Professional Documents
Culture Documents
Nadharia Katika Uchambuzi Wa Kazi Za Fas
Nadharia Katika Uchambuzi Wa Kazi Za Fas
Utangulizi
Kazi za fasihi huchunguzwa kwa kina ili kupata uhakika wa maudhui na kufafanua vipengele
muhimu kama lugha ilivyotumika. Nadharia nyingi zimewekwa ili kuhakiki kazi hizi za fasihi.
Kwanza, dhana hii ya nadharia imetolewa maelezo na wasomi mbalimbali; kama vile
(J. S Mdee na wenzake, 2011) wanaeleza kwamba nadharia ni mpango wa mawazo uliotungwa
ili kuelekeza jinsi ya kufanya au kutekeleza jambo fulani. Kwa msingi huo nadharia hubeba
mawazo, dhana au maelezo yatolewayo kwa nia au kwa lengo la kueleza hali fulani, chanzo,
muundo, utendaji na mwingiliano wa ndani na nje. Sengo naye (2009) anafasili nadharia kuwa
ni wazo kuu, fikra kuu, mwongozo mkuu wa mtu, watu au jamii ya pahala fulani, wakati fulani
na kwa sababu fulani. Tukirejelea mawazo yake, tunaweza kufasiri dhana hii kuwa dira na
mwongozo wa kulikabili jambo kifalsafa, kidini, kimantiki, kijamii na kiutamaduni. Pia inaweza
elezwa kuwa ni mawazo au mwongozo unaomwongoza mtafiti au mchambuzi wa jambo fulani
ili kuweza kulikabili jambo hilo ambalo halijapata kupatiwa ufumbuzi au ukweli wake.
TUKI (2004) wanafasiri nadharia kuwa ni mawazo, maelezo au mwongozo uliopangwa ili
kusaidia kueleza, kutatua au kutekeleza jambo fulani. Kulingana na maelezo ya Wafula R. M
(2004) nadharia husheheni mwongozo wa mikakati ya usomaji wa kazi ya fasihi na hucheza
nafasi ya dira katika kuhakiki na kufanya unamuzi fulani. Kwa upande mwingine wasomi
Wafula na Njogu (2007) wanafafanua na kupambanua nadharia kuwa jumla ya maelekezo
yanayomsaidia msomaji au mhakiki kuifahamu kazi ya fasihi kwa kufuata utaratibu maalumu.
Wanadokeza zaidi kuwa dhana hii hurejelea istilahi ya kijumla inayomaanisha mwongozo
unaomwelekeza msomaji wa kazi ya fasihi kuifahamu kazi hiyo vizuri katika vipengele
mbalimbali vya kazi ya fasihi na namna vinaunganika kuleta umoja katika kazi husika. Kwa
mfano jinsi maudhui hulingana na manthari au jinsi mandhari yanavyolingana na wahusika
katika kazi ya fasihi.
Mwalimu Wamitila (2003) anaeleza kuwa nadharia hutumiwa kumaanisha kauli za kijumla au
kaida zinazomwongoza msomaji katika ufasiri wa maana uliopo katika fasihi. Kwa mfano
katika kuelewa maudhui katika kazi ile ya fasihi. Fauka ya hayo, anasema kuwa ni njia ya
kisayanzi inayohusika na kanuni za kijumla na zinazohusika katika utatuzi wa swala fulani
katika kazi ya kifasihi na pia ni nyenzo ya kufikia malengo fulani ya kiusomi.
Nadharia za kuhakiki hata hivyo ni nyenzo tu ya kutusaidia kulifikia lengo fulani na kila nyenzo
huwa na ubora na udhaifu. Vilevile nadharia huzuka katika mazingira maalum ambayo yana
1
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Zaidi ya hayo, nadharia hizi zimegawika katika makundi mengi kutegemea malengo na mbinu
zake. Kunazo zinazomulika maswala bia ya kiulimwengu yanayotokeza katika fasihi,
zinazohusiana na saikolojia kama vile saikolojia changanuzi, zinazohusiana na visasili,
zinazojihusisha na maswala ya jamii, za umuundo wa fasihi miongoni mwa zingine nyingi.
Baadhi ya nadharia hizi ni kama vile, nadharia za kisosholojia, za kifeministi, semiotiki,
naratolojia n.k
Nadharia ya Ufeministi
Ufeministi ni dhana itokanayo na neno la kilatini 'femina' linalomaanisha mwanamke. Dhana
hii inarejelea uwakilishaji wa haki za wanawake kufuatana na imani ya usawa wa kijinsia.
Imejikita sana katika mwamko wa wanawake unaolenga kupigania na kukomesha udhalimu
dhidi yao na kufichua matatizo wanayoyapitia katika jamii.
2
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
hazikuchapishwa kama anavyodai Bonny Onyoni (2002). Kwa mfano, katika nchi ya Ufaransa
kuanzia mwaka 1789 hadi mwaka 1795, inadaiwa kulikuwa na maandamano ya wanawake
kutetea kudunishwa walichokiita 'Msimbo wa Napoleon'. Katika tetesi zao, walidai kuwa
kiongozi Napoleon alikuwa amesema kuwa, akili za wanawake ni dhaifu zikilinganishwa na za
wanaume. Kwa hivyo, wanawake walifaa kupewa elimu ya kiwango cha chini kama ya
ushonaji. Hili lilipelekea wanawake hao kuandamana wakitaka madai hayo kutupiliwa mbali.
Marekani Kaskazini mwaka wa 1848 pia kulikuwa na kundi la wanawake lililoungana katika
juhudi za kuleta ukombozi wa wanawake. Kulifanyika mkutano jijini New York ambapo
wanawake walitangazwa kuwa huru katika misingi ya kukubaliwa kupiga kura, kupewa elimu
ya kutosha, kupewa nafasi sawa za kufanya biashara, usawa wa kupata fidia, usawa wa kisheria
na kupata ajira. Ithibati za kimaandishi za kifeministi zenye utaratibu na zilizowekea msingi
nadharia ya ufeministi ni ‘A vindication of the Rights of Women’ ya Mary Wollstonecraft
(1792) na ‘A Room of One's Own ya Virginia’ Woolf (1929). Mary Woollstonecraft ni
mwandishi aliyeasisi mazungumzo kuhusu maswala ya wanawake na kulalama kuhusu hali
wanawake walikuwa wanapitia katika jamii. Simone de Beauvoir katika kazi yake ya ‘The
Second Sex’ mwaka wa 1952 alichangia pakubwa maendeleo ya uhakiki wa kifeministi. Katika
kazi yake alibainisha, kukosoa na kupiga vita asasi zilizomdhalilisha au kumdunisha
mwanamke. Alizifafanua asasi zinazowadunisha wanawake kama vile dini, ndoa na utamaduni.
Beauvoir anasema kuwa dini humkandamiza mwanamke kwa kumfundisha kunyenyekea. Ndoa
nayo imejengwa kwenye misingi na imani ya uwezo mkubwa alionao mwanamume
akilinganishwa na mwanamke. Kulingana naye ndoa, humsawiri mwanamke katika tamathali
hasi na duni.
Mwandishi mwingine ni Kate Millett katika kazi ya ‘Sexual Politics’ anaonyesha athari kubwa
katika historia ya Ufeministi. Millett aliwashambulia sana waandishi wanaume kama vile Henry
Miller, Norman Miller, Jean Gennet na D.H.Lawrence kutokana na jinsi walivyowasawiri
wahusika wa kike. Kutokana na aliyoyagundua katika kazi hizo, Millett anabainisha kuwa
miundo ya kijamii pamoja na asasi zake zinashirikiana kumkandamiza mwanamke. Millett
vilevile anaikosoa mikabala ya saikolojia changanuzi ya Sigmund Freud kwani ina mapendeleo
makubwa kwa mfumo wa ki-ubabedume. Mwanasaikolojia huyu alidai kuwa mtoto wa kike
huanza kujichukia mara tu anapogundua kuwa hana kiungo cha kiume. Hali hii husababisha
alichokiita `wivu’ wa zubu'. Kutokana na wazo la 'wivu wa zubu' la Freud, Millet anaeleza kuwa
3
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
wivu uliopo ni wa uwezo alio nao mwanamume kutokana na muundo wa kijamii. Mwanamke
anakuwa na wivu wa kinachoashiriwa na hilo zubu wala sio zubu kama kiungo cha mwili.
4
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Tapo hili linashikilia kwamba, wanawake wana namna yao ya kipekee ya kuandika na kujieleza.
Aidha, wanasema kuwa kuna dhamira zinazorudiwarudiwa katika tungo za wanawake.
Wanashugulikia kazi za fasihi zilizotungwa na wanawake na pia wanaume maadamu zinaongea
juu ya wanawake.
5
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
kijadi. Vilevile ni mtazamo unaokuza na kuendeleza hisia za umoja wa wanawake kama kundi
linalodhulumiwa. Aidha, lengo muhimu la nadharia hii ni kuvumbua na kuziweka wazi kazi za
sanaa zilizotungwa na wanawake ambazo zimepuuzwa kwa sababu ya utamaduni
unaompendelea mwanamume.
Pia inanuia kuchunguza historia ya fasihi ya jadi ya kike na kuwamulika waandishi wa kike
waliotambua hali za wanawake na ambao wanaweza kuchukuliwa kama vielelezo kwa
wasomaji wao. Mbatiah anaeleza kuwa lengo kuu la uhakiki wa kifeministi na hasa Ufeministi
wa Kiafrika ni kuzua mikakati ambayo itaangazia kutathmini jinsia ya kike, mitazamo, thamani
na matakwa ya wanawake sio tu katika fasihi, bali nyanja zote za maisha ya binadamu.
Nadharia hii hunuia kuzindua mwamko kwa wanawake na jinsi wanavyojiona na uhusiano wao
na watu wengine.
Nadharia ya Semiotiki
Neno semiotiki limetokana na mnyambuliko wa neno la Kigiriki ‘semeion’ lenye maana ya
ishara linalowakilisha vikundi vya wafuasi wa mielekeo fulani kulingana na maelezo ya John
Selden. Kwa upande mwingine Wamitila anapambanua kwamba ‘ semiotiki’ ni neno la lugha ya
Kiyunani lenye maana ya ishara na ambalo linatumiwa kuelezea mielekeo ya makundi fulani ya
kihakiki. Wamitila anakubaliana na Selden kuhusu asili ya neno semiotiki kwa kuwarejelea
wasomi Bailey, Matejk na Steiner walioeleza kuwa‘ semiotiki ni mchakato ambapo vitu na
matukio huja kutambuliwa kama ishara na kiumbe hai ambacho kinahisi. Kulingana na Selden
semiotiki ni taaluma ambayo hufanya kazi kwenye desturi pana za kiutamaduni zinazohusisha
ishara violwa na ishara tajwa. Anapozungumzia semiotiki ya kisasa anasema kuwa inatumiwa
kurejelea uwanja unaoendelea kubadilika wa elimu ya masomo ambayo huangaza fenomena ya
maana katika jamii.
Mwanafalsafa wa kiitalia Umberto Eco anaeleza kuwa semiotiki inahusishwa na kila kitu
kinachoweza kuchukuliwa kuwa ishara. Dhana hii ya semioiki vile vile imefasiriwa na kutolewa
mawazo na wataalamu na waandishi mbalimbali kama vile; Massamba anasema kuwa semiotiki
ni taaluma ya kisayansi inayojishughulisha na uchunguzi na uchanganuzi wa mifumo ya ishara
mbalimbali ikiwa inazingatia zaidi uhusiano baina ya kiwakilishi na kiwakilishwa.
6
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Nadharia ya semiotiki imegawika katika matawi tofauti tofauti. Msomi Nauta anadai kuwa
kuna matawi matatu makuu ya semiotiki ambayo ni semiotiki fafanuzi, semiotiki tekelezi na
semiotiki halisi. Umberto Eco anatafiti na kuongezea kundi la semiotiki ya wanyama (zuolojia)
ambalo ni kiwango cha chini kabisa,kundi hili linahusu tabia za kimawasiliano za viumbe
visivyo binadamu.
Makundi haya manne makuu ya semiotiki yamegawanywa katika vipera vya semioti kisintaksia
ambalo linahusiana na uhusiano wa ishara katika miundo rasmi ya vipengele vya kifasihi. Pili ni
la semiotiki pragmatiki inayohusiana na ishara na athari zake kwa wanaozitumi. Semiotiki
semantiki linahusiana na ishara na maana ya vitu inavyorejelea na semiotiki wasilishi.Pia kuna
migao mingine kama vile, semiotiki ya kiakili, semiotiki ya
kiutamaduni, semiotiki viumbe hai, semiotiki ya kifasihi, semiotiki ya kimuziki, semiotiki ya
kijamii, semiotiki ya violwa n.k
Fauka ya hayo, semiotiki inamulika jinsi kazi ya fasihi inavyowasiliana na wasomaji. Nadaharia
hii inaeleza zaidi jinsi matini yanavyofasiriw na namna inavyooana na wasomaji wake.
Mihimili ya Nadharia ya Semiotiki
Nadharia hii imejikita katika maelezo ya mwanaisimu mashuhuri Ferdinard de Saussure
aliyeeleza kuwa lugha ni mfumo wa ishara ambazo huangaza na kuunda mkufu wa ishara.
Alidai kuwa kila ishara huwa na sehemu mbili ambazo ni ishara yambwa/kiashirii husimamia
sauti au wasilisho la kimaandishi/matini na kifasiri/kiashiriwa ambayo ni maana ya kiashirii.
Maelezo haya yanadhihirisha kuwa kiashirii ni neno lenyewe na kiashiriwa ni maana yenyewe
7
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
ya kiashirii. Madai haya yanamaanisha kuwa kiashirii ni picha-sauti ilhali kiashiriwa ni dhana
na ishara ni jumla ya matokeo ya uhusiano baina ya kiashirii na kiashiriwa Kwa mujibu wa
Ferdinard semiotiki huangalia matini yoyote ile kama iliyosheheni ishara mbalimbali
zinazofungamanishwa na maana ya kifasihi. Kwa mfano, kiashirii cha neno ‘chui’ ni sauti ya
kiutamkaji au herufi za kiuandikaji lakini kiashiriwa ni mnyama anayefugwa wa porini. Kwa
hivo uhusiano uliopo ni wa kinasibu.
Wanasemiotiki hata hivyo wanashikilia kuwa, kiashirii huweza kuwa kile kile bali
kinachoashiriwa kinaweza kuwa tofauti. Kwa mfano, huko Ulaya, neno ‘pombe’ huweza kuwa
ishara ya urafiki, pongezi, wema, ukarimu au mapenzi lakini kiashirii kinabaki kuwa neno
‘mvinyo’. Kwa hivyo, tunaweza kusema kuwa kiashirii kimoja kinakuwa na viashiriwa vingi
katika lugha ya kawaida. Mwanaisimu mwingine Peirce anaendeleza uchunguzi wa Saussure
wa ishara kuwa na sehemu mbili kiashirii na kiashiriwa na anaongezea kipengele cha tatu
ambacho ni sehemu ya kifasiri. Anaeleza kuwa ishara ina misingi inayoibua aina tatu za ishara
ambazo ni kielekezi, ishara-tanakali na taashira. Kielekezi kulingana naye hueleza na kufafanua
uhusiano uliopo baina ya ishara na kinachoashiriwa. Kwa mfano katika kazi ya fasihi,
kunaweza tokea kilio katika giza na kuashiria kuwepo kwa mtu fulani. Kwa upande mwingine,
ishara-tanakali huonyesha mahali au hali ambapo pana uhusiano kati ya ishara na kiashiriwa.
Katika kipengele hiki,michoro au picha ni ishara- tanakali zinazoeleweka. Kwa mfano milio,
‘miaoo’ ni ishara- tanakali wa paka. Hatimaye Peirce aligusia dhana ya taashira ambayo
aliitumia kuelezea aina ya ishara inayoashiria kutegemea matumizi ya kinasibu na kikawaida au
ya kidhahania.
Peirce anamedai kuwa ishara hutegemezwa kwenye msingi fulani ili kufasiriwa, na hili linaoana
na dai la Mswisi Saussure kuwa ishara hazina upekee wa maana ila zinapofasiriwa. Kupitia
juhudi zake, nadharia ya semiotiki haikuishia kuzisambaza sifa za kitaaluma sana kama
ulivyofanya umuundo.
Hata hivyo, Wafula na Njogu wamedhihirisha kwamba Mswizi katika uchanganuzi wake wa
kisemiotiki, alijikita sana katika dhima ya ishara katika jamii naye Peirce akatafiti namna ishara
zilivyotumiwa kufafanua vitendo maalum na maana ya ishara hiyo ikitokana na sheria fulani za
kiutamaduni, kitanzu na lugha.
Nadharia ya Simulizi/Naratolojia
8
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Nadharia hii inahusiana na usimulizi wa hadithi. Hadidhi ni fabula inayoelezewa kwa mtiririko
wa kimantiki unaosimulia kuhusu tukio fulani. Prince anafafanua dhana ya simulizi kama
uelezaji wa tukio moja au mengi ya kihalisia au kibunilizi.
Wahakiki wa kinaratolojia wamebainisha dhana mbili katika usimulizi; wakati hadithi na wakati
matini. wakati hadithi ni wakati inaochukua hadithi husika kuanzia mwazo hadi mwisho. Wakati
unaweza kueleweka kwa urahisi kwa kuwa unaweza kuwa baina ya siku moja, miezi mitatu au
miaka mingi inayohusisha vizazi.
Dhana ya wakati matini ni wakati inayochukua wakati fulani kusomwa. Wakati huu ni vigumu
kutathminiwa ila itategemea muda atakaouchukua msomaji na kasi yake. Hali kadhalika, kuna
wakati ambapo wakati matiniunakuwa mrefu ukilinganishwa na wakati hadithi. Hili
limejitokeza katika hadithi ya S. A Mohammed ya Kiza katika Nuru, ambapo Mvita amefika
ofisini na hajatenda lolote bado kwa muda mrefu ilhali msomaji anaendelea kusoma.
9
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Nadharia ya Udhanaishi
Kimani Njogu na Rocha Chimerah (1999) wanafasiri Udhanaishi kuwa nadharia ambayo
inajibidisha na dhana ya Maisha. Wasomi hawa wanajaribu kuuliza swali la kifalsafa kuwa
10
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Maisha ni nini?. Kwa undani wanajikita kutafiti nafasi ya mwanadamu ulimwenguni. Kwa
upande mwingine.
Mwanafalsafa huyu anaeleza kuwa binadamu ni kikaragosi cha nguvu zilizomuumba ni katika
kuzicha mtu huyu hupata utulivu wa kiroho .Kulingana naye, udhanaishi ni dhana ya hofu pale
ambapo binadamu huogopa adhabu kutoka kwa mungu kwa hivyo amefunikwa na wasiwasi
hataki na kumkosea mungu na kuhimiza ubinafsi wa binadamu. Friedrich Nietzche (1927)
katika kazi yake ya joyful wisdom” asema kuwa mungu amekufa. Tamko hili lake pamoja na
misimamo ya wenzake vinakuwa misingi muhimu ya kuzuka kwa udhanaishi wa ukanaji
mungu.
Nadharia hii ilishika sana baada ya vita vikuu vya dunia ambapo watu walikata tamaa maishani.
Kulingana na wanafalsafa walioshikilia dhana hii walidai kuwa mtu anapozaliwa, hujipata
ametumbukia katika ombwe la aina fulani.Vilevile mtu yuko huru kuishi tu na kukabiliana
11
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Mihimili ya Udhanaishi
Nadharia hii imejengeka katika nguzo kadhaa kama ilivyoasiriwa na wanafalsafa mbalimbali.
Kwa kuwa ilizalishwa baada ya Vita Kuu ya Kwanza vya Dunia, wakati binadamu alikaa kukata
tamaa, imejikita katika mihimili ifyatayo
Wanafalsafa hawa pia hawaamini uwepo wa Mungu na uumbaji wake wa ulimwengu. Kwa
kuzingatia maafa yaliyokuwa yakiwasibu wanadamu wakati wa vita vya dunia. Madai haya
yalipata mashiko miongoni mwa wanafalsafa waliodai kuwa iwapo mungu angalikuwepo basi
hangeruhusu watu kuendelea kutenda uovu na kuwanyanyasa watu waso hatia.
Udhanaishi inatambua uhuru wa watu wa uchaguzi na hatua ya wazi katika mambo mawili. Tu
kwa njia ya uchaguzi wao wa kuchukua hatua, watu wanaweza kutambua kwamba bure, kwa
sababu asili ya binadamu ni waliochaguliwa na matendo yao wenyewe kuamua.
Vilevile, nadharia hii huamini katika juhudi za mtu binafsi kujisaka au kupambana na maisha
huishia katika umauti. Inashikilia kuwa binadamu imejaa mateso na pindi tu binadamu
anapozaliwa hivyo basi huwa amejipata katika ulimweng wa mateso na shida hivyo basi kifo tu
ndiyo huwa hatima ya kila kitu. Hali kadhalika, hujadili hali kama vile mashaka na uchovu wa
mambo mbalimbali yanayotutatiza maishani na jinsi yanavyoathili maisha ya yetu.
Maudhui yanayotajwa na wadhanaishi ni kama vile uhuru wa mtu binafsi, uwezo wake wa
kujifikilia na kujiamlia. Udhanaishi unafafanua jinsi uhuru wa binadamu umeshikwa na pingu
za utamaduni wa jadi na mila. Kulingana na washikilizi, ni bora kutambua umuhimu wa
kuchagua na kutenda kulingana na uchaguzi na kujitolea majukumu ya maisha
Pia hujadili na kugusia maudhui ya ukengeushi ambapo binadamu huwa amekata tamaa au
amekosa uhakika maishani. Huwa imembidi kubadilika na kuanza maisha ambayo ni kinyume.
12
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
Nadharia hii kwa ufupi inayarejelea maisha ya binadamu, uhusiano wa binadamu katika
ulimwengu na masaibu...
HITIMISHO
Nadharia kama dira ya kuhakiki kazi ya fasihi, pia huwa na dhima ya kuchunguza, kuainisha na
kutafiti kazi hizi. Kwa ufupi nadharia hufanya kazi ya fasihi kueleweka vyema. Kwa kuwa
fasihi ina dhima kubwa sana katika jamii.
13
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI
Mwalimu Mwingisi
MAREJELEO
Wafula Richard na Kimani Njogu (2007) Nadharia na Uhakiki wa Fasihi, Jomo Kenyatta
Foundation.
Kyallo W. Wamitila (2002) Uhakiki wa Fasihi ,Misingi na vipengele vyake, Phoenix publishers
foundation.
14
Mwalimumwingisi@gmail.com,
Chuo Kikuu Cha NAIROBI