Professional Documents
Culture Documents
Sayansi Huduna Ya Kwanza
Sayansi Huduna Ya Kwanza
mbele kidogo.
b) Mwambie mgonjwa abane pua kwa dakika tano kwenye
MIMEA
Mimea imegawanyika katika makundi mawili, makundi hayo ni
mimea inayotoa maua na mimea isiyotoa maua. Mimea inayotoa
maua imegawanywa katika makundi mawili, makundi hayo ni
1)Mimea aina ya Monokotiledoni
Mimea aina ya monokotiledoni vena za majani yake ni
sambamba, ina mizizi ya nyuzinyuzi ambayo imejitokeza
kwenye kitako cha shina, haina mzizi mkuu na mbegu zake ina
kotiledoni moja. Mfano wa mimea hiyo ni mahindi,
mtama ,uwele na mpunga.
2)Mimea aina ya Daikotiledoni
Mimea aina ya daikotiledoni imegawanyika katika jamii ya
mikunde na isiyo ya mikunde, Mimea jamii ya mikunde mizizi
yake ina vinundu na pia husaidia kurutubisha udongo, mfano:
karanga ,mkunde na mharagwe.Na pia mimea isiyo ya mikunde
mizizi yake haina vinundu, mfano: mwembe na mpera.
SEHEMU ZA MBEGU
Mbegu ina sehemu kuu tatu
Gamba au testi (sehemu ya nje ya mbegu)
Kiinitete (mmea mchanga)
Ghalambegu au kotiledoni (sehemu ya kuhifadhia chakula
kwa ajili ya mmea mchanga).
WANYAMA
Wanyama wamegawanyika katika makundi mawili nayo ni
Protozoa -wenye chembe hai (seli)moja tu mfano:Amiba na
Paramesiam.
Metazoa wenye chembehai zaidi ya moja
mfano:binadamu.
Wanyama wamegawanyika katika aina mbili nazo ni
Wenye uti wa mgongo
Wasio na uti wa mgongo