Professional Documents
Culture Documents
Nani Kabadili Sabato Kwenda Jumapili
Nani Kabadili Sabato Kwenda Jumapili
- MUNGU MWENYEWE
Je, nani kabadili siku ya ibada kutoka Sabato kwenda Dominika (Jumapili)?
Jibu fupi
Biblia ipo wazi kabisa kuhusu mabadiliko ya Sabato kwenda Dominika (Jumapili).
Mosi, mabadiliko hayo yalitabiriwa na Hosea (rej. Hos 2:11). Yeye alitabiri
akisema, “Tena nitaikomesha furaha yake yote na sikukuu zake, na siku zake za
mwandamo wa mwezi na sabato zake na makusanyiko yake yote yaliyoamriwa.”
Pili mabadiliko hayo yalifafanuliwa kwa maneno na matendo ya Yesu Kristo (rej.
vifungu mbalimbali vya Injili, hususan, Mt 12:1-12, Mk 3:2-4, Lk 13:14-16, 14:1-
5, Yn 9:16).
Tatu, mabadiliko yametangazwa katika Ebr 4:4-10. Hapa tunasoma hivi, “Basi,
ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuiogope, mmoja wenu asije
akaonekana ameikosa. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile
vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu
halikuchanyikana na imani ndani yao waliosikia. Maana sisi tulioamini tunaingia
katika raha ile: Kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu,
1
Hawataingia rahani mwangu: ijapokuwa zile kazi zilimalizika tangu kuwekwa
misingi ya ulimwengu. Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi,
Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote; na hapa napo,
Hawataingia rahani mwangu.
Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na
wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi
kwao, AWEKA TENA SIKU FULANI, akisema katika Daudi baada ya muda
mwingi namna hii, Leo kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo, kama mtaisikia sauti
yake, Msifanye migumu mioyo yenu. Maana kama Yoshua angaliwapa raha,
asingalinena siku nyingine baadaye. Basi, imesalia raha ya Sabato kwa watu wa
Mungu. Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe
katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi yake. Basi, na tufanye
bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu yeyote asije akaanguka kwa mfano
huo huo wa kuasi.”
Nne, Sabato imebainishwa kuwa ilikuwa kivuli tu Kol 2:16. Hapa tunasoma hivi,
“Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya
sikukuu au mwandamo wa mwezi, au Sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo
yajayo; bali mwili ni wa Kristo”. Na hatimaye siku zote zimetangazwa katika Rum
14: 4-10 kuwa sawa mbele ya Mungu mwenyewe. Hapo tunasoma ifuatavyo:
“Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake
mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana
aweza kumsimamisha. Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku; mwingine
aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.
Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana,
kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia
amshukuru Mungu. Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi
yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake. Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa
Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu
mali ya Bwana. Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki
waliokufa na walio hai pia. Lakini wewe, je! mbona wamhukumu ndugu yako? Au
wewe je! mbona wamdharau ndugu yako? Kwa maana sisi sote tutasimama mbele
ya kiti cha hukumu cha Mungu.”
2
Hicho ndicho kitabu cha Ufunuo, kitabu ambacho kinatangaza vifo vya vitu vingi.
Mambo yalipinduliwa hivyo na Mungu mwenyewe. Hebu nikuorodheshea kidogo
mambo yanayosimuliwa na kitabu cha Ufunuo kwamba yalikufa kwa kusudi ya
kuyapisha mambo mapya muhimu. Kinasimulia kwamba hekalu la Yerusalemu
lilikufa kulipisha hekalu la kweli yaani makazi ya Mungu mwenyewe mbinguni.
Ukuhani wa Kiyahudi ulikufa kuupisha ukuhani mkamilifu na wa milele wa Yesu
Kristo pamoja na watu wote wanaobatizwa katika jina lake. Sadaka za Kiyahudi
zilikufa kuipisha sadaka timilifu ya Yesu Kristo msalabani. Kumbe ni katika
tangazo hili la kifo, kitabu cha Ufunuo kinapotangaza kwamba Sabato iliuawa
kuipisha Siku ya Bwana, yaani Jumapili.
Hata hivyo, haikuwa wote walioelewa suala hilo, wengine wakawa bado
wanaililia Sabato hiyo. Kufuatia kituko hicho, mwandishi wa Barua kwa
Waebrania akawaandikia wazi wazi wazi habari hiyo (Ebr 4:1-10) naye Paulo
akakizima kilio cha wasiokubali mabadiliko katika Rum 14:4-10 na
kuwatawanyisha wapigakelele waliokuwa wakiwahangaisha wenzao juu ya Sabato
na sikukuu zingine za kiyahudi kwa maneno murua yaliyomo katika Kol 2:16-17.
Mabadiliko Yalitabiriwa
Sasa hebu tujipatie muda wa kuliweka jibu hili kirefu. Tufuatane kwa utulivu sasa.
Awali ya yote, Biblia inaonesha kwamba Mungu alishamfanya Hosea ayatabiri
mabadiliko hayo. Hosea 2:11 inasomeka wazi wazi kabisa: “Nitazikomesha starehe
zake zote, sikukuu zake za mwezi mwandamo na za Sabato na sikukuu zote
zilizoamriwa”. Neno Sabato katika Kiebrania “shabat” linamaanisha “kupumzika”.
Kwa wayahudi siku hiyo ilikuwa siku ya Bwana wa huruma na walipaswa kuiweka
wakfu kwake (rej. Law 23:3). Siku hiyo walimheshimu Mungu (rej. Mt 12:5, Yn
3
7:23) kwa kumtolea sadaka, kusali na kupumzika kazi kabisa (rej. Isa 56:2, 58:13-
14).
Kama kivuli cha mapumziko halisi yatakayopatikana mbinguni kwa njia ya kifo na
ufufuko wa Yesu Krsto, Mungu aliwawekea wayahudi Sabato kusudi wajipatie
picha ya mambo halisi yajayo mbele yao. Ndipo alipowapa sababu za kujifunza
kupumzika kama mazoezi ya maonjo ya mapumziko halisi. Sababu alizowapa
zilikuwa tatu: kwanza kwamba wamwige Yeye mwenyewe aliyepumzika baada ya
kukamilisha kazi ya kuumba ulimwengu pamoja na vitu na watu waliomo ndani
yake (rej. Kut 20:8-11), pili kwamba Sabato ni ishara ya Mungu kwa wayahudi
kwamba ndiye aliyewatakasa na kuwafanya taifa lake teule (rej. Kut 31:13-18, Eze
20:20) na tatu waishike kama kumbukumbu ya kukombolewa kwao kutoka Misri
(rej. Kum 5:11-15).
Kwa mtindo huu wa mambo, ikadhihirika wazi kwamba mtu alikuwa anawajibika
kwa Sabato kana kwamba aliumbwa kwa ajili hiyo, wakati Sabato iliwekwa kwa
ajili ya binadamu apate kustarehe na hivyo kujionjesha Sabato ya kweli
itakayokuja mwishoni mwa historia. Kifupi, kiutendaji, mtu aligeuzwa mtumwa
kwa Sabato, starehe ikakosekana kukabaki mashaka na wasiwasi mwingi sana.
Wayahudi waliiogopa sana Sabato, si hasa kwa sababu ya kumpenda na kumtii
Mungu isipokuwa kwa sababu ya adhabu zake, hasa kuangamizwa kwa
Yerusalemu na kupelekwa utumwani (rej. Yer 17:19-27, Eze 20:20-24).
4
Mabadiliko ya Sabato kwenda Dominika (Jumapili) yalifafanuliwa kirefu kwa
maneno na matendo ya Yesu Kristo (rej. sehemu mbalimbali za Injili). Mungu
alipowaona wayahudi wakihangaika na Sabato akazidi kuchanua katika nia yake
ya kuifuta. Ndipo, Bwana wetu Yesu Kristo, alipokuja akawaelimisha watu
kwamba binadamu hakuumbwa mtumwa wa Sabato hata kidogo. Badala yake,
Yesu Kristo, aliwaelimisha wote, kwa maneno na matendo yake kwamba Yeye
alikuwa ni Bwana wa Sabato na hivyo, kwa mamlaka hayo na kwa utume wake
aliopewa na Baba, anawaalika watu kutenda mema badala ya kujiumiza kwa wasi
wasi wa kuivunja Sabato na hivyo labda kuadhibiwa na Mungu (rej. Mk 2:27f).
Yesu alijitangaza kuwa Mungu mwenye mamlaka ya kuibadili hiyo Sabato kwa
sababu aliiweka yeye mwenyewe. Na hiyo ni kawaida na mantiki, aliyeitunga
sheria ndiye anayeweza kuitangua. Yesu aliwaambia Wayahudi, “Sabato ilifanyika
kwa ajili ya mwanadamu, si mwandamu kwa ajili ya Sabato, Basi Mwana wa
Adamu ndiye Bwana wa Sabato pia” (Mk 2:27f). Japokuwa Yesu alitangaza jambo
hili, Wayahudi hawakumwelewa hata kidogo na kwa namna hiyo walimlalamkia
yeye na wafuasi wake ambao kutokana na kumwelewa mwalimu wao walishaanza
kuonesha dalili za kutoitilia maanani Sabato kwa mtindo wa kiyahudi (rej. Mt
12:1-12, 3:2-4, Lk 13:14-16, 14:1-5, Yn 9:16).
5
Juhudi hizi za Yesu hazikuzaa matunda mara moja. Kumbe, elimu aliyotoa Yesu
Kristo kuhusu Sabato, kwa maneno na matendo tunayoyaorodhesha hapa,
haikuingia kabisa vichwani mwa wayahudi na hata wafuasi wake walisitasita
kuipokea. Kwa kisa hicho, baada ya Yesu kupaa mbinguni, wayahudi waliendelea
kuishika Sabato na kukusanyika kwa ibada katika siku hiyo. Basi Mtume Paulo
alipotaka kuwakuta Wayahudi wamekusanyika kwa wingi pamoja aliwatafuta
katika siku ya Sabato (rej. Mdo 13:14, 42, 44, 16:13, 17:2, 18:4), kwa Wakristo
alijua ilikuwa siku ya Dominika (rej. Mdo 20:7). Hata hivyo, kiujumla, kwa
sababu ya uzito na woga wa kubandukana na siku waliyoizoea kusudi kuifuata siku
mpya, wafuasi wa Yesu walikuwa njia panda na hivyo wakawa wanahudhuria
Sabato pamoja na wayahudi wote na SIKU YA BWANA ilipofika wakawa
wanajikusanya peke yao ili kusali, kusoma maandishi yao (ndiyo yaliyogeuka
baadaye Agano Jipya) na kuumega mkate (rej. Mdo 20:7).
Ombi la kumi na mbili halikuwa ombi, bali sala ya kulaani waasi wa dini na hivyo
wakiwamo ndani yake Wakristo. Ombi hilo lilisema: “Kusiwe na tumaini kwa
waasi wa dini na uung’oe kwa haraka utawala wenye kiburi (dola ya kirumi)
katika siku zetu. Wanazareni (wayahudi Wakristo) na ‘minim’ (wayahudi wazushi)
wafe mara moja; wafutwe kwenye kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na
wenye haki”. Mwisho mwa ombi hili, kama ilivyotakiwa kwa kila ombi, watu
waliokusanyika kwa ibada iliwapasa kuitikia, “Utukuzwe wewe, Bwana
unayenyenyekesha kiburi”.
Kwa kweli, kwa ombi hili au laana hii, Roho Mtakatifu, mfariji na mkumbushaji
wa mafundisho ya Yesu, aliwakumbusha wafuasi wa Yesu kwamba Bwana wao
6
alishawawekea siku mpya, yaani ile SIKU YAKE, ndiyo siku ya kwanza ya juma.
Siku hiyo ilikuwa njema na bora kwa kila hali kwani ilikuwa ni siku ya ufufuko wa
Bwana mwenyewe, siku ya kuimarishwa kwao na Roho Mtakatifu na kuzaliwa
Kanisa la Kristo (Pentekoste), siku aliyoitumia Yesu kuwatokea wafuasi wake
baada ya ufufuko wake na hata, kihistoria, siku Mungu alipoanza kuumba
ulimwengu. Na mathali, Pasaka au ufufuko wa Bwana ni uumbaji mpya wa
ulimwengu, siku ya kwanza ya juma ilikuwa kama siku mambo yalipoumbwa
upya. Kwa sifa hizo zote, Wakristo wa mwanzo waligundua haja na uhalali wa
kuhamia siku mpya na kuiadhimishwa kwa Bwana.
Basi Wakristo, mara wakaacha kabisa kuhudhuria ibada za Sabato, wakawa tangu
wakati huo wanakusanyika Dominika tu. Hivyo akitafutwa mtu aliyeanza kuiacha
Sabato turudi hadi kwa mitume katika karne ile ile ya kwanza. Kwa nini walifanya
hivyo? Walifanya hivyo kwa sababu walimwelewa vizuri Kristo kwamba busara
inadai usishonee kiraka kipya kwenye nguo ya zamani na wala usitie divai mpya
kwenye viriba vya zamani. Hayo aliyasema Yesu alipokuwa akiwaeleza Wayahudi
kwamba mafundisho yake mapya hayaoani na desturi zao za kale. Alisema,
“Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; maana kile
kilichotiwa huondoa kipande cha lile vazi, na pale palipotatuka huzidi. Wala watu
hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; na kama wakitia, vile viriba hupasuka,
divai ikamwagika na viriba vikaharibika; bali hutia divai mpya katika viriba vipya,
vikahifadhika vyote” (rej. Mt 9:16-17).
7
kiyahudi anaendelea kusema, “Ni upumbavu kuwa na Yesu midomoni na wakati
huo huo kufuata mila za kiyahudi” (rej. namba 10-15).
8
Basi kwa ukweli huu, siku ye yote inaweza kuadhimishwa kwani anaadhimishwa
kwa Bwana na wala si kwa siku kama siku (rej. Rum 14: 4-10). Biblia, ni kitabu
kilichoandikwa kwa uvuvio na si utunzi wa akili za waandishi tu. Hilo
linadhihirika pia kwenye suala hili hili la Sabato. Kumbe Mtume Paulo
alisemeshwa kinabii na Roho Mtakatifu atufunulie jambo lingelilojulikana vyema
baadaye kwa kukua kwa elimu ya jiografia na kosmolojia. Mtume Paulo katika
Rum 14:4-10 alisemeshwa atuambie tuache mabishano juu ya Sabato, kwa sababu,
mbele ya Bwana, siku zote ni sawa. Jambo hilo kumbe ni kweli kama mtu
atajielimisha katika jiografia.
Kama hujanielewa hebu nikulete, mara moja, kwenye kitendawili cha kitoto. Ikiwa
watu, huku magharibi, watang’ang’ania kwenda kusali Jumamosi, watakuwa
wamekwenda kusali siku gani kwani masaa yale yale kwa upande wa magharibi ni
bado Ijumaa? Au siku moja baadaye, wengine watakapokwenda kusali
waking’ang’ania kuwa Jumapili, wanakuwa wanakwenda kusali siku gani wakati
huko magharibi ndiyo Jumamosi? Kumbe siku ni mbili kwa binadamu
tunaotegemea kuzipima siku zetu kwa jua. Mbele ya Mungu, asiye na siku, siku
yake ni moja ile ile. Kwa hali hiyo, ukweli unakuwa mmoja kwamba, mbele ya
9
Mungu, siku zote ni sawa na hivyo ye yote anayekusudia kuadhimisha siku,
aiadhimishe kwa Bwana tu asijisumbue na jina la siku (rej. tena Rum 14:4-10).
Kwa vile Wakristo waligundua kwamba Jumapili, ndiyo iliyokuwa siku yao,
walijizoeza kukutana Jumapili kusali, kumsifu Mungu, kutoa sadaka na michango
kwa ajili ya wenye dhiki. Kwamba mambo yalikwenda hivyo tunasoma katika
Biblia hususan katika 1 Kor 16:1-2. Hapa tunasoma, “Kwa habari ya ile michango
kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi
fanyeni vivyo. Siku ya kwanza ya juma (ndiyo siku ya Bwana, Jumapili) kila mtu
kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikwa kwake; ili kwamba
michango isifanyike hapo nitakapokuja.”
Baada ya Biblia kuweka sawa habari za Sabato namna hiyo, na Wakristo kujasiri
kuishika siku ya Bwana badala ya siku muflisi, Sabato, katika miaka ya karne ya
nne, alitokea katika historia Kaisari aliyeupenda ukristo. Yeye alikuwa ni matokeo
ya sala za Wakristo kuwaombea viongozi wa dunia wausaidie ukristo ukue
duniani. Kaisari huyo aliitwa Konstantino, aliyetawala tangu 306-337 B.K.,
aliupatia ukristo amani kutoka kwenye madhulumu ambayo makaisari wengi
walikuwa wakilifanyia Kanisa. Yeye akatangaza rasmi kwamba ile siku
inayoshikwa na Wakristo kwa masuala ya sala kwa Mungu wao iwe siku rasmi ya
mapumziko kwa watu wote katika dola yake, yaani dola ya kirumi. Ndipo
mapumziko ya Dominika yakawa rasmi tangu wakati ule. Hii maana yake ni
kwamba Konstantino siye aliyeiunda Dominika na wala siye aliyeanzisha mambo
ya ibada yawe katika siku hiyo. Yeye anakuja kuipatia Jumapili nguvu ya kidola
tu.
10
iliyotolewa hapo juu, yaani mintarafu nyakati za Yesu na baadaye wanafunzi wake,
ndiyo inayotuonesha kwamba Dominika ilianza kuwa siku ya ibada kwa Wakristo
zamani za karne ya kwanza tayari na wala siyo katika karne ya nne. Basi,
kichekesho cha kumtaja Konstantino au Papa fulani kama mwanzilishi wa
Dominika kinaweza kulingana na kichekesho cha mtu atakayemtaja kiongozi
fulani wa leo kama mwanzilishi wa taratibu ya kula au kuvaa kwa binadamu.
Itakuwa ni kichekesho cha mwaka kwa sababu watu wamekuwa wakila na kuvaa
hata kabla kiongozi huo hajaliona jua la ulimwengu huu. Ndivyo ilivyo kwa
Konstantino, hawezi kuanzisha kitu katika karne, kitu kilichoanza kabla hajazaliwa
mwenyewe katika karne ya kwanza.
11
nini? Jibu kwa swali lako hilo ni rahisi kabisa. Ni kwamba hakuna mizani wala
darubini nyingine tofauti na Maandiko Matakatifu hayo hayo.
Zaidi ya hapo, ukipima tena maono hayo kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu,
uongo wenyewe umejipandikiza katika kupingana na kauli ya Mwana wa Mungu,
mwalimu wa kwanza na wa kweli kupita wanadamu wote wenye nyama na mwili.
Yesu alipoulizwa amri ipi ni kuu kuliko zingine, alijibu mara moja kwamba ni ile
ya kumpenda Mungu na jirani aliye sawa nasi (rej. Mt 22:34-40, Mk 12:28-34, Lk
10:25-28). Hata Yesu Kristo ametuachia upendo kama amri na alama
itakayotutambulisha Wakristo po pote duniani wala siyo Sabato (rej. Yn 13:31-35).
Sasa wakati Yesu Kristo anasema hayo yote iweje Nabii Bibi Hellen White awe na
jibu la Sabato? Tazama, mbona anachosema Bi Hellen ni tofauti na kile alichosema
Kristo hata kabla ya yeye hajazaliwa?
Kama huo si upinga Kristo, ni nini tena? Hapo ndipo anapoingia Bi Hellen na siku
hizi msimamo wake kuendelezwa na wafuasi wake. Na Maandiko yanasema mtu
12
akianza tu na hatua ya kupingana na Kristo anakuwa sababu ya mabishano,
magomvi na fujo zingine hatari na mwishowe kuishia katika shughuli za biashara
ndani ya dini. Ndugu yangu, jambo hili ni la kweli asilimia mia moja na ni bayana
kwa kila anayeweza kumtathimini vizuri Bi Hellen na sasa wafuasi wake
wanaomfuata baada ya kuasiana na Kanisa Katoliki.
Hapa mimi natoa uhuru kwa kila msomaji wa kijitabu hiki. Ni kwamba hapa kila
Mkristo aamue mwenyewe kumfuata Yesu Kristo Bwana wake au kusikiliza vioja
vya Bibi Hellen White na pia kujiunga na Wasabato wanaojaribu kututiriza
Wakristo wenzao kana kwamba tumewakosea. Mimi na roho yangu naisikiliza
Biblia na kumfuata Yesu Kristo, Bwana wangu. Mimi siwezi kumfuasa
mwanadamu ambaye kwa vipimo dhahiri vya Maandiko Matakatifu anapingana na
Kristo Bwana wangu. Siwezi kumfuata mpinga Kristo, labda niwe nimelewa au
nimechanganyikiwa! Wewe, ndugu yangu, amua mwenyewe leo baada ya maelezo
haya.
13
hayakuletwa na Wakatoliki wala na viongozi wao, wala si na Papa fulani wala
mfalme Kostantino. Hilo tumeoneshwa wazi wazi katika Maandiko Matakatifu
ambayo yanatuwekea wazi ukweli kwamba Bwana Mungu wetu ametuwekea siku
nyingine badala ya Sabato ya kale. Tuasindikie mate wino ungalipo. Ushuhuda wa
kwamba Sabato ilifutwa na kuwekwa siku nyingine uko wazi kabisa kwani katika
Maandiko Matakatifu tunasoma hivi:
“Basi, ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuiogope, mmoja wenu
asije akaonekana ameikosa. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema
vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu
halikuchanyikana na imani ndani yao waliosikia. Maana sisi tulioamini tunaingia
katika raha ile: Kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu,
Hawataingia rahani mwangu: ijapokuwa zile kazi zilimalizika tangu kuwekwa
misingi ya ulimwengu. Kwa maana ameinena siku ya saba mahali fulani hivi,
Mungu alistarehe siku ya saba, akaziacha kazi zake zote; na hapa napo,
Hawataingia rahani mwangu.
Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na
wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi
kwao, AWEKA TENA SIKU FULANI, akisema katika Daudi baada ya muda
mwingi namna hii, Leo kama ilivyonenwa tangu zamani, Leo, kama mtaisikia sauti
yake, Msifanye migumu mioyo yenu. Maana kama Yoshua angaliwapa raha,
asingalinena siku nyingine baadaye. Basi, imesalia raha ya Sabato kwa watu wa
Mungu. Kwa maana yeye aliyeingia katika raha yake amestarehe mwenyewe
katika kazi yake, kama vile Mungu alivyostarehe katika kazi yake. Basi, na tufanye
bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu yeyote asije akaanguka kwa mfano
huo huo wa kuasi “(Ebr 4:1-10).
14
Kurudia Sabato ni Kuukarabati Mkeka Uliotupwa
Kwa kuwa ukweli ndio huo nilikueleza hadi sasa, si busara kuukarabati wala
kuuokota mkeka wa zamani kama mwenye nyumba ameamua kuleta mkeka mpya.
Mungu alishaitupilia mbali Sabato iweje tuirudie tena? “Tumerogwa”?
Hayo yote yalikuwa maamrisho ya mfano wa ukombozi wetu halisi. Si hilo tu, bali
maelezo na taarifa hii kwamba Sabato ya kiyahudi imesitishwa imetoka kinywani
mwa Mwana wake wa pekee, ndiye Yesu Kristo ambaye wote tumeamriwa
tumsikilize kwani ndiye ufunuo wa kweli wa Mungu (rej. Ebr 1:1-4). Narudia
kusema, yale yote yalikuwa ni mfano tu. Mahali pa Musa palikuwa pa Yesu
mwenyewe na mahali pa kivuli cha Sabato palikuwa pa Siku ya Bwana ndiyo
Dominikla au Jumapili. Lakini husikika pia hoja ya kuchekesha kwamba eti
ukishika Jumapili ambayo inaitwa “Sun-day” unamwabudu mungu jua ambaye
alikuwa akiabudiwa siku hiyo.
Ndugu zanguni hii ni hoja kweli? Mbona hii ni hewa tu? Ikiwa ni hivyo nani
anasalimika na uabudu miungu? Mbona kila siku kulikuwa na mungu fulani
anayeabudiwa? Tuache utoto. Hiyo ingekuwa na maana Waislamu wanaoabudu
siku ya Ijumaa, wanamwabudu mungu aliyekuwa anaabudiwa Ijumaa. Na hapo
hapo ingemaanisha kuishika Sabato ambayo inaitwa Saturday kwa Kiingereza
maana yake ni hiyo hiyo yaani kumwambuidu “mungu satur” ambaye alikuwa
akiabudiwa siku hiyo, yaani Sabato ya Wayahudi. Basi, tuache hoja isiyo na
mashiko kama hii. Majina ni mbali na ibada kwa mungu fulani ni mbali. Ibada
haikai kwenye jina la siku au mwezi isipokuwa katika nia kamili ya mtu, imani na
matendo halisi ya kumsujudia huyo anathaminiwa kama mungu.
15
Ubora na Utukufu wa Siku Mpya, Jumapili
Tukirudia mada yetu, ni kwamba wala haina utata siku iliyowekwa pahala pa
Sabato, ni siku ya ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambapo hata uzima wetu
unafufuliwa na ni siku hiyo pia Roho Mtakatifu alipowashukia mitume na
kuanzisha Kanisa takatifu na kazi ya uinjilishaji duniani (ndiyo siku ya Pentekoste)
kama tunavyosoma bila shida katika Mdo 2:1-13. Kwa sababu hiyo, Dominika ni
siku tukufu kuliko siku zingine zote kwa vile ndiyo utimilifu wa lengo la Sabato na
kupita Sabato. Basi, kwa mujibu wa amri ya kwanza na ya tatu ya Mungu, Kanisa
huadhimisha SIKU YA BWANA. Ndipo binadamu tumeamriwa kufanya kazi kwa
siku sita, yaani kutenda mambo yetu yote, lakini tuiweke siku ya Sabato ya Bwana
(Dominika) kama siku takatifu kwa Bwana na kustarehe kabisa.
Nani amegeuka mkondo wa mambo hata kugeukia tena Sabato wakati Wakristo wa
kwanza kwa kumwelewa vyema Yesu Kristo walishaitupilia mbali? Jibu ni wazi.
Ni mmoja wa waanzilishi wa dhehebu la Wasabato, yule mama anayejulikana
kama nabii. Kwa taarifa yako waanzilishi wa dhehebu la Wasabato ni akina Hiram
Edson, Joseph Bates, E.G. Harmon na Hellen White. Katika hawa aliyekuja na
moto wa kurudisha Sabato ni huyo mama ambaye alikuwa mke wa E.G. Harmon.
Mwanamke huyo anaheshimiwa na Wasabato kama nabii na vitabu vyake, kama
vile Vita Kuu, Afya na Raha na Ushindaji, vinasomwa na Wasabato karibu kama
misahafu.
16
wa kweli hata tutishike nao? Hapana, wala si wa kweli. Unabii wa mama huyu
lazima tuukatae. Kwa nini tuukatae?
Ni kwa sababu kuna sababu tatu zinazotuhalalisha tumkatae kama nabii. Mosi,
kitabu cha Ufunuo kinaonesha kufungwa kwa unabii, yaani kwamba baada ya
mambo yaliyoandikwa humo kusingekuwa na ufunuo wowote wa pekee.
Ukamilifu wa ufunuo ulitokea katika ujio wa Yesu Kristo. Alichosema yeye
ndicho kitu cha kilele. Sasa Bi Hellen anakujaje na mapya kumpikua Yesu Kristo?
Tunasoma, “Mungu ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa
sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi, amesema na sisi katika
Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.
Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wa wake na chapa ya nafsi yake,
akavichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi,
aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu, amefanyika bora kupita malaika kwa
kadiri jina alilorithi liliyo tukufu kuliko lao” (Ebr 4:1-4).
Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale
wazee, Mwanakondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye
pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika
dunia yote. Akaja , akakitwaa kile kitabu katika mkono wa kuume wake yeye
aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi. Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai
wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya Mwanakondoo, kila
17
mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni
maombi ya wakatakatifu, nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe
kukitwaaa hicho kitabu na kizifungua muhuri zake, kwa kuwa ulichinjwa,
ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na
taifa, ukawafanya kuwa ufalme wa makuhani, kwa Mungu wetu, nao wanamiliki
juu ya nchi” (Ufu 5:1-10).
Pili, tuukatae unabii wake kwa vile zile anazoziita njozi, kama elfu mbili hivi, ni
batili kwani zinaonesha jinsi alivyojaa chuki kwa Baba Mtakatifu na Kanisa
Katoliki nasi tunajua kwamba si kazi ya Mungu Roho Mtakatifu kumjaza mtu
chuki kali hivyo dhidi ya mwanadamu mwingine. Kazi hiyo hufanywa na Shetani
nayo huonesha kwamba moyo wa mtu umejaa uovu kwani kilichomjaa mtu
moyoni ndicho kimtokacho. Tunasoma, “Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao
matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; kwa kuwa kila mti
hutambulikana kwa matunda yake; maana katika miiba hawachumi tini, wala
katika michongoma hawachui zabibu. Mtu mwema katika hazina njema ya moyo
wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa
yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake”
(rej. Lk 6:43-45). Hakika chuki dhidi ya Baba Mtakatifu na Kanisa Katoliki
inatoka katika moyo uliofurika uovu. Na kwa jinsi hii maono yake hayawezi
kutoka kwa Roho Mtakatifu.
Tatu, tuukatae unabii wake kwa sababu mafundisho yake yanaonesha kwamba
haijui Biblia. Hoja hii ya tatu nimeshaishuhudia tayari. Nimesema ameota ndoto
akaona huko mbinguni kuna hekalu wakati Maandiko yanatakaa jambo kama hilo
(rej. tena Ufu 22:22-24). Kisha nimeshashuhudia kwamba kule kusisitiza kwamba
18
Sabato ndiyo amri kuu kunapinga na kile alichotuambia Bwana wetu Yesu Kristo
aliyesisitiza kwamba amri kuu ni upendo (rej. tena Mt 22: 34-40). Naomba itoshe
nilivyokuambia nawe uyapuuze maono ya Mrs. Harmon tunayemchambua hapa.
Naomba hadi hapa shtaka la kwamba Kanisa Katoliki limebadili majira, yaani
kutoka Sabato kwenda Dominika (Jumapili), lififie kabisa. Si unajua kwamba hoja
yenyewe hukokotolewa kutoka Dan 7:25 mahali palipoandikwa, “Naye atanena
maneno kinyume chake Aliye Juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye
Juu, naye ataazimu kubadili majira na sheria”.
Kama unavyoisoma sasa, hoja hii haitaji Kanisa Katoliki bali kwa kinyume chake
inawataja Wasabato wenyewe. Ndugu zangu Wasabato hawalifahamu jambo hili
kwa sababu ndivyo ilivyo, “Jambo usilolifahamu ni sawa na usiku wa giza.” Kwa
19
vipi? Ni hivi, kama Yesu kwa maneno na matendo yake alisema Sabato si lolote na
wala si chochote “maana mtu hakuuumbwa kwa ajili ya Sabato”, mtu anayesema
Sabato ndiyo yote katika yote ndiye anayeazimu kubadili majira na sheria. Na
moja kwa moja mtu huyo anakuwa ndiye mpinga Kristo kwa sababu anapingana
na kauli ya Kristo mwenyewe. Hilo ndilo alilofanya Nabii Hellen na
kuwasadikisha maelfu ya watu kauli yake kengeufu.
Aidha, kama Yesu alisema kwamba amri kuu ni upendo (rej. Mt 22:37) na akataka
iwatambulishe wafuasi wake popote watakapokuwapo (rej. Yn 13:35), anapokuja
Nabii Hellen na kusema eti amri kuu ni Sabato ni upinga Kristo wa wazi wazi na
kumfuasa mpinga Kristo kama huyo ni kuwa wapinga Kristo wadogo wadogo
nyuma ya huyo mkubwa. Ona ushuhuda wa Maandiko Matakatifu. Bila shaka, hata
wewe unakumbuka Yesu aliulizwa swali juu ya amri ya kwanza na kuu naye
akatoa jibu mwafaka hata wasomi na walimu wa enzi zake wakamvulia kofia.
Kwa sasa hitimisha fikra zako kwa nukuu hii: “Basi, mtu asiwahukumu ninyi
katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi ,
au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. Mtu
asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe
20
na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake
za kimwili; wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na
kuungamanishwa na viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa
Mungu” (Kol 2:16-19).
21