You are on page 1of 33

UANDISHI

WAKUMBUKUMBU
NA
DAKTARI WA KISWAHILI
FAGIL
Kumbukumbu ni kuhifadhi kimaandishi ya mambo
yanayojadiliwa katika mkutano. Kumbukumbu hutumiwa
kama ithibati na ukumbusho wa yale yaliyozungumzwa katika
mkutano. Katika uandishi wa kumbukumbu, mwandishi
afuatie utaratibu maalum kwa kuzingatia sifa zifuatazo;
 Andika mada au kichwa cha kumbukumbu; kichwa lazima
kionyeshe-jina rasmi la kikundi/shirika, mahali pa mkutano,
tarehe na saa za mkutano. Kwa mfano;
KUMBUKUMBU ZA MKUTANO WA SHIRIKA LA MSALABA MWEKUNDU ULIOFANYIKA
KATIKA UKUMBI WA SHULE YA KIJENSI MBARARA MNAMO IJUMAA TAREHE
08.09.20173SAA SITA ADHUHURI

 Andika mahudhurio; Andika orodha ya majina ya waliohudhuria


mkutano, waliokosa kuhudhuria kwa udhuru, waliokosa kuhudhuria
bila ya udhuru, wageni (waalikwa) (silazima)
 Andika Ajenda; Hii ni orodha ya mambo yatakayoshughulikiwa hatua
kwa hatua mkutanoni. Mambo katika ajenda yafuatie utaratibu.
 Kiini; ni sehemu ya yale yaliotokea nakuafikiwa mkutanoni. Kila hoja
inakuwa na “kumbu”namba
 Kuvunjwa kwa mkutano; baada ya mambo kadha kujadiliwa,
mwenyekiti huvunja mkutano.Weka saa za kikao/mkutano kuvunjwa
na shauri la mwisho la mwenyekiti.
 Hitimisho; weka nafasi ya mwenyekiti na katibu watakapoweka
majina, sahihi na tarehe.

Angalia mfano hapa chini


SWALI: 1. Jivalishe viatu vya kaibu mkuu wa kamati ya maswala
ya kiakademia shuleni kwako na mna mkutano wa kujadili
maswala nyeti ya kiakademia. Andika kumbukumbu za mkutano
huo.

KUMBUKUMBU ZA MKUTANO WA KAMATI YA MASWALA YA


KIAKADEMIA YA SHULE YA KEJENSI MBARARA ULIYOFANYIKA
JUMA PILI KUANZIA SAA SITA MCHANA TAREHE 12/5/2013
UKUMBINI MWA SHULE.

WALIOHUDHURIA. CHEO
1. Bw. Mapese.mnene Mwenyekiti
2. Bi.Atim Kosoro Katibu mkuu
3. Bw. Lusidu Sango Mwanakamati
4. Bw. Oken James Mwanakamati
5. Bi.Juma Mpole Mwanakamati
6. Bi.Nazifa Lenana Mwanakamati
Waliokosa kuhudhuria kwa udhuru
1.Bw. Aijuka Samson
Mwanakamati
Waliokosa kuhudhuria bila ya udhuru
Bi. Polina Okoth
Mwanakamati

Ajenda
 Dua la kwanza
 Mawaidha ya mwenyekiti
 Usajili wa wanafunzi
 Ulipaji wa Karo
 Mengineyo
Kumb:01/mk/01/2023; Dua la kwanza
Mkutano ulianza saa sita za mchana na maombi kutoka kwa mwanakamati ambaye
akamuomba mola kuwa kiongozi wayatakayo jadiliwa.
Kumb:02/mk/01/academia2017; Mawaidha ya mwenyekiti
 Mwenyekiti alianza mkutano kwa kumshukuru Rabana ambaye aliwawezesha

wanakamati kuwa na uwezo wa kuhudhuria mkutano kwa idadi kubwa.


 Mwenyekiti pia akashukuru wanakamati kuwa wazalendo wa shule na kufanya

kazi za shule kwa bidii sana.


 Pia aliwashauri kutekeleza kazi zao vilivyo ili maendeleo ya shule yaonekane.

 Mwenyekiti aliwatakia mjadiliano barabara mkutanoni na kuwashukuru tena kwa

kusikiliza.

Kumb:03/mk/01/2023;Usajili wa wanafunzi.
 Wanakamati walikubaliana kwamba shule iwasajili wanafunzi wengine arobaini
wa
 ziada (40) katika kidato cha tano ili kukidhi mahitaji.
 Kamati iliamua kwamba viti zaidi vinunuliwe kutosheleza ongezeko hilo la
wanafunzi.
 Kamati ilipendekeza wanafunizi wafike shuleni tarehe 07/07/2023.

Kumb:04/mk/01/academia2023;ulipajiwakaro
Wanakamati walikubaliana kwamba gharama ya chakula ipandishwe ili kukidhi
malalamiko ya wanafunzi kuhusu chakula kidogo kinachowapewa.
 Waliamua kwamba kila mwanafunzi alipe karo kamili kabla ya kusajiriwa.
 Kamati iliamua kwamba kila mwanafunzi alipe shilingi elfu mbili (2000/=)
za ukarabati na ununuzi wa vifaa vya ziada.

Kumb 05/mk/01/2023: Mengineyo


 Kamati ilifahamishwa kuhusu mipango ya kuwapeleka wanafunzi kwenye
maonyesho ya kilimo ya Nairobi na ikaamua fedha zitengewe mradi huo
 Kamati ilijulishwa kuhusu kuja kwa walimu wawili wapya, mmoja wa somo
la Kiswahili na mwengine wa somo la hesabu
 Kamati ilipendekeza kwamba jambo la kuongeza pesa za chakula cha
wanafunzi lizingatiwe kwenye mkutano wa maandalizi ya siku za wazazi.

 Kumb 06/mk/01/2023: Kufunga mkutano


Yote yaliyokuwa kwenye ajenda yalijadiliwa kwa utaratibu na ali
mwenyekiti akafunga mkutano mnamo saa nane unusu mchana.
Kumbukumbu zimendikwa na; Zimehakikishwa na;
.......……………………..
……………………………….
BI. ATIM KOSORO BW. MAPESE
KATIBUMKUU MWENYEKITI
ZOEZI ZAIDI

1. Ikiwa wewe ni karani wa kamati inayoshughulikia


maswala ya michezo shuleni. Andika kumbukumbu
kuhusu mkutano wa kamati hiyo ukizingatia mbinu
za kuimarisha michezo katika shule yako.
2. Wewe ni katibu mkutano wa watahiniwa wa kidato
cha nnena cha sita. Swala kuu ni kuhusu mpango
wa mhula wa tatu 2023. Andika kumbukumbu za
mkutano huo.
3. Wewe ni katibu wa chama cha Kiswahili shuleni
kwako na mna mkutano wa kukaribisha wanafunzi
wapya katika chama cha Kiswahili. Andika
kumbukumbu hizo.

You might also like