Professional Documents
Culture Documents
KATIKA
UCHUMI MDOGO KWENDA UCHUMI MKUBWA.
Utangulizi:
Tunaishi katika nyakati ambazo ili mtu aweze kuyamudu maisha vizuri, anahitaji
kuwa na vyanzo kadhaa vya kimapato na sio chanzo kimoja.
Ujasiliamali ndio moja ya kitu kitakachoweza kuleta suluhisho la kiuchumi na
kuboresha maisha ya mtu.
Kuongeza kipato zaidi ya mshahara unao upata.
• Ukipata pesa wekeza kwanza kisha kula kinachobaki. Tofauti ya Masikini na Tajiri
o Masikini akipata pesa anakula kwanza kisha anawekeza kama itakuwa imebakia.
o Tajiri akipata pesa anawekeza kwanza kisha anakula inayobaki.
• Jifunze kuweka vipaumbele juu ya mahitaji muhimu utakayo fanya kwa pesa iliyopo
mkononi mwako.
o Usijaribu kutaka kutekeleza kila hitaji.
o Mahitaji ni mengi hutaweza kuyamaliza.
o Michango ni mingi hutaweza kumchangia kila mtu.
o Madeni ni mengi hutaweza kuyalipa yote kwa mara moja.
o Sio kila unacho kitaka ni lazima ukipate.
o There is difference bebween what you want and what you need.
MAISHA YA MAFANIKIO
“Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama
Usilipe mkopo kwa pesa zako, bali lipa kwa pesa za watu wengine. Kigezo hiki
kinamaanisha kwamba uchukue mikopo mizuri, mikopo ambayo inazalisha na siyo
mikopo inayokugharimu wewe. Kwa kutumia kigezo hiki, Mkopo pekee unaoweza
kuchukua ni mkopo wa uzalishaji kama vile mkopo kwa ajili ya biashara ambayo tayari
imeshasimama na hivyo unaupeleka mkopo huo moja kwa moja kwenye sehemu yenye
faida, kwa lengo la kuongeza faida zaidi. Faida utakayopata kwenye biashara ndiyo
itatumika kulipa mkopo huo na siyo fedha kutoka kwenye vyanzo vyako vingine.
Hivyo, yakupasa ukokotoe vizuri hesabu zako na ujiridhishe kuwa faida utakayopata
itatosha angalau kulipa mkopo na wewe ukabakiwa na sehemu ya faida.
Kujua tofauti kati ya mikopo mizuri na mikopo mibaya Unaweza pia kupata
kitabu kizuri kuhusu elimu ya mikopo na mambo mengine kuhusu fedha
Usihadaike na Kauli za Wakopeshaji Kuna watu huwa wanajikuta wamechukua
mikopo baada ya kushawishiwa na kauli za wakopeshaji na hata watu wengine ambao
wana mikopo. Kwa kuwa siku hizi taasisi za kukopesha ni nyingi, ukiwa mfanyakazi
ambaye mshahara ni wa uhakika au unafanya biashara ya uhakika na una mali za
kuweka dhamana, wakopeshaji watakuwinda sana wakukuposhe maana watakuwa na
uhakika kuwa utaweza kurejesha mkopo wao. Kwa sababu hiyo watatumia kila mbinu
kukushawishi wakitumia kauli mbalimbali. Kumbuka kuwa mikopo ni biashara kama
biashara nyingine. Mojawapo ya mbinu ya kupata wateja katika biashara niushawishi.
Hivyo, wakopeshaji nao wako kwenye biashara, na ili wapate wateja lazima
wawashawishi watu kwa mbinu mbalimbali. Baadhi ya kauli za wakopeshaji ni kama
vile “wewe unakopesheka” au “mfanya biashara asipokopa hawezi kukua kibiashara” au
“Mtu huwezi kuishi bila kudaiwa” au ‘usipokopa utachelewesha maendeleo yako” au
“hakuna mtu anayeendelea duniani bila kukopa” au “kama serikali inadaiwa, sembuse
wewe?” na kauli nyingine nyingi. Kosa ambalo hupaswi kulifanya ni kukopa kwa
sababu tu eti wengine wanakopa au kwa sababu wakopeshaji wamekuambia
unakopesheka au kwamba usipokopa unajicheleweshea maendeleo Mkopeshaji
anapokwambia “unakopesheka” hana maana kuwa mkopo huo utakuwa mzuri kwako au
ana uchungu sana na maendeleo yako, bali anachomaanisha ni kwamba mkopo
anaokushawishi kuchukua, ana uhakika kuwa una uwezo wa kuulipa. Hivyo, usikope
kwa sababu unakopesheka bali kopa kwa sababu unahitaji mkopo na kwamba mkopo
huo ni mzuri kwako.
matumizi ya fedha zao. Huenda watu hawajui, lakini yapo makampuni makubwa duniani
ambayo hayana mkopo wowote na mengi kati ya hayo hayajawahi kuchukua mkopo wa
aina yoyote.
Ukiacha makampuni, wapo pia watu binafsi waliofikia mafanikio makubwa ya kiuchumi
bila mikopo. Kwa leo sitawataja kwa kuwa sijapata ridhaa yao. Naomba kwa leo
nikutajie tu baadhi ya makampuni yasiyo na mikopo.. Baadhi ya makampuni hayo ni
kama ifuatavyo:
Apple – Hii ni kampuni ya kimataifa ya teknolojia ya Marekani ambayo inaunda na
kuuza bidhaa mbalimbali za teknolojia, programu za kompyuta na huduma za
mtandaoni. Bidhaa za kampuni ya Apple ni pamoja na simu za mkononi za iPhone,
vishikwambi vya iPad, kompyuta za Mac na bidhaa zingine.
Hii ndiyo kampuni inayoongoza kwa thamani kubwa duniani.
Amazon – Hii ni kampuni kubwa kabisa duniani ya uuzaji wa bidhaa mtandaoni. Kwa
kipimo cha mapato na mtaji wa soko, ni kampuni ya pili baada ya Alibaba Group kwa
jumla ya mauzo. Amazon ni kampuni ya pili kwa thamani duniani (nyuma ya kampuni
ya Apple), kampuni kubwa ya intaneti kwa mapato duniani, na baada ya Walmart, ni
mwajiri wa pili mkubwa nchini Marekani. Mwanzilishi wa Amazon ni Jeff Bezos
ambaye kwa sasa ndiye tajiri namba mbili duniani na kabla ya hapo aliwahi kuwa tajiri
namba moja duniani kwa muda wa miaka minne mfululizo (2017-2020) kabla
hajazidiwa na Elon Musk.
Zaidi ya hapo, kamwe usichukue mkopo. Hata hivyo, hata mkopo wa kukuwezesha
kuokoa maisha yako au ya watu wa karibu nao unaepukika ikiwa utajioanga vizuri na
kuweka mipango mizuri ya kukabiliana na dharura na majanga kama vile kuweka akiba
na kuwa na bima
2. MJASIRIA MALI.
SIFA ZA MJASIRIA MALI.
Mbunifu.
Mvumilivu, asiyekata tamaa.
Anayekubaliana na kukabiliana na matokeo ; faida au hasara.
Mwenye kutumia changamoto zake ama za wenzake , kwa kuzigeuza kuwa fursa
na kujipatia faida.
3. Nyenzo za ujasiriamali.
Utafiti.-Taarifa hizi zitamsaidia mjasiria mali kupanga na kuamua huduma gani
inafaa kwa eneo husika.
Mtaji.-Kianzio/fedha itumikayo katika ukusanyaji wa mahitaji kwenye uzalishaji
na utoaji wa huduma.
Bidhaa. Ni jumla ya vitu ama huduma aitoayo mjasiria mali kwa wateja wake
Wateja. Watu ambao wanaoihitaji kuipata huduma ama bidhaa toka kwa mjasiria
mali, kwa malipo halali na halisi.
AINA ZA WATEJA.
1. Mteja wa kudumu (mteja mfalme)
2. Mteja kuuliza bei. "window shopping" kuuliza bei hata kwa bidhaa asiyotaka
kununua. Akijiridhisha bei, hurudi kununua japo bidhaa moja hapa, nyingine
kule kulingana na unafuu wa bei.
3. Mteja "nipunguzie".
4. Mteja mtafiti- Huyu bei zote anazijua. Anaweza kupata huduma na akalipia bila
kuuliza bei.
5. Mteja deko-Anataka kunyenyekewa na kubembelezwa. Hupenda sana kuomba
kuongezwa, hata ikibidi kwa nguvu au kwa lazima, wana lawama pia.
6. Mteja daiwa- Hata kama ana pesa mfukoni, atataka umkopeshe tu. Wakati
mwingine wasumbufu kulipa na mwishowe nao pia wana lawama.
Mfano sokoni. Ni mahali ambapo mjasiria mali na wateja wake wanakutana kwa ajili ya
kubadilishana huduma kama malipo halali na stahiki.
AINA ZA MASOKO.
1. Soko huria. Kila mtu ana Uhuru wa kuingia na kutoka bila masharti. Ushindani ni
mkubwa na hakuna mfumo wa udhibiti wa bei kati ya muuzaji na mnunuzi.
2. Soko Hodhi. Mtoa huduma anakuwa peke yake tuu. Mf TANESCO. Na aina
zingine za masoko makubwa kulingana na mfumo wa Ujasiriamali mkubwa.
MATANGAZO.
Biashara inafaa kutangazwa kwa mabango na sauti ili wateja wafahamu huduma yako.
Hapa kuna bidhaa, bei, mahali ulipo na promosheni.
i. Hasara inayotabirika.
Kuishiwa na bidhaa Mara kwa Mara - kuuza Hamna. Kuharibika, expired date, kuoza
nk. Magonjwa na wadudu waharibifu, - Kilimo na Mifugo. Bidhaa kukaa muda mrefu
bila kunuliwa au kubaki. Utunzaji wa bidhaa mf kuganda kwa simenti, kuwepo kwa
panya na mchwa, kuchacha na kuharibika kwa vinywaji. Kutozingatia kanuni za
ujasiriamali. Kutowakarimu wateja Kwa lugha za biashara.
8. UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU.
Risiti/stakabadhi, ledger, counter book, Petty cash voucher, computer nk.
KAZI YA KUFANYA. Tambua faida na hasara kwenye ujasiria mali wako. Hapa kuna
faida mbili, faida ghafi na faida halisi.