Mahdi ni Tumaini la Mataifa
252. Kuchagua Mchumba
253. Mazungumzo ya Umoja – Ukosoaji na Usahihishaji
254. Utamaduni wa Mwamko wa Kijamii
255. Hekima za kina za Swala
256. Kanuni za Sharia za Kiislamu
257. Utamaduni kufuatana na Qur’ani na Utekelezaji wa Kivitendo
(Sehemu ya Kwanza)
258. Kauli sahihi zaidi katika kufafanua Hadithi

164

17_16_Ramadan Dua_16_June_2016.indd 164 6/16/2016 4:29:26 PM

You might also like