You are on page 1of 4

UZOEFU KUHUSU BIASHARA HII

Supermarkets zinaushindani sana kwa makampuni makubwa, hata hivyo


makampuni mengi siku hizi yanafunga supermarkets zao kutokana na hasara
kubwa wanayopata. Kwa mazingira ya Tanzania tunahitaji supermarkets chache
kwa sababu wengi wetu hawapendelei kununua huko kwa sababu ya nchi yetu
bado haijawa industrialized. Vyakula ambavyo havijawa processed ndivyo vyenye
soko kubwa kuliko hivi vya supermarket ambavyo vingi
vimeshakuwa processed, na mapokeo ya wengi wa kiwango changu tunaogopa
vyakula vya aina hivyo kwa kuhofia madawa yatumikayo kuzindikia na kuhifadhia
kuathiri afya kama kansa nk.

Kuharibika kwa bidhaa nyingi ambazo ni parishable food kama alivyodokeza


mmoja hapo juu ni jambo muhimu kulitilia maanani. Vyakula vingi kwenye
maduka aina hiyo huwa ni vya muda vinavyodumu kwa siku au majuma kadhaa na
vichache kwa miezi kadhaa, hivyo kujikuta vyakula vingi ukivitupa na hivyo
kuongeza bei ya bidhaa zako ili kufidia vile unavyotupa kutokana na kuisha muda
wake kutotumika zaidi kiafya. Ughali wa bidhaa utawafanya wateja wabadilili
mwelekeo afadhali kwenda Kariakoo, Manzese, nk ambako wanapata organic food
for cheap. Kwa kiwango cha biashara hiyo hata mayai yanatakiwa yawe na muda
maalum wa kuyauza si kama waswahili tulivyozoea. Ingawa nchi zilizoendelea
vyakula hivi vya organic tuanvyoviuza kwenye masoko ya kienyeji ni bora zaidi
na ni vya bei mbaya, wenye uwezo tu ndio wanaomudu. Tofauti ya bongo
machungwa toka Afrika kusini yana bi ghali ambayo si bora kama yetu ambayo
ni organicyanayouzwa kwa bei ya kutupa

Ushauri wangu kwa mazingira ya sasa ya Tanzania, bora kuwa


na groceries ambazo vyakula vyake ni vichache na unaweza kumudu na kujua
wastani wa wateja wako utakaokuwa nao, vinginevyo unaweza jikuta umeingia
hasara kubwa sana, na kujutia kupoteza mtaji wako.

Unaweza kuona na kujifunza jinsi dunia ya leo soko la bidhaa za wese la


kuendesha motokaa, ndege na mitambo linazidi kuumiza na wengi wanaamua
kuachana nalo hasa mtaifa makubwa, tanzania bado tunalalamika tu kwa sababu ya
kutojua halihalisi yanayoendelea katika soko la dunia cause and effect yake, kwaa
wafanya biashara waliozoea kutengeneza super net profit na mazingira ya
watumiaji kwa sasa v/s wazalishaji. Hali hiyo leo imebadilika ghafla.

Mwisho gharama za uendeshaji wa supermarket ni kubwa sana kutokana na baadhi


ya vyakula kuhitaji matunzo ya pekee kama kuwa na coolers ambazo
zitakuingizia bills kubwa ya matumizi ya umeme. Utahitaji wafanyakazi wengi
zaidi ili kuweza kumudu kuiweka sawa supermarket yako. Kwa vyo vyote si
kujiingiza kichwa kichwa, bali fanya utafiti wa kutosha wa eneo, kiwango cha
wateja walengwa, makampuni yatakayo supply vyakula hapo ya ndani na
nje (vendors). Na mwisho usikose kupata ushauri kwa idara ya afya ya mji
unakotaka kuanzisha biashara yako maana biashara hiyo si kama yacorner
kiosk, biashara hiyo ina taratibu na sheria zake kutokana na kiwango na ukubwa
wake kukithi masharti ya leseni unayokusudia.

Biashara ya supermarket ndogo (Mini Supermarket)


Enzi hizo biashara za supermarket wanunuzi wake walikuwa wachache wenye
kipato cha ziada ila kwa sasa supermarket zimekuwa zikipata wateja wa kila aina.
Tafiti zinaonesha kuwa katika kila watu kumi wa mijini watu watano hupendelea
kununua bidhaa katika supermarket (ama angalau mini supermarket). Mabadiliko
haya yametokana na kuzagaa kwa supermarket kila kona na kuongezeka kwa idadi
ya watu wanaopata kipato cha kati. Hivyo basi, kuazisha mini supermarket
kwaweza kuwa wazo zuri sana la kibiashara endapo una mtaji wa kutosha kuweka
kila kitu ndani yake. Acha leo niongelee jinsi unavyoweza kuanzisha mini
supermarket yako mwenyewe. Sitoongelea supermarket kubwa bali zile ndogo
ndogo.

ENEO:
Ndani ya Dar es Salaam, mwanza ama arusha, kupata eneo linalotosha kuweka
supermarket ndogo unahitaji kati ya Tshs 800,000 hadi 3,000,000 kutegemea na
ukubwa wa chumba cha biashara na wingi wa watu katika eneo husika.

Kuna msemo huwa naupenda sana. Msemo huo si mwingine bali ni ule usemao
“Vidogo Vyavutia”. Tuchukue hiki kiwango cha chini cha Tshs 800,000. Tunalipa
miezi sita inakuwa Tshs 4,800,000. Mh, acha kuguna. Usije ukaogopa mpaka
ukaacha kuwaza kuanzisha biashara hiyo. Jua kuwa asilimia kubwa ya pesa
utayolipa kwenye mini supermarket ni kodi ya upangaji.

LESENI NA VIBALI:
Ili kufanya biashara ya mini supermarket unahitaji vibali mbali mbali na leseni.
Usiumize kichwa juu ya hili maana hata uendapo ugenini unahitaji kujua nauli za
daladala za kule japo hakuna anaejishuhulisha kuulizia. Unachotakiwa kujua ni
bajet ya kuandaa kwa nauli za daladala ama texi kule uendako. Ili usisumbuke na
suala la vibali na leseni weka bajet ya Tshs 600,000 itamaliza kila kitu.

BIDHAA:
Wapo wasambazaji kadhaa walio tayari kusambaza bidhaa mbali mbali kwenye
mini supermarkets. Hawa husambaza mlango hadi mlango. Unahitaji kujiandaa na
kati ya Tshs 10,000,000 na 20,000,000 kujaza bidhaa ndani ya supermarket.
Kwakuwa “Vidogo Vyavutia” acha tuanze na Tshs 10,000,000.

WATUMISHI:
Kwa supermarket ya bidhaa za milioni 10, hapo wapaswa uwe na watu wasiozidi 5
watakaofanya kwa shift ya watatu watatu. Hawa watakugarimu kama Tshs
2,000,000 kwa mwezi.

FAIDA:
Mini supermarkets hutoa faida kati ya Tshs 2,000,000 na 3,000,000 kwa mwezi.
Kwakuwa tumeamua kuanza kile “Kidogo Kinachovutia” faida yetu itakuwa Tshs
2,000,000 kwa mwezi.

CHANGAMOTO:
Huwa hakuna biashara isiyo na changamoto. Changamoto ya kwanza kwa
supermarket ndogo ni wizi. Wamiliki wengi wa supermarket ndogo ndogo
hulalamikia suala la wizi kutoka kwa wateja na watumishi wao. Ni rahisi mtumishi
wako kukwepa wizi wake na kusingizia wateja. Wapaswa kuweka mitego mbali
mbali ya kupunguza suala la wizi ili unufaike na faida itokanayo na biashara yako.
Moja ya mitego hiyo ni cctv camera. Kwa kawaida ukiweka camera hata mbili tu
zitasaidia sana. Hii hugarimu wastani wa Tshs 1,200,000.

Changamoto nyingine ni bidhaa kufikia mwisho wa matumizi (yaani kuexpire).


Wasambazaji kadhaa wapo tayari kuchukua bidhaa zinazoisha muda wake japo sio
wote. Kupunguza uwezekano wa kupata hasara kutokana na bidhaa kuisha muda
wake wa matumiz kabla hazijanunuliwa, jaribu kununua bidhaa zako nyingi kwa
wasambazaji walio tayari kuchukua bidhaa zilizokweisha muda wake. Pia jitahidi
kununua bidhaa ambazo zimetengenezwa muda mchache ulipita ikiwezakana hata
kuwapa masharti wasambazaji kuwa bidhaa zinazozidi mwezi wasikuletee.

Pia kuna bidhaa ambazo hazitouzika kabisa na wapo wateja watakaohitaji bidhaa
ambazo wewe hauna. Hii ni changamoto ila isije kukuvunja moyo kwani
itakusumbua mwanzoni tu na baadae utakuwa mzoefu.

Biashara ya mini supermarket ni biashara yenye faida sana ila huhitaji mtaji
usiopungua Tshs 17,000,000 na uangalizi wa karibu ili kushamiri.

Credits: Juma Kessi/miamia.co.tz

You might also like