You are on page 1of 16

MAFUA YA KUKU

Habarini wafugaji nimeona nijaribu kuliongelea swala


la mafua sababu nitatizo kubwa sana kwenye ufugaji
hapa tz.

Mafua nini kwa mtazamo wa kawaida!?


Hizi ni sauti tofauti tofauti zinazotoka kwenye mfumo
wa hewa wa kuku na uteute mweupe kwenye koo
● chafya
● kukoroma
● sauti ya kuhema kwa shida
Tunapoz
● utete
Vyote hivyo tukiviona na kuvisikia tunaita mafua na
kwenda kutafuta dawa ya mafua.

Tunayoyaita mafua yanasababishwa na nini!?


1.sababu za kimazingira
2.magonjwa

1.sababu za kimazingira
Hapa vipo visababishi vingi vya kimazingira vitakavyo
sababisha kati ya zile sauti tuzisikie
▪ mzunguuko wa hewa bandani unapokua mdogo
husababisha
▪ amonia (mbolea) panapokua na mbolea ambayo
ikazalisha amonia kwa kiwango cha juu lazima kuku
wako watapiga chafya
▪ baadhi ya chakula kinapokua na ulaini ambao
unaweza ukawasumbua kuku kipindi wanakula na
vivumbivumbi vikaingia kwenye mfumo wa hewa sauti
tufazisikia
2.Magonjwa
Sababu hii ndo imenifanya niandike juu ya swala
hili tunaloliita mafua.kuna magonjwa ambayo kuku
akiyapata yanapelekea kuharibu mfumo wa hewa na
kutoa viashiria vya (mafua)
● infectious bronchitis (IB)(nimeupa jina kata
mayai)
● Infectious laryngotracheitis (ILT) (nimeupa jina
koo damu)
● Infectious coryza
● Mycoplasmosis
● Avian influenza
● ornitho bacteriosis
● dalili ya awali ya Newcastle (kideli) nk.
Yapo magonjwa mengi yanayohusishwa na mafua
nitaongelea 6 kati ya hayo amboyo nimekutana nayo
kwa wafugaji na nimeona yanaathari kubwa.

1. ● infectious bronchitis (IB)(nimeupa jina kata


mayai)
Huu ugonjwa nimeupa jina hilo (kata mayai) sababu
kwa marayakwanza nimekutananao kwa mfugaji nilijua
ni dalili zilezile za mafua ya kawaida baada ya kufanya
treatment niligundua kuwa ni (IB) kwa athari ulioacha
kwa kuku wale.

>kisababishi cha huu ugonjwa


Coronavirus
Ndio ni jamii ya corona spp virus ndio
husababisha huu ugonjwa

Dalili za (infectious bronchitis) kata mayai


》 kukoroma hasa nyakati za usiku( tusema mafua
makali)*
》 kushusha utagaji 70%
》 mayai kuwa meupe na ganda laini

Mayai yalioathiriwa na ugunjwa(IB)

◇MADHARA YA HUU UGONJWA


Unaathari kubwa sana kwa kuku wamayai
kuwatashusha utagajo zaidi ya 70% na kuja
kurudi kwenye hali yake itachukua wiki 6-8 na
kunauwezekano kuku kutokutaga tena kama jitihada
za kutibu hazitafanikiwa na madhara kwa kuku yakawa
makubwa.
Kutokana na hawa virus hishambulia kwenye mfumo
wa mayai na kuukausha

Mfumo wa mayai ulio athiriwa na (IB)


Figo za kuku zilizo athiriwa na (IB)

MATIBABU
Magonjwa ya virusi kutibika ni ngumu
Hapa tunachotibu ni zile dalili za ugonjwa
zinazoonekana (tunayoita mafua)
Dawa
Tylodox(tylosin & doxycycline) from Holland
Ilifanya vizuri kwa mfugaji nilipo itumia kutibu mafua
(Matumizi sahii ya dozi hukupa matokeo mazuri zaidi).

◇USHAURI
Kwa wafugaji tz nawaomba tumieni ile chanjo ya New‐
castle +infectious bronchitis (mnaiita chanjo ya New‐
castle ilichanganyikana na ya mafua) hiyo mnayosema
mafua ndo huo ugonjwa sasa athari zake ni kubwa.


2. Infectious laryngotracheitis (ILT) (nimeupa jina
koo damu)
Ugonjwa no 2 nimeupa jina hilo pia naushuhudia athari
zake kwa kuku unaharibu sana njia ya hewa na kuvilia
damu kwenye koo la hewa unapenda kuambatana
e.coli inapotokea maambukizi ya pili ya bacteria na
kugandisha ute unaokua kwenye njia ya hewa na
kuziba njia ya hewa na kupelekea kifo.

>Kisababishi cha ugonjwa


herpesvirus

Dalili za huu ugonjwa

》kukoroma (tunaita mafua makali)


》kupunguza kiwango cha mayai
》kunyoosha shingo juu
》ikikomaa kutoa uteute wenye damu
》kuku wataonyesha dalili ya kuumwa mafua kati ya
90-100%
》vifo ni 10-70%
》dalili nyingine ni za kawaida kama magonjwa
mengine kupunguza ulaji kiasi cha majo kwa siku
kujikunyata nk.

DALILI KWA PICHA NA MABADILIKO NDANO YA


MWILI.
Koo la hewa lililoathiriwa na (ILT) na e.coli

Nilifanya upasuaji kwa mfugaji mmoja nikakutana na


huu ugonjwa nikaamua kuupa jina (koo damu)
Kuku mwenye ugonjwa akinyoosha shingo juu kuhema
kwa shida

MATIBABU
¿Magonjwa ya virus hayana dawa kesi hii nimejaribu
kutibu kwa dalili kutumia dawa za kutibu mfumo wa
hewa bila mafanikio vifo bado vinatokea nimejaribu
kutibu e.coli kumbunguza vifo

USHAURI
ugonjwa huu unaleta hasara kubwa kwa wafugaji
virusi hawa hufa kwa urahisi na dawa za kukinga
maambukizi shambani
Zile zinazotumiwa kufanya usafi mabandani na
zinawekwa milangoni kabala ya kuingia bandani.
Nashauri kufanya spray ya mazingira yako shambani
kila mwezi kutoruhusu muingiliano wa watu shambani
kuweka maji yenye dawa mlangoni kabla ya kuongia
bandani.
3.infectious coryza
Niugonjwa wa mfumo wa upumuji mara nyingi watu
huujua kama ugonjwa wa kuvimbisha kichwa .

>kisababishi cha ugonjwa


Haemophilus paragallinarum ni bacteria

DALILI
•Uvimbe wa uso.
• Kutokwa na machozi
• Kupiga chafya.
•Kuhema kwa shida (Dyspnoea). •Kupoteza hamu ya
kula
uzalishaji wa mayai kupungua kati ya 10-40%.

DALILI KWA PICHA

Kuku alieathirika na coryza


Kuku alieathirika na infectious coryza
Kukua alieathirika na infectious coryza

MATIBABU.
DAWA
Streptomycin,
Dihydrostreptomycin,
sulphonamides,
tylosin, (tylodox)
erythromycin.
Flouroquinolones

USHAURI
ugonjwa huu unaleta hasara kubwa kwa wafugaji
virusi hawa hufa kwa urahisi na dawa za kukinga
maambukizi shambani
Zile zinazotumiwa kufanya usafi mabandani na
zinawekwa milangoni kabala ya kuingia bandani.
Nashauri kufanya spray ya mazingira yako shambani
kila mwezi kutoruhusu muingiliano wa watu shambani
kuweka maji yenye dawa mlangoni kabla ya kuongia
bandani

4.Mycoplasmosis
Huu ni ugonjwa unaoathiri mfumo wa upumuaji
hasa unapendelea kwenye kuku wa broiler na layers
pia wanapata wenye umri wowote ule .unaweza
kuambukizwa kwenye mayai kama kuku mama atakua
anaumwa basi kifaranga kinauwezekano kikatotolewa
na kupata maambukizi kwenye yai.ni ugonjwa wa
(bacteria)
Kisababishi cha ugonjwa
Mycoplasma gallisepticum

Dalili za huu ugonjwa


▪ kukoroma
▪ kupiga chafya
▪ kuhema kwa shida
▪ kutoka uteute puani
▪ broiler kupunguza ukuaji
▪ kupunguza kiwango cha utagaji
▪ walioathirika bandani niwengi na wanaonyesha dalili
lakini vifo vichache

Dalili kwa picha

Kuku abaesumbuliwa na Mycoplasma (mafua)


Muonekano wa sehemu ya kwenye utumbo yenye
majimaji (Mycoplasma
TIBA YA MYCOPLASMA
》 tylosin
》 doxycycline (tylodox) from Holland imeonekana
ikifanya vizuri zaidi kama ikitumiwa kwa kiwango
sahihi cha dozi

Ushauri.

Kwa wafugaji wa broiler huu ugonjwa ni kawaida


nimara chache sana unaweza ukafuga broiler asipate
(mafua) na mara nyingi broiler ni wahanga wakubwa
wa Mycoplasma. Hivyo na shauri kutibu na kukinga kila
inapofika siku 9-12 wapatie kuku tylodox kwa ulinzi na
kutibu uwe umeona dalili au hujaona na kwenye kulea
vifaranga vya layers pia siku 9-12 wapatiwe tylodox
kwa kiwango sahihi


5. dalili ya awali ya Newcastle (kideli)
Nimeona niliweke hili kama sababu moja wapo ya
chanzo cha hayo tunayoita mafua Newcastle (kideli)
pia inaathiri mfumo wa upumuaji hivyo kuku akiathirika
na Newcastle ataonyesha ishara za awali kama
anamafua.

Ushauri.
Unapopta tatizo kuhusu mafua jaribu kuita mtaalamu
aweze kubaini ni aina gani ya mafua na dawa gani ni
nzuri ya kutibu

Matumizi sahihi ya dozi yatasaidia matibabu yenye


matokeo mazuri
Matibabu holela au kutumia dawa chini ya kiwango
yatakomaza ugonjwa na utatumia dawa tofautitofauti
bila mafanikio.

Imeandaliwa na..
Vet.chuma.
0694258206
0622359072
Instagram:vet_chuma

Last modified: 18:31

You might also like